Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Kama nilivyoweka msimamo wangu hapo juu ni lazima uchunguzi wa kipolisi upewe nafasi ili tujue yote kinagaubaga.yaliyofichwa yavumbuliwe zaidi na yaliyosemwa yachunguzwe zaidi.hatuwezi kuchezewa akili tuu bila sababu na watu wawili watatu ambao masl;ahi yao ni very shady.

Hivi mkulu unafikiri polisi gani atachunguza na kukwambia kuwa JK anausika kwenye RD, haiwezekani hata kidogo, kwenye hili JK aliamua kumtosa EL kwa makusudi kabisa kwani hata yeye anasitahili kuwajibika kama waziri wake mkuu alikiuka maelekezo ya balaza la mawaziri yeye kama bosi alichukua hatua gani kuakikisha kuwa anamwajibisha kabla ya tume ya bunge.

Huu ni usanii na ndo maana EL amechukia sana kwani deal walicheza wote halafu akamtoa kafara peke yake.
 
Wiki moja iliyopita suala la kuwa Mwakyembe alificha baadhi ya mambo ili kulinda heshima ya serikali ilizua gumzo ila kama gazeti la Mwanahalisi linavyodai ya kwamba probably aliyoyaficha Mwakyembe ni haya makuu mawili.

kwanza uvumi ya kwamba mmoja wa wake za mawaziri waliojiuzulu anadaiwa aliiomba kamati ifiche baadhi ya mabo kumlinda mumewe an kwamba kanda ya rekodi ya mwanamama huyo ipo na waandishi wawili wa gazeti hilo wamekiri kuisikia na kumtambua mke wa kigogo huyo.
Nilifanikiwa kuongea na mmoja wa wandishi wa gazeti hili akakiri ya kwamba baadhi yao waliisikia kanda hiyo na kwamba mke huyo wa kigogo wao wanavyodhani ni Mama Lowassa.Hili la Mama Lowassa its a rumor for the time being ila its to be substantiated.

La pili ambalo linadhaniwa lilifichwa ni kwamba mmoja wa Mwaziri waliopo madarakani hivi sasa(jina sijalipata) alifahamishwa jitihada ya baadhi ya washutumiwa wakifanya juu chini kuhamisha documents zilizokuwa chini ya jina la Richmond kwenda jina la Dowans.

Sasa haya ndiyo makuu mawili yanayodhaniwa kufichwa na Mwakyembe kulinda heshima ya serikali.Inadhaniwa ya kwamba Spika alipata maelezo yote hata hiyo kanda ila alipoulizwa alikana kuwa nayo.

Kevo,
Je inawezekana Mwakyembe aliyaweka haya kikombo ili ayatumie kama akina Lowassa wakileta nyodo kama wafanyavyo hivi sasa?

Mwakyembe amesema anataka hili suala lifunguliwe upya ili ukweli uonekane, sio kuwa ndio anataka aweke shahidi zake zote, including kumuumbua huyo mama ambaye hapo awali aliona haitapunguza nguvu ya hoja yake?

Kwa maoni yangu ni kuwa, labda hayo aliyoyaacha yasingebadili sura ya kesi na matokeo aliyoyataka, yaani kumpiga chini Lowassa. Lakini sasa anapoona vioja vyao ndio anaona kama ilivyo kwa mwanasheria yeyote mjanja, kutumia ushahidi wake wote alionao kummaliza muungwana. Nafikiri anayehitajika kusikilizwa tena ni Mwakyembe, upolisi unawza kutoa ripoti sawa na ya uchawi wa Chenge.
 
Kama nilivyoweka msimamo wangu hapo juu ni lazima uchunguzi wa kipolisi upewe nafasi ili tujue yote kinagaubaga.yaliyofichwa yavumbuliwe zaidi na yaliyosemwa yachunguzwe zaidi.hatuwezi kuchezewa akili tuu bila sababu na watu wawili watatu ambao masl;ahi yao ni very shady.

Hakuna polisi anayeweza kufanya kazi hii Tanzania. Mfano rahisi umeuona kwenye issue ya AC na vijiunga vyake bungeni.
 
Kuna kiza kinene mbele .....

Kiza hicho ndio mimi na wewe tunapaswa kukiangazia macho mkuu na siyo kukaa tuu.Its time to react and push the government to do so hasa kama uko kwenye ofisi husika.
 
Bomu la Mwakyembe lalipuka

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele

Ni katika Sakata la Richmond
Mke wa waziri alipigia magoti Kamati
Mwingine afumwa usiku wa manane

MKE wa mmoja wa mawaziri watatu waliojiuzulu kutokana na sakata la Richmond, alipigia magoti baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge akiomba wamlinde mume wake, imefahamika.

Hili ni moja ya mambo ambayo hayamo ndani ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge na ambayo yalipaswa kuwekwa wazi.

Timu ya waandishi wa habari za uchunguzi ya MwanaHALISI imegundua kuwa mke wa kigogo huyo (jina tunalo), alikwenda mbele ya wajumbe wa Kamati kwa lengo la kushawishi Kamati “imlinde” mumewe.

Hata hivyo, mwanamke huyo aliambiwa kuwa asubiri ripoti itoke kwa kuwa wao walitumwa kuchunguza na siyo kuhukumu.

Gazeti hili pia limegundua kuwa mmoja wa mawaziri wa sasa “aliwafuma” vigogo wawili (majina tunayo) katika ofisi ya serikali, usiku wa manane wakiwa katika harakati za kubadilisha mkataba huo kutoka Richmond Development Company (LLC) kwenda kwa dada yake Dowans.

Haikufahamika haraka kama hili ni moja ya mambo ambayo mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe alisema kamati yake haikuyataja kwa shabaha ya “kulinda serikali.”

Akichangia mjadala wa bajeti ya ofisi ya Waziri mkuu, wiki mbili zilizopita, Dk.Mwakyembe alisema kama kuna mtu anadhani hakujitetetea vya kutosha, basi mjadala uanze upya kuliko kutenda kinyume na Kanuni za Bunge.

Alituhumu baadhi ya wabunge akisema wamevunja Kanuni za 54 na 55 za Bunge zinazozuia jambo ambalo lilikwishajadiliwa bungeni kurejewa kujadiliwa.

“Kama watuhumiwa wana mambo hawakuyasema, turudishe mjadala huu upya. Waseme wanaoyajua na sisi tupo tayari kueleza hata yale ambayo tuliacha kueleza kwa kulinda heshima ya serikali,” alisema.

Kauli ya Dk. Mwakyembe ilitokana na kile kinachoelezwa kuwa jitihada za baadhi ya wabunge na vyombo vya habari kutaka “kuwasafisha” watuhumiwa.

Inaelezwa kwamba mke wa kigogo aliyepigia magoti baadhi ya wajumbe wa Kamati, alirekodiwa na kanda yake imetolewa nakala na kuhifadhiwa na baadhi ya wajumbe.

MwanaHALISI haikuweza kuthibitisha kama kanda hizo zilimfikia Spika wa Bunge Samwel Sitta ambaye alipoulizwa kuhusu suala hili alisema ana taarifa na alichopewa peke yake.

Waandishi watatu wa gazeti hili walisikiliza kanda hiyo na hawakuwa na utata katika kutambua mara moja sauti ya mke huyo wa kigogo aliyekuwa akitafuta huruma kwa mume wake.

Naye Mwakyembe alipoulizwa kuhusu taarifa za mke wa kigogo na kanda zake, alijibu haraka, “Kazi yetu iliisha zamani. Hakuna mjadala mpya.”

Imebainika kuwa Richmond, kampuni ya kufua umeme, ilipewa zabuni kwa upendeleo. Aidha, imedhihirika kuwa kampuni hiyo iligawa mkataba wake kwa kampuni ya Dowans kinyume cha taratibu.

Kutokana na hali hiyo, wiki iliyopita, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) lilitangaza kuvunja mkataba wa Dowans na kuitaka kampuni hiyo kuodoa mitambo yake nchini.
 
Ripoti ya Richmond imeleta changamoto nyingi katika Serikali na Jamii na kwa kamati yenyewe.Wewe unaonaje?
 
Mimi binafsi, naona Ripoti hiyo, imemtambulisha Mwakyembe ni nani: Aliyefanikisha fitina za kumzulia kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, anahusika na Richmond, mpaka akaamua kuachia ngazi.

Ushahidi wa Mwakyembe kuwa Lowassa anahusika ni habari za "kung'ata sikio" na kudokezwa na baadhi ya watu nje ya kiapo kuwa "jeuri yote inaonyesha kuwa kuna mkubwa fulani" anahusika!

Ushahidi mwingine ni maandishi ya gazeti la Saed Kubenea la MwanaHalisi, ambalo habari zake ni kuwaandama "watu fulani" na siyo kuandika "issues".

Imethibitika kuwa Lowassa hakuhusika, lakini akajiuzulu kwa kuwajibika kisiasa!

Kilichokosewa awali ni kutowajibishwa kwa aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha, ambaye ndiye aliyewajibika Wizarani mpaka Kampuni ya Richmond ikapewa zabuni na baadaye ikajitoa kwa kushindwa kazi.

Mwakyembe, pamoja na Spika, waliukataa kata kata na kuutupilia mbali, ushahidi wa Lowassa wa maandishi kuwa alimuandikia Msabaha Septemba 2006, kumtahadharisha kuwa ni vema ajiridhishe uwezo wa Kampuni hiyo, lakini Msabaha alishindwa kujiridhisha na hakuchukuliwa hatua wakati huo, mpaka alipolazimika kujiuzulu baada ya WM kusema anajiuzulu! Mambo haya sasa yanafukuka na ukweli, ambao kwa kawaida huwa haukubali kugubikwa na uongo, unajitokeza!

Miaka mitatu ya Richmond, EPA, Ufisadi, imeigharimu CCM na Serikali yake kusuasua kutekeleza Ilani ya Uchaguzi. Walianza vizuri na Shule (Sekondari za Kata, Chuo Kikuu cha Dodoma), chini ya usimamizi wa Lowassa, lakini wakashindwa kutekeleza Afya (Zahanati kila Kijiji na Kituo cha Afya, Kila Kata).

Serikali ya CCM sasa imekuja na "Kilimo Kwanza", ni mpango mzuri, lakini baada ya kuchelewa sana kutokana na porojo za kisiasa zisizokuwa na tija za Richmond, EPA, Ufisadi n.k. Umaarufu gani kwa Mwakyembe, wakati chama chake cha CCM kinaharibikiwa kwa porojo na fitina za kisiasa zinazochelewesha maendeleo ya nchi hii?

Bwassa
 
nimeshangazwa sana na hii habari inakatisha tamaa

Richmond yazimwa




Na Mwandishi wetu


27th October 2009

Mkutano wa 17 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioanza leo mjini Dodoma hautajadili suala la mkataba wa kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond kwa kuwa Bunge lilishataka majadiliano ya suala hilo yafikie ukomo.
Kaimu Katibu wa Bunge, Thomas Joel, amekaririwa leo asubuhi na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) akisema kuwa, kama kamati hiyo itaona hairidhiki na utekelezaji wa Serikali kuhusiana na azimio hilo, basi inaweza kuleta mabadiliko ya azimio Bungeni yakajadiliwa.
Hata hivyo, amesema suala hilo halijafikia hatua ya kuleta mabadiliko ya azimio hilo Bungeni.
Sakata la Richmond lililitikisa Bunge baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa kujiuzulu mwenyewe kufuatia kuhusishwa na mkataba huo tata. Kadhalika mawaziri wawili, Dk. Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi waliachiwa ngazi kutokana na kuhusishwa na zali hilo hilo.
Kadhalika vigogo wengine wawili waliohusishwa na sakata hilo wameshaachia ofisi zao na kufanya idadi kamili kufikia watano.
Mwanasheria Mkuu Johnson Mwanyika ameenda likizo ya kustaafu hadi Novemba 6 mwaka huu atakapoachia ngazi rasmi ilhali jana, Rais Jakaya Kikwete alitangaza kumuweka kando Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Arthur Mwakapugi, kutokana na maelezo kuwa muda wake wa kustaafu kwa lazima umewadia. Inadaiwa kuwa naye (Mwakapugi), ameshaanza likizo ya kustaafu.
Hadi sasa, mmoja wa watu wanaoendelea kushikilia nyadhifa zao licha ya kutakiwa na bunge kuwajibishwa kuhusiana na sakata la Richmond ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea.
Kuhusiana na mgodi wa North Mara unaodaiwa kumwaga sumu, Kaimu Katibu huyo amesema kuwa suala hilo halitajadiliwa katika mkutano huu.
Amesema taarifa ya kamati iliyoundwa na Spika kuchunguza sakata hilo, imepeleka ripoti yake kwenye kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ambayo bado inaipitia.

CHANZO: ALASIRI
 
Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz ameibuka hadharani na kusisitiza msimamo wake mpya akitaka iundwe tume huru ya majaji, kuchunguza upya kashfa ya mkataba wa kifisadi kati ya Tanesco na Kampuni ya Richmond Development (LLC).

Hii ni mara ya kwanza kwa Rostam kujitokeza hadharani kuzungumzia msimamo huo na chombo cha habari baada ya taarifa zisizo rasmi kumkariri kwamba, alitoa kauli kama hiyo mbele ya Kamati ya Mwinyi, ilipokutana na wabunge wa CCM mjini Dodoma, ambako makombora mazito yalirushwa.

Akijibu maswali ya gazeti hili kuhusu taarifa hizo alizozitoa mbele ya Kamati ya Mzee Mwinyi, Rostam alisema asingependa kuongelea masuala ya vikao vya ndani ya chama, lakini maoni yake ni kwamba tume hiyo ya majaji iundwe na iwapo itamuona ana hatia, achukuliwe hatua za kisheria.

Mbunge huyo alipendekeza pia afukuzwe katika nafasi zote anazoshikilia kwenye chama na Bunge iwapo atabainika kuhusika na ufisadi wowote katika kashfa hiyo ya Richmond.

Rostam ni mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM, lakini amekuwa akitajwa kama mmoja wa vigogo walioshiriki katika kufanikisha Richmond kupewa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura katika mazingira tata.

Mkataba na kampuni hiyo yenye taarifa tata za kutoka Costa Rica na Marekani, ulisainiwa na Tanesco Juni 23, 2006.

Lakini baada ya kusakamwa kwa muda mrefu, alipopata nafasi katika kikao cha kamati ya Mzee Mwinyi na wabunge wa CCM, iliripotiwa kuwa Rostam aliongelea kuundwa kwa tume huru kuchunguza kashfa nzima ya Richmond kwa madai ile ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe ilipotosha.

Hata hivyo, katika majibu yake kwa gazeti la Mwananchi, baada ya kuwasiliana naye kwa kumtangulizia maswali kuhusu ukweli na mantiki ya kauli hiyo, Rostam alisema hawezi kuzungumzia kikao cha CCM, lakini ana maoni kuhusu sakata la Richmond.

"Ripoti ya Richmond imeidhalilisha serikali kwa maslahi ya kisiasa. Ili mambo yaishe ni vema uchunguzi huru ukafanyika. Tusipofanya hivyo tutaendelea kuwachanganya wananchi," alisema Rostam.
"Msimamo wangu tangu kamati teule ya Bunge itoe taarifa yake bungeni, uko pale pale. Ripoti ilijaa upotoshaji na uongo. Nilitaka kuongea bungeni nikazuiwa."

Rostam alifafanua kwamba suluhisho na kukata mzizi wa fitina kati ya pande mbili zinazopingana ni kuunda tume huru ya majaji kufanya uchunguzi.

"Yaliyo ndani ya ripoti hiyo si ya kweli kabisa..., ukweli ni kwamba mimi sihusiki na kashfa ya Richmond... haikutenda haki kabisa," alisema.

Alifafanua kwamba endapo tume hiyo itagundua yeye alihusika kwa namna yoyote na Kampuni ya Richmond basi vyombo vya sheria vimfikishe mahakamani na afukuzwe uongozi ndani ya CCM.

Kamati teule ya Bunge ilisema katika taarifa yake kuwa Rostam aliitwa ili aeleze uhusiano wake na Richmond kutokana na kampuni hiyo kutumia anuani ya barua pepe na fax ya Caspian na sababu za kuitafutia Richmond kampuni ya ushauri wa mambo ya habari, lakini mbunge huyo wa Igunga hakujitokeza.

Rostam alijieleza katika mchango wake wa maandishi wakati wa kujadili ripoti ya Richmond kuwa Kamati ya Mwakyembe ilimuita kumuhoji Desemba 24, wakati ikijua kuwa siku hiyo asingeweza kupatikana kwa sababu ya siku kuu.

Hata hivyo, Dk Mwakyembe alijibu utetezi huo katika mahitimisho yake kuwa watu wengine wanne walioitwa siku hiyo, akiwemo mkurugenzi wa Takukuru, Dk Edward Hoseah, walijitokeza siku hiyo na kuhojiwa.

Msimamo mpya wa Rostam umekuja zaidi ya mwaka mmoja baada ya jaribio jingine la kuhoji ripoti ya Kamati ya Mwakyembe kuibuka bungeni kiasi cha mbunge huyo wa Kyela kulazimika kusimama na kuhoji sababu za Bunge kuwa kigeugeu, akisema kama hawaridhiki na ripoti hiyo basi suala hilo liwasilishwe upya na wataanika uozo zaidi ambao waliusitiri kwa manufaa ya taifa.

Katika mkutano wa Kamati ya Mwinyi na wabunge, ripoti hiyo ya Mwakyembe ililaumiwa kuwa iliwaonea waathirika, hasa Edward Lowassa, aliyelazimika kuachia uwaziri mkuu na kutaka kuundwa kwa tume huru.

Lakini Dk Mwakyembe alionya wabunge kuacha mara moja kuongelea ripoti ya kamati yake kwa kuwa ni msimamo wa Bunge.

Dk Mwakyembe aliweka bayana kwamba wabunge wanaoendelea kuihoji ripoti hiyo wanaweza kujikuta wakifungwa.

Tayari Spika wa Bunge, Samuel Sitta ameshaapa kwamba suala la Richmond halitarudi nyuma na aliazimia limalizwe katika mkutano wa 17 uliomalizika, lakini serikali ilicheza karata dume na kulipiga chenga Bunge.

Baada ya Dk Mwakyembe kuwasilisha ripoti ya Richmond Februari mwaka jana, Lowassa na mawaziri wengine wawili waliowahi kuongoza Wizara ya Nishati na Madini, Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi waliachia nyadhifa zao.

Lakini huo ukawa mwanzo wa makundi ndani ya CCM ambayo sasa yamefikia hatua ya kuvuana nguo kutokana na kujikita zaidi katika kuzungumzia mwandani.

Source: Mwananchi la kesho
 
Huu ni uhuni sasa, ni mbinu ya kuwamaliza watu kitaratibu! Wengine hamtanielewa leo. Ni heri liwalo na liwe, mjadala huu ufungwe before 2010!
 
Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz ameibuka hadharani na kusisitiza msimamo wake mpya akitaka iundwe tume huru ya majaji, kuchunguza upya kashfa ya mkataba wa kifisadi kati ya Tanesco na Kampuni ya Richmond Development (LLC).




Source: Mwananchi la kesho​


Naona Rostam Aziz na Zitto Kabwe wamegongana kimawazo. Maana wazo hili hili la tume ya majaji lilitolewa na Zitto awali; swali la kujiuliza, ni nani wa kuteua hao majaji? Na vipi taarifa ya kamati tuele kuhusu richmond imekuwa tofauti sana na ya TAKURU? Sasa tuuende chombo cha tatu kwa suala hilo hilo?

........ndiyohiyo
 
Inji hii sasa haina uelekeo kabisa, ukiangalia kushoto Richmonduli, Chadema wanatafunana wenyewe kwa wenyewe, ukiangalia nyuma CUF wamewa-disappoint wafuasi/wanachama wake bara + visiwani(muafaka with Karume) ukiangalia mbele GIZA!!!

What next???
 
Naona Rostam Aziz na Zitto Kabwe wamegongana kimawazo. Maana wazo hili hili la tume ya majaji lilitolewa na Zitto awali; swali la kujiuliza, ni nani wa kuteua hao majaji? Na vipi taarifa ya kamati tuele kuhusu richmond imekuwa tofauti sana na ya TAKURU? Sasa tuuende chombo cha tatu kwa suala hilo hilo?

........ndiyohiyo
Si wanasema kitu kikishajadilwia bungeni hakiwezi kuhojiwa nje ya Bunge!!!! Sasa hao majaji watachunguza kwa msingi gani?
 
Ni kuzidi kupoteza bure pesa za wapiga kura na walipa kodi, kwanini wasinunulie madawati watoto wetu waache kukaa chini. Tume baada ya tume LOL....tumelogwa?
 
Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz ameibuka hadharani na kusisitiza msimamo wake mpya akitaka iundwe tume huru ya majaji, kuchunguza upya kashfa ya mkataba wa kifisadi kati ya Tanesco na Kampuni ya Richmond Development (LLC).
Source: Mwananchi la kesho​

Jiwe la kuwatumbukiza baharini naona lishkaba koo!!
Alikuwa wapi kutoa ushirikiano muda wote wa miaka miwili?
Kusafishana kwa kutumia viongozi serikalini, waliotumika kama toilet paper inaelekea kumegonga mwamba.
 
Bhayanda,

Inchiiii sasa imeisha poteza kweli mwelekeo yawezekana ikawa ni Viongozi wetu ni mbumbu wa kutizama alama za nyakati kwa visingizio kuwa wanaonewa au kuoneana!

Jamani kama wewe kiongozi wajua fika hukubaliki sasa jamani mtupishe na hizi kashfa zenu zimetuchoshaaaaaaaaa eeeeh bwana kila kukicha mwatumia vyombo vya habari kutu propaganda zenu,

Weeeeeee Tanzanian tu mechoshwa sasa na kutumia Medias kujilazimisha kujisafisha jamani hamuoni kuwa we umeambiwa umechemka kama we wazani hujachemka si basi uwapishe hao wanojifanya wao ndio viongozi bora wang'ang'ania nini hayo madaraka????

Napenda kuwaaaambieni Madhala ya kumchagua Nani wae Rais wetu 2005 pale chimwaga Dodoma dio haya sasa yanajirudi,

Turudi na Ukweli na sina ubaya na mtu to be honesty ni kwamba Urais 2005 kati ya Dr. S. Ahame na M.J Kikwete ni wazi palichezwa mizengwe JK alikuwa hana ubavu wa kung'oa Dr. S. Ahamed wanamtandao walilijua hilo na wakatembeza $'s na Mi pound kwa kwenda mbele.

Pili ni kosa kubwa sana kumwingiza mfanyabiashara kwenye chama na ndicho Kime gharimu CCM kumbukeni Mwl. JK Nyerere matajiri walipa pesa na alikuwa na uwezo wa kujenga hoja sasa kipindi hiki viongozi tulio nao hawawezi kujenga hoja na matajiri waweze kuwa saidia matokeo yake ndio haya sasa

Tajiri hakustahili kuingia kwenye mambo ya chama yeye alipaswatoa michango kwa kusaidia chama na sio ati awe na sauti ndani ya chama, hilo mlikubali wana CCM.

Uadilifu wa viongozi huko wapi jamaniiiii RA anataka nini mbona yule mbunge wasingida anaitwa na Dewej au ni Manji mnisaidie hapo hayuko kwa scandal iweje huyu ndg yangu RA.

RA hatukutaki ujisafiche tunacho kuomba Jiuzulu period nothing more
 
Nahisi huyu Jamaa anaogopwa yaani anaomba apelekwe Kwa Kamati ya Mapilato? Duh Kaaazi Kweli kweli
 
Msimamo mpya wa Rostam umekuja zaidi ya mwaka mmoja baada ya jaribio jingine la kuhoji ripoti ya Kamati ya Mwakyembe kuibuka bungeni kiasi cha mbunge huyo wa Kyela kulazimika kusimama na kuhoji sababu za Bunge kuwa kigeugeu, akisema kama hawaridhiki na ripoti hiyo basi suala hilo liwasilishwe upya na wataanika uozo zaidi ambao waliusitiri kwa manufaa ya taifa.

huu ndo upumbavu wa huyu mtu..i take him very low and to me he is like a comedian..they had time to dig and report everything asking to be given another chance si upumbavu huu...
 
Naona Rostam Aziz na Zitto Kabwe wamegongana kimawazo. Maana wazo hili hili la tume ya majaji lilitolewa na Zitto awali; swali la kujiuliza, ni nani wa kuteua hao majaji? Na vipi taarifa ya kamati tuele kuhusu richmond imekuwa tofauti sana na ya TAKURU? Sasa tuuende chombo cha tatu kwa suala hilo hilo?

........ndiyohiyo

Zitto akisema mambo hawayakubali kwa kuwa hayuko CCM...lakini baadaye ukweli unakuja kuonekana na wanafanya yale yale wanayoambiwa na wanaowaita wapinzani
 
Back
Top Bottom