Revenge: Napeleka kilio kwa binti fulani siku ya kupeleka barua

Revenge: Napeleka kilio kwa binti fulani siku ya kupeleka barua

Kwa ufupi hii ni taarifa tu, so ushauri wako hautabadili chochote wala kuongeza chochote, vipi lakin uzima upo??

Ni hivi, mi huwa siumizwi alafu anayeniumiza akabaki salama, nikiumizwa mi nakuumiza mara 10 alafu fresh, maisha yenyewe mafupi haya, mi niwe na stress alafu wew ucheke ili kiwe nini... sipendagi ubwege kabisa, na nitabaki kwenye kumbukumbu zako milele ukijifanya kuniletea habari za ajabu..

Miez 8 iliyopita nilidate na dada mmoja hivi mrembo, height moja hivi mauzo sana na mzigo wa kuvuta huko nyuma haukuwa haba, kifupi mvuto wa yule dem hauna shaka, kama ni maksi basi A ya 95+... mapema nikamwambia mambo ya kiboya sitaki, km utacheat jitahidi nisijue, nikijua umeumia....Akajifanya hadi kulia pale kwamba ananilove nyang'anyang'a na kamwe hakuna mwanaume kama mimi, nikasema poa but take my words ukinizingua hutoamini nitakachokufany, na km hunitaki niache uende, na kama pia itakuw mechi za dharula tu alafu kimya tuambiane, moyo wangu hauchezewi.. akasema nisiwe na shaka ananipenda, nikasema poa.

Tabia yangu ni kwamba kamwe siwezi kuwa na mpenzi zaid ya mmoja kwa wakati mmoja, so nikiwa na mmoja huyo huyo. Sasa mwezi mmoja nyuma nikausoma mchezo dizain kama demu wangu analiwa hivi, sikumuuliza, nikakomaa hadi nikapata password zake facebook na insta.. nikazama inbox yake, daah ni balaa tupu, ashapigwa mashine na mshikaji mmoja hivi, then jamaa dizain kama anakomaa naye amle 0715 hiv sema demu anabana.. text yake hii hapa..

"Baby naridhika sana nawew, ila unanibania side B, nyimbo za side A zote nimeskiliza why uninyime za side B mpenz?, kama side A nilsikilza kwa elfu 70 bas side B lazma dau lipande.. nielewe bas"

Demu akajibu..

"Mi nina mtu na tuna malengo je akigundua na kuniacha itakuwaje"

Jamaa..

"Hawezi gundua, kwani huwa anakagua huko, ila navyokujua huwez nibania.. nitakutoa out ukafanye shopping ya maana, na nitakutumia 100,000 kesho"

Demu...

"Mmh poa tutaangalia tukikutana tar.22 jamaa akiondoka kama tulivyopanga".

Zipo nyingi nying but hizo kiufupi,....

Mimi kwa huyu demu..., nampa nachopata, najinyima sana apate yeye, nishamtoa shopping za maana mara kibao na tayari nishaandaa pesa nzuri tu kwa ajili yake, Krismass na mwaka mpya, maana tar.hizo sitakuwepo kutokana na majukum ya kazi yangu, nammudu kiujumla, nguo, usafiri, pesa ya kula, malazi nafanya mimi.. yeye hana chochote zaid ya gamba lake la diploma. Muda wote huo sina demu zaid yake.. na on bed naperfom fresh hadi anaomba poo yeye..

Nilichokifanya baada ya kugundua hilo, nimescreenshot charting zote hadi picha walizopiga wakiwa lodge wametumiana kupitia fb messenger nimejitumia kwenye simu yangu, then nimeuchuna.. kifupi tayari nimeshampiga chini ila siwez kumwambia tuachane kiboya boya hiv bila yeye kuonja joto la jiwe kidogo, na kamwe sitafanya naye mapenz tena.. ambacho kimebaki kwake ni kumpa kidonda cha milele..

Ifahamike ananipenda japo tamaa anazo, ashanitambulisha kwa rafiki zake wote, dada yake, hadi mama yake.. kifupi anaitwa mrs mimi... na uchafu anaoufanya ni siri kubwa sana na ndo maana anatumia fb messenger maana anajua siwez hisi chochote huko.. tayari tarehe ya kupeleka barua ishapangwa, tarehe 07 jan... mashangazi zake wote wanajiandaa kwa tukio hilo.. upande wetu pia tunajiandaa..

Nataka nifanye nini?? Siku hiyo ya tukio la kwenda kwao kujitambulisha rasmi ndo siku yangu ya kumuumiza, maana kwao anaaminika sana, anaimba kwaya kanisan, ana vyeo vingi ving vya huko kanisani.. na huwezi mzania hata kidogo kama ni mshenzi.. siku hiyo mbele ya Mchungaji wake, ndugu zake, mama ake, mashangazi na marafiki zake wakiwa na smartphone zao naenda umiza mtu vibaya sana, sio kwamba nitampiga hapana, ila nataka nimafanyie tukio ambalo litaweka maumivu ya kudumu kwenye moyo wake na kamwe hatokuja nisahau..

Tarehe 7 january, save the date....

USIPOTEZE MUDA KUNISHAURI CHOCHOTE, HUWA NIKIPANGA SIPANGUI..
========

UPDATE: Mrejesho tayari fuatilia

Kufuatilia mrejesho wa tukio hili bonyeza link hapo chini

Mrejesho: Sehemu ya kwanza
Mrejesho: Sehemu ya pili

Mrejesho: Sehemu ya tatu
Mrejesho: Sehemu ya nne

Mrejesho: Sehemu ya tano
Mrejesho: Sehemu ya sita

Mrejesho: Sehemu ya saba
Mwisho
Duuuh
 
MREJESHO....

Naomba kwanza niwaombe radhi wote mliokuwa mnasubiria mrejesho hadi mkachoka, niwashukuru pia wale waliokuja PM kunishauri na polen maana ushauri wenu haukuzingatiwa.

Tarehe 07 january kila mwaka itakuwa ni siku yangu ya kumbukumbu.

Kwanza nianze kwa kusema kisasi ni haki ya mtu aliyefanyiwa ubaya pasipo yeye kufanya ubaya, siku tajwa hapo juu ni siku niliyeachana na mwanamke wangu ambaye ndo tulikuwa kwenye hatua muhimu za kuoana, mwanamke aliyenifanyia ushenzi wa kishenzi na mim nikawa sina namna zaidi ya kumfanyia ushenzi wa kishenzi kama yeye.

Siku ilianza vema kwa safari ndefu kuelekea kwa wazazi wake, nikiwa na mshenga na mzazi wangu na baadhi ya ndugu, njian stori zilikuwa za kunipongeza kwa kuchukua uamuzi huu wa kuoa, wakati wote mim nilikuwa kimya nikizid kutafakari zaid jinsi nitakavyopeleka kilio kikuu kwa yule binti, nikiri kwamba nilifikiria pia kuhusu wazazi wake na wangu pamoja na ndugu, jamaa na marafiki watakaokuwepo ila bad luck ni kwamba option ilikuw moja tu.

Majira ya saa 2 hv usiku tukawasili nyumbani kwa binti, tulipokelewa kwa bashasha na shamra shamra sana, tukapikiwa chakula kisha tukapelekwa sehemu ya kupumzika na kesho saa 4 asubuhi ikawa ndo muda muafaka wa tukio la mahari ili pia sisi tuweze kurudi mapema.

Asubuhi ilikucha vema sana, nikiwa nimeprint messages zote na zile picha tayari kwa kumpiga mtu tukio, muda wa kwenda sehemu iliyoandalia ya mazungumzo ukafika, kama mnavyojua muoaji huwa anaitwa mwishoni baada ya wazee kukabidhiana mahari waliyokubaliana, ikabidi mimi niombe kuvunja utaratibu kwa kuomba niwepo kwenye kutoa mahari hiyo km haitakuwa shida sana, mshenga akasema sio shida inawezekana tu, kweli niliruhusiwa na mshenga akapiga maneno maneno pale ikawa uwepo wangu pale wala sio shida.

Baada ya kukaribishwa na upande wa kikeni ukafika muda wetu sasa wa kujimwambafy kwa kutoa mpunga then taratibu zingine zifuate hapo mim nikainterven kwa kuomba niongee kdg, baba wa binti akasema niruhusiwe maana ile ni kwa ajili yetu, basi nikaomba binti aitwe pale kwenye kikao, ni km walitaka kudadisi kitu ila mim nikaomba binti aje kabla hatunaendelea, niliongea politely sana wala sikuwa na hasira, binti akaitwa na kumbe alikuwa kwenye kuandaa chakula hivyo ikabidi akimbie bafun faster kisha akaja.

Pamoja na wazazi wa binti lakin pia kulikuwa na wajomba, baba wadogo shangazi yake mmoja na kaka zake. Sikua na maneno mengi nikasema straight tu, nimeghairi kuoa na mahari isilipwe na nimeona niliseme hili mbele ya binti na kikao hiki kikubwa ambacho kinahusisha familia zote mbili, watu wakabaki na butwaa, walitaman kuhis nimechanganyikiwa lakin kwa jinsi nilivyokuwa naongea ikabid wafute hayo mawazo, wakawa buzy sasa kunisikiliza.

Nikamwita binti kwa jina lake, nikamuomba binti aweke wazi kila kitu pale kuhusiana nayeye kuwa na mwanaume mwingine, mama wa binti jasho likamtoka akaanza kumuuliza binti yake km ni kweli alikuwa anafanya ushenzi ule, binti akakana akasema sio kweli na hajawahi kujihusisha na mwanaume yeyote tangu nimchumbie huku machozi yanamtoka akaanza kuapa kwa majina yote ya mungu wake, akaanza kujifanya anataja vifungu vya biblia, asee walokole ni wanafiki nafiki sana.

Kikao kikawa kimebadilika sura, kila mtu akabaki ana hamu ya kuujua ukweli, mshenga akaniita tutoke nje kidogo nikakataa, nikamwambia binti aache kupretend aseme ukweli, akaendelea kukataa pale, basi baba wa binti akasimama akasema yeye km mzazi wa binti na mkuu wa ile familia ile ni aibu kubwa na km nitashindwa kuthibitisha basi ataenda kwenye vyombo vya sheria kudai fidia ya binti yake, kwanza ya kumpotezea muda na pili ya kumdhalilisha na kumuumiza kisaikolojia binti yake.

Baada ya kuona binti anakomaa kwamba sio kweli na mzee wangu akawa yupo tu haelewi aseme nini sasa, nikazama kwenye begi na nikatoa picha na printing za screenshots za msg, nilikuwa nazo za kutosha, nikamkabidhi mzee wake nyingine nikampa yeye mwenyewe na zingine mshenga wangu, nikamwambia aendelee kubisha sasa, kukawa kimya kwa muda baadaye binti akakosa nguvu akaanguka na kuzimia, ikabidi akambizwe hospital.

Baba yangu alinilaumu sana kwa kitendo kile, hata mshenga akasema nilitakiwa niseme mapema tungepiga simu tu kwamb tumeahirisha kuliko nilichokifanya, nikawajibu tu moyo wangu usingeridhika kufanya kirahis vile lakn pia binti angepata nafasi ya kuwaongopea wazazi wake na wangemwamin kwa kuwa ni binti yao, namim kwa wazazi wa yule binti ningebaki kwenye kumbukumbu mbaya milele, nikawaomba wanielewe tu hakuna namna.

Ikapangwa jion tuwe ni kikao tuone nini kinafuata sasa.

ITAENDELEA...

Mrejesho: Sehemu ya pili
Hahaha
 
TUENDELEE..

Jioni ile binti alizinduka, lakin Daktari akaomba binti abaki wodin maana mapigo yake ya moyo hayapo vizuri na presha ipo juu kupita maelezo, lakin kutokana na nature ya tatizo lenyewe ni bora binti abaki kwa uangalizi na counseling maana anaweza kuchukua maamuzi mabaya, binti akabaki hospital na mama yake, wengine wakarudi home. Jioni ikafika kikao kikaitishwa.

Baba wa binti akaongea mengi km kunilauma mim, nikaon ananiletea uhuni, nikamchana kwamba nilishamweleza kwamba akifanya ushenzi namim nitafanya ushenz na hizo msg kwenye simu zipo na kama binti atakataa nazionesha vile vile jinsi tulivyokubaliana, basi ikabid busara zitumike, hasa mjomba wake ambaye alijitahidi kutuomb radhi kwa binti yao kukosa maadili kiasi kile japo limekuja wakat mbaya lakin lmesaidia sana kuelewa uhalisia wa binti yao ambao walikuwa hawaujui.

Baada ya dk kidogo mama yake akaja kutoka hospital akatukuta kwenye kikao, akaomba sana niende hospital nikamuone binti yake maana hakuna anachotaka zaid ya mimi na hayupo tayari kuishi km sitamsamehe, akaniomba sana niende hospital nikamtamkie msamaha hata wa kinafiki, nikakataa na sikwenda, nikawaambia wazee tusepe hapa hakuna jipya tena, hapakuwa na jins maana nilikaza kila kona, moyo wangu kwa dhati ulikusudia kulipa kisasi.

Nikatoka nje nikawaacha wazee wakiongea ongea, usiku ulikuwa umeshaingia tukaingia kwenye gari safari ya kwenda hom ikaanza.

Nyumban taarifa zilikuwa zimeshafika, kuna ambao waliona sawa na kuna wajinga na dhaifu wakasema ningesamehe tu nimuoe, wapuuzi.

Maisha mapya yalianza, siku moja nikawa nipo porini huko kwenye mishe zangu zikiwa zimepita km siku 4 hivi nikapigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwamba ni mwasaikolojia, akanambia kuhusu lile tukio na kwamba anaomba niongee na yule binti chochote kwa kuwa hataki kula na muda wote anachungwa maana anaonesha dalili zote za kutafuta namna ya kujinyonga, nikakataa. Nikamwambia aachane namimi kabisa.

Simu zilikuwa nying, mama yake, baba, na ndugu zake wengine lakin sikuwa na mpango tena, nikaona nibadili laini za simu zote. Nikajua nimesolve tatizo sasa, of course wakawa wanaongea na mzee wakiomba aongee namim niongee chochote na binti yao, nikakataa. Miezi kadhaa ikapita, siku moja nikiwa Tanga huko nikapokea simu ya rafik yangu akanijuza kwamba yule binti amekuja ghafla kwake, amekonda na kuchakaa. Kumbe alikuwa ametoroka kwao ili aje anitafute, alikuja kwangu kukawa kumefungwa akaona aende kwa mshikaji.

Nikamwambia kifupi tu, aishi naye pale kwake km anamhitaji ila mim kwa upande wangu ni hapana, jamaa akasema ameoa na ana familia so nafasi pale kwake ni ndogo na binti hataki kuelewa na amekataa kutoka pale kwake akaniomba niongee na yule binti, nikakataa.

Kumbe yule binti aliiba hela za baba ake dukan maana baba ake aliamua kumuweka auze duka la jumla la vifaa vya ujenzj ili angalau apunguze mawazo, akatoka na million 4 akatoroka na kuja kwa mshkaji, akakatalia kutoka hadi anione.

Jamaa akanisimulia mengi kwa kadri binti alivyomuelekeza, Na akaniomba nionane naye ili nimsaidie, nikakataa

Baada ya kukaa km wiki pale jamaa akashindwa ikabid amfukuze kwa nguvu, binti akaamua asafiri aende kwetu kwa wazazi wangu. Muda wote huo kwao hawajui binti yupo wapi, wakaenda kutoa taarifa polisi..

ITAENDELEA WAKUU.

Mrejesho: Sehemu ya tatu
Hahaha
 
TUENDELEE...

Baada ya binti kufika kwa wazazi wangu, akajieleza jinsi anavyopata shida na hawezi kuishi bila mimi, jinsi malengo yake yalivyokufa na maisha yake yalivyobadilika. Mzee akanipigia simu na kunieleza ujio wa yule binti pale nyumbani, nikamwambia ampeleke polisi arudi kwao sina muda wa kupoteza kuongelea kitu ambacho jibu lake linajulikana.

Mzee na Bi mkubwa wakaniomba sana niende pale home tukaongee, kwa heshima ninayowapa wazazi wangu ikabidi niende, mzee akawasiliana na wazazi wa binti kuwapa taarifa kwamba binti yao yupo pale, mama wa binti akajipanga kuja kumuona bint yake, baada ya siku 2 nikaenda hom, nikakuta mama wa binti yupo pia, baada ya kufika binti akaanza kuangua kilio akisistiza asemehewe, akaomba km itashindikana kbs basi aishi namim km mfanyakazi wangu hata wa ndani, alikuwa anaongea upuuzi.

Tukawa na kikao kifupi, nikaongea wazi kwamba ukurasa wa yule binti nimeufunga, hana nafasi tena kwangu kwahiyo mama amchukue mwanae arudi naye kwao, akaolewe na wengine huko ila kamwe haiwezi kuwa mimi, hapakuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na msimamo wangu, mama yake akaomba basi niwe angalau naongea na binti yake japo awe ananiskia, nikaona ni ujinga wa hali ya juu mimi kufanya hivyo, nikakataa kufanya huo upuuzi.

Kwa shida shida binti ikabidi aondoke na mama yake kurudi kwao, lakin bado hakua na amani, wakat anaondoka pale alijua nipo Tanga na nafanya kazi na taasisi gani. Alipofika kwao bado hakuwa na utulivu wakat wote alikuwa analia na alipoteza hamu ya kula, akazidi kukonda, habari ile ilikuwa pia imeenea kwahiyo aibu nayo ikawa inamtesa, nikarudi zangu Tanga kuendelea na majukumu mengine.

Mzazi wa yule binti aliongea na mzee akapata namba yangu ya simu akawa ananipigia na kuniomba sana nimsamehe mwanawe maana maisha ya binti yake yamebadilika na yeye km mama anajiskia vibaya sana, akaomba niseme hata kiasi cha pesa ili akilipe km fidia ya ufusika wa binti yake, nikakataa. Akawa ananipigia simu mara kwa mara na ananisistiza kwamba amefanya kila kitu kuhus binti yake lakn hakuna improvement na hakuna namna ya binti yake kuwa sawa zaidi ya mimi kuwa naye karibu.

Nikawa naona ananipigia kelele, sirudigi nyuma, maisha yakaendelea. Nikiwa Tanga naendelea na majukumu yangu nikapigiwa simu na baba wa binti, akaniomba niseme nilipo ili aje tuongee ana kwa ana km wanaume, nikakataa, nikamwambia aongee kwa simu tu tena dk chache, akaniomba kiume kwamba habari za kumuoa binti yake najua haiwezekani tena lakin wao km wazazi wananiomba niwasaidie kt kumfanya yule binti awe sawa, maana wao wamefany kila kitu lakn imekuwa ngumu kwa binti kuwa sawa, nikaona upuuzi, hainihusu chochote. Nikamkatalia.

Ikapita miezi km 3 hv nikiwa tu napokea msg mara kwa mara kutoka kwa wazazi wa binti, nikawa sizijibu. Baadaye nikaoata mapumziko ya kama wiki 2 hivi nikarudi dsm kupumzika. Wiki ya kwanza ikaisha vizuri ila wiki ya 2 ya mapumziko nikapata ugeni pale hom kwangu, ni aliyekuwa rafiki wa karibu na binti, alisema alikuwa anakuja mara kwa mara pale hom kunibahatisha maana hata namba za simu zilikuwa hazipatikani so safari hii ameshukuru kunikuta, akaomba tuongee, nikamwambia poa.

Kwa kuwa nilitoka muda mrefu sana hom, nyumba ilikuwa chafu sana, akafanya usafi akapika, tukiwa tunakula mazungumzo yakaanza...

ITAENDELEA.

Mrejesho: Sehemu ya nne
Hahaha
 
Kuna watu humu wananiita mimi katili lakin wanasahau ukatili niliifanyiwa na huyu binti, mazee huyu binti nimewahi kumpa million 1 na laki 2 kwaajili ya kumsaidia kweny msala fulan, nikiona itafaa nitaujumuisha huko mbele. Nilimpenda na kumpa good life la viwango vya juu. Acheni nyie
Hahaha duuh
 
TUENDELEE...


Nikaona mambo yasiwe mengi, nikamwambia poa aende akamrudishe rafiki yake kwenye ndoa yake and mimi nitamfkiria kuhusu ombi lake, nilishajua tayari ashakuwa dhaifu kwangu so hawezi kunizid maujanja, hata km anasema uongo bado hauwez kuniathiri maana lazima nimzid akili, kwanza ananipenda kimapenz hivyo tayari yupo kwenye ugonjwa wa akili hawezi kushindana namimi mwenye akili timamu, and nikapanga kabisa kwamba siwezi kuwa naye yule manzi.

Akaenda akamdanganya kwamba nimepata ajali na nina hali mbaya nimekimbizwa India, na kwa jinsi hali ilivyo sijui km nikipona nitabaki na uwezo wa kufanya chochote Kwahiyo akamwambia rafiki yake akakomae tu na ndoa yake, na akaishi na yule mwanaume maana kwangu tena maji yameshamwagika, binti akaona hakuna jinsi akarudi kwa mume wake, jamaa ndo hivyo akampokea maana ndo km anakopatia ridhiki, nasikia kumbe kipindi anakuja huku alikuwa tayari kanasa ujauzito wa mshikaji, ndo huyu rafiki yake akawa ananiambia alikuja kugundua baadaye km ni mjamzito means km mimi ningejichangnya kuwa naye kipind hiki basi ningetupiwa hilo zigo kumbe la mume wake huko.

Japo binti hana amani kwenye ndoa ile so dizain km anapanga mbinu amtoroke aende akaishi maisha yake peke yake. Huyu rafiki yake akaniambia yupo kwenye process ya kutoa ile mimba maana hataki kuzaa na mshkaji wake, then apotee kokote akaishi mwenyewe. By the way hainuhusu hiyo sasa, azae asizae, aishi au aondole anajua yeye.

Maisha yangu yameanza upya na dizain km yule demu karidhika na kuamin kwamba sipo nchini nipo India kwa matibabu, maana baadaye ikanilazimu nibadili tena namba za simu, sasa mtihan ninao kwa huyu rafiki yake maana ananipenda na anataka nitimize ahad maana kazi ameshaifanya. Hadi leo sijamla na sitamla, na hili kwangu ni dogo sana na nitalimaliza tu kirahisi.

Nimepata aman sana na sikumbuki ubaya na maumivu yote aliyonitendea yule binti, nimeridhika kwa hiki.

Yapo mambo mengine nimeyaexclude maana stori ingekuwa ndefu sana, ahsanten kwa kunifuatilia tangu mwaka 2017 hadi leo 2021.

MWISHO,
Asante sana
 
Alifanya ukatili sana ategemee malipo na yeye kwann hakumuacha tu na maisha yake? Atakuwa na matendo magumu sana atajikuta anaoa kila siku......anafanya ivo ukute ata mtu anayemuita baba ake sio biological faza ata maza ake alikuwa na mazambi vilevile
Idiot
 
Alifanya ukatili sana ategemee malipo na yeye kwann hakumuacha tu na maisha yake? Atakuwa na matendo magumu sana atajikuta anaoa kila siku......anafanya ivo ukute ata mtu anayemuita baba ake sio biological faza ata maza ake alikuwa na mazambi vilevile
Id
 
Hii story ni ya ukweli nishakujua wewe ni nani na zamani nlikua na picha zako japo umejitahidi kusimulia kwa code kali sana ila nshakujua ila nikupe hongera hakika ulimpenda sana yule dada wa kimakonde na alikua mzuri wa sura haswa na kale ka rangi kake sasa sema nlikwambia wanawake wa vile sio wife material kabisa ni wakutumia tu maana msichana alikua anapenda bata yule loh....ngoja niishie hapa kwa leo....najua ushanijua
Hahaha
 
Matumizi mabaya ya akili, issue iiikua kumla tu yeye na rafiki zake na Mama yake ukoo mzima ndicho kisasi chenye utu. Sasa hiki cha kihindi ona kimekugharim miaka zaid ya minne.
Hahaha
 
2022-2024, kuna vitu kimetokea very interesting. Kumbe yule jamaa aliyetembea naye aliyekuwa anataka na side B alikuwa HIV+. Na km mnakumbuka tang nigundue kwamba simuelew elewi sikuwahi kulala naye tena, so nipo salama kbs sina VVU..

Ilikuwaje nimejua? Nani alinambia? Kuna mambo yalitokea hapa katikati pia.. kuna msala mzito sana ulitokea wa Polisi kupewa pesa na baba ake binti waje wanifanyie kitu mbaya, labda mzee alijua mi ni mwepesi, ***** moto uliowaka plan ikabackfire hadi polis wakajuta kujiingiza kweny mambo ya kifala, ikapelekea msala kumrudia yule mzee hadi akataka kujinyonga, hii nayo ilikuwaje??

Kuna demu wa JF alikuja PM alijua mim ni Pimbi, ni jimama lina pesa pesa hv kdg, huyu naye ana mkasa wake.. aliyakanyaga huyu, hii naye ilikuwaje?

Wengine pia wanatak kujua yule binti wa Kimburu kiunaga ubaga jinsi nilivyomalizana naye Hadi nikampiga chini, hapa napo pana balaa lake zito pia.

Mambo yapo mengi, nipo chaka sana kwasasa nafanya project moja hivi tough sana.. but Nitarudi niwape mikasa yote hii.

Andaa popcorn zako.

NB: kuna ambao wanadhan huu mkasa ni uongo, siku moja mbele ya safari nitafanya interview na nitawajuza, ila sio hv karibuni.
Hahaha duuh
 
TUENDELEE...


Nikaona mambo yasiwe mengi, nikamwambia poa aende akamrudishe rafiki yake kwenye ndoa yake and mimi nitamfkiria kuhusu ombi lake, nilishajua tayari ashakuwa dhaifu kwangu so hawezi kunizid maujanja, hata km anasema uongo bado hauwez kuniathiri maana lazima nimzid akili, kwanza ananipenda kimapenz hivyo tayari yupo kwenye ugonjwa wa akili hawezi kushindana namimi mwenye akili timamu, and nikapanga kabisa kwamba siwezi kuwa naye yule manzi.

Akaenda akamdanganya kwamba nimepata ajali na nina hali mbaya nimekimbizwa India, na kwa jinsi hali ilivyo sijui km nikipona nitabaki na uwezo wa kufanya chochote Kwahiyo akamwambia rafiki yake akakomae tu na ndoa yake, na akaishi na yule mwanaume maana kwangu tena maji yameshamwagika, binti akaona hakuna jinsi akarudi kwa mume wake, jamaa ndo hivyo akampokea maana ndo km anakopatia ridhiki, nasikia kumbe kipindi anakuja huku alikuwa tayari kanasa ujauzito wa mshikaji, ndo huyu rafiki yake akawa ananiambia alikuja kugundua baadaye km ni mjamzito means km mimi ningejichangnya kuwa naye kipind hiki basi ningetupiwa hilo zigo kumbe la mume wake huko.

Japo binti hana amani kwenye ndoa ile so dizain km anapanga mbinu amtoroke aende akaishi maisha yake peke yake. Huyu rafiki yake akaniambia yupo kwenye process ya kutoa ile mimba maana hataki kuzaa na mshkaji wake, then apotee kokote akaishi mwenyewe. By the way hainuhusu hiyo sasa, azae asizae, aishi au aondole anajua yeye.

Maisha yangu yameanza upya na dizain km yule demu karidhika na kuamin kwamba sipo nchini nipo India kwa matibabu, maana baadaye ikanilazimu nibadili tena namba za simu, sasa mtihan ninao kwa huyu rafiki yake maana ananipenda na anataka nitimize ahad maana kazi ameshaifanya. Hadi leo sijamla na sitamla, na hili kwangu ni dogo sana na nitalimaliza tu kirahisi.

Nimepata aman sana na sikumbuki ubaya na maumivu yote aliyonitendea yule binti, nimeridhika kwa hiki.

Yapo mambo mengine nimeyaexclude maana stori ingekuwa ndefu sana, ahsanten kwa kunifuatilia tangu mwaka 2017 hadi leo 2021.

MWISHO,
Kumbe videmu vya kilokole ni vinafki sana ee!
 
Back
Top Bottom