RIWAYA: BONDIA
MTUNZI: HUSSEIN ISSA TUWA
Lango kuu la gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam lilifunguliwa na mtu mmoja mrefu alitoka nje ya lango lile kwa hatua za kujiamini na kusimama kiasi cha hatua zipatazo tano nje gereza lile. Nyuma yake, lile lango lilifungwa, na hivyo kufungia historia ya miaka miwili ya taabu, mateso, kazi ngumu na uchungu mwingi ambayo mtu huyu alipitia alipokuwa upande wa pili wa lango lile. Ilikuwa ni saa tatu na robo asubuhi siku ya jumatano.
Jamaa aliangaza kulia na kushoto pale nje huku akivuta pumzi ndefu zilizoingiza hewa nyingi mapafuni mwake, kisha akashusha pumzi zile zikiambatana na mguno wa faraja, iliyotokana na kuvuta hewa ile ya ulimwengu huru, akiwa mtu huru. Hili ni jambo alilokuwa akilisubiri kwa hamu katika muda wote ule aliokuwa akitumikia kile kifungo chake cha miaka miwili.
Pamoja na kimo chake kirefu, mtu huyu alikuwa na mwili ulioshiba pamoja na kuwa alikuwa kifungoni. Hii ni kutokana na mazoezi mazito aliyokuwa akijilazimisha kufanya akiwa kule gerezani kwa lengo maalum. Misuli yake ya mikono iliyojaa vizuri ilijidhihirisha wazi kwa kututumka na kufanya mikono ya fulana yake ya mikono mifupi ionekane kumbana. Vivyo hivyo, misuli yake ya mapaja ilionekana kututumka na kuifanya ile suruali yake ya jeans nayo ionekane kuwa inambana.
Bila kugeuka nyuma, jamaa alianza kutembea kwa hatua moja moja zilizokuwa zikivutwa bila ya haraka yoyote kuelekea barabara kuu iliyokuwa mbele yake, akiliacha lile jengo la gereza nyuma yake akiwa na azma ya kutorejea tena ndani ya kuta za jengo lile maishani mwake.Bora kufa, kuliko kurudi tena gerezani.
Alishaazimia hivyo muda mrefu, na bado alibaki na azma hiyo.
Kwake yeye mji aliuona ukiwa umebadilika sana ndani ya miaka ile miwili, lakini hilo halikuwa na maana yoyote kwake, kwani alijua kitambo kuwa pindi atakapotoka gerezani angekuta mabadiliko mengi sana jijini. Alikuwa akitembea huku akijaribu kutazama mambo yote yaliyokuwa mbele yake kwa jicho la kudadisi. Aliona kuwa magari ya usafirishaji wa abiria yalikuwa yamechorwa mistari ya rangi, tofauti na hali aliyoiacha wakati anaingia gerezani. Kidogo hili lilimpa taabu, kwani alianza kujiuliza ni jinsi gani ataweza kujua ni rangi ipi ndio ilikuwa ikiwakilisha basi la kuelekea sehemu ambayo alikuwa ameazimia kwenda baada ya kutoka gerezani.
Aliweka sawa mkoba wake mdogo alioupitisha begani kwake na kuuacha ukining'inia mgongoni na kuzidi kuikurubia ile barabara ambayo juu yake, magari yalikuwa yakipita kwa kasi sana kiasi cha kumkosesha amani.
Jamaa alikuwa na sura ya kuvutia ambayo baada ya miaka miwili gerezani, ilikuwa imeingia ukomavu fulani ambao haukuwepo hapo kabla, na ambao kwa namna yake uliongezea mvuto kwenye sura ile.
Lakini wakati akitembea taratibu kwa mwendo wake wa hatua moja moja kukiendea kituo cha mabasi yaelekeayo katikati ya jiji kilichokuwa upande wa pili wa barabara, uso wake ule wenye mvuto ulionekana wazi kuwa ulikuwa una dhamira thabiti juu ya nini alikuwa anataka kufanya baada ya kutoka gerezani, kwani baada ya miaka miwili ya kupanga na kupangua akiwa kule gerezani, hakika alikuwa anajua ni nini haswa alichotakiwa kukifanya.
Kwenye kituo cha mabasi yaliyokuwa yakielekea maeneo ya Kariakoo na katikati ya jiji kilichokuwa upande wa pili wa ile barabara kuu, mmoja wa watu waliokuwa wakisubiri mabasi pale kituoni alikuwa akifuatilia kila hatua ya yule mtu mrefu aliyetoka kule gerezani, ambaye sasa alikuwa akisubiri nafasi muafaka ya kuvuka barabara ili naye aende pale kituoni.
Alikuwa ni mwanamke aliyejitanda khanga mwili mzima hadi kichwani, kama jinsi wanawake wengi wa pwani wapendavyo kujitanda, na usoni alikuwa amevaa miwani myeusi iliyoficha kabisa sura yake. Ingawa alionekana kuwa ni msafiri miongoni mwa wale wasafiri wengi waliokuwa wakisubiri daladala pale kituoni, ukweli ni kwamba mwanadada yule aliyejitanda khanga, alikuwa akimsubiri yule mtu mrefu aliyetoka gerezani asubuhi ile!
Jamaa alivuka barabara na alikuwa akikiendea kile kituo cha mabasi, wakati mlango wa mbele wa gari dogo aina ya Hyundai nyeupe yenye namba za serikali ulipofunguka na msichana mmoja mwenye kimo cha kawaida alipoteremka na kusimama nje ya lile gari huku mkono mmoja bado ukiwa umeshikilia mlango wa gari lake.
Huyu naye alikuwa amevaa miwani ya jua, ingawa yeye alikuwa amevaa gauni refu la kitambaa laini chenye maua madogo madogo lililokuwa na mpasuo mpana upande mmoja. Kichwani alikuwa amebana nywele zake ndefu zilizotiwa dawa za kulainisha na kupendezesha nywele katika ile staili ya Pony Tail , ambapo kile kimkia cha nywele kilichokuwa kikining'inia kisogoni mwake kilikuwa kimechomoza kutokea kwenye sehemu ya nyuma ya kofia aina ya kapelo aliyokuwa ameivaa. Aliweka mkono wale wa pili juu ya paa la gari na kumtazama yule jamaa akipita upande wa pili wa lile gari akielekea kule kituoni.
"Roman!" Aliita.
Jamaa alisimama katikati ya hatua na kugeuka taratibu ule upande ilipotokea sauti iliyoita jina lake. Alimtazama yule dada mwenye kapelo na miwani ya jua huku akikunja uso kujaribu kumtambua. Yule dada aliendelea kumtazama bila ya kusema neno zaidi, akimpa muda yule mtu aliyemwita kwa jina la Roman amtambue.
Kule kituoni yule mwanamke aliyejitanda khanga naye alianza kupata waiswasi baada ya kuona yule jamaa aliyekuwa akimvizia akisimama na kumgeukia yule dada aliyetoka kwenye lile gari lenye namba za serikali.
Ni nini tena pale?
Jamaa alimtazama kwa makini zaidi yule dada na alihisi kuwa alishapata kuiona ile sura wakati fulani huko nyuma, ingawa bado hakuweza kuioanisha sura ile na kumbukumbu zake za miaka miwili iliyopita.
"Miaka miwili ni mingi kiasi cha kukufanya unisahau Roman?" Hatimaye yule dada alimuuliza yule jamaa huku akitoa miwani usoni kwake, na hapo jamaa akaachia mdomo kwa mshangao."Afande Fatma...?" Yule dada alirudisha tena miwani yake usoni. "Sasa nimekuwa Inspekta...Inspekta Fatma."
Jamaa alikunja uso, safari hii ikiwa ni kwa kukereka, na kubetua midomo kwa namna ambayo ilionesha kuwa hakufurahishwa na hali ile."Unataka nini Inspekta?" Roman aliuliza, huku akitilia mkazo wa kebehi lile neno "Inspekta."
"We need to talk Roman...you and me! (Tunahitaji kuzungumza Roman...mimi na wewe!)" Inspekta Fatma alimwambia yule jamaa bila ya kujali kebehi na kukereka kwake kwa wazi. Roman alitikisa kichwa kwa masikitiko.
"Yaani siku yangu ya kwanza nikiwa mtu huru! Halafu mtu wa kwanza kukutana na kuongea naye ni askari! What's this (Nini maana yake hii)?" Roman alisema kwa hasira."We need to talk Roman, and we need to talk now!(Tunahitaji kuzungumza Roman, na tunahitaji kuzunguza wakati huu!)"
"About what (Kuhusu nini)? Nimetumikia kifungo changu, nimemaliza. Sasa mimi ni raia huru..."
"Ingia kwenye gari Roman!" Inspekta Fatma alimkatisha. Na sauti yake ilikuwa imebeba mamlaka yote aliyokabidhiwa na jamhuri kama afisa wa jeshi la polisi mwenye jukumu juu ya usalama wa raia wote wa Tanzania.
Kule kituoni yule mwanamke aliyejitanda khanga alizidi kujichanganya katikati ya kundi la watu waliokuwepo pale kituoni huku akizidi kufuatilia kwa makini kila kilichokuwa kikiendelea kule kwenye lile gari dogo lenye namba za serikali. Na kwa kadiri ilivyokuwa, ni wazi kuwa kile kitendo cha yule mtu aliyeitwa Roman kusimama na kuongea na yule dada aliyetoka kwenye lile gari lenye namba za serikali kilimchanganya sana.
Ni nini kinaendelea pale? Roman alibetua mabega na kuuliza kwa kukereka kwa hali ya juu. "Ili iweje afande? Ni lazima niingie kwenye hilo g-" "Sio lazima. Lakini ni muhimu tuongee. Nataka kukupa lifti..."
Mtu aliyeitwa Roman alimtazama yule askari wa kike kwa muda, na yule askari aliendelea kumtazama bila ya kutetereka. Kisha, bila ya kusema neno zaidi, Roman alipiga hatua moja kubwa na kufungua mlango wa upande wa abiria wa lile gari na kuingia. Inspekta Fatma aliingia nyuma ya usukani na kuliondoa lile gari kutoka eneo lile kwa ustadi mkubwa.
Huku kituoni, mwanamke aliyejitanda khanga alichanganyikiwa vibaya sana. Alilitazama lile gari likiondoka kutoka eneo lile kwa fadhaa iliyochanganyika na hasira.
***
"Unaelekea wapi?" Inspekta Fatma aliuliza huku akiwa amekaza macho yake barabarani. Roman alikuwa amegeuzia uso wake nje ya dirisha akiangalia mandhari ya jiji alilolikosa kwa muda wa miaka miwili. Hakufanya juhudi yoyote kuficha jinsi alivyokereka na hali ya kuwa na yule askari ndani ya lile gari.
"Umesema unataka kuongea. Ongea nami nakusikiliza.
Unaweza kuzunguka jiji lote hili wakati tunaongea...sio lazima ujue niendako!" Alimjibu kwa hasira huku bado akitazama nje ya dirisha. "Nimesema tunahitaji kuongea...mimi na wewe. Hivyo natarajia na wewe uwe unaongea. Na ndio maana nimekuuliza swali ambalo naomba unijibu. Unaelekea wapi Roman?""Hiyo inakuhusu nini? Wewe si ndugu yangu, si jamaa yangu, na wala si mke wangu! Sasa sioni swala la mimi ninaelekea wapi linaingiaje kwako.
Mimi ni mtu huru bwana!" Roman alimjibu kwa jazba. Inspekta Fatma alimtupia jicho la pembeni halafu akabaki kimya kwa muda, akijishughulisha na kuendesha gari, ingawa uso wake ulionesha kuwa na mawazo mazito. Roman alifumbata mikono yake kifuani na kuendelea kutazama nje ya dirisha la lile gari.
Safari iliendelea katika hali ile kwa muda mrefu, na katika muda ule walikuwa wameanza kuingia katikati ya jiji.
Walipita uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam, na mwendo mfupi baadaye, Inspekta Fatma alipunguza mwendo wa gari na kuingia kulia ambapo aliliegesha kwa ufundi mkubwa nje ya mgahawa maarufu wa Best Bite katika lile tawi lake lililopo barabara ya Nyerere, zamani Pugu Road.
"Okay, Roman, nadhani hapa tunaweza kuongea kwa kituo zaidi."
Inspekta Fatma alimwambia yule mtu mrefu mwenye mwili ulioshiba huku akiteremka kutoka kwenye gari. Bila ya kuongea neno, lakini akionesha wazi kuwa alikuwa amechukia, Roman aliteremka na mkoba wake kutoka kwenye lile gari na kumfuata yule afisa wa polisi mrembo ndani ya ule mgahawa mzuri.
Baada ya kuagiza soda aina ya Coca Cola kwa ajili yake na bilauri ya juisi ya nanasi kwa ajili ya Roman kwa mujibu wa utashi wake, Inspekta Fatma alianzisha tena maongezi. "Roman, najua kuwa utakuwa unanichukia sana hivi sasa kwa kufanya haya niyafanyayo, lakini naomba uelewe kuwa hii ni kwa faida yako na si vinginevyo..."
Roman alimtazama yule binti bila ya kusema neno, na Fatma aliendelea."...najua kuwa baada ya kumaliza kifungo chako utakuwa tayari una mipango uliyojipangia katika maisha yako mapya. Basi na iwe ya kheri Roman, vinginevyo itakuwa mbaya sana kwako."
Roman alizidi kumtazama tu yule dada bila ya kusema neno. "Mimi nimeamua kuja kukusubiri pale Ukonga leo hii kwa sababu najali maisha yako, na kwa jinsi ninavyohisi, naona una hatari ya kurudi tena gerezani kama hutaamua kusahau yaliyopita na kutazama mbele."
Inspekta Fatma alizidi kumueleza kwa upole na msisitizo wa hali ya juu. Bado Roman alikuwa akimtazama kwa macho makavu bila ya kusema neno lolote wala kupitisha hisia yoyote usoni mwake ambayo ingeweza kusomwa na macho makini ya yule askari wa kike. Lakini Inspekta Fatma alikuwa anajua ni nini alichokuwa anataka Roman aelewe, hivyo hali ile haikumkatisha tamaa hata kidogo.
"Sahau yaliyopita Roman, na uanze maisha mapya sasa. Kama utahitaji msaada mimi niko tayari kukusaidia kwa kadiri nitakavyoweza, lakini achana kabisa na mawazo uliyonayo Roman, hayatakusaidia kitu..."
Hapo Roman hakuweza kuendelea kubaki kimya.
"Mnhu! Yaani we' unataka kuniambia kuwa unajua mi' n'na mawazo gani? Achana na mimi kabisa afande!"
***NINI kilimfanya ROMA atumikie kifungo cha miaka miwili gerezani???
**ANA mipango gani katika maisha yake baada ya kifungo ambayo Inspekta anayatilia mashaka??
**MWANAMKE mwenye baibui ni nani na anataka nini??
NA KWANINI INAITWA BONDIA ?
#SEHEMU YA 1
#SEHEMU YA 2
#SEHEMU YA 3
#SEHEMU YA 4
#SEHEMU YA 5
#SEHEMU YA 6
#SEHEMU YA 7
#SEHEMU YA 8
#SEHEMU YA 9
#SEHEMU YA 10
jonnie_vincy Khantwe mbalu byb sac mlyn VAN HEIST nrango mangimeza muuza ubuyu Jullie Z Igunga Moja culbby mugaru
MTUNZI: HUSSEIN ISSA TUWA
SEHEMU YA KWANZA
Lango kuu la gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam lilifunguliwa na mtu mmoja mrefu alitoka nje ya lango lile kwa hatua za kujiamini na kusimama kiasi cha hatua zipatazo tano nje gereza lile. Nyuma yake, lile lango lilifungwa, na hivyo kufungia historia ya miaka miwili ya taabu, mateso, kazi ngumu na uchungu mwingi ambayo mtu huyu alipitia alipokuwa upande wa pili wa lango lile. Ilikuwa ni saa tatu na robo asubuhi siku ya jumatano.
Jamaa aliangaza kulia na kushoto pale nje huku akivuta pumzi ndefu zilizoingiza hewa nyingi mapafuni mwake, kisha akashusha pumzi zile zikiambatana na mguno wa faraja, iliyotokana na kuvuta hewa ile ya ulimwengu huru, akiwa mtu huru. Hili ni jambo alilokuwa akilisubiri kwa hamu katika muda wote ule aliokuwa akitumikia kile kifungo chake cha miaka miwili.
Pamoja na kimo chake kirefu, mtu huyu alikuwa na mwili ulioshiba pamoja na kuwa alikuwa kifungoni. Hii ni kutokana na mazoezi mazito aliyokuwa akijilazimisha kufanya akiwa kule gerezani kwa lengo maalum. Misuli yake ya mikono iliyojaa vizuri ilijidhihirisha wazi kwa kututumka na kufanya mikono ya fulana yake ya mikono mifupi ionekane kumbana. Vivyo hivyo, misuli yake ya mapaja ilionekana kututumka na kuifanya ile suruali yake ya jeans nayo ionekane kuwa inambana.
Bila kugeuka nyuma, jamaa alianza kutembea kwa hatua moja moja zilizokuwa zikivutwa bila ya haraka yoyote kuelekea barabara kuu iliyokuwa mbele yake, akiliacha lile jengo la gereza nyuma yake akiwa na azma ya kutorejea tena ndani ya kuta za jengo lile maishani mwake.Bora kufa, kuliko kurudi tena gerezani.
Alishaazimia hivyo muda mrefu, na bado alibaki na azma hiyo.
Kwake yeye mji aliuona ukiwa umebadilika sana ndani ya miaka ile miwili, lakini hilo halikuwa na maana yoyote kwake, kwani alijua kitambo kuwa pindi atakapotoka gerezani angekuta mabadiliko mengi sana jijini. Alikuwa akitembea huku akijaribu kutazama mambo yote yaliyokuwa mbele yake kwa jicho la kudadisi. Aliona kuwa magari ya usafirishaji wa abiria yalikuwa yamechorwa mistari ya rangi, tofauti na hali aliyoiacha wakati anaingia gerezani. Kidogo hili lilimpa taabu, kwani alianza kujiuliza ni jinsi gani ataweza kujua ni rangi ipi ndio ilikuwa ikiwakilisha basi la kuelekea sehemu ambayo alikuwa ameazimia kwenda baada ya kutoka gerezani.
Aliweka sawa mkoba wake mdogo alioupitisha begani kwake na kuuacha ukining'inia mgongoni na kuzidi kuikurubia ile barabara ambayo juu yake, magari yalikuwa yakipita kwa kasi sana kiasi cha kumkosesha amani.
Jamaa alikuwa na sura ya kuvutia ambayo baada ya miaka miwili gerezani, ilikuwa imeingia ukomavu fulani ambao haukuwepo hapo kabla, na ambao kwa namna yake uliongezea mvuto kwenye sura ile.
Lakini wakati akitembea taratibu kwa mwendo wake wa hatua moja moja kukiendea kituo cha mabasi yaelekeayo katikati ya jiji kilichokuwa upande wa pili wa barabara, uso wake ule wenye mvuto ulionekana wazi kuwa ulikuwa una dhamira thabiti juu ya nini alikuwa anataka kufanya baada ya kutoka gerezani, kwani baada ya miaka miwili ya kupanga na kupangua akiwa kule gerezani, hakika alikuwa anajua ni nini haswa alichotakiwa kukifanya.
Kwenye kituo cha mabasi yaliyokuwa yakielekea maeneo ya Kariakoo na katikati ya jiji kilichokuwa upande wa pili wa ile barabara kuu, mmoja wa watu waliokuwa wakisubiri mabasi pale kituoni alikuwa akifuatilia kila hatua ya yule mtu mrefu aliyetoka kule gerezani, ambaye sasa alikuwa akisubiri nafasi muafaka ya kuvuka barabara ili naye aende pale kituoni.
Alikuwa ni mwanamke aliyejitanda khanga mwili mzima hadi kichwani, kama jinsi wanawake wengi wa pwani wapendavyo kujitanda, na usoni alikuwa amevaa miwani myeusi iliyoficha kabisa sura yake. Ingawa alionekana kuwa ni msafiri miongoni mwa wale wasafiri wengi waliokuwa wakisubiri daladala pale kituoni, ukweli ni kwamba mwanadada yule aliyejitanda khanga, alikuwa akimsubiri yule mtu mrefu aliyetoka gerezani asubuhi ile!
Jamaa alivuka barabara na alikuwa akikiendea kile kituo cha mabasi, wakati mlango wa mbele wa gari dogo aina ya Hyundai nyeupe yenye namba za serikali ulipofunguka na msichana mmoja mwenye kimo cha kawaida alipoteremka na kusimama nje ya lile gari huku mkono mmoja bado ukiwa umeshikilia mlango wa gari lake.
Huyu naye alikuwa amevaa miwani ya jua, ingawa yeye alikuwa amevaa gauni refu la kitambaa laini chenye maua madogo madogo lililokuwa na mpasuo mpana upande mmoja. Kichwani alikuwa amebana nywele zake ndefu zilizotiwa dawa za kulainisha na kupendezesha nywele katika ile staili ya Pony Tail , ambapo kile kimkia cha nywele kilichokuwa kikining'inia kisogoni mwake kilikuwa kimechomoza kutokea kwenye sehemu ya nyuma ya kofia aina ya kapelo aliyokuwa ameivaa. Aliweka mkono wale wa pili juu ya paa la gari na kumtazama yule jamaa akipita upande wa pili wa lile gari akielekea kule kituoni.
"Roman!" Aliita.
Jamaa alisimama katikati ya hatua na kugeuka taratibu ule upande ilipotokea sauti iliyoita jina lake. Alimtazama yule dada mwenye kapelo na miwani ya jua huku akikunja uso kujaribu kumtambua. Yule dada aliendelea kumtazama bila ya kusema neno zaidi, akimpa muda yule mtu aliyemwita kwa jina la Roman amtambue.
Kule kituoni yule mwanamke aliyejitanda khanga naye alianza kupata waiswasi baada ya kuona yule jamaa aliyekuwa akimvizia akisimama na kumgeukia yule dada aliyetoka kwenye lile gari lenye namba za serikali.
Ni nini tena pale?
Jamaa alimtazama kwa makini zaidi yule dada na alihisi kuwa alishapata kuiona ile sura wakati fulani huko nyuma, ingawa bado hakuweza kuioanisha sura ile na kumbukumbu zake za miaka miwili iliyopita.
"Miaka miwili ni mingi kiasi cha kukufanya unisahau Roman?" Hatimaye yule dada alimuuliza yule jamaa huku akitoa miwani usoni kwake, na hapo jamaa akaachia mdomo kwa mshangao."Afande Fatma...?" Yule dada alirudisha tena miwani yake usoni. "Sasa nimekuwa Inspekta...Inspekta Fatma."
Jamaa alikunja uso, safari hii ikiwa ni kwa kukereka, na kubetua midomo kwa namna ambayo ilionesha kuwa hakufurahishwa na hali ile."Unataka nini Inspekta?" Roman aliuliza, huku akitilia mkazo wa kebehi lile neno "Inspekta."
"We need to talk Roman...you and me! (Tunahitaji kuzungumza Roman...mimi na wewe!)" Inspekta Fatma alimwambia yule jamaa bila ya kujali kebehi na kukereka kwake kwa wazi. Roman alitikisa kichwa kwa masikitiko.
"Yaani siku yangu ya kwanza nikiwa mtu huru! Halafu mtu wa kwanza kukutana na kuongea naye ni askari! What's this (Nini maana yake hii)?" Roman alisema kwa hasira."We need to talk Roman, and we need to talk now!(Tunahitaji kuzungumza Roman, na tunahitaji kuzunguza wakati huu!)"
"About what (Kuhusu nini)? Nimetumikia kifungo changu, nimemaliza. Sasa mimi ni raia huru..."
"Ingia kwenye gari Roman!" Inspekta Fatma alimkatisha. Na sauti yake ilikuwa imebeba mamlaka yote aliyokabidhiwa na jamhuri kama afisa wa jeshi la polisi mwenye jukumu juu ya usalama wa raia wote wa Tanzania.
Kule kituoni yule mwanamke aliyejitanda khanga alizidi kujichanganya katikati ya kundi la watu waliokuwepo pale kituoni huku akizidi kufuatilia kwa makini kila kilichokuwa kikiendelea kule kwenye lile gari dogo lenye namba za serikali. Na kwa kadiri ilivyokuwa, ni wazi kuwa kile kitendo cha yule mtu aliyeitwa Roman kusimama na kuongea na yule dada aliyetoka kwenye lile gari lenye namba za serikali kilimchanganya sana.
Ni nini kinaendelea pale? Roman alibetua mabega na kuuliza kwa kukereka kwa hali ya juu. "Ili iweje afande? Ni lazima niingie kwenye hilo g-" "Sio lazima. Lakini ni muhimu tuongee. Nataka kukupa lifti..."
Mtu aliyeitwa Roman alimtazama yule askari wa kike kwa muda, na yule askari aliendelea kumtazama bila ya kutetereka. Kisha, bila ya kusema neno zaidi, Roman alipiga hatua moja kubwa na kufungua mlango wa upande wa abiria wa lile gari na kuingia. Inspekta Fatma aliingia nyuma ya usukani na kuliondoa lile gari kutoka eneo lile kwa ustadi mkubwa.
Huku kituoni, mwanamke aliyejitanda khanga alichanganyikiwa vibaya sana. Alilitazama lile gari likiondoka kutoka eneo lile kwa fadhaa iliyochanganyika na hasira.
***
"Unaelekea wapi?" Inspekta Fatma aliuliza huku akiwa amekaza macho yake barabarani. Roman alikuwa amegeuzia uso wake nje ya dirisha akiangalia mandhari ya jiji alilolikosa kwa muda wa miaka miwili. Hakufanya juhudi yoyote kuficha jinsi alivyokereka na hali ya kuwa na yule askari ndani ya lile gari.
"Umesema unataka kuongea. Ongea nami nakusikiliza.
Unaweza kuzunguka jiji lote hili wakati tunaongea...sio lazima ujue niendako!" Alimjibu kwa hasira huku bado akitazama nje ya dirisha. "Nimesema tunahitaji kuongea...mimi na wewe. Hivyo natarajia na wewe uwe unaongea. Na ndio maana nimekuuliza swali ambalo naomba unijibu. Unaelekea wapi Roman?""Hiyo inakuhusu nini? Wewe si ndugu yangu, si jamaa yangu, na wala si mke wangu! Sasa sioni swala la mimi ninaelekea wapi linaingiaje kwako.
Mimi ni mtu huru bwana!" Roman alimjibu kwa jazba. Inspekta Fatma alimtupia jicho la pembeni halafu akabaki kimya kwa muda, akijishughulisha na kuendesha gari, ingawa uso wake ulionesha kuwa na mawazo mazito. Roman alifumbata mikono yake kifuani na kuendelea kutazama nje ya dirisha la lile gari.
Safari iliendelea katika hali ile kwa muda mrefu, na katika muda ule walikuwa wameanza kuingia katikati ya jiji.
Walipita uwanja wa ndege wa kimataifa wa Dar es Salaam, na mwendo mfupi baadaye, Inspekta Fatma alipunguza mwendo wa gari na kuingia kulia ambapo aliliegesha kwa ufundi mkubwa nje ya mgahawa maarufu wa Best Bite katika lile tawi lake lililopo barabara ya Nyerere, zamani Pugu Road.
"Okay, Roman, nadhani hapa tunaweza kuongea kwa kituo zaidi."
Inspekta Fatma alimwambia yule mtu mrefu mwenye mwili ulioshiba huku akiteremka kutoka kwenye gari. Bila ya kuongea neno, lakini akionesha wazi kuwa alikuwa amechukia, Roman aliteremka na mkoba wake kutoka kwenye lile gari na kumfuata yule afisa wa polisi mrembo ndani ya ule mgahawa mzuri.
Baada ya kuagiza soda aina ya Coca Cola kwa ajili yake na bilauri ya juisi ya nanasi kwa ajili ya Roman kwa mujibu wa utashi wake, Inspekta Fatma alianzisha tena maongezi. "Roman, najua kuwa utakuwa unanichukia sana hivi sasa kwa kufanya haya niyafanyayo, lakini naomba uelewe kuwa hii ni kwa faida yako na si vinginevyo..."
Roman alimtazama yule binti bila ya kusema neno, na Fatma aliendelea."...najua kuwa baada ya kumaliza kifungo chako utakuwa tayari una mipango uliyojipangia katika maisha yako mapya. Basi na iwe ya kheri Roman, vinginevyo itakuwa mbaya sana kwako."
Roman alizidi kumtazama tu yule dada bila ya kusema neno. "Mimi nimeamua kuja kukusubiri pale Ukonga leo hii kwa sababu najali maisha yako, na kwa jinsi ninavyohisi, naona una hatari ya kurudi tena gerezani kama hutaamua kusahau yaliyopita na kutazama mbele."
Inspekta Fatma alizidi kumueleza kwa upole na msisitizo wa hali ya juu. Bado Roman alikuwa akimtazama kwa macho makavu bila ya kusema neno lolote wala kupitisha hisia yoyote usoni mwake ambayo ingeweza kusomwa na macho makini ya yule askari wa kike. Lakini Inspekta Fatma alikuwa anajua ni nini alichokuwa anataka Roman aelewe, hivyo hali ile haikumkatisha tamaa hata kidogo.
"Sahau yaliyopita Roman, na uanze maisha mapya sasa. Kama utahitaji msaada mimi niko tayari kukusaidia kwa kadiri nitakavyoweza, lakini achana kabisa na mawazo uliyonayo Roman, hayatakusaidia kitu..."
Hapo Roman hakuweza kuendelea kubaki kimya.
"Mnhu! Yaani we' unataka kuniambia kuwa unajua mi' n'na mawazo gani? Achana na mimi kabisa afande!"
***NINI kilimfanya ROMA atumikie kifungo cha miaka miwili gerezani???
**ANA mipango gani katika maisha yake baada ya kifungo ambayo Inspekta anayatilia mashaka??
**MWANAMKE mwenye baibui ni nani na anataka nini??
NA KWANINI INAITWA BONDIA ?
#SEHEMU YA 1
#SEHEMU YA 2
#SEHEMU YA 3
#SEHEMU YA 4
#SEHEMU YA 5
#SEHEMU YA 6
#SEHEMU YA 7
#SEHEMU YA 8
#SEHEMU YA 9
#SEHEMU YA 10
jonnie_vincy Khantwe mbalu byb sac mlyn VAN HEIST nrango mangimeza muuza ubuyu Jullie Z Igunga Moja culbby mugaru