Ripoti Maalumu Mikopo Chechefu, Mabilioni ya Shilingi yakwapuliwa, wengine wagoma kulipa

Ripoti Maalumu Mikopo Chechefu, Mabilioni ya Shilingi yakwapuliwa, wengine wagoma kulipa

PendoLyimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
969
Reaction score
1,055
JItihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kukaribisha na kuhamasisha uwekezaji wa ndani na kutoka nje ya nchi kuja kuwekeza nchini unaelezwa kutiwa kigingi na tabia chafu inayozidi kuota mizizi ya baadhi ya wafanyabiashara wakubwa kushirikiana na baadhi ya majaji wa mahakama kuu wasio waaminifu kuyatapeli mabenki ya ndani na nje ya nchi kwa na hivyo kuwanyima fursa wafanyabiashara wadogo na wakati kushindwa kuaminiwa na kupata mikopo.

Orodha ya wafanyabiashara wanaotumia mahakama kutapeli na kudhulumu mabenki iliyofanyiwa uchunguzi na kuthibitishwa na gazeti hili, inaonyesha kuwa wengi kati ya wafanyabiashara hao wanajihusisha na biashara za Mafuta na ushafirishaji ambapo wastani wa shilingi za kitanzania Trilioni 1.3 wamekopa katika benki mbalimbali za ndani nan je ya nchi na kukataa kulipa kisha kukimbilia mahakamani ambako pia wanadaiwa kupata ushindi kwa njia zisizo za kawaida

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wafanyabiashara hao wanaoheshimika nchini wakionekana machoni mwa watu kuwa ni matajiri na wengine wakijionyesha kama wacha Mungu na wenye kumuogopa Mungu huku wengine wakijinasibu kama wana michezo na wawekezaji wakubwa wanaitumia mahakama hasa mahakama ya biashara kama kichaka chao cha kufanyia uhalifu huo wa kimkakati

Mfanyabiashara wakubwa wadaiwa kudhulumu mabenki kutumia mahakama

Wachota mabilioni ya akiba za wateja na kujinufaisha, wagoma kulipa wkimbilia mahakamani mahakama yabariki.

Mmoja akwapua bilioni 40 TADB, akakwapua bilioni 70 Azania, akakwapua bilioni 110 Equity kisha akapiga bilioni 220 ujerumani.

Mwengine kachukua bilioni 15 NMB, akachukua bilioni 80 EQUITY akagoma kulipa akakimbilia mahakamani Jaji akampa ushindi anaendelea kutanua mitaani.

Jaji huyo huyo na kwa staili hiyo hiyo akampa ushindi mfanyabiashara mwingine aliyekwapua dola milioni 15 KCB.

Jitihada za Rais Dkt. Samia kuvutia uwekezaji zinazidi kukwamishwa, BOT, TIC, watakiwa kujipanga upya

Chanzo: Jamvi la Habari

Pia soma:
 
Nilistuka sana lkn nilivyoona habari imeletwa na kipeperushi cha kufungia vitumbua nimeishia kusunya.....
 
Hapa kunaupigaji mkubwa sana na serikali inatakiwa itolemacho sana Mambo ya mataasisi kuiba HeLa za watu na kukimbilia mahakaman
 
Jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kukaribisha na kuhamasisha uwekezaji wa ndani na kutoka nje ya nchi kuja kuwekeza nchini unaelezwa kutiwa kigingi na tabia chafu inayozidi kuota mizizi ya baadhi ya wafanyabiashara wakubwa kushirikiana na baadhi ya majaji wa mahakama kuu wasio waaminifu kuyatapeli mabenki ya ndani na nje ya nchi kwa na hivyo kuwanyima fursa wafanyabiashara wadogo na wakati kushindwa kuaminiwa na kupata mikopo.

Orodha ya wafanyabiashara wanaotumia mahakama kutapeli na kudhulumu mabenki iliyofanyiwa uchunguzi na kuthibitishwa na gazeti hili, inaonyesha kuwa wengi kati ya wafanyabiashara hao wanajihusisha na biashara za Mafuta na ushafirishaji ambapo wastani wa shilingi za kitanzania Trilioni 1.3 wamekopa katika benki mbalimbali za ndani nan je ya nchi na kukataa kulipa kisha kukimbilia mahakamani ambako pia wanadaiwa kupata ushindi kwa njia zisizo za kawaida.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wafanyabiashara hao wanaoheshimika nchini wakionekana machoni mwa watu kuwa ni matajiri na wengine wakijionyesha kama wacha Mungu na wenye kumuogopa Mungu huku wengine wakijinasibu kama wana michezo na wawekezaji wakubwa wanaitumia mahakama hasa mahakama ya biashara kama kichaka chao cha kufanyia uhalifu huo wa kimkakati.

hebu fikiria, mtu amekwenda TADB amekopa bilioni 40, akaenda Azania benki akakopa bilioni 70, hajaishia hapo akaenda Equity benki akakopa bilioni 110, halafu akapanda ndege hadi ujerumani akavidanganya baadhi ya viwanda vya huko kuwa anaenda kuwekeza mafuta Kahama, nako wakamkopesha mali na mtaji wa zaidi ya bilioni 220, halafu anakataa kulipa mkopo makusudi kwa kukimbilia Mahakamani na Jaji anampa ushindi bila kuzingatia Ushahidi na ukweli kuwa hizo bilioni 220 za ndani na bilioni 220 alizochukua ujerumani zote kwa pamoja zinaingia kwenye deni la Taifa na kukataa kwake kulipa mkopo kunatunyima fursa sisi wafanyabiashara wadogo kuaminiwa’’. Anasema Christopher Kabison mfanyabiashara wa vifaa vya simu Kariakoo

Kabison anaongeza kuwa kama Serikali haitachukua hatua za haraka kuingilia kati hali hii basi jitihada za Rais kutaka mabenki yakopeshe wafanyabiashara kwa riba nafuu zitabaki kuwa ndoto kwani hakuna benki itakayokuwa tayari kuendelea kupoteza mitaji yake huku mahakama zinazotarajiwa kuwa ni sehemu ya haki zikitumika kuhalalisha uchafu huo

‘’juzi nilikuwa napitia hukumu za mahakama, nimeshuhudia jaji mmoja amempa ushindi Stati oili ambaye alikopa dola milioini 26 equiti benki halafu akakataa kulipa, ukizipitia hizi hukumu unaweza ukajiuliza kama jaji wakati anatoa hukumu alikuwa sawa sawa ama ameonja kidogo..na jaji huyo huyo akahukumu hukumu kama hiyo kwa kampuni ya derina ambayo ilikopa zaidi ya bilioni 40 na kukataa kulipa benki ya KCB. Sasa hapa tukisema mahakama inatumika kuhalalisha ujambazi dhidi ya watanzania tutakuwa tumeionea’’. Aliongeza Kobisoni

Kwa mujibu wa taarifa na nyaraka ambazo gazeti hili linazo zinaonyesha kuwa miongoni mwa makampuni yanayoongoza kufilisi mabenki huku wakitumia mahaka ni pamoja na KOM GROUP ambayo imeweka kibindoni zaidi ya bilioni 440 na kukataa kulipa na kuziacha solemba benki za TADB,AZANIA pamoja na EQUITY sambamba na ujerumani

Wengine wanaoongoza genge la kukwamisha jitihada za Rais Dkt. Samia katika kukuza mitaji ya wafanyabiashara wadogo na wa kati kwa kukataa kulipa mikopo na kisha kukimbilia mahakamani na mahakama kuwapa hukumu za ushindi ni pamoja na kampuni ya TSN iliyozidhulumu benki za NMB na Equity, Derina Group iliyozidhulumu benki za CRDB na KCB huku BIG BON ikitajwa kuidhulumu benki ya NBC kama ambavyo Masasi construction inavyopambana kuidhulumu benki ya Equity kwa kutumia mahakama

Sambamba na kampuni hizo, nyingine ni Global Agency, State Oil inayomilikwa na Nilesh Suchak kama ilivyo kwa NAS HAULIERS na Continental reliable zinazotamba kuwadhulumu CRDB, NMB, NBC,EQUITY, KCB na nyinginezo

Ikiwa kitendo hiki cha wafanyabiashara hawa wakubwa kukopa na kuacha kulipa madeni kisha kukimbilia mahakamani na mahakama kuwapa ushindi kitaachwa kuendelee kuota mizizi kitapelekea Taifa kuwa na kikundi ‘GANG’ cha wafanyabiashara wanaoutawala Uchumi wa nchi na hivyo kuhatarisha amani ya Taifa

Kuwepo nje ya mzunguko wa benki hizi mabilioni hayo ya shilingi ni kiashiria kibaya katika ukuzaji wa Uchumi huku Gavana wa benki kuu akiombwa kuchukua hatua za haraka kuingilia sintofahamu hii inayozidi kushika kasi

"Kama BOT hawatakuwa serious na kuingilia kati kunusuru hili jambo, benki zitafungwa hizi, ama zisipofungwa basi Uchumi utahama kutoka kuwa rasmi na kuwa Uchumi wa kihuni unaondeshwa na wahuni, lazima benki kuu iingilie kati haraka’’. Alisema Juma Hamad mchambuzi wa masuala ya kiuchumi
 
MTANDAO MPANA MIKOPO CHECHEFU

- Orodha ya mabenki na makampuni waliokopa mikopo na kukataa kurejesha kisha kukimbilia mahaamani yaendelea kuvuja

- kampuni za UKOD OIL ,Oil com, Dar Lux, Uhuru height, Sumry Buses, Chobbo Investments na Global Agency zachota zaidi ya bilioni 200 Stanbic, CRDB,EXIM, na NCBA

- Wakopaji waliokacha madeni wanatamba kumiliki magari ya kifahari na apartments zinazotokana na pesa za dhuruma

Na Mwandishi wetu,

Wakati vijana wa kitanzania, kina mama na walemavu wakishangilia kurejeshwa kwa mikopo ya asilimia 10 ya Halimashauri mikopo ambayo hapo awali walikuwa wakikopeswa kwa vikundi vikundi ili kujikimu na Maisha kwa kushindwa kukopeshwa na mabeki kwa kinachoitwa kukosekana kwa vigezo vya kukopesheka, imebainika kuwa mabilioni yanayotafunwa na wafanyabiashara wanaokopa benki na kukataa kulipa wakitumia mahakama mchakato wake unaratibiwa na mtandao mpana nchini

Taarifa zinasema kuwa kampuni za UKOD OIL ,Oil com, Dar Lux, Uhuru height, Sumry Buses, Chobbo Investments na Global Agency zachota zaidi ya bilioni 200 Stanbic, CRDB,EXIM, na NCBA huku wakopaji waliokacha madeni wanatamba kumiliki magari ya kifahari na apartments zinazotokana na pesa za dhuruma

Inaelezwa kuwa kampuni ya Ukod oil international imekopa na kulitekeleza deni la shilingi bilioni 25 kwa benki ya Stanbic wakati Global Agency wao wakiitapeli CRDB kiasi cha bilioni 26 sambamba na Abla Apartment walioidhulumu benki hiyo bilioni 13 huku uhuru height wakipiga shere Exim benki kiasi cha dola milioni 25

Wengine ni kampuni yam abasi ya Sumry iliyoichabanga CRDB bilioni 11 na kuingia mitini huku Dar Lux yenyewe ikiibia benki ya NCBA bilioni 19 wakati chobbo investment ikitafuna bila huruma bilioni 12

Zaidi tembelea www.jamvilahabari.co.tz


View: https://x.com/JAMVILAHABARI/status/1782984441524101140?t=ElYU8gUdN_q1OoFlJr9iWQ&s=09
 
Hii inaonekana kama ni Nongwa au Husda au kutaka kuchafuana hivi.
Hao wakopaji walikopa kwa utaratibu naamini katika utaratibu huo kuna dhamana waliweka ili ikitokea wameshindwa kulipa "Defaulting" dhamana zao zikamate ziuzwe kufidia deni.
Au hizo benki ziliwakopesha bila dhamana, si washike dhamana au wafanye "Claim of ownership"?

Hakuna mahakama duniani inaweza mtetea Mkopaji alieshindwa kulipa deni yaani "Defaulter" anaedaiwa kwa utaratibu. Mahakama huwa inahakikisha tuu utaratibu unafuatwa katika kulipa deni husika.

Huwezi kopa fedha ukashindwa kulipa ukategemea mahakama ikukingie kofua usilipe deni.
 
WAMEJIKAANGA KUKWEPA KUSAJILI MIKOPO BOT

- Sheria ya Fedha za Kigeni inakataza wakopaji kutokusajili mikopo yao Benki kuu ya Tanzania, ikielekeza kuwa ni lazima wakopaji kusajili mkopo BOT

- Kitendo cha wakili Malongo wa mikopo chechefu kutamba kuwa walishinda kesi mahakama ya biashara baada ya BOT kutoa ruhusa ya kwa wateja wake kuwa wasilipe mikopo hiyo kwa kuwa haijasajili, kinawatia hatiani wateja wake kuliko kuwasaidia

- Kanuni inataka mtu ama taasisi yeyote aliyekwepa kusajili BOT mkopo uliotoka mkopo uliotoka nje ya nchi atozwe faini ya shilingi milioni 4 kila siku kwa siku zote alizokwepa au afungwe jela miaka 14 au adhabu zote kwa pamoja

- Kuingiza mikopo nchini bila kuisajili kunasababisha uwalakini wa matumiz ya mikopo hiyo na kuwafanya kitengo cha Intelijensia ya fedha ‘Financial Intelligence Unit’ kifupi FIU kuwa na jukumu la haraka kuchunguza ni kwanini miamala hii haijasajiliwa

ADHABU,
‘Kanuni ya fedha za kigeni nchini inayosimamiwa na sheria ya fedha za kigeni CAP 271 iliyotolewa na Gazeti la serikali kwa tangazo namba 294 na kuchapishwa tarehe 13 mwezi mei 2022 na marekebisho yake yaliyotolewa kwa tangazo la serikali namba 622 lililochapishwa septemba mosi 2023 inakataza vikali wapokeaji kupokea mikopo kutoka nje ya nchi na kukwepa kuisajili na adhabu ya kufanya kosa hilo ni kulipa faini ya kiasi cha shilingi milioni nne kwa kilasiku ambayo mkopo huo umeishi bila kusajiliwa benki kuu au kufungwa jela kwa kipindi kisichozidi miaka 14 ama vyote kwa pamoja’

Na. Mwandishi wetu,

Wakili mtetezi wa mikopo chechefu, Frank Mwalongo amewatia kitanzini wateja wake wa makampuni sita aliyoyataja kuwa anawatetea kwa kutumia utetezi unaovunja sheria za nchi katika udhibiti wa fedha za kigeni nchini unaowalazimu watu wote, taasisi zote wanaokopa pesa, mali, bidhaa au huduma kutoka nje ya nchi kusajili mikopo hiyo kwa Benki kuu ya Tanzania mara tu baada ya kukopeshwa na kutokufanya hivyo kunapelekea kutendwa kwa kosa la kisheria linalopelekea adhabu kali.

Taarifa za zinasema kuwa kitendo cha watumiaji wa fedha zinazotoka nje kuzipokea na kutozisajili BOT, kinaashiria walakini wa matumizi ya fedha hizo kama zimetumika kwa matumizi gani kwa kuwa taarifa zake hazipo kwenye kumbukumbu za Taifa

Kwa mantiki hiyo basi, wakati wakili mwalongo anatamba na kufurahia wateja wake kukatazwa na BOT kulipa madeni waliyokopa kwa sababu mikopo yao haijasajiliwa BOT, licha ya kwamba kutokusajiliwa mikopo hakuzuii wakopaji kutimiza wajibu wa mkopaji wa ‘DAWA YA DENI NI KULIPA’ bali kumewaingiza matatani na kutakiwa kuweka wazi matumizi ya hayo mabilioni waliyopokea kutoka nchi za nje na kwanini walikwenpa kusajili mikopo hiyo BOT

Aidha kitendo cha wakili huyo kusema hadharani kuwa mikopo hiyo haijasajiliwa BOT ni kana kwamba amevivua nguo vyombo vya ulinzi na usalama vinavyojihusisha na udhibiti wa fedha zinazoingia na kutoka nchini ambavyo vina wajibu wa kisheria na kikanuni kufuatilia na kuzuia miamala yote inayowekewa mashaka na kutokusajili muamala BOT ni chanzo namba moja cha kutiliwa Mashaka kwa mpokeaji wa mualama huo

Bado haijafahamika ni kwa kiasi gani kitengo cha intelijensia ya Fedha cha serikali (Financial Intelligence Unit – FIU) kama kilifahamu juu ya kuingia na kutumika kwa miamala hii nchini ambapo wakili amethibitishia umma katika video yake ya dakika 13 aliyorekodiwa akizungumza na wanahabari kwamba mikopo ya wateja wake wote sita anaowatetea haijasajiliwa BOT

Ni kwa mashaka hayo pia ndipo Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini ‘TAKUKURU’ haijaweka wazi bado kama nayo imejiridhisha kuwa matendo ya wafanyabiashara kukwepa kusajili mikopo waliyoingiza kutoka nje ya nchi na kutumia mchezo huo kama kigezo halali cha kushinda kesi na Jaji wa mahakama ya biashara akijua kuwa kufanywa hivyo ni uvunjifu wa sheria nab ado akawapa ushindi watu waliotakiwa kuelekezwa kufuata na kuheshimu sheria za nchi, kuwa hakuna harufu ama dalili za rushwa ama njama za kutakatisha fedha

Katika kufahamu zaidi tembelea www.jamvilahabari.co.tz


View: https://x.com/JAMVILAHABARI/status/1783268672909246868?t=xSD3ZPEkwJPDis7NFwli7g&s=09
 
JItihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kukaribisha na kuhamasisha uwekezaji wa ndani na kutoka nje ya nchi kuja kuwekeza nchini unaelezwa kutiwa kigingi na tabia chafu inayozidi kuota mizizi ya baadhi ya wafanyabiashara wakubwa kushirikiana na baadhi ya majaji wa mahakama kuu wasio waaminifu kuyatapeli mabenki ya ndani na nje ya nchi kwa na hivyo kuwanyima fursa wafanyabiashara wadogo na wakati kushindwa kuaminiwa na kupata mikopo.

Orodha ya wafanyabiashara wanaotumia mahakama kutapeli na kudhulumu mabenki iliyofanyiwa uchunguzi na kuthibitishwa na gazeti hili, inaonyesha kuwa wengi kati ya wafanyabiashara hao wanajihusisha na biashara za Mafuta na ushafirishaji ambapo wastani wa shilingi za kitanzania Trilioni 1.3 wamekopa katika benki mbalimbali za ndani nan je ya nchi na kukataa kulipa kisha kukimbilia mahakamani ambako pia wanadaiwa kupata ushindi kwa njia zisizo za kawaida

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wafanyabiashara hao wanaoheshimika nchini wakionekana machoni mwa watu kuwa ni matajiri na wengine wakijionyesha kama wacha Mungu na wenye kumuogopa Mungu huku wengine wakijinasibu kama wana michezo na wawekezaji wakubwa wanaitumia mahakama hasa mahakama ya biashara kama kichaka chao cha kufanyia uhalifu huo wa kimkakati

Mfanyabiashara wakubwa wadaiwa kudhulumu mabenki kutumia mahakama

Wachota mabilioni ya akiba za wateja na kujinufaisha, wagoma kulipa wkimbilia mahakamani mahakama yabariki.

Mmoja akwapua bilioni 40 TADB, akakwapua bilioni 70 Azania, akakwapua bilioni 110 Equity kisha akapiga bilioni 220 ujerumani.

Mwengine kachukua bilioni 15 NMB, akachukua bilioni 80 EQUITY akagoma kulipa akakimbilia mahakamani Jaji akampa ushindi anaendelea kutanua mitaani.

Jaji huyo huyo na kwa staili hiyo hiyo akampa ushindi mfanyabiashara mwingine aliyekwapua dola milioni 15 KCB.

Jitihada za Rais Dkt. Samia kuvutia uwekezaji zinazidi kukwamishwa, BOT, TIC, watakiwa kujipanga upya

Chanzo: Jamvi la Habari

Pia soma:
chechefu
 
Hii inaonekana kama ni Nongwa au Husda au kutaka kuchafuana hivi.
Hao wakopaji walikopa kwa utaratibu naamini katika utaratibu huo kuna dhamana waliweka ili ikitokea wameshindwa kulipa "Defaulting" dhamana zao zikamate ziuzwe kufidia deni.
Au hizo benki ziliwakopesha bila dhamana, si washike dhamana au wafanye "Claim of ownership"?

Hakuna mahakama duniani inaweza mtetea Mkopaji alieshindwa kulipa deni yaani "Defaulter" anaedaiwa kwa utaratibu. Mahakama huwa inahakikisha tuu utaratibu unafuatwa katika kulipa deni husika.

Huwezi kopa fedha ukashindwa kulipa ukategemea mahakama ikukingie kofua usilipe deni.
heri kama iko hivyo
 
Back
Top Bottom