"Zamani nikiwa mjinga nilishawahi kuwa Mwenyekiti wa Vijana CHADEMA wilaya ya Iringa, lakini zamani hiyo hiyo, nikiwa mjinga zaidi nilishawahi kuwa Katibu wa CHADEMA jimbo la Isimani, nilikua mgombea wa Udiwani kata ya Mboliboli mwaka 2020 kupitia CHADEMA, Safari yangu kuikataa CHADEMA ilianza tarehe 20 mwezi wa saba pale Mwembetogwa nikiwa pamoja na Mchungaji Msigwa".
Pia soma: Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mchungaji Peter Msigwa ahamia CCM
Hayo yamesemwa na Richard Joseph Ligoha aliyekuwa Kiongozi ndani ya CHADEMA ambapo kwa sasa ni Mwanachama wa CCM, aliyasema hayo alipopewa nafasi ya kuzungumza katika Baraza la Vijana UVCCM Iringa Vijijini likiongozwa na Mwenyekiti wa UVCCM Iringa Vijijini, Eliah Kidavile.