Ripoti ya siri ya kusikitisha shule ya sekondari Olasiti Arusha kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza"

Waziri wa elimu ingilia kati swala hili mapema sana'
 
VIFAA VINGINE MUHIMU
(i)Viatu vya ngozi jozi mbili visivyo na visigino virefu na view vya kufunga na kamba
(ii)Soksi nyeusi kwa wavulana na nyeupe kwa wasichana
(iii)Daftari(counter) kumi au zaidi
(iv)T-shirt,Bukta na raba kwa ajili ya michezo(Rengi mtepewa siku ya kuripoti)
(v)Bunda moja la karatasi A4
(VI)Begi la kubebea madaftari
(vii)Jembe,Slasha,ndoo,Skwiza, Fagio(soft broom1 na hard broom 1)
(viiii)Kalamu za wino,Penseli na mkebe wa Hisabati
(ix)Faili(flat file) rangi ya khaki
Hivi vyote mwanafunzi anapaswa anunuwe tofauti na shilingi 425,000/= anazolipa jumlisha mwenye utapa jumla,kisha jiulize ndio maisha bora;

 
Haya ndiyo masuala ambayo watu wa chini wanakutana nayo kila siku.

Watu wa matawi ya juu hawatayaona haya kwa sababu kwanza watoto wao hawasomi kwenye hizo shule za kata anaway.

Pesa ya kitabulisho ni zaidi ya mara mbili ya ada. Huu ni wizi wa waziwazi.

Pia wanachangishiwa pesa ya vitabu, kiti na meza? Ndiyo tumefika huku?

Pia kama hutalipa pesa ya tuition hautaruhusiwa kuingia kwenye hiyo shule? Seriously?

Kweli siyo tuu elimu ya Tanzania sucks, bali ukiwa na kacheo fulani kwenye taasisi ya uma unaweza kufanya chochote utakacho tena kwa maandishi bila wasiwasi.
 
Shule ya kulala haina hizo garama iweje shule ya kata ya kutwa iwe na garama kubwa kuliko ya kulala? Usijadili kwa ushabiki hata kidogo tuweke uzalendo wa taifa kwanza;
 
Kwa michango hiyo ya kushangaza,wanajamii wanaoizunguka shule husika,wanapaswa kuchukua hatua mara moja maana ni wazi kuna wizi wa dhahiri.Kabla ya kufikiri kulipa michango hiyo,wazazi na walezi wangetakiwa kwanza kuhoji matumizi ya fedha za ruzuku ya serikali,inayotolewa kila mwaka,kwa kila shule.
Ni jukumu la wanajamii kukomesha ubabaishaji wa Mkuu wa Shule.Uhalali wa michango iliyoainishwa punde hauwezi kutetewa na yeyote.
 
Shule ya kulala haina hizo garama iweje shule ya kata ya kutwa iwe na garama kubwa kuliko ya kulala? Usijadili kwa ushabiki hata kidogo tuweke uzalendo wa taifa kwanza;

Hiyo shule ni ya day kumbe? Duh!
 
Serekali lazima iangalie kwa umakini hili swala.
 

elimu ni gharama kaka..hiyo haijafika hata laki 5..kuna wanaolipa million 2 na kuendelea.
 
Ada haifika hata laki tano kwa mwaka kwa secondary?. Mbona ni ndogo sana?. Ni sawa na kuchangia Sh. chini ya 30,000/= kwa mwezi. au sh. 1000 kwa siku.

Acha upongo wewe
 

if u think education is expensive try ignorance.
 
hii michango imezidi kiwango. kwanza hela ya taaluma na remedial kwanini? wakati shule nyingine remedial ni elfu 7500 kwa mwezi.
 
Mwanafunzi aliyekamisha malipo tu ndiye atakayepokelewa shuleni.
Malipo yote yafanyike benki ya NBM,jina la Akauti:Olasiti Sekondari,Namba ya akauti:40810001529(weke ada tu) na 40810001528(weka michango mingine)
‘‘ PESA TASILIMU HAZITAPOKELEWA SHULENI”

2.1 VIFAA VINGINE MUHIMU
(i)Viatu vya ngozi jozi mbili visivyo na visigino virefu na view vya kufunga na kamba
(ii)Soksi nyeusi kwa wavulana na nyeupe kwa wasichana
(iii)Daftari(counter) kumi au zaidi
(iv)T-shirt,Bukta na raba kwa ajili ya michezo(Rengi mtepewa siku ya kuripoti)
(v)Bunda moja la karatasi A4
(VI)Begi la kubebea madaftari
(vii)Jembe,Slasha,ndoo,Skwiza,Fagio(soft broom1 na hard broom 1)
(viiii)Kalamu za wino,Penseli na mkebe wa Hisabati
(ix)Faili(flat file) rangi ya khaki
Paulina A.Bagoye
( Mkuu wa Shule )

Swali kwa kila mtanzania ,Mtoto wa mkulima,mchoma mahindi,msukuma mkokoteni,mchoma mihogo,Watasoma? [/QUOTE]

hii ndiyo elimu ya bule kwa mtanzania hapao hujaweka nauli ya kwenda shule na kurudi
 
elimu ni gharama kaka..hiyo haijafika hata laki 5..kuna wanaolipa million 2 na kuendelea.

Kwa kuwa wanaweza. Wengine wanajitutumua mpkaka dakika ya 90 ili wasiaibike mtaani.
Kwa kauli yako, nakumbuka Mh. Raisi foleni za magari ni ishara ya maendeleo.
 
Nachukia sana kuona wale buk7 huwaoni kuja kujadili maumivu haya ya Watanzania bali wao 24/7 ni kujadili Zitto na Chadema au Chadema itakufa kabla jua halijazama. Uji.nga mtupu! Watanzania wengi wameshaona jinsi CCM ilivyoshindwa kuendesha nchi.
Nenda huko vijijini utayaona ya kutoa machozi lakini kuna watu wamejaa upu.uzi hawayaoni hayo ya watoto kushindwa kusoma, watu kufa kwa kukosa hata dozi ya malaria ,maji safi, na huduma zingine ambazo baadhi ya nchi za kiafrika washasahau kuwa hizo nazo ni shida.



 
Halafu walim wapo sita, maabara analipa lakini hata msingi wa jengo la maabara ukute hamna,. duuh| Nchi ngum hii

  • :couch2:
 
Kwa hali kama hii tutegeme nini haswa kwenye elimu yetu?
 
aise hapa bora aende shule ya private kabisa sijaona tofauti hata chembe, sasa hapo kwenye njano kuna tofauti gani kati ya ujenzi na ukarabati, yaani wizi mtupu, hii inatia hasira sana yaani nasikia hadi hasira sana. Bora private unalipa hela nyingi but you get the best

Chuo cha Ualimu Mhonda nao eti;
serikali ya wanafunzi sh. 5000 kwa muhula
registration sh. 5000 kwa muhula

yaani wao vitu vingi unalipa kwa muhula sasa sijui wanamaanisha nini yaani wizi kabisa, kwa stahili hii watoto wa wakulima watakuwa wanasikia shule kwenye radio tu na watabaki wanasoma wenye uwezo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…