Kama hayana akili tu! Kelele zote hizo za nini sasa! subiri tutakavyo wasurubisha huko majimboni! unafikiri wananchi vijijini hawajui! Wapinzani hii ni habari njema tumieni mwanya huu! Tuwazomee CCM kwenye mikutani yote, yaani zomea zomea! wakitoa tarkrima kula! halafu kimaliza endelea kuzomea!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Ripoti ya Richmond Bungeni
February 9, 2008
1.0 UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 119 ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007, naomba kutoa taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa tarehe 13 Novemba, 2007 na Bunge hili Tukufu kuchunguza mchakato wa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura uliofanyika mapema mwaka 2006 na kuipa ushindi Richmond Development Company LLC ya Houston, Texas, Marekani.
Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba kuchukua fursa hii kwa niaba ya wajumbe wenzangu wa Kamati Teule kukupongeza wewe binafsi na Bunge lako Tukufu kwa uamuzi wa kuunda kamati hii maalum kwa lengo la kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya kikatiba ya Bunge katika kuisimamia na kuishauri Serikali na vyombo vyake kwa niaba ya wananchi.
Mheshimiwa Spika, baada ya hoja ya kuundwa kwa Kamati Teule kuwasilishwa na kuafikiwa na Bunge, uliwateua Wabunge watano wafuatao kuunda Kamati Teule ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni ya 104(3) ya Kanuni za Bunge, Toleo la 2004:
(a) Mhe. Dk. Harrison George Mwakyembe, Mb
(b) Mhe. Eng. Stella Martin Manyanya, Mb
(c) Mhe. Mohamed Habib Juma Mnyaa, Mb
(d) Mhe. Lucas Lumambo Selelii, Mb
(e) Mhe. Herbert James Mntangi, Mb
Kamati Teule ilianza kuandaa hati (summons) kwa mujibu wa vifungu 13(1) na 14(1) na (2) vya Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge ya Mwaka 1988 (Sura ya 296) za kuita mashahidi mbalimbali waliohusika kwa njia moja au nyingine katika mchakato wa zabuni hiyo ya uzalishaji wa umeme wa dharura.
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 15 Disemba, 2007 jumla ya mashahidi 46 walihojiwa na maswali 2061 kuulizwa. Pamoja na Kamati Teule kutumia vyombo vya habari kuwatia moyo watu wenye ushahidi kuhusu suala hili ili wajitokeze na kuieleza Kamati Teule,
hakuna shahidi hata mmoja aliyekuja kwa hiari yake mwenyewe bila kupelekewa hati ya kuitwa. Aidha, mashahidi wote waliotuletea maelezo kimaandishi kwa njia ya simu au barua, hawakuweka majina yao wala anuani zao, hivyo kuipa Kamati Teule wakati mgumu kufuatilia kauli zao.
Mheshimiwa Spika, matokeo haya yanaonesha hali halisi iliyopo Tanzania, hali ya uoga na ya kutojiamini inayowakumba Watanzania walio wengi wanapotakiwa kuelezea kwa uwazi maneno yale yale wanayoyanongona pembeni kwa hamasa kubwa.
Kwa mtindo huu Taifa letu linaweza kuishia kuwa la walalamishi wasio na ujasiri wala dhamira ya dhati ya kukemea maovu pale inapobidi.
Mheshimiwa Spika, mashahidi wengi walioitwa kwa hati hususan kutoka TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Wizara ya Katiba na Sheria walionyesha hofu, mashaka na hali ya kutojiamini kwa kutoa majibu yaliyofanana ya kiitifaki-itifaki na yaliyokosa mvuto na ushawishi wa kawaida mithili ya watu walioketishwa pamoja na kukaririshwa hoja za kujibu.
Wataalam wa TANESCO, mathalan, waliikataa Richmond Development Company LLC mara tatu wakati wa kutathmini zabuni ya umeme wa dharura, kwa hoja za kitaalam kuwa haifai kwa vigezo vyote muhimu.
Walipofika mbele ya Kamati Teule, wakawa wapambe nambari moja wa kampuni hiyo, wote wakiimba sifa za kulazimisha za kampuni hiyo!
Aidha, nyaraka nyingi ambazo Kamati Teule ilizipata toka Serikalini na taasisi mbali mbali, zilikuwa nakala zilizokosa mtiririko wa kimasijala. Kamati Teule ilipodai nyaraka halisi kulinganisha na nakala ilizokuwa nazo, ilipewa majalada yaliyoonyesha dalili zote za kukarabatiwa.
Mheshimiwa Spika, hali hii ilijitokeza zaidi kwa TANESCO na Wizara ya Nishati na Madini. Jalada halisi kutoka TANESCO lilichukua siku tatu kuifikia Ofisi Ndogo ya Bunge likiwa na nyaraka zenye namba zilizokosa mtiririko stahili.
Wizara ya Nishati na Madini ndiyo iliyotia fora kwa kumtuma Msaidizi wa Katibu Mkuu, Ndugu Julius Sarota tarehe 18 Disemba 2007 akiwa na maagizo ya kuwafungulia Wajumbe wa Kamati Teule kurasa maalum tu na si nyinginezo hivyo kuinyima Kamati Teule mtiririko halisi wa mawasiliano.
Kamati Teule haikuridhishwa na utaratibu huo, hivyo ilimtaka Msaidizi huyo wa Katibu Mkuu aondoke na majalada yake na kumpelekea hati ya kuitwa Katibu Mkuu, Ndugu Arthur Mwakapugi afike yeye mwenyewe na majalada hayo.
Wakuu wote JF, wasalaaam waleiykum!
- Katika siku za karibuni wananchi wa Tanzania tumejionea jinsi watawala wetu either wasivyo na maadili na uongozi tuliowapatia kama dhamana tu, wasivyo na adabu na sisi tuliowachagua, wasivyo na heshima kwa katiba na sheria za jamhuri yetu, wasivyo na utu, wengine walevi, waropokaji hovyo hovyo, incompetent, wasiowawajibikaji na ubaradhuli mwingi sana unaoonyesha kutotujali kabisa wananchi wa taifa hili.
- Ningependa sana kuwasikia wapinzani au kwa wale mlio karibu nao, kwamba wanafanya nini kuka-capitalize on yote haya ya uozo wa CCM? Na je tukiwapa uongozi hivi ni kweli watafanya tofauti na hawa waliopo kwenye uongozi wa sasa yaani CCM?
- I was just, thinking aloud!
Respect.
Field Marshall Es!
That will be the End of Tanzania." I dream Edward Lowassa to be the president of this country oneday and Rostam Aziz will be his prime minister"
- Now look, sasa huyu Rostam analilia nini hasa na kwenda kusafishwa na majaji, kati ya mashahidi 75 ni wanne tu waliojitokeza bila kulazimishwa na summons, halafu tizama juhudi za kuwarubuni wabunge kuikana ripoti, pamoja na yote haya kuna wanaosema kwamba eti wamesafishwa na ishu imekwisha, hizo ni ndoto za mchana sana! Sasa kama ishu imekwisha kwa nini Rostam analilia kwenda kwa majaji?Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2007 siku ilipowasilisha taarifa yake kwako, Kamati Teule ilikuwa imewahoji jumla ya mashahidi 75 na kuuliza maswali 2717 na kuzipitia nyaraka na kumbukumbu 104. Mashahidi 4 kati ya hao walikuja kwa hiari yao bila kupelekewa hati za kuitwa. Mashahidi 7 waliitwa mara mbili. Mashahidi wawili, Ndugu Daniel Yona na Mhe. Rostam Aziz, (Mb) walipelekewa hati za kuitwa mbele ya Kamati Teule lakini hawakufika kwa maelezo kwamba walikuwa nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika, Ndugu Daniel Yona alitakiwa na Kamati Teule atoe maelezo kuhusu msingi wa uamuzi wake wa kuipa Richmond Development Company LLC, haki maalum ya kipekee (exclusive right) ya miezi 18 kuhusu mradi wa Bomba la Mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza mwaka 2004 wakati huo akiwa Waziri wa Nishati na Madini. Maelezo ya ziada ya mradi huu nitayatoa baadaye.
Mheshimiwa Spika, vilevile Mhe. Rostam Aziz alitakiwa atoe maelezo kuhusu uhusiano wake na Kampuni za Richmond Development Company LLC na Dowans Holdings S.A baada ya mashahidi kadhaa kudai kuwa ana uhusiano nazo.
Aidha, alitakiwa na Kamati Teule aeleze kwa nini anwani ya barua pepe ya kampuni yake ya Caspian Construction Ltd ilitumiwa na Dowans. Kamati Teule ilitaka vilevile kupata ufafanuzi kutoka kwake kuhusu baadhi ya wafanyakazi wa kampuni yake wanaosemekana kuwa ni watumishi vilevile wa Dowans Holdings S.A.
Mheshimiwa Spika, leo tunapowasilisha taarifa hii mbele ya Bunge lako tukufu, tunajisikia kuutua mzigo mzito sana ulioanza kutuelemea kutokana na kuzongwa kila kukicha na kila aina ya uzushi, uchochezi, uchonganishi na hata vitisho. Tumezushiwa kuhongwa magari ya kifahari na fedha taslimu; tumetuhumiwa kuendesha vita dhidi ya Waislamu na mara nyingine tuhuma hiyo ikageuka kuwa vita dhidi ya Wakristo ndani ya Serikali; tumesingiziwa kuibadilisha taarifa yetu mara mbili, baadhi wakisema kwa ushawishi wa fedha, wengine wakidai kwa shinikizo la Mhe. Spika na wengine kwa shinikizo la Waziri Mkuu;
tumeshuhudia pilikapilika za usiku na mchana za kujipanga na kuwashawishi baadhi ya Mawaziri na Wabunge kuikana taarifa hii na mapendekezo yake kiasi cha wengine wetu kujiuliza: kulikoni mtu asiye na hatia kuweweseka?
Niliyasema haya Novemba 10 mwaka jana... Wala hayajachukua muda!Huu ni uhuni sasa, ni mbinu ya kuwamaliza watu kitaratibu! Wengine hamtanielewa leo. Ni heri liwalo na liwe, mjadala huu ufungwe before 2010!