Ripoti ya ajali ya ndege kunani? Ukweli unaendelea kujifunua

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
16,295
Reaction score
33,994
Kidumu Chama changu cha Mapinduzi, zidumu fikra zilizosahihi za Mweyekiti zisizo sahihi tuzifute, wananchi nawasalimu sana.

Tushirikishane hapa, kuna jambo linakwepwa sana na halisemwi, nalo ni kwakuwa chapa ya ndege yetu itashuka ikionekana hakukuwapo uwajibikaji wa wahudumu na shirika kwa usalama wa abiria;

1. Kwanini Mbalawa anajua kwamba report ilikuwa ndiyo ile ile inayosambazwa na Zitto lakini akamtumia ujumbe Msigwa kwamba ikanushwe kwanza kuna jambo haliko sawa? Na hii ni baada ya kuvuja kupitia kwa Zitto kabla ya kuihakiki wanavyotaka iende mtandaoni.

2. Mimi ni CCM ninayependa kudadisi mambo na kuhoji sana masuala ya msingi. Kwanini uchunguzi na ukamilishaji wa repoti hiyo ulihusisha mawasiliano ya mara kwa mara na Michael Lyakurwa ambaye ni Senior manager wa Precision Air, ambaye kwa taarifa zisizo rasmi zaidi alikuwa na mawasiliano pia na mzee wangu, Mwenyekiti Msaidizi wa chama chetu, ambaye pia ni Mjumbe kwenye Bodi ya Wakurugenzi kwenye Precision Air?

3. Abiria aliyerejea Dar es Salaam na kuhojiwa, alipigiwa simu kupitia namba +255 765 737 500, kwamba ajiandae kurejea Dar es Salaam kutumia ndege yao shirika hilo hilo na anaweza kuwa na mahojiano na waandishi wa habari wakati wa safari. Na ticket alikuwa na ya njia moja lakini ya pili ikawa bure, na maelezo aliyotoa yanatofautiana na ya abiria wengine waliokuwa huko.

4. Kwanini Precision Air walihangaika sana kutafuta mwandishi wa habari wa Magazeti ya Citizens na wengine waliomba namba za wapinzani wawape taarifa za kugeuza umakini wa akili za Watanzania?

Kuna mambo ya msingi ya kujiuliza juu ya mambo haya.
Cc barafu Pascal Mayalla
Britanicca
 
We ndo Britanicca wa Twitter? Nauliza tena maana ni watu Tofauti kwenye kufikiria! Kuna mambo hayako sawa kwenye report Kabisa hii

Mwalimu
 
Duh...!.
P
 
Kama kweli kuna conflict of interest kuhusu ile ajali iliyotokea, basi sioni tena maana ya kusubiri hiyo report namba mbili, zaidi ya kuliingiza jina la shujaa Majaliwa, haitakuwa na lingine lolote jipya.

Unless ufanyike uchunguzi huru, viongozi wa serikali wasihusike.

Zaidi, naona umemhusisha Lema kwenye hilo suala kwa sababu ya hiyo sms uliyotuwekea, napata shaka kuamini nia yako, isije kuwa umefanya hivyo ili ku-balance story yako, ionekane viongozi wa CDM, ACT, na CCM walihusika.

Naandika hivyo kwasababu, naona umetuwekea meseji toka kwa hiyo namba inayoonesha Lema akitafutwa, lakini hujatuwekea inayoonesha kama alipatikana, na kama alipatikana, alitoa ushirikiano wa aina gani kuhusu hilo unalodai alitafutwa nalo, je, alikubali au alikataa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…