Ripoti TCRA: Dar yaongoza kwa idadi kubwa ya Watumiaji wa huduma za Simu Tanzania

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Katika kipindi cha miaka 5 kumekuwa na ongezeko la Watumiaji 16,327,131 wa Huduma za Simu Nchini kutoka 47,685,232 mwaka 2019, sawa na 88% ya Idadi ya Watu hadi 64,088,651, sawa na 101.5% ya Idadi Watu

Mikoa yenye Idadi kubwa ya Watumiaji wa Huduma za Simu Tanzania Bara ni Dar es Salaam (18.68%), Mwanza (6.72%) na Arusha (6.11%). Yenye idadi ndogo ni Njombe (1.79%), Lindi (1.76%) Rukwa (1.67), na Katavi (1.05%)

Kati ya Aprili hadi Juni 2023, Watumiaji wa Huduma za Simu wamefikia 64,088,651 (Ongezeko la 3.6%) kutoka Milioni 61.9 Machi 2023. #Vodacom imeongoza kwa idadi kubwa ya Watumiaji waliofikia 19,116,166 (30%)

#Airtel imefikisha Watumiaji 17,505,139 (27%), #Tigo 17,484,387 (27%), #Halotel 8,410,029 (13%), #TTCL 1,559,090 (3%), #Smile 13,840 (0%) na imepoteza Watumiaji 1,331. Kwa mujibu wa #TCRA kuna ongezeko la 1.5% kulinganisha na ongezeko la 0.59% Januari - Machi 2023

Hii inamaanisha kuwa #TaarifaBinafsi za Watumiaji zaidi ya Milioni 64.1 ziko kwa Wakusanyaji na Wachakataji. Je, unafahamu Taarifa Binafsi zako zinatumikaje na zinalindwaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…