Rest In Peace/Requiescat in pace/R.I.P Maana yake ni nini? Je Kuna ulazima wowote kutumia neno hili?

Rest In Peace/Requiescat in pace/R.I.P Maana yake ni nini? Je Kuna ulazima wowote kutumia neno hili?

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2011
Posts
3,763
Reaction score
5,607
Hili ni nino lililojichukulia umaarufu mkubwa Duniani. R.I.P ni neno ambalo japo mzizi wake ni kwenye madhahebu ya kikristo maarufu lipo katika lugha za nchi nyingi mbalimbali duniani bila kujali dini wala muelekeo wa imani. Na wakati mwingine linatumiwa na hata wasiomuamini Mungu.

Mfano;
1:Urusi ( Покойся с миром )
2: Waarabu (Orqod fi salaam)
3:Wachina (Ān xī, )
4:Wakorea (Samga goinui myeongbogeul bimnida)
........ na wengine wengi nafasi haitoshi.

HISTORIA YA FUPI YA R.I.P.
R.I.P sio neno lililoanza leo, historia inaonyesha limeanza kutumiaka toka karne ya 8. . R.I.P ilianza kushamiri kwenye makaburi hasa ya wakristo na kuanza kutumika kama salamu ya kumuombea heri marehemu karne ya 18. Changamoto ikaja kuwa hakukua na ushahidi wowote wakujitosheleza kuamini kuwa Kuna roho inaenda sehemu ambayo inauwezekano isiwe na amani kwa hiyo inahitaji kutakiwa amani huko iendako. Muda mwingi kabla ya salamu hii ulielekezwa kuwapa pole wafiwa na kuwapa matumaini ipo siku yote haya yataisha.

Maswali kadhaa yanaibuka kuhusu heri/salamu hii anayotakiwa Marehemu.
1: Je kuna ushahidi wa kutosha nje ya imani kuhusu uhalali wa salamu/heri hii, au salamu/heri hii huwa inamfikia mlengwa?

2:Je, Kwa watu ambao hawaamini uwepo wa maisha baada ya kifo, kuna ulazima wa hii salamu?
3:Kuna uwezekano au uhakika wowote kuwa salamu au heri hii inamnufaisha mlengwa?

4:Kama salamu/heri hii ilianzishwa na imani moja ya dini, nini kilisababisha itapakae dunia nzima kwa watu wa imani nyingi zinazopingana?

5: Je dunia inaneno moja katika mazingira kama haya litakalokubalika na watu wote, wa imani zote na wasio na imani yoyote?

5:Ni njia ipi bora kama hii ikioneka haikidhi viwango vyako vya imani au kama hauamini Mungu itakayofaa katika mazingira ya kuondokewa na wenzetu?



Najaribu kuwaza,........
Nini maoni yako
 
Yapo mambo mengi sana binadamu tunayafanya kwasababu tu tunadhani yana kheri au uzuri fulani japokuwa kimsingi tunakuwa hatuna sababu za msingi.Miongoni mwa mambo hayo ni hili.Binadamu tunafikiria kuwa,nje ya dini,mtu anapoondokewa na uhai kuna mahali anakwenda na imani hii inapaliliwa mizizi sana na imani kuwa mtru anapoondokewa na uhai huo kuna mahali anakwenda kwa maana ya roho yake......

Sitaki kusema kuwa kuna ukweli kwenye suala hili la roho kwenda mahali au hakuna maana hii ni mada nyingine kabisa lakini, kimsingi imani ya mahali ambapo roho ya mtu inakwenda ndiyo msingi mkubwa sana wa jambo hili au salamu au "aina hii ya kumuaga au kumtakia kheri" mwenzetu anapoondokewa na uhai.....

Ni jambo gumu sana kujua kama kweli salamu hii inamfikia mlengwa kwasababu kujua kama inamfikia ni kuthibitisha kuna mahali anakwenda.Kwakuwa hatuwezi kuthibitisha kuhusu mahali alipo [kumbuka hapa naandika haya nje ya imani ya kidini] basi inakuwa ngumu sana kujua hilo.....

Msingi wa salam hii ni kama nilivyosema kuwa ni kutakiana kheri huko aendako,kama mtu haamini katika imani ya dini haimaanishi kuwa haamini kuwa mtu anapokufa "anapumzika",kwa maana hii bado salamu au neno hili akalitumia......

Inawezekana kuwa salam hii ilianzishwa na ikani fulani ya kidini lakini sidhani kama inazuia wengine kuitumia....

Nadhani neno hili limeshakubalika na wengine pia hivyo sioni shida likatumika kwa wote liwe lina maana halisi au iwe ni hali tu ya kujifariji......

Kwangu mimi siamini kama salamu hii inaweza kubadilisha chochote kwa mlengwa isipokuwa tu anayeweza kubadili aendako ni mhusika mwenyewe.Hili ni sawa na ajali,ajali huwa hizuiliwi wakati imeshatokea bali kabla ya kutokea,kwa maana hiyo ni vyema tukajiandalia mahali pa kwenda wakati tukiwa hai kuliko kusubiri wakati ambao hatuwezi kubadili matokeo.....
 
Mimi ni mwanazuoni wa Taalimungu(Theology) naomba kuchangia uelewa kidogo. Kihistoria jambo hili ni gumu sana na ni moja ya sababu iliyomfanya Martin Luther kuanzisha Imani ya Kiprotestanti baada ya kuishutumu Kanisa Katoliki na mafundisho yake.

Imani ya Kanisa Katoliki inafundisha kwamba roho inapotengana na mwili kwa wengine "kufa", huwa ina sehemu 3 za kwenda, mbinguni, motoni, au toharani. Hii sehemu ya 3 ndio inaleta ubishani sana. Kanisa ueleza kwamba kuna baadhi ya watu kutokana na maisha yao hapa duniani roho zao haziwezi kwenda mbinguni moja kwa moja au motoni moja kwa moja. Hawana mema sana ya kurithi mbingu wala mabaya mno ya kuwastahili moto. Roho hizi hukaa toharani. Wahusika hawana tena uwezo wakubadili hali za roho zao. Ndio hapa sasa waamini walioko bado duniani ualikwa kwa sala na sadaka zao kuziombea roho za marehemu waliko toharani, lupitia sala na sadaka, roho hizo hutakaswa na kupokelewa mbinguni.

Kama nilivyotangulia kusema jambo hili hubishaniwa sana na wanazuoni ambao sio wakatoliki. Wakatoliki wana msingi gani wa kuamini hivi? soma Maandiko Matakatifu kitabu cha Makabayo 2 sura ya 12. Nasisitiza soma Maandiko Matakatifu na sio Biblia kwa sababu Biblia zote isipokuwa ya Wakatoliki haina hichi kitabu. Ilikuwaje Martin Luther aliviondoa baadhi ya vitabu kutoka katika orodha ya Maandiko Matakatifu. Kwa ufupi Biblia zote wa Waprotestanti zina vitabu 66 badala ya 72(Somo linguine refu)

Wakati Vatikani inashambuliwa na maadui waliamua kujenga ukuta upo mpaka leo kuzunguka makao makuu ya kanisa. Walihimiza wakatoliki wote kutoa pesa, na kadiri pesa zilivyokuwa zinatolewa na waamini kadiri hiyo hiyo roho zilikuwa zinatolewa motoni. Huenda ilikuwa ni kweli au ni mbinu tu ya kupata ya pesa( Mimi sio hakimu)

Mpaka leo kanisa katoliki lina utaratibu wa kuhadhimisha misa kwa ajili ya marehemu - Requiem Mass, ndio msingi wa neon Requiscat in Pace, roho ya marehemu huombewa heri na pumziko la Amani.

Bado kuna maswali kadhaa: Je waamini hufahamu vipi kama roho za marehemu wao ziko mbinguni, motoni au toharani. Kimsingi, zile za mbinguni na motoni haziombewi. Hakuna mwenye hakika na roho ya mtu yeyote iliyoko motoni kwa sbb hiyo ni kazi ya Mungu, sisi sio wa kutoa hukumu. Inakuwaje sasa kama naiombea roho ambayo tayari iko mbinguni, kanisa hufundishakwamba, katika hali hiyo, sala na sadaka hiyo itazifaa roho nyingine zilizoko toharani, au hata na wewe mwombaji mwneyewe ambae bado huko hai.

Kwa kumalizia, kanisa lina waamini wa aina tatu, kanisa la mbinguni, kanisa la washindi eg watakatifu. Kanisa la wateswa, roho zilizoko toharani, kanisa la wasafiri, sisi ambao bado tuko duniani.

Kanisa limeweka mwezi Novemba, ni mwezi maalumu wa kuwaombea marehemu.
 
Hakuna kitu hapo ukifa umekufa tu sawa na mbwa, kuku au bata anavyokufa....!!!! Labda Mungu aje adhibitishe kilicho nyuma ya mtu akifa.....vinginevyo ukifa unakuwa tu mzoga Wa kawaida...et mahali pema peponi ...huu ujinga kweli
 
Mimi ni mwanazuoni wa Taalimungu(Theology) naomba kuchangia uelewa kidogo. Kihistoria jambo hili ni gumu sana na ni moja ya sababu iliyomfanya Martin Luther kuanzisha Imani ya Kiprotestanti baada ya kuishutumu Kanisa Katoliki na mafundisho yake.

Imani ya Kanisa Katoliki inafundisha kwamba roho inapotengana na mwili kwa wengine "kufa", huwa ina sehemu 3 za kwenda, mbinguni, motoni, au toharani. Hii sehemu ya 3 ndio inaleta ubishani sana. Kanisa ueleza kwamba kuna baadhi ya watu kutokana na maisha yao hapa duniani roho zao haziwezi kwenda mbinguni moja kwa moja au motoni moja kwa moja. Hawana mema sana ya kurithi mbingu wala mabaya mno ya kuwastahili moto. Roho hizi hukaa toharani. Wahusika hawana tena uwezo wakubadili hali za roho zao. Ndio hapa sasa waamini walioko bado duniani ualikwa kwa sala na sadaka zao kuziombea roho za marehemu waliko toharani, lupitia sala na sadaka, roho hizo hutakaswa na kupokelewa mbinguni.

Kama nilivyotangulia kusema jambo hili hubishaniwa sana na wanazuoni ambao sio wakatoliki. Wakatoliki wana msingi gani wa kuamini hivi? soma Maandiko Matakatifu kitabu cha Makabayo 2 sura ya 12. Nasisitiza soma Maandiko Matakatifu na sio Biblia kwa sababu Biblia zote isipokuwa ya Wakatoliki haina hichi kitabu. Ilikuwaje Martin Luther aliviondoa baadhi ya vitabu kutoka katika orodha ya Maandiko Matakatifu. Kwa ufupi Biblia zote wa Waprotestanti zina vitabu 66 badala ya 72(Somo linguine refu)

Wakati Vatikani inashambuliwa na maadui waliamua kujenga ukuta upo mpaka leo kuzunguka makao makuu ya kanisa. Walihimiza wakatoliki wote kutoa pesa, na kadiri pesa zilivyokuwa zinatolewa na waamini kadiri hiyo hiyo roho zilikuwa zinatolewa motoni. Huenda ilikuwa ni kweli au ni mbinu tu ya kupata ya pesa( Mimi sio hakimu)

Mpaka leo kanisa katoliki lina utaratibu wa kuhadhimisha misa kwa ajili ya marehemu - Requiem Mass, ndio msingi wa neon Requiscat in Pace, roho ya marehemu huombewa heri na pumziko la Amani.

Bado kuna maswali kadhaa: Je waamini hufahamu vipi kama roho za marehemu wao ziko mbinguni, motoni au toharani. Kimsingi, zile za mbinguni na motoni haziombewi. Hakuna mwenye hakika na roho ya mtu yeyote iliyoko motoni kwa sbb hiyo ni kazi ya Mungu, sisi sio wa kutoa hukumu. Inakuwaje sasa kama naiombea roho ambayo tayari iko mbinguni, kanisa hufundishakwamba, katika hali hiyo, sala na sadaka hiyo itazifaa roho nyingine zilizoko toharani, au hata na wewe mwombaji mwneyewe ambae bado huko hai.

Kwa kumalizia, kanisa lina waamini wa aina tatu, kanisa la mbinguni, kanisa la washindi eg watakatifu. Kanisa la wateswa, roho zilizoko toharani, kanisa la wasafiri, sisi ambao bado tuko duniani.

Kanisa limeweka mwezi Novemba, ni mwezi maalumu wa kuwaombea marehemu.
Mkulu kwanza nakushukuru kwa kuniongezea msamiati TAALIMUNGU. Huu nimeuchukua mzimamzima.
Kwa hiyo, orgin ya Hilo fundisho inawalakini. Kwa nini dunia nzima wanasiasa, na watu wa kada mbalimbali wanatumia msemo huu bila kuhoji? Hukumu ya mwisho inamaana gani kama Kuna watu wanateswa kunzia Sasa kabla ya kiyama general judgement of mankind. Huoni kama Mungu anafanya unfair judgement? Mtazamo wangu.
 
Hili ni nino lililojichukulia umaarufu mkubwa Duniani. R.I.P ni neno ambalo japo mzizi wake ni kwenye madhahebu ya kikristo maarufu lipo katika lugha za nchi nyingi mbalimbali duniani bila kujali dini wala muelekeo wa imani. Na wakati mwingine linatumiwa na hata wasiomuamini Mungu.

Mfano;
1:Urusi ( Покойся с миром )
2: Waarabu (Orqod fi salaam)
3:Wachina (Ān xī, )
4:Wakorea (Samga goinui myeongbogeul bimnida)
........ na wengine wengi nafasi haitoshi.

HISTORIA YA FUPI YA R.I.P.
R.I.P sio neno lililoanza leo, historia inaonyesha limeanza kutumiaka toka karne ya 8. . R.I.P ilianza kushamiri kwenye makaburi hasa ya wakristo na kuanza kutumika kama salamu ya kumuombea heri marehemu karne ya 18. Changamoto ikaja kuwa hakukua na ushahidi wowote wakujitosheleza kuamini kuwa Kuna roho inaenda sehemu ambayo inauwezekano isiwe na amani kwa hiyo inahitaji kutakiwa amani huko iendako. Muda mwingi kabla ya salamu hii ulielekezwa kuwapa pole wafiwa na kuwapa matumaini ipo siku yote haya yataisha.

Maswali kadhaa yanaibuka kuhusu heri/salamu hii anayotakiwa Marehemu.
1: Je kuna ushahidi wa kutosha nje ya imani kuhusu uhalali wa salamu/heri hii, au salamu/heri hii huwa inamfikia mlengwa?

2:Je, Kwa watu ambao hawaamini uwepo wa maisha baada ya kifo, kuna ulazima wa hii salamu?
3:Kuna uwezekano au uhakika wowote kuwa salamu au heri hii inamnufaisha mlengwa?

4:Kama salamu/heri hii ilianzishwa na imani moja ya dini, nini kilisababisha itapakae dunia nzima kwa watu wa imani nyingi zinazopingana?

5: Je dunia inaneno moja katika mazingira kama haya litakalokubalika na watu wote, wa imani zote na wasio na imani yoyote?

5:Ni njia ipi bora kama hii ikioneka haikidhi viwango vyako vya imani au kama hauamini Mungu itakayofaa katika mazingira ya kuondokewa na wenzetu?



Najaribu kuwaza,........
Nini maoni yako
Huku ukijaribu kuwaza, kwa heshima naomba nami uniruhusu kuwaza mambo yafuatayo:

1. Fikra hizi na mfuatano huu wa kufikiri (mfuatano unaumuhimu kuliko fikra) na kwa tafsiri zako ni wa kuzaliwa au wa kujijongesha mwenyewe au vyote viwili!!.

2... Nafikiri nisubiri majibu ya kufikiri kwako. Asante kiongozi. I'm inspired.
 
Hili ni nino lililojichukulia umaarufu mkubwa Duniani. R.I.P ni neno ambalo japo mzizi wake ni kwenye madhahebu ya kikristo maarufu lipo katika lugha za nchi nyingi mbalimbali duniani bila kujali dini wala muelekeo wa imani. Na wakati mwingine linatumiwa na hata wasiomuamini Mungu.

Mfano;
1:Urusi ( Покойся с миром )
2: Waarabu (Orqod fi salaam)
3:Wachina (Ān xī, )
4:Wakorea (Samga goinui myeongbogeul bimnida)
........ na wengine wengi nafasi haitoshi.

HISTORIA YA FUPI YA R.I.P.
R.I.P sio neno lililoanza leo, historia inaonyesha limeanza kutumiaka toka karne ya 8. . R.I.P ilianza kushamiri kwenye makaburi hasa ya wakristo na kuanza kutumika kama salamu ya kumuombea heri marehemu karne ya 18. Changamoto ikaja kuwa hakukua na ushahidi wowote wakujitosheleza kuamini kuwa Kuna roho inaenda sehemu ambayo inauwezekano isiwe na amani kwa hiyo inahitaji kutakiwa amani huko iendako. Muda mwingi kabla ya salamu hii ulielekezwa kuwapa pole wafiwa na kuwapa matumaini ipo siku yote haya yataisha.

Maswali kadhaa yanaibuka kuhusu heri/salamu hii anayotakiwa Marehemu.
1: Je kuna ushahidi wa kutosha nje ya imani kuhusu uhalali wa salamu/heri hii, au salamu/heri hii huwa inamfikia mlengwa?

2:Je, Kwa watu ambao hawaamini uwepo wa maisha baada ya kifo, kuna ulazima wa hii salamu?
3:Kuna uwezekano au uhakika wowote kuwa salamu au heri hii inamnufaisha mlengwa?

4:Kama salamu/heri hii ilianzishwa na imani moja ya dini, nini kilisababisha itapakae dunia nzima kwa watu wa imani nyingi zinazopingana?

5: Je dunia inaneno moja katika mazingira kama haya litakalokubalika na watu wote, wa imani zote na wasio na imani yoyote?

5:Ni njia ipi bora kama hii ikioneka haikidhi viwango vyako vya imani au kama hauamini Mungu itakayofaa katika mazingira ya kuondokewa na wenzetu?



Najaribu kuwaza,........
Nini maoni yako
R.I.P. Hutumika tu kufarijiana kwa kutakia mema mtu ambaye amefariki. Kimantiki halina uzito wowote wa kumfanya kweli huyo mtu abadilishiwe kile kinachomstahili. Maisha yetu na mahusiano yetu na Mungu ndicho cha muhimu zaidi kwa umilele wetu. Kama R.I.P. ina uwezo unaofikirika basi kuzimu kutakuwa kweupe kabisa (hakutakuwa na wahanga wa huko).
 
Mimi ni mwanazuoni wa Taalimungu(Theology) naomba kuchangia uelewa kidogo. Kihistoria jambo hili ni gumu sana na ni moja ya sababu iliyomfanya Martin Luther kuanzisha Imani ya Kiprotestanti baada ya kuishutumu Kanisa Katoliki na mafundisho yake.

Imani ya Kanisa Katoliki inafundisha kwamba roho inapotengana na mwili kwa wengine "kufa", huwa ina sehemu 3 za kwenda, mbinguni, motoni, au toharani. Hii sehemu ya 3 ndio inaleta ubishani sana. Kanisa ueleza kwamba kuna baadhi ya watu kutokana na maisha yao hapa duniani roho zao haziwezi kwenda mbinguni moja kwa moja au motoni moja kwa moja. Hawana mema sana ya kurithi mbingu wala mabaya mno ya kuwastahili moto. Roho hizi hukaa toharani. Wahusika hawana tena uwezo wakubadili hali za roho zao. Ndio hapa sasa waamini walioko bado duniani ualikwa kwa sala na sadaka zao kuziombea roho za marehemu waliko toharani, lupitia sala na sadaka, roho hizo hutakaswa na kupokelewa mbinguni.

Kama nilivyotangulia kusema jambo hili hubishaniwa sana na wanazuoni ambao sio wakatoliki. Wakatoliki wana msingi gani wa kuamini hivi? soma Maandiko Matakatifu kitabu cha Makabayo 2 sura ya 12. Nasisitiza soma Maandiko Matakatifu na sio Biblia kwa sababu Biblia zote isipokuwa ya Wakatoliki haina hichi kitabu. Ilikuwaje Martin Luther aliviondoa baadhi ya vitabu kutoka katika orodha ya Maandiko Matakatifu. Kwa ufupi Biblia zote wa Waprotestanti zina vitabu 66 badala ya 72(Somo linguine refu)

Wakati Vatikani inashambuliwa na maadui waliamua kujenga ukuta upo mpaka leo kuzunguka makao makuu ya kanisa. Walihimiza wakatoliki wote kutoa pesa, na kadiri pesa zilivyokuwa zinatolewa na waamini kadiri hiyo hiyo roho zilikuwa zinatolewa motoni. Huenda ilikuwa ni kweli au ni mbinu tu ya kupata ya pesa( Mimi sio hakimu)

Mpaka leo kanisa katoliki lina utaratibu wa kuhadhimisha misa kwa ajili ya marehemu - Requiem Mass, ndio msingi wa neon Requiscat in Pace, roho ya marehemu huombewa heri na pumziko la Amani.

Bado kuna maswali kadhaa: Je waamini hufahamu vipi kama roho za marehemu wao ziko mbinguni, motoni au toharani. Kimsingi, zile za mbinguni na motoni haziombewi. Hakuna mwenye hakika na roho ya mtu yeyote iliyoko motoni kwa sbb hiyo ni kazi ya Mungu, sisi sio wa kutoa hukumu. Inakuwaje sasa kama naiombea roho ambayo tayari iko mbinguni, kanisa hufundishakwamba, katika hali hiyo, sala na sadaka hiyo itazifaa roho nyingine zilizoko toharani, au hata na wewe mwombaji mwneyewe ambae bado huko hai.

Kwa kumalizia, kanisa lina waamini wa aina tatu, kanisa la mbinguni, kanisa la washindi eg watakatifu. Kanisa la wateswa, roho zilizoko toharani, kanisa la wasafiri, sisi ambao bado tuko duniani.

Kanisa limeweka mwezi Novemba, ni mwezi maalumu wa kuwaombea marehemu.
Upagani mtupu[emoji115] . Tokeni huko gizani mje kwa Yesu
 
Mimi ni mwanazuoni wa Taalimungu(Theology) naomba kuchangia uelewa kidogo. Kihistoria jambo hili ni gumu sana na ni moja ya sababu iliyomfanya Martin Luther kuanzisha Imani ya Kiprotestanti baada ya kuishutumu Kanisa Katoliki na mafundisho yake.

Imani ya Kanisa Katoliki inafundisha kwamba roho inapotengana na mwili kwa wengine "kufa", huwa ina sehemu 3 za kwenda, mbinguni, motoni, au toharani. Hii sehemu ya 3 ndio inaleta ubishani sana. Kanisa ueleza kwamba kuna baadhi ya watu kutokana na maisha yao hapa duniani roho zao haziwezi kwenda mbinguni moja kwa moja au motoni moja kwa moja. Hawana mema sana ya kurithi mbingu wala mabaya mno ya kuwastahili moto. Roho hizi hukaa toharani. Wahusika hawana tena uwezo wakubadili hali za roho zao. Ndio hapa sasa waamini walioko bado duniani ualikwa kwa sala na sadaka zao kuziombea roho za marehemu waliko toharani, lupitia sala na sadaka, roho hizo hutakaswa na kupokelewa mbinguni.

Kama nilivyotangulia kusema jambo hili hubishaniwa sana na wanazuoni ambao sio wakatoliki. Wakatoliki wana msingi gani wa kuamini hivi? soma Maandiko Matakatifu kitabu cha Makabayo 2 sura ya 12. Nasisitiza soma Maandiko Matakatifu na sio Biblia kwa sababu Biblia zote isipokuwa ya Wakatoliki haina hichi kitabu. Ilikuwaje Martin Luther aliviondoa baadhi ya vitabu kutoka katika orodha ya Maandiko Matakatifu. Kwa ufupi Biblia zote wa Waprotestanti zina vitabu 66 badala ya 72(Somo linguine refu)

Wakati Vatikani inashambuliwa na maadui waliamua kujenga ukuta upo mpaka leo kuzunguka makao makuu ya kanisa. Walihimiza wakatoliki wote kutoa pesa, na kadiri pesa zilivyokuwa zinatolewa na waamini kadiri hiyo hiyo roho zilikuwa zinatolewa motoni. Huenda ilikuwa ni kweli au ni mbinu tu ya kupata ya pesa( Mimi sio hakimu)

Mpaka leo kanisa katoliki lina utaratibu wa kuhadhimisha misa kwa ajili ya marehemu - Requiem Mass, ndio msingi wa neon Requiscat in Pace, roho ya marehemu huombewa heri na pumziko la Amani.

Bado kuna maswali kadhaa: Je waamini hufahamu vipi kama roho za marehemu wao ziko mbinguni, motoni au toharani. Kimsingi, zile za mbinguni na motoni haziombewi. Hakuna mwenye hakika na roho ya mtu yeyote iliyoko motoni kwa sbb hiyo ni kazi ya Mungu, sisi sio wa kutoa hukumu. Inakuwaje sasa kama naiombea roho ambayo tayari iko mbinguni, kanisa hufundishakwamba, katika hali hiyo, sala na sadaka hiyo itazifaa roho nyingine zilizoko toharani, au hata na wewe mwombaji mwneyewe ambae bado huko hai.

Kwa kumalizia, kanisa lina waamini wa aina tatu, kanisa la mbinguni, kanisa la washindi eg watakatifu. Kanisa la wateswa, roho zilizoko toharani, kanisa la wasafiri, sisi ambao bado tuko duniani.

Kanisa limeweka mwezi Novemba, ni mwezi maalumu wa kuwaombea marehemu.

Mkuu nataman sana nijue kwann luther aliondoa hivyo vitabu.

Na hayo maandiko matakatifu tunayapataje.

Mtaani zimejaa biblia za kawaida tu naamin ndo hizo EDITED

Mkulu kwanza nakushukuru kwa kuniongezea msamiati TAALIMUNGU. Huu nimeuchukua mzimamzima.
Kwa hiyo, orgin ya Hilo fundisho inawalakini. Kwa nini dunia nzima wanasiasa, na watu wa kada mbalimbali wanatumia msemo huu bila kuhoji? Hukumu ya mwisho inamaana gani kama Kuna watu wanateswa kunzia Sasa kabla ya kiyama general judgement of mankind. Huoni kama Mungu anafanya unfair judgement? Mtazamo wangu.

Mkuu suala la kutumiwa na watu hatutakiwi kuhoji kwann wanalitumia

Hao wanasiasa naamin hawajui hata origin yake kama nilivyo kuwa mimi.


Hii imekuwa kawaida ya wanadamu kufanya mambo kwa sababu tuliyakuta na tunakuwa wavivu kufukua historia

Upagani mtupu[emoji115] . Tokeni huko gizani mje kwa Yesu

Sawa mzee wa UPAKO
 
Huku ukijaribu kuwaza, kwa heshima naomba nami uniruhusu kuwaza mambo yafuatayo:

1. Fikra hizi na mfuatano huu wa kufikiri (mfuatano unaumuhimu kuliko fikra) na kwa tafsiri zako ni wa kuzaliwa au wa kujijongesha mwenyewe au vyote viwili!!.

2... Nafikiri nisubiri majibu ya kufikiri kwako. Asante kiongozi. I'm inspired.
mkuu sijaona dhumuni la kujua chanzo cha fikra hizi maana thread iko wazi kuhitaji kila mwenye kujisikia kutoa maoni yake juu ya suala hili, Labda uniweke sawa hapo kwanza kama hatujaelewana vyema. Karibu mkuu kwa maoni huru
 
Hili ni nino lililojichukulia umaarufu mkubwa Duniani. R.I.P ni neno ambalo japo mzizi wake ni kwenye madhahebu ya kikristo maarufu lipo katika lugha za nchi nyingi mbalimbali duniani bila kujali dini wala muelekeo wa imani. Na wakati mwingine linatumiwa na hata wasiomuamini Mungu.

Mfano;
1:Urusi ( Покойся с миром )
2: Waarabu (Orqod fi salaam)
3:Wachina (Ān xī, )
4:Wakorea (Samga goinui myeongbogeul bimnida)
........ na wengine wengi nafasi haitoshi.

HISTORIA YA FUPI YA R.I.P.
R.I.P sio neno lililoanza leo, historia inaonyesha limeanza kutumiaka toka karne ya 8. . R.I.P ilianza kushamiri kwenye makaburi hasa ya wakristo na kuanza kutumika kama salamu ya kumuombea heri marehemu karne ya 18. Changamoto ikaja kuwa hakukua na ushahidi wowote wakujitosheleza kuamini kuwa Kuna roho inaenda sehemu ambayo inauwezekano isiwe na amani kwa hiyo inahitaji kutakiwa amani huko iendako. Muda mwingi kabla ya salamu hii ulielekezwa kuwapa pole wafiwa na kuwapa matumaini ipo siku yote haya yataisha.

Maswali kadhaa yanaibuka kuhusu heri/salamu hii anayotakiwa Marehemu.
1: Je kuna ushahidi wa kutosha nje ya imani kuhusu uhalali wa salamu/heri hii, au salamu/heri hii huwa inamfikia mlengwa?

2:Je, Kwa watu ambao hawaamini uwepo wa maisha baada ya kifo, kuna ulazima wa hii salamu?
3:Kuna uwezekano au uhakika wowote kuwa salamu au heri hii inamnufaisha mlengwa?

4:Kama salamu/heri hii ilianzishwa na imani moja ya dini, nini kilisababisha itapakae dunia nzima kwa watu wa imani nyingi zinazopingana?

5: Je dunia inaneno moja katika mazingira kama haya litakalokubalika na watu wote, wa imani zote na wasio na imani yoyote?

5:Ni njia ipi bora kama hii ikioneka haikidhi viwango vyako vya imani au kama hauamini Mungu itakayofaa katika mazingira ya kuondokewa na wenzetu?



Najaribu kuwaza,........
Nini maoni yako
Ni kama kustaarabiana tu pale umjuaye anapokufa,ila kumwambia mfu alale mahala pema hiyo ni kazi ya MUNGU mwenyewe,waweza mwambia mfu lala pema peponi,hii ni kujidanganya

1.Anaweza asilale pema
2.Kulala pema au pabaya ni kazi yake MOLA
3.Inawezekana mtu akifa anazaliwa kiumbe kingine,unamlilia kumbe keshakua kuku hapo nyumbani anakuchek tu
4.Mfu na azikwe tu kisha watu watawanyike kivyao
 
Kwa waislam: never use the word "R.I.P",Mafundisho sahihi katika dini ya kiislamm endapo mtu atafariki ni kusema :" Inna Lillahi Wa Inna Ilayhi Raaji'un "
 
Kwa waislam: never use the word "R.I.P",Mafundisho sahihi katika dini ya kiislamm endapo mtu atafariki ni kusema :" Inna Lillahi Wa Inna Ilayhi Raaji'un "
Mkuu, tafsiri ya hilo neno kwa kiswahili ni ipi?
 
Back
Top Bottom