Shida siyo kuwa na vielelezo vingi, shida iko kwenye ushahidi unaokubaliwa na mahakama (admissible evidence). Unaweza ukawa na vielelezo vingi, lakini mbele ya sheria vinaweza vikawa havina uzito au viñaweza kuwa vinahitaji ushahidi mwingine wa kuvi'support' ambao haujatolewa/haupo. Ukisoma hukumu nyingi za mahakama ya rufaa utaona hilo likijitokeza mara kwa mara na ndiyo maana unaweza kukuta kesi ambayo tangu mwanzo ushahidi ulimwelemea mshtakiwa, anakuja kukombolewa na kukata rufaa mahakama ya rufaa. Hivyo, mambo ya sheria na uamuzi wa mahakama yanahitaji unyenyekevu sana. Kuna wakati nilishakwenda na jamaa mahakamani na alikuwa na uhakika mahakama ingekuwa upande wake na hakujiandaa kwenda na fedha za faini in case mambo yakibadilika maana aliamini angeshinda, lakini hukumu ikamgeukia na tulimwacha akiwa ndani maana ndiye aliyekuwa na hatia.