RC Makalla: Mkoa wa Dar upo salama Baada ya kufanikiwa kuwakamata Watuhumiwa 135 na Vifaa mbalimbali vilivyoibwa

Kwanini tuendeshe operation ya nguvu wakati wa matukio wakati tuna Askari wa kutosha.
 
Kwa hiyo baada ya saa 12 jioni basi na polisi wanaenda kulala, sasa kuna faida gani ya kuwa na polisi kwenye nchi hii. Hapo mnawaambia majambazi sasa ni wakati wenu muanze kuwaumiza watu. Polisi kwenye nchi za wenzetu wanafanya kazi masaa 24, wetu wanafanya zamu ya masaa 12, ikifika jioni ndiyo muda wao wa kazi umeisha, kwa jinsi hiyo hii nchi vibaka na majambazi hawataisha. Hizi operation za kupewa taarifa za uongo haziaminiki, si ajabu hata waliouawa si hao panya road, ni kundi la vijana wanaenda zao kwenye mambo yao wakakutwa barabarani ikawa bahati mbaya, wameuawa kuficha ushahidi, zipo wapi picha na video za polisi wakipambana na hao Panya road? Au wananchi walishuhudia hayo mapambano wapi? Msitudanganye, wewe mkuu wa mkoa ndiyo bure kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…