Rivers United Wameshinda mechi 12 kati ya 14 walizocheza nyumbani katika michuano ya CAF

Rivers United Wameshinda mechi 12 kati ya 14 walizocheza nyumbani katika michuano ya CAF

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1680778623382.png

Baada ya anguko la klabu za Enyimba, Enugu Rangers na Heartland klabu bora za Nigeria, Ndipo zilipoibuka klabu za Kano Pillars, Plateau United na Rivers United. Ni timu za kiazi kipya kwenye mafanikio.

Ushiriki wao kwenye CAF umeanza hivi karibuni mwaka 2017, Hizi rekodi zao wakiwa nyumbani ambako ndio huwa hatari zaidi.

Michezo kumi na nne ya CAF [14] waliocheza nyumbani wamepoteza Mmoja [1] dhidi ya Far Rabat 1-0, Wameshinda mara kumi na mbili [12] na Sare 1 dhidi ya Disables Noirs.

Miongoni mwa timu ngumu walizowahi kuzifunga nyumbani ni Enyimba, Club Africain, Asec Mimosas, El Merrick, Wydad Casablanca na Bloemfontein.

Credit: Gharib Mzinga
 
Hao jamaa kuwafunga kwao umefanya kazi ya ziada

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Wana record nzuri sana wakiwa kwao, benchi la ufundi na wachezaji wapunguze kufanya makosa hasa mipira ya kutengwa ili kutoruhusu goli, pia kule mbele wanatakiwa kutumia nafasi chache zitakazopatikana ili kupata goli la ugenini. Hii nahisi inaweza kuwa timu ngumu kuliko zitakazokutana na Yanga nusu fainali. Na ugumu unakuja kutokana na record yao wakiwa kwao inatisha sana.
 
wasifieni ili tukiwapiga mkose kichaka ya kujifichia...

kwenye nbc mnasema bahasha,
kwenye shirikisho mnasema kombe la luza mara ooh mazembe ya sasa siyo kama ya zamani...

tukiwapiga na hao sijui mtasema nini....
Baadaye hawachelewi kusema tumekutana na vibonde! Mashabiki wa simba wana nongwa sana.
 
Ali kamwe siku hizi amekuwa wa hovyo sana yaani ukiwa kwenye hizi team za simba na yanga akili zinaruka kabisa ni kama kuwa mbunge wa chama tawala.
 
Back
Top Bottom