Riba za mikopo kwa watumishi, CRDB na NMB

Kwa maana hiyo mkopo sio kitu cha kukimbilia.
 
Mfano me nilichukua mil 10 nakatwa 253,000 kws miaka mitano mkuu so kwenye mkataba inaonekana mwanzo mwenga,ila crdb is the best kwa wote
Du Yani kwa miaka unalipa zaidi ya m 15,mh hiyo ni too much.
12*5*253,000=15180000
 
Bora serikali ingekomaa na kukopesha watumishi wake,hawa wenye mabenk wangushusha tu riba..riba ni janga kwa kweli
 
Interest rate most of the time ni 18% yearly ambayo inakuwa 51% for 5 years, au 43% for 4years, so inadepend unataka kurudisha kwa muda gani, jinsi muda wa marejesho unavoongezeka ndivo interest inavoongezeka but montly return inapungua pia,

Kazi kwako hapo.
 
Tena wanaoumia zaid ni wale wanakopa halaf wanajenga,,inawaumiza sana kwa miaka hiyo mitano,,ila anaekopa akawekeza kitu ambacho anawezankufidia ile hela inayokatwa kiukwel haumii kama anaepeleka kwenye ujenz bila kuzalisha
 
Mfano me nilichukua mil 10 nakatwa 253,000 kws miaka mitano mkuu so kwenye mkataba inaonekana mwanzo mwenga,ila crdb is the best kwa wote
Mbona marejesho yake ni makubwa sana,karibia deni na riba mpaka kwisha ni takribani Milioni 30,360,000
 


RIBA KATIKA UISLAM
Kwa mujibu wa Qur’an tukufu, kuchukua riba ni dhambi ambalo linasababisha adhabu kali kabisa kutoka kwa Allah swt. Adhabu za kuchukua na kutoza riba ni kali kabisa kuliko madhambi mengine. Kama ilivyoelezwa katika Surah Aali Imran, 3, : 130 - 131:
‘Enyi Mlioamini! Msile riba, mkizidisha mara dufu kwa mara dufu; na mcheni Allah ili muweze kuwa na ufanisi’
‘Na ogopeni moto wa Jahannam ambao umetayarishiwa makafiri.’
Inamaanisha kuwa ukali wa moto ambao umetayarishwa kwa ajili ya wale ambao huchukua riba kama vile moto utakavyokuwa mkali kwa ajili ya makafiri.
Allah swt anatuambia katika Surah al Baqarah, 2, Ayah ya 275 :
‘ Wale wanaokula riba, hawasimami ila kama anavyosimama yule ambaye Shaitani kamzuga kwa kumsawaa; na haya ni kwa sababu wamesema, ‘biashara ni kama riba’, Allah ameihalalisha biashara na kaiharamisha riba. N a aliyefikiwa na mauidha kutoka kwa Mola wake, kishaakajizuia, basi yamekwisha mthibitikia yale (mali) aliyoipata; na hukumu yake iko kwa Allah. Lakini wanaorejea (kula riba) basi hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele.
 
Tusichanganye mambo, sio wote wanaamini katika hiyo Quran tukufu, wapo wanaoamini Biblia pia na wengine hawaamini kati ya hivyo vyote, ko acheni mambo ya kaisari yaende kama yalivyopangwa, na ya Mungu yaenende kulingana na miongozo yake
 
H
Kwa hiyo kiuhalisia unarufisha mara mbili ya hela uliyochukua
ahahah watatuuua asa mbna wananufaika wao
 
ni r

ni rahisi mkuu. Inategemea na riba hiyo inakatwa wapi kwenye mkopo unaobaki au kwenye mkopo wa mwano

mfono (kwenye mkopo unaobaki)
nakopa 10m riba 17% kwa mwaka, muda wa mkopo miaka 5

soln
riba mwaka 1 = 10,000,000 x 17/100 = 1,700,000
mkopo unaobaki = 10,000,000 - 1,700,000 = 8,300,000

riba mwaka 2 = 8,300,000 x 17/100 = 1,411,000
mkopo unaobaki = 8,300,000 - 1,411,000 = 6,889,000

riba mwaka 3 = 6,889,000 x 17/100 = 1,171,130
mkopo unaobaki = 6,889,000 - 1,171,130 = 5,717,870

riba mwaka 4 = 5,717,870 x 17/100 = 972037.9
mkopo unaobaki = 5,717,870 - 972,037.9 = 4,745,832.1

riba mwaka 5 = 4745832.1 x 17/100 = 806,791.46

jumla ya riba zote za miaka mitano = 1,700,000 + 1,411,000 + 1,171,130 + 972037.9 + 806,791.46
= 6,060,959.4
jumla ya fedha unazodaiwa = mkopo + riba =10,000,000 + 6060959.4 =16,060,959.4

makato kwa mwezi = jumla ya fedha unazodaiwa gawa kwa idadi ya miezi = 16,060,959.4/12x5 = 267,682.65
 
Mkuu inaonekana haya mambo unayajua Jua.
Naomba kuuliza let's say umekopa milioni 13.5 unalipa miaka sita.(Miezi 72) Rejesho Kwa mwezi ni 308000.Ukawa umerejesha miaka miwili na nusu (Miezi 30) ambayo ni 9.24m.Sasa Kwa bahati nzuri ukataka kulipa deni lako au kukomboa mkopo wako.Ukaomba wakuangalizie deni lako( Balance) ili ulipe.Unakuta unadaiwa milioni 10.
Hapa naomba kuuliza mbona deni halipungui haraka? Ina maana miaka ya mwanzo unaanza kulipa Riba tu then badaye na mkopo wenyewe.Hesabu ipoje hapo?
 
Hiyo mil10 unayodaiwa ni pamoja na riba ya miaka iliyobaki lets say 3yrs. Ukitaka kufuta mkopo riba inaondolewa unalipa japo wana penalty ya 5%/6% ya kiasi bila riba.
 
Saiv wanasema wameshusha riba mpaka 17% ila kwa MTU aliechukua mkopo kipindi cha nyuma ukitazama alichukua hela nyingi sana kuliko wanazotoa sasa hivi mpaka najiuliza wanapigaje hesabu zao hasa CRDB maana kwa salary ile ile jamaa alipata milioni 12 kwa miaka mitano, leo hii mimi wanataka kunipa m9 na point.
 
nakatwa 270, ABC wamenipa 8
BancABC hao riba zao balaa, jamaa alikopa milioni 5.4 kwa miaka 6 kwa makato ya 191760 kila mwezi ambapo hapo ukizidisha pesa ya mwezi anayokatwa na muda wa miaka 6 ni Tsh million 13 na laki nane yani ni zaidi ya mkopo Mara mbili.

Kopa kote Ila Abc na Bayport hapafai kabisa.

Sehemu za kukopa ni nmb, crdb, nbc na posta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…