Ripoti: Askari 6 wa Uhifadhi wameuawa kwa kushambuliwa na Wananchi Mwaka 2022

Ripoti: Askari 6 wa Uhifadhi wameuawa kwa kushambuliwa na Wananchi Mwaka 2022

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Jeshi la Uhifadhi la Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba, 2022, limepoteza askari sita kwa kuuawa baada ya kushambuliwa na wananchi nyakati tofauti, wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya uhifadhi.

Kamishna wa Uhifadhi TFS, Profesa Dos Santos Silayo, alisema hayo Desemba 21,2022 wilayani Mvomero, mkoani Morogoro, alipotembelea kituo cha hifadhi ya msitu wa Pagale, ambacho kilivamiwa na watu zaidi ya 50 kwa lengo la kutaka kuwadhuru askari wa uhifadhi wa kituo hicho .

Profesa Silayo alisema matukio hayo yametokea kwa nyakati tofauti katika kipindi cha kuanzia Januari 2022 hadi Desemba 2022 katika hifadhi za Kanda ya Magharibi, Kanda ya Ziwa na Kanda ya Mashariki.

"Tunalaani vikali matukio haya ya uvamizi katika vituo vyetu, ambao umesababisha hasara kubwa kwa serikali, lakini hata kugharimu maisha ya askari wetu sita tangu mwaka huu umeanza pamoja na raia, ambao wamekuwa wakitusaidia katika uhifadhi kusabaishiwa ulemavu wa kudumu," alisema Profesa Silayo.

Chanzo: Habari Leo
 
Watuambie pia ni wananchi wangapi waliuawa kwa kushambuliwa na askari wa hifadhi kwa mwaka 2022,tusizungumzie askari tu maana nao wanaua raia,wengine wanawapa ulemavu wa kudumu au kuwafilisi ila hatuambiwi.

Wananchi nani anawazungumzia?
 
Watuambie pia ni wananchi wangapi waliuawa kwa kushambuliwa na askari wa hifadhi kwa mwaka 2022,tusizungumzie askari tu maana nao wanaua raia,wengine wanawapa ulemavu wa kudumu au kuwafilisi ila hatuambiwi.

Wananchi nani anawazungumzia?
Welldone mkuu kwa comment nzuri ambayo ipo fair, tunahitaji two sides of story, upumbavu mtoa taarifa ni professor!,hope's sip wa majalalani
 
Watuambie pia ni wananchi wangapi waliuawa kwa kushambuliwa na askari wa hifadhi kwa mwaka 2022,tusizungumzie askari tu maana nao wanaua raia,wengine wanawapa ulemavu wa kudumu au kuwafilisi ila hatuambiwi.

Wananchi nani anawazungumzia?
Askari wa TFS hata kirungu hawana sasa wataua mwananchi kwa mikono? Wananchi, hasa wafugaji, acheni kuvamia hifadhi za taifa.
 
Kwa mwaka kupotezA Askari 6 kwenye uhifadhi..sounds genocidal
 
Matumizi ya kutumia nguvu siyo tiba ya changamoto za Uhifadhi. Nchi nyingi za Kiafrika zinadhani kutumia nguvu dhidi ya raia inaweza kuwatisha Wananchi na kufanikiwa kulinda rasilimali hizi. Masuala ya rasilimali za Wanyama na Misitu yanahitaji kushughulikia mzizi wa sababu za changamoto hizi. Matumizi ya nguvu yanaleta chuki, na hizi chuki zinaleta vita dhidi ya wahifadhi na raia.
 
Pakitokea changamoto mahali siyo suala la kukimbilia kutumia nguvu, inabidi kukaa chini na kujiuliza ni kwa nini raia hao wameamua kufanya hivyo kisha tushughulikie sababu zilizopelekea wao kufanya hivyo.
 
Maaskari wa wanyama Pori ndo Askari wenye roho mbaya kuliko Askari yyte duniani, wala rushwa na wakatili ajabu
Bora ukutane na mnyama mkali porini unaweza ukanusurika kuliko hao jamaa wakuweke mtu kati.
 
Askari wa wanyama pori ni wanyama kuliko wanyama wenyewe!
Hawa ndio Askari katili kuliko wote
 
Kama Haujawahi kukutwa na mkasa wa hao Jamaa ataongea siasa sana humu
Ila jamaa wana roho mbaya Kuliko Mtu yyt yule hapa Duniani
Ni wakatili, na Hawaogopi kukufanya chochote kile wanachojisikia!!
 
Waache ubabe na ukatili wa kikaburu dhidi ya watanganyika wenzao, wajenge mahusiano mazuri na jamii zinzozunguka hifadhi, after all hao ndio waliozitunza hizo hifadhi na ndio wazawa.
 
Nchi hii MTU akishakua Askari hata wale SUMA JKT wa benki, wanajiona matawi kweli.
 
Askari wa TFS hata kirungu hawana sasa wataua mwananchi kwa mikono? Wananchi, hasa wafugaji, acheni kuvamia hifadhi za taifa.
Unaishi nchi gani wewe?Kama hujui kusoma basi angalia hata picha
1671637086085.jpg
 
Back
Top Bottom