RC Mtaka, una nia njema lakini...

RC Mtaka, una nia njema lakini...

Mlalamikaji daily

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2014
Posts
744
Reaction score
1,621
Najua unajua wazi kuwa Mkuu wa Mkoa yupo chini ya waziri, ama kwa lugha nyingine waziri yoyote yule ni boss wako wewe, kumtaja waziri wazi wazi kana kwamba si kitu, sio jambo jema.

Unaposema waziri akiuliza kuhusu makambi "wamjibu kwa kumuuliza kuwa watoto wake yeye wanasoma wapi?" unajua fika kuwa hii kauli ni wewe unayeuliza kwa huyo "waziri" indirect, maana hakuna RAIA mwenye uwezo wa kujibizana na waziri wazi wazi, wadau wa mambo wanasema hii ni kauli yako ya pili kutaja "waziri" katika namna ambayo binafsi sikuona kama inafaa.

Nakujua wewe ni mjenga hoja mzuri, na kuhusu kauli yako hii ya makambi niseme wazi kuwa una NIA NJEMA sana! kuinua elimu yetu nchini na hususani kwa mkoa wako! sasa twende sawa hapa! ILANI YA CCM INASEMA ELIMU BURE! na wazazi wanapigwa marufuku kuchangishwa michango inayoitwa ya hovyo hovyo! nadhani ikiwemo na hii ya makambi!

lakini pia, muda huo wa ziada kwa walimu hao unaangaliwaje? nani atakaye walipa walimu hao muda wa ziada posho? ama utawashurutisha walimu kwenye hayo makambi?

Lakini je NJIA PEKEE YA KUJIANDAA KWA MITIHANI NI KUWEKA KAMBI? kwamba bila kuweka kambi watoto hawawezi kufaulu? binafsi naona hapa mzigo huu unaangukia kwa wazazi na walimu! Mheshimiwa najua una nia njema lakini kumbuka ule msemo kuwa "SHAUKU ILIYOPITILIZA HAIUI PANYA PEKEE" asante.
 
Nimemsikia na kuon akiongea na wazaz ambao wana nyuso zenye kiu ya elimu kw watoto, ila moyoni wanamzigo mkubwa wa wapi tutapata pesa za kugharamia makambi!!?

Makambi ni mazuri pia ingawa sio njia pekee kutumiwa.

Ila ni gharama san na nna uzoef wa zoez hilo kushindw kufanikiw kutokan na wazaz kushindw kuchanga.

Rai yangu serikali ijikite kuboresh swala la elimu tangu awali ili mtt atoke akiw na ujuzi wa kumwezesha kukabilian na mazingira halisi ya mtaani.

Na sio kufany jitihada za kufaulu mitihani ya mwisho tu kwa kukakarirish watoto.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Umeuliza maswali mazuri sana na binafsi nakubaliana sana na waziri utaratibu wa kusoma kwa mda uliopangwa ni mzuri zaidi kwani hii ilipangwa baada ya kufanya utafiti kwa mwanafunzi na hata mwl,huu utaratibu mpya utawachosha walimu ambao wanatarajia kufanya kazi hadi kwenye 60 yrs hadi wakati huo watakuwa wamechoka
 
Najua unajua wazi kuwa Mkuu wa Mkoa yupo chini ya waziri, ama kwa lugha nyingine waziri yoyote yule ni boss wako wewe, kumtaja waziri wazi wazi kana kwamba si kitu, sio jambo jema.

Unaposema waziri akiuliza kuhusu makambi "wamjibu kwa kumuuliza kuwa watoto wake yeye wanasoma wapi?" unajua fika kuwa hii kauli ni wewe unayeuliza kwa huyo "waziri" indirect, maana hakuna RAIA mwenye uwezo wa kujibizana na waziri wazi wazi, wadau wa mambo wanasema hii ni kauli yako ya pili kutaja "waziri" katika namna ambayo binafsi sikuona kama inafaa.

Nakujua wewe ni mjenga hoja mzuri, na kuhusu kauli yako hii ya makambi niseme wazi kuwa una NIA NJEMA sana! kuinua elimu yetu nchini na hususani kwa mkoa wako! sasa twende sawa hapa! ILANI YA CCM INASEMA ELIMU BURE! na wazazi wanapigwa marufuku kuchangishwa michango inayoitwa ya hovyo hovyo! nadhani ikiwemo na hii ya makambi!

lakini pia, muda huo wa ziada kwa walimu hao unaangaliwaje? nani atakaye walipa walimu hao muda wa ziada posho? ama utawashurutisha walimu kwenye hayo makambi?

Lakini je NJIA PEKEE YA KUJIANDAA KWA MITIHANI NI KUWEKA KAMBI? kwamba bila kuweka kambi watoto hawawezi kufaulu? binafsi naona hapa mzigo huu unaangukia kwa wazazi na walimu! Mheshimiwa najua una nia njema lakini kumbuka ule msemo kuwa "SHAUKU ILIYOPITILIZA HAIUI PANYA PEKEE" asante.
Najiuliza kwani walimu hawawezi kulipwa overtime ambayo itasainiwa na mkuu wa shule?
 
Mtaka amekuwa akisifiwa mno, pengine bila hata sababu za msingi…. kibinadamu unaweza kuona kabisa mdudu keshaingia kwenye embe.🤏[emoji2535][emoji36]
 
Makambi yalifanikiwa Simiyu
Kwa mfano shule nyingi za kata wanafunzi wanatoka mbali
 
Kwa sisi tulioathirika na suala la ukosefu wa walimu na tulimaliza shule kibishi tu,tunaona nia njema ya Mh Mtaka.

Kusema ukweli hakuna waziri anayeniudhi kama Ndalichako.Ni mtu mwenye mawazo mgando,hana uchungu wowote na watoto maskini.Ni moja ya watu wanaosubiri kuwatukana watoto wa watu kuwa wao ni vilaza,kisa amefeli physics ambayo hajawahi kumona mwalimu wake darasani.

Binafsi nilimwona mwalimu wa basic math form two,tena muhula wa pili,na kidato cha tatu tu.Kidato cha kwanza na cha nne sikuwahi kumwona mwalimu wa hisabati.Hata hivyo nilifanikiwa kupata C.
Ninaelewa sana umuhimu wa shule kadhaa kuweka kambi ambapo wata share walimu walio nao.

Ninaomba Mungu atokee Rais ambaye atarudisha usawa katika elimu.Shule zote zitakuwa English medium. Hakuna cha eti shule za maskini ndio wasome kiswahili,shule za viongozi na matajiri wasome kiingereza. Hamjui tu hili ni Bomu mnatengeneza.Ipo siku likilipuka wengi mtahama nchi
 
Kwa sisi tulioathirika na suala la ukosefu wa walimu na tulimaliza shule kibishi tu,tunaona nia njema ya Mh Mtaka.

Kusema ukweli hakuna waziri anayeniudhi kama Ndalichako.Ni mtu mwenye mawazo mgando,hana uchungu wowote na watoto maskini.Ni moja ya watu wanaosubiri kuwatukana watoto wa watu kuwa wao ni vilaza,kisa amefeli physics ambayo hajawahi kumona mwalimu wake darasani.

Binafsi nilimwona mwalimu wa basic math form two,tena muhula wa pili,na kidato cha tatu tu.Kidato cha kwanza na cha nne sikuwahi kumwona mwalimu wa hisabati.Hata hivyo nilifanikiwa kupata C.
Ninaelewa sana umuhimu wa shule kadhaa kuweka kambi ambapo wata share walimu walio nao.

Ninaomba Mungu atokee Rais ambaye atarudisha usawa katika elimu.Shule zote zitakuwa English medium. Hakuna cha eti shule za maskini ndio wasome kiswahili,shule za viongozi na matajiri wasome kiingereza. Hamjui tu hili ni Bomu mnatengeneza.Ipo siku likilipuka wengi mtahama nchi
 

13a6a3d0-0710-4283-907d-86aa7bf01bae.jpg

Ila ameomba radhi
 
RC Mtaka ametoa mawazo yake....

Tuyaheshimu......

Viongozi wetu wote wanalitumikia taifa letu kuntu.....

Mgongano wa fikra ndio ukomavu wa TAIFA letu bora....

Ila maslahi ya TAIFA yatabaki kuwa ndilo lengo letu kuu hususani katika dunia hii ibadilikayo kila uchao......

#NchiKwanza
#KaziIendelee
 
Najua unajua wazi kuwa Mkuu wa Mkoa yupo chini ya waziri, ama kwa lugha nyingine waziri yoyote yule ni boss wako wewe, kumtaja waziri wazi wazi kana kwamba si kitu, sio jambo jema.

Unaposema waziri akiuliza kuhusu makambi "wamjibu kwa kumuuliza kuwa watoto wake yeye wanasoma wapi?" unajua fika kuwa hii kauli ni wewe unayeuliza kwa huyo "waziri" indirect, maana hakuna RAIA mwenye uwezo wa kujibizana na waziri wazi wazi, wadau wa mambo wanasema hii ni kauli yako ya pili kutaja "waziri" katika namna ambayo binafsi sikuona kama inafaa.

Nakujua wewe ni mjenga hoja mzuri, na kuhusu kauli yako hii ya makambi niseme wazi kuwa una NIA NJEMA sana! kuinua elimu yetu nchini na hususani kwa mkoa wako! sasa twende sawa hapa! ILANI YA CCM INASEMA ELIMU BURE! na wazazi wanapigwa marufuku kuchangishwa michango inayoitwa ya hovyo hovyo! nadhani ikiwemo na hii ya makambi!

lakini pia, muda huo wa ziada kwa walimu hao unaangaliwaje? nani atakaye walipa walimu hao muda wa ziada posho? ama utawashurutisha walimu kwenye hayo makambi?

Lakini je NJIA PEKEE YA KUJIANDAA KWA MITIHANI NI KUWEKA KAMBI? kwamba bila kuweka kambi watoto hawawezi kufaulu? binafsi naona hapa mzigo huu unaangukia kwa wazazi na walimu! Mheshimiwa najua una nia njema lakini kumbuka ule msemo kuwa "SHAUKU ILIYOPITILIZA HAIUI PANYA PEKEE" asante.
Alafu likitokea la kutokea huko makambini atajibia nani?

Shule anazozitaja zina vibali maalum na yeye alipaswa kuomba Kibaki kwa karibu mkuu.

Huyu RC kaota mapembe na kalewa sifa,anapingana na Serikali kama nani? Kama hukubaliani you quit and leave sio kudharau mamlaka.
 
RC Mtaka ametoa mawazo yake....

Tuyaheshimu......

Viongozi wetu wote wanalitumikia taifa letu kuntu.....

Mgongano wa fikra ndio ukomavu wa TAIFA letu bora....

Ila maslahi ya TAIFA yatabaki kuwa ndilo lengo letu kuu hususani katika dunia hii ibadilikayo kila uchao......

#NchiKwanza
#KaziIendelee
Ametoa mawazo kama nani? Kwa kutumia platform ipi na kofia gani?
 
Mtaka ni Mtu wa Mara..Kule Mara Kisu kinaitwa Kisu na hata Gari inaitwa Gari hivyo hivyo...Nchi imejaa wanafiki hii kama husimamii unachokiamini wewe hujui unaishi kwa ajili ya Nini...Kipindi cha Magufuli Wakuu wa Wilaya walikua wanakamata sana watu hovyo hovyo yeye Alikataa ujinga ule Mkoa aliokua anauongoza....Msimsakame kwasbabu ya Jamii yetu hii iliyojaa unafiki...

Tukirudi kiuhalisi ni Waziri Gani mtoto wake anasoma Hizi shule za Umma?? Wanasiasa wanajua darasa ndio elimu...Kwenye elimu kuna janga kubwa sana... Kubwa Sana Mm nimeona mtu kamaliza la Saba hajui hata Kuandika Jina...Huku Kuna janga ni kubwa mnoo...
 
RC
Atatumbuliwa
Kachoma Kwenye Mshono Sasa Hivi
😁😀😃😃😄😄😂😁😁😆😘😍
 
Ameomba Radhi; huenda alipanick lakini ilikuwa kwa nia njema. Aliongea kwa hisia. Ni kweli kwa namna alivyozungumza vile ni insurbordination.
 
Back
Top Bottom