Rivers utd wadai kupuliziwa sumu na kuibiwa pesa

Kwahiyo umeconfirm alieiba ni shabiki wa Yanga? Maana kwenye umati wa watu kuna mengi ndani yake.
Sasa kama mashabiki wa yanga ndo walienda kuwapokea sasa walaumiwe akina nani?
Mashabiki wa yanga wengi ni vibaka walisha wahi muibia pochi hadi bosi wao injinia Hersi.
 
Wanaweka milioni kwenye basi ufunguo walibaki nao?

Vv
 
Kwahio wewe akili yako imeamini yanga imefanya hii

Ukirejea uongo wa hawa jamaa 2021
Huo ni msala wenu hadi Supersport wanauongelea tena gemu hata haijaanza.

Nyie si ndiyo tulipokuwa tunawaambia gemu iliyopita hao Wanigeria hawana lolote mlikuwa mnawasifia kuwa ni timu kubwa iliyowafunga Wydad. Leo ndiyo mnawaona wahuni?
 
Hao wanaigeria urojo mtupu, wanataka pointi za mezani tu za uwanjani zimeshawashinda..
Kelele za nini..mpira si dk 90 kusubiri matokeo ya uwanjani ni kuonyesha ukomavu..au mmesahau ya Taifa stars na Uganda cranes, kutangulia si kufika..dk 90 ndio msemakweli, badilikeni watz, kila mtu mdomo unawasha kukashifu wengine mwisho wa mchezo mmefungwa..Tanzania inakuwa km nchi ya majuha tu, maneno meeengi, kumbe upuuzi mtupu.
 
Sasa wewe ndio unawafundisha..si umeona walitoa taarifa kwa head wa security wa CAF alyekuja kwa ajili ya mchezo pengine akaingia hata kwenye gari ili kuthibisha madai..hakuna haja ya kukashifu na kubeza watu, CAF watatoa majibu ya madai.
 
Sasa wewe ndio unawafundisha..si umeona walitoa taarifa kwa head wa security wa CAF alyekuja kwa ajili ya mchezo pengine akaingia hata kwenye gari ili kuthibisha madai..hakuna haja ya kukashifu na kubeza watu, CAF watatoa majibu ya madai.
Sasa wewe mtu mwenyewe unaandika pengine yani huna hata uhakika na unachokisema! Hiyo taarifa wewe umeiona? Umeona kua ina scientific evidence kuprove kua kulikua na sumu? Hata kama huyo security wa CAF aliingia ndani ya basi,je alithibitishaje kua kuna sumu? Hivi vitu vinahitaji vivid evidence na sio maneno tu,

Halafu wapi nimebeza na kukashifu?

Soma tena comment yangu na uzingatie alama za question mark,sio kila anayechangia hapa basi anachangia kwa ushabiki wa kiteam.
 
Me sio shabiki wa yanga ila siwaamini wapopo hata siku moja,hao jamaa ni matapeli dunia nzima inajua
 
Sawa, taarifa iliyowekwa hapa ni Rivers kuwajulisha CAF madai ya kuwekewa sumu, anayetakiwa kutoa scientific evidence ni Rivers, Yanga au CAF? Kama sumu ni spray inayosambaa na kwisha baada ya muda mfupi kwa hali hiyo Rivers wakisema wamepuliziwa sumu kwenye gari, ni scientific evidence ipi ndio utaiamini na nani aitoe..
Kingine, taarifa tunazopata kupitia media zozote huwa ni fupi sana si rahisi kueleza mambo yote hadi ushahidi kama wanaolalamika wanao..sisi audience hatuna base yoyote kukosoa au kuongeza lolote zaidi ya kusubiri jibu kwa mamlaka zilizopelekewa kushughulikia jambo lililolalamikiwa.
 
Sasa kama mashabiki wa yanga ndo walienda kuwapokea sasa walaumiwe akina nani?
Mashabiki wa yanga wengi ni vibaka walisha wahi muibia pochi hadi bosi wao injinia Hersi.
Umechanganya madesa, ni MO ndiye aliyeibiwa simu na mashabiki wa Simba akiwa uwanjani siku ya Simba day..

 
uwezo wako wa kufikiria ni mdogo, Yanga wanahusika nini na ulinzi wa mali zao? wana kampuni ya ulinzi? miaka hii unatembea na hela kwenye gari kwanini wasiache Hotel walipofikia?
Ni lini kutembea na pesa ilianza kuwa kosa kisheria?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…