Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
RIWAYA YA CONNECTION
Mtunzi: Robert Heriel
Mwaka 2024
Riwaya; CONNECTION
Kazi hii itarushwa katika mitandao kwa akaunti hizi:
Facebook: Robert Heriel Tz
Jamii Forum: Robert Heriel Mtibeli
WhatsApp +255693322300
Maandishi ya Robert Heriel Kwa Lugha ya Kiswahili. Hairuhusiwi kunakili na kusambaza kazi hii bila ruhusa ya Mwandishi.
TAIKON PUBLISHERS.
CONNECTION Ep 01
WAHUSIKA
1. Peter Mirambo
2. Kalage Nyundo
3. Lucy Njama
4. Koloa Katani
5. Julieta RangiMoto
6. Beatrice Saimon
7. Amanda Ka
8. Amini Boko
9. ( Na wengineo)
DAR ES SALAAM
Ni nje ya jengo refu la Ghorofa, Asubuhi majira ya saa moja kasoro, watu kadhaa pamoja na polisi walikuwa wamezunguka Maiti ya mwanamke iliyopasuka vibaya matumbo yakiwa yamemwagika nje na damu zikiwa zimetapakaa pale chini. Polisi waliendelea kufanya kazi yao kwa kuzungushia eneo lile utepe maalumu kwaajili ya uchunguzi wa tukio lile ambalo lilikuwa la kutisha na lililoacha hofu, huzuni na taharuki kwa kila aliyekuwa shuhuda. Alikufa kifo kibaya sana.. Kadiri muda ulivyosonga ndivyo watu walivyokuwa wanazidi kuongezeka eneo lile.
Nini kimetokea, ilikuwaje, nini kimempata mwanamke mrembo kama huyu ambaye licha ya kuharibika vibaya lakini bado uzuri wake haukuweza kupotezwa. Maswali mengi kwa kila aliyekuwa eneo lile yalikuwa yakizichaji akili za mashuhuda. Huku baadhi ya mashuhuda wakianza kugeuka watunzi wa kusimulia tukio lile.
“ Mrembo kama huyu hawezi kujirusha kwenye jengo hili. Nini kimfanye ajiue, kwanza anaonekana maisha safi. Lazima kuna mkono wa mtu. Huyu kasukumwa ghorofani” Kijana mmoja ambaye angetambulika kama dereva bodaboda alikuwa akiongea ongea huku akiwatazama Polisi waliokuwa wakihangaika kila mmoja na kazi yake. Polisi wengine walikuwa wakipiga picha kila jambo waliloona linafaa kwa kuweka kumbukumbu. Mwanaume mmoja aliyevalia kiraia alikuwa akiandika jambo Fulani kwenye kidaftari chake. Polisi Mwingine alikuwa akiukagua mwili wa Yule mwanamke aliyekufa akiwa amevalia gloves mikononi. Polisi mwingine alikuwa ameshaita Gari ya kubebea wagonjwa.
“ Acha ujinga! Unaakili sawasawa? Angekuwa Dadaako au mkeo ungempiga picha? Kuwa muungwana” Polisi mmoja alifoka huku akimnyang’anya simu kijana mmoja aliyekuwa akirekodi lile tukio. Kisha akaipiga chini kwa hasira, ile simu ikapasuka, na isingefaa kwa matumizi. Jambo hilo likafanya wengine waliokuwa wakirekodi tukio lile kuficha simu zao.
“ Nisamehe Afande. Nisamehe sana nakuomba” Yule kijana alikuwa akimsihi Polisi ambaye alikuwa amemkwida. Yule Polisi akamtazama Yule kijana kwa macho makali kisha akamsukuma huko. Yule kijana akaanguka chini.
“ Afande, hamkufanikiwa kupata simu yake?” Mwanaume mmoja aliyevalia kiraia aliuliza, ndiye Yule aliyekuwa anaandika kwenye kidaftari. Tofauti na Askari wengine waliokuwa wamevalia sare. Askari huyu hakuwa amevaa sare, alikuwa amevaa Suruali ya kadeti ya rangi ya ugoro, Tisheti nyeusi yenye kola, kapero ambayo ilificha Draid zake ndogo zilizoko kichwani. Jina lake ni Peter Mirambo, Jasusi na Komando ambaye taifa lilikuwa linajivunia kuwa na mtu wa aina yake.
“ Inashangaza Mkuu. Hatujaona simu yake” Afande mmoja akasema.
“ Sawa. Nafikiri alianguka pengine kuangushwa kutokea pale” Peter Mirambo akasema huku akatazama juu, watu wote eneo lile pamoja na askari nao wakanyanyua nyuso zao kutazama kule alikokuwa anaonyesha. Muda huo Gari ya kubebea wagonjwa iliyokuwa inapiga ving’ora ilikuwa ikiingia watu wakiwa wanaipisha. Baada ya gari ya wagonjwa kusimama, mlango wake wa nyuma ukafunguka kisha kitanda chenye matairi kikateleza mpaka chini. Alafu wanaume watatu waliovalia makoti ya kidaktari waliokuja na gari ya wagonjwa wakashuka, wakiwa wamevaa Gloves mikononi mwao wakaubeba ule mwili na kuupakiza kwenye kile kitanda chenye matairi, kisha wakauingiza ule mwili ndani ya gari kwa usaidizi wa polisi.
Vyombo vya habari vikubwa na vile vidogo vilikuwa vimeshapata habari hiyo. Vilikuwa vikikimbizana kufika eneo lile. Huku waliokwisha kutangulia wakijaribu kupata fununua na habari za kile kilichotokea.
“ Bado ni mapema mno. Hatuwezi kusema amejiua au kauawa. Jeshi la Polisi litatoa taarifa rasmi baada ya uchunguzi. Ila kwa sasa tunaweza kusema aliyekufa katika tukio hili ni mwanamke ambaye jina lake halijajulikana bado, umri wake upo kati ya miaka ishirini na nne mpaka ishirini na saba. Mweupe. Tunaomba wananchi muwe na utulivu katika wakati huu huku taratibu zingine za kipolisi zikiendelea. Nitoe rai kwa yeyote ambaye anaishi na mwanamke mwenye sifa nilizozieleza anaweza kuja kituoni kisha tutaenda kwaajili ya utambuzi” Kamanda Mkuu wa Dar akamaliza.
Picha na video za kutisha na kuhuzunisha za maiti ya Yule mwanamke aliyekutwa chini ya ghorofa zilikuwa zikivuma na kusambaa kwa kasi mitandaoni. Huku wengine wakilaani kwa kitendo cha watu kurusha picha na video hizo mtandaoni ambapo ilionekana kama ukosefu wa maadili. Kwa upande mwingine waandishi na waandaji wa maudhui mtandaoni waliiona kama fursa ya kujipatia fedha. Yalizuka makundi mawili ya wachangiaji wa maoni huko mtandaoni juu ya tukio la kifo cha Yule mwanamke. Kundi la kwanza lilikubali kuwa mwanamke Yule alijirusha ghorofani. Huku kundi jingine likikataa hoja hiyo kwa kusema kuwa mwanamke Yule aliuawa. Basi ilimradi kila mtu na uhuru wa kutoa maoni na vile akili yake ionavyo.
************
“ Siwezi kukusaidia katika hilo. Wewe mwenyewe unafahamu unachoniomba ni kosa kisheria. Unataka nivunje sheria?” Akasema,
“ Nafahamu profesa, lakini nitafanya nini? Wewe pekee ndiye wakunisaidia?”
“ Huna chakufanya zaidi ya kukubali kuwa umefeli kozi hii na itakupasa urudie mwakani. Wakati huo wenzako watakuwa wapo mitaani wakitafuta kazi, huku wengine wakiwa tayari wamepata kazi. Wewe utarudi hapa kukimbizana na coursework na vimbweta” Profesa alikuwa akisema hayo huku akimtazama Lucy Njama, mwanafunzi wa mwaka wa nne katika kitivo cha sheria.
“ Hakuna njia yoyote ya kunisaidia Profesa?” lucy akauliza kwa masikitiko huku akimtazama Profesa kwa macho ya kutaka huruma.
“ Unamaana gani Lucy?”
“Nipo tayari kufanya chochote utakachoniambia, hata kutoa pesa nitatoa Profesa” Lucy akasema huku akimtazama Profesa, kisha akaendelea,
“ Prof nipo tayari, namaanisha nipo tayari hata unambie nikupe hii..” Hapo akawa amesimama, akawa anajidengulisha na kuuonyesha urembo wake.
“ Uko serious Lucy?” Profesa akasema huku akiutazama mwili wa Lucy ulivyokuwa unavutia. Lucy alikuwa mwanamke mrembo sana. Alikuwa mzuri mwenye umbo namba nane, mwenye macho mazuri ya kisu, mwenye rangi nyeupe. Usingekataa kama ungemwona Lucy yakuwa ni moja ya wanawake wa kiwango cha juu cha uzuri ambaye uzuri wake haukuwa mbali kufanana na malaika.
“ Nipo Serious Prof, wewe niambie unahitaji pesa au penzi. Nitakuwa mwaminifu katika kuhakikisha unafurahia ilimradi unisaidie” Lucy akasema, wakati huu aliamini kuwa Prof ameshaingia kwenye mtego wake. Lakini haikuwa hivyo.
“ Mimi sipo kama unavyodhani binti. Ni kweli wewe ni mwanamke mzuri. Lakini uzuri wako hauwezi kushinda heshima niliyonayo. Ninajiheshimu, ziada ni kuwa mimi ni mwanaume bora ninayeweza kushindana na tamaa ya mwili. Mbali na hayo, wewe ni kama binti yangu”
“ Profesa sijasema wewe sio mwanaume bora, wala sijasema wewe hujiheshimu. Nakuona kama mwanaume bora ambaye unaweza kunipa msaada. Hilo tuu ndio naomba. Sahau kuhusa nilichokisema, tena uniwie radhi” Lucy aliongea kwa unyonge baada ya kugundua kuwa Profesa hakushawishika na ofa aliyoitoa.
“ Njia pekee ilikuwa kusoma, mimi nilishamaliza kazi ya kukufundisha. Kozi yenyewe inaitwa Criminology. Unataka nifanye uhalifu? Nimekuwa Profesa wa sheria kwa sababu kuu tatu. Mosi, nilikuwa napenda haki na kuchukia uhalifu na dhulma. Hii ikanifanya sio tuu nisome sheria bali kuwa mwalimu wa sheria ambaye nitawafundisha vijana na mabinti kama wewe waweze kusimamia na kulinda haki katika jamii. Pili, Kwa sababu ninaakili na ninaimudu taaluma hii. Mwisho, napenda kuona haki inatendeka hasa ikiwa katika njia yangu. Binti, ninasikitika kusema kuwa sina lolote la kukusaidia. Zaidi ninahasira kwa kuwa sijivunii wewe kuitwa mwanafunzi wangu. Ni haki yako kurudia mwaka, huna ziada..” Lucy akagonga meza kwa hasira kisha akakaa na akasimama akiwa anamtazama Profesa kwa hasira, akasema “wewe ni panya mdogo mbele ya Paka. Tutaona kama mimi na wewe nani atashinda katika hili” alafu akatoka na kubamiza mlango.
************
Ilikuwa imebaki juma moja ili wanachuo waingie katika mitihani ya mwisho ya kufunga mwaka. Lucy bado hakuwa anajua hatma yake. Ingawaje Profesa alikataa katakata kumsaidia lakini haikumfanya kukata tamaa. Lucy alikuwa akijiamini sana. Uzuri wake wa ajabu, rangi yake nyeupe ambayo ilikuwa rangi inayopendwa na wanaume wengi wa kitanzania ilichochea jeuri yake. Umbo lake lenye mfanano na namba nane liliimarisha kiburi katika nafsi yake. Asingejiamini bure, lilikuwepo jiwe kuu la msingi ambalo alilitegemea katika kuhakikisha mambo yake yanaenda. Jiwe hilo ndilo lililomsaidia kwa miaka yote tangu akiwa mwaka wa kwanza mpaka hivi leo yupo mwaka wa mwisho. “ Profesa Saimon hawezi kunishinda. Atajua mimi ni nani. Kama alizoea kuwakazia wengine kwangu amekikwaa kisiki. Kwanza nimemfanyia upendeleo tuu. Nitamwonesha” Lucy alikuwa akiwaza akiwa mwenyewe ameketi katika Moja ya Fukwe nzuri za kulipia majira ya saa moja jioni, mbele yake ikiwepo meza yenye vinywaji. Akiwa anachati na Dora ambaye ni rafiki yake anayesoma naye chuoni kozi moja. “Shoga huyo profesa ndivyo alivyo. Mwaka jana wali carryover watu arobaini. Sidhani kama kama utafanikiwa” Ujumbe kutoka kwa Dora alikuwa akiusoma Lucy. Naye akamwandikia; “Subiri utaona. Mimi ndiye Lucy. Hapa amekikwaa kisiki. Utaniambia” Akaituma, kisha akaiweka simu yake mezani alafu akatoa kioo kwenye mkoba akaanza kujiangalia kwenye kioo na kujiremba mahali alipoona hakuko sawa. Lucy alijipenda sana.
Baada ya kujiridhisha kuwa amekaa sawa Akairejea simu yake kisha akabonyeza bonyeza kwenye kioo likatokea jina la Mhe. Casto Baruani ambaye ni Waziri wa Nishati na Madini, wakati akibonyeza bonyeza mbele yake akasimama kijana mmoja mwenye urefu wa kati, mweusi ambaye upaa umemuanza kwa mbali. “Naweza kuketi?’ Yule kijana akasema huku akimtazama Lucy aliyekuwa kaboreka, Lucy akamtazama kwa macho ya koboreka kisha akaendelea kubonyeza simu na kuiweka sikioni. Yule kijana akawa amesimama tuu asijue chakufanya, “ Sorry Cute May i sit here..” kabla hajamaliza kuongea Lucy akaanza kuongea kwenye simu.
“ Hello Honey! Nimefika… uko wapi, annhaa! Nimekuona! Angalia mkono wa kushoto, nimevaa kigauni cha maruni kile ulichoninunulia, sio huko angalia upande wenye hizi boat zenye parachute nimenyosha mkono… muonee” Lucy akaachia tabasamu baada ya Mhe. Casto kumwona.
“ What is wrong with you? My Big Dady already here, Please naomba upotee uniondolee kiwingu” Lucy akasema, kisha akazipindua nywele zake zilizoko mgongoni akazileta mbele zikafunika uso wake kisha akazirudisha kwa mapozi na kuziweka sawa na mkono wake laini wenye kucha zilizopakwa rangi zenye kuvutia, na bangili tatu za rangi ya silver zilizokuwa zikiushikilia mkono wake na kuufanya uwe mkono wenye thamani. Yule kijana hakushangazwa na mashauzi ya mrembo aliyembele yake asiyemfahamu japokuwa alimwona kama moja ya malaika walowezi waliopo duniani. Yule kijana pasipo kusema neno lolote akaingiza mkono mfukoni akatoa businesicard na kuiweka meza. “ Sorry if i mistaken. It was not my intention. Hii ni contact. Please naomba tuwasiliane” Lucy akamkatisha “ Ngoja ukutwe hapa, shauri yako”
Yule kijana akaondoka baada ya kushtushwa kumwona Mhe. Casto akiwa anakuja, moja kwa moja akajua huyo ndiye Big Dady wa mrembo Yule.
Lucya kwa upesi akaichukua ile businesicard ili Mhe. Casto asijekuikuta pale. Akaiweka kwenye Mkoba wake. Tayari Mhe. Casto alikuwa amefika, Lucy akasimama na kumkumbatia kimadeko kisha akaanza kulia. Mhe. Casto akawa anambembeleza kwa kumpapasa na kumgongagonga mgongoni kimahaba. Wakaketi wakiwa wamekaribiana sana.
“ Unajua nimetoka kwenye kikao muhimu kwaajili yako Mpenzi?” Mhe. Casto.
“ Kwa sababu mimi ni muhimu kuliko hicho kikao. Mimi ni Malkia wako. Kwani nasema uongo?”
“ Hahaha! Sure! Kwangu wewe ni malaika wa furaha, unanipa raha wewe mtoto. Kila siku nakuambia naomba nikuoe….”
“Hilo tulishamaliza Mpenzi. Wewe ndiye huna maamuzi. Unampenda mkeo kuliko mimi…. Mbona najua mimi kwako ni kama mdangaji..”
“Usiseme hivyo..”
“Unataka nisemeje? Huo ndio ukweli. Nilikuambia siwezi kuwa mke mwenza on my deadbody. Sina nilichokosa. Mimi ni mwanamke mzuri kuliko, alafu nijidhalilishe kuolewa kwa mafungu.”
“Tuachane na hayo. Vipi lakini mambo mengine vipi. Maana simu hizi za ghafla lazima kutakuwa na jambo”
“ mmmh!” Lucy akashusha pumzi kama mtu aliyechoka, kisha akaendelea, “ Kuna kijibwa kinanitafuta ubaya. Nataka nikionyeshe kuwa mimi ni zaidi ya anijuavyo” Akachukua glass ya wine kisha akameza fumba kadhaa alafu akairudisha kwenye meza. Mhe. Casto alikuwa akimtazama pasipokusema chochote, akimsubiri aendelee kuzungumza.
“Nimekuwa muungwana sana kwake. Nikuulize swali?”
“ Uliza tuu Mpenzi”
“ Ukiniangalia mimi ni mtu wa kurudia mwaka chuo?”
“ Kwani vipi umefeli?” Mhe Casto akauliza swali ambalo likamchefua sana Lucy.
“ Mimi ni mjinga? Unaniona sina akili kumbe. Kumbe na wewe ni walewale. Kama huwezi kunisaidia I can handle this issue myself”
“ No Lucy! You got me wrong. Sikumaanisha hivyo. Nimekuuliza tuu. Mimi najua wewe unaakili. Sasa kama huna akili ungefikaje mpaka chuo tena ukachukua kozi ngumu ya Sheria. Hakuna asiyejua kuwa kozi ya sheria inahitaji mtu mwenye akili za juu ili aweze kuimudu” Mhe. Casto alijitetea, alivyokuwa akijitetea mbele ya Lucy ambaye ni binti mdogo aliyemzidi miaka ya kutosha ambayo ingetosha kumuita binti yake. Mbali na hivyo yeye ni Waziri cheo ambacho ni kikubwa katika taifa letu.
Lakini ndio hivyo mapenzi hayana mbabe. Hayaangalii umri wako, cheo chako, taaluma yako au vyovyote uwavyo. Mapenzi yanaweza kukufanya ufanye vitu ambavyo kikawaida ni ngumu kuvifanya.
“Nilikuambia nipo kwaajili yako Lucy. Nambie unahitaji nikusaidie nini?” Hapo Lucy akatabasamu alivyosikia maneno hayo.
“ Nataka umpigie simu sasa hivi pofesa Saimon, umwambie…..”
“ Profesa Saimon ndio nani?” Mhe, Casto akamkatisha.
“ Sikujua kuwa unaweza ukawa mjinga na ukawa Profesa. Hivi hilo kwenu wanasiasa inawezekana?” lucy akasema mara hii akiwa ameimarika.
“ Kisiasa inawezekana kabisa mjinga kumfundisha mwerevu. Mpumbavu kumwongoza mwenye hekima. Kipofu kuona zaidi ya wenye macho..”
“ Basi ndivyo ilivyo kwa Yule Profesa wa ujinga ambaye anafundisha sheria pale chuo cha taifa. Yeye anataka nirudie mwaka lakini yeye ndiye atarudia kusoma huo uprofesa wake sio mimi”
“ Sasa unataka nifanyaje?”
“ Nataka umfundishe adabu profesa Saimon?”
“ Nikadhani unataka umalize chuo,,,”
“ Nataka vyote. Kumaliza chuo na kumfundisha adabu huyo profesa wa ujinga. Atajuta. Nimejikomba kwake kumstahi yeye analeta ujuaji”
“ Sikiliza Lucy. Yote hayo yanawezekana lakini mimi nafikiri cha muhimu sasa wewe umalize chuo. Hizo zingine ni hasira tuu. Msamehe” Mhe. Casto akasema,
“ Unamtetea? Hujui alivyonifanyia nilipomfuata. Mimi sio wa kudharauliwa na mjinga kama Yule. Kwanza mimi sio level zake”
“ Najua! Embu tulia mpenzi. Kunywa hii hasira zipungue. Alafu hili tutalimaliza kirahisi sana” akammnywesha Lucy Wine akiwa kamshika kwenye bega. Lucy alipomaliza kunywa akasema,
“ Naomba simu yako?”
“ Simu yangu!” “Ndio”
“Mmmh!” Mhe. Casto akaguna hapohapo Lucy akamnyang’anya simu, “ toa lock” lucy akasema huku akimrudishia Mhe. Casto simu.. “ Mbona nimekamatika, yaani naendeshwa na haka kabinti kama mtoto” Mhe. Akawaza huku akitoa Lock ya simu yake kisha akampa.
Lucy akachukua simu na kuanza kunakili namba Fulani kutoka kwenye simu yake kwenda kwenye simu ya Mhe. Casto. Baada ya kunakili akaipigia ikawa inaita. Muda wote Mhe. Casto alikuwa akitazama alichokuwa anakifanya Lucy kwenye simu yake.
“ Shika! Ongea naye” Lucy akasema,
“ Nani?” “ Profesa mjinga”
“ Subiri kwanza, unataka nimwambie nini mpenzi?” “
“ Hujui cha kumwambia….” “ Shiiii” mara simu ikapokelewa. Mhe. Casto akamnyamazisha Lucy.
“ Hello! Habari yako Profesa Saimon” Mhe. Casto akasema, Lucy akasogea karibu zaidi na kubonyeza simu sehemu ya sauti kubwa, kisha sauti ya Profesa ikawa inasikika.
“ Salama kabisa, samahani nazungumza na nani?”
“ Huyu ni Waziri wa Nishati na Madini”
“ Waziri wa Nishati na Madini? Unamaanisha Mhe. Casto Baruani?”
“ Naam! Ni mimi Profesa”
“ Habari yako Mhe. Waziri” Sauti ya profesa ilikuwa ikizungumza kwa mashaka na kutokuamini.
“ Huku tuko salama. Kuna ishu nahitaji unisaidie kama mkubwa mwenzangu”
“ Mimi nikusaidie wewe au wewe unisaidie mimi? Hahaha! Wewe ni mkubwa kwangu kicheo, sidhani kama kuna jambo naweza kukusaidia, wewe ndiye unaweza kunisaidia” Profesa akasema,
“ hahahah! Hamna Profesa, Ukubwa haimaanishi huwezi pata msaada kutoka kwa waliochini yako. Nisaidie”
Hapo kukawa kimya kwa kitambo, bila shaka Profesa alikuwa anawaza ni jambo gani ambalo Waziri wa Nishati na madini anahitaji msaada. Yeye hakuwa na mazoea na wanasiasa. Pengine aliwaza litakuwa jambo la kisheria hasa sheria za Mambo ya madini.
“ Profesa! Profes..” Mhe. Casto akaita “ Nipo hewani Mheshimiwa”
“ Embu msaidie Lucy amalize shule salama, Lucy ni binti yetu. Mchukulie kama mtoto wako. Hutokosa chochote kitu. Nitaandaa donge nono kwaajili yako”
“ Mhe. Casto nakuheshimu sana. Ten asana. Lakini kwa hili utanisamehe. Nilishamalizana na Lucy mwenyewe. Nilimuelewesha akaelewa. Anahitajika kurudia hiyo kozi ili awe bora zaidi. Hiyo ndio nzuri niliyoamua kumsaidia. Na sheria za chuo ziko wazi” Profesa akasema kwa utulivu mkubwa na kila neno akiwa ameliwekea msisitizo.
“Nafahamu maadili yako ya kazi hayakutaki uvunje kanuni na sheria. Lakini hii kwako ni kama amri. Hizo sheria zinatungwa na serikali. Wewe sio serikali. Mimi kama moja ya viongozi wa serikali ambaye pia ni kiongozi wako ninayomamlaka ya kupita juu, juu kabisa ya hizo sheria. Hiyo sheria kwangu ipo chini kabisa, wala sio kitu. Ni sheria ndogo ambayo inasimamia watumishi na wanafunzi. Sio mimi” Mhe. Casto alikuwa akiongea hasira zikianza kumchochea, hakutegemea kuwa angepata upinzani kutoka kwa Profesa kutokana na cheo chake cha uwaziri.
“ Mhe. Casto, unakosea sana. Lakini sihitaji kukufundisha kuhusu hizo sheria unazoziita ndogo na kubwa. Ninachoweza kukuambiwa siwezi kukusaida chochote. Kama kuna jambo jingine unaweza kunambia lakini katika hilo jalada lake nilishalifunga hata angekuja nani..” Profesa akasema lakini Lucy akaingilia.
“ Wewe ndiye utarudia huo uprofesa wako ambao sijui hata umeupataje. Lakini sio Mimi Lucy. Umeingia sehemu mbaya sana Mzee..” Mhe. Casto akamziba Mdomo Lucy asiendelee kuongea. Kisha akasema.
“ Profesa, nashukuru sana kwa kuniabisha. Nimekubali.”
“ Sijakuabisha Mhe.. Wewe ndiye umejiingiza kwenye aibu isiyo na ulazima. Mimi nafanya kazi kwa kanuni na maadili. Hayo ndio yanayoniongoza” Profesa akasema lakini kabla hajamaliza Mhe. Casto akakata simu.
“ Bastard!” Mhe. Casto akasema akiwa amefura kwa hasira.
“ Nilikuambia huyu Profesa anadharau sana. Unaona ambavyo amekujibu na wewe” Lucy akasema huku akimchochea Mhe. Casto azidi kuchukia. Mhe. Casto alikuwa kimya akitafakari jambo kwa kitambo.
“ Kwa hiyo tunafanyaje my Bigdad? Maana sasa sio jambo langu tena, limegeuka letu. Sikutegemea akudharau mbele yangu. Bora angenidharau mimi binti mdogo nisiye na cheo, lakini vipi wewe?” Lucy akasema akiwa kamsogelea zaidi Mhe. Casto huku akishika ndevu zake. Mhe. Casto hakuongea kitu akaangalia saa yake ya mkononi, ilikuwa saa mbili na nusu za usiku.
“ Muda umekimbia, nitalishughulikia jambo hili. Ni ishu ndogo mno. Wala usiwe na hofu” Akasema,
“ Lakini siku zilizobakia ni chache, hili lifanyike kwa upesi. Mimi sitaki kurudia mwaka”
“Usijali. Lipo ndani ya uwezo wetu” “ Unauhakika Mpenzi? Maana huyu profesa kama ulivyomsikia inaonekana yupo tayari kwa lolote hata kupoteza kazi”
“ Mimi ni mwanasiasa, nadili na taifa mtu mmoja hawezi kunishinda. Nishakuambia hii ni ishu ndogo. Zimebaki siku ngapi?”
“ Siku nne Mpenzi. Nimeanza kuingiwa na hofu” Usihofu, siku nne ni nyingi. Mpaka kesho kutwa hili litakuwa limeisha”
“Utafanyaje?” “ Ninajua nini nitafanya, subiri simu kutoka kwa huyohuyo Profesa yeye mwenyewe ndiye atakupigia akikuambia hautarudia mwaka na utaingia kwenye mitihani yako ya mwisho, utamaliza malkia wangu” Mhe. Casto akasema, macho yake muda mwingi yalikuwa yakiangalia saa yake ya mkononi.
“ Nimefurahi mpenzi. Nakupenda Bigdad wangu. Kwako najihisi salama. Kwa kweli nitakupa zawadi kubwa kama utanisaidia nimalize chuo. Sitaki kurudia. Kwanza nimechoka kusoma”
“ Nafikiri nikuache, ninakikao kingine na Rais majira ya saa tatu. Muda umekimbia, nina kama dakika ishirini tuu.”
“ Sawa mpenzi. Kama ukiona inakusumbua mwambie hata shemu Darlin Rais, huyu Profesa ajue kuheshimu wakubwa zake”
“ Hahahah! I will handle it myself. Shika hii ya pizza leo usiku” Mhe. Casto akasema akimkabidhi Lucy kiasi cha shilingi laki moja. Kisha wakaagana
ITAENDELEA
Pia itakuwa inaendelea kwenye Channel ya WhatsApp. Bonyeza Link hii 👉🏼Tibeli Star | WhatsApp-Kanal
0693 322 300
Mtunzi: Robert Heriel
Mwaka 2024
Riwaya; CONNECTION
Kazi hii itarushwa katika mitandao kwa akaunti hizi:
Facebook: Robert Heriel Tz
Jamii Forum: Robert Heriel Mtibeli
WhatsApp +255693322300
Maandishi ya Robert Heriel Kwa Lugha ya Kiswahili. Hairuhusiwi kunakili na kusambaza kazi hii bila ruhusa ya Mwandishi.
TAIKON PUBLISHERS.
CONNECTION Ep 01
WAHUSIKA
1. Peter Mirambo
2. Kalage Nyundo
3. Lucy Njama
4. Koloa Katani
5. Julieta RangiMoto
6. Beatrice Saimon
7. Amanda Ka
8. Amini Boko
9. ( Na wengineo)
DAR ES SALAAM
Ni nje ya jengo refu la Ghorofa, Asubuhi majira ya saa moja kasoro, watu kadhaa pamoja na polisi walikuwa wamezunguka Maiti ya mwanamke iliyopasuka vibaya matumbo yakiwa yamemwagika nje na damu zikiwa zimetapakaa pale chini. Polisi waliendelea kufanya kazi yao kwa kuzungushia eneo lile utepe maalumu kwaajili ya uchunguzi wa tukio lile ambalo lilikuwa la kutisha na lililoacha hofu, huzuni na taharuki kwa kila aliyekuwa shuhuda. Alikufa kifo kibaya sana.. Kadiri muda ulivyosonga ndivyo watu walivyokuwa wanazidi kuongezeka eneo lile.
Nini kimetokea, ilikuwaje, nini kimempata mwanamke mrembo kama huyu ambaye licha ya kuharibika vibaya lakini bado uzuri wake haukuweza kupotezwa. Maswali mengi kwa kila aliyekuwa eneo lile yalikuwa yakizichaji akili za mashuhuda. Huku baadhi ya mashuhuda wakianza kugeuka watunzi wa kusimulia tukio lile.
“ Mrembo kama huyu hawezi kujirusha kwenye jengo hili. Nini kimfanye ajiue, kwanza anaonekana maisha safi. Lazima kuna mkono wa mtu. Huyu kasukumwa ghorofani” Kijana mmoja ambaye angetambulika kama dereva bodaboda alikuwa akiongea ongea huku akiwatazama Polisi waliokuwa wakihangaika kila mmoja na kazi yake. Polisi wengine walikuwa wakipiga picha kila jambo waliloona linafaa kwa kuweka kumbukumbu. Mwanaume mmoja aliyevalia kiraia alikuwa akiandika jambo Fulani kwenye kidaftari chake. Polisi Mwingine alikuwa akiukagua mwili wa Yule mwanamke aliyekufa akiwa amevalia gloves mikononi. Polisi mwingine alikuwa ameshaita Gari ya kubebea wagonjwa.
“ Acha ujinga! Unaakili sawasawa? Angekuwa Dadaako au mkeo ungempiga picha? Kuwa muungwana” Polisi mmoja alifoka huku akimnyang’anya simu kijana mmoja aliyekuwa akirekodi lile tukio. Kisha akaipiga chini kwa hasira, ile simu ikapasuka, na isingefaa kwa matumizi. Jambo hilo likafanya wengine waliokuwa wakirekodi tukio lile kuficha simu zao.
“ Nisamehe Afande. Nisamehe sana nakuomba” Yule kijana alikuwa akimsihi Polisi ambaye alikuwa amemkwida. Yule Polisi akamtazama Yule kijana kwa macho makali kisha akamsukuma huko. Yule kijana akaanguka chini.
“ Afande, hamkufanikiwa kupata simu yake?” Mwanaume mmoja aliyevalia kiraia aliuliza, ndiye Yule aliyekuwa anaandika kwenye kidaftari. Tofauti na Askari wengine waliokuwa wamevalia sare. Askari huyu hakuwa amevaa sare, alikuwa amevaa Suruali ya kadeti ya rangi ya ugoro, Tisheti nyeusi yenye kola, kapero ambayo ilificha Draid zake ndogo zilizoko kichwani. Jina lake ni Peter Mirambo, Jasusi na Komando ambaye taifa lilikuwa linajivunia kuwa na mtu wa aina yake.
“ Inashangaza Mkuu. Hatujaona simu yake” Afande mmoja akasema.
“ Sawa. Nafikiri alianguka pengine kuangushwa kutokea pale” Peter Mirambo akasema huku akatazama juu, watu wote eneo lile pamoja na askari nao wakanyanyua nyuso zao kutazama kule alikokuwa anaonyesha. Muda huo Gari ya kubebea wagonjwa iliyokuwa inapiga ving’ora ilikuwa ikiingia watu wakiwa wanaipisha. Baada ya gari ya wagonjwa kusimama, mlango wake wa nyuma ukafunguka kisha kitanda chenye matairi kikateleza mpaka chini. Alafu wanaume watatu waliovalia makoti ya kidaktari waliokuja na gari ya wagonjwa wakashuka, wakiwa wamevaa Gloves mikononi mwao wakaubeba ule mwili na kuupakiza kwenye kile kitanda chenye matairi, kisha wakauingiza ule mwili ndani ya gari kwa usaidizi wa polisi.
Vyombo vya habari vikubwa na vile vidogo vilikuwa vimeshapata habari hiyo. Vilikuwa vikikimbizana kufika eneo lile. Huku waliokwisha kutangulia wakijaribu kupata fununua na habari za kile kilichotokea.
“ Bado ni mapema mno. Hatuwezi kusema amejiua au kauawa. Jeshi la Polisi litatoa taarifa rasmi baada ya uchunguzi. Ila kwa sasa tunaweza kusema aliyekufa katika tukio hili ni mwanamke ambaye jina lake halijajulikana bado, umri wake upo kati ya miaka ishirini na nne mpaka ishirini na saba. Mweupe. Tunaomba wananchi muwe na utulivu katika wakati huu huku taratibu zingine za kipolisi zikiendelea. Nitoe rai kwa yeyote ambaye anaishi na mwanamke mwenye sifa nilizozieleza anaweza kuja kituoni kisha tutaenda kwaajili ya utambuzi” Kamanda Mkuu wa Dar akamaliza.
Picha na video za kutisha na kuhuzunisha za maiti ya Yule mwanamke aliyekutwa chini ya ghorofa zilikuwa zikivuma na kusambaa kwa kasi mitandaoni. Huku wengine wakilaani kwa kitendo cha watu kurusha picha na video hizo mtandaoni ambapo ilionekana kama ukosefu wa maadili. Kwa upande mwingine waandishi na waandaji wa maudhui mtandaoni waliiona kama fursa ya kujipatia fedha. Yalizuka makundi mawili ya wachangiaji wa maoni huko mtandaoni juu ya tukio la kifo cha Yule mwanamke. Kundi la kwanza lilikubali kuwa mwanamke Yule alijirusha ghorofani. Huku kundi jingine likikataa hoja hiyo kwa kusema kuwa mwanamke Yule aliuawa. Basi ilimradi kila mtu na uhuru wa kutoa maoni na vile akili yake ionavyo.
************
“ Siwezi kukusaidia katika hilo. Wewe mwenyewe unafahamu unachoniomba ni kosa kisheria. Unataka nivunje sheria?” Akasema,
“ Nafahamu profesa, lakini nitafanya nini? Wewe pekee ndiye wakunisaidia?”
“ Huna chakufanya zaidi ya kukubali kuwa umefeli kozi hii na itakupasa urudie mwakani. Wakati huo wenzako watakuwa wapo mitaani wakitafuta kazi, huku wengine wakiwa tayari wamepata kazi. Wewe utarudi hapa kukimbizana na coursework na vimbweta” Profesa alikuwa akisema hayo huku akimtazama Lucy Njama, mwanafunzi wa mwaka wa nne katika kitivo cha sheria.
“ Hakuna njia yoyote ya kunisaidia Profesa?” lucy akauliza kwa masikitiko huku akimtazama Profesa kwa macho ya kutaka huruma.
“ Unamaana gani Lucy?”
“Nipo tayari kufanya chochote utakachoniambia, hata kutoa pesa nitatoa Profesa” Lucy akasema huku akimtazama Profesa, kisha akaendelea,
“ Prof nipo tayari, namaanisha nipo tayari hata unambie nikupe hii..” Hapo akawa amesimama, akawa anajidengulisha na kuuonyesha urembo wake.
“ Uko serious Lucy?” Profesa akasema huku akiutazama mwili wa Lucy ulivyokuwa unavutia. Lucy alikuwa mwanamke mrembo sana. Alikuwa mzuri mwenye umbo namba nane, mwenye macho mazuri ya kisu, mwenye rangi nyeupe. Usingekataa kama ungemwona Lucy yakuwa ni moja ya wanawake wa kiwango cha juu cha uzuri ambaye uzuri wake haukuwa mbali kufanana na malaika.
“ Nipo Serious Prof, wewe niambie unahitaji pesa au penzi. Nitakuwa mwaminifu katika kuhakikisha unafurahia ilimradi unisaidie” Lucy akasema, wakati huu aliamini kuwa Prof ameshaingia kwenye mtego wake. Lakini haikuwa hivyo.
“ Mimi sipo kama unavyodhani binti. Ni kweli wewe ni mwanamke mzuri. Lakini uzuri wako hauwezi kushinda heshima niliyonayo. Ninajiheshimu, ziada ni kuwa mimi ni mwanaume bora ninayeweza kushindana na tamaa ya mwili. Mbali na hayo, wewe ni kama binti yangu”
“ Profesa sijasema wewe sio mwanaume bora, wala sijasema wewe hujiheshimu. Nakuona kama mwanaume bora ambaye unaweza kunipa msaada. Hilo tuu ndio naomba. Sahau kuhusa nilichokisema, tena uniwie radhi” Lucy aliongea kwa unyonge baada ya kugundua kuwa Profesa hakushawishika na ofa aliyoitoa.
“ Njia pekee ilikuwa kusoma, mimi nilishamaliza kazi ya kukufundisha. Kozi yenyewe inaitwa Criminology. Unataka nifanye uhalifu? Nimekuwa Profesa wa sheria kwa sababu kuu tatu. Mosi, nilikuwa napenda haki na kuchukia uhalifu na dhulma. Hii ikanifanya sio tuu nisome sheria bali kuwa mwalimu wa sheria ambaye nitawafundisha vijana na mabinti kama wewe waweze kusimamia na kulinda haki katika jamii. Pili, Kwa sababu ninaakili na ninaimudu taaluma hii. Mwisho, napenda kuona haki inatendeka hasa ikiwa katika njia yangu. Binti, ninasikitika kusema kuwa sina lolote la kukusaidia. Zaidi ninahasira kwa kuwa sijivunii wewe kuitwa mwanafunzi wangu. Ni haki yako kurudia mwaka, huna ziada..” Lucy akagonga meza kwa hasira kisha akakaa na akasimama akiwa anamtazama Profesa kwa hasira, akasema “wewe ni panya mdogo mbele ya Paka. Tutaona kama mimi na wewe nani atashinda katika hili” alafu akatoka na kubamiza mlango.
************
Ilikuwa imebaki juma moja ili wanachuo waingie katika mitihani ya mwisho ya kufunga mwaka. Lucy bado hakuwa anajua hatma yake. Ingawaje Profesa alikataa katakata kumsaidia lakini haikumfanya kukata tamaa. Lucy alikuwa akijiamini sana. Uzuri wake wa ajabu, rangi yake nyeupe ambayo ilikuwa rangi inayopendwa na wanaume wengi wa kitanzania ilichochea jeuri yake. Umbo lake lenye mfanano na namba nane liliimarisha kiburi katika nafsi yake. Asingejiamini bure, lilikuwepo jiwe kuu la msingi ambalo alilitegemea katika kuhakikisha mambo yake yanaenda. Jiwe hilo ndilo lililomsaidia kwa miaka yote tangu akiwa mwaka wa kwanza mpaka hivi leo yupo mwaka wa mwisho. “ Profesa Saimon hawezi kunishinda. Atajua mimi ni nani. Kama alizoea kuwakazia wengine kwangu amekikwaa kisiki. Kwanza nimemfanyia upendeleo tuu. Nitamwonesha” Lucy alikuwa akiwaza akiwa mwenyewe ameketi katika Moja ya Fukwe nzuri za kulipia majira ya saa moja jioni, mbele yake ikiwepo meza yenye vinywaji. Akiwa anachati na Dora ambaye ni rafiki yake anayesoma naye chuoni kozi moja. “Shoga huyo profesa ndivyo alivyo. Mwaka jana wali carryover watu arobaini. Sidhani kama kama utafanikiwa” Ujumbe kutoka kwa Dora alikuwa akiusoma Lucy. Naye akamwandikia; “Subiri utaona. Mimi ndiye Lucy. Hapa amekikwaa kisiki. Utaniambia” Akaituma, kisha akaiweka simu yake mezani alafu akatoa kioo kwenye mkoba akaanza kujiangalia kwenye kioo na kujiremba mahali alipoona hakuko sawa. Lucy alijipenda sana.
Baada ya kujiridhisha kuwa amekaa sawa Akairejea simu yake kisha akabonyeza bonyeza kwenye kioo likatokea jina la Mhe. Casto Baruani ambaye ni Waziri wa Nishati na Madini, wakati akibonyeza bonyeza mbele yake akasimama kijana mmoja mwenye urefu wa kati, mweusi ambaye upaa umemuanza kwa mbali. “Naweza kuketi?’ Yule kijana akasema huku akimtazama Lucy aliyekuwa kaboreka, Lucy akamtazama kwa macho ya koboreka kisha akaendelea kubonyeza simu na kuiweka sikioni. Yule kijana akawa amesimama tuu asijue chakufanya, “ Sorry Cute May i sit here..” kabla hajamaliza kuongea Lucy akaanza kuongea kwenye simu.
“ Hello Honey! Nimefika… uko wapi, annhaa! Nimekuona! Angalia mkono wa kushoto, nimevaa kigauni cha maruni kile ulichoninunulia, sio huko angalia upande wenye hizi boat zenye parachute nimenyosha mkono… muonee” Lucy akaachia tabasamu baada ya Mhe. Casto kumwona.
“ What is wrong with you? My Big Dady already here, Please naomba upotee uniondolee kiwingu” Lucy akasema, kisha akazipindua nywele zake zilizoko mgongoni akazileta mbele zikafunika uso wake kisha akazirudisha kwa mapozi na kuziweka sawa na mkono wake laini wenye kucha zilizopakwa rangi zenye kuvutia, na bangili tatu za rangi ya silver zilizokuwa zikiushikilia mkono wake na kuufanya uwe mkono wenye thamani. Yule kijana hakushangazwa na mashauzi ya mrembo aliyembele yake asiyemfahamu japokuwa alimwona kama moja ya malaika walowezi waliopo duniani. Yule kijana pasipo kusema neno lolote akaingiza mkono mfukoni akatoa businesicard na kuiweka meza. “ Sorry if i mistaken. It was not my intention. Hii ni contact. Please naomba tuwasiliane” Lucy akamkatisha “ Ngoja ukutwe hapa, shauri yako”
Yule kijana akaondoka baada ya kushtushwa kumwona Mhe. Casto akiwa anakuja, moja kwa moja akajua huyo ndiye Big Dady wa mrembo Yule.
Lucya kwa upesi akaichukua ile businesicard ili Mhe. Casto asijekuikuta pale. Akaiweka kwenye Mkoba wake. Tayari Mhe. Casto alikuwa amefika, Lucy akasimama na kumkumbatia kimadeko kisha akaanza kulia. Mhe. Casto akawa anambembeleza kwa kumpapasa na kumgongagonga mgongoni kimahaba. Wakaketi wakiwa wamekaribiana sana.
“ Unajua nimetoka kwenye kikao muhimu kwaajili yako Mpenzi?” Mhe. Casto.
“ Kwa sababu mimi ni muhimu kuliko hicho kikao. Mimi ni Malkia wako. Kwani nasema uongo?”
“ Hahaha! Sure! Kwangu wewe ni malaika wa furaha, unanipa raha wewe mtoto. Kila siku nakuambia naomba nikuoe….”
“Hilo tulishamaliza Mpenzi. Wewe ndiye huna maamuzi. Unampenda mkeo kuliko mimi…. Mbona najua mimi kwako ni kama mdangaji..”
“Usiseme hivyo..”
“Unataka nisemeje? Huo ndio ukweli. Nilikuambia siwezi kuwa mke mwenza on my deadbody. Sina nilichokosa. Mimi ni mwanamke mzuri kuliko, alafu nijidhalilishe kuolewa kwa mafungu.”
“Tuachane na hayo. Vipi lakini mambo mengine vipi. Maana simu hizi za ghafla lazima kutakuwa na jambo”
“ mmmh!” Lucy akashusha pumzi kama mtu aliyechoka, kisha akaendelea, “ Kuna kijibwa kinanitafuta ubaya. Nataka nikionyeshe kuwa mimi ni zaidi ya anijuavyo” Akachukua glass ya wine kisha akameza fumba kadhaa alafu akairudisha kwenye meza. Mhe. Casto alikuwa akimtazama pasipokusema chochote, akimsubiri aendelee kuzungumza.
“Nimekuwa muungwana sana kwake. Nikuulize swali?”
“ Uliza tuu Mpenzi”
“ Ukiniangalia mimi ni mtu wa kurudia mwaka chuo?”
“ Kwani vipi umefeli?” Mhe Casto akauliza swali ambalo likamchefua sana Lucy.
“ Mimi ni mjinga? Unaniona sina akili kumbe. Kumbe na wewe ni walewale. Kama huwezi kunisaidia I can handle this issue myself”
“ No Lucy! You got me wrong. Sikumaanisha hivyo. Nimekuuliza tuu. Mimi najua wewe unaakili. Sasa kama huna akili ungefikaje mpaka chuo tena ukachukua kozi ngumu ya Sheria. Hakuna asiyejua kuwa kozi ya sheria inahitaji mtu mwenye akili za juu ili aweze kuimudu” Mhe. Casto alijitetea, alivyokuwa akijitetea mbele ya Lucy ambaye ni binti mdogo aliyemzidi miaka ya kutosha ambayo ingetosha kumuita binti yake. Mbali na hivyo yeye ni Waziri cheo ambacho ni kikubwa katika taifa letu.
Lakini ndio hivyo mapenzi hayana mbabe. Hayaangalii umri wako, cheo chako, taaluma yako au vyovyote uwavyo. Mapenzi yanaweza kukufanya ufanye vitu ambavyo kikawaida ni ngumu kuvifanya.
“Nilikuambia nipo kwaajili yako Lucy. Nambie unahitaji nikusaidie nini?” Hapo Lucy akatabasamu alivyosikia maneno hayo.
“ Nataka umpigie simu sasa hivi pofesa Saimon, umwambie…..”
“ Profesa Saimon ndio nani?” Mhe, Casto akamkatisha.
“ Sikujua kuwa unaweza ukawa mjinga na ukawa Profesa. Hivi hilo kwenu wanasiasa inawezekana?” lucy akasema mara hii akiwa ameimarika.
“ Kisiasa inawezekana kabisa mjinga kumfundisha mwerevu. Mpumbavu kumwongoza mwenye hekima. Kipofu kuona zaidi ya wenye macho..”
“ Basi ndivyo ilivyo kwa Yule Profesa wa ujinga ambaye anafundisha sheria pale chuo cha taifa. Yeye anataka nirudie mwaka lakini yeye ndiye atarudia kusoma huo uprofesa wake sio mimi”
“ Sasa unataka nifanyaje?”
“ Nataka umfundishe adabu profesa Saimon?”
“ Nikadhani unataka umalize chuo,,,”
“ Nataka vyote. Kumaliza chuo na kumfundisha adabu huyo profesa wa ujinga. Atajuta. Nimejikomba kwake kumstahi yeye analeta ujuaji”
“ Sikiliza Lucy. Yote hayo yanawezekana lakini mimi nafikiri cha muhimu sasa wewe umalize chuo. Hizo zingine ni hasira tuu. Msamehe” Mhe. Casto akasema,
“ Unamtetea? Hujui alivyonifanyia nilipomfuata. Mimi sio wa kudharauliwa na mjinga kama Yule. Kwanza mimi sio level zake”
“ Najua! Embu tulia mpenzi. Kunywa hii hasira zipungue. Alafu hili tutalimaliza kirahisi sana” akammnywesha Lucy Wine akiwa kamshika kwenye bega. Lucy alipomaliza kunywa akasema,
“ Naomba simu yako?”
“ Simu yangu!” “Ndio”
“Mmmh!” Mhe. Casto akaguna hapohapo Lucy akamnyang’anya simu, “ toa lock” lucy akasema huku akimrudishia Mhe. Casto simu.. “ Mbona nimekamatika, yaani naendeshwa na haka kabinti kama mtoto” Mhe. Akawaza huku akitoa Lock ya simu yake kisha akampa.
Lucy akachukua simu na kuanza kunakili namba Fulani kutoka kwenye simu yake kwenda kwenye simu ya Mhe. Casto. Baada ya kunakili akaipigia ikawa inaita. Muda wote Mhe. Casto alikuwa akitazama alichokuwa anakifanya Lucy kwenye simu yake.
“ Shika! Ongea naye” Lucy akasema,
“ Nani?” “ Profesa mjinga”
“ Subiri kwanza, unataka nimwambie nini mpenzi?” “
“ Hujui cha kumwambia….” “ Shiiii” mara simu ikapokelewa. Mhe. Casto akamnyamazisha Lucy.
“ Hello! Habari yako Profesa Saimon” Mhe. Casto akasema, Lucy akasogea karibu zaidi na kubonyeza simu sehemu ya sauti kubwa, kisha sauti ya Profesa ikawa inasikika.
“ Salama kabisa, samahani nazungumza na nani?”
“ Huyu ni Waziri wa Nishati na Madini”
“ Waziri wa Nishati na Madini? Unamaanisha Mhe. Casto Baruani?”
“ Naam! Ni mimi Profesa”
“ Habari yako Mhe. Waziri” Sauti ya profesa ilikuwa ikizungumza kwa mashaka na kutokuamini.
“ Huku tuko salama. Kuna ishu nahitaji unisaidie kama mkubwa mwenzangu”
“ Mimi nikusaidie wewe au wewe unisaidie mimi? Hahaha! Wewe ni mkubwa kwangu kicheo, sidhani kama kuna jambo naweza kukusaidia, wewe ndiye unaweza kunisaidia” Profesa akasema,
“ hahahah! Hamna Profesa, Ukubwa haimaanishi huwezi pata msaada kutoka kwa waliochini yako. Nisaidie”
Hapo kukawa kimya kwa kitambo, bila shaka Profesa alikuwa anawaza ni jambo gani ambalo Waziri wa Nishati na madini anahitaji msaada. Yeye hakuwa na mazoea na wanasiasa. Pengine aliwaza litakuwa jambo la kisheria hasa sheria za Mambo ya madini.
“ Profesa! Profes..” Mhe. Casto akaita “ Nipo hewani Mheshimiwa”
“ Embu msaidie Lucy amalize shule salama, Lucy ni binti yetu. Mchukulie kama mtoto wako. Hutokosa chochote kitu. Nitaandaa donge nono kwaajili yako”
“ Mhe. Casto nakuheshimu sana. Ten asana. Lakini kwa hili utanisamehe. Nilishamalizana na Lucy mwenyewe. Nilimuelewesha akaelewa. Anahitajika kurudia hiyo kozi ili awe bora zaidi. Hiyo ndio nzuri niliyoamua kumsaidia. Na sheria za chuo ziko wazi” Profesa akasema kwa utulivu mkubwa na kila neno akiwa ameliwekea msisitizo.
“Nafahamu maadili yako ya kazi hayakutaki uvunje kanuni na sheria. Lakini hii kwako ni kama amri. Hizo sheria zinatungwa na serikali. Wewe sio serikali. Mimi kama moja ya viongozi wa serikali ambaye pia ni kiongozi wako ninayomamlaka ya kupita juu, juu kabisa ya hizo sheria. Hiyo sheria kwangu ipo chini kabisa, wala sio kitu. Ni sheria ndogo ambayo inasimamia watumishi na wanafunzi. Sio mimi” Mhe. Casto alikuwa akiongea hasira zikianza kumchochea, hakutegemea kuwa angepata upinzani kutoka kwa Profesa kutokana na cheo chake cha uwaziri.
“ Mhe. Casto, unakosea sana. Lakini sihitaji kukufundisha kuhusu hizo sheria unazoziita ndogo na kubwa. Ninachoweza kukuambiwa siwezi kukusaida chochote. Kama kuna jambo jingine unaweza kunambia lakini katika hilo jalada lake nilishalifunga hata angekuja nani..” Profesa akasema lakini Lucy akaingilia.
“ Wewe ndiye utarudia huo uprofesa wako ambao sijui hata umeupataje. Lakini sio Mimi Lucy. Umeingia sehemu mbaya sana Mzee..” Mhe. Casto akamziba Mdomo Lucy asiendelee kuongea. Kisha akasema.
“ Profesa, nashukuru sana kwa kuniabisha. Nimekubali.”
“ Sijakuabisha Mhe.. Wewe ndiye umejiingiza kwenye aibu isiyo na ulazima. Mimi nafanya kazi kwa kanuni na maadili. Hayo ndio yanayoniongoza” Profesa akasema lakini kabla hajamaliza Mhe. Casto akakata simu.
“ Bastard!” Mhe. Casto akasema akiwa amefura kwa hasira.
“ Nilikuambia huyu Profesa anadharau sana. Unaona ambavyo amekujibu na wewe” Lucy akasema huku akimchochea Mhe. Casto azidi kuchukia. Mhe. Casto alikuwa kimya akitafakari jambo kwa kitambo.
“ Kwa hiyo tunafanyaje my Bigdad? Maana sasa sio jambo langu tena, limegeuka letu. Sikutegemea akudharau mbele yangu. Bora angenidharau mimi binti mdogo nisiye na cheo, lakini vipi wewe?” Lucy akasema akiwa kamsogelea zaidi Mhe. Casto huku akishika ndevu zake. Mhe. Casto hakuongea kitu akaangalia saa yake ya mkononi, ilikuwa saa mbili na nusu za usiku.
“ Muda umekimbia, nitalishughulikia jambo hili. Ni ishu ndogo mno. Wala usiwe na hofu” Akasema,
“ Lakini siku zilizobakia ni chache, hili lifanyike kwa upesi. Mimi sitaki kurudia mwaka”
“Usijali. Lipo ndani ya uwezo wetu” “ Unauhakika Mpenzi? Maana huyu profesa kama ulivyomsikia inaonekana yupo tayari kwa lolote hata kupoteza kazi”
“ Mimi ni mwanasiasa, nadili na taifa mtu mmoja hawezi kunishinda. Nishakuambia hii ni ishu ndogo. Zimebaki siku ngapi?”
“ Siku nne Mpenzi. Nimeanza kuingiwa na hofu” Usihofu, siku nne ni nyingi. Mpaka kesho kutwa hili litakuwa limeisha”
“Utafanyaje?” “ Ninajua nini nitafanya, subiri simu kutoka kwa huyohuyo Profesa yeye mwenyewe ndiye atakupigia akikuambia hautarudia mwaka na utaingia kwenye mitihani yako ya mwisho, utamaliza malkia wangu” Mhe. Casto akasema, macho yake muda mwingi yalikuwa yakiangalia saa yake ya mkononi.
“ Nimefurahi mpenzi. Nakupenda Bigdad wangu. Kwako najihisi salama. Kwa kweli nitakupa zawadi kubwa kama utanisaidia nimalize chuo. Sitaki kurudia. Kwanza nimechoka kusoma”
“ Nafikiri nikuache, ninakikao kingine na Rais majira ya saa tatu. Muda umekimbia, nina kama dakika ishirini tuu.”
“ Sawa mpenzi. Kama ukiona inakusumbua mwambie hata shemu Darlin Rais, huyu Profesa ajue kuheshimu wakubwa zake”
“ Hahahah! I will handle it myself. Shika hii ya pizza leo usiku” Mhe. Casto akasema akimkabidhi Lucy kiasi cha shilingi laki moja. Kisha wakaagana
ITAENDELEA
Pia itakuwa inaendelea kwenye Channel ya WhatsApp. Bonyeza Link hii 👉🏼Tibeli Star | WhatsApp-Kanal
0693 322 300