Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Quote:- Fact

2. However, if some MPs are dissatisfied with any decisions made on this (Richmond saga) issue, we should agree to annul the provisions prohibiting us from deliberating on the matter to allow them to speak their minds.``


Kwakweli ninakuwa guided na huu ukweli hapa juu katika hoja yangu, umesema mengi lakini kwangu it comes down to this, kwamba kuna ambayo hakusema kwa sababu ya kubanwa na sheria za kulinda siri za serikali.

Mengine yote uliyosema ni kweli tupu, lakini integrity ya Mwakyembe abdo iko pale pale kwa sababu ya sheria iliyomzuia asiseme yote, ikivunjwa kama alivyomuomba Spika, na akashindwa basi integrity ya Mwakyembe itakuwa na tatizo, lakini so far bado ni shujaaa wangu na integrity yake iko sawa sana.


Mkuu FMES, heshima yako. hapo ndio unapochanganya mambo na nahisi kwamba ni kwa makusudi tu. Hakuna sheria yoyote iliyomzuia mheshimiwa Mwakyembe asiseme yote yaliyo kwenye ripoti yake zaidi ya muda tu. Kama ipo tutafurahi ukitufahamisha hapa.Sheria/kanuni ambayo mheshimiwa Mwakyembe anataka/anaomba ivunjwe ni ile inayotaka mjadala ambao umeishajadiliwa bungeni usirudiwe kujadiliwa tena bila kuvunjwa kwa sheria/kanuni husika namba 53/54kama sijakosea sana.

Kwa maana hiyo mheshimiwa Mwakyembe anaomba kanuni/sheria hiyo ivunjwe
ili mjadala wa Richmond urudishwe tena bungeni kujadiliwa ili watuhumiwa wajitetee tena na yeye "aseme hata kile alichokuwa ameacha kukisema kwa ajili ya kulinda heshima ya serikali".

kauli hii ina maana kuwa hakuna sheria yoyote inayomzuia kusema kile anachotaka kusema zaidi ya hiyo ya kuwa ni lazima sheria/kanuni husika ivunjwe kwanza ili mjadala urudishwe tena bungeni!

Tunaweza tukazungusha maneno tunavyotaka katika kumtetea mheshimiwa lakini ukweli uko pale pale hata kama tunajitahidi kutouona. Pamoja na kazi yake njema aliyotufanyia ambayo tunamshukuru kwayo, kwa hili la 'kuilindia heshima serikali' ametokota na lazima tumuambie maana ameturudisha kule kule kwa kulindana tunakotaka kutoka!
 
Mkuu nimekusikia sana, ninaomba ku-retire kutoka hii topic maana nimesema ya kutosha na sasa kama kawa yangu huwa ninaawaachia wananchi waamue mchele na pumba zilipo, ila ahsante sana kwa ujumbe wako.
 
Dk. Mwakyembe anamlinda nani?

Tahariri
Tanzania Daima

KAULI ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kati ya Kampuni ya Richmond ya Marekani na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuwa Spika aruhusu kuvunja kwa kanuni za Bunge ili kutoa fursa ya kujadili kwa kina sakata hili, bado inaendelea kutufikirisha mbali.

Tulieleza mapema kuwa, tunakubaliana na kauli hiyo ya Dk. Mwakyembe baada ya kubaini kuwa kumbe kulikuwa na mambo yaliyofichwa katika ripoti hiyo kwa sababu alizoeleza kuwa ni kulinda heshima ya serikali. Jambo hili bado linatufanya kujiuliza maswali mengi pasipo kupata majibu sahihi.

Kikubwa tunachojiuliza ni nani aliyelindwa katika ripoti ya kamati hiyo, ambaye kutajwa kwake hadharani kuwa naye alihusika katika sakata hilo kunaweza kuondoa heshima ya serikali?

Katika ripoti ya kamati hiyo iliyosomwa bungeni na Dk. Mwakyembe, kulikuwa na mambo mazito yaliyoivua nguo serikali kwa kuhusishwa kwa baadhi ya watendaji wake wa ngazi za juu kwa namna moja au nyingine na sakata hilo. Jambo lililolazimisha wajiuzulu.

Waliolazimika kuachia nyadhifa zao kutokana na kutajwa katika ripoti hiyo ni aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa pamoja na mawaziri wengine, Nazir Karamagi aliyekuwa Wizara ya Nishari na Madini wakati huo na Dk. Ibrahim Msabaha aliyekuwa Wizara ya Afrika Mashariki. Dk. Msabaha ndiye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati mkataba huo unasainiwa.

Ikumbukwe kwamba, baada tu ya Lowassa kutajwa katika ripoti hiyo, aliposimama bungeni hakutaka kujitetea, bali alieleza masikitiko kwa kile kilichoelezwa na kamati hiyo juu yake kuwa kilimfedhehesha sana, kulimdhalilisha na sana na alikuwa ameonewa sana. Kisha akatangaza kuachia ngazi.

Kwa maana nyingine ni kwamba, Lowassa hakuwa anakubaliana moja kwa moja na ripoti ile.

Kama Lowassa, Karamagi naye hakukubaliana moja kwa moja na ripoti hiyo, alikubali kuachia ngazi kwa shingo upande, na mpaka sasa amekuwa akieleza wazi kuwa kamati ya Dk. Mwakyembe ilimuonea na anataka iundwe tume huru ya wanasheria kuchunguza utata huo.

Mbali na hao, hata Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ambaye pia alitajwa katika ripoti ya kamati ya Dk. Mwakyembe naye amesikika mara kadhaa akieleza kuwa kilichofanywa na kamati hiyo ya Bunge si sahihi. Zaidi kwamba zipo tetesi za muda mrefu sasa za kuwepo kwa ripoti mbili zilizoandaliwa na kamati hiyo.

Ingawa madai ya kuwepo kwa ripoti mbili yalionekana kupuuzwa na wengi, lakini mwenendo wa mambo ulivyo sasa unaashiria kuwa waliokuwa wakidai hivyo ni wale waliojua kuwa Dk. Mwakyembe hakueleza kila kitu kilichogunduliwa na kamati yake, kuna watu aliwalinda.

Tunajiuliza, kama ripoti hiyo ilimtaja aliyekuwa Waziri Mkuu naye akalazimika kuachia ngazi kwa fedheha, kigogo mwingine aliye juu ya Waziri Mkuu ambaye kamati iliamua kumhifadhi ili kuilinda serikali ni nani?

Viongozi walio juu ya Waziri Mkuu wanafahamika kuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano na Makamu wa Rais kwa Tanzania Bara na kwa Tanzania Visiwani ni rais wa visiwa hivyo.

Kama Waziri Mkuu alitajwa, ni wazi kuwa anayefichwa katika ripoti ya kamati hiyo ni mzito kuliko Waziri Mkuu ambaye kutajwa kwake kunaweza kuchafua heshima ya serikali.

Tunapenda wajumbe wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza utata huo watambue kuwa, viongozi wote wa kisiasa waliopo madarakani ni kwa ridhaa ya wananchi ambao wanakamuliwa jasho lao ili kuhakikisha wanaishi maisha yenye heshima na hadhi ya juu. Hivyo kama wanahusika na kashfa ya aina yoyote, hasa ya kufuja mali za waliotoa fedha zao kuwatunza, jamii ina haki ya kuwafahamu hata kama haitawahukumu.

Vinginevyo, kama jamii itanyimwa haki hiyo, tutalazimika kusadiki kwamba ripoti ya Dk. Mwakyembe ina upungufu mwingi, na yanayolalamikiwa na waathirika wa ripoti hiyo yana msingi.
 
Wakuu,

Kwa mazingira ya TZ, alichofanya Dr. Mwakyembe ni kikubwa mno na lazima tumpongeze sana. Mapungufu ya kamati yao ni madogo kuliko kile walichoweza ku achieve kwenye hiyo kamati.

Lazima tuelewe, Tanzania bado tuko nyuma sana kwenye mambo ya ukweli na uwazi. Si ajabu kila kitu kingeliwekwa wazi hata spika angeogopa kukubali hiyo report isomwe bungeni.

Kumlaumu Dr. Mwakyembe kwa hili naona ni kumuonea. Ndio tungependa kila kitu kisomwe ili kuanike nje nje ujangili wote wa viongozi wa CCM. Lakini kumng'oa waziri mkuu na mawaziri wawili sio kazi ndogo kwa mazingira ya Afrika.

Labda sasa muhimu ni kwa wabunge wote kuiga ushujaa wa akina Mwakyembe na wenzake na pia kuanza kutetea maslahi ya taifa badala ya kulinda heshima za vyama vyao.

Tukimuunga mkono Dr. Mwakyembe itasaidia hata kwa wabunge wengine lakini tukimrushia madongo kwa makosa yake machache, mafisadi nao watapata nguvu ya kumshambulia zaidi.

Of course ni muhimu kuweka wazi mapungufu ya hiyo kamati kwa lengo la kujifunza na sio ku discredit kile walichofanikiwa.
 
...Of course ni muhimu kuweka wazi mapungufu ya hiyo kamati kwa lengo la kujifunza na sio ku discredit kile walichofanikiwa.

Hakuna aliye "discredit kile walichofanikiwa."

Una distort criticism iliyotolewa dhidi ya Mwakyembe.

Tumesema Mwakyembe shujaa, lakini kachemsha kusema eti aruhusiwe kuja kusema aliyo yaacha moyoni kulinda heshima ya Serikali. Ina maana hana integrity ya kweli ya kutunza heshima ya serikali huyu.

Pili, kama ili kithibitisha mabaya ya Lowassa ilibidi atoe yaliyo moyoni, ina maana hakuthibithisha, kwa maana hakuyasema hayo ya moyoni ili kulinda heshima ya Serikali.

La tatu, ni swali kwa Mwakyembe: Kabla hujaruhusiwa kurudi upya uthibitishe mabaya uliyo yaacha moyoni, na Lowassa arudishiwe cheo chake kwanza?

Mwakyembe acha kuchemka. You know better.
 
Dk. Mwakyembe anamlinda nani?

Kama Waziri Mkuu alitajwa, ni wazi kuwa anayefichwa katika ripoti ya kamati hiyo ni mzito kuliko Waziri Mkuu ambaye kutajwa kwake kunaweza kuchafua heshima ya serikali.

Vinginevyo, kama jamii itanyimwa haki hiyo, tutalazimika kusadiki kwamba ripoti ya Dk. Mwakyembe ina upungufu mwingi, na yanayolalamikiwa na waathirika wa ripoti hiyo yana msingi
.

Asante mwandishi kwa kuweka bayana! Mwakyembe na kamati yake waweke wazi tu, serikali imeshapoteza hadhi, kila kukicha hadhi inazidi kupungua, akichelewa sana kuweka wazi itafika wakati hiyo siri walioificha itakuwa chamtoto kwa mambo yanayoendelea kufumuka kila siku.
 
Hapa kwa kweli huyu Mheshimiwa sio tu kwamba alijikwaa, bali alichemka! Ajifunze na sifa zisimleweshe
 
Asante mwandishi kwa kuweka bayana! Mwakyembe na kamati yake waweke wazi tu, serikali imeshapoteza hadhi, kila kukicha hadhi inazidi kupungua, akichelewa sana kuweka wazi itafika wakati hiyo siri walioificha itakuwa chamtoto kwa mambo yanayoendelea kufumuka kila siku.

Naam na hicho ndiyo wengi tunakitaka, kila kitu walichokiona wakati wa uchunguzi wao kianikwe hadharani, hatutaki haya mambo ya 'kulinda heshima ya serikali' wakati serikali yenyewe imeshajivunjia heshima hiyo. Kama vile tunavyosema mtu mzima hovyoo! basi hii nayo ni serikali hovyooo!
 
Mimi nafikiri hao waliotajwa kwenye ripoti watahojiwa na bunge na watasema kila kitu!
Badala ya kuanza kuwa majaji ama mahakimu kwa kusema hiki kimefichwa...ama kile nk. Ni bora tuweke msisitizo kwa wao kuhojiwa na bunge na kama hawatasema ukweli basi wao ndio watakwenda na maji!
Hakuna haja ya kumkaba mwakyembe! Hao wanaotoa habari kwenye vyombo vya habari na kudai kuwa vita vitatokea basi waende wakaseme huko bungeni ni kwanini wanafikiri kuwa wakifikishwa mahakamani kutakuwa hakuna AMANI!
Na wengine ndiyo wanaitafuta hiyo amani makanisani na kwenye kwaya?
At the same time akizungumzia kuwa waombe na kupokea pesa zake(milioni saba) ili amani ibaki?
 
Naam na hicho ndiyo wengi tunakitaka, kila kitu walichokiona wakati wa uchunguzi wao kianikwe hadharani, hatutaki haya mambo ya 'kulinda heshima ya serikali' wakati serikali yenyewe imeshajivunjia heshima hiyo. Kama vile tunavyosema mtu mzima hovyoo! basi hii nayo ni serikali hovyooo!


Bubu unajua hata kama serikali ikiwa chafu kiasi gani ni lazima kuwe na uongozi. Pamoja na kuwa tunataka nchi yetu iwe corruption free, sio rahyisi kuwaondoa mafisadi wote at once. Suppose leo unaambiwa bunge, mahakama na executive wote ni corrupt, can we change them overnight? No we can't. Kwa hiyo naweza kuelewa mantiki ya Dr Mwakyembe. Kama aliyoweka kando yalimhususu moja kwa moja rais, kulikuwa na usahihi ya kutoweka kwenye ripoti lakini kiustaarabu ni lazima yawekwe mahali pengine ili yaje klushughulikiwa baadaye. Kama angefanya vile kuwa-attck wote basi kungekuwa na vurumai ambazo kwa sasa hatuzihitaji.
 
...Kwa hiyo naweza kuelewa mantiki ya Dr Mwakyembe. Kama aliyoweka kando yalimhususu moja kwa moja rais, kulikuwa na usahihi ya kutoweka kwenye ripoti lakini kiustaarabu ni lazima yawekwe mahali pengine ili yaje klushughulikiwa baadaye. Kama angefanya vile kuwa-attck wote basi kungekuwa na vurumai ambazo kwa sasa hatuzihitaji.

Basi amevunja haki za EL za kikatiba. Katiba hairuhusu uchague wa kum target inapokuja kwenye kuwajibisha watu kisheria.

HAKI NA WAJIBU MUHIMU: Haki ya Usawa, Ibara 13 (1)

"Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria."
 
Tulieleza mapema kuwa, tunakubaliana na kauli hiyo ya Dk. Mwakyembe baada ya kubaini kuwa kumbe kulikuwa na mambo yaliyofichwa katika ripoti hiyo kwa sababu alizoeleza kuwa ni kulinda heshima ya serikali. Jambo hili bado linatufanya kujiuliza maswali mengi pasipo kupata majibu sahihi.

Kikubwa tunachojiuliza ni nani aliyelindwa katika ripoti ya kamati hiyo, ambaye kutajwa kwake hadharani kuwa naye alihusika katika sakata hilo kunaweza kuondoa heshima ya serikali?


tatizo ni kuwa it is faulty reasoning on the part of the TD editorial.... kwanini wanafikiri kilichofichwa ni "mtu"...? How do they leap from "mambo yaliyofichwa" to "nani anayelindwa"? it boggles my mind.
 
tatizo ni kuwa it is faulty reasoning on the part of the TD editorial.... kwanini wanafikiri kilichofichwa ni "mtu"...? How do they leap from "mambo yaliyofichwa" to "nani anayelindwa"? it boggles my mind.


Mwanakijiji,

I wanted to point the same out, nikaona labda there is something I am missing, kumbe na wewe umeona hili... au wanajua what we don't? Kwamba muungwana anahusika? Maana unaweza kufikiri watu wana faulty reasoning kumbe kuna kitu kinaitwa "method to the madness"
 
Pundit.. kama kuna watu wanajua walitakiwa waandike badala ya kuhoji tu.. tatizo wanaweza kuwa wanafikiri wanajua na hivyo swali lao kuwa halina msingi (kama unajua kitu kwanini unauliza?)
 
Mwanakijiji,

I wanted to point the same out, nikaona labda there is something I am missing, kumbe na wewe umeona hili... au wanajua what we don't? Kwamba muungwana anahusika? Maana unaweza kufikiri watu wana faulty reasoning kumbe kuna kitu kinaitwa "method to the madness"

Hili la muungwano kuhusika sio tena speculation au hypothesis, it is real and true. Kumbuka mahojiano yake na gazeti la the Guardian (IPP) mwaka juzi wakati sakata hili linaanza na jinsi alivyosimama kidete kuitetea kampuni ya Richmond na kuwathibitishia watanzania kuwa hiyo ni kampuni ya uhakika. Labda kama mtu anaweza kutunyanyulia tena ile article ya the guardian.

Mwakyembe alisema anatunza "heshima ya serikali". Sasa serikali sio majengo, ni watu wanaofanya kazi katika taasisi hizo za serikali. Sasa anaposema alinda heshima ya serikali ni kwamba analinda heshima ya watendaji hao wa serikali, akiwemo muungwano. I don't see why TD editorial should be blamed on what they wrote. We should not look for scapegoats; Mwakyembe is to blame himself for what he said. We should hold politicians accountable for what they say and do, and Mwakyembe is no exception.

Hebu jitahidini kutafuta namna nyingine nzuri zaidi ya kumtetea Mwakyembe; so far hiyo kauli yake ime-misfire na imezodoa na kumomonyosha heshima na hadhi ya report yake. Someni pia article ya Peter Nyange ya jana, kuna kitu.
 
Bubu unajua hata kama serikali ikiwa chafu kiasi gani ni lazima kuwe na uongozi. Pamoja na kuwa tunataka nchi yetu iwe corruption free, sio rahyisi kuwaondoa mafisadi wote at once. Suppose leo unaambiwa bunge, mahakama na executive wote ni corrupt, can we change them overnight? No we can't. Kwa hiyo naweza kuelewa mantiki ya Dr Mwakyembe. Kama aliyoweka kando yalimhususu moja kwa moja rais, kulikuwa na usahihi ya kutoweka kwenye ripoti lakini kiustaarabu ni lazima yawekwe mahali pengine ili yaje klushughulikiwa baadaye. Kama angefanya vile kuwa-attck wote basi kungekuwa na vurumai ambazo kwa sasa hatuzihitaji.

Oh, yes we can! (Sorry, Obama!) Nothing is Impossible under the sun!!!!
 
Wiki moja iliyopita suala la kuwa Mwakyembe alificha baadhi ya mambo ili kulinda heshima ya serikali ilizua gumzo ila kama gazeti la Mwanahalisi linavyodai ya kwamba probably aliyoyaficha Mwakyembe ni haya makuu mawili.

kwanza uvumi ya kwamba mmoja wa wake za mawaziri waliojiuzulu anadaiwa aliiomba kamati ifiche baadhi ya mabo kumlinda mumewe an kwamba kanda ya rekodi ya mwanamama huyo ipo na waandishi wawili wa gazeti hilo wamekiri kuisikia na kumtambua mke wa kigogo huyo.
Nilifanikiwa kuongea na mmoja wa wandishi wa gazeti hili akakiri ya kwamba baadhi yao waliisikia kanda hiyo na kwamba mke huyo wa kigogo wao wanavyodhani ni Mama Lowassa.Hili la Mama Lowassa its a rumor for the time being ila its to be substantiated.

La pili ambalo linadhaniwa lilifichwa ni kwamba mmoja wa Mwaziri waliopo madarakani hivi sasa(jina sijalipata) alifahamishwa jitihada ya baadhi ya washutumiwa wakifanya juu chini kuhamisha documents zilizokuwa chini ya jina la Richmond kwenda jina la Dowans.

Sasa haya ndiyo makuu mawili yanayodhaniwa kufichwa na Mwakyembe kulinda heshima ya serikali.Inadhaniwa ya kwamba Spika alipata maelezo yote hata hiyo kanda ila alipoulizwa alikana kuwa nayo.
 
wangeyatoa tu hayo hadharani hakuna heshima ya serikali hapo. mi nilifikifi alificha jina la kikwete?? mi nina mashaka bado si hayo tu, yapo mengi ngoja tuendelee kudodosa
 
wangeyatoa tu hayo hadharani hakuna heshima ya serikali hapo. mi nilifikifi alificha jina la kikwete?? mi nina mashaka bado si hayo tu, yapo mengi ngoja tuendelee kudodosa

Nakushukuru mkuu kwa kulitambua hilo ndio maana hata mimi nimeweka doubts.Ila tuendelee tuu kuna mengi zaidi ya haya na makuu zaidi.
 
Kama nilivyoweka msimamo wangu hapo juu ni lazima uchunguzi wa kipolisi upewe nafasi ili tujue yote kinagaubaga.yaliyofichwa yavumbuliwe zaidi na yaliyosemwa yachunguzwe zaidi.hatuwezi kuchezewa akili tuu bila sababu na watu wawili watatu ambao masl;ahi yao ni very shady.
 
Back
Top Bottom