Real Estate business?

Real Estate business?

Nimekosea kidogo
350,000*12=4,200,000
Ndani ya mwaka pesa inakuwa imesharudi tayari
Tatizo linakuja kwenye huo mkopo kaka, maana hali halisi ni kama watakuchaji riba kubwa, kifupi hela yoyote ukichukuwa benki watataka urudishe zaidi ya labda 2.55. Namaanisha ukichukuwa mkopo sema wa 3.5m/- watataka urudishe 8.925m/=. Sasa kwa hesabu zako kama utapata kodi 4.2m/- kwa mwaka, inamaanisha itakuchukuwa miaka 2 labda na miezi 2 kurudisha mkopo wao, na hapo usitafune hiyo kodi, labda uombe kwa miaka 3.
Hela yoyote uchukuwapo kama mkopo wewe zidisha mara 2.55 utapata thamani utakayotakiwa kuwarudishia wenyewe..Kila la kheri..
 
Wakuu, vipi kuhusu hii biashara kibongobongo? Prospects zake zikoje? Inalipa au bado haina nguvu sana? Naona watu wengi wanaiongelea ongelea.
Hii biashara ipo kwa naamna mbili yenye kufuata sheria na yenye kufuata taratibu za kimazoea japo kuwa kwa sasa imepoa kidogo kutokana na halialisi ya kutokueleweka ya kiuchumi.
Nianzie na yenye kufuata sheria
Hii kidogo inahitaji mtaji kiasi kulingana na unako lenga hasa kwa mfano unataka kuwa developer, broker nk hapa utapaswa kukidhi vigezo vyote na kulipa kodi zote hivyo lazima uwe umejipanga

Kufuata taratibu
Huku kuna loophole nzuri ya kukuza mtaji kwa haraka na unaweza anza katika level yoyote, huku ndiko mheshimiwa Lukuvi husema watu wana tembea na briefcase imejaa pesa maeneo ya kigamboni na b/moyo unachukua heka zako za bei nafuu unagawanya viwanja unauza chap chap kama njugu wanunuzi watapima wenyewe we unasonga mbele kutafuta sehemu nyingine ya kuwauzia...
Kama briefcase imenuna unaweza anza kama dalali , kama uko sharp zaidi unaweza nunua kwa maneno na maridhiano na wamiliki ukawalipa taratibu kila unapo uzaa.......
Kama ulikimbia umande hapa ndio penyewe.
 
Izi biashara za Real Estate (biashara ya makazi) ni biashara yenye kuitaji kuwa na pesa ya kutosha na sio kanjanja na mikopo hii ya milioni 5 kushuka chini. Kwanza banks [emoji542] zinakopesha watu wenye kipato na biashara ambayo inazunguka (current business) na lengo la biashara ni kufanya biashara na sio kusaidiana ujenge na upate faida bila wao kupata faida
 
Real Estate Business ni pana sana sana, Watu wengi wanaongelea Real Estate Business katika Angle ya Developer(Kujenga nyumba au kununua Viwanja na Kuuza). Real State Business inahusisha Udalali, Utathimin (Valuation), Property Management, Appraisals, property Market, Mortgage Underwriting etc...Ukitaka kujua soko vizuri unatakiwa kwanza kujua unataka Fanya real estate business katika angle gan..
 
Hii sector inahitaji akili zaidi kuliko pesa. Akili ya kuangalia value ya kiwanja, nyumba au frem ya biashara kwa miaka kama mitano au kumi ijayo.

Real estate ya Tanzania awali ya yote usiifanye ki proffessional sana. Achana na mambo mortgage, sijui ma engineer etc. Ukienda ki proffessional utashangaa nyumba ya million 30 umeijenga kwa milioni 70.

Kitu kikubwa anza wewe kama wewe hata kama una mtaji wa milion 20 soma mazingira tafuta hata vile viwanja vya 3,000,000 ingia hapo same chukua mafundi wa bei chee room moja gharama za ujenzi hata 120000 wanakufanyia. Wewe kwa kitu kama 15,000,000 unajenga room zako nne safi za biashara. Hapo ukipiga rent 70000 kwa mwezi kwa mwaka ni kama 3.3 M hizo unazuchukua paaaap unanunua uwanja mngine.

Kama umeajiriwa ukipata salary ya miezi mitatu hapo ni tofali kama 3000 mwezi wa nne ni cement na mchanga mwezi wa 5 hela ya mafundi na ujenzi unaanza.

Ki ufupi tu kama alivosema mdau hapo itakuchukua mda mpaka uje kuona matunda ya uwekezaji huo. Lakini kama upo organised na determined ndani ya miaka 6 au 7 unaweza kuwa tayar na real estate worth 100 million.

Mi kuna mahesabu ya ujenzi nnayo nikiwaambia watu unaweza jenga nyumba safi kwa m 30 watu wanabisha kabisa. Coz hivo vitu havipo kwenye fikra zao. Wao wakisikia nyumba basi mawazo yao ni M 100.

Sasa ndo ujiloge ujenge nyumba ya milioni 100 kwa mortgage halafu utegemee kuirudisha kwa kupangisha... Hahahahahh.. Mbona utaweza kuzaa na benki. Kwanza real estate haihitaji nyumba za luxury. Unaweza ku design chumba sebule choo jiko halafu uweke sokoni kwa 30 M hapo bado ni faida tu. Kwa mwaka ukiweza ku develop nyumba kama hizo simple hukosi 10 M faida kwa kila unit.

Hata Trump kuna sehem aliandika kama huna mentality ya penny pinching au cost minimization Real Estate itakuwa kitu kigumu sana. Na ndicho naona kina gharimu watu wengi mpaka kesho

So real estate ni mentality zaidi kuliko pesa

Umeongea uhalisia mwingi wa mazingira ya kiujenzi kuliko ule wa vitabuni na ulio akilini mwa wengi...safi sana
 
Real Estate Business ni pana sana sana, Watu wengi wanaongelea Real Estate Business katika Angle ya Developer(Kujenga nyumba au kununua Viwanja na Kuuza). Real State Business inahusisha Udalali, Utathimin (Valuation), Property Management, Appraisals, property Market, Mortgage Underwriting etc...Ukitaka kujua soko vizuri unatakiwa kwanza kujua unataka Fanya real estate business katika angle gan..
Mkuu nipe darasa nataka kuwa developer na udalali,je unanishauri vipi mkuu?
 
Hii sector inahitaji akili zaidi kuliko pesa. Akili ya kuangalia value ya kiwanja, nyumba au frem ya biashara kwa miaka kama mitano au kumi ijayo.

Real estate ya Tanzania awali ya yote usiifanye ki proffessional sana. Achana na mambo mortgage, sijui ma engineer etc. Ukienda ki proffessional utashangaa nyumba ya million 30 umeijenga kwa milioni 70.

Kitu kikubwa anza wewe kama wewe hata kama una mtaji wa milion 20 soma mazingira tafuta hata vile viwanja vya 3,000,000 ingia hapo same chukua mafundi wa bei chee room moja gharama za ujenzi hata 120000 wanakufanyia. Wewe kwa kitu kama 15,000,000 unajenga room zako nne safi za biashara. Hapo ukipiga rent 70000 kwa mwezi kwa mwaka ni kama 3.3 M hizo unazuchukua paaaap unanunua uwanja mngine.

Kama umeajiriwa ukipata salary ya miezi mitatu hapo ni tofali kama 3000 mwezi wa nne ni cement na mchanga mwezi wa 5 hela ya mafundi na ujenzi unaanza.

Ki ufupi tu kama alivosema mdau hapo itakuchukua mda mpaka uje kuona matunda ya uwekezaji huo. Lakini kama upo organised na determined ndani ya miaka 6 au 7 unaweza kuwa tayar na real estate worth 100 million.

Mi kuna mahesabu ya ujenzi nnayo nikiwaambia watu unaweza jenga nyumba safi kwa m 30 watu wanabisha kabisa. Coz hivo vitu havipo kwenye fikra zao. Wao wakisikia nyumba basi mawazo yao ni M 100.

Sasa ndo ujiloge ujenge nyumba ya milioni 100 kwa mortgage halafu utegemee kuirudisha kwa kupangisha... Hahahahahh.. Mbona utaweza kuzaa na benki. Kwanza real estate haihitaji nyumba za luxury. Unaweza ku design chumba sebule choo jiko halafu uweke sokoni kwa 30 M hapo bado ni faida tu. Kwa mwaka ukiweza ku develop nyumba kama hizo simple hukosi 10 M faida kwa kila unit.

Hata Trump kuna sehem aliandika kama huna mentality ya penny pinching au cost minimization Real Estate itakuwa kitu kigumu sana. Na ndicho naona kina gharimu watu wengi mpaka kesho

So real estate ni mentality zaidi kuliko pesa
Interesting..!! Sooo gud. Umeni-inspire sana. Safi
 
Mkuu nipe darasa nataka kuwa developer na udalali,je unanishauri vipi mkuu?
Mkuu as A Developer soko limeyumba tofauti na miaka miwili nyuma, Lakin ukiwa na Real estate Marketing nzuri basi unaweza uka survive kwenye soko....Udalali sio mbaya....
 
Tatizo linakuja kwenye huo mkopo kaka, maana hali halisi ni kama watakuchaji riba kubwa, kifupi hela yoyote ukichukuwa benki watataka urudishe zaidi ya labda 2.55. Namaanisha ukichukuwa mkopo sema wa 3.5m/- watataka urudishe 8.925m/=. Sasa kwa hesabu zako kama utapata kodi 4.2m/- kwa mwaka, inamaanisha itakuchukuwa miaka 2 labda na miezi 2 kurudisha mkopo wao, na hapo usitafune hiyo kodi, labda uombe kwa miaka 3.
Hela yoyote uchukuwapo kama mkopo wewe zidisha mara 2.55 utapata thamani utakayotakiwa kuwarudishia wenyewe..Kila la kheri..
utakuwa unakopaga kwa maloan shark sio bank,
hakuna bank inakukopa milioni 3.5 eti marejesho yawe milioni 8,
no way
 
utakuwa unakopaga kwa maloan shark sio bank,
hakuna bank inakukopa milioni 3.5 eti marejesho yawe milioni 8,
no way
Wewe eleza kwa kujuwa kwako utarudisha ngapi ukikopa hizo 3.5m/=??!! Wafikiri wale wako pale kukusaidia wewe ukope shs. 1 urudishe Shs. 1 au shs. 1.5?! Watalipaje mishahara kwa wafanyakazi wao, bonasi, safari, matangazo?! Tupe majibu..Maana kumbuka mabenki nayo yanakopa hizo hela!
 
Wewe eleza kwa kujuwa kwako utarudisha ngapi ukikopa hizo 3.5m/=??!! Wafikiri wale wako pale kukusaidia wewe ukope shs. 1 urudishe Shs. 1 au shs. 1.5?! Watalipaje mishahara kwa wafanyakazi wao, bonasi, safari, matangazo?! Tupe majibu..Maana kumbuka mabenki nayo yanakopa hizo hela!
Even though, lakini sio kwa hio concept yako...
 
Even though, lakini sio kwa hio concept yako...
Sawa ndio nieleze benki utarudisha shs ngapi? Hata kama pungufu ya hapo sidhani kama itakuwa hivyo, tueleze wachukuwa 3.5m/- warudisha shs?
 
Sawa ndio nieleze benki utarudisha shs ngapi? Hata kama pungufu ya hapo sidhani kama itakuwa hivyo, tueleze wachukuwa 3.5m/- warudisha shs?
haiwezi kuzidi milioni 4.5 mkuu,kwa vyovyote vile,

kurudisha milioni 8.5 ni sawa karibu interest ya 60% kitu ambacho hata kisheria huo ni wizi na haikubaliki
 
Sawa ndio nieleze benki utarudisha shs ngapi? Hata kama pungufu ya hapo sidhani kama itakuwa hivyo, tueleze wachukuwa 3.5m/- warudisha shs?
haiwezi kuzidi milioni 4.5 mkuu,kwa vyovyote vile,

kurudisha milioni 8.5 ni sawa karibu interest ya 60% kitu ambacho hata kisheria huo ni wizi na haikubaliki
 
Ni moja ya biashara nzuri zisizo na presha, ila inahitaji capital isiyo ya stress..
Mkuu Nktlogistics nashida na wewe nakutafuta kweli kama hutojali naomba uni PM sababu me nimeshindwa kukuPM nadhani sababu ya settings za privacy kwenye account yako, pindi utakaposoma reply yangu usisite kunitafuta mkuu.

Nktlogistics
 
Back
Top Bottom