Reuben Ndege kavae viatu vya jasiri uingoze njia

Reuben Ndege kavae viatu vya jasiri uingoze njia

Reuben ndo umeamua kuja kujisifia hukuuu. Huko scanad si ukafanya mpaka Kampuni ikataka kupelekwa mahakamani kisa madeni ulivokuwa country manager kwa masaa hadi ukarudishwa cheo chako cha kutengeneza matangazo tu. Hebu wacha sifa zisizo na tija viatu vya Ruge utaweza wewe ndugu yangu????? Mwenzako alikuwa anaongea na kila mtu na anamskiliza kila mtu wewe kacheo tu ulichopewa scanad unawazungushia kiti watu hadi mkapoteza biashara yote kwa kampuni zingine... ukweli ni mwenye uwezo anaonekana ila sio wewe ndugu yangu. endelea kujisifia na wewe ukipewa kiti clouds mwaka tu nakuhakikishia wataondoka wote mmoja mmoja wateja hadi wafanyakazi kama walivooondoka scanad, labda kama umebadilika. Anyway hongera kwa kujisifu mkuuu sio kwamba nakusema ah ah..ila badilika ndugu yana ubrazameen mwingi sanaa huyu jamaa ndo ataiuaaa kabisa clouds, ila ndio vizuri maana anahitajika mtu mwingine tasnia ya redio atawale... natumai EFM na Times wanacheka huko waliko, huuu ndio muda wao eh bwana ehhh kweli Clouds maji ya shingo hadi huyu jamaa bogus bogus kapewa nafasi nyeti ka hiyo...tutaona kama utaweza kuendeleza mawasiliano ya Ruge..yetu macho labda ka ameokoka hehehehehe
Kumbe Ana mambo ya ajabu. Ndiyo maana Dina,wa watu alishindwa
 
Uti wa mgongo wa chonbo chochote cha habari ni matangazo ya biashara
Kusaga ana akili sana
 
Soso fresh katika ubora wa awali wenye asili halisi!!
Nitafurahi siku nikisikia ML chris na DJ bonny Love nao wamerejea mjengoni... kuna watu wanaujua entertainment na wanafanya kama kazi wanayoipenda!!
kweli kabisa
 
Uti wa mgongo wa chonbo chochote cha habari ni matangazo ya biashara
Kusaga ana akili sana
kabisa bila matangazo hata mishahara huwezi kulipa, umeme utashindwa kununua Redio itakufa, yule pia karudishwa kimkakati kuwin Akaunti ambazo alifanya nazo kazi za matangazo
 
Weakness ya Ncha kali ni maganja. Very few people ambao ni chain smokers wa weed na wana rational thinking, tolerance na humble.

Ikiwa kumuongoza Mswahili dina marius ameshindwa ataweza Kuvaa viatu vya marehemu jasiri muongoza njia. Scanad ilipotea kwenye anga za marketing sababu ya Poor management. VTL alipotoa mkono wake kuwapa kazi scanad ilipotea kabisa
hayo ni mapungufu yake, tupe pia mafanikio yake alipokuwa SCANAD
 
Kwani huyu Ndege ni nani mkuu? Hebu fafanua vizuri.
Nimepatwa na furaha sana baada ya kuona taarifa kwenye ukurasa wako wa mtandao wa Instagram ukiufahamisha umma/mashabiki kuwa kwa sasa umerejea CMG, Clouds Media Group, imekuwa furaha kwa wengi ila hofu kwa wengi pia.

Reuben Ndege almaarufu Nchakali, ulipikwa Clouds na jasiri marehemu Ruge ukawa zao bora na hatimae SCANAD wakaona hapana wakakukaribisha na kukupa nafasi uuoneshe uuma upande wako wa creativity uko vipi.

Ukiwa SCANAD ulipaza sauti na wachache hawakuelewa ila walioko kwenye tasnia ya Advertisement waliumia kichwa na kuwaza haya madini huyu mtu anayatoa wapi, Kampuni kubwa umeshiriki kuandaa kampeni za bidhaa kwa njia ya matangazo, Coca Cola, Vodacom, Tigo, Kvant, Chai Bora, etc.

Naweza sema uzalendo na Upendo ulionao Clouds ndio umekurejesha na ni heshima kwa Ruge huko aliko anatabasamu nakuona viatu vyake mvaaji amepatikana,sidhani kama umeangalia sana maslahi, kama ni maslah SCANAD naamin walikuwa na uwezo wa kukuretain kwa nafasi uliokuwa nayo na ungebaki ila la hasha.

Wengi walijiuliza viatu vya jasiri angevaa nani, na jina lako lilikuwa midomoni mwa kila mtu naona ule msemo wa Sauti ya watu ni sauti ya Mungu umejidhihirisha, kapambane na tukutakie kila kheri wale waliohisi Mawingu imefika Mwisho nadhani wameanza kuona ndio kwanza Imezaliwa upya.

Kila la heri Reuben Ndege (Nchakali).
 
Seba Maganga namuona anaweza,Ncha kali ana element za usela.
Sio lazima ahitajike mtu mwenye element za ubabu ama utuuzima ili kushika executive position tena kwenye brand ambayo yenyewe consumer wake asilimia 70 ni vijana kutokana na content zinazozalishwa.

Biashara ya Radio na vyombo vya habari yategemea sana matangazo maana hao wanauza airtime, uzoefu wa ncha kali kufanya kazi na Agency ya kimataifa kama SCANAD wanao deal na matangazo yeye akiwa country manager inamfanya kuwa right candidate, sababu anakwenda kuleta tija kibiashara maana anajua soko linataka nini.
 
Sio lazima ahitajike mtu mwenye element za ubabu ama utuuzima ili kushika executive position tena kwenye brand ambayo yenyewe consumer wake asilimia 70 ni vijana kutokana na content zinazozalishwa.

Biashara ya Radio na vyombo vya habari yategemea sana matangazo maana hao wanauza airtime, uzoefu wa ncha kali kufanya kazi na Agency ya kimataifa kama SCANAD wanao deal na matangazo yeye akiwa country manager inamfanya kuwa right candidate, sababu anakwenda kuleta tija kibiashara maana anajua soko linataka nini.
For me mtu ninaye mwona ana fiti katika hiyo nafasi Seba,yupo vizuri kwanza anaijua CMG vizuri sana,kishashika nafasi nyingi CMG,kafanya kazi na Marehemu Ruge kwa ukaribu kwa hiyo hata some strategies ambazo alikuwa akizitumia marehemu ktk uongozi atakuwa anazijua vizuri,nne hana usela yaani ni presentable ,hata akipropose kitu kwa makampuni mbalimbali wanamwelewa.
 
Back
Top Bottom