tutafikatu
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 3,327
- 4,624
Ni rahisi kuanzisha uzushi. Huhitaji kuwa mhubiri kama Reinhard Bonnke ili kuuza madawa kama Escobar.Nilipata kusikia mahubiri yake kwenye kanda ya redio ,kuna ile sehemu ya jamaa na Chicken sikumbuki vizuri , wengi walisema ni muuza madawa ya kulevya
kumbe wewe ni mmalawiNimewahi hudhuria mkutano wake Malawi mwaka 1985 uliokuwa na miujiza kibao.
nakumbuka mabango yalikuwa yameandika " IDZANI MUDZAONE ZOZIZWA ZA MPAMVU YA MULUNGU ZOCHITIKA MMOYO WANU"
acha kupotosha si mkwe wake bali ni mtoto wake wa kiroho (his mentor and spiritual fadher)He is retired, Mkwe wake ndo kashika nafasi yake
wanaliwa nini , na busara zinasema ni kheri kuwa mjinga kuliko kuwa mpumbavu. tuelimisheWajinga Ndiyo Waliwao.
wanaliwa nini , na busara zinasema ni kheri kuwa mjinga kuliko kuwa ********. tuelimishe
Lile kusanyiko Kubwa la aina yake lililowahi kutokea nchini mwanzoni mwa utawala wa B.W. Mkapa June 1996 (miaka 20 iliyopita) leo lipo mjini Mwanza ambapo mwinjilisti wa kimataifa R. Bonnke atalitikisa jiji la miamba al maarufu Rock City kwa mahubiri yake ambayo huwavuta wengi.
Kusanyiko hili huvutia watu wengi wengine kutoka mikoa ya jirani ambapo pamoja na wengi kuja kushuhudia mahubiri wengine huvutiwa kushuhudia maandalizi makubwa ambayo hufanywa kufanikisha kutaniko hilo.
Matumizi ya teknolojia za kisasa na ghali ambazo huchukua muda wa kutosha kufungwa katika viwanja vya Furahisha, promo za kutosha kupitia vyombo vya habari na mapokezi makubwa ambayo hupewa mhubiri huyu naamini vitasababisha viwanja vya furahisha kutapika.
Mliokuwepo na kushuhudia mkutano wa 1996 mnakumbuka nini?
Mkutano huu utaacha gumzo kama la 1996 lililochukua muda kusahaulika?
Tuendelee kupeana updates za yale yanayoendelea hapo jijini na eneo la mkutano, picha mbalimbali zitanogesha zaidi habari hii.
Nipo nje ya jiji.
Wewe endelea kufuga majini sisi tunayababadua.Wajinga Ndiyo Waliwao.
hapana, mimi ni Mgiriama natokea Mijikenda, malawi tulikuwa tunaishi tu.kumbe wewe ni mmalawi
Ni zaidi ya saa moja nimeona kile ambacho kimefanyiwa kazi na jicho pevu kwanza nianze kumpongeza Mohamed Ally kwa weledi mkubwa kwa kufichua ufedhuri wa Victor kanyari na hii ipo sana kwenye ulimwengu wa leo kwa kila dini , muhimu ni kuwa na elimu ya kuyendea mambo ,
Hiyo ni huduma.
Hata Rais anaweza akawa na mualiko mahala na akamtuma mwakilishi; lakini officially yatakayoongelewa na mwakilishi yanahesabika yametoka kwa Rais.
Utapeli wa Global Church Mission Tz-Mwanza Serikali Wapi?Ni zaidi ya saa moja nimeona kile ambacho kimefanyiwa kazi na jicho pevu kwanza nianze kumpongeza Mohamed Ally kwa weledi mkubwa kwa kufichua ufedhuri wa Victor kanyari na hii ipo sana kwenye ulimwengu wa leo kwa kila dini , muhimu ni kuwa na elimu ya kuyendea mambo ,
kingine faiza unapo ona ubaya jua pia na uzuri upo kwa maana kwamba si wote wanahubiri kutaka fedha kam Mohamedy mchambuzi makini tofauti na wewe Faiza alivyo muhoji Askofu ambaye alikiri uwepo wa mambo haya kama yalivyotabiriwa kwenye maandiko matakatifu
sasa unaweza kudhibitisha hicho cha Askofu kanyari na mahubiri yanayoendelea Mwanza kuwa yana ufanano na hiki ulicho post?
Sasa naomba ujibu swali langu kuwa mahubiri yanayofanyika Mwanza yanahusiano gani na hoja ya utapeli?
Hovyo mwenyewe, uliza ujibiweHuu uzi ni aina ya promo yenye ubunifu, kasema unafiki lakini hakuna sehemu kagusia, pia kajidai kakosea muhubiri kwa kufanya masahihisho pale mwishoni mwa uzi. Hovyo kabisa