Rekodi za Umoja wa Mataifa juu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Rekodi za Umoja wa Mataifa juu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,325
Kwa mujibu wa Ibara ya 102(a) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa, kila mkataba na makubaliano yaliyofanywa na mwanachana yoyote wa Umoja wa Mataifa lazima isajiliwe na kuchapishwa na Sekretariati ya Umoja wa Mataifa. Hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni mkataba au makubaliano ya kimataifa yaliyofanywa baina ya wanachama wawili wa Umoja wa Mataifa wa wakati huo, yaani Tanganyika na Zanzibar kuwa nchi moja. Kwa maana hiyo basi, Hati ya Muungano ilitakiwa isajiliwe na kuchapishwa na Sekretariati ya Umoja wa Mataifa kwa mujibu wa Ibara ya 102(a) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa.

Umoja wa Maraifa ina kitu kinaitwa UN Treaty Collection ambapo mikataba na makubaliano yote ya kimaitaifa huifadhiwa na kuchapishwa. Taarifa
zinazohusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zinapatikana kwenye Document A/5701 ya May 18, 1964. Document hiyo ina barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenda kwa wawakilishi wa kudumu wa wanachama wa Umoja wa Mataifa akiwataarifu kupata "note" kutoka kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuhusiana na kuanzishwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar chini ya Rais Mwalimu Nyerere.

Katika barua hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aliambatanisha barua kutoka kwa Waziri wa Mambo ya nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ya tarehe May 6, 1964 ikimtaarifu Katibu wa Umoja wa Mataifa kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana tarehe 26/04/1964 na kuwa nchi moja baada ya kusaini Hati ya Muungano (Articles Union). Nimeambatanisha D
ocument A/5701 hapo chini. Pia waweza kuisoma hapa: http://ask.un.org/data/answers/files/178094/A5701-E.pdf

Ukisoma hiyo document hakuna sehemu yoyote inayosema kuwa katika barua yake, Waziri aliambatanisha Hati ya Muungano. Kama aliambatananisha Hati ya Muungano hata kama ni feki lazima ingeambatanishwa kwenye Document A/5701 kama barua ya Waziri ilivyoambatatishwa. Maandishi mengine ya Umoja wa Mataifa kuhusu historia ya Tanzania, yanasema kuwa katika mawasiliano mengine yaliyofanywa na Ubalozi wa Kudumu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar November 2, 1964, kwenda kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa yalimtaarifu kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar itajulikana kama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baada Serikali ya Jamhuri ya Muungano ilimwandikia Katibu wa Umoja wa Mataifa ikimtaarifu kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuheshimu mikataba iliyosainiwa na kwa niaba ya Tanganyika: https://treaties.un.org/Pages/HistoricalInfo.aspx?#"United Republic of Tanzania"

It is questionable kama Hati ya Muungano iliwasilishwa au itawasilishwa lini mbele ya Sekretatiati ya Umoja wa Mataifa ili isajiliwe na kuchapishwa kwa mujibu wa Ibara ya 102(1) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Maana kama ilishawasilishwa lazima ingechapishwa na kuonekana kwenye UN Treaty Collection.
Nini matokeo ya kisheria kwa kutosajiliwa na kuchapishwa kwa Hati ya Muungano na Secretariati ya Umoja wa Mataifa?

Ibara ya 102(b) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa inasema kuwa nchi iliyoingia kwenye mkataba or makubaliano ya kimataifa haitaweza kuutumia mkataba au makubaliano hayo mbele ya chombo chochote za Umoja wa Mataifa mpaka hapo huo mkataba au makubaliano yatakapokuwa yamesajiliwa na kuchapishwa na Secretariati ya Umoja wa Mataifa.

Article 102 of the UN Charter

(1) Every treaty and every international agreement entered into by any Member of the United Nations after the present Charter comes into force shall as soon as possible be registered with the Secretariat and published by it.

(2) No party to any such treaty or international agreement which has not been registered in accordance with the provisions of paragraph 1 of this Article may invoke that treaty or agreement before any organ of the United Nations.
 
Watetezi wa Muungano ni Wasaka Tonge......wala usijisumbue nao.....
 
Kama walijua watanzania bado hatufatili mambo sasa imekula kwao!!!watu wanachimba mambo na kuja na full data na maelezo ya kutosha.
 
EMT

Are we as good as non-members at the UN then when it comes to this matter?

How did the UN allow the Zanzibari and Tanganyikan seats to be dissolved and their places to be taken by Tanzania without proper documentation?
 
Last edited by a moderator:
Kwa mujibu wa Ibara ya 102(a) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa, kila mkataba na makubaliano yaliyofanywa na mwanachana yoyote wa Umoja wa Mataifa lazima isajiliwe na kuchapishwa na Sekretariati ya Umoja wa Mataifa. Hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni mkataba au makubaliano ya kimataifa yaliyofanywa baina ya wanachama wawili wa Umoja wa Mataifa wa wakati huo, yaani Tanganyika na Zanzibar kuwa nchi moja. Kwa maana hiyo basi, Hati ya Muungano ilitakiwa isajiliwe na kuchapishwa na Sekretariati ya Umoja wa Mataifa kwa mujibu wa Ibara ya 102(a) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa.

Umoja wa Maraifa ina kitu kinaitwa UN Treaty Collection ambapo mikataba na makubaliano yote ya kimaitaifa huifadhiwa na kuchapishwa. Taarifa
zinazohusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zinapatikana kwenye Document A/5701 ya May 18, 1964. Document hiyo ina barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenda kwa wawakilishi wa kudumu wa wanachama wa Umoja wa Mataifa akiwataarifu kupata "note" kutoka kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuhusiana na kuanzishwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar chini ya Rais Mwalimu Nyerere.

Katika barua hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aliambatanisha barua kutoka kwa Waziri wa Mambo ya nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ya tarehe May 6, 1964 ikimtaarifu Katibu wa Umoja wa Mataifa kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana tarehe 26/04/1964 na kuwa nchi moja baada ya kusaini Hati ya Muungano (Articles Union). Nimeambatanisha D
ocument A/5701 hapo chini. Pia waweza kuisoma hapa: http://ask.un.org/data/answers/files/178094/A5701-E.pdf

Ukisoma hiyo document hakuna sehemu yoyote inayosema kuwa katika barua yake, Waziri aliambatanisha Hati ya Muungano. Kama aliambatananisha Hati ya Muungano hata kama ni feki lazima ingeambatanishwa kwenye Document A/5701 kama barua ya Waziri ilivyoambatatishwa. Maandishi mengine ya Umoja wa Mataifa kuhusu historia ya Tanzania, yanasema kuwa katika mawasiliano mengine yaliyofanywa na Ubalozi wa Kudumu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar November 2, 1964, kwenda kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa yalimtaarifu kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar itajulikana kama Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baada Serikali ya Jamhuri ya Muungano ilimwandikia Katibu wa Umoja wa Mataifa ikimtaarifu kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuheshimu mikataba iliyosainiwa na kwa niaba ya Tanganyika: https://treaties.un.org/Pages/HistoricalInfo.aspx?#"United Republic of Tanzania"

It is questionable kama Hati ya Muungano iliwasilishwa au itawasilishwa lini mbele ya Sekretatiati ya Umoja wa Mataifa ili isajiliwe na kuchapishwa kwa mujibu wa Ibara ya 102(1) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Maana kama ilishawasilishwa lazima ingechapishwa na kuonekana kwenye UN Treaty Collection.
Nini matokeo ya kisheria kwa kutosajiliwa na kuchapishwa kwa Hati ya Muungano na Secretariati ya Umoja wa Mataifa?

Ibara ya 102(b) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa inasema kuwa nchi iliyoingia kwenye mkataba or makubaliano ya kimataifa haitaweza kuutumia mkataba au makubaliano hayo mbele ya chombo chochote za Umoja wa Mataifa mpaka hapo huo mkataba au makubaliano yatakapokuwa yamesajiliwa na kuchapishwa na Secretariati ya Umoja wa Mataifa.

Article 102 of the UN Charter

(1) Every treaty and every international agreement entered into by any Member of the United Nations after the present Charter comes into force shall as soon as possible be registered with the Secretariat and published by it.

(2) No party to any such treaty or international agreement which has not been registered in accordance with the provisions of paragraph 1 of this Article may invoke that treaty or agreement before any organ of the United Nations.

Kama kweli kuna makosa hayo basi wa kwanza kulaumiwa ni UN wenyewe ambao wameshindwa kusimamia taratibu hizo na kuiruhus serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupata haki zote za uanachama huku ikiwa haijatimiza masharti.

lakini pia mkataba unaweza kupata uhalali kwa vitendo contract by conduct,kwa kipindi chote hicho cha 50yrs watanzania wamekuwa waki exercise mambo mengi ambayo yameanishwa katika mkataba ule wa muungano, kwa kwa dhamira zilizodhihilika kwa vitendo hiyo inatafsiriwa kama mkataba halali.

Jambo jingine mimi sijawahi sikia kwamba kule UN kuna tatizo la soveregnity ya jamhuri ya muungano wa Tanzania hii tafsiri yake ni kwamba Jamhuri ya muungano wa Tanzania ni halali mbele ya UN kama sio halali pangekuwa na tatizo hilo la soveregnity.
 
Baadhi ya maandiko ya A.Babu juu ya muungano ni msukumo wa MAREKANI WAKAIHOFIA COLD WAR. Hivyo inawezekana kabisa lobbying ya USA ilipelekea recognition at good intention kuwa procedures zingeendelea.
 
Jambo jingine mimi sijawahi sikia kwamba kule UN kuna tatizo la soveregnity ya jamhuri ya muungano wa Tanzania hii tafsiri yake ni kwamba Jamhuri ya muungano wa Tanzania ni halali mbele ya UN kama sio halali pangekuwa na tatizo hilo la soveregnity.

Ibara ya 102 haihusiani au haidhuru sovereignty kisa hiyo hati kutosajiliwa. Soma tena hiyo Ibara.
 
EMT

Bungeni Waziri wa Mambo ya Nje Mh. Membe kasema hati ilipelekwa UN hiyo 1964
 
Last edited by a moderator:
EMT

Bungeni Waziri wa Mambo ya Nje Mh. Membe kasema hati ilipelekwa UN hiyo 1964

Mbona haonekekani kwenye rekodi za Umoja wa Mataifa?

Au Umoja wa Mataifa waliambiwa wasichapishe hiyo hati kwa vile ni ya siri?
 
EMT

Are we as good as non-members at the UN then when it comes to this matter?

How did the UN allow the Zanzibari and Tanganyikan seats to be dissolved and their places to be taken by Tanzania without proper documentation?

Kwa mujibu wa Bei Mbaya, Waziri wa Mambo ya Nje kasema Bungeni kuwa hati ilipelekwa UN tokea 1964.
 
Last edited by a moderator:
Katika nchi hii Kuna mambo mengi yanahitajika yawe wazi angalau kidogo tu, kwanini UN ilikubali sheria yake ivunjwe??
 
Mbona haonekekani kwenye rekodi za Umoja wa Mataifa?

Au Umoja wa Mataifa waliambiwa wasichapishe hiyo hati kwa vile ni ya siri?

Ndio sintofaham kwani sifaham kwa utaratibu wa UN ni mikataba ipi confidential na ipi sio?

Mheshmiwa maelezo yake yaliishia hapo zaidi ilikuwa kutia hofu watu kupitia historia ati Soviet Union na shirikisho la ujerumani yamevunjika sababu ya muundo.
Na hata Catalunya inayoingiza mapato mengi ya utalii imenyimwa mamlaka kamili na Spain sababu muundo utapelekea kujitenga
 
Wengi mnafanya kosa moja kubwa sana la kimantiki; inapaswa kujiuliza: Je, ni kwanini Umoja wa Mataifa ulikubali kuitambua nchi ya Tanzania badala ya Tanganyika na Zanzibar? Je barua tu tena toka kwa Waziri wa Mambo ya Nje yatosha kufuta uanachama wa nchi nyingine (Zanzibar)? Kweli mnataka tuamini au watu waamini kuwa UM umetuma barua ya kutambulisha Muungano wa Tanzania kwa nchi nyingine kwa sababu ya barua moja tu ya utambulisho? seriously?

Ni kitu gani kilifanya UM wakubali kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni halali kimataifa? Hili mnatakiwa kulijibu na mahali pa kupata jibu ni UM.
 
Asante sana mkuu EMT hakika umetoa ufafanuzi unaojitosheleza hasa. Kwa hiyo iwapo utaibuka mgogoro wa muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar international law itazitreat kama nchi mbili tofauti maana Hati ya Muungano haikusajiliwa UN? Naomba ufafanuzi wako wa kisheria mkuu EMT.

Kama nilivyoandika hapo juu, Ibara ya 102(b) ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa inasema wazi kuwa nchi iliyoingia kwenye mkataba or makubaliano ya kimataifa haitaweza kuutumia mkataba au makubaliano hayo mbele ya chombo chochote za Umoja wa Mataifa mpaka hapo huo mkataba au makubaliano yatakapokuwa yamesajiliwa na kuchapishwa na Secretariati ya Umoja wa Mataifa.

Hivyo basi, kinadharia mtu anaweza kusema kuwa
kama ikitokea malumbano baina ya pande mbili zilizotia saini hati ya Muungano halafu upande mmoja ukataka ku-rely kwenye hiyo hati mbele ya chombo chochote cha UN, upande wa pili unaweza ku-argue kuwa hiyo hati ya Muungano cannot be relied upon by the other party before the UN because it has not be registered by the UN Secretariat in accordance with Article 102(1) of the UN Charter.
 
Tumefuatilia kuhusu kiti cha UN cha Zanzibar na matatizo yapo kwa watawala wetu. Wakiamua kwenda UN hapo hapo tunapewa nafasi yetu ndio maana CCM wameshikilia kwa njia yeyote ile wapinzani wasitawale Z'bar.
 
Wengi mnafanya kosa moja kubwa sana la kimantiki; inapaswa kujiuliza: Je, ni kwanini Umoja wa Mataifa ulikubali kuitambua nchi ya Tanzania badala ya Tanganyika na Zanzibar? Je barua tu tena toka kwa Waziri wa Mambo ya Nje yatosha kufuta uanachama wa nchi nyingine (Zanzibar)? Kweli mnataka tuamini au watu waamini kuwa UM umetuma barua ya kutambulisha Muungano wa Tanzania kwa nchi nyingine kwa sababu ya barua moja tu ya utambulisho? seriously?

Ni kitu gani kilifanya UM wakubali kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni halali kimataifa? Hili mnatakiwa kulijibu na mahali pa kupata jibu ni UM.

Kwa kuwa muungano ulikuwa wa maslahi ya wakubwa kuna uwezekano mkubwa pia some assistance of smooth registration big fish pia!!! Maana hawezekani UN wakaacha tu hivi hivi, hata kama vigezo vingine vilikuwa vipo! Naanza kuamini kuwa kuna mambo yalifanywa kwa makosa na kwa kujulikana ili kuficha essence ya muungani wenyewe!!

Kama tunataka kuanza vyema na kwa kuwa hakuna mtu yuko tayari kushudia dola zaTanganyika na Zanzibar peke yake kwanza kabla ya kujadili muungano, tuache urongo na tuanze vyema!!
 
Apart from other issue related to URT Union saga, We have to establish why, the article of Union was not registered by UN Secretariat...
 
Apart from other issue related to URT Union saga, We have to establish why, the article of Union was not registered by UN Secretariat...

Nauliza hivi: Je, Umoja wa Mataifa wameulizwa rasmi na Mamlaka wanayoitambua, kwa mfano Ikulu, Mambo ya Nje, Balozi wa TZ huko UN, Minister Plenipotentiary with Full Powers kwa maandishi na wakakana?
 
Back
Top Bottom