Homera huwa ana mihemko sana, fuatilia historia yake hapo mbeya utagundua kitu,
Huu ni uonevu, posho za wafanyakazi hao ziko kisheria yeye Kama mkuu wa mkoa kafuata sheria ipi inayomruhusu kuchukua posho za watu na kupeleka kwenye miradi ya kiserikali?!
Anataka aonekane mzuri kwa Rais kumbe anavunja sheria na kutozingatia utawala wa kisheria na kuheshimu katiba ya nchi. Huu ni udikteta hata Magufuli hajawahi kuuufanya! Ni uonevu , ukandamizaji na ukiukwaji wa sheria na uvunjifu wa katiba unapaswa ukemewe na watu wote wapenda haki.