Real Estate business in Tanzania

Real Estate business in Tanzania

Wadau,
Mimi bado ni mchanga au mgeni katika biashara ya real estate. Sasa hivi nipo katika sekta ya ajira serikalini, ila ningependa siku moja kuacha kazi za kuajiriwa na kujiairi mwenyewe. Niliamua kuingia kwenye Real Estate baada ya kuona atleast ina future na pia kitu ninachopenda kukifanya.

Nimewahi kutembelea site mbalimbali kujionea shughuli za ujenzi wa majumba hasa appartments, kwa kweli nimehamasika sana. Pamoja na kwamba biashara hii ni nzuri ila pia ina changamoto zake, ikiwa ni pamoja na utapeli katika ununuzi wa viwanja au nyumba.

Ningependa kupata ushauri wenu, hasa kutoka kwa wale uzoefu katika real estate, wa jinsi ya kuanza kufanya biashara hii na pia jinsi ya kufanikiwa. Michango yenu ni muhimu sana, nakaribisha kwa yeyote mwenye "success story" aweze kushare na sisi.

Asante.

hakuna kitu kibaya km uoga ktk ujasiriamali."if you can not take the risk you ll end up be employed by those who dare to take it"

mimi nina ambition km yako ila mimi nipo ktk stage ya ku rise capital. miimi ni graduate wa computer. na niliajiriwa kwa miaka saba sehem ambayo nilikuwa nakutana na watu nyeti sana chini ya jua. mfano raisi bush. Obama na rais wa china ndo raisi wa mwisho kupata huduma yangu then niliamua kuomba kuacha kazi. japo uingozi ulikataa kuniachia lkn vision yangu ipo mikinoni mwangu. na suala linalogusa maisha yangu hua nalipa kipaumbele sana. kwa kifupi niliacha kazi kwa kuwa nilikuwa star wa afrika mashariki ktk computer communication lkn bahati mbaya mshahara wangu mpaka naacha kazi march 2013 ni chini ya mullion moja bila hata kupata cent kumi nje ya mshahara. hivo niliacha kazi nikiamini ujuzi wangu ndo silaha yangu. nilisema naelekea kuwa big investor so natakiwa kurise capital kwa step. na kutumia njia ya kuuza maarifa. hivyo niliingia ktk mitaa nikajifunza mambo mengi kuhusu real estate. ilibidi nijifunze umeme wa majumbani. capentry. glass works. metal fabrication. tiles na material yanapopatikana na ubora wake. kupaua nyumba nk. hivi vitu ni ngumu sana mtu kuamini ninavifanya kwa ustadi wa hali ya juu tena kwa mikono yangu. sasa nimeajiri vijana 3 katika workshop yangu. huwa nasimamia nyumba za watu. natengeneza mageti na madirisha ya nyumba za watu. sasa mungu akiniwezesha mwakani nitafungua kitengo cha archtectural yaani ramani za nyumba. mradi wa matofali ya biashara na duka la hardware. nikifuzu kufika hapo nitajenga nyumba 1 ya majaribio ya kuuza. nitajenga kwa bei rahisi kwani hakuna wa kunidanganya. meterial . labour na skills ni zangu. nyumba naweza pata faida ya mpaka 10m. nami nitaanzia hapo kuwa house developer. storii yangu ni ndefu ila kuna kitu utajifunza ......mungu aniongoze
 
Haka kathread kalikuwa wapi Mbona katamu hivi.

Mkuu Myelife na OLESAIDIMU nita watafuta nikishuka huko. Mimi pia kama washiriki wengine nina Ndoto ya kuzama kwenye hii kitu

Kitu kilicho nifurahisha na hakika naamini asilimia Kubwa ya Walio onyesha interest kwenye hii thread wata fanikiwa ni kwamba wengi mnaonekana kuwa na interest(kupenda hii industry).

Ukipenda unachofanya then Changamoto zitakuwa Sio ishu Kwako.Binafsi nimekuwa nafuatilia hii kitu kwa Muda wa miaka miwili sasa. Mimi napenda kumiliki ardhi,huwa najisikia raha kumiliki ardhi hata kama sina mpango nayo wa baadae.

Kuhusu mtaji wala msijali wakuu,unaanza taratibu na Uzuri faida ya real estate huwa ni kubwa. Mimi Mwaka huu nimeanza rasmi kukusanya mtaji, njia niliyotumia ni kupitia kuuza viwanja.

Nimeshirikiana na mwenzangu tumenunua ekari 7 baada ya Kufanya upembuzi yakinifu wa eneo ili kujua sehemu potential na bei ya kununulia na kuuzia katika eneo husika.

Tunatarajia mpaka Mwakani Mwezi wa pili Mchakato wa kupima utakuwa umeisha na nitaanza kuuza. Tayari nina market strategy ambayo inalenga vijana ambao wameanza kazi.

Ekari tumenunua kwa 3M kila moja but tulitoa 20M kwa zote saba,gharama ya kupima eneo itakuwa around 8M(hata ikiongeza haitozidi 10M). Gharama jumla ni 30M including emergence,kila mtu katoa 15M. Tuna tarajia kupata 90M tukiviuza,so utagundua kuwa faida ni mara Tatu ya mtaji.

Ushauri:
Bei ya ekari bado ni nzuri Kidogo kwa Sasa bongo hivyo huu ndio wakati wa kununua ekari kama chizi vile. Lakini hakikisha unatembea ujue market value ya Eneo husika,mimi Mwaka jana kila wikend nilikuwa nashinda kigamboni mpaka shemeji yenu akawa ana kasirika,lkn ni kwasababu nilikuwa najenga network na kuifahamu vizuri kigamboni ili nijue eneo ambalo ni potential zaidi

Pili mnaweza kujiunga watu wawili kama sisi tulivyofanya,so imekuwa rahisi.Binafsi hiyo 15M niliyotoa nilikopa kwenye saccoss yenye masharti nafuu

Kuwa strategic,wakati unakusanya mtaji endelea kufanya utafiti wa lengo lako kuu. Binafsi kinacho niletaga humu JF mara nyingi ni matangazo ya viwanja na mashamba. Na Mara kwa Mara huwa napitia website za matangazo ya real estate ili kujua nini kunaendelea hasa swala la prices
 
Last edited by a moderator:
zipo njia nyingi, mojawapo ni hii,

unaweza kupita maeneo mbali mbali ya jiji hasa yale maeneo ya ardhi zenye thamani zaid mfano, Sinza, mwenge, mikocheni, mbezi, magomeni, na kwingineko, katika pitapita zako ukaona eneo ambalo kwa mtizamo wa ki'real estate, au mtizamo wa architectural, (hapa ni ngumu kidogo kufafanua, maana mitizamo inatofautiana) lakini mtizamo wako ikiwa eneo hilo linafaa kwa real estate jaribu kuanza kucheki na mmiliki wa eneo, mkataba wa mmiliki wa eneo unaweza kuwa wa aina nyingi, kwa kuuziwa ama kwa kushiriki pamoja kwenye mradi, ila kabla hamjafikia makubaliano onana na msanifu majengo kwanza (architect) kwa ushauri, architect ndo mwenye mtizamo wa mwisho kuhusu plot na idadi ya apartment na aina ya apartment zitakazofaa hapo, kwa kuanzia ndo unaweza ku'calculate gharama za kuwekeza hapo na bei utakayouza na faida utakayopata, (hapo pia itabidi uonane na mshauri wa kibiashara, huyu anaweza kukuandalia business proposal ya huo mradi,

kufikia hapo unaweza kujikuta hujatumia gharama yeyote zaidi ya mawazo na ukajikuta umepata faida kubwa, 90% ideas, only 10% money
 
Haka kathread kalikuwa wapi Mbona katamu hivi.

Mkuu Myelife na OLESAIDIMU nita watafuta nikishuka huko. Mimi pia kama washiriki wengine nina Ndoto ya kuzama kwenye hii kitu

Kitu kilicho nifurahisha na hakika naamini asilimia Kubwa ya Walio onyesha interest kwenye hii thread wata fanikiwa ni kwamba wengi mnaonekana kuwa na interest(kupenda hii industry).

Ukipenda unachofanya then Changamoto zitakuwa Sio ishu Kwako.Binafsi nimekuwa nafuatilia hii kitu kwa Muda wa miaka miwili sasa. Mimi napenda kumiliki ardhi,huwa najisikia raha kumiliki ardhi hata kama sina mpango nayo wa baadae.

Kuhusu mtaji wala msijali wakuu,unaanza taratibu na Uzuri faida ya real estate huwa ni kubwa. Mimi Mwaka huu nimeanza rasmi kukusanya mtaji, njia niliyotumia ni kupitia kuuza viwanja.

Nimeshirikiana na mwenzangu tumenunua ekari 7 baada ya Kufanya upembuzi yakinifu wa eneo ili kujua sehemu potential na bei ya kununulia na kuuzia katika eneo husika.

Tunatarajia mpaka Mwakani Mwezi wa pili Mchakato wa kupima utakuwa umeisha na nitaanza kuuza. Tayari nina market strategy ambayo inalenga vijana ambao wameanza kazi.

Ekari tumenunua kwa 3M kila moja but tulitoa 20M kwa zote saba,gharama ya kupima eneo itakuwa around 8M(hata ikiongeza haitozidi 10M). Gharama jumla ni 30M including emergence,kila mtu katoa 15M. Tuna tarajia kupata 90M tukiviuza,so utagundua kuwa faida ni mara Tatu ya mtaji.

Ushauri:
Bei ya ekari bado ni nzuri Kidogo kwa Sasa bongo hivyo huu ndio wakati wa kununua ekari kama chizi vile. Lakini hakikisha unatembea ujue market value ya Eneo husika,mimi Mwaka jana kila wikend nilikuwa nashinda kigamboni mpaka shemeji yenu akawa ana kasirika,lkn ni kwasababu nilikuwa najenga network na kuifahamu vizuri kigamboni ili nijue eneo ambalo ni potential zaidi

Pili mnaweza kujiunga watu wawili kama sisi tulivyofanya,so imekuwa rahisi.Binafsi hiyo 15M niliyotoa nilikopa kwenye saccoss yenye masharti nafuu

Kuwa strategic,wakati unakusanya mtaji endelea kufanya utafiti wa lengo lako kuu. Binafsi kinacho niletaga humu JF mara nyingi ni matangazo ya viwanja na mashamba. Na Mara kwa Mara huwa napitia website za matangazo ya real estate ili kujua nini kunaendelea hasa swala la prices

Mkuu Xfactor umenigusa sana kwenye huu uzi hasa hapo kwenye kumiliki ardhi hata kama huna manufaa nayo kwa sasa. Huo ni ugonjwa wangu pia mkuu. Imefika mahali naona kama si sawa kwa mtanzania hata mwenye kipato cha kawaida kbs kutokumiliki ardhi japo kdg kwani terms si ngumu kivile.Nasema hivi kwa experience ndogo niliyoipata kwenye nchi chache nilizopata bht kuzitembelea.

Sijawahi kufanya hiki mnachofanya na partner wako Kigamboni. Huenda huu ni wakati mwafaka so ukisikia eneo huko Kigamboni au kokote ambako ni potential pliz niambie.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zumbe, kwa faida ya wengi natamani ufafanue zaidi hapo kwenye ratio ya 99:10 panaonekana patamu sana!
 
Mkuu Zumbe, kwa faida ya wengi natamani ufafanue zaidi hapo kwenye ratio ya 99:10 panaonekana patamu sana!
mkuu asante, nimegundua pia nilikosea mara ya kwanza kwa kuweka 10% capita badala ya money,

anyway nilichomaanisha ni kwamba ukiwa na mawazo yeyote ya kibiashara hela isikuumize sana kichwa, muhimu kwanza ni ideas kwa asilimia 90, hivyo vingine vitajileta tu, nimetoa mfano hapo juu kwamba ukipata eneo portential si lazima ulinunue kama huna hela, ongea na mwenye eneo kwa kick kubwa, kama anakomaa kuliuza tengeneza idea fasta ya real estate, onana na washauri, then kaa mezani na wawekezaji, yaani utakuwa unafanya kazi ya kutafuta mchoro, business plan na wawekezaji kwa niaba ya mmiliki wa plot, mmiliki anaweza kuamua kuuza eneo lake ama akaingia mkataba na muwekezaji, vyovyote itakavyokuwa hapo tayari umeshakuwa sehemu ya huo mradi, huo ni mfano tu mdogo kwamba hujatumia hela au umetumia kidogo sana, ila zaidi kilichotumika ni ideas
 
mkuu asante, nimegundua pia nilikosea mara ya kwanza kwa kuweka 10% capita badala ya money,

anyway nilichomaanisha ni kwamba ukiwa na mawazo yeyote ya kibiashara hela isikuumize sana kichwa, muhimu kwanza ni ideas kwa asilimia 90, hivyo vingine vitajileta tu, nimetoa mfano hapo juu kwamba ukipata eneo portential si lazima ulinunue kama huna hela, ongea na mwenye eneo kwa kick kubwa, kama anakomaa kuliuza tengeneza idea fasta ya real estate, onana na washauri, then kaa mezani na wawekezaji, yaani utakuwa unafanya kazi ya kutafuta mchoro, business plan na wawekezaji kwa niaba ya mmiliki wa plot, mmiliki anaweza kuamua kuuza eneo lake ama akaingia mkataba na muwekezaji, vyovyote itakavyokuwa hapo tayari umeshakuwa sehemu ya huo mradi, huo ni mfano tu mdogo kwamba hujatumia hela au umetumia kidogo sana, ila zaidi kilichotumika ni ideas

Thanks Zumbe hapa sasa hata div 5 anakuelewa bila shida yeyote?
 
Kwa Mahitaji ya Nyumba, viwanja na magari. Follow me on instagram uncledalali
 
Last edited by a moderator:
mkuu asante, nimegundua pia nilikosea mara ya kwanza kwa kuweka 10% capita badala ya money,

anyway nilichomaanisha ni kwamba ukiwa na mawazo yeyote ya kibiashara hela isikuumize sana kichwa, muhimu kwanza ni ideas kwa asilimia 90, hivyo vingine vitajileta tu, nimetoa mfano hapo juu kwamba ukipata eneo portential si lazima ulinunue kama huna hela, ongea na mwenye eneo kwa kick kubwa, kama anakomaa kuliuza tengeneza idea fasta ya real estate, onana na washauri, then kaa mezani na wawekezaji, yaani utakuwa unafanya kazi ya kutafuta mchoro, business plan na wawekezaji kwa niaba ya mmiliki wa plot, mmiliki anaweza kuamua kuuza eneo lake ama akaingia mkataba na muwekezaji, vyovyote itakavyokuwa hapo tayari umeshakuwa sehemu ya huo mradi, huo ni mfano tu mdogo kwamba hujatumia hela au umetumia kidogo sana, ila zaidi kilichotumika ni ideas

Kiongozi hapo ume eleza vizuri.
Hapa tuna mwenye Eneo,Mwekezaji na mimi ambaye ni Facilitator sasa ktk mtazamo wa kisheria Mimi nasimama wapi na nitapataje gawiwo. Kwani naona Mmiliki wa ardhi na Mwekezaji ndio wahusika wakuu
 
Kiongozi hapo ume eleza vizuri.
Hapa tuna mwenye Eneo,Mwekezaji na mimi ambaye ni Facilitator sasa ktk mtazamo wa kisheria Mimi nasimama wapi na nitapataje gawiwo. Kwani naona Mmiliki wa ardhi na Mwekezaji ndio wahusika wakuu
mkuu hapo kwanza ulipaswa make chini na mwekezaji mkubaliane kiasi kwa maandishi, pia ungekaa chini na mmiliki wa ardhi nae muweke terms,
hata hivyo kabla ya kuwakutanisha ulipaswa uwe facilitator kwa kupitia kampuni yako, mkiwekeana ahadi za mdomo tu ni rahisi kurukwa hasa kama una'deal na wahindi, soko la real estate limetekwa sana na wakenya na wahindi, wametoka kwao huko hawana kitu wametajirikia hapa bongo,
faida nyingine unayoweza kupata ni wakati ujenzi unaendelea unaweza kujipatia vijitenda hapo, ila pia wakati wakutafuta wateja wanyumba pia hutakosa,
..
 
Haka kathread kalikuwa wapi Mbona katamu hivi.

Mkuu Myelife na OLESAIDIMU nita watafuta nikishuka huko. Mimi pia kama washiriki wengine nina Ndoto ya kuzama kwenye hii kitu

Kitu kilicho nifurahisha na hakika naamini asilimia Kubwa ya Walio onyesha interest kwenye hii thread wata fanikiwa ni kwamba wengi mnaonekana kuwa na interest(kupenda hii industry).

Ukipenda unachofanya then Changamoto zitakuwa Sio ishu Kwako.Binafsi nimekuwa nafuatilia hii kitu kwa Muda wa miaka miwili sasa. Mimi napenda kumiliki ardhi,huwa najisikia raha kumiliki ardhi hata kama sina mpango nayo wa baadae.

Kuhusu mtaji wala msijali wakuu,unaanza taratibu na Uzuri faida ya real estate huwa ni kubwa. Mimi Mwaka huu nimeanza rasmi kukusanya mtaji, njia niliyotumia ni kupitia kuuza viwanja.

Nimeshirikiana na mwenzangu tumenunua ekari 7 baada ya Kufanya upembuzi yakinifu wa eneo ili kujua sehemu potential na bei ya kununulia na kuuzia katika eneo husika.

Tunatarajia mpaka Mwakani Mwezi wa pili Mchakato wa kupima utakuwa umeisha na nitaanza kuuza. Tayari nina market strategy ambayo inalenga vijana ambao wameanza kazi.

Ekari tumenunua kwa 3M kila moja but tulitoa 20M kwa zote saba,gharama ya kupima eneo itakuwa around 8M(hata ikiongeza haitozidi 10M). Gharama jumla ni 30M including emergence,kila mtu katoa 15M. Tuna tarajia kupata 90M tukiviuza,so utagundua kuwa faida ni mara Tatu ya mtaji.

Ushauri:
Bei ya ekari bado ni nzuri Kidogo kwa Sasa bongo hivyo huu ndio wakati wa kununua ekari kama chizi vile. Lakini hakikisha unatembea ujue market value ya Eneo husika,mimi Mwaka jana kila wikend nilikuwa nashinda kigamboni mpaka shemeji yenu akawa ana kasirika,lkn ni kwasababu nilikuwa najenga network na kuifahamu vizuri kigamboni ili nijue eneo ambalo ni potential zaidi

Pili mnaweza kujiunga watu wawili kama sisi tulivyofanya,so imekuwa rahisi.Binafsi hiyo 15M niliyotoa nilikopa kwenye saccoss yenye masharti nafuu

Kuwa strategic,wakati unakusanya mtaji endelea kufanya utafiti wa lengo lako kuu. Binafsi kinacho niletaga humu JF mara nyingi ni matangazo ya viwanja na mashamba. Na Mara kwa Mara huwa napitia website za matangazo ya real estate ili kujua nini kunaendelea hasa swala la prices
Nami ndo nimeanza kujipenyeza kigamboni kaka ila dah hapo pa shemeji yetu ni kweli coz hata Wife anachukiaga maana Monday to Friday narudi job usiku then Sataurday and Sunday nashinda kigamboni kunyemelea viwanja vya bei nafuu. Hii biashara tuwe wavumilivu kaka inalipa sana nimeifuatilia kwa muda sasa. Tayari nina hekari tatu nimeshaziwekea mazingira mazuri nitaziuza mwisho wa mwaka 2014 Inshallah...
 
Nami ndo nimeanza kujipenyeza kigamboni kaka ila dah hapo pa shemeji yetu ni kweli coz hata Wife anachukiaga maana Monday to Friday narudi job usiku then Sataurday and Sunday nashinda kigamboni kunyemelea viwanja vya bei nafuu. Hii biashara tuwe wavumilivu kaka inalipa sana nimeifuatilia kwa muda sasa. Tayari nina hekari tatu nimeshaziwekea mazingira mazuri nitaziuza mwisho wa mwaka 2014 Inshallah...

Hekari moja unauza sh ngapi? Umeshapimisha? Eneo lipo nje ya huo mradi wanaodai ni wa serikali?
 
Mabenki ya Kitz mkuu yanalala tu lakini hii ni avenue inayoweza kuwalipa sana bila jasho!!! Ukijenga ghorofa la vumba 100 kabla hata halijaisha utakuwa umepata wapangaji!!!
Tatizo mtaji, watu wanaviwanja lakini mtaji hawana, hapo ndio mabenki yanapoingia mabenki wapeni pesa wenye viwanja/wajengeeni wakianza kulipwa na tenants wao waanze kurudisha pesa ya mkopo 70%
Mathalani una vyumba 100, chumba kimoja ni sh 100000 kwa mwezi, unauwezo wa kulipa mil 84 kwa mwaka na unauwezo wa kurudisha mil 250,ndani ya miaka 3

Sasa ukikopa mil 250. Unawezaje kupata 100 rooms itakayokuwezesha kulipa 84mil/yrs kuweza kulipa mkopo wa mil250 ndani ya miaka 3?
 
Hekari moja unauza sh ngapi? Umeshapimisha? Eneo lipo nje ya huo mradi wanaodai ni wa serikali?
Sijapimisha. Anayetaka kwa sasa ni 20M kwa hekari. Ni eneo ambalo mradi haujafika lakini siku sio nyingi tunaweza kujikuta tumeingizwa kwenye mradi manake jirani na hapo wameandikishwa kuingizwa mradini kwa habari ya chini ya kapeti wameambiwa anayetaka 20,000TShs@SQM. Bei ya serikali DSM ni 35,000TShs@SQM wamepigwa cha juu 15,000TShs@SQM. Ziko kwenye barabara kubwa yaani full kujidai, pesa yako tu.
 
Umbali gani toka feri?? Serikali haifanyi biashara hiyo bei elekezi ni ya kisiasa tu, anyway ni imani yangu hiyo 20mil/acre ni negotiable wacha nipange ratiba vizuri nikutafute
 
Umbali gani toka feri?? Serikali haifanyi biashara hiyo bei elekezi ni ya kisiasa tu, anyway ni imani yangu hiyo 20mil/acre ni negotiable wacha nipange ratiba vizuri nikutafute
Umbali sijui lakini ni jirani na kizuda. Sio kama serikali inafanya biashara bali inatoa bei elekezi kwa maana tungetegemea wawekezaji kama NSSF ambao ndio wanaonunua pale wangeanzia hiyo bei. Not negotiable. Hapo nikikosa mtu by end of the year, basi early 2015 najenga kibanda cha uzushi nasubiri bei kubwa zaidi...may be after a year or two nitaneemeka. 🙂
 
Wadau,
Mimi bado ni mchanga au mgeni katika biashara ya real estate. Sasa hivi nipo katika sekta ya ajira serikalini, ila ningependa siku moja kuacha kazi za kuajiriwa na kujiairi mwenyewe. Niliamua kuingia kwenye Real Estate baada ya kuona atleast ina future na pia kitu ninachopenda kukifanya.

Nimewahi kutembelea site mbalimbali kujionea shughuli za ujenzi wa majumba hasa appartments, kwa kweli nimehamasika sana. Pamoja na kwamba biashara hii ni nzuri ila pia ina changamoto zake, ikiwa ni pamoja na utapeli katika ununuzi wa viwanja au nyumba.

Ningependa kupata ushauri wenu, hasa kutoka kwa wale uzoefu katika real estate, wa jinsi ya kuanza kufanya biashara hii na pia jinsi ya kufanikiwa. Michango yenu ni muhimu sana, nakaribisha kwa yeyote mwenye "success story" aweze kushare na sisi.

Asante.

Nimefanya kazi katika real estate agent and development, kama miezi sita tu, mwaka 2006, nilikuwa Kama officer of maintenance. Nipo busy kidogo, Nitarudi kukupa changamoto, na ushauri.
Ghibuu
 
Nimefanya kazi katika real estate agent and development, kama miezi sita tu, mwaka 2006, nilikuwa Kama officer of maintenance. Nipo busy kidogo, Nitarudi kukupa changamoto, na ushauri.
Ghibuu

Utatufaa wengi mkuu GHIBUU fanya mema kwa faida ya wengi tafadhali
 
Last edited by a moderator:
Katika business hii lazima uwe na advocate. Mpangaji yoyote lazima mukubaliane kwa maandishi.
Kuwepo na term conditions katika mkataba wa nyumba.
Katika suala la viwanja kabla hujauza lazima hati uzihakikishe kwa kupitia wizara ya ardhi. Kama original or fake.

Unatakiwa uwe na accountant, business hii ni professional. Unaweza kufanya biashara ku exchange wateja na agency mwengine. Make sure unapata percentage yako, katika mwaka mwezi mmoja wako, na kama utaletewa mteja na dalali mwezi mmoja wake kila mwaka.

Ikiwa utauza kiwanja au nyumba ya mtu 10 percentage yako katika malipo.

Ikiwa wewe ni agency tu hauna nyumba zako za kupangisha, unaweza uka deal na estate agency wengine. Wasiliana nao agency wengine wape term conditions zako basi mchezo ndo huo.
Unahitaji usafiri wa kuweza kukusaidia kurahisisha kazi yako,mana sio ndogo unaweza kuimaliza masaki, mikocheni, mbezi na kwengine unatafuta nyumba, mteja anaweza kuja atakuwambia anataka nyumba maeneo hayo soon as possible.

Kama Huna uwezo wa kujenga, kama mteja wako ana project kubwa ili kuweza kupata hio tenda inakubidi utafute construction company kutiliana ubia, tena kwa maandishi. Advocate hapo mshirikishe, yaani yeye kazi yake kukuandikia mikataba.
 
Back
Top Bottom