THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 419
- 652
- Thread starter
- #21
*************************
Victor Smith akiwa ofisini kwake, uliingia ujume katika simu yake. Alipoufunguwa, ulikuwa ni ujumbe ulioambatana sanduku la posta pamoja na sehemu na nyumba unayokwenda. Damu itamwagika, wakati mwingine havitakuwa viungo vya mtu mwengine bali ni vya kwenu ulisomeka hivyo.
Victor akachukuwa karatasi na kuuandika ujumbe huwo kisha akachukuwa kile kifuko kilichokuwa na vidole pamoja na meno. Akaambatanisha na ujumbe huwo kisha akatia kwenye bahasha. Akanyanyua simu nyingine na kubonyeza tarakimu moja, akaongea na kuirudisha mezani. Baada ya dakika moja akafika mtu, akamkamkabidhi ujumbe na kumwambia pale unapotakiwa kupelekwa.
Mtu huyo baada ya kupokea maelezo hayo akaaga na kuondoka, safari ya kuelekea kule
unapotakiwa kufika ujumbe huwo ikaanza. Kutokana na foleni za jiji la Dar-es-salaam, akachukuwa muda mrefu kuliko ule alokusudia.
Baada ya saa nusu akawasili nje ya mlango wa nyumba alioelekezwa. Akagonga mlango, baada ya sekunde kama ishirinin mlango ukafunguliwa. Alikuwa ni Bahati, nimeambiwa niletee hii bahasha hapa aliongea na kumkabidhi. Hakumpa nafasi ya kuuliza chochote akaaga na kuondoka.
Bahati alipoinuwa kichwa mtu huyo akawa kashapotea tayari katika upeo wake wa macho yake. Akapotezea na kufunga mlango, moja kwa moja mpaka chumbani kwake. Akaifunguwa bahasha hiyo, akajikuta jasho likimtoka bila kutarajia japo feni ilikuwa ianzunguka.
Kwa pupa akatoa simu yake na kutafuta jina kisha akapiga. Ommy, msala ndugu. Misheni imefeli aliongea punde tu baada ya simu hiyo kupokea. Tulia kwanza, nakuja hapo tuongee vizuri Ommy akaongea na kukata simu.
Jasho liliendelea kumtoka bahati, hakutegema hata mara moja kama ndugu yao huyo angeweza kufanya hivyo. Akiwa katika hali hiyo akakumbuka ugomvi mkubwa kati ya Abedi na baba yao.
Abedi ukiendelea kufanya hivyo, mimi nitakukana kama mwanangu. Mimi siwezi kuishi na mtu katili kama wewe.
Lakini kazi yangu ndio inayoleta chakula mezani, kama si mimi tungekuwa tumeshanyauka hapa ndani.
Unathubutu kunijibu mimi baba yako, umekosa nidhamu kiasi hicho. Nasema hivi humu kwangu ondoka
Maneno hayo yalijirudia sana kichwani mwa Bahati maana hakuwa akifahamu kazi aliokuwa akiifanya ndugu yao huyo mpaka kukwazana na baba yao kiasi kile. Akiwa katika dimbwi la mawazo,
Simu yake ikaita. Loh! Akaruka na kujificha nyuma ya kochi, ah kumbe simu akajisemea na
kuipokea. Akatoka chumbani na kwenda kufunguwa malngo, afadhali umekuja Ommy alijisemea
akiongoza njia kuelekea chumbani kwake. Hivi ni vidole na mezo ya yule jamaa tulomtupa
awafuatilie watoto wa Abedi aliongea akimkabidhi kile kijifuko chenye vile viungo.
Ommy akaviangalia kisha akashusha pumzi, hii ni kazi yake bila shaka aliongea akikaa kwenye
kochi. Una maanisha nini, hilo tutaongea siku nyingine ila kwa sasa tunahitaji kukaa kimya. Mara ya pili atakuja kwa ajili ya maisha yetu.
Yule ni mbweha katika ngozi ya kondoo, ni mtu mwema usoni tu, ana roho ya alama ya kuuliza aliongea Ommy. Sasa tunafanya nini, mimi hata hapa sitaki kukaa tena pamoja na kujifanya mbabe ila Bahati alikuwa muoga sana. Alikiogopa sana kifo, ama mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.
Kwa kipindi hiki, tusifanye kitu.
Hatofanya kitu chochote mpaka tumchokonie tena. Inabidi tujipange upya, mali yake lazima iwe yetu kwa njia yeyote ile aliongea Ommy na kukunja ngumi. Wakaendelea kuongea na baada kama saa mbili hivi Ommy akaondoka. Alipotoka tu, Bahati akafunga akafunga mlango kwa funguo, kisha akatia komeo na kukimbilia chumbani na kujifungia.
Akafunguwa kabati na kutoapakiti ndogo yenye unga mweupe, akatoa kichupa kidogo chenye maji ndani. Akachanganya na ule unga kisha akachukuwa bomba dogo la sindano, akavuta ule ule
mchanganyiko kisha akajichomea. Akashusha pumzi na kuegemea kitanda, taratibu mkojo ukaanza
kumtoka. Hapo akajisikia vizuri na kuanza kutabasamu, ute mwembamba ukamchuruzika teja.
Victor Smith akiwa ofisini kwake, uliingia ujume katika simu yake. Alipoufunguwa, ulikuwa ni ujumbe ulioambatana sanduku la posta pamoja na sehemu na nyumba unayokwenda. Damu itamwagika, wakati mwingine havitakuwa viungo vya mtu mwengine bali ni vya kwenu ulisomeka hivyo.
Victor akachukuwa karatasi na kuuandika ujumbe huwo kisha akachukuwa kile kifuko kilichokuwa na vidole pamoja na meno. Akaambatanisha na ujumbe huwo kisha akatia kwenye bahasha. Akanyanyua simu nyingine na kubonyeza tarakimu moja, akaongea na kuirudisha mezani. Baada ya dakika moja akafika mtu, akamkamkabidhi ujumbe na kumwambia pale unapotakiwa kupelekwa.
Mtu huyo baada ya kupokea maelezo hayo akaaga na kuondoka, safari ya kuelekea kule
unapotakiwa kufika ujumbe huwo ikaanza. Kutokana na foleni za jiji la Dar-es-salaam, akachukuwa muda mrefu kuliko ule alokusudia.
Baada ya saa nusu akawasili nje ya mlango wa nyumba alioelekezwa. Akagonga mlango, baada ya sekunde kama ishirinin mlango ukafunguliwa. Alikuwa ni Bahati, nimeambiwa niletee hii bahasha hapa aliongea na kumkabidhi. Hakumpa nafasi ya kuuliza chochote akaaga na kuondoka.
Bahati alipoinuwa kichwa mtu huyo akawa kashapotea tayari katika upeo wake wa macho yake. Akapotezea na kufunga mlango, moja kwa moja mpaka chumbani kwake. Akaifunguwa bahasha hiyo, akajikuta jasho likimtoka bila kutarajia japo feni ilikuwa ianzunguka.
Kwa pupa akatoa simu yake na kutafuta jina kisha akapiga. Ommy, msala ndugu. Misheni imefeli aliongea punde tu baada ya simu hiyo kupokea. Tulia kwanza, nakuja hapo tuongee vizuri Ommy akaongea na kukata simu.
Jasho liliendelea kumtoka bahati, hakutegema hata mara moja kama ndugu yao huyo angeweza kufanya hivyo. Akiwa katika hali hiyo akakumbuka ugomvi mkubwa kati ya Abedi na baba yao.
Abedi ukiendelea kufanya hivyo, mimi nitakukana kama mwanangu. Mimi siwezi kuishi na mtu katili kama wewe.
Lakini kazi yangu ndio inayoleta chakula mezani, kama si mimi tungekuwa tumeshanyauka hapa ndani.
Unathubutu kunijibu mimi baba yako, umekosa nidhamu kiasi hicho. Nasema hivi humu kwangu ondoka
Maneno hayo yalijirudia sana kichwani mwa Bahati maana hakuwa akifahamu kazi aliokuwa akiifanya ndugu yao huyo mpaka kukwazana na baba yao kiasi kile. Akiwa katika dimbwi la mawazo,
Simu yake ikaita. Loh! Akaruka na kujificha nyuma ya kochi, ah kumbe simu akajisemea na
kuipokea. Akatoka chumbani na kwenda kufunguwa malngo, afadhali umekuja Ommy alijisemea
akiongoza njia kuelekea chumbani kwake. Hivi ni vidole na mezo ya yule jamaa tulomtupa
awafuatilie watoto wa Abedi aliongea akimkabidhi kile kijifuko chenye vile viungo.
Ommy akaviangalia kisha akashusha pumzi, hii ni kazi yake bila shaka aliongea akikaa kwenye
kochi. Una maanisha nini, hilo tutaongea siku nyingine ila kwa sasa tunahitaji kukaa kimya. Mara ya pili atakuja kwa ajili ya maisha yetu.
Yule ni mbweha katika ngozi ya kondoo, ni mtu mwema usoni tu, ana roho ya alama ya kuuliza aliongea Ommy. Sasa tunafanya nini, mimi hata hapa sitaki kukaa tena pamoja na kujifanya mbabe ila Bahati alikuwa muoga sana. Alikiogopa sana kifo, ama mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.
Kwa kipindi hiki, tusifanye kitu.
Hatofanya kitu chochote mpaka tumchokonie tena. Inabidi tujipange upya, mali yake lazima iwe yetu kwa njia yeyote ile aliongea Ommy na kukunja ngumi. Wakaendelea kuongea na baada kama saa mbili hivi Ommy akaondoka. Alipotoka tu, Bahati akafunga akafunga mlango kwa funguo, kisha akatia komeo na kukimbilia chumbani na kujifungia.
Akafunguwa kabati na kutoapakiti ndogo yenye unga mweupe, akatoa kichupa kidogo chenye maji ndani. Akachanganya na ule unga kisha akachukuwa bomba dogo la sindano, akavuta ule ule
mchanganyiko kisha akajichomea. Akashusha pumzi na kuegemea kitanda, taratibu mkojo ukaanza
kumtoka. Hapo akajisikia vizuri na kuanza kutabasamu, ute mwembamba ukamchuruzika teja.