Elections 2010 Ripoti ya wasimamizi wanasheria: Mchakachuo mtupu

Elections 2010 Ripoti ya wasimamizi wanasheria: Mchakachuo mtupu

Mimi ni mwanachama kwa mujibu wa sheria lakini ni chama kinachoongozwa na watu ambao ni UWT au wale wanaonufaika na utawala uliopo. Ndio maana huwa kuna kampeni chafu sana kuhakikisha kuwa wanaogombea na kupata uongozi katika chama hicho ni wale wanaokubalika na serikali. Sijahudhuria mikutano yake kwa zaidi ya miaka 7 kutokana na kupoteza kwake muelekeo. Mwaka 2003 niliiambia kamati ya TLS ilyokuwa inaongozwa na Marehemu Prof. Mwaikusa kutokana na mimi kushikwa na kushtakiwa kwa kesi ya uchochezi wakati nikwatetea watu wa Bulyanhulu kuwa "Pale katika nchi yoyote ile duniani ambapo wanasheria wanalala kitanda kimoja na kula sahani moja na wanasiasa basi nchi hiyo imekufa". Bado ninarudia na kusema hivyo. Tanzania imekufa kwa kuwa wanasheria wengi wanajikomba kwa watawala na wanasahau jukumu lao takatifu la kupigania haki na demokrasia ya nchini.

Umesema vizuri lakini kususia kushiriki ndio unatoa nafasi kubwa ya wao kuendeleza madudu wanayotufanyia,ingekuwa vizuri ukaungana na wenzio ambao wanapenda TLS ifanye kazi kwa matarajio ya uundwaji wake nafikiri matatizo yaliyopo mngeweza kuyaondoa kabisa.
 
Hakuna Kitu Kichwani au Wanaonekana Wanaandika Ripoti ili JK Bosi Wao Asome. Hii Sio kwa Malengo ya Watanzania ni Kwa Ajili ya Halmashauri ya CCM. Inawezekana Hii Ripoti Sio Yetu Sisi, Wamekosea Wikileak Wameiba na Kutopa Online.

Wananchi Siku Zote Wanazungumzia Wasomi Wasomi Ndio Watasaidia Inchi Yao Kumbe Baadhi Kama Hao Serikalini Ndio Wanaimaliza Inchi Yao. Sheria Gani Wamesoma Hawa ili Kuandika au Kusuggest Laws? Katiba ni Muhimu Sana kwa Inchi Yetu na Wanainchi Tutanufaika Sana na Hawa Wanasheria Wanaopenda Hongo Hawatapata Hii Nafasi Kutudanganya Tena. Hii Inaonyesha Mawazo Duni na Utawaliwa wa Utumwa. Huu Uchaguzi Umeandaliwa na Chama Kimoja, Tume ya Chama Kimoja, Kuhesabiwa Kura na Chama Kimoja na Kutangazwa na Chama Kimoja. Hao Wanachama wa Vyama Vingine Hawana Haki Kwa Sababu Gani? Maskini Wanamaliza Vyuo na Kukaa Mitaani Bila Kazi Kwa Sababu Hawana Connections ni Nani Atawabadilisha Kimaisha? Nani Atawateua Wizarani Ziwe 70? Hao Wanasheria Wanaona Utajiri Unaelekea Katika Baadhi ya Familia Inchini, Kwani Wao ni Wanahaki Gani Tanzania?

"Mabadiliko Siku Zote Hayaanzii Juu kwa Viongozi, Siku Zote Yanatoka Chini na Tutalazimika Kufanya Hivi Hata Kama Itakuwa Nguvu"
 
Back
Top Bottom