Ridhiwani Kikwete amezindua Kikao kazi cha Mafunzo kwa Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi

Ridhiwani Kikwete amezindua Kikao kazi cha Mafunzo kwa Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
MHE. RIDHIWANI AZINDUA KIKAO CHA WENYEVITI MABARAZA YA ARDHI NA NYUMBA, ASISITIZA UADILIFU NA KUKEMEA VIKALI RUSHWA.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Ridhiwani Kikwete Jana Aprili 05, 2022 amezindua Kikao kazi cha Mafunzo kwa Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya nchini, Kikao chenye lengo la kuwaongezea Wenyeviti hao mafunzo ya namna bora ya kuendesha mashauri ya Ardhi.

Uadilifu unaolenga haki ndiyo msingi wa kumaliza mashauri yanayopelekwa Kwenye Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya, alihimiza Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza na Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi, Waliokutana Tanga.

Katika Kikao hicho pia, Mhe. Ridhiwani amekea vikali rushwa katika Mabaraza ya Ardhi na kusisitiza kuondoa mlundikano wa mashauri ili haki itendeke kwa wakati.

Kikao hicho cha Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kinacholenga kuwaongezea ujuzi zaidi wa kutatua migogoro mbalimbali ya Ardhi ni cha siku 4 na kimeanza Aprili 04 na kinatarajiwa kumalizika kesho Alhamisi tarehe 07 Aprili 2022.

IMG-20220406-WA0006.jpg


IMG-20220406-WA0007.jpg

IMG-20220406-WA0008.jpg


IMG-20220406-WA0002.jpg

IMG-20220406-WA0003.jpg

IMG-20220406-WA0004.jpg

IMG-20220406-WA0005.jpg
 
Huwez zuia rizk ya mtu utaichelewesha tu. Ridh1, Nape, January na Kinana ni mfano. Pia Hussein Bashe 2010 alivyofanyiwa fitina Nzega na Kigwa.

Uzuri wa hawa maborn town wanakupotezea kimaksud ila baadae. Huoni wanavyompotezea Bashite hadi analeta dharau eti anatazoom. Hawanaga haraka.
 
Vikao vingine vipunguzwe, kubana matumizi ya serikali. Fedha zielekezwe kwenye sekta za msingi kama mafuta ili kupunguza gharama za maisha. Vitu vingine vinahitaji maamuzi magumu kama ya Jiwe, mfano, fedha za kukimbiza mwenge nchi nzima zipo ila fedha za kustabilize bei ya nishati hakuna. Fedha zitolewe kulingana na umuhimu hasa wa maisha ya watanzania wanyonge
 
Kuna kikao au jambo lolote, Waziri atafanya hapo wizarani bila ya kuomba kibali/ruhusa ya naibu waziri.?
 
Back
Top Bottom