LGE2024 RC Zainab Telack Ahimiza Wananchi Kujiandikisha Ili Kupiga Kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 RC Zainab Telack Ahimiza Wananchi Kujiandikisha Ili Kupiga Kura Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kujiandikisha kwenye Daftari la Mkazi ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 11 hadi 20, 2024 na upigaji wa kura Novemba 27, 2024 ili kuchagua viongozi wa serikali za mitaa.

Wito huo ameutoa leo Septemba 30, 2024 katika Viwanja vya Kilwa Kivinje ambako Kivinje Jogging Club waliandaa bonanza na kualika klabu mbalimbali kutoka mikoa ya Dodoma, Mtwara, Pwani na Dar es Salaam likiwa na lengo la kudumisha afya, ushirikiano, upendo, umoja na hamasa ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa angalizo kwa wananchi ambao hawana taarifa sahihi kuhusu vitambulisho walivyo navyo na zoezi la kujiandikisha katika daftari la mkazi.

"Wapo wenzetu ambao wanasema tayari wanavitambulisho vya kupiga kura, kwa hiyo hawaoni sababu ya kujiandikisha tena, vile vitambulisho ni kwa ajili ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka kesho lakini kwa uchaguzi huu wa serikali za mitaa, serikali zamitaa, vijiji na vitongoji tunakwenda kujiandikisha kwenye daftari la mkazi," amefafanua Telack.

Screenshot 2024-09-30 at 18-17-32 TBC Digital (@tbc_online) • Instagram photos and videos.png
Screenshot 2024-09-30 at 18-17-44 TBC Digital (@tbc_online) • Instagram photos and videos.png
Screenshot 2024-09-30 at 18-15-53 David Mwakiposa Kihenzile (@david_mwakiposa_kihenzile) • Ins...png
Screenshot 2024-09-30 at 18-18-03 TBC Digital (@tbc_online) • Instagram photos and videos.png
 
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kujiandikisha kwenye Daftari la Mkazi ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 11 hadi 20, 2024 na upigaji wa kura Novemba 27, 2024 ili kuchagua viongozi wa serikali za mitaa.

Wito huo ameutoa leo Septemba 30, 2024 katika Viwanja vya Kilwa Kivinje ambako Kivinje Jogging Club waliandaa bonanza na kualika klabu mbalimbali kutoka mikoa ya Dodoma, Mtwara, Pwani na Dar es Salaam likiwa na lengo la kudumisha afya, ushirikiano, upendo, umoja na hamasa ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa angalizo kwa wananchi ambao hawana taarifa sahihi kuhusu vitambulisho walivyo navyo na zoezi la kujiandikisha katika daftari la mkazi.

"Wapo wenzetu ambao wanasema tayari wanavitambulisho vya kupiga kura, kwa hiyo hawaoni sababu ya kujiandikisha tena, vile vitambulisho ni kwa ajili ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka kesho lakini kwa uchaguzi huu wa serikali za mitaa, serikali zamitaa, vijiji na vitongoji tunakwenda kujiandikisha kwenye daftari la mkazi," amefafanua Telack.

View attachment 3111434View attachment 3111435View attachment 3111436View attachment 3111438
 

Attachments

  • Screenshot_2024-07-16-21-00-20-1.png
    Screenshot_2024-07-16-21-00-20-1.png
    420.8 KB · Views: 2
Ehh watu wa kivinje nao wanakimbizwa jogging 😄

Ova
 
Back
Top Bottom