THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 419
- 652
- Thread starter
-
- #181
Black Star 2: Astra 33
"Binadamu unadhani una sifa za kuwa bwana wangu" sauti hiyo aliisikia Garaaji peke yake.
"Nani alikwambia mimi nataka niwe bwana wako, tokea siku tulioingia makubaliano mimi na wewe yalikuwa ni makubaliano yenye usawa" alijibu
"Hahaha, unanifurahisha sana. Ila uwezo wako bado uko chini sana. Ili kuingia mkataba na mimi unatakiwa angalau kuwa daraja la Kyodan" alijibu Veremin.
Fahad akasogea mpaka alipo Garaaji na kukaa nyuma yake, "umekidhi vigezo vya kupanda daraja" aliongea na kumgonga sehemu kadhaa mgongoni. Radi yenye rangi ya dhambarau ikashuka kwa kasi na kumpiga Garaaji.
"Mkataba umekamilika" aliongea Veremin na hapo Garaaji akashumtuka, lile yai likapasuka na kutoa moshi mwingi sana wa zambarau. Moshi huwo ukajikusanya sehemu moja na ulipotoweka, mbele ya Garaaji kulikuwa kiumbe mkubwa mwenye rangi ya dhambaray iliyowamba na yenye kumeremeta. Kichwani alikuwa na pembe mbili kubwa kiasi na pembeni ya pande zote mbili za mdomo alikuwa na sharubu ndefu.
Veremin hakuwa nyoka tena bali sasa alikuwa ni dragon, akatembea kwa kasi na kuanza kupaa. Alipofika angani akanguruma kwa nguvu, kila aliesikia mngurumo huwo aliziba masikio.
Gorigo akatoka kwenye mwili wa Fahad na kupaa kwa kasi, "wewe mwehu jua nafasi yako" nae akanguruma. "Wewe unanambia hivyo kama nani" aliongea Veremin akionekana kukerwa na maneno hayo.
"Inaonekana umesahau nafasi yako, na umenisahau mimi si ndio" aliongea Gorigo na kupaa juu zaidi, akatanuwa mbawa zake mpaka mwisho na kuachia ukwenzi mkali sana. Alikuwa akimuonesha Veremin nani ni mwamba kati yao wawili.
"Achana nao, kila mmoja anataka kumtambia mwenzake" aliongea Fahad na kutabasamu. Akaendelea "hongera kwa kufika daraja la Kyodan, atakuja mtu kukuchukuwa akakuoneshe utakapokuwa unaishi. Tumia usiku wa leo kuzoea nguvu mpya ulioipata na kesho tutakwenda kumchukuwa mwanao" aliongea Fahad na kuruka kwa kasi sana. Akatuwa mgongoni kwa Gorigo na kumuamuru waondoke.
Veremin alipomuona Fahad tu, akashusha kichwa. Alielewa kabisa mtu huyo hakuwa kwenye ligi yake. Gorigo akaondoka kwa kasi na kupotelea angani. Veremin akashuka na kuingia katikwa mwili wa Garaaji kwa ajili ya kupumzika.
*********
"Unamuonaje Veremin" aliuliza Fahad wakati Gorigo akiwa angani juu ya mawingu kabisa akielea.
"Pale alipofika sasa ndio kwanza uzao wake wa pili, akifika uzao wa tatu atakuwa na nguvu za huyu mfalme hapa" alijibu Gorigo akimaanisha yeye.
"Hahaha! Ila ukiendelea kuzembea utakutana na mbabe atakae kuweka chini".
"Sidhani" alijibu Gorigo.
"Kwanini unasema hivyo"
"Kabla sijajibu hilo swali, nikuulize jambo kwanza"
"Uliza tu"
"Kwanini unaficha uwezo wako halisi?"
"Oh! Inaonekana umechungulia katika siri zangu".
"Hahaha! Hapana kwasababu ya mkataba tu, kuna mambo huwa nayajua tu kama wewe unavyojua baadhi ya siri zangu".
"Najiandaa na vita hilo ni moja lakini pia mwili kwa ulivyo sasa hauwezi kuhimili uwezo wangu wote. Utavunjika na kifo kitakuwa hakiepukiki"
"Vita, nilijua mapema tu. Jinsi unavyopigana na jinsi unavyochagua watu wako wa karibu. Kwa wengine watadhani unachagua tu kutokana na upendeleo lakini mimi nimeona unachotafuta".
"Hahaha! Ni kipi hicho nitafutacho"
"Hilo nitakuambia siku nyingine lakini jua ukiachilia mimi kuwa mnyama wa kiroho, nina rithi taaluma kutoka kwa mama yangu. Jambo moja ambalo kila nikikuangalia linanijia kichwani ni miezi kumi na mbili. Kwasasa sijapata ufunuo kamili lakini naamini ndani ya muda nitajua" alifafanua Gorigo.
"Una jicho zuri, haya niambie kwanini hakuna myama mwengine atakaekutisha"
"Kwasababu yako, katika mwili wako mpaka sasa kuna nguvu aina nne za asili. Ila mimi pia sijaonesha uwezo wangu wote. Ninaogopa ikiwa nitakuzidi sana, nitakuzuia kufika unapotaka kwa muda. Najua unafahamu uwezo wangu halisi mpaka sasa. Ukifika daraja la uzima wa milele mimi ndio nitaanza kutumia uwezo wangu halisi kwasababu kuanzia hapo tutakuwa katika njia iliyojaa damu na vifo"
"Nipe miaka mitatu nitakuwa katika daraja hilo, mpaka wakati huwo endelea kunilinda" aliongea Fahad na kusimama kisha akajirusha kutoka katika mgongo wa Gorigo na kuanza kushuka chini kwa kasi.
Gorigo akaachia ukwenzi mkali na kufunga mbawa zake, akaanza kushuka kwa kasi. Kwa watu wa mbali walioona tukio jilo walibakiwa na kumbukumbu katika mioyo yao jinsi imani ya kweli ilivyokuwepo kati ya binadamu na mnyama wa kiroho.
Walipokaribia chini, Gorigo akazunguka kwa kasi nankupita chini ya Fahad. Akatua mgongoni na ndege huyo akafungua mbawa zake kubwa. Kasi ikapungua kabla ya kutua kisha akapotea na kurudi mwilini kwa Fahad.
Fahad akaelekea chumbani kwake kwa ajiki ya kupumzika, "nimekusubiri sana mume wangu" sauti laini ya kike ilisikika ikiongea kwa deko.
"Kuna mambo nilikuwa nayaweka sawa" alijibu Fahad akivua nguo na kuzitundika sehemu. Mikono laini ikatarizi kutokea mgongoni kwake na kukutana katika kifua chake. "Mume wangu, nataka mtoto" alinong'oneza na kumpuliza Fahad sikioni.
"Acha nikaoge kwanza, mambo ya watoto tutaongea nikirudi" alijibu Fahad akijitahidi kupotezea mapapai laini yaliokuwa yakijikandamiza mgongoni kwake.
"Nitakuwa nakusubiri" aliongea Nephira na kumuachia Fahad, akarudi kitandani na kujilaza. Ndani ya chumba hicho kulikuwa kunanukia uturi si wa kawaida. Fahad akaelekea nje kwenye bwawa dogo lenye chemchem ya maji ya vugu vugu na kujitumbukiza. Akaegemea jiwe kubwa, na kuacha maji hayo yenye hali ya umoto kuifanya misuli yake ilainike.
**********
Katika pango lenye kiza sana, kelele za mwanamke aliekuwa akilia kwa maumivu zilisikika. Mara kadhaa vilisikika vibao na sauti ya kiume ikifoka.
"Kazi yangu imekamilika, fanyeni mnachotaka na kesho mumlete ngomeni" alitoka mtu mwenye gagulo jeusi lililofunika mpaka kichwani. Akapiga mkofi, mnyama mkubwa mweusi akatuwa kwenye kiza. Akapanda na kuondoka.
"Tumepewa ruhusa tufanye tunachotaka" aliongea mlinzi mmoja akionekana mwenye furaha sana akielekea ndani.
"Ah! Malaya huyu kang'ata ulimi" aliongea kwa nguvu, wenzake wakafika na wote wakaangaliana.
"Oya acha upuuzi, kula hivyo hivyo" aliongea mmoja.
"Ah! Mi siwezi fanya hivyo naogopa hasira za mungu wa kifo" aliongea akiondoka. Kutokana na hilo wote hawakuwa na namna zaidi ya kumfunika mwanamke huyo.
Siku ya pili jioni.
Msafara mkubwa wenye walinzi wengi ulikuwa njiani kuelekea njia ya Lorei. Katika msafara huwo sala na gari iliyokuwa ikivutwa na farasi wawili waliofunikwa kwa vitambaa vya dhahabu.
Wakiwa njiani taratibu mvua ndogo ikaanza kunyesha, "malkia nashauri tusimame kwanza kwa muda mrefu tutaingia katika njia ya milima ambayo itakuwa hatari kama tutaingia na mvua" aliongea mtu mmoja.
"Sawa" sauti laini ikasikika kutoka ndani ya gari hiyo, yule mtu akaiwasilisha amri hiyo kwa wingine na msafara ukasimama. Watu wakatawanyika na kutengeza makazi ya muda mfupi mpaka mvua hiyo itakapopita ili waendelee na safari bila kuwa na shaka ya kupata ajali njiani.
"Binadamu unadhani una sifa za kuwa bwana wangu" sauti hiyo aliisikia Garaaji peke yake.
"Nani alikwambia mimi nataka niwe bwana wako, tokea siku tulioingia makubaliano mimi na wewe yalikuwa ni makubaliano yenye usawa" alijibu
"Hahaha, unanifurahisha sana. Ila uwezo wako bado uko chini sana. Ili kuingia mkataba na mimi unatakiwa angalau kuwa daraja la Kyodan" alijibu Veremin.
Fahad akasogea mpaka alipo Garaaji na kukaa nyuma yake, "umekidhi vigezo vya kupanda daraja" aliongea na kumgonga sehemu kadhaa mgongoni. Radi yenye rangi ya dhambarau ikashuka kwa kasi na kumpiga Garaaji.
"Mkataba umekamilika" aliongea Veremin na hapo Garaaji akashumtuka, lile yai likapasuka na kutoa moshi mwingi sana wa zambarau. Moshi huwo ukajikusanya sehemu moja na ulipotoweka, mbele ya Garaaji kulikuwa kiumbe mkubwa mwenye rangi ya dhambaray iliyowamba na yenye kumeremeta. Kichwani alikuwa na pembe mbili kubwa kiasi na pembeni ya pande zote mbili za mdomo alikuwa na sharubu ndefu.
Veremin hakuwa nyoka tena bali sasa alikuwa ni dragon, akatembea kwa kasi na kuanza kupaa. Alipofika angani akanguruma kwa nguvu, kila aliesikia mngurumo huwo aliziba masikio.
Gorigo akatoka kwenye mwili wa Fahad na kupaa kwa kasi, "wewe mwehu jua nafasi yako" nae akanguruma. "Wewe unanambia hivyo kama nani" aliongea Veremin akionekana kukerwa na maneno hayo.
"Inaonekana umesahau nafasi yako, na umenisahau mimi si ndio" aliongea Gorigo na kupaa juu zaidi, akatanuwa mbawa zake mpaka mwisho na kuachia ukwenzi mkali sana. Alikuwa akimuonesha Veremin nani ni mwamba kati yao wawili.
"Achana nao, kila mmoja anataka kumtambia mwenzake" aliongea Fahad na kutabasamu. Akaendelea "hongera kwa kufika daraja la Kyodan, atakuja mtu kukuchukuwa akakuoneshe utakapokuwa unaishi. Tumia usiku wa leo kuzoea nguvu mpya ulioipata na kesho tutakwenda kumchukuwa mwanao" aliongea Fahad na kuruka kwa kasi sana. Akatuwa mgongoni kwa Gorigo na kumuamuru waondoke.
Veremin alipomuona Fahad tu, akashusha kichwa. Alielewa kabisa mtu huyo hakuwa kwenye ligi yake. Gorigo akaondoka kwa kasi na kupotelea angani. Veremin akashuka na kuingia katikwa mwili wa Garaaji kwa ajili ya kupumzika.
*********
"Unamuonaje Veremin" aliuliza Fahad wakati Gorigo akiwa angani juu ya mawingu kabisa akielea.
"Pale alipofika sasa ndio kwanza uzao wake wa pili, akifika uzao wa tatu atakuwa na nguvu za huyu mfalme hapa" alijibu Gorigo akimaanisha yeye.
"Hahaha! Ila ukiendelea kuzembea utakutana na mbabe atakae kuweka chini".
"Sidhani" alijibu Gorigo.
"Kwanini unasema hivyo"
"Kabla sijajibu hilo swali, nikuulize jambo kwanza"
"Uliza tu"
"Kwanini unaficha uwezo wako halisi?"
"Oh! Inaonekana umechungulia katika siri zangu".
"Hahaha! Hapana kwasababu ya mkataba tu, kuna mambo huwa nayajua tu kama wewe unavyojua baadhi ya siri zangu".
"Najiandaa na vita hilo ni moja lakini pia mwili kwa ulivyo sasa hauwezi kuhimili uwezo wangu wote. Utavunjika na kifo kitakuwa hakiepukiki"
"Vita, nilijua mapema tu. Jinsi unavyopigana na jinsi unavyochagua watu wako wa karibu. Kwa wengine watadhani unachagua tu kutokana na upendeleo lakini mimi nimeona unachotafuta".
"Hahaha! Ni kipi hicho nitafutacho"
"Hilo nitakuambia siku nyingine lakini jua ukiachilia mimi kuwa mnyama wa kiroho, nina rithi taaluma kutoka kwa mama yangu. Jambo moja ambalo kila nikikuangalia linanijia kichwani ni miezi kumi na mbili. Kwasasa sijapata ufunuo kamili lakini naamini ndani ya muda nitajua" alifafanua Gorigo.
"Una jicho zuri, haya niambie kwanini hakuna myama mwengine atakaekutisha"
"Kwasababu yako, katika mwili wako mpaka sasa kuna nguvu aina nne za asili. Ila mimi pia sijaonesha uwezo wangu wote. Ninaogopa ikiwa nitakuzidi sana, nitakuzuia kufika unapotaka kwa muda. Najua unafahamu uwezo wangu halisi mpaka sasa. Ukifika daraja la uzima wa milele mimi ndio nitaanza kutumia uwezo wangu halisi kwasababu kuanzia hapo tutakuwa katika njia iliyojaa damu na vifo"
"Nipe miaka mitatu nitakuwa katika daraja hilo, mpaka wakati huwo endelea kunilinda" aliongea Fahad na kusimama kisha akajirusha kutoka katika mgongo wa Gorigo na kuanza kushuka chini kwa kasi.
Gorigo akaachia ukwenzi mkali na kufunga mbawa zake, akaanza kushuka kwa kasi. Kwa watu wa mbali walioona tukio jilo walibakiwa na kumbukumbu katika mioyo yao jinsi imani ya kweli ilivyokuwepo kati ya binadamu na mnyama wa kiroho.
Walipokaribia chini, Gorigo akazunguka kwa kasi nankupita chini ya Fahad. Akatua mgongoni na ndege huyo akafungua mbawa zake kubwa. Kasi ikapungua kabla ya kutua kisha akapotea na kurudi mwilini kwa Fahad.
Fahad akaelekea chumbani kwake kwa ajiki ya kupumzika, "nimekusubiri sana mume wangu" sauti laini ya kike ilisikika ikiongea kwa deko.
"Kuna mambo nilikuwa nayaweka sawa" alijibu Fahad akivua nguo na kuzitundika sehemu. Mikono laini ikatarizi kutokea mgongoni kwake na kukutana katika kifua chake. "Mume wangu, nataka mtoto" alinong'oneza na kumpuliza Fahad sikioni.
"Acha nikaoge kwanza, mambo ya watoto tutaongea nikirudi" alijibu Fahad akijitahidi kupotezea mapapai laini yaliokuwa yakijikandamiza mgongoni kwake.
"Nitakuwa nakusubiri" aliongea Nephira na kumuachia Fahad, akarudi kitandani na kujilaza. Ndani ya chumba hicho kulikuwa kunanukia uturi si wa kawaida. Fahad akaelekea nje kwenye bwawa dogo lenye chemchem ya maji ya vugu vugu na kujitumbukiza. Akaegemea jiwe kubwa, na kuacha maji hayo yenye hali ya umoto kuifanya misuli yake ilainike.
**********
Katika pango lenye kiza sana, kelele za mwanamke aliekuwa akilia kwa maumivu zilisikika. Mara kadhaa vilisikika vibao na sauti ya kiume ikifoka.
"Kazi yangu imekamilika, fanyeni mnachotaka na kesho mumlete ngomeni" alitoka mtu mwenye gagulo jeusi lililofunika mpaka kichwani. Akapiga mkofi, mnyama mkubwa mweusi akatuwa kwenye kiza. Akapanda na kuondoka.
"Tumepewa ruhusa tufanye tunachotaka" aliongea mlinzi mmoja akionekana mwenye furaha sana akielekea ndani.
"Ah! Malaya huyu kang'ata ulimi" aliongea kwa nguvu, wenzake wakafika na wote wakaangaliana.
"Oya acha upuuzi, kula hivyo hivyo" aliongea mmoja.
"Ah! Mi siwezi fanya hivyo naogopa hasira za mungu wa kifo" aliongea akiondoka. Kutokana na hilo wote hawakuwa na namna zaidi ya kumfunika mwanamke huyo.
Siku ya pili jioni.
Msafara mkubwa wenye walinzi wengi ulikuwa njiani kuelekea njia ya Lorei. Katika msafara huwo sala na gari iliyokuwa ikivutwa na farasi wawili waliofunikwa kwa vitambaa vya dhahabu.
Wakiwa njiani taratibu mvua ndogo ikaanza kunyesha, "malkia nashauri tusimame kwanza kwa muda mrefu tutaingia katika njia ya milima ambayo itakuwa hatari kama tutaingia na mvua" aliongea mtu mmoja.
"Sawa" sauti laini ikasikika kutoka ndani ya gari hiyo, yule mtu akaiwasilisha amri hiyo kwa wingine na msafara ukasimama. Watu wakatawanyika na kutengeza makazi ya muda mfupi mpaka mvua hiyo itakapopita ili waendelee na safari bila kuwa na shaka ya kupata ajali njiani.