Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Kwa kawaida kazi ya kamati ya uchunguzi kama ilivyokuwa ile ya Mwakyembe ni kutafuta, kujua na kuanika ukweli na ukweli wote.

Kwa kawaida, meaning kwamba sio kwa kisheria hapo tayari kuna dosari ya hoja mkuu.

Sasa swali linakuja, je Kamati ya Mwakyembe ilitafuta, kujua na kuanika ukweli wote kama tulivyoambiwa awali?

Again tuliambiwa na nani? So far hatukuambiwa na sheria ya jamhuri, ila ni maneno ya kawaida ya kisiasa.

Binafsi nilishatoa maoni yangu tangu awali kwamba kitendo cha kamati ya Mwakyembe kutokumhoji mhusika mkuu wa saga la Richmond Ndugu Edward Lowasa ilikuwa ni mapungufu makubwa yaliyotia dosari ya kutisha credibility ya report. Mpaka hapo kwangu mie report ya Mwakyembe ilikuwa shwari na nzuri sana ukiacha hii methodological fault.

Kamati haikutaka kumuita Lowassa, kwa sababu kama alivyosema Mwakyembe ni kuwa walikuwa na ushaidi wa kutosha against Lowassa, na Mwakyembe alisema wazi kuwa uchunguzi wa kaamti haukuanza under the probable course ya Lowassa, au Lowassa kama kinara wa kuchunguzwa,

hapana wao walikuwa wanatafuta tu ukweli wa kilichotokea, ingawa ni kweli kama Lowassa, leo akiitwa kwenye mikono ya sheria kuhusiana na ile ripoti kutakuwa na good argument toka kwenye defence yake on this ya kutokuitwa kwake na kamati, lakini ninataka kumuamini Mwenyekiti wa kamati Mwakyembe aliposema kuwa kanuni zilizokuwa zikiilinda kamati ziko wazi kwenye hili la kumuita Lowassa au kutomuita zimekuwa fullfilled, lakini mbele ya sheria kunatakiwa kuwa na tatizo.
 
kauli ya Mwakyembe ya kwamba wapewe nafasi ingine ili waseme yale ambayo hawakusema kuhusu uchunguzi wao ni tatizo la pili kwenye report yao ambalo kusema kweli ni kubwa. Tatizo lenyewe ni kwamba kumbe after all kamati ya ndugu yetu Mwakyembe haikutuambia ukweli wote kama tulivyodhani!!

Hapana kamati haikuutoa ukweli wote uliokuwemo kwenye ile ripoti kwa public kutokana na kuwemo kwa siri za serikali ambazo zinalindwa kisheria, kutotolewa kwa public,

kamati ingekuwa haina ukweli basi hakukuwa na sababu ya Lowassa na wenziwe kujiuzulu, kamati ilisema ukweli lakini ukweli mwingine ulibakizwa kwa kulindwa na sheria za siri za serikali, hili haliwezi kuwa tatizo la kamati au Mwakyembe mwenyewe, hapa wabunge hasa wa upinzani walipaswa kuja juu na kudai sheria itenguliwe ili ripoti yote isomwe wazi.


Again, this a serious flaw that further waters down the credibility of the report and,

Kutosomwa kwa ripoti yote mbele ya umma au bunge kwa sababu za kisheria, kunapunguza vipi credibility ya kamati au ripoti? Kwenye ripoti ya Ken Starr against Clinton, kulikuwa na sehemu nyingi sana ambazo zilikuwa zimezibwa na serikali kwa sababu hizi hizi kama za kwetu, yaani sheria za kulinda siri za serikali, lakini bado ile ripoti ilpelekea kuwa-impeached kwa Clinton na The House, kule US,

Hapa again the argument ni hakuna kabisa mkuu, kwa sababu kwanza sio kosa la kamati wala la Mwakyembe kwamba hakuweza kuisoma ripoti yote, tatizo ni sheria yetu ya jamhuri, sasa hili linawezaje kupunguza credibility ya ripoti I do not get it?


unfortunately, strongly strengths the arguments of those alleged in the report that the committee was more intrumental politically than a significant step towards addressing the problem of corruption and public resources vandalisation in our country. Kwa hiyo kwa maoni yangu tukubaliane kwamba kuna makosa ya msingi katika uandaji na yaliyomo katika report ya Mwakyembe.

Again sioni hoja hapa, ripoti haikuwa na mapungufu hiyo ni fact, so far kati ya waliomo kwenye ripoti hakuna hata mmojawao anayesema kuwa ripoti ni ya uongo, hiyo ni fact, tatizo la Lowassa anasema hakuitwa lakini hajawahi kulia kuwa ripoti imejaa uongo, again hii ni fact, hakuna makosa ya kimsingi kabisa kwenye hii ripoti na the way kamati nzima ilivyofanya kazi yake mapoungufu hapa yarushiwe sheria zetu ambazo zinailinda jamhuri kutoanikwa hadharani,

Kama Lowassa na wenzake wanaamini haya maneno yako Kitila, hawajawahi kuyasema to the public, na kama kweli maneno yako ni ya kweli, basi walikuwa ni wenda wazimu kujiuzulu na kuanza kulia lia pembeni, ripoti haina makosa, kamati haina makosa so far, lakini endapo Lowassa angeitwa kwenye mkono wa sheria, anaweza kuwa na argument kuwa hakuitwa, lakini still bado kuna sheria zilizokuwa zinailinda ile kamati ambazo Mwakyembe amesema kuwa haikuwa lazima kumuita Lowassa mbele ya kamati kwa sababu Lowassa hakuwa mtuhumiwa wakati kamati inaanza kazi yake au kupewa kazi yake ya uchunguzi, jina la Lowassa limejitokeza sana kwenye process ya kukusanya uchunguzi, lakini hakuwa mtuhumiwa kwa kamati ndio maana Mwakyembe na kamati hawakuona sababu ya kumuita, hii ni kutokana na maneno yao wenyewe kuanzia Mwakyembe mpaka wajumbe wote wa kamati.
 
Je, makosa haya yanamtoa ndugu Mwakyembe kwenye orodha yetu ya "mashujaa" wa taifa? Mimi nasema hapana. Hata hivyo natoa wito kwamba tunapoendelea na mijadala hii ya ufisadi na tunapowaunga mkono na kuwatia moyo wenzetu waliopo katika mstari wa mbele wa mapambano tusijefika mahala tukawaona kwamba wao hawawezi kukosea.

So far hawakukosea sasa nhatuwezi kulazimsha hoja ya kukosea na kukosoa bila kuwepo kosa, sheria kulinda serikali na ukweli wa ripoti ya kamati haiwafanyi kina Mwakyembe wawe na makosa ya kukosolewa.

Kufumbia macho makosa ya "mashujaa" wetu hakuwasaidii wao katika kuongoza vita tuliyoianzisha. Tuwakosoe constructively kwa lengo la kuwajenga ili waimarike zaidi. Sisis pia tujitahidi kujua ukweli wote hata ule ambao pengine hatuupendi au ni mchungu kwetu lakini ni mtamu kwa maadui zetu, yaani mafisadi. Haya makosa mawili niliyoyataja hapo juu ni wazi kwamba ni machungu sana kwetu tunaowaunga mkono ndugu zetu wapambanaji, lakini pia ni wazi kwamba makosa haya yanatoa mwanya wa kutosha kwa mafisadi wa Richomond kujitetea na kuisambaratisha report ya Mwakyembe.

Mkuu Kitila,

This is a big lie, so far hujatihibitisha anything cha kuweza kuita tatizo, kama ni tatizo lipo kwa sheria zetu zinazolinda siri zake, mimi siwezi kumkosoa Mwakyemeb kwenye hilo la kushindwa kuisoma ripoti yote kwa public kwa sababu aliyoyaacha yanalindwa na sheria za serikali, ninamkosoa Mwakyembe for what?

Au nimkosoe Mwakyembe kwa kuomba kanuni za bunge zivunjwe ili aimalize ripoti? Eti mafisadi wanaweza kuisambaratisha ripoti wakati tunasikia kuwa na Rostam sasa yuko njiani kujiondoa kwenye uongozi kwa sababu ya hii hii ripoti? Ninaomba kusema hivi vyama vyetu vya siasa visiwe kama dini kwamba tunafikia hatua hatuwezi kuuona ukweli just because ukweli ule haukutolewa na vyama vyetu vya siasa, tufike mahali tuache ushabiki wa Yanga na Simba, timu ambazo toka tupate uhuru hata ubingwa wa Afrika tu umekuwa ndoto, lakini makelele mitaani kila siku,

Mwakyembe ni bina-adam kama sisi wengine wote ana mapungufu yake tena mengi sana, mimi nilitegemea by now yatakuwa yametolewa hapa, lakini kama kawaida huwa hatuna ukweli ila kujaribu kulazimisha mapungufu tu ili mradi tuonekane kuwa tunajua better huo ni mufilisi wa kuanzia hoja mpaka elimu kwa wananchi wengine wanaokuja hapa kuelimika, haiwezekani kiongozi wetu kushindwa kusoma ripoti yote kwa kuzuiwa na sheria ikawa ni mapungufu on his part that is nonesense, ingekuwa ripoti ina uongo mimi ningekubali hoja kuwa Mwakyembe ni a thug kama hao wengine,

Kutokumuita Lowassa, mbele ya kamati ni tatizo iwapo tu ishu itakwenda mbele ya sheria, lakini still bado ni weak argument kwa sababu kama kamati hii ya Mwakyembe haikuwa na nguvu zozote za kisheria, ingekuwa basi Rostam na Yona sasa hivi walitakiwa wawe jela kwa kugoma kwenda mbele ya kamati, sasa nashangaa tunapoambiwa kuwa kuna wanaolalalamika, wakati aliyelalamika ni mmoja tu Lowassa, kuwa hakuitwa mbele ya kamati, hata yeye pia anajaribu tu kutuchezea kwa sababu anajua wazi kuwa kamati ile haikuwa na nguvu zozote kisheria ingekuwa saa hizi angekuwa Segerea, kwa hiyo argument yake anaitoa kwa wananchi wasioelewa na masikini ya Mungu kuna wanaodhani kuwa ana hoja nzito, tena mpaka ndani ya hii forum that is very sad kama sio pathetic!

Tupunguze ushabilki wa vyama vya siasa, unauwa taifa letu pole pole tukiwa tunaliona kwa macho yetu! Sisi tutaendelea kuwapa moyo na big support viongozi wote wa taifa letu wanaotujali yaani sisi wananchi walalahoi, bila ya kujali wanatoka chama gani cha siasa.
 
Hapana kamati haikuutoa ukweli wote uliokuwemo kwenye ile ripoti kwa public kutokana na kuwemo kwa siri za serikali ambazo zinalindwa kisheria, kutotolewa kwa public,

kamati ingekuwa haina ukweli basi hakukuwa na sababu ya Lowassa na wenziwe kujiuzulu, kamati ilisema ukweli lakini ukweli mwingine ulibakizwa kwa kulindwa na sheria za siri za serikali, hili haliwezi kuwa tatizo la kamati au Mwakyembe mwenyewe, hapa wabunge hasa wa upinzani walipaswa kuja juu na kudai sheria itenguliwe ili ripoti yote isomwe wazi.




Kutosomwa kwa ripoti yote mbele ya umma au bunge kwa sababu za kisheria, kunapunguza vipi credibility ya kamati au ripoti? Kwenye ripoti ya Ken Starr against Clinton, kulikuwa na sehemu nyingi sana ambazo zilikuwa zimezibwa na serikali kwa sababu hizi hizi kama za kwetu, yaani sheria za kulinda siri za serikali, lakini bado ile ripoti ilpelekea kuwa-impeached kwa Clinton na The House, kule US,

Hapa again the argument ni hakuna kabisa mkuu, kwa sababu kwanza sio kosa la kamati wala la Mwakyembe kwamba hakuweza kuisoma ripoti yote, tatizo ni sheria yetu ya jamhuri, sasa hili linawezaje kupunguza credibility ya ripoti I do not get it?




Again sioni hoja hapa, ripoti haikuwa na mapungufu hiyo ni fact, so far kati ya waliomo kwenye ripoti hakuna hata mmojawao anayesema kuwa ripoti ni ya uongo, hiyo ni fact, tatizo la Lowassa anasema hakuitwa lakini hajawahi kulia kuwa ripoti imejaa uongo, again hii ni fact, hakuna makosa ya kimsingi kabisa kwenye hii ripoti na the way kamati nzima ilivyofanya kazi yake mapoungufu hapa yarushiwe sheria zetu ambazo zinailinda jamhuri kutoanikwa hadharani,

Kama Lowassa na wenzake wanaamini haya maneno yako Kitila, hawajawahi kuyasema to the public, na kama kweli maneno yako ni ya kweli, basi walikuwa ni wenda wazimu kujiuzulu na kuanza kulia lia pembeni, ripoti haina makosa, kamati haina makosa so far, lakini endapo Lowassa angeitwa kwenye mkono wa sheria, anaweza kuwa na argument kuwa hakuitwa, lakini still bado kuna sheria zilizokuwa zinailinda ile kamati ambazo Mwakyembe amesema kuwa haikuwa lazima kumuita Lowassa mbele ya kamati kwa sababu Lowassa hakuwa mtuhumiwa wakati kamati inaanza kazi yake au kupewa kazi yake ya uchunguzi, jina la Lowassa limejitokeza sana kwenye process ya kukusanya uchunguzi, lakini hakuwa mtuhumiwa kwa kamati ndio maana Mwakyembe na kamati hawakuona sababu ya kumuita, hii ni kutokana na maneno yao wenyewe kuanzia Mwakyembe mpaka wajumbe wote wa kamati.

Somo zuri sana Mkuu. Limenitia moyo kuona utetezi mzuri ulioutoa dhidi ya wale wanaotaka kuonyesha kuwa Mh. Mwakyembe hafai kwa kitu ambacho hata undani wake hawaujui.
 
Somo zuri sana Mkuu. Limenitia moyo kuona utetezi mzuri ulioutoa dhidi ya wale wanaotaka kuonyesha kuwa Mh. Mwakyembe hafai kwa kitu ambacho hata undani wake hawaujui.

Mkuu Heshima mbele, ukweli ni kwamba hata wanachokizungumzia hawakijui,

unajua mkuu niliwahi kukaa Bunazi, kama miezi sita hivi baada ya vita vya Idd Amini, nilienda na wa-Holanzi flani hivi kuwasaidia kufufua kiwanda cha sukari pale Kagera Sugar, kule jamaa walinifundisha neno moja huwa silisahau, linaitwa Nshomile, ndio hasa ninachokiona on wale wanaomshambulia, nothing but Nshomile lakini hoja siioni kabisa.

Nimegundua kuwa hapa forum tunahitaji kuwa macho sana na this Nshomile thing!
 
Mkuu Heshima mbele, ukweli ni kwamba hata wanachokizungumzia hawakijui,

unajua mkuu niliwahi kukaa Bunazi, kama miezi sita hivi baada ya vita vya Idd Amini, nilienda na wa-Holanzi flani hivi kuwasaidia kufufua kiwanda cha sukari pale Kagera Sugar, kule jamaa walinifundisha neno moja huwa silisahau, linaitwa Nshomile, ndio hasa ninachokiona on wale wanaomshambulia, nothing but Nshomile lakini hoja siioni kabisa.

Nimegundua kuwa hapa forum tunahitaji kuwa macho sana na this Nshomile thing!

Kuna mtu anayejua kitu hapa JF zaidi ya FMES!!! Hakuna wewe ndiyo mjuzi wa kila kitu. Sasa sijui na Wahaya wamekukosea nini hata uingize lugha yao kwenye mjadala huu.

Mwakyembe mwenyewe katamka hadharani kwamba kama Spika atavunja kanuni za Bunge ili yale ambayo hakuyaandika katika ripoti ile ili 'kulinda heshima' ya serikali wayajadili kwa mapana na marefu.

Katika kupewa kazi ya kuchunguza mkataba wa Richmond na TANESCO, Mwakyembe hakupewa mamlaka ya yeyote kuandika yale anayoyataka yeye na yale anayoyaona hayafai ili 'kulinda heshima ya serikali' basi asiyaandike.

Mwakyembe siyo Mungu, ni Mungu peke yake na Mitume wake ndiyo hawakosolewi. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ana ushujaa zaidi kwa yale aliyoifanyia Tanzania na Afrika kwa ujumla na bado Watanzania mbali mbali ukiwemo wewe mwenyewe bado mnamkosoa kila kukicha, nami sioni ubaya wa Mwalimu kukosolewa hata yeye mwenyewe alipokuwa hai aliwa kutamka kwamba hakufanikiwa katika yote aliyoyatarajia kuyafanya kwa Watanzania.

Bado wengi tunaona kazi aliyoifanya Mwakyembe katika kuchunguza na kuandika ripoti ni nzuri, lakini kujipa mamlaka ambayo hakuwa nayo ya kuamua nini cha kuandika na nini cha kutoandika ni makosa na anastahili kukosolewa maana hatujui uzito wa hayo aliyoaacha ni mkubwa kiasi gani ukilinganisha na hayo aliyoyaandika kwenye ripoti ile.

Kama Watanzania tunaweza kumkosoa Mwalimu (Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi~AMEN pamoja na kuwa hayuko nasi huu ukiwa ni mwaka wa tisa, basi pia tunaweza kumkosoa Mwakyembe ambaye ushujaa wake wa kuandika ripoti ya Richmond kamwe hauwezi kulinganishwa na ule wa Mwalimu kwa Tanzania na Afrika nzima.
 
Kuna mtu anayejua kitu hapa JF zaidi ya FMES!!! Hakuna wewe ndiyo mjuzi wa kila kitu.

Off course, wakati wowote mnapokuja na ishus ambazo hamzielewi na hamkuzifanyia utafiti, sio kosa langu, mimi ninakuwa na uhakika kwanza na ninachotaka kukisema, ndio ninakisema mifano ipo wazi tena kwenye thread nyingi sana humu, kama topic siijui siigusi hata siku moja, sasa kama hiyo inanifanya niwe kama unavyosema so be it!

Sidhani kama mwananchi anahitaji kwua professor kuelewa hili, kuwa Mwakyembe ahkusioma ripoti yote kwa sababu ilikuwa na siri za serikali ambazo zinalindwa na sheria kutosemwa to public unless bunge au Spika, avunje kanuni ndio isomwe yote, ni kipi kigumu hapa kuelewa? Ninahitaji kujua kila kitu ili kuelewa hili?


Sasa sijui na Wahaya wamekukosea nini hata uingize lugha yao kwenye mjadala huu.

Hapana cheap shot hiyo mkuu, ninachosema ni kuwa ninajaribu kuwa careful na maneno mengi ya kishule kumbe ni empty au hewa tupu!and yes I said it!

Mwakyembe mwenyewe katamka hadharani kwamba kama Spika atavunja kanuni za Bunge ili yale ambayo hakuyaandika katika ripoti ile ili 'kulinda heshima' ya serikali wayajadili kwa upana na marefu. Katika kupewa kazi ya kuchunguza mkataba wa Richmond na TANESCO, Mwakyembe hakupewa mamlaka ya yeyote kuandika yale anayoyataka yeye na yale anayoyaona hayafai ili 'kulinda heshima ya serikali' basi asiyaandike.

Mwakyembe hakusema haya, amesema ataomba Spika avunje kanuni ili aweze kusema yote yaliyomo kwenye ripoti, hakusema kuwa aseme ambayo hakuyaandika mkuu, amesema ili ripoti yote isomwe upya maana kuna yaliyoachwa kwenye kuisoma, haya mengine ni yako tu mkuu!
 
Quote;- Tanzania Daima

Sababu nyingine kubwa inayofanya tukubaliane na kauli ya Dk. Mwakyembe ya kutaka Spika avunje kanuni na kurejesha suala la Richmond bungeni

Mkuu soma tena hii quote, hivi kweli inasema kuwa Mwakyembe ameomba aongeze kwenye ripoti ambayo hajaandika?
 
WENGINE TUMEMWELEWA MWAKYEMBE VIZURI KABISA!
Tutake, tusitake, Kamati ya Mwakyembe imefanyakazi nzuri ambayo Watanzania hatujawahi kuiona. Hata TAKUKURU wanaolipwa kwa kupeleleza, wamefundishwa kazi na Kamati ya Mwakyembe! Sasa akiona Kevo wanaokimbilia kuwachafua watu waliofanyakazi nzuri sana, walishafanya nini wao cha maana, cha kitaifa, cha kizalendo? Mimi nilimwelewa Mwakyembe aliposema "na sisi tutasema hata yale ambayo hatukutaka kusema kulinda heshima ya Serikali". He is right. Kila Serikali inayo mambo nyeti ambayo hayasemwi tu until it is necessary. Ndiyo maana ya kula kiapo cha Wabunge. Ni tofauti na kiapo cha mwana JF, cha kutapika anything. The bottomline here is that Mwakyembe kawanyamazisha wale waliokuwa wanaimba nyimbo za kinafiki kumsafisha Lowassa, Karamagi na Rostam bila aibu kwa kuwaambia "tutasema yote"! Tatizo liko wapi wakati mafisadi wamewajibishwa kwa kujiuzulu? Nina wasiwasi Kevo & co. wanaweza kuwa vibaraka wa Rostam ambaye kawanunua almost nusu ya waandishi wa Bongo kwa hela yake haramu. Tusijaribu kuchafua kazi nzuri kwa arguments za juu juu. Msubirini Mwakyembe mwenyewe ajieleze, nina uhakika alikuwa na sababu nzuri zaidi ya hizi ninazotoa. Ufisadi ziiii!!!
 
Nimesoma makala ya mwandishi mmoja nikakutana na hili kwa kweli Mwakyembe kama ni kukosea hapa ulikosea sana. Inakuwaje anasema kuwa 'walificha baadhi ya mambo kulinda 'heshima' ya serikali?'. Naomba nieleweshwe kidogo hapa. Ni heshima gani hii serikali inayo kama siyo ujinga. Angesema wanaficha baadhi ya mambo 'kulinda usalama wa taifa' hapo angeeleweka japo kidogo.

Ni bora mheshimiwa huyu ambaye siku za karibuni amejizolea sifa kemkem kama shujaa wetu yeye na kamati yake kufafanua hii kauli tete.

Hivyo basi hatutashangaa hata pale mmoja wa 'majeruhi' mmoja wa kisiasa kudai kulikuwa na uwezo wa 'kuchomekea' baadhi ya mambo ili kuhalalisha makosa ya baadhi ya waheshimiwa waliotuhumiwa na kamati hiyo?

Mheshimiwa kwa niaba ya wakereketwa wengi tunakuomba utoe ufafanuzi wa ziada kuhusu kauli yako.
Mwakyembe anatufaa sana, Pengine weye mwenzetu!
Kevo kanichefua. Vita imepigwa, tumeshinda, waanza kumlaumu Jemadari kwa maneno usiyo na tafsiri yake sahihi! Mwakyembe mwanasheria bwana, kasema alichosema, ni haki yake. Weye nani kumhukumu kwa vita ya wengi ambayo wengi tumeifurahia? Ulitaka akae kimya kama weye? Maneno yote aliyosema hayana maana, umechukua matatu hayo na kuyajengea jukwaa la kumvunja moyo jemadari. Hatutakuruhusu ati!
 
Soma vizuri kaka vaa miwani kama huoni vizuri, nimeandika 'kuyajadili na siyo kuyaongeza kwenye ripoti hiyo

Mwakyembe hakuomba kama Tanzania Daima inavyoonyesha hapa, kutaka na kuomba ni vitu viwili tofauti.

Tunakubaliana na Mwakyembe
Tanzania Daima

TUMEGUSWA sana na kauli ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), aliyoitoa mwishoni mwa wiki hii bungeni, akitaka Spika wa Bunge aruhusu kuvunjwa kwa kanuni za Bunge ili kutoa fursa kwa wabunge kulijadili kwa kina sakata la Richmond.

Kauli hiyo ya Dk. Mwakyembe ina uzito wa pekee kulingana na mwenendo wa mambo ulivyo sasa nchini, kuhusu jinsi suala hilo lilivyoshughulikiwa na Kamati Teule ya Bunge iliyoteuliwa kuchunguza utata wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kati ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Kampuni ya Richmond ya Marekani. Dk. Mwakyembe alikuwa mwenyekiti wa kamati hiyo.

Tangu kusomwa kwa ripoti ya kamati hiyo iliyosababisha kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, pamoja na mawaziri wengine - Nazir Karamagi, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini; na Dk. Ibrahim Msabaha, aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Dk. Msabaha alikuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati mkataba wa Richmond unasainiwa mwaka 2006.

Haja ya suala hili kuwa na mjadala mpana zaidi, ilianza kuonekana baada ya Dk. Mwakyembe kumaliza kusoma ripoti yake. Lowassa aliyetajwa katika ripoti hiyo na kutakiwa kupima mwenyewe uzito wa yaliyoelekezwa kwake, aliamua kujiuzulu huku akilalamika kuwa amedhalilishwa sana, amesononeshwa sana pia kuonewa na ripoti hiyo.

Karamagi naye hakukubaliana moja kwa moja na ripoti hiyo na hadi sasa hakubaliani nayo na amekwishatamka kuwa anatamani suala hilo lichunguzwe na majaji na ikibainika kuwa alihusika kwa namna yoyote na kashfa ya Richmond, ataachia wadhifa wa ubunge.

Mbali na hao, kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na malumbano makali bungeni yanayowahusisha wabunge, baadhi wakipinga jinsi suala hilo lilivyoshughulikiwa hadi kuwalazimisha baadhi ya vigogo kuachia nyadhifa zao, na wengine wakikubaliana na ripoti ya kamati na hatua ya vigogo hao kuaachia madaraka waliyokuwa wakishikilia.

Haya yote yanaonyesha kuwa wapo wananchi, wabunge na mawaziri ambao hawakuridhiki na ripoti ya kamati na hata uamuzi wa bunge, jambo lililoonyesha ulazima wa suala hilo kurejeshwa bungeni ili lijadiliwe upya.

Sababu nyingine kubwa inayofanya tukubaliane na kauli ya Dk. Mwakyembe ya kutaka Spika avunje kanuni na kurejesha suala la Richmond bungeni ni kuwa watayaanika hata yale ambayo walibaki nayo moyoni kwa ajili ya kuinusuru serikali.[/size]

[size=6]Hapa ni dhahiri kuna madudu mengine katika suala hili yaliyogunduliwa na kamati ambayo hayakuwekwa katika ripoti iliyosomwa na Dk. Mwakyembe.[/size]
labda kiswahili kimebadilika lakini kitu kama hakikuwekwa kwenye ripoti ina maana hakikuandikiwa


Soma tena hii article yote ili uelewe kilichoandikwa

Tunakubaliana na Mwakyembe

Tanzania Daima

TUMEGUSWA sana na kauli ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), aliyoitoa mwishoni mwa wiki hii bungeni, akitaka Spika wa Bunge aruhusu kuvunjwa kwa kanuni za Bunge ili kutoa fursa kwa wabunge kulijadili kwa kina sakata la Richmond.

Kauli hiyo ya Dk. Mwakyembe ina uzito wa pekee kulingana na mwenendo wa mambo ulivyo sasa nchini, kuhusu jinsi suala hilo lilivyoshughulikiwa na Kamati Teule ya Bunge iliyoteuliwa kuchunguza utata wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kati ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Kampuni ya Richmond ya Marekani. Dk. Mwakyembe alikuwa mwenyekiti wa kamati hiyo.

Tangu kusomwa kwa ripoti ya kamati hiyo iliyosababisha kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, pamoja na mawaziri wengine - Nazir Karamagi, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini; na Dk. Ibrahim Msabaha, aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Dk. Msabaha alikuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati mkataba wa Richmond unasainiwa mwaka 2006.

Haja ya suala hili kuwa na mjadala mpana zaidi, ilianza kuonekana baada ya Dk. Mwakyembe kumaliza kusoma ripoti yake. Lowassa aliyetajwa katika ripoti hiyo na kutakiwa kupima mwenyewe uzito wa yaliyoelekezwa kwake, aliamua kujiuzulu huku akilalamika kuwa amedhalilishwa sana, amesononeshwa sana pia kuonewa na ripoti hiyo.

Karamagi naye hakukubaliana moja kwa moja na ripoti hiyo na hadi sasa hakubaliani nayo na amekwishatamka kuwa anatamani suala hilo lichunguzwe na majaji na ikibainika kuwa alihusika kwa namna yoyote na kashfa ya Richmond, ataachia wadhifa wa ubunge.

Mbali na hao, kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na malumbano makali bungeni yanayowahusisha wabunge, baadhi wakipinga jinsi suala hilo lilivyoshughulikiwa hadi kuwalazimisha baadhi ya vigogo kuachia nyadhifa zao, na wengine wakikubaliana na ripoti ya kamati na hatua ya vigogo hao kuaachia madaraka waliyokuwa wakishikilia.

Haya yote yanaonyesha kuwa wapo wananchi, wabunge na mawaziri ambao hawakuridhiki na ripoti ya kamati na hata uamuzi wa bunge, jambo lililoonyesha ulazima wa suala hilo kurejeshwa bungeni ili lijadiliwe upya.

Sababu nyingine kubwa inayofanya tukubaliane na kauli ya Dk. Mwakyembe ya kutaka Spika avunje kanuni na kurejesha suala la Richmond bungeni ni kuwa watayaanika hata yale ambayo walibaki nayo moyoni kwa ajili ya kuinusuru serikali.

Hapa ni dhahiri kuna madudu mengine katika suala hili yaliyogunduliwa na kamati ambayo hayakuwekwa katika ripoti iliyosomwa na Dk. Mwakyembe.

Katika hali tuliyo nayo sasa ya viongozi wa nchi yetu kuandamwa na kashfa za ufisadi na matumuzi mabaya ya madaraka, tunadhani si jambo jema kuficha ukweli wa jambo lolote kwa ajili ya kumsuru mtu au serikali.

Aidha, inawezekana pia hata waliotajwa wanalalamika kwa sababu wanajua kuwa ripoti hiyo ilitoa upendeleo kwa baadhi ya wahusika wa kashfa hiyo, ambao haikuwataja na hadi sasa wanaendelea kula raha kana kwamba ni wasafi kuliko hao wanaolalamika kuonewa na kamati.

Tunaamini alichokisema Dk. Mwakyembe ndicho kinachotakiwa kufanyika, ili ipatikane fursa ya kujua nani mkweli na kumaliza hali tete iliyopo sasa kuhusu ripoti ya kamati na uamuzi wa Bunge.
 
KAMA MWAKYEMBE HAKUFAI, ANAKUFAA NANI: ROSTAM?
"Kwa hili Mwakyembe hutufai Watanzania"! Huyu mwana JF hakai TZ kujua feelings za watu, Watanzania wenyewe! Kazi ambayo Mwakyembe na wenzake akina Selelii, Manyanya, mnyaa na Mntangi, ni kubwa, ni nzuri, haifutwi na maneno ya kudandia!
 
Mkuu Bubu,

Heshima tena mbele, mimi ninasimamia hoja yangu ya msingi kuwa:-

1. Mwakyembe hajafanya kosa lolote, kwa kutoisoma ripoti yote kwa sababu ya kubanwa na vifungu vya sheria ya jamhuri, vinavyolinda siri za serikali.

2. Ripoti ya Mwakyembe ina ukweli mtupu tena 100%, na ndio maana hata wabunge karibu wote waliiunga mkono kuwa ni kweli, Lowassa mpaka leo hajawahi kulalamikia uongo kuwemo ndani ya ile ripoti, anacholilia ni kutoitwa mbele ya kamati,

huu ni ujanja wake tu kwa sababu alijua kuwa hawezi kujitetea mbele ya bunge against ile ripoti, ndio akaamua kutafuta kashimo ka kutokea kwa kudai hakuitwa mbele ya kamati, lakini anajua fika kuwa ni uhuni tu alioufanya.

3. Msabaha na Karamagi, wao hawajwahi hata kusema kitu kwa sababu ukweli ulikuwa very clear kwenye ripoti, hata kwenye hiizi video ni aibu sana jinsi wabunge walivyowashupalia ikabidi waaondoke tu!

Ninsema hivi kama kuna uongo ndania ya ile ripoti usemwe hapa tumshike sikio Mwakyembe, so far siioni hoja ya msingi ya kumkosoa Mwakyembe kulingana na ile ripoti, ninachoona ni maneno mengi ya kishule tu kujaribu kuharibu jina la Shujaa Wa Taifa Mwakyembe, lakini hoja na ukweli sijauona kabisa mkuu labda huko mbele ya safari!

Ahsante Mkuu!
 
Ijab Issa,
Tofauti ya kutaka na kuomba ni semantic tu. Na khasa kwa kuwa makala imepitia kwenye mikono ya mwandishi mimi sioni tofauti yoyote. Kumtaka Spika au kumwomba Spika matokeo yake yatakuwa ni yale yale. Tofauti ni kwamba moja ni more authoritative kuliko jengine.
 
WENGINE TUMEMWELEWA MWAKYEMBE VIZURI KABISA!
Kila Serikali inayo mambo nyeti ambayo hayasemwi tu until it is necessary. Ndiyo maana ya kula kiapo cha Wabunge. Ni tofauti na kiapo cha mwana JF, cha kutapika anything. The bottomline here is that Mwakyembe kawanyamazisha wale waliokuwa wanaimba nyimbo za kinafiki kumsafisha Lowassa, Karamagi na Rostam bila aibu kwa kuwaambia "tutasema yote"

Mtindi,
Hapa umenimaliza mbavu kwa hiki kiapo cha JF. Nilikuwa sijui kuwa siku najiunga hapa niliapa kuwa Ntatapika bin Kuchonga BIN Kubwabwaja yote. Ukiangalia mdomo wa KEVO unaona kabisa jamaa ALIAPA kweli kweli....
 
Mkuu Bubu,

Heshima tena mbele, mimi ninasimamia hoja yangu ya msingi kuwa:-

1. Mwakyembe hajafanya kosa lolote, kwa kutoisoma ripoti yote kwa sababu ya kubanwa na vifungu vya sheria ya jamhuri, vinavyolinda siri za serikali.

2. Ripoti ya Mwakyembe ina ukweli mtupu tena 100%, na ndio maana hata wabunge karibu wote waliiunga mkono kuwa ni kweli, Lowassa mpaka leo hajawahi kulalamikia uongo kuwemo ndani ya ile ripoti, anacholilia ni kutoitwa mbele ya kamati,

huu ni ujanja wake tu kwa sababu alijua kuwa hawezi kujitetea mbele ya bunge against ile ripoti, ndio akaamua kutafuta kashimo ka kutokea kwa kudai hakuitwa mbele ya kamati, lakini anajua fika kuwa ni uhuni tu alioufanya.

3. Msabaha na Karamagi, wao hawajwahi hata kusema kitu kwa sababu ukweli ulikuwa very clear kwenye ripoti, hata kwenye hiizi video ni aibu sana jinsi wabunge walivyowashupalia ikabidi waaondoke tu!

Ninsema hivi kama kuna uongo ndania ya ile ripoti usemwe hapa tumshike sikio Mwakyembe, so far siioni hoja ya msingi ya kumkosoa Mwakyembe kulingana na ile ripoti, ninachoona ni maneno mengi ya kishule tu kujaribu kuharibu jina la Shujaa Wa Taifa Mwakyembe, lakini hoja na ukweli sijauona kabisa mkuu labda huko mbele ya safari!

Ahsante Mkuu!


Ahsante Mkuu,

Na mimi pia nasimamia hoja yangu kwamba Mwakyembe kama Mwenyekiti wa kamati ya kuchunguza mkataba kati ya TANESCO na Richmond hakupewa mamlaka wala mipaka ya nini cha kuandika au kutoandika ili 'kulinda heshima ya serikali'

Kama utakumbuka Kamati hiyo iliundwa baada ya watanzania kulalamika sana ilipokuja kujulikana kwamba kampuni hiyo ni ya kitapeli ambayo ilikuwa haijui chochote kuhusu umeme, bali biashara yao kubwa ilikuwa ni stationeries. Pia hawakuwa hata na mtaji wa kuanzia mkataba wao.

Pamoja na kushindwa kuzalisha umeme wakati nchi ilikuwa imegubikwa kwenye giza nene waliendelea kulipwa shilingi 152 millioni ambazo Watanzania wengi tuliona hawastahili kulipwa.

Hivyo jukumu alilopewa Mwakyembe kama mwenyekiti wa kamati ile na kamati yake ni kuchunguza kama kulikuwa na ufisadi wowote uliofanyika katika mkataba ule. Kama utakumbuka Wataalamu wa TANESCO walitoa ushauri wao kwamba Richmond walikuwa hawajui chochote kuhusu umeme na hawakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme, lakini wakapingwa na hatimaye kupewa ule mkataba.

Pia kama utakumbuka kulikuwa na rumours kwamba mtoto wa Lowassa ama ndiye alikuwa mwenye Richmond ama mmoja wa owners pamoja na baadhi ya vingune waliomo serikalini.

Hivyo alichotakiwa kufanya Mwakyembe ni kuandika kila kitu ambacho waligundua wakati wa uchunguzi wao bila kubakisha chochote kwa minajili ya 'kulinda heshima ya serikali'. Kwa maoni yangu serikali inakuwa haina heshima kwa wale inawaongoza pindi mtu mwenye wadhifa mkubwa kama Waziri Mkuu anahusishwa na tuhuma nzito za Richmond kwa namna moja au nyingine.

Alichofanya Mwakyembe pamoja na kamati yake ya kujipa madaraka ambayo hawakuwa nayo kuhusu nini cha kuandika ni makosa. Pamoja na kuwa walifanya kazi nzuri kuna baadhi yetu tunaona kuna haki ya kuwakosoa na pia watufahamishe hayo waliyaacha ili 'kulinda heshima' ya serikali ni yapi.

Watanzania lazima tusimame kidete ili wajumbe wa hizi kamati ambazo zinatumia mabilioni ya pesa za walipa kodi wajue fika kwamba wanaripoti kwa Watanzania ambao wanataka full report siyo ripoti nusu au robo ili 'kulinda heshima ya serikali'. Huku kulindana ndiko kulikoifikisha nchi yetu njia panda, kama tusipokuwa na umoja basi mafisadi wataendelea kuiangamiza Tanzania kila kukicha.

Hakuna mtu ambaye ana nia ya kumchafua Mwakyembe. Leo kafanya Mwakyembe, kama Watanzania hatukumkemea itaundwa kamati nyingine (kama unavyofahamu Tanzania kamati za kuchunguza ufisadi zinaundwa kila kukicha) na mwenyekiti wa kamati hiyo akaona kama Mwakyembe aliweza kuamua nini cha kuandika na nini cha kuacha, basi na yeye akaona anaweza kufuata nyayo za Mwakyembe na kamati yake. Umefika wakati Watanzania tuwaambie hadharani huu upumbavu wa kulindana na kulinda heshima ya serikali tumeuchoka.

Ahsante Mkuu
 
MP Mwakyembe: Attempts to clear scam suspects improper

2008-06-26 11:06:42
By Lusekelo Philemon, Dodoma

Kyela Member of Parliament Harrison Mwakyembe has warned that continued attempts by his fellow ruling CCM legislators to absolve people implicated in the Richmond emergency power generation scandal allegations put the status of the National Assembly at serious risk.

Contributing to debate on the 2008/09 budget estimates of the Prime Minister`s Office in the House here yesterday, he said the attempts were ill-timed and therefore improper, uncalled-for and a disgrace to the House.

Dr Mwakyembe reminded the House that he chaired a parliamentary select committee formed last year to look into the circumstances under which the government awarded Richmond Development Corporation the power generating contract.

The team`s report was presented to the National Assembly early this year and the government is understood to be still working on its recommendations.

The legislator said what his colleagues were doing contravened the House rules and regulations because MPs had already formally discussed the committee`s findings and recommendations.

He added: ``According to provisions in the House Standing Orders, all deliberations must finally come to an end.

However, if some MPs are dissatisfied with any decisions made on this (Richmond saga) issue, we should agree to annul the provisions prohibiting us from deliberating on the matter to allow them to speak their minds.``

He said if the House decided that way, ``then it will be only fair for the parliamentary select committee to spill the beans by saying even those things we decided not to reveal as a way of safeguarding the government`s integrity``.

Members of the committee were more than ready to relinquish their legislative seats if it were proved that they implicated anyone in their report out of sheer malice, Dr Mwakyembe noted.

He urged those out to ``cleanse`` government officials named in the report to be ready to surrender all their leadership positions if they fail to prove that those mentioned were unfairly treated.

``If necessary, we will need to annul some of the provisions in the Standing Orders and have the matter brought back to the House so that the public can know the full details of the saga,`` he said.

``How can the public out there continue to hold members of the august House in high esteem if we keep discussing issues that we have been already discussed and concluded?`` he wondered.

Dr Mwakyembe`s charged remarks came only a day after a CCM legislator Samwel Chitalilo (Buchosa) took time in the National Assembly to defend prominent people implicated in arguably one of the most damaging grand corruption scandal allegations in recent memory in Tanzania.

The key figures he defended include immediate former President Benjamin Mkapa, who is said to be closely linked to the controversial privatisation of Kiwira Coal mines.

One of the others is immediate former Prime Minister Edward Lowassa, who resigned some time ago after being widely associated with the Richmond scam allegations but went away vehemently denying any involvement.

Chitalilo argued that it was a complete waste of time to continue discussing the public figures who also include immediate former Infrastructure Development minister Andrew Chenge, who resigned recently over reports that he had a staggering 1.2bn/- allegedly banked in a suspicious bank account on Jersey Island in the UK.

Richmond Development Corporation, which is said to be US-based, was contracted to bring in generators to make available 100 megawatts a day after a serious drought in early 2006 led to severe power cuts.

However, the firm failed to provide the emergency power during a power crisis. By the time the company was ready to start operations, the country�s power problems were over.

All the same, according to the terms of the contract, the government was obliged to pay the firm more than $100,000 a day in capacity charges even if there was no electricity generated and supplied.

It was when things came to a head after the tabling of the Mwakyembe Committee report in the National Assembly that the then Prime Minister Lowassa and ministers Nazir Karamagi (Energy and Minerals) and Ibrahim Msabaha (East African Cooperation) resigned over the scam allegations, citing political responsibility.

The three resignations made President Jakaya Kikwete dissolve the cabinet, naming Mizengo Pinda as Lowassa`s successor.

SOURCE: Guardian
 
Kama kuna mchango muhimu kwa Taifa letu umefanywa na Bunge, ni Ripoti ya Kamati ya Mwakyembe. Imefufua matumaini ya Watz wote na kuchochea uwazi na uwajibikaji kwa viiongozi waliokuwa wanakula bila kujali, bila kunawa na kufuta midomo yao. Leo, kuanza mjadala wa kusema Mwakyembe hafai eti kwa sababu ya maneno mawili aliyotumia akiwashughulikia mafisadi, ni utoto kama siyo umamluki. Kwanza sijui kama tulimwelewa vema mwanasheria huyo. Pili, kulinda heshima ya Serikali ni dhana ya kila kiongozi aliyeapishwa. Inaweza kuwa si dhana ya wana JF, lakini huo ndo ukweli. Lakini cha msingi, utamuuaje Jemadari aliyepiganisha vita tukashinda ati kwa maneno mawili usiyoyaelewa vizuri aliyosema baada ya ushindi? Chonde chonde, tusiingie mtego wa kuwasafisha akina Lowassa, Karamagi, Rostam na Mzee wa Vijisenti kwa kuwalaumu bila sababun ya msingi waanzilishi wa mapambano marefu na magumu ya ukombozi wa TZ.
 
Yale makaripio aliyoyatoa Mwakyembe kuwanyamazisha wale walioamua kuwaogesha maji mafisadi watakate ili waendelee kuvaa suti zetu huyu Mh. Mwakyembe aliyatoa kwa jazba kwa lengo la kuwanyamazisha ila kwa kweli katika kamati yake aliona mengi. Huwezi kumuaibisha "Mzee" kuwa kakaa vibaya mbele ya wadogo zako. Heshima lazima iwepo ila Mh. Pinda anachotakiwa ni kuifanyia kazi hadi kuwueleza "Mzee" kwamba kakaa vibaya ili siku nyingine asikae vibaya mbele ya watoto. Idumu JF
 
Jamani; Sio Mwakyembe PEKE yake, yumo pia Mh. Seleli, Eng. Manyanya, Mh. Mnyaa,... na Spika aliyewateua!
 
Back
Top Bottom