RC Said Mtanda wa Mwanza hastahili kuwa kiongozi wa umma kwa kutaka kuzima kesi ya Binti Tumsiime anayedai kulawitiwa na Dkt. Nawanda

Wanawake hampendani
 
Mtu ameshasema alikuwa mpenzi wake sasa tukiulize imekuwaje hadi aanze kulalamika leo huyu binti kuna kitu anatuficha ,kiufupi kanatumika na maadui wa huyo mpenzi wake
Mazingira ya kesi inaonesha kuna ulawiti umefanyika na labda si mara moja na sasa binti amechoka, tukubali tu kuwa ni kweli haya mambo yametokea hata kama habari hizi hazitupendezi, ukatili umefanywa na mteuele wa Rais akisaidiwa na mteule mwenzake RC wa Mwanza anaetaka kuzima kesi kibabe kwakuwa haimuumi Tumsime si binti yake.

Hapa utajiuliza mabinti wangapi wako mapenzini na viongozi wakubwa? Nenda Dodoma ukaone, Labda tuseme mabinti 100, je mbona hatujasikia wakishtaki ulawiti? Kwanini iwe Tumsime? Hawa ma RC wawili hawafai watumbuliwe
 
Ebhanaeeeee 😆
 
Damu kumeagika kuna mapigano hapo ya kutoana roho? Mi nauliza tu kwa nyinyi wajuzi wa mambo!
 
Hoja nzito 💯.
 
Walikosa ushahidi wa kilainishi. Wanajiuliza ataingiliwaje bila kilainishi? Au ana shimo la choo?
Kwahiyo wanaolawitiwa wote kwa kubakwa ni LAZMA wapakwe kilainishi?

Mimi naangalia hoja iliyopo mezani ya huyo Said Mtanda kujaribu kuzima kesi. Huyu Said Mtanda alimkandamiza mtoto wa marehemu dada yangu kipindi akiwa DC wa Arusha mjini.

Huyu mpwa wangu hana mume na ana watoto lakini kwakuwa aliemtendea uhalifu alikuwa rafiki wa mtanda, mtanda alibatilisha maamuz yaliyofikiwa kipindi Cha mtangulizi wake na swala hili LILIKUWA limeshatatuliwa. Mtangulizi wa Mtanda alikuwa mh. Sophia Mjema. Mtanda alimwambia mpwa wangu "we mwanamke" UKIJARIBU kwenda kushtaki huko juu nitakuwekea vizingiti na vikwazo na hutafanikiwa. Na alifanya hivyo aliandika barua na report za kumkandamiza huyu mama.

Mtanda hakuwaza mustakabali wa maisha ya watoto wa huyo mama, bali alijali kumkomoa, kumzima na kufurahisha maswahiba zake. Mpaka Leo mama yule anazungushwa tu kisa ni huyo Said Mtanda. Ana dharau wanawake sana.

Hapo alidharau maamuzi yaliyofanyika kipindi mtangulizi wake ni mwanamke na nimemshuhudia sio mara moja hapa Arusha mjini akifanya vitendo vya kudharaulisha utu wa mwanamke.

Kisha anawatishia watu yeye ni mtu wa karibu na baadhi ya viongozi wa zamani na wa sasa. Nakumbuka hiyo siku akijigamba kwamba yule mama atamwekea vikwazo alijinasibu alikuwa campaign manager wa kiongozi flani wa juu, na alionyesha dhahiri kabisa chuki yake na dharau dhidi ya wanawake.

Ifike mahali hawa viongozi wafahamu hii nchi ni yetu sote wasitumie madaraka kuumiza wananchi.

Kwa muktada huu naamini kabisa Said Mtanda amerudia jaribio la kuzima haki za watu kwa kutumia MADARAKA yake kama alivyofanya Arusha.

Mamlaka za teuzi zimtizame kwa jicho la tatu, na zichunguze hizi tuhuma.. kwa issue hii Mtanda alipaswa kuviacha vyombo vya usalama kufanya kazi kwa uhuru Ili haki ya Kila mmoja ipatikane.
 
Kuwa wapenzi sio kibali cha kulawiti,
Hata mke wako wa ndoa wa miaka 30 ukimlawiti ni kosa la jinai kwa sheria za nchi hii.
Mkuu hata mke wako wa miaka 30 si anaweza kukushitaki kwa kumbaka?
 
imagine, huyo naye ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa mkoa mzima. analinda usalama wa nani kama wanaolawitiwa anawashut up? fukuza kabisa walawiti hawa.
 
Huyu Binti mpaka anafanya media tour hivi basi kuna kitu kinatafutwa nyuma yake.

Mana kitendo cha aibu kama hicho mtu huwezi kutoka hadharani na kuongea ulichofanyiwa tena na radio changa kama hiyo crown

Kuna kitu nyuma yake .Amini kwamba
nadhani watu tu wa HAKITV wameamua kumsaidia ku air hiyo habari, baada ya kuona binti hana nguvu yeyote kutafuta haki yake. na bila kufanya hivyo binti angeweza hata kuuliwa.
 
Hata kama wangekuwa mke na mme; ulawiti ni kosa la jinai kwa mujibu wa Sheria.
Najuwa, Ila nahisi kwasababu walikuwa kwenye mahusiano, kutakuwa na “he said she said” nyingi ambazo sasa mwisho wa siku ushahidi utakaopelekwa especially kutoka kwa daktari.

Kama haikuwa mara yake ya kwanza kuingiliwa kinyume na maumbile, kunaweza kukazuka maswali mengi kutoka kwenye kambi ya utetezi.

Maana hili suala limekuwa kawaida sana kwa wa dada wengi kuingiliwa kinyume cha maumbile tena wengine wakijisifia kabisa mfano Zuchu.
 
hujui hata unachoongelea, hapa unaongelea kesi za kubaka ujue. ambazo ushahidi wa victim ni wa kuaminiwa sana. ukijumlisha na conduct za uyu jamaa za kuhonga mahela, kuomba mamsamaha, kupiga masimu n.k, unashindwaje kuamini?

cha kwanza cha kuestablish ni hivi:

1. binti anafahamiana na RC na alikuwa mpenzi wake.
2. Binti alikutana na rc siku ya tukio.
3. Binti anafafanua vizuri namna tukio lilivyotokea (credibility yake iwe vyema).
4. Binti anathibitisha rc alituma watu kwa mama yake kuomba radhi na alitoa pesa.
5. mama atakuja kuongeza ushahidi kwamba jamaa alikuja kwake kuomba radhi.
6. bank statement itatolewa kuthibitisha kwamba RC aliweka pesa kwenye account
7. daktari atakuja kutoa PF3 na kueleza alivyoona.
8. nguo chafu za binti zitakuja kutolewa.
9. watatoa pia cctv footage ya pale rockcity mall, zipo.
10. marafiti wa binti anaosoma nao watatoa ushahidi namna alivyowapigia mno kuomba connection msamaha.

kwa ushahidi kama huu, RC anachomokea wapi? halafu kwa akili ya kawaida tu, kama RC hakuwa na uhusiano na binti na hakulawiti, kwanini amenyamaza sana hata hajaita press na kujisafisha? kweli nani mwenye uwezo kumsingizia RC kwa ujasiri namna ile? na RC gani ambaye angesingiziwa akatulia kimyaaa kutapatapa kuhonga kama hakufanya icho kitu. msingizie kama makonda hivi uone kama hapatawaka moto, atakavyoleta ushahidi kinzani hata nje ya mahakama.

nakuambia, kama angekuwa amesingizia tu sasaivi binti angekuwa ndani amefungwa gerezani.
 
Just imagine zamani viongozi wakubwa kama hawa walikuwa wanaheshimika tulikuwa tunawacgukulia kama wazazi najaribu kuwaza hivi angekuwa binti wa mtanda amefanyiwa kitendo hicho angemlazimisha kufuta kesi kweli na kumlazimisha asiendelee nayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…