Richmond case study: Je, Waziri Mkuu Majaliwa atavuka kikwazo cha Lowassa kwa ma-V 8 haya?

Richmond case study: Je, Waziri Mkuu Majaliwa atavuka kikwazo cha Lowassa kwa ma-V 8 haya?

USSR

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2015
Posts
10,904
Reaction score
26,184
Balozi wa USA Mark Green kipindi cha Richmond aimbia dunia kuwa kilichomponza Lowassa ni kuonekana ni tishio kwa wanaotazamiwa kumrithi Kikwete (alipaniwa).

Hapa kuna mtu anayeonekana kuwa frontline kumrithi Magufuli kwa uwezo, utendaji, dini, ukanda na umri, Kassim Majaliwa anazunguka zongo linalomuandama la magari ya kufru yaliyopitishwa chini ya ofisi zake, yalipitishwaje na mtu anayeonekana yupo makini sana walioko chini yake wanamnyooshea kidole.

Akihojiwa na tume ya Dkt. Mwakyembe na baadae bungeni aliyekuwa naibu waziri wa nishati na madini wa wakati huo Ibrahim Msabaha anasema "Naona mimi nitakuwa mbuzi wa kafara kwa hili " maDED wote wanasema ihojiwe ofisi ya waziri mkuu wao wasiwe mbuzi wa kafara.

Kama umemsiliza waziri mkuu kule Mwanza anaona kuwa wenye makosa ni walioitisha ombi la ununuzi wa magari hivyo wawajibike baada ya uchunguzi, walioagiza wanasema shida sio wao kuomba maana ombi lina kukubaliwa na kukataliwa hivyo aliyelipokea na kuidhisha ndie mchawi hapa na huyu si mwingine ni ofisi ya waziri mkuu.

"Tulifuata utaratibu wa ununuzi wa umma kuanzia kwenye kamati ya halmashauri, baraza la madiwani, wizara ya ujenzi na baadae ofisi ya waziri mkuu" DED wa Geita anaongea kwa kujiamini kuwa kwa nini walipewa na aliyetoa anasema kwanini waliomba, kuna utata hapa.

Watanzania hawataki kujua mambo ya nani aliomba na nani alitoa wanataka kufahamu kwanini pesa zao million 400 zote zinunue gari la mtu mmoja tu huku wakiwa na matatizo chungu mzima.

Rais anaonekana yuko wa wananchi wanaolia pesa zao kufujwa na kutaka waliohusika wawajibishwe, waliohusika wanarushiana mpira.

Kwa kuwa hofu kuwa Majaliwa anaandaliwa hakuna anayeweza kumhoji na badala yake yeye ndio anahoji (hapa kuna utata).

Maadui wa Majaliwa kisiasa wanaojipanga kuelekea 2025 wanakesha wanachochea kuni ili kitumbua kiiingie mchaga.

My take; Ule msemo wa kuwa waziri mkuu wa Tanzania hawezi kuwa Rais unaweza ukajitokeza hapa tena!

Soma

USSR
 
Jambo hili linafikirisha sana, binafsi linamuweka njia panda hon Majaliwa, ni kweli isiyo shaka kuwa majaliwa ndiye anayeoneka kufaa zaidi kumrithi JPM, hii ni kutokana na uchapa kazi alionao Hon. Majaliwa

Hoja iko hapa je mwanafunzi aliyeomba ruhusa isiyo halali na baadae mwalimu kumruhusu aende huku huyu mwalimu akijua kuwa ruhusa aliyotoa siyo halali, je, mwenye makosa ni mwalimu au mwanafunzi?

Mungu amnusuru PM na hili janga
 
Jengeni mifumo imara acheni kujenga personalities! Zile VX-R V8 T CCM 2020 zilizofunika nchi nzima kwa maelfu ziliidhinishwa na nani? Ni mali ya CCM? Zinafanya nini kwa sasa? Kama kuna kipindi ubadhirifu wa kutisha umewahi kufanyika nchi hii.
 
Jambo hili linafikirisha sana,binafsi linamuweka njia panda hon Majaliwa,ni kweli isiyo shaka kuwa majaliwa ndiye anayeoneka kufaa zaidi kumrithi JPM, hii ni kutokana na uchapa kazi alionao hon.Majaliwa

Hoja iko hapa je mwanafunzi aliyeomba ruhusa isiyo halali na baadae mwalimu kumruhusu aende huku huyu mwalimu akijua kuwa ruhusa aliyotoa siyo halali ,je, mwenye makosa ni mwalimu au mwanafunzi?
Pale ofisi ya PM kuna shida sana na yule DED namuona chenga sana, sisi hatuhitaji kujua mambo ya PPRA tunahoji kiwango cha pesa hivi anafikiri shida ni magari tu
 
Kiuhalisia Mheshimiwa waziri mkuu amelamba mchanga, nilimuona juzi Kati katika vyombo vya habari akiwa Mwanza akijaribu kuukwepa huu msalaba huku akionekana mwenye wasi wasi Sana.

Haya yanafanyika kwa kuidhinishwa na ofisi yake, Je, anapataje uhalali wa kulalamikia haya manunuzi ya hilo Shangingi la kijapani? 400 Milioni taslimu za kitanzania zinaweza kusaidia vijiji zaidi ya nane kuchimba visima vya maji.

Kuna shida sehemu, he can't avoid this allegation against his office.
 
Moja kati ya mjadala bora sana hapa jukwaani.

Katika suala hili la magari haya ya vigogo huenda likawa doa kwa Mh. Majaliwa. Ile sifa yake ya utendaji na uchapa kazi huenda ikaharibiwa na skendo ndogo tu hii kama asipokuwa makini.

Mtu pekee anayeweza kumuokoa mh Majaliwa ni mh jiwe. Kama kweli Majaliwa ana nia ya dhati kuongoza taifa hili, naomba ajinyenyekeze kwa jiwe kutoka katika hili.

Nasema jiwe kwa sababu, ukubali au ukatae Magufuli ndio mtu pekee mwenye ushawishi wa namna yoyote kwa sasa hapa Bongo.
Lakini pia skendo hii hii inaweza kumtemesha kibarua mh. Majaliwa."waziri mkuu hana guarantee "_jiwe siku ya kumuapisha majaliwa.
Yote kwa yote tusubiri mda utaongea.

#jr
#uvccm taifa
 
Jambo hili linafikirisha sana,binafsi linamuweka njia panda hon Majaliwa,ni kweli isiyo shaka kuwa majaliwa ndiye anayeoneka kufaa zaidi kumrithi JPM, hii ni kutokana na uchapa kazi alionao hon.Majaliwa

Hoja iko hapa je mwanafunzi aliyeomba ruhusa isiyo halali na baadae mwalimu kumruhusu aende huku huyu mwalimu akijua kuwa ruhusa aliyotoa siyo halali ,je, mwenye makosa ni mwalimu au mwanafunzi?
Mwalimu ndiye mwenye makosa.
 
Jambo hili linafikirisha sana,binafsi linamuweka njia panda hon Majaliwa,ni kweli isiyo shaka kuwa majaliwa ndiye anayeoneka kufaa zaidi kumrithi JPM, hii ni kutokana na uchapa kazi alionao hon.Majaliwa

Hoja iko hapa je mwanafunzi aliyeomba ruhusa isiyo halali na baadae mwalimu kumruhusu aende huku huyu mwalimu akijua kuwa ruhusa aliyotoa siyo halali ,je, mwenye makosa ni mwalimu au mwanafunzi?
... the final approver must be accountable.
 
Kiuhalisia Mheshimiwa waziri mkuu amelamba mchanga, nilimuona juzi Kati katika vyombo vya habari akiwa Mwanza akijaribu kuukwepa huu msalaba huku akionekana mwenye wasi wasi Sana....
Mkuu unaonaje kama atawatimua wote waliopitisha hili na waliomba hili na yale magari yauzwe tununue madawati ya form one ili ajisafishe badala ya kusubiria tume ya uchunguzi inayopoteza muda bure na magari yanazidi kuchakaa (depreciation )
 
Pale ofisi ya pm kuna shida sana na yule DED namuona chenga sana sisi hatuhitaji kujua mambo ya PPRA tunahijo kiwango cha pesa hivi anafikiri shida ni magari tu
Hata hivyo naona Kuna Vita ya wazi inaweza kuibuka Kati ya;

1. Msukuma dhidi ya DED & PM
2. PM dhidi ya Msukuma
3. DED dhidi ya PM maana hata kubali abebe msalaba pekee.

Hapa lazima mwisho mbaya.
 
Mkuu unaonaje kama atawatimua wote waliopitisha hili na waliomba hili na yale magari yauzwe tununue madawati ya form one ili ajisafishe badala ya kusubiria tume ya uchunguzi inayopoteza muda bure na magari yanazidi kuchakaa (depreciation )
... hayo mamigari ya 400m/- yaliyojaa kama utitiri huko serikali ya wanyonge utamuuzia nani? Hayanunuliki jombaa labda watanzania wachache mno na wenye uwezo huo wanaagiza brand new hawanunui used mengine yamewekewa matunguli na walioyatumia!
 
Mkuu unaonaje kama atawatimua wote waliopitisha hili na waliomba hili na yale magari yauzwe tununue madawati ya form one ili ajisafishe badala ya kusubiria tume ya uchunguzi inayopoteza muda bure na magari yanazidi kuchakaa (depreciation )
Itakuwa vyema sana lakini haitaondoa ukweli kuwa Hilo Ni doa kubwa Sana, pia inaweza kutafsiriwa kuwa amewatoa kafara hao watendaji wake ili yeye abaki salama.
 
... hayo mamigari ya 400m/- yaliyojaa kama utitiri huko serikali ya wanyonge utamuuzia nani? Hayanunuliki jombaa labda watanzania wachache mno na wenye uwezo huo wanaagiza brand new hawanunui used mengine yamewekewa matunguli na walioyatumia!
Tunaweza kuyauza nje wapo watu wanaweza kununua au kuuuzia asasi za kiraia ishu ya matunguli sio ishu sana
 
Back
Top Bottom