SoC01 RC Makalla na Uongozi wa Dar: Fuateni ushauri huu Dar es Salaam itakuwa na mazingira safi kuliko Moshi

SoC01 RC Makalla na Uongozi wa Dar: Fuateni ushauri huu Dar es Salaam itakuwa na mazingira safi kuliko Moshi

Stories of Change - 2021 Competition

Tomaa Mireni

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2015
Posts
2,395
Reaction score
2,391
Kwanza kabisa kuondolewa kwa mifuko ya plastiki bado hakujafanya mazingira kuwa safi. Nini tatizo kwa mkoa wa Dar es Salaam?

Jibu ni rahisi tu, tatizo ni msongamano wa watu pamoja na wafanyabishara wadogo (machinga) huu ndio ukweli. Japo ili kufanya mkoa huu kuwa safi si lazma uwatoe ila unaweza kutengeneza mtandao wa usafi na mkoa ukang'aa.

Cha kwanza utaratibu wa usafi unapaswa kuwa ni ule ule ila wawepo wasimamizi (walinzi) wa kila siku. Kwa sababu ya ugumu wa kumfuatilia mtu alietupa taka sehemu fulani mashauri haya.

Upitishwe sheria ndogo kwa ,mfanya biashara yeyote, wakaazi wa mitaani na wapangaji wana wajibu wa kusimamia usafi kwenye maeneo yao,mkaguzi wa takataka akija na kukuta kuna uchafu/takataka katika eneo alilopo atapigwa faini ya 50,000/= bila kujali katupa yeye au mwingine.

Kama utamwona mtupaji wa taka si lazma umkamate,unaweza kuzungumza nae na kumpa elimu kuhusu usafi,huku ikisisitiza achukue taka yake aondoke nayo kama akikataa uombe usaidizi kwa raia wengine mumkamate.

Vituo vya kuwafikisha wachafuzi viwe serikali za mtaa kwanza sababu ndio zipo nyingi kuliko ofisi nyingine. Akilipa 50,000 kamishileni ya mkamataji iwe 20,000(ili kuhamasisha)

Uwepo wa sheria hiyo utafanya kila mtu awe makini kwenye eneo atakalokuwepo iwe kasimama stendi,mchoma mahindi, mmachinga hata majumbani pia.

UMAKINI UTAKUWA HIVI KWA KILA MTU

Kila mtu akuwa analinda eneo alilokuepo na hata kama kakuta uchafu ataokota na kuweka sehemu husika hata kama hajatupa yeye sababu tayari sheria hiyo inambana.

Mfano: nimeenda kituo cha daladala nasubiri gari lakini naona kuna chupa zimetupwa hovyo huku pembeni kuna dastibin itanilazimu kuokota na kuzihifadhi sababu tayari naogopa bwana afya au usafi akinikuta nimesimama hapo na hizo chupa zipo atanipiga faini mimi japo sijatupa.

Ili kutofautisha wasimamizi na matapeli, wasimamizi wapewe vitambulisho maalumu vitakavyomtambulisha au kumtofautisha na raia wa kawaida.

Tukifuata huu utaratibu ni nani atakubali kuoigwa faini? Nani atakubali kukaa au kusimama na uchafu? Nani atakwepa kufanya usafi tena?
 
Upvote 3
Umeongelea zaidi kuhusu kupiga faini watupa taka ila hujaelezea wajibu wa serikali.
Na sio kua watu wanatupa taka hovyo kwa makusudi, hapana si wote hufanya hivyo ila ni kutokana na uhaba wa vyombo vya kuwekea huo uchafu.

Maeneo mengi hayana dustbin, watu watuoe taka wapi, daladala nyingi sana hazina dustbin matokeoa yake watu wanatupa vitu hovyo wakiwa njiani.

Serikali iwajibike na sio kuumiza watu kwa kuwaweka hao walizi ambao mara nyingi ni wala rushwa tu. Dustibin zikiwepo maeneo mengi, na usafi ukiwa unafanyika, si rahisi kwa mtu kutupa taka eneo safi lenye dustibin.
 
Umeongelea zaidi kuhusu kupiga faini watupa taka ila hujaelezea wajibu wa serikali.
Na sio kua watu wanatupa taka hovyo kwa makusudi, hapana si wote hufanya hivyo ila ni kutokana na uhaba wa vyombo vya kuwekea huo uchafu.

Maeneo mengi hayana dustbin, watu watuoe taka wapi, daladala nyingi sana hazina dustbin matokeoa yake watu wanatupa vitu hovyo wakiwa njiani.

Serikali iwajibike na sio kuumiza watu kwa kuwaweka hao walizi ambao mara nyingi ni wala rushwa tu. Dustibin zikiwepo maeneo mengi, na usafi ukiwa unafanyika, si rahisi kwa mtu kutupa taka eneo safi lenye dustibin.
Masokoni hakuna dastibin? Mbona bado uchafu uko mwingi,vituo vya daladala nako hakuna? Mbona bado uchafu upo,au unataka zipangane mitaani?

Nakukumbusha tu kuwa serikali inaweka dastibin sehemu za uma tu ww mchoma mahindi, mmachinga na muuza duka hakikisha una kifaa chako na hilo lipo kisheria kabisa,kama kuna duka halina kapu la uchafu faini ni 50,000.

Haiwezekani kuweka kila sehemu sababu yatageuka kuwa uchafu tena. Kama una taka yako hifadhi mpaka ufikie dastibin ndio utupe na sio unatupa tu sehemu ni sehem.
 
Masokoni hakuna dastibin? Mbona bado uchafu uko mwingi,vituo vya daladala nako hakuna? Mbona bado uchafu upo,au unataka zipangane mitaani?

Nakukumbusha tu kuwa serikali inaweka dastibin sehemu za uma tu ww mchoma mahindi, mmachinga na muuza duka hakikisha una kifaa chako na hilo lipo kisheria kabisa,kama kuna duka halina kapu la uchafu faini ni 50,000.

Haiwezekani kuweka kila sehemu sababu yatageuka kuwa uchafu tena. Kama una taka yako hifadhi mpaka ufikie dastibin ndio utupe na sio unatupa tu sehemu ni sehem.
Mkuu dar hii masoko mengi hizo dustbin hakuna ila tu kuna mahali ambapo huwa unatupwa uchafu then gari inakuja kusomba.

Na sijajua ni vituo gani vya daladala unavyoviongelea, mfano. Ukitoka segerea mpaka mnazi mmoja vituo vyote hivyo hakuna dustibin unakuja kuikuta mnazi mmoja, ukitoka ubungo mpaka mjini pia dustbin hakuna labda uingie kwenye kituo cha mwendokasi ambacho huwezi kuingia kablda hujalipa Tsh. 650 pale. Posta stendi kabisa pale hakuna dustbin. Sasa maeneo kama hayo hakuna dustbin unataka unilipishe 50k mkuu kwelii.

Kikubwa waongeze usafi na izo dustibin. Mfano tembelea maeneo baadhi ya orsterbay(sijui ka nmepatia kuiandika), maeneo ya kule ni masafi hata mtu kutupa taka unaona aibu hata kama uko peke ako.
 
Hapo kwenye faini, na mtoa taarfa kupewa chochote hio kwa kazi yake hio imekaa vizuri na itasaidia kuwa kila mtu atakuwa mlinzi wa mwenzake

Lkn yote hayo itategemea na utayari wa serikali ya eneo husika, mana mara nyingi tunaona sheria, kanuni na miongozo inaletwa alf mwisho wa siku inapotezewa ama tunaishia njian bila kufikia lengo
 
Mkuu dar hii masoko mengi hizo dustbin hakuna ila tu kuna mahali ambapo huwa unatupwa uchafu then gari inakuja kusomba.

Na sijajua ni vituo gani vya daladala unavyoviongelea, mfano. Ukitoka segerea mpaka mnazi mmoja vituo vyote hivyo hakuna dustibin unakuja kuikuta mnazi mmoja, ukitoka ubungo mpaka mjini pia dustbin hakuna labda uingie kwenye kituo cha mwendokasi ambacho huwezi kuingia kablda hujalipa Tsh. 650 pale. Posta stendi kabisa pale hakuna dustbin. Sasa maeneo kama hayo hakuna dustbin unataka unilipishe 50k mkuu kwelii.

Kikubwa waongeze usafi na izo dustibin. Mfano tembelea maeneo baadhi ya orsterbay(sijui ka nmepatia kuiandika), maeneo ya kule ni masafi hata mtu kutupa taka unaona aibu hata kama uko peke ako.
Mazingira ya Moshi hayana tofauti na ya Dar, population tu ndio tofauti lakini kila mtu ni msafi na anajua wajibu wake.

Moshi ya 2000 haikuwa hivyo,watu walilipishwa sana faini mpaka akili ikawakaa sawa,kwa hiyo mtu bora abebe gunzi lake hata kama dastibin hakuna akatupe mbele (shambani) kuliko akamatwe.
 
Hapo kwenye faini, na mtoa taarfa kupewa chochote hio kwa kazi yake hio imekaa vizuri na itasaidia kuwa kila mtu atakuwa mlinzi wa mwenzake
Lkn yote hayo itategemea na utayari wa serikali ya eneo husika, mana mara nyingi tunaona sheria, kanuni na miongozo inaletwa alf mwisho wa siku inapotezewa ama tunaishia njian bila kufikia lengo
Hilo ni tatizo la watendaji,ndio maana nikamshauri RC afanye hivyo,adili na waliokutikana na uchafu sio watupaji wa uchafu.
 
shaka ondoeni hili suala litamalizwa na pesa itakayovunwa kwenye miamala ya simu. tumeni pesa kwa kadiri muwezavyo matokeo yake mtayaona mama samia si mjinga ana akili
 
Mazingira ya Moshi hayana tofauti na ya Dar, population tu ndio tofauti lakini kila mtu ni msafi na anajua wajibu wake.

Moshi ya 2000 haikuwa hivyo,watu walilipishwa sana faini mpaka akili ikawakaa sawa,kwa hiyo mtu bora abebe gunzi lake hata kama dastibin hakuna akatupe mbele (shambani) kuliko akamatwe.
Huku kudanganyana sasa mkuu, mazingira ya moshi ni kama dar??
Okay tuassume ni hivo usemavyo, bado suala la faini mi sikubaliani nalo.
Moshi unakuta mitaa ni misafi, achana na faini tu mtu unaejielewa si rahisi kutupa taka eneo kama hilo. Hata dar maeneo masafi taka hakuna, ila yale maeneo ambayo ni kama yametengwa dustbins hakuna ndio hayo korofi sasa.

Mimi nnachoshauri ni kua jiji lisafishwe dustbin ziwepo, halafu sasa hizo faini ndio zitiliwe mkazo. Ila sio hali kama hii halafu idai faini nadhani ndio maana hata watendaji wanaona aibu kudai izo 50k japo kisheria kutupa taka hovyo hapa jiji faini ni hiyo 50k.
 
Huku kudanganyana sasa mkuu, mazingira ya moshi ni kama dar??
Okay tuassume ni hivo usemavyo, bado suala la faini mi sikubaliani nalo.
Moshi unakuta mitaa ni misafi, achana na faini tu mtu unaejielewa si rahisi kutupa taka eneo kama hilo. Hata dar maeneo masafi taka hakuna, ila yale maeneo ambayo ni kama yametengwa dustbins hakuna ndio hayo korofi sasa.

Mimi nnachoshauri ni kua jiji lisafishwe dustbin ziwepo, halafu sasa hizo faini ndio zitiliwe mkazo. Ila sio hali kama hii halafu idai faini nadhani ndio maana hata watendaji wanaona aibu kudai izo 50k japo kisheria kutupa taka hovyo hapa jiji faini ni hiyo 50k.
Fanya utafiti kidogo tu kwa Dar,ukikuta muuza mahindi au muuza miwa afu angalia mazingira aliyopo uniambie yanaonekana vip? Je akija bwana afya atahitaji kutafuta ushahidi tena wa aliechafua hilo eneo hata kama hakuna dastibin?.

Yani mimi nachosisitiza hata kama dastibin hakuna isiwe kigezo cha kuchafua mazingira, usafi unapaswa kuanza kwa kila mtu na sio kila kitu serikali iwawekee.

Moshi machinga wote,wauza matunda,wanaweka taka zao kwenye karai ili akiondoka akamwage sehemu husika, hategemei dastibin iliyowekwa na serikali.
 
Back
Top Bottom