RC Said Mtanda wa Mwanza hastahili kuwa kiongozi wa umma kwa kutaka kuzima kesi ya Binti Tumsiime anayedai kulawitiwa na Dkt. Nawanda

RC Said Mtanda wa Mwanza hastahili kuwa kiongozi wa umma kwa kutaka kuzima kesi ya Binti Tumsiime anayedai kulawitiwa na Dkt. Nawanda

Hapa nasikiliza video ya Binti Tumsiime anayedaiwa kulawitiwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Nawanda. Binti ameelezea kwa kina sakata zima la kulawitiwa, mpaka msukumo mzima wa kutaka kuzima kesi.

Binti Tumsiime ameelezea kuwa baada ya kufanyiwa kitendo kile, aliripoti kituo cha polisi kwa hatua za kisheria zaidi. Wakati akiwa na Polisi wakifanya uchunguzi na kukusanya ushahidi, ghafla alitafutwa na RC Mtanda ambaye alitaka waonane ofisini kwake, binti anadai alikataa na kusema yupo na polisi lakini RC Mtanda alitumia mamlaka yake na hatimaye kuonana na binti huyo.

Binti anadai baada ya kufika Ofisini kwa Mtanda, RC huyo alimsihi suala hilo aliondoe polisi ili limalizwe kifamilia ila binti aliamua kukaza. Anadai kuwa akiwa ofisini RC Mtanda aliongea kilugha na Dkt. Nawanda (nadhani kimakonde).

RC Mtanda aliwaita Polisi waliokuja na binti huyo na kuwaambia ameshaongea na Binti na kesho wampokee vizuri anakuja kufuta kesi. Binti hakufanya hivyo kama alivyotakiwa kufanya na RC Mtanda.

Kwa mujibu wa binti huyo, RC Mtanda aliendelea kuinjinia mpango mzima wa kuzima sakata ikiwa ni pamoja na kushiriki kumwandikisha barua feki ya kufuta kesi, kumshawishi mama mzazi wa binti nk nk.

Hoja yangu hapa; RC Mtanda kama kiongozi wa umma alipaswa kuwa mstari wa mbele kuheshimu na kusimamia sheria, badala yake anatumia mamlaka ambayo tumempatia kutaka kudhulumu haki ya Tumsiime.

Rais Samia, Watanzania hatutakuelewa endapo RC Mtanda ataendelea kuwa Mkuu wa mkoa, amekosa sifa za kuwa mfano wa kuigwa.

Aione mama yetu Dkt. Gwajima D

Pia soma
Hii kesi ya Ulawiti dhidi ya huyo binti (Mwanafunzi) inabidi kuchunguzwa kwa makini sana. Bado kuna maelezo mengi sana hata kwa binti mwenyewe.

Kuanzia kukutana na RC, RC kumtaka kimapenzi na yeye kukubali ilihali anatambua bado ni Mwanafunzi na kisha kwenda na RC maeneo ya faragha kwa kusudi ya kuvunja amri ya sita.

Na alivyoingiwa kinyume na maumbile, kiukweli bado kuna maswali mengi sana... Hapa inabidi uchunguzi/upelelezi wa kina kufanyika na sio kutumia hisia. Kamwe tusiruhusu hisia kutuongoza.
 
True but sidhani kama Binti ni Chizi. Tufike mahali tuwe na utu. Angekuwa mtu wa kawaida saa hz anaongelea Segerea. Binadamu wote siyo sawa mbele ya Sheria au?
Ni kweli, anaweza asiwe chizi, but what if ni njama na michezo ya kuchafuana kisiasa, let's say binti ametumwa/ametumika n.k, hizi ndio doubts tunazozungumzia, lazima mahakama ithibitishe beyond reasonable doubts, hakuna kesi inayoamuliwa kwa kusikiliza upande mmoja, hakuna Sheria ya namna hiyo duniani kote, LAW IS LAW. Huwezi kufanya maamuzi ya kisheria kwa kutumia hisia, sympathy.
 
Mpuuzi sana Mtanda,angekuwa mwanae angepokea hela ili isuluhishwe?
 
Sasa hapo kwa maelezo yako Sijaona alipovunia SHERIA
7bu kuongea na mlalamikaji na kuomba wamalize kifamilia sio kosa kama mlalamikaji mwenyewe akiridhia
Ikiwa ajaridhia kesi inaenda mbele kama angeridhia kesi isingeenda mbele kama hvyo anavyotaka MLALAMIKAJI
Ila JINAI ingekuwa IPO vilevile JINAI haifi Wala haifutiki ikiwa haijatolewa HUKUMU na mshtakiwa akaitumikia
Hvyo labda kama una matatizo BINAFSI namkuu wa mkoa wa MWANZA ila kwa ulivyoandika SIJAONA kosa lake
 
mm najiulizaga tu, binti wa miaka 21, unaombwa unakataa, kisha unaambiwa twende kwenye gari, unaenda kwa kujiachia kabisa, unaingia kwa gari (gari yenyewe crown) unalawitiwa upo tu hata kupiga kelele kuvunja hata kioo kuomba msaada hapana, unasikilizia tu, baada ya shughuli unaenda polisi kuripoti umelawitiwa, like seriously??!!
 
Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa simiyu Dr. Nawanda anatuhumiwa kwa kumlawiti Binti mmoja aliyekuwa mwanafunzi wa SAUT ( nasema alikuwa kwasababu nasikia amesitisha masomo).
Kwa nafasi ya kimamlaka na hadhi ya cheo hicho ni fedheha kwa mhusika lakini ni fedheha kubwa mno kwa serikali hasa mamlaka ya uteuzi.
Mimi nilitarajia mamlaka ya uteuzi ingesimama kidete kuhakikisha hatua kali zinachukuliwa kwa huyu shetani na si kuushia kutengua tu.
Mimi nimesikitika pale nilipomuona yule Binti analalamika kuwa lile sakata linataka kuzimwa Tena akimtaja mkuu wa mkoa wa mwanza kwa jina la mtanda kwamba ndiye kinara wa kuzima sakata hili. Wewe mkuu wa mkoa wa mwanza unavaa kanzu ya Nini Kama unatetea walawiti? Nani unamuongoza mwanza wakati huna maadili? Unaenda msikitini kufanya Nini wakati una maadili ya kishetani? Hufai kufanya hiyo kazi na ulipaswa kuondolewa mara Moja.
Wewe uliyemteua Nawanda na mtanda jiulize kama angefanyiwa Ndugu yako wa karibu ungejisikia vipi? Je serikali ya sasa inalea walawiti? Kwanini sakata hili linataka kuzimwa Hadi Binti analalamika hadharani?
Je ni kweli ninyi ni viongozi au genge la wahalifu? Kwanini mnashindwa kutetea wananchi wasiokuwa na sauti?
Najiuliza kama Nawanda angefanya haya Enzi za Rais Magufuli ingekuwa vipi?
Kazi kwenu viongozi. Ukweli ni kwamba kitendo cha mkuu wa mkoa kutuhumiwa kwa kulawiti ni aibu kwa serikali hii.
Ishara ya mapenzi...
 
Kwanini shauri lisipelekwe mahakamani shida inakuwa wapi na mbona tunaambiwa nguvu kubwa inatumiwa na rc wa Mwanza kuzima sakata hili kwa maana nyingine sheria zinafanya kazi kwa wanyonge tu waliopo madarakani haziwagusi
 
True but sidhani kama Binti ni Chizi. Tufike mahali tuwe na utu. Angekuwa mtu wa kawaida saa hz anaongelea Segerea. Binadamu wote siyo sawa mbele ya Sheria au?
Huyo binti alikuwa na kiherehere. Kweli kaacha kusoma kaende kudanga ndani ya gari. Yawezekana ilitereza ikaingia mtaa wa pili shughuli ikaendelea. Hao walikubaliana. Binti katumika huyo
 
Unajua kwa kawaida wanasema mlawiti nae kuna muda analawitia ushapata majibu nadhani sitaki kumalizia mana Katavi mbali saanaa🤣🤣
 
Hii kesi ya Ulawiti dhidi ya huyo binti (Mwanafunzi) inabidi kuchunguzwa kwa makini sana. Bado kuna maelezo mengi sana hata kwa binti mwenyewe.

Kuanzia kukutana na RC, RC kumtaka kimapenzi na yeye kukubali ilihali anatambua bado ni Mwanafunzi na kisha kwenda na RC maeneo ya faragha kwa kusudi ya kuvunja amri ya sita.

Na alivyoingiwa kinyume na maumbile, kiukweli bado kuna maswali mengi sana... Hapa inabidi uchunguzi/upelelezi wa kina kufanyika na sio kutumia hisia. Kamwe tusiruhusu hisia kutuongoza.
Unataka UCHUNGUZ Gani ufanyike na alishapelekwa hospital na akatibiwa na akaandikiwa dawa?? Polisi walimpeleka hospital... Report ya doctor unasemaje?? CCTV footages je?
 
Mkuu wa mkoa wa mwanza SAID MTANDA amesema amevumilia vya kutosha kuhusu tuhuma zinazosemwa na binti aliyelawitiwa TUMSIME kwamba yeye alihusika kutaka kesi hiyo ifutwe ?ameenda mbali kwa kusema yeye anaviachia kazi vyombo vya uchunguzi vifanye kazi kuona kama yeye amehusika na sakata Hilo , cha kujiuliza NI kwamba yeye NI mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na USALAAMA mkoa sasa vyombo vinawezaje kufanya kazi akiwa yeye yupo ofisini na NI mwenyekiti wa vyombo hivyo ? Hivi MTANDA anaona watanzania wa sasa hawana Uelewa hadi anatamka maneno hayo kwenye media ! Hata raisi anamshangaa yeye kuongea maneno hayo
 
Mbali na upuuzi huo, Bwana Mtanda ni kiongozi mzuri sana na anajiamini nami namuamini sana. Ila ndo hayo ya kifo Cha nyani.....
 
Mbali na upuuzi huo, Bwana Mtanda ni kiongozi mzuri sana na anajiamini nami namuamini sana. Ila ndo hayo ya kifo Cha nyani.....
Uzuri gani, jambo dogo la kujua nini unapaswa kuongea hadharani limemshinda..watu wengine kichwani kuna takataka tu..mpangilio wa maneno yako unaonyesha unamsifia sabab ni muislam mwenzio..mna matatizo nyinyi!
 
Hili jambo linaenda kuamua aina ya viongozi tutakaowapigia kura serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
 
Kuwajibika ni kazi sana, wengi wamezoea kuwajibishwa tena wakati mwingine wakiajibishwa wanaenda kwenye midia kutafuta huruma ya watu.
 
Aisee...
Pole Sana kwake.

Binti kafunguka Sana yule. Hana ujanja.
 
Back
Top Bottom