Real Madrid ilipomaliza mechi bila kuwa na shot on target hata moja

Real Madrid ilipomaliza mechi bila kuwa na shot on target hata moja

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Kuna wakati unasikiliza baadhi ya watu huku mitandaoni unabaki kujiuliza hawa watu wanaujua kweli mpira au naongea na bots (kwa wasiojua bots ni mifumo ya kicomputer inayoact kama binadamu mitandaoni ikiwemo kupost comments).

Mambo mengi ambayo tunashadadia ni ya kawaida sana kwenye ulimwengu wa mpira. Timu kubwa inaweza kutandikwa goli za kutosha hadi ukashangaa. Timu ndogo sana usiyoitegemea inaweza kuifunga timu kubwa bila mtu yoyote kutarajia. Ndiyo ni mambo ya kushangaza ila yakitokea siyo mara ya kwanza na siyo ishara ya kiama!

Kuna hili limeibuka baada ya mechi ya Al Ahly Tripoli vs Simba, ambapo watu wanaonyesha kushangaa hadi wengine wanafikiria kuweka mabango kisa Simba imeshindwa kupata shot on target hata moja katika mechi nzima.

Nikiweka mfano mmoja wa haraka, ni mwaka jana tu hapo 2023 wala siyo mbali, Real Madrid akicheza nyumbani dhidi ya Barcelona walifungwa 0-1 na wakamaliza mechi bila kuwa na shot on target hata moja. Real Madrid ilikuwa full mkoko, Vinicious, Modric, Benzema, Camavinga, nk. wote ndani.

Mambo kama haya yakitokea unaweza na unaruhusiwa kushangaa ila usipitilize sana, mbona yanatokeaga sana tu? Kwanza kutokuwa na shots on target haimaanishi haukufika langoni mwa mpinzani na haimaanishi haikufanya attempt yoyote ya kufunga dakika zote 90, ni kwamba katika mashuti yote na vichwa vyote mlivyopiga hakukuwa na hata moja lililokuwa target ndani ya milingoti ile 3. Nothing more nothing less. Ukielewa hivyo wala hautawaza saaana.

Jifunzeni mpira nyie bots.
 
Kelele zinakuja wapi bro Mfano Madrid Hana on target hata moja ndiyo ila atajipanga mechi zijazo awe Bora na kuwa na on target,Simba mara kadhaa akikutana na timu Bora hasa za kaskazini changamoto hizi zinakuwa nyiingi tu kwa hio comment za watu zina msingi mzuri sana na lengo ni lile lile tuache Mpira wa makaratasi tuwe na mpira wa uwanjani
 
Kelele zinakuja wapi bro Mfano Madrid Hana on target hata moja ndiyo ila atajipanga mechi zijazo awe Bora na kuwa na on target,Simba mara kadhaa akikutana na timu Bora hasa za kaskazini changamoto hizi zinakuwa nyiingi tu kwa hio comment za watu zina msingi mzuri sana na lengo ni lile lile tuache Mpira wa makaratasi tuwe na mpira wa uwanjani
Anayecheza mpira wa makaratasi ni nani sasa? Niambie lini Simba ilishindwa kupata magoli au kufanya attempt za kutosha dhidi ya hizo timu za Kaskazini?
 
Anayecheza mpira wa makaratasi ni nani sasa? Niambie lini Simba ilishindwa kupata magoli au kufanya attempt za kutosha dhidi ya hizo timu za Kaskazini?
Ntajie mechi 3 katika Miaka Hii ya Simba inafuzu robo fainali Ambayo imeshinda dhidi ya timu za kaskazini.

Simba anacheza mpira wa makaratasi..Ukiwa Bora huhitaji nguvu kubwa kutuaminisha mambo yanaonekana TU
 
Real Madrid hawakupata shot on target mechi ya PSG ya 2019 ambayo Di Maria alifunga goli mbili mguuni na goli moja lilifungwa dakika za lala salama nakumbuka mtangazaji alisema wamecheza mechi 578 zote wamepata target hii ya 579 imekua ngumu kwao hiyo ya Barc siikumbuki mkuu emu nikumbushe maana mwaka jana karibu mechi zote barc alikua anatokea kwenye kwapa harafu wasipate target ni ngumu sana..
 
Ntajie mechi 3 katika Miaka Hii ya Simba inafuzu robo fainali Ambayo imeshinda dhidi ya timu za kaskazini.

Simba anacheza mpira wa makaratasi..Ukiwa Bora huhitaji nguvu kubwa kutuaminisha mambo yanaonekana TU
Mmeanza kuhamisha goli, mnaongea shot on target sasa hivi unahamishia kushinda robo fainali dhidi ya timu za kaskazini. Anayetumia nguvu ni nyie wazee wa propaganda, mnaozusha hoja zisizo za kimpira na kuzikomalia. Nitajie timu ambayo haipati shida dhidi ya timu hizo za kaskazini?
 
Real Madrid hawakupata shot on target mechi ya PSG ya 2019 ambayo Di Maria alifunga goli mbili mguuni na goli moja lilifungwa dakika za lala salama nakumbuka mtangazaji alisema wamecheza mechi 578 zote wamepata target hii ya 579 imekua ngumu kwao hiyo ya Barc siikumbuki mkuu emu nikumbushe maana mwaka jana karibu mechi zote barc alikua anatokea kwenye kwapa harafu wasipate target ni ngumu sana..
Sasa kama unaitaja hiyo ya PSG hauoni ndiyo unazidi kuthibitisha hoja yangu kuwa haya mambo yapo na siyo ya kuyastaajabu kihiiivyo kama bots wanavyofanya, mimi nimesema nimetoa mfano mmoja tu tena wa haraka haraka. Hiyo mechi ya Madrid vs Barcelona ilifanyika March.

Hata Man City mwaka jana hiyo hiyo alitoka bila on target. Mifano ipo mingi tukisema tuanze kuchimbua.
 
Mmeanza kuhamisha goli, mnaongea shot on target sasa hivi unahamishia kushinda robo fainali dhidi ya timu za kaskazini. Anayetumia nguvu ni nyie wazee wa propaganda, mnaozusha hoja zisizo za kimpira na kuzikomalia. Nitajie timu ambayo haipati shida dhidi ya timu hizo za kaskazini?

Mmeanza kuhamisha goli, mnaongea shot on target sasa hivi unahamishia kushinda robo fainali dhidi ya timu za kaskazini. Anayetumia nguvu ni nyie wazee wa propaganda, mnaozusha hoja zisizo za kimpira na kuzikomalia. Nitajie timu ambayo haipati shida dhidi ya timu hizo za kaskazini?
Screenshot_20240918-101640_1.jpg

Ngoja nitunze Nguvu zangu Kwa Sasa hio hapo game ya 2023 ,Simba vs Wydad Casablanca..Hakuna on target mlikuja na msemo mmekufa kiume ...Nioneshe lini Real Madrid matatizo kama haya yamejirudia back to back...Kaa chini utulie.Maana tunazungumzia Simba unahamishia Mpira nitaje timu ambazo hazishindi kaskazini naona umechanganyikiwa asee tulia
 
View attachment 3099375
Ngoja nitunze Nguvu zangu Kwa Sasa hio hapo game ya 2023 ,Simba vs Wydad Casablanca..Hakuna on target mlikuja na msemo mmekufa kiume ...Nioneshe lini Real Madrid matatizo kama haya yamejirudia back to back...Kaa chini utulie.Maana tunazungumzia Simba unahamishia Mpira nitaje timu ambazo hazishindi kaskazini naona umechanganyikiwa asee tulia
Kwani baada ya Wydad, Simba haijacheza tena na timu za kaskazini, inakuwaje unatumia maneno "matatizo hayo yamejirudia back to back" au haujui maana ya "back to back"?

Baada ya hapo Simba kamfunga Wydad 2-0 na kuwatoka mashindanoni, Simba kacheza na Al Ahly na katoa sare za magoli mechi zote mbili. Unalitafuta tatizo ambalo halipo.
 
Sijasoma haya mashudu uliyoandika ila haijastify kushindwa kupiga short on target dhidi ya waarabu huku mkishikishwa ukuta na kupelekewa moto pale Libya. 😀😀😀
 
Sijasoma haya mashudu uliyoandika ila haijastify kushindwa kupiga short on target dhidi ya waarabu huku mkishikishwa ukuta na kupelekewa moto pale Libya. 😀😀😀
Kama haujasoma unajibu ya nini sasa shoga angu?
 
Tukubali ukweli kwamba timu yetu mbovu, ilielemewa, haina mipango ya kutafuta goli na kwa mkapa hatutoki(tusiende uwanjani na matokeo yetu mfukoni)
 
Ntajie mechi 3 katika Miaka Hii ya Simba inafuzu robo fainali Ambayo imeshinda dhidi ya timu za kaskazini.

Simba anacheza mpira wa makaratasi..Ukiwa Bora huhitaji nguvu kubwa kutuaminisha mambo yanaonekana TU
Umesema mechi tatu dhidi ya timu za kaskazini,mie nakupa mechi nne, Simba kashinda mara mbili dhidi ya Wydad, 2-0 na 1-0,Simba 1 Al Ahly 0,Simba 3 JS Saura 0
 
View attachment 3099375
Ngoja nitunze Nguvu zangu Kwa Sasa hio hapo game ya 2023 ,Simba vs Wydad Casablanca..Hakuna on target mlikuja na msemo mmekufa kiume ...Nioneshe lini Real Madrid matatizo kama haya yamejirudia back to back...Kaa chini utulie.Maana tunazungumzia Simba unahamishia Mpira nitaje timu ambazo hazishindi kaskazini naona umechanganyikiwa asee tulia
🤣🤣🤣
 
Tukubali ukweli kwamba timu yetu mbovu, ilielemewa, haina mipango ya kutafuta goli na kwa mkapa hatutoki(tusiende uwanjani na matokeo yetu mfukoni)
Daaaa! MCHOME_MAPOVU kumbe hata huku upo? We kazi yako, ni kuiponda tu "timu yako" Simba tu!
 
Back
Top Bottom