Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
MKUU wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Michael Gaguti, amepiga marufuku wananchi wa mkoa wake kuishangilia Simba, pindi itaposhuka uwanjani leo kuvaana na Kagera Sugar.
Gaguti amefikia hatua hiyo akiwa na lengo la kuanzisha kampeni ya kuwahamasisha wananchi kuipenda timu yao na kuisapoti pindi itakapokuwa ikicheza na timu kubwa katika michezo yote ya ligi kuu msimu huu.
Kagera itakuwa katika Uwanja wa Kaitaba, kuvaana na Simba, ikiwa ni Mara ya kwanza timu hizo zinakutana msimu huu.
Akizungumzia hatua hiyo Gaguti alisema: “Umefikia wakati wa watu wa Mkoa wangu wa Kagera kuungana na kuisapoti timu yetu inapocheza na timu yoyote katika Uwanja wa Kaitaba na hatua hiyo inaanza kesho (leo) pindi Kagera Sugar itakapocheza na Simba, mkiwa huko pembeni shangilieni hizo timu zenu, ila hapa wote tunaishangilia Kagera Sugar.”
Kwa upande wa Meneja wa Simba, Patrick Rweyemamu amesisitiza wamejipanga kushinda mchezo huo na wala hawana mchecheto wowote.
Iyo kampen itakua endelevu au kwa sababu wanacheza n Mabigwa wa Nchi
Mwanajeshi yeye kila kitu anachukulia amri za kijeshi, anasahau huku uraiani anaonekana kituko
Leo Mikia wapo ugenini nchini Bukoba wakicheza na Club Athletic Du Kagera Sugar.
Kama nyieSababu simba inaonekana kuikamia kagera sugar badala ya kuikamia mashujaa ya kigoma au wale mashujaa wa kijani
in IGP Sirro voiceMwanajeshi yeye kila kitu anachukulia amri za kijeshi, anasahau huku uraiani anaonekana kituko
Dk 11 simba 1-0 kagera. CC : Gaguti