Re: Jaman huu utaratibu wa English Medium Schools na Waalim wao Vipi?

Mkuu wangu Frank, hayo ni makosa ya regulatory board, ukaguzi wa shule (unaokufa) aina ya walimu waliopo jatika shule hizi wanatoa notes zao kwenye ma abbot,ma nelkon wanaona hayo ndo wanayopenda wazazi, kama kule kijijini mginjwa akienda hosp asipochomwa sindano. Kazi ipo.
 

Huo ni ufundishaji tu mkuu lakini mbona mtihani unakuwa mmoja tu ila katika lugha mbili tofauti. vipi kuhusu english medium za serikali zinatumia mtaala upi? na kama wanatumia mtaala tofauti kabisa mbona mtihani wa taifa wanafanya mmoja na ufaulu ni sawa tu. Japo matokeo ya lasaba kumi bora nyingi ziliongoza za english medium kama Tusiime, Feza n.k
 
Jamani ni bora mkafanya utafiti kwanza badala ya kuja na hoja zenu goigoi
 

Jamani hapa sidhani kama ni suala lakusema mpeleke shule za Kayumba. Kwanza Dhihaka hazijengi. Kikubwa hapa ni kuangaliahoja ya mtoa mada. Kwani kama kweli watoto wanapelekeshwa na ma- home work yanayopita kiwango si afya kwamtotovilevile.Pamoja na kupenda watoto wafaulu lakini sijui kama kukarirsha maswali na majibu ni vizuri. Sijui pia kama kuwafundisha watoto kiasi kuwa hawapati muda wakupumzikani vizuri pia.

Kwa upande wangu sina hakika kama Wizara husika inafuatilia vya kutosha hizi shule kwa kweli kwani nyingine ni majanga. ada kubwa kupita kiasi, na ada hiyo ndiyo inayojenga shule sidhani kama hii ni sahihi!! Wakati juhudi za kuhakikisha shule za (baadhi wanazozikebehi) ambazo kwa kweli zina curriculum nzuri ufuatiliaji ndio tatizo. Wizara ifanye juhudi ufuatiliaji wa shule hizo za public zirudie ile hadhi ya zamani jamani. Nakumbuka nilivyochaguliwa kujiunga Forodhani Secondary Shool, DSM shule ya public nilivyofurahi.Wakati huo huo shule za Binafsi zifuatiliwe pia sio tu viwango bali hata namna ya utoaji wa elimu kwa watoto kwa ajiliya afya ya kimwili na kisaikolojia pia. Waangalie elimu itolewe kwa kiasi kinachoendana na umri wa mtoto kwa kweli.

Kuna mifano ya shule kama 'Agakhan' nayoifayamu miaka ya 90s , mtoto anapata best education, anapata muda wakucheza, kupumzika, kuwa oriented katika kuweza kujisomea vitabu nk.
 
Mi wa kwangu anaenda shule saa 2 hadi 5 na nusu au 6 kesharudi. Na homeworks wanapewa Fri hadi Fri. Huyo wa nursery.
Na nijuavyo mimi hao wanochelewa kurudi wanakula na kulala huko huko shuleni. Wanacheza pia.
 
Mi wa kwangu anaenda shule saa 2 hadi 5 na nusu au 6 kesharudi. Na homeworks wanapewa Fri hadi Fri. Huyo wa nursery.
Na nijuavyo mimi hao wanochelewa kurudi wanakula na kulala huko huko shuleni. Wanacheza pia.

Na huo ndo ukweli ila wengi wanaosema hapa inaweza kuwa wazazi lakini wale wasiofatilia maendeleo au ratiba za watoto wao mashuleni.Hakuna shule inayorudisha mtoto jioni bila kulala na kucheza hao wakiwaona kwenye vischool bus jioni wanarudi wanadhani since morning walikuwa class tu kitu ambacho sio kweli.
 
Yaonekana wazi una chuki tu na hizi shule za English medium na wala si uhalisia unaouongea, huwezi ukawa serious kudai kwamba hawa watoto wa English medium wanazidiwa na hao wa Kayumba kinadaharia tu bila kuwa na ushahidi wa hicho unachokiongea, takwimu zipi unazotumia wewe kusema hayo?
Acha kupotosha, ukweli upo wazi kwamba shule hizi za English medium zina kiwango bora cha elimu ukilinganisha na hizo za kayumba. japo zipo chache zinazoongozwa na Makanjanja wa elimu mimi siziweki lakini nyingi ni nzuri kupita hizo za kayimba unazozizungumzia. Usitake kupotosha hapa
 

Ni kweli mkuu,maana ukiangalia masomo ya mwanafunzi wa darasa la tatu ni form two.
Yaani majanga matupu,maana hata akifika huko form two hana hata moja,na mbaya zaidi zimekuwa hazifanyi vizuri sana maana wao wanarukia topics za mbele kuliko mtu anachoenda kufanyia mtihani wa taifa kinakuwa chini ya uwezo wake.
 

Hili nalikubali,Kayumbas zinawakimbiza sana kwenye Darasa la saba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…