zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
Habari za weekend wanajukwaa natumaini wote wazima bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye mada ya leo.
UTANGULIZI
Richard sorge a.k.a Ramsay alikuwa jasusi wa urusi ya zamani yaani Jamhuri ya kijamaa ya soviet (USSR) na alitumika wakati na kabla ya vita kuu ya pili ya dunia akiwa kama mwandishi wa habari huko ujerumani ya wakati wa hitler na japan akikusanya taarifa mbalimbali ambazo zilikuwa muhimu katika kuamua hatma ya vita kuu ya pili ya dunia na anatazamiwa kuwa moja ya majasusi muhimu zaidi katika historia ya tasnia hiyo.
Sorge alizaliwa nchini arzebaijan (iliokuwa chini ya Urusi) kwa mzazi wa kijerumani na mama wa kirusi mwaka 1895 na Baba yake alikuwa mhandisi wa uchimbaji madini huko Baku,Arzebaijan ila baadae wakarudi ujerumani. Alipofika miaka 18 alijiunga na jeshi la ujerumani na kupigana vita kuu ya kwanza ya dunia mwaka 1914 ila bomu lilimjeruhi vibaya mikono na miguu hivyo baadae aliachishwa jeshini. Wakati huu ndio ulibadilisha taswira nzima ya maisha yake maana aliingia kwenye tafakuri ndefu na kusoma vitabu vya kijamaa (karl marx) akaona alipigana vita isiyo na maana sababu hivyo akaamua kujiunga na sera za kijamaa/kikomunisti ambazo kwa muda ule zilikuwa zinatamalaki Urusi na wakati huo anahitimu masomo ya uchumi na baadae Siasa ngazi ya PhD akajiunga na chama cha kikomunisti cha ujerumani ila baada ya msimamo yake mikali alitimuliwa na akaamua kuhamia urusi ambako huko alichukuliwa kuwa jasusi wa Urusi ila aliyevaa uandishi wa habari mwaka 1924.
MISSION ZAKE
Moja ya mission zake akiwa kama jasusi wa urusi ilikuwa kupandikizwa china 1930-32,ujerumani na uingereza (1929) na japan 1933 ambapo kote huko alikuwa mwandishi wa habari mahiri na aliaminika hivyo kuwa nafasi nzuri ya kupata taarifa nyeti. Mfano ujerumani alikuwa mshabiki mkubwa wa hitler na alisoma vitabu vyake na kujichanganya na chama chao cha NAZI na aliaminika kiasi hata kiongozi mwandamizi wa NAZI Joseph goebbels alihudhuria sherehe ya kuagwa kwake pale alipotumwa kwenda kuripoti habari za japan kwa ajili ya magazeti ya ujerumani. Hivyo ushawishi wake huu ulimbeba hata alipoelekea japan ambapo alikuwa muandishi maarufu zaidi wa ujerumani maana Frankfurter Zeitung lilikuwa gazeti maarufu zaidi ujerumani na kikubwa zaidi akapewa cheo kisicho rasmi cha kuwa mshauri na msaidizi kwa balozi wa ujerumani huko japan!!! Yaani jikoni kabisa kiasi hata mipango ya kivita na kisiasa ya ujerumani ililetwa kwake ili amshauri balozi!!!
Pia akiwa japan alikuwa mkandiaji wa siasa za Urusi na alishabikia sana utawala wa kidikteta wa japan na Ujerumani hivyo kupendwa sana na mataifa hayo maadui wa Urusi. Akiwa huko alitengeneza timu ya watoa taarifa wake ambao walijipenyeza kwa kufungua biashara kubwa mwingine alifanyia kazi kampuni ya habari ya ufaransa n.k hao wote ndio walikuwa wakiongoza genge la majasusi hao urusi ambapo walifanikiwa kudukua siri nyingi za Hitler na Emperor Hirohito ambapo ziliisaidia Urusi kushinda vita kuu ya pili ya dunia.
UMAARUFU
Sorge ametambulika zaidi kwenye dunia ya kijasusi na inteligentsia kwa taarifa zake mbili muhimu zaidi ambazo ndio ziliamua kwa namna moja ama nyingine ushindi wa Urusi na kuangushwa kwa Adolf Hitler. Mwaka 1941-42 akiwa japan aliweza kuvujisha mpango wa Hitler kuvamia urusi hivyo ikawapa nafasi Urusi kufanya maandalizi mapema ya kimbinu kupambana na Hitler hivyo alipovamia haikuwa mshtuko zaidi waliweza kumzuia na mwishowe kumtandika na kumfurusha hadi ujerumani.
Ikumbukwe wakati huo wa uvamizi wa Ujerumani huko urusi ukiwa umepamba moto hasa battle ya "operation barbarossa" ambapo urusi ilionekana kuzidiwa jasusi huyu aliweza kudukua taarifa kuwa mshirika mkuu wa Hitler yaani Japan hana mpango wa kuingia upande wa hitler kuvamia Urusi maana alishapanga kuivamia marekani na uingereza huko pacific. Taarifa hii ilikuwa muhimu ikizingatiwa mnamo miaka ya 1930s japan ilishavamia jimbo la manchuria huko china ambalo lilikuwa linatawaliwa na Urusi na hivyo urusi ilimuona japan ni tishio kuliko ujerumani ukizingatia kwenye vita ya russo-japanese mwaka 1905 urusi alipigwa vibaya sana na wajapan hivyo walikuwa wamejaza majeshi kwenye mpaka wa mashariki ili kujihami na uvamizi wa majeshi ya japan.
Hivyo, uwepo wa taarifa hii muhimu ilisababisha warusi waondoe vikosi zaidi ya 18 yaani wanajeshi takribani laki 2 kutoka huko siberia iliyo karibu na japan na kuvielekeza moscow ambapo vilienda kuongeza nguvu kwa vikosi vilivyokuwa vinamzuia hitler kuivamia moscow na vikosi vile vilipowasili vilileta nguvu mpya na hivyo kumzidi nguvu hitler na ndipo ujerumani akachakazwa na tokea hapo nguvu yake ikamalizwa na mwishowe akapinduliwa na Urusi, yote haya ni kutokana na intelijentsia iliyotukuka ya bwana sorge.
MWISHO WAKE
Richard sorge mwezi mmoja baada ya kutoboa siri hii ya japan kwa Urusi na ambapo ujerumani alitandikwa, polisi walifanya msako mkali sana na inasemekana kuna mmoja wa kikundi chao alisaliti kwa kutoboa siri ya Sorge kuwa ni communist mwenzao!! Baada ya kukamatwa waliwekwa gerezani baada ya mateso makali mnamo November 7, 1944 Sorge na mwenzake alieitwa ozaki walinyongwa kwenye gereza la sugamo na ili kuwaumiza zaidi waliwanyonga siku ya kuadhimisha siku ya mapinduzi ya kikomunisti ya urusi. Na huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya jasusi huyu wa kirusi.
HITIMISHO
kuna mengi sana ameyafanya huyu mtu ila mengi yanatufundisha kuwa unaweza toa kafara furaha yako kwa ajili ya furaha ya wengine kama ambavyo sorge licha ya kuonywa aondoke Japan aligoma na hata kutumia pesa binafsi ili kuendesha genge lake maana alisukumwa na uzalendo kwa urusi na ndio maana hata alipokamatwa hakujuta wala kulialia aokolewe bali alifurahi maana alikuwa ameokoa nchi yake dhidi ya uvamizi wa kijeshi. Ila ambacho hakijapata majibu ya kueleweka je ni kipi hasa kilisababisha agundulike ilihali miaka yote 9 hakuwahi kushtukiwa i hope great thinkers wote humu mtanisaidia hapa
Naomba kuwasilisha
UTANGULIZI
Richard sorge a.k.a Ramsay alikuwa jasusi wa urusi ya zamani yaani Jamhuri ya kijamaa ya soviet (USSR) na alitumika wakati na kabla ya vita kuu ya pili ya dunia akiwa kama mwandishi wa habari huko ujerumani ya wakati wa hitler na japan akikusanya taarifa mbalimbali ambazo zilikuwa muhimu katika kuamua hatma ya vita kuu ya pili ya dunia na anatazamiwa kuwa moja ya majasusi muhimu zaidi katika historia ya tasnia hiyo.
Sorge alizaliwa nchini arzebaijan (iliokuwa chini ya Urusi) kwa mzazi wa kijerumani na mama wa kirusi mwaka 1895 na Baba yake alikuwa mhandisi wa uchimbaji madini huko Baku,Arzebaijan ila baadae wakarudi ujerumani. Alipofika miaka 18 alijiunga na jeshi la ujerumani na kupigana vita kuu ya kwanza ya dunia mwaka 1914 ila bomu lilimjeruhi vibaya mikono na miguu hivyo baadae aliachishwa jeshini. Wakati huu ndio ulibadilisha taswira nzima ya maisha yake maana aliingia kwenye tafakuri ndefu na kusoma vitabu vya kijamaa (karl marx) akaona alipigana vita isiyo na maana sababu hivyo akaamua kujiunga na sera za kijamaa/kikomunisti ambazo kwa muda ule zilikuwa zinatamalaki Urusi na wakati huo anahitimu masomo ya uchumi na baadae Siasa ngazi ya PhD akajiunga na chama cha kikomunisti cha ujerumani ila baada ya msimamo yake mikali alitimuliwa na akaamua kuhamia urusi ambako huko alichukuliwa kuwa jasusi wa Urusi ila aliyevaa uandishi wa habari mwaka 1924.
MISSION ZAKE
Moja ya mission zake akiwa kama jasusi wa urusi ilikuwa kupandikizwa china 1930-32,ujerumani na uingereza (1929) na japan 1933 ambapo kote huko alikuwa mwandishi wa habari mahiri na aliaminika hivyo kuwa nafasi nzuri ya kupata taarifa nyeti. Mfano ujerumani alikuwa mshabiki mkubwa wa hitler na alisoma vitabu vyake na kujichanganya na chama chao cha NAZI na aliaminika kiasi hata kiongozi mwandamizi wa NAZI Joseph goebbels alihudhuria sherehe ya kuagwa kwake pale alipotumwa kwenda kuripoti habari za japan kwa ajili ya magazeti ya ujerumani. Hivyo ushawishi wake huu ulimbeba hata alipoelekea japan ambapo alikuwa muandishi maarufu zaidi wa ujerumani maana Frankfurter Zeitung lilikuwa gazeti maarufu zaidi ujerumani na kikubwa zaidi akapewa cheo kisicho rasmi cha kuwa mshauri na msaidizi kwa balozi wa ujerumani huko japan!!! Yaani jikoni kabisa kiasi hata mipango ya kivita na kisiasa ya ujerumani ililetwa kwake ili amshauri balozi!!!
Pia akiwa japan alikuwa mkandiaji wa siasa za Urusi na alishabikia sana utawala wa kidikteta wa japan na Ujerumani hivyo kupendwa sana na mataifa hayo maadui wa Urusi. Akiwa huko alitengeneza timu ya watoa taarifa wake ambao walijipenyeza kwa kufungua biashara kubwa mwingine alifanyia kazi kampuni ya habari ya ufaransa n.k hao wote ndio walikuwa wakiongoza genge la majasusi hao urusi ambapo walifanikiwa kudukua siri nyingi za Hitler na Emperor Hirohito ambapo ziliisaidia Urusi kushinda vita kuu ya pili ya dunia.
UMAARUFU
Sorge ametambulika zaidi kwenye dunia ya kijasusi na inteligentsia kwa taarifa zake mbili muhimu zaidi ambazo ndio ziliamua kwa namna moja ama nyingine ushindi wa Urusi na kuangushwa kwa Adolf Hitler. Mwaka 1941-42 akiwa japan aliweza kuvujisha mpango wa Hitler kuvamia urusi hivyo ikawapa nafasi Urusi kufanya maandalizi mapema ya kimbinu kupambana na Hitler hivyo alipovamia haikuwa mshtuko zaidi waliweza kumzuia na mwishowe kumtandika na kumfurusha hadi ujerumani.
Ikumbukwe wakati huo wa uvamizi wa Ujerumani huko urusi ukiwa umepamba moto hasa battle ya "operation barbarossa" ambapo urusi ilionekana kuzidiwa jasusi huyu aliweza kudukua taarifa kuwa mshirika mkuu wa Hitler yaani Japan hana mpango wa kuingia upande wa hitler kuvamia Urusi maana alishapanga kuivamia marekani na uingereza huko pacific. Taarifa hii ilikuwa muhimu ikizingatiwa mnamo miaka ya 1930s japan ilishavamia jimbo la manchuria huko china ambalo lilikuwa linatawaliwa na Urusi na hivyo urusi ilimuona japan ni tishio kuliko ujerumani ukizingatia kwenye vita ya russo-japanese mwaka 1905 urusi alipigwa vibaya sana na wajapan hivyo walikuwa wamejaza majeshi kwenye mpaka wa mashariki ili kujihami na uvamizi wa majeshi ya japan.
Hivyo, uwepo wa taarifa hii muhimu ilisababisha warusi waondoe vikosi zaidi ya 18 yaani wanajeshi takribani laki 2 kutoka huko siberia iliyo karibu na japan na kuvielekeza moscow ambapo vilienda kuongeza nguvu kwa vikosi vilivyokuwa vinamzuia hitler kuivamia moscow na vikosi vile vilipowasili vilileta nguvu mpya na hivyo kumzidi nguvu hitler na ndipo ujerumani akachakazwa na tokea hapo nguvu yake ikamalizwa na mwishowe akapinduliwa na Urusi, yote haya ni kutokana na intelijentsia iliyotukuka ya bwana sorge.
MWISHO WAKE
Richard sorge mwezi mmoja baada ya kutoboa siri hii ya japan kwa Urusi na ambapo ujerumani alitandikwa, polisi walifanya msako mkali sana na inasemekana kuna mmoja wa kikundi chao alisaliti kwa kutoboa siri ya Sorge kuwa ni communist mwenzao!! Baada ya kukamatwa waliwekwa gerezani baada ya mateso makali mnamo November 7, 1944 Sorge na mwenzake alieitwa ozaki walinyongwa kwenye gereza la sugamo na ili kuwaumiza zaidi waliwanyonga siku ya kuadhimisha siku ya mapinduzi ya kikomunisti ya urusi. Na huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya jasusi huyu wa kirusi.
HITIMISHO
kuna mengi sana ameyafanya huyu mtu ila mengi yanatufundisha kuwa unaweza toa kafara furaha yako kwa ajili ya furaha ya wengine kama ambavyo sorge licha ya kuonywa aondoke Japan aligoma na hata kutumia pesa binafsi ili kuendesha genge lake maana alisukumwa na uzalendo kwa urusi na ndio maana hata alipokamatwa hakujuta wala kulialia aokolewe bali alifurahi maana alikuwa ameokoa nchi yake dhidi ya uvamizi wa kijeshi. Ila ambacho hakijapata majibu ya kueleweka je ni kipi hasa kilisababisha agundulike ilihali miaka yote 9 hakuwahi kushtukiwa i hope great thinkers wote humu mtanisaidia hapa
Naomba kuwasilisha