Record za Yanga SC mechi tano za kimataifa nyumbani zinatisha

Record za Yanga SC mechi tano za kimataifa nyumbani zinatisha

Expensive life

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2020
Posts
2,971
Reaction score
9,437
Wananchi wana jambo lao mapema mwezi huu dhidi ya Al Hilal ya Sudan, wenyewe wanasema iwe mvua iwe jua hatoki mtu kwa Mkapa.

Licha ya hamasa kubwa waliyonayo kuelekea mchezo huo Yanga SC kwa miaka ya hivi karibuni wamekuwa na rekodi mbaya wanapocheza uwanja wa nyumbani.

Kwa ujumla viongozi na mashabiki wa Yanga SC wanashauku ya kuiona timu yao japo inafuzu hatua ya makundi barani Africa. Ili kuvuka hatua hii Yanga wanapaswa kuutumia vizuri uwanja wa nyumbani, hivyo wanapaswa kujipanga kisawasawa kwa maana timu wanayokwenda kucheza nayo inauzoefu wa kutosha kwenye michuano hii.

Hizi hapa mechi tano za kimataifa za mwisho Yanga walizocheza nyumbani.

Yanga vs Goh Mahia 0 - 3

Yanga vs Zesco United 1 - 1

Yanga vs Pyramid 1 -2

Yanga vs Rivers united 1 - 2

Yanga vs Zalan 5 - 0

Kila lakheri wananchi kuelekea mchezo ujao.

D6514696-5B40-48F0-A50E-6DCAB6B8809D.jpeg
 
Leo una lipi la kusema au ndio utakuja na hoja ya kombe la looser?
 
Back
Top Bottom