Richard Sorge: Jasusi aliyeamua hatma ya Vita kuu ya pili ya Dunia

aisee huyo jasusi kweli alikua na moyo mgumu, maana miaka ile kuwa mCommunist alafu ukaenda kujichanganya na wajerumani sio mchezo,

alafu inawezekana na ujasiri wake ulitokana na kwamba alishawahi kuishi ujerumani na kuwapigania vita kabisa....hasira ya kufukuzwa pia labda ilimfanya atake kuangusha utawala wa hitler,

sasa hapo kwenye ilikuaje akakamatwa lazima patakua na siri, haya mambo ya ujasusi kutoana kafara ni kawaida sana...huenda labda baada ya kufanikisha ushindi wa vita ile kubwa hakuitajika tena maana kumbuka pia jamaa alikua na asili ya mataifa yote mawili hapo....na mataifa yote yanajua umahiri wake na misimamo yake,

wanasema "prevention is better than cure" waRusi naona walijihami mapema labda....sina uhakika lkn.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unachosema ni kweli mkuu haya mambo ya ujasusi wakishakutumia wanakuwa hawakuamini tena wanaweza kukutoa kafara ikumbukwe huyu jamaa akiwa kizuizini wajapan waliweka mpango na warusi kwamba wabadilishane maspy wao waliokamatwa ila cha kushangaza alikataa dili hili maana alihisi jama anaweza kurudi kumbe akawa double agent!!! Hivyo wakaona wasimuokoe pia ukizingatia baba yake ni mjerumani naona hawakutaka kumuamini kabisa. All in all hawa jamaa huwa wana kazi ngumu sana ila cha kushangaza sifa zote wanapewa wanasiasa ilihali 80% ya mzigo wanaubeba majasusi.
 
wanaisasa ni wahuni tu...wanawatumia wengine kwa manufaa yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nataman siku zije story za majasusi wa Tanzania ambao waliisaidia nchi kwa namna moja au nyengine mpka tukafanikiwa jambo fulani. Maybe hatuna hao majasusi huku kwetu

sent using samsung galaxy s8
Wapo wengi tu,waulize makaburu wa south afrika,msumbuji,commoro,idd amini wa uganda,huwezi pigana vita bila ya kua na taarifa za uhakika za adui yako ukashinda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hii sababu imekuwa ikirudiwa na wachambuzi wa masuala ya kijeshi kwamba kama Hitler angeshambulia baada ya msimu wa baridi basi angempiga Stalin!!! Naweza kukubali kwamba Ujerumani alikuwa ana silaha na mbinu bora kuliko Urusi lakini pia tukumbuke chanzo hakikuwa hicho pekee kwa sababu ikumbukwe hitler alivamia Urusi kwa mara ya kwanza majira ya joto june,1941 kupitia mission ilioitwa operation barbarossa ila kuna wakati walikaribia moscow lakini hitler aliwaambia wasubiri kwanza na wavamie Kiev,ukraine hivyo wengine wanasema hiyo Subiri subiri ndio ilimponza hitler urusi na sio baridi hata kidogo sababu aliwapa muda wa kujipanga upya.

Ilipofika october hitler aliamua wavamie rasmi moscow (Baridi halijaanza). Walipovamia wakafika kilometer chache tu nje ya jiji lakini hali mbaya ya hewa hasa mvua ndio iliwakwamisha lakini pia ujerumani ilikuwa tayari inapigana maeneo mengi hivyo supply kama mafuta,chakula,silaha na watu ikawa ngumu kufikiwa haraka kwa misaada hiyo tofauti kama angeamua kuvamia urusi kwanza ndipo aanzishe vita nyingine maeneo mengine ssa akawa anapigana kuanzia Afrika mpaka ulaya magharibi, kaskazini na sasa ulaya mashariki yaani ni vita kila upande hii pia ilichangia sana kuwamaliza nguvu kiasi kwamba baridi lilipokuja ndio likamaliza kila kitu.

Pia hata wakati wa baridi ulipofika ujerumani bado waliweza kusogea mpaka kilometer 8 kutoka moscow ila walishakuwa wameishiwa supply za kutosha na hata majenerali waliposema waretreat ili wajipange upya hitler alikataa hivyo warussia walipo counter-attack waliweza kummaliza kabisa nguvu ujerumani za kushambulia tena na tokea hapo ujerumanu haikuweza kurudisha nguvu zake

Kiufupi maamuzi mabovu ya hitler,kupigana vita nyingi kwa wakati mmoja,ukubwa wa ardhi na wingi wa watu urusi na ikichangiwa na hali ya hewa ndio ilipelekea ujerumani kupigwa ila tukisema baridi pekee haitakuwa kweli maana walishaanza shambulia wakati wa kiangazi

Labda mtaalam Malcom Lumumba atupe maoni yake
 
Mkuu zitto junior hongera kwa bandiko zuri, tunahitaji mabandiko kama haya.
Naomba nisiseme sana lakini ni kwamba NKVD walikuwa wametambaa dunia nzima wakieneza ukomunisti hasa baada ya Stalin kuwa kiongozi ndiyo wakafika hadi Marekani. Kuhusu kukamatwa hao majasusi wa Urusi kikubwa ni kwamba Ujerumani kabla ya vita alikuwa anashirikiana na Uingereza na Ufaransa (Anti Communist Coalition) katika kupambana na ukomunisti barani ulaya. Jambo jinge ni kwamba Ujerumani alikuwa na shirika la kijasusi la kijeshi kama The Abhwer ambalo liliundwa tokea kipindi cha wakina Kaiser Wilhelm na kuja kufahamika rasmi mwaka 1921 . Ukisoma harakati za Abhwer utakuja kushangaa kwamba walikuwa na mtandao mzito sana barani ulaya hata kabla ya vita ya kwanza ya dunia, na baada ya kuchukua madaraka mwaka 1933 Hitler aliendelea kulitumia hilo shirika mpaka mwaka 1945.
 
Mkuu nimekuelewa sana ila najiuliza hivi inakuaje system zina rely kwenye taarifa za spy moja kiasi anaweza kuwa double agent na kuwauza.... Mfano sorge hapo ingekuwa amewauza kuwa japan hawatovamia urusi in the near future hivyo wangehamisha majeshi yote moscow ssa ingetokea Japan anavamia siberia si ingekuwa catastrophic?? Kwa faida ya sote humu unaweza kutusaidia jinsi wanavyoweza kuhakiki uhakika wa taarifa za kijasusi kabla hawajazikubali maana inashangaza jinsi gani mtu anaweza kuwa pandikizi wanashindwa kugundua na wanaamini taarifa zake bila kuwaza mara mbili.

Cc Richard
 

Hahaha,
Mkuu Zitto kule Japan George hakuwa peke yake, kulikuwa na jasusi mwingine kama Hotsumi Ozaki ambaye alikuwa mshauri wa Waziri Mkuu wa Japan. Kikubwa zaidi Intelligence Bureau huwa zikipata taarifa huwa hawazifanyii kazi moja kwa moja tu inabidi zichambuliwe na zithibitishwe halafu yafanyike maamuzi.


Pia jasusi anapopelekwa kufanya kazi sehemu mara nyingi lazima hasa nje ya mipaka lazima huwa anakuta mazingira yameshaandaliwa na Jasusi Mkazi (Resident Spy) au Handler ambao mara nyingi huwa mabalozi au maafisa ubalozi. Hivyo taarifa nyingi za kijasusi huwa hazitoki kwa jasusi moja kwa moja kwenda kwa mkuu wa nchi, bali hutoka kwa jasusi (Field Officer) kwenda kwa Jasusi mkazi (Resident Spy) ambaye yeye na jopo lake ambao wako kwenye nchi ya adui huweza kufanya uthibitisho wa taarifa.

Kikubwa jasusi kama Sorge huwa hafanyi kazi peke yake bila kuwa anafuatiliwa au mashirika ya kijasusi kuwa na leverage kwake. Ndiyo maana anaweza kuwa yuko Japan lakini familia yake iko Moscow, akituma taarifa za wongo imekula kwake. AU NKVD na KGB walikuwa na mchezo wa kufanya recruitment kwa njia ya Honey Trap au Rushwa. Ambapo wanakulazimisha uwapelekee taarifa au wanavujisha mauchafu yako. Kuna jasusi wa MI6 aliwahi kufanyiwa hivyo: Sasa kwa mwendo huo sidhani kama litakuwa jambo la busara kuwadanganya waliokutuma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…