Riwaya: I died to save my President

Riwaya: I died to save my President

I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 23

wapi ilipo kompyuta yake.Elvis
naomba usiniache hapa.take me
anywhere safe.Ni mara yanguya
kwanza kukuona lakini I feel safe
around.macho yako yananifanya
nikuamini” akasema Graca huku
macho yake yakilengwa na
machozi
“ Nitakusaidia
Graca.Nitakuondoa hapa na
kukupeleka sehemu salama
kabisa ambako si baba yako wala
yeyote anayekutafuta
atakupata.Lakini kabla ya kufanya
hivyo kuna jambo nataka
kulifahamu toka kwako.Nataka
kufahamu ndani ya hilo begi
kulikuwa na kitu gani cha
muhimu kiasi cha kupelekea
baba yako kufanya haya yote
aliyoyafanya?Kompyuta hiyo uliyoichukua ilikuwa na jambo
gani na iko wapi kwa sasa?
Graca akamtazama Elvis na
kusema
“Siwezi kukueleza chochote
kwa sasa hivi hadi hapo
nitakapohakikisha kwamba niko
sehemu salama.Take me
somewhere safe and I will tell you
everythingI know na nitakueleza
kompyuta hiyo iko wapi” akasema
Graca
“ Graca ninaelewa hofu yako
lakini naomba uniamini na
uniambie kuhusiana na
ulichokigunuda kwa baba
yako.Tafadhali naomba
ushirikiane nani.Usiniogope mimi
si mtu mbaya” akasema Elvis
“ Elvis najua umefunga safari
ndefu kuja huku kuonana na mimi kwa nia njema kabisa na
kama nilivyokueleza awali kwamba
ninakuamini na niko tayari
kukueleza kila kitu lakini kwa
sasa siwezi kukueleza jambo lolote
ninalolifahamu hadi hapo
nitakapohakikisha kwamba niko
salama.Mkoba ule na kilichomo
ndani yake ndiyo kinga yangu kwa
sasa kwa hiyo fanya
nilivyokuelekeza na nitakueleza
kila unachokitaka” akasema Graca
“ Graca !!... Elvis akataka
kusema kitu lakini Graca
akamzuia
“ Elvis hakuna chochote
utakachoniambia kitakachoweza
kuubadili msimamo wangu.Ninazo
taarifa nyeti sana ambazo
ninaamini zitakuwa ni za msaada
mkubwa sana kwako lakini siwezi kukueleza hadi hapo
nitakapohakikisha kwamba niko
salama” akasemaGraca.Elvis
akamtazama kwa makini usoni na
kuamini kile alichokisema Graca
“ She’s telling the
truth.hawezi kunieleza chochote
bila kufanya anavyotaka” akawaza
Elvis na kusema
“Nimekuelewa
Graca.Naomba unipe muda
kidogo niangalie namna ya
kufanya.I promise you I’ll get
you out of here.”akasema
Elvis.Bila kusema chochote
Graca akainuka na kutembea
taratibu kuelekea ndani.Elvis
akamtazama namna
alivyokuwa akitembea kwa
unyonge akamuonea huruma
sana lazima nimsaidie.Siwezi
kumuacha hapa akiendelea
kuteseka.Akawaza Elvis
halafu akaelekea katika meza
waliyokuwa wamekaa Bongan
na Dr Susan
“ Tayari mmekwisha
ongea? Umefanikiwa kupata
ulichokuwa unakihitaji? Akauliza
Bongani
“ Bongani mambo si rahisi
kama nilivyitegemea" akasema
Elvis
“ Nini kimetokea Elvis,Graca
hajakupa ushirikiano? ” akauliza
Bongani.Elvis akamvuta pembeni
kidogo ili waongee.Akamweleza
kila kitu alichoongea na Graca
“kwa hiyo mambo yako
namna hiyo Bongani.Graca kuna
jambo kubwa analifahamu kuhusiana na baba yake lakini
hayuko tayari kuliweka wazi bila
kwanza kuwa na uhakika wa
usalama wa maisha yake”
akasemaElvis
“ kwa hiyo tutafanya nini
Elvis ili tuweze kuzipata taarifa
hizo toka kwa Graca?akauliza
Bongani
“hakuna njia nyingine ya
kufanya zaidi ya kufanya vile
anavyotaka yaani kumpeleka
sehemu salama.Bongani naomba
unisaidie katika hili ili niweze
kumuondoa Graca hapa
hospitali.Pamoja na kuwa na kitu
cha muhimu ninachokihitaji lakini
nimeguswa sana na mateso ya
binti huyu,ameteseka kiasi cha
kutosha na siko tayari kumuacha akiendelea kuteseka
hapa.Tafadhali naomba unisaidie”
Bongani akafikiri kwa muda
na kusema
“ Hata mimi nimeguswa sana
na histora ya huyu binti na
nitakusaidia ili tuweze kumtoa
hapa.Ninachotaka kufahamu ni
kuhusu usalama wa maisha yake
endapo tutafanikiwa kumuondoa
hapa.Una hakika atakuwa
salama?akauliza Bongani.Elvis
akawaza kidogo na kusema
“Bongani suala la usalama wa
Graca lina changamoto nyingi
lakini hilo ni jukumu langu
ambalo sina budi kulibeba na
nitahakikisha kwamba anakuwa
salama.Nitamlinda dhidi ya yeyote
mwenye nia ya kumdhuru” “Bongani akainama akafikri
kidogo na kusema
“ sawa Elvis
.Nitakusaidia,naomba unipe muda
wa dakika kama kumi nikaongee
na Dr Susan nione kama anaweza
akatusaidia”
“ una hakika atatusaidia?
Akauliza Elvis
“ Nina uhakika lakini hatuna
budi kujaribu.Nina mahusiano
naye mazuri.Tuliwahi kuwa katika
mahusiano ya kimapenzi wakati
tukiwa chuo kikuu na mpaka sasa
bado tuna mahusiano mazuri”
akasema Bongani na kuelekea
katika ofisi ya Dr Susan
“Nahisi kuna suala zito sana
ambalo liko nyuma ya pazia kiasi
kwamba Frank alikuwa tayari hata
kutaka kumuua mwanae kwa ajili ya kulificha.Lazima nilifahamu
suala hilo .Nitamsaidia Graca kwa
namna yoyote ile nitakayoweza na
nitamuondoa hapa.Nitamlinda
dhidi ya yeyote yule anayetishia
maisha yake.”akawaza Elvis
Bongani alitumia zaidi ya
dakika kumi na tano kuongea na
Dr Susan kumuelezea kuhusiana
na tatizo la Graca.Hadi anamaliza
kumueleza Dr Susan alikuwa
anahisi baridi.Alionekana kuzama
katika mawazo mengi
“ Siku zote nilijua lazima
kuna jambo haliko sawa kwa
Graca.Sikutaka kuharakisha
kumuuliza nini kilichokuwa
kinamsumbua na ndiyo maana
nikajenga ukaribu mkubwa kati
yangu naye ili siku moja aweze
kunieleza tatizo lake.Namuoenea huruma sana binti huyu kwa
mateso makubwa aliyonayo.Huu
ni mtihani mkubwa kwangu lakini
lazim animsaidie” Dr Susan akiwa
katika mawazo mengi mara
akastuliwa na Bongani
“ Dr Susan !!...
Akainua kichwa na kumtazama
Bongani
“Unasemaje Bongan? Akauliza
“ natumani umenisikia na
kunielewa.Nini mawazo yako?
Akaulizia Bongani .Dr Susan
akavuta pumzi ndefu na kusema
“Bongani nashindwa niseme
nini lakini naomba nikiri kwamba
nimegswa mno na historia nzima
ya Graca.Siku zote nilikuwa
nikifahamu kwamba Graca ana
tatizo kubwa linalomsumbua
tofauti na ugonjwa wa akili lakini sikuweza kumshawishi anieleze
tatizo lake.Maelezo uliyonipa
yamenistua mno”akasema Dr
Susan
“ Dr Susna sote tumeguswa
na tatizo la Graca na ndiyo maana
tunatafuta namna ya kumsaidia
na mtu pekee ambaye
tunamtegemea kwa sasa ni wewe”
akasema Bongani .Dr Susan
akaonekana kuzama mawazoni
halafu akakohoa kidogo na
kusema
“ Una hakika kwamba Elvis
ana nia ya dhati kumsaidia Graca
na si mmoja wa watu wa baba
yake ambaye anataka kumchukua
na kwenda kumdhuru?
Bongani akatabasamu na
kusemaElvis anafanya kazi kama
ninayofanya mimi na lengo lake ni
kumsaidia Graca hivyo nakuomba
usiwe na hofu naye hata kdogo”
akasema Bongani.Dr Susan
akaegemea kti chake akatazama
juu kwa sekunde kadhaa na
kusema
“ Nitamsaidia.Ninakuamini
sana na nina hakika baada ya
kutoka hapa Graca atakuwa
katika mikono salama”
“ Ahsante sana Dr Susan
.Ahsante sana kwa msaada wako”
akasema Bongani kwa furaha.
“Tutafanya hivi.Graca
nitaondoka naye mimi katika gari
langu.Hataondoka na kitu
chochote hapa kila kitu chake
atakiacha hapa ili kutoleta udadisi
pindi itakapobainika kwambaametoweka.Baada ya kama dakika
kumi nitakapoondoka ninyi
mtafuata kwa nyuma.Nitawasubiri
pale kwa Pamela
Thambo”akasemaDr Susna
naBongani akatoka mle ofisini kwa
Dr Susan akamfuata Elvis
“ What happened? amekubali
kutusuaidia?akauliza Elvis kwa
wai wasi mara tu alipomuona
Bongani
“ Ndiyo! Amekubali
kutusaidia” akasema Bongani
“ Thank you Lord! Akasema
Elvis huku akiinua mikono
kumshukuru Mungu.Bongani
akamueleza Elvis namna mpango
utakavyokuwa kisha wakaelekea
katika kantini ya hospitali hapo
wakaagiza vinywaji baridi.Wakati
wakiendelea na vinwyaji mara ikapita gari ya Dr Susan
ikafunguliwa geti na kutoka bila
kukaguliwa . Dakika kumi baada
ya Dr Susan kutoka Bongani na
Elvis nao wakaelekea lilipo gari
lao,wakaingia na kuondoka.Katika
lango kuu walikaguliwa na
kuruhusiwa kupita wakaondoka.
******************
Katika nyumba kubwa
iliyokuwa na utulivu
mkubwa,Bongani ,Elvis na Graca
walikuwa wamekaa wakijaribu
kuangalia ni kwa namna gani
Elvis na Graca watakavyoweza
kurejea Tanzania salama.Graca
alionekana mchovu sana hali
iliyomlazimu alale sofani na kuwaacha Bongani na Elvis
wakiendelea kujadiliana
“ Kuna njia nyingi za kuweza
kuwaondoa hapa na kuwarudisha
Tanzania lakini tunahitaji kupata
usafiri wa haraka wa kuweza
kuwaondoa hapa leo hii
.Hamtakiwi kulala hapa leo”
akasema Bongani
“ Hilo ni jambo la msingi sana
.Kwa hali ilivyo hatutakiwi kulala
hapa leo.Tutawezaje basi kupata
usafiri wa haraka wa kutuondoa
hapa? “ akauliza Elvis .Bongani
akainama akafikiri kidogo na
kusema
“ Usihofu kuhusu suala hilo
Elvis.Ni jukumu langu
kuhakikisha kwamba unapata
usafiri na unaondoka hapa
salama.Ngoja kwanza niwasiliane na washirika wangu kadhaa nione
namna watakavyoweza kunisaidia”
akasema Bongani kisha akainuka
na kuelekea chumbani .Elvis
akamtazama Graca aliyekuwa
amelala sofani .Graca akageuza
shingo na kugonganisha macho na
Elvis ,akatabasamu kidogo na kwa
sauti ndogo akauliza
“ Mbona unanitazama hivyo?
Elvis akainuka na kwenda kukaa
katika sofa lililokuwa pembeni ya
Graca
“ Unajisikiaje Graca?
Akauliza
“ Ninajisikia vizuri tu.Ni yale
madawa waliyokuwa wakinichoma
ndiyo yanayonifanya nionekane
naumwa sana lakini mimi siumwi”
akasema Pole sana Graca.Kuna kitu
chochote unahitaji kwa sasa?
“Elvis Kwa sasa Ninachohitaji
ni kwenda sehemu salama”
“ Usihofu Graca.Nimeibeba
dhamana hiyo ya usalama wako
na nitahakikisha unakuwa salama
na hakuna atakayekudhuru”
“ Nitashukuru sana kwa hilo
Elvis….” Akasema Graca na mara
Bongani akaingia pale sebuleni
“ Vipi kuna mafanikio yoyote ?
akauliza Elvis
“ Ndiyo.Kunaweza kuwa na
uwezekano.Nimewasiliana na
mmoja wa rafiki zangu
amenidokeza kwamba kuna ndege
ya jeshi inaondoka usiku wa leo
kuelekea Zambia.Nimewasiliana
na mmoja wa makamanda wa
jeshi amenitaka nionane naye sasa hivi.Ngoja nikaonane naye
nimsikilize ni mtu ambaye nina
hakika anaweza akanisaidia”
akasema Bongani
“ Ahsante sana Bongani kwa
msaada wako huu
mkubwa.Ninaomba Mungu
ufanikiwe ili tuweze kuondoka
hapa” akasema Elvis
“ Usihofu Elvis.Ngoja
nikaonane na huyu mkuu
nitarejea baada ya muda mfupi”
akasema Bongani na kutoka.
“ Huyu rafiki yako ana roho
nzuri sana.Ni nadra sana katika
dunia ya sasa kumpata mtu
ambaye anaweza akakuhangaikia
kama huyu.” Akasema Graca
baada ya Bongani kuondoka.Elvis
akatabasamu na kusema Anaitwa Bongani.Naye
anafanya kazi kama ninayoifanya
mimi na vile vile ni rafiki yangu
sana.Ni jadi yetu kusaidiana
tunapokuwa na matatizo na hata
yeye akija Tanzania na akiwa na
tatizo ni jukumu langu
kuhakiksha kwamba nimemsaidia
kwa kila namna.Hivyo ndivyo
tunavyofanya kazi” akasema Elvis
“ Natamani na mimi siku
moja ningefanya kazi kama yako”
akasema Graca
“ Unaipenda kazi hii?
Akauliza Elvis
“ Ndiyo nimetokea kuipenda
sana” akasema Graca
“ Kwa nini unaipenda kazi
hii?
“ Mambo yaliyonikuta ndiyo
yananifanya niipende na na nitake kufanya kazi kama yako.Nataka
nipambane na watu makatili wasio
na hata chembe ya huruma kwa
binadamu wenzao.Vile vile nataka
nilipe kisasi kwa baba yangu
pamoja na washirika wake kwa
kusababisha maisha yangu yawe
namna hii.Unawezaje kunisaidia ili
niweze kuifanya kazi hii? akauliza
Graca
Elvis akavuta pumzi ndefu
akamtazama Graca ambaye
hakuonyesha kama alikua
akitania
“ Graca naomba unisikilize
mdogo wangu .Kwanza kabisa
naomba ufahamu kwamba kuna
maisha mazuri zaidi
yanayokusubiri pale utakapokuwa
huru na unastahili maisha
mazuri.Umri wako bado unaruhusu wewe kuendelea na
masomo na baadae ukaishi
maisha yale ambayo umekuwa
ukiyaota kwa siku nyingi hivyo
naomba uondoe kabisa kichwani
mwako wazo la kutaka kufanya
kazi kama hii.Kazi hii ni ngumu
mno na ina mambo mazito ndani
yake .Inahitaji mtu mwenye roho
ngumu kama ya paka.Mara tu
uingiapo katika kazi hii hutakuwa
na maisha ya kawaida tena kwani
muda wote unakuwa
umezungukwa na maadui ambao
dhamira zao si njema hata kidogo
na walio tayari kuua muda wowote
.Kazi hii inakuweka katika hatari
muda wote.Wengi wetu tumeingia
katika kazi hii bila kufahamu
tunakwenda kukutana na mambo
gani na kwa sasa tumekwisha zoea na kuiona ni ya kawaida lakini
naomba nikuhakikishie kwamba
hii si kazi rahisi kuifanya na wala
usiitamani.Niko tayati kukusaidia
kwa kila namna niwezavyo
kuyajenga maisha yao lakini si
kukusaidia ili uingie katika kazi
hii.Umenielewa Graca? Akaulizia
Elvis
“ Nimekuelewa Elvis japokuwa
bado moyo wangu unataka sana
kuifanya kazi hii ili niweze
kuufutilia mbali mtandao wote wa
baba” akasema Graca na kuzidi
kumvutia zaidi Elvis
“ Mtandao upi Graca? Baba
yako ana mtandao
unaoshughulika na nini? Akauliza
Elvis
“ Usiwe na haraka
Elvis.Utafahamu kila kitu ila naomba ufuate makubaliano yetu
.Nipeleke sehemu salama na
nitakueleza kila kitu
ninachokifahamu” akasema Graca
“ Sawa nitahakikisha
unakuwa salama.Ninahitaji sana
taarifa zako”
“ Usijali Elvis,nitakueleza kila
kitu,” akasema Graca halafu
ghafla akaonekana kama kuna
kitu anakiwaza
“ Elvis kuna kitu ambacho
nilisahau kukwambia”
“ Kitu gani Graca?
“ Kuna watu wawili pale
hospitali wamekuwa
wakinichunguza.Kuna mpishi
mmoja pamoja na mlinzi.Watu
hawa wamekuwa wakinifuatilia
sana na nina hakika watakuwa
wanalipwa na baba ili wanichunguze nyendo
zangu.Japokuwa sina hakika sana
lakini kwa namna walivyokuwa
wakinifuatilia nina hisi lazima
watakuwa wamepewa kazi ya
kunichunguza” akasema Graca
“ Usijali kuhusu hao
watu.Hata kama wamewekwa na
baba yako kukuchunguza hawana
uwezo wa kupambana na
mimi.Usihofu kitu ukiwa na mimi”
akasema Elvis
“ Ahsante sana Elvis”
akasema Graca na kimya kifupi
kikapita
Ilipita saa moja na dakika ishirini
Bongani akarejea
“ Hallow Elvis.Mko salama
wote?
“ Tuko salama.Mambo
yamekwendaje huko? Mambo yamekwenda vizuri
sana .Kuna ndege ya jeshi
inayowapeleka wanajeshi kwenye
mazoezi nchini Zambia na tayari
nimekwisha ongea na kiongozi wa
kikosi hicho na amenikubalia
kuwachukua na ninyi.Hakukuwa
na ugumu wowote kwani wakuu
wengi wa jeshi ni marafiki
zangu.Pale Lusaka nimekwisha
wasiliana na mtu mmoja anaitwa
Stanley Chiteta.Huyu ni rafiki
yangu mkubwa na ni mfanyakazi
wa idara ya usalama wa taifa ya
Zambia.Yeye ndiye
atakayewapeleka hadi katika
mpaka wa Tanzania na Zambia
katika mji wa Tunduma na tokea
pale hamtakuwa na wasi wasi tena
mtakuwa mmekwisha ingia nchini
kwenu na mtatafuta usafiri wa kuelekea Dar es salaam.Stanley ni
mzoefu na nina hakika atakuwa ni
msaada mkubwa kwenu” akasema
Bongani
“ Bongani sina namna ya
kukushukuru kwa msaada wako
huu mkubwa uliotusaidia.”
Akasema Elvis .Bongani
akatabasamu na kusema
“ Usijali Elvis ni jukumu
langu kukusaidia na nimefanya
kile ninachopaswa kukifanya .Kwa
kuwa hatuna muda wa kutosha ni
wakati sasa wa kujiandaa kwa
safari.” Akasema Bongani na
kumpatia Graca mfuko uliokuwa
na nguo na vitu vingine mbali
mbali alivyomnunulia.Graca
akaingia chumbani kujiandaa na
baada ya kuwa tayari safari ya kuelekea uwaja wa ndege wa jeshi
ikaanza
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Ni saa moja za jioni ,kiza
tayari kimetanda angani,Patricia
na Doreen rafiki yake wamekaa
katika kibaraza nyumbani kwa
Doreen wakiongea.Walionekana
kuzama katika maongezi mazito
“ Kwa hiyo Doreen maisha
yangu yanazidi kuwa magumu
siku hadi siku.Umeona wewe
mwenyewe ujumbe ninaotumiwa
katika simu na ndugu za
Elvis.Wanayafanya maisha yangu
yawe magumu sana.Hakuna mtu
anayejali upendo mkubwa uliopo
kati yangu na Elvis.Wao
wanachotaka ni mtoto tu” akasema Patricia kwa
uchungu.Doreen akamtazama
akamuonea huruma rafiki yake
“ Pole sana Patricia
.Ninafahamu ni kiasi gani
unaumizwa na suala hili na kama
nilivyokueleza toka awali kwamba
niko tayari kukusaidia katika
jambo hili.Sipendi kukuona
ukiumia namna hii” Akasema
Doreen
“ Doreen nashukuru sana
kwa kukubali kunisaidia ingawa
najua haikuwa rahisi kukubali
kufanya jambo kama hili lakini
tutafanya nini tena wakati mpango
wetu ulishindikana? Akasema
Patricia .Kimya kikatanda kila
mmoja alikuwa anawaza lake.Ni
Doreen ndiye aliyeuvunja ukimya Patricia naomba usikate
tamaa ndugu yangu. Ni kweli
tulijaribu ikashindikana lakini
hatupaswi kukata tamaa
.Tunapaswa kufikiri namna
nyingine tutakayoweza kufanya ili
kumfanya Elvis akubaliane na
wazo letu” akasema Doreen
“ Doreen unionavyo hapa
tayari nimekwisha fikiri sana na
ninatumai akili yangu imefikia
kiwango chake cha mwisho cha
kufikiri na bado sijapata jibu”
akasema kwa uchungu
Patricia.Doreen akamshika bega
na kumwambia
“ Patricia its too early to give
up.Nina hakika lazima tutapata
njia ya kufanya .Kitu cha msingi
ni kujaribu kutuliza akili na kuja na mpango mpya.Nina hakika
tutafanikiwa “ akasema Doreen
“ Doreen sina shaka nawe
hata kidogo najua uko tayari
kunisadia lakini tatizo liko kwa
Elvis.Ananipenda kupindukia na
hayuko tayari kufanya jambo
kama hili tunalolipanga.Suala la
kumuomba azae na mwanamke
mwingine kwake yeye ni sawa na
usaliti kwangu kwa hiyo hataki
kabisa
kulisikia.Nimechanganyikiwa
Doreen na sijui tutafanya nini na
ndugu za Elvis ndo hao wanadai
mtoto kila leo” akasema Patricia
“ Unaonaje endapo tutakaa
naye na kuongea naye kwa pamoja
kuhusiana na suala hili pengine
anaweza akatuelewa” Akasema
Doreen Elvis ni mtu mwenye
msimamo mkali sana na akisema
hapana katika jambo Fulani basi
huwa ni vigumu sana
kumbadili.Sina hakika kama hata
tukimueleza ukweli anaweza
akatuelewa.Mpango ule
ulioshindikana ulikuwa mzuri
sana” akasema Patricia
“ Pamoja na hayo Patricia ni
mapema mno kukata tamaa.Bado
kuna njia nyingi tu tunaweza
kufanya ili kumfanya Elvis
akubaliane nasi” Akasema Doreen
Patricia akamtazama na
kuonyesha wasi wasi
“ Unazungumzia njia gani
Doreen? Kama unazungumzia
masuala ya waganga mimi siko
tayari kwa hilo.Ni bora niendelee kuteseka kuliko kwenda kwa
waganga”
Doreen akacheka na kusema
“ Hapana Patricia.Mimi si
muumini wa masuala hayo na
tangu utoto wangu siamini kabisa
katika mambo hayo ya
waganga.Nilikuwa namaanisha
kutafuta njia nyingine za kuweza
kulifanikisha jambo hili hata kama
Elvis hataki kuliko kukata tamaa”
akasema Doreen
“ Hilo ndilo jambo la msingi
ambao tunapaswa kulifanya kwa
sasa.Ngoja kwanza niende
nikapumzishe kichwa ili nije na
wazo jipya.” Akasema Patricia
huku akinyanyua mkoba wake na
kupiga hatua kuelekea lilipo gari
lake Sikuwahi kuota kama siku
moja nitakuwa na wakati mgumu
kama nilionao hivi sasa. Kuna
wakati ninajuta hata kuolewa
.Ningekuwa peke yangu haya yote
yasingenitokea.Anyaway
ninampenda Elvis na nitalipigania
penzi letu kwa gharama zozote
zile” akawaza Patricia
********************
Ni shamba lenye ekari zaidi ya
kumi lililoko njekidogo ya jiji la dar
es salaam.Ndani ya shamba hilo
lililosheheni mazao mbalimbali
kulikuwa pia na mifugo kama vile
kuku,ng’ombe n.k.Kati kati ya
shamba lile kuwa kulikuwa na
jumba kubwa la kifahari la ghorofa
tatu.Hili ni shamba linalomilikiwa na Brigedia jenerali Frank
kwaju.Jioni hii ukimya mzito
ulitawala kulizunguka jumba
hili.Ni milio ya mifugo tu ndiyo
iliyokuwa ikisikika .Hakukuwa na
zile pita pita za kila siku za
wafanyakazi
Saa mbili na dakika tatu za
usiku,gari tatu zikawasili katika
geti la kuingilia shambani
hapo.Geti kubwa likafunguliwa na
walinzi na kisha gari zile
zikaikamata barabara iliyokuwa
inaelekea moja kwa moja katikati
ya shamba liliko jumba lile kubwa
lililozungukwa na ukuta mkubwa
na nyaya za umeme juu yake.Geti
likafunguliwa na gari zikaingia
Watu kumi wakashuka toka
katika zile gari wakiongozwa na
Brigedia jenereli Frank halafu wakalekea ndani katika ukumhi
wa siri wa mikutano ulioko ndani
ya jumba lile.Ukumbi tayari
ulikwisha andaliwa maalum kwa
ajili ya kikao hiki kizito
kinachotaratiwa kufanyika usiku
huu.Baada ya kama dakika
ishirini toka akina Frank wawasili
pale numbani,zikawasili gari mbili
na akashuka waziri mkuu mstaafu
Daud Sichoma akiwa
ameongozana na watu wengine
watano wakapokelewa na Brigedia
Frank na kupelekwa katika
ukumbi wa mikutano ambako
wajumbe wote waliokuwa
wakitakiwa katika kikao kile
walikwisha wasili na aliyekuwa
akisubiriwa ni Mheshimiwa Daudi
Sichoma na ujumbe wake.Mara tu
walipoingia katika chumba cha mikutano,watu wote wakasimama
kuonyesha heshima kwa wgeni
waliowasili.Daudi na ujumbe wake
wakaonyeshwa viti wakaketi na
bila kupoteza wakati mwenyekiti
wa kikao kile brigedia Frank
akafungua kikao.Kwanza alianza
kwa kufanya utambulisho.Baada
ya wajumbe kufahamiana kwa
majina na sehemu watokako
Frank akaendelea
“ Ndugu wajumbe nadhani ni
wakati sasa wa kuwatambulisha
wageni wetu wakuu waliotufanya
tukusanyike hapa usiki
huu.Wageni wetu watasimama na
kujitambulisha wao ni akina nani
na kisha tutaendelea na kile
kilichotuleta” akasema Frank na
kuwaomba wageni wale wawili wasimame mmoja mmoja na
kujitambulisha
“ naitwa Mustapha Al
jamal”akaanza kujitambulisha
mgeni wa kwanza
“ Mimi ni raia wa Iran na ni
mmiliki wa wa kampuni moja
kubwa ya mafuta katika
mashariki ya kati.Kwa sababu za
kiusalaam naomba nisiitaje
kampuni yangu hadi hapo
mbeleni” akamaliza
kujitambulisha ndugu Mustapha
na kumpa nafasi mwenzake
aliyeambatana naye
“ Mimi naitwa Alhafidh
Sadiq.Na mimi kama mwenzangu
aliyetangulia ni mmiliki wa
kampuni kadhaa kubwa za mafuta
katika eneo la mashariki ya
kati.Vile vile kama alivyofanya mwenzangu nisingependa na mimi
kuziweka wazi kampuni zangu”
akasema Alhafidh
“ Ahsanteni sana wageni wetu
kwa kujitambulisha.Sisi ni
wenzenu na tumefurahi sana
kuwa nanyi hapa kwa usiku
huu”akasema Frank akameza
mate na kuendelea
“ Ndugu wajumbe baada ya
kuwafahamu wagheni wetu
naomba sasa tuendelee na kikao
chetu.” Akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“ Wageni wetu hawa
wamekuja na jambo zito sana
ambalo utekelezaji wake
unatuhitaji sana sisi.Endapo
jambo hili likifanikiwa basi sisi
sote pamoja wao tutafaidika
sana.Kwa hiyo basi sitaki kuchukua muda mwingi kwani
muongeaji mkuu yupo na ndiye
atakayetueleza kila kitu.Karibu
ndugu Alhafidh ili uweze kutueleza
nini hasa kilichowaleta hapa
Tanzania” akasema Frank.Alhafidh
akaweka sawa koo lake akafungua
faili lililokuwa mbele yake
akaisoma karatasi ya kwanza kana
kwamba kuna mambo
anajikumbusha halafu akasema
“ Ndugu zangu ni furaha
kubwa kwetu kukutana nanyi
usiku huu.Kwa niaba ya
mwenzangu napenda kuchukua
nafasi hii kuwashukuru nyote kwa
kuacha shughuli zenu na kuja
kutusikiliza.Napenda
kuwahakikishia kwamba
hamtajutia kufika kwenu hapa
usiku huu kwani suala tulilowaitia hapa ni lenye manufaa makubwa
kwenu na kwetu pia.Brigedia
jeneral Frank ni rafiki yangu sana
wa muda mrefu.Tumefahamiana
katika shughuli zetu za kibiashara
na ninyi nyote aliowachagua
kuhuddhuria kikao hiki nina
imani ni watu makini na
anaowaakini hivyo natumaini
mazungumzo yetu yatakwenda
vizuri” Alhafidh akanyamza kidogo
akameza mate na kuendelea
“ Nadhani ninyi nyote hapa
mnafahamu hali halisi ya eneo
zima la masharaiki ya kati
inavyoendelea hivi sasa.Katika kila
taarifa ya habari inayotangazwa
duniani hakukosekani taarifa
kuhusiana na mashariki ya
kati.Lakini nini hasa kiini cha
machafuko yote katika eneo hili la mashariki ya kati?.Chanzo chote
cha machafuko ni nchi za
Marekani na washirika wake.Nchi
hizi za magharibi zimekuwa
zikiendesha chochoko dhidi ya
serikali za mashariki ya kati na
hivyo kusababisha machafuko
kusambaa katika eneo zima la
masharikiya kati.Lakini naomba
nyote mjiulize kwa nini mashariki
ya kati? Kwa nini nchi za
magharibi zinachochea migogoro
na mifarakano mashariki ya kati?
Jibu hapa ni jepesi sana.Ni kwa
sababu ya utajiri mkubwa wa
mafuta ulioko katika eneo
hili.Migogoro hii inapotokea
wanaofaidika ni Marekani na
washirika wake kwani hujitokeza
na kuingilia kati huku wakibeba
na kujiwekea akiba kubwa ya mafuta katika nchi zao huku
wakiwaacha maelfu ya watu wasio
na hatia wakiuana.Suala hili
limeamsha hasira na chuki kubwa
dhidi ya marekani na washirika
wake na ndiyo maana mnasikia
kila mara vinaibuka vikundi
mbalimbali vya kigaidi ambavo
vingi adui yake mkubwa ni
Marekani na washirika wake.Hii ni
sababu kubwa iliyopeleka
Marekani kuanza kujitoa taratibu
katika siasa za mashariki ya kati
na kuanza kupunguza utegemezi
wa mafuta toka mashariki ya kati
.Kwa hivi sasa marekani
imeongeza juhudi katika kuzalisha
mafuta ya ndani ikiwemo mafuta
yatokanayo na mimea
.Wamewekeza katika teknolojia
mpya ili watengeneze magari na mitambo visivyohitaji mafuta
mengi.” Alhafidh akanyamaza
kidogo halafu akaendelea.
“ Baada ya utafiti wa miaka
mingi kuhusiana na uwepo wa
mafuta na gesi katika bahari kuu
nchini Tanzania na kulitolewa
taarifa iliyoushangaza
ulimwengu.Kumegunduliwa kiasi
kikubwa cha mafuta nchini
Tanzania ambacho kinasemekena
ni kikubwa kuliko hata
kilekinachoweza kupatikaana eneo
zima la mashariki ya kati.Huu ni
ugunduzi mkubwa sana kuwahi
kufanyika katika miaka ya hivi
karibuni.Ugunduzi huu unaifanya
Tanzania kuingia katika
ulimwengu mpya kwani mataifa
yote makubwa hivi sasa
yameelekeza macho yao nchini Tanzania.Uchumi wa Tanzania
utapaa kwa kasi kubwa na ndani
ya muda mfupi ujao nchi yenu
itaingia katika nchi tajiri duniani”
Alhafidh akatulia na kuwatazama
wajumbe ambao wote walikuwa
wakitabasamu kutokana na taarifa
ile
“ Rais wa marekani
amemaliza ziara ya siku nne
nchini Tanzania ikiwa ni ziara
ndefu kuwahi kufanywa na rais
wa marekani katika taifa moja
husan haya ya bara la
Afrika.Ninathubutu kusema
kwamba hii imekua ni ziara yenye
mafanikio makubwa sana kwa
marekani.Mambomengi mazuri
yamefanyika katika ziara hiyo
ikiwa ni pamoja na kuzindua
miradi mikubwa ya nishati ,reli na maji,Pamoja na mambo hayo
makubwa huku watanzania walio
wengi wanaamni ni neema kubwa
wameipata lakini nataka mjiulize
kwa nini iwe sasa? Kwanini rais
wa marekani aitembelee Tanzania
sasa tena ikiwa ni ziara ndefu
kuwahi kufanywa na kiongozi
yoyote wa taifa la marekani katika
nchi yoyote ya afrika? Jibu hapa
ni rahisi tu.Nikwa sababu ya
neema kubwa ya mafuta na gesi
iliyogunduliwa Tanzania..Sababu
ya pili ni kujiimarisha kijeshi kwa
kujenga kambi yake hapa
Tanzania ili kuendeleza
mapambano dhidi ya wale wote
wenye kupambana na taifa hili
bila kuchoka na hasa vikundo vya
kigaidi kama vile
Alqaeda,alshabaab,Boko haram, n.k ambavyo vimekuwa
vikijimarisha sana kwa siku za
karibuni” Alhafish akanyamaza
kidogo na kuwatazama wajumbe
wa kikao kile ambao wote
walikuwa kimya kabisa
wakimsikiliza kisha akaendelea
“ Kama nilivyowafahamisha
kwamba ziara hii ya rais wa
Marekani nchini Tanzania ilikuwa
ni kwa sababu maalum zenye
manufaa kwa taifa hilo.Ukiacha
sababu za kiusalama ,kubwa
lililomleta hapa ni suala la mafuta
na gesi.Mtakumbuka awali
niliwaeleza kwamba kwa sasa
Marekani wanapunguza utegemezi
wa mafuta ya mashariki ya kati na
na kuifanya itegemee mafuta yake
ya ndani.Ugunduzi huu wa
kiwango kikubwa cha mafuta na gesi nchini Tanzania umeifanya
Marekani ianze kitolea macho
tanzania nchi ambayo imekuwa
ikipokea misaada mingi toka
Marekani.Katika ziara hii ya rais
wa Marekani kumesainiwa
mikataba kadhaa mikubwa baina
ya serikali ya tanzania na
wawekezaji wakubwa wa mafuta
na gesi toka Marekani.Katika
mikataba hiyo Serikali ya
Tanzania imeyaruhusu
makampuni makubwa ya
marekani kufanya uwekezaji
mkubwa katka sekta ya mafuta
na gesi Tanzania.Hii ina maana
moja kubwa kwamba makampuni
ya kimarekani ndiyo
yatakayoliongoza soko la mafuta
duniani .Marekani haitakuwa tena
na tatizo la mafuta na haitahitaji tena mafuta toka mashariki ya
kati.Washirika wa Marekani pia au
nchi zile kubwa zinazoongoza kwa
viwanda duniani hazitakuwwa
tena na wasi wasi kuhusiana na
suala la mafuta na gesi
,watahamia katika mafuta
yatokayo Tanzania.Bei ya mafuta
duniani itaporomoka na hali hii
itayalazimisha makampuni ya
mafuta ya mashariki ya kati
kupunguza bei ya mafuta ili
kuendana na bei itakayokuwepo
katika soko la dunia.Kushuka kwa
bei ya mafuta kwa nchi za
mashariki ya kati inamaanisha
kwamba hata uchumi wa nchi hizi
lazima utaporomoka kwa sababu
uchumi wao unategemea sana
biashara ya mafuta.Lengo kuu la
Marekani ni kuhakikisha kwamba uchumi wa nchi za mashariki ya
kati unazorota kutokana na
kudorora kwa biashara ya mafuta”
akanyamaza akanywa maji kidogo
kisha akaendelea.
“Nadhani hadi hivi sasa kuna
picha ambayo tayari mmekwisha
ipata kuhusiana na ziara ya rais
wa Mareani” akasema Alhafidhi na
wajumbe wote wakatikisa vichwa
ishara kwamba wanakubaliana
naye.Akatabasamu halafu
akaendelea
“ Suala hili limekuwa
likiumiza vichwa sana
makampuni makubwa ya mafuta
ya masharki ya Kati na hata
serikali zao kwa ujumla.Ni suala
linalohusu maslahi mapana ya
mataifa haya ambayo uchumi
wake unategemea mafuta.Hatutaki makampuni yetu yatetereke
kutokana na kuyumba kwa bei ya
mafuta katika soko la
dunia.Hatutaki uchumi wa
mataifa yetu uzorote kutokana na
kuyumba kwa bei ya mafuta .Vita
vya wenyewe kwa wenyewe katika
eneo zima la mashariki ya kati
vimesababisha chumi za mataifa
haya zilizokuwa zikikua kwa kasi
kuzozorota .Endapo litaatokea
tena baa hilo la kuporomoka kwa
bei ya mafuta mataifa haya
yatakuwa yakichungulia katika
lindi kubwa la umasikini kwani
chumi zao hazitaweza kustawi
kamwe.Ni kutokana na hali hiyo
kumekuwa na mazungumzo ya
kina kati ya serikali za mashariki
ya kati na makampuni makubwa
ya mafuta ya wazawa wa mashiriki ya kati.katika mazungumzo hayo
yote suala la Marekani kuendesha
sekta ya mafuta ya Tanzania
limepingwa vikali.Hatuko tayati na
hatutakuwa tayari kuiacha
Marekani itawale sekta hii nyeti
sana ambayo ndiyo hasa uchumi
wetu sisi watu wa mashariki ya
kati.Narudia tena kwamba hatuko
tayari na wala hatuwakuwa tayari
kuiacha Marekani itawale sekta ya
mafuta ya dunia.Kwa maana hiyo
basi tumefikia uamuzi wa
kuusimamisha na kuuzima kabisa
mpango wa marekani wa
kuidhibiti sekta ya mafuta
duniani.” Alhafidh akatoa
kitambaa na kujifuta jasho halafu
akanywa maji kidogona kuendelea.
“ Serikali ya Tanzania tayari
imekwisha sainiana mikataba mikubwa na makampuni ya
kimarekani na hivyoo suala hilo
kwa sasa lipo kisheria .Hakuna
namna tunayoweza kufanya ili
kutengua mikataba hiyo mikubwa
sana.Kuna njia moja tu ambayo
tunaweza kuifanya ili kulimaliza
suala hili” Alhafidh akanyamaza
na kuziangalia nyuso za wajumbe
waliokuwa kimya
wakimsikiliza.Akanyanyua glasi ya
maji na kupiga funda moja
akaiweka chini akatoa kitambaa
na kujifuta jasho lililokuwa
likimtoka usoni licha ya ukumbi
ule mdogo kuwa na kiyoyozi.Hii
ilitokaa na uzito wa suala
walilokuwa wakiliongelea
“ Ndugu wajumbe njia pekee
ya kuweza kulipatia ufumbuzi suala hili ni kwa kuiangusha
serikali iliyoko madarakani”
Kimya kizito kikatanda mle
ndani.Sura za wajumbe
zilionyesha mabadiliko ya
ghafla.Minong’ono ya chini kwa
chini ikasikika.Mara Daudi
Sichoma akasimama na
kumuelekezea macho Brigedia
Frank huku midomo yake
ikitetemeka
“ What is this Frank? Hiki
ndicho kitu cha muhimu
ulichoniitia? I cant believe this
!!!....akasema Daudi kwa ukali
.wajumbe wengine wanne
wakasimama wakionyesha
kustushwa na kauli ile.Hali
ilibadikika mle chumbani
ikamlazimu Brigedia Frank
asimame. Please calm down
guys.Nawaombeni mtulie na
tusikilizane.Mr David tafadhali
naomba ukae chini na
tusikilizane”akasema Frank na
wale wajumbe waliokuwa
wamesimama wakiongozwa na
Daudi Sichoma wakaketi na
ukimya ukatawala mle ndani
.Frank alipohakikisha wajumbe
wote wametulia kaendelea
“ Ninauona mstuko mkubwa
katika nyuso zenu.Nilitegemea
kitu kama hiki kutokea.Hii si
taarifa nyepesi hata kidogo.Ni
taarifa nzito na yenye kustusha
lakini nyote niliowachagua
kuhudhuria kikao hiki
ninauhakika mkubwa kwamba
hizi ni taarifa njema sana
kwenu.Naomba msiwe na jazba na twende taratibu tutaelewana”
akasema Frank
“Frank kuiangusha serikali si
suala rahisi hata kidogo kama
unavyodhani” akasema David
Sichoma .Frak akatabasamu na
kusema
“ Ninafahamu
unachokimaanisha David lakini
nina uhakika mkubwa hakuna
kitakacho
shindikana.Nime………”kabla
Frank hajaendelea zaidi Daudi
Sichoma akamkatisha
“Frank you know nothing
.Suala ulilolileta ni suala
lisilowezekana kabisa” akasema
Daudi
“ Unaweza kuwa sahihi David
kwamba sijawahi kuwa katika
serikali lakini ninafahamu kila kinachoendelea
serikalini.Ninawafahamu viongozi
wakubwa serikalini.Ninaifahamu
seriali nje na ndani.Daudi
Sichoma ninakufahamu vyema
umewahi kushika nyadhifa
mbalimbali za uongozi serikalini
na hatimaye ukafanikiwa kwa
waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania.Nafahamu
ndoto yako kubwa ilikuwa ni kuwa
rais wa Tanzania lakini kwa bahati
mbaya ndoto yako hiyo
haikuwezekana kutimia kwa
sababu watu ndani ya serikali
waliligundua hilo na hawakuwa
tayari kukuona ukishika nafasi ya
urais na ndiyo maana walianza
kukuandama kwa mambo mengi
na hatimaye kukuzushia kashfa
kubwa na ukaondolewa katika nafasi yako ya uwaziri
mkuu.Ninafahamu madai yale
yaliyotolewa dhidi yako kuhusiana
na kashfa ile hayakuwa ya kweli
na zilikuwa ni njama za kisisasa
na kuhakikisha unapotea kabisa
katika ulingo wa siasa.Lengo lao
limefanikiwa kwani wamefanikiwa
kabisa kukuondoa katika ulingo
wa siasa.Hausikiki tena viywani
mwa watu.Umekwisha sahaulika
kabisa na ndoto yako ya urais
imepotea.Najua unajitahidi sana
kutaka kujirudisha katika medani
za siasa lakini wabaya wako
hawataki kukupa tena
nafasi.Vikwazo vimekuwa vingi na
wamepambana hadi kuhakikisha
kwamba umaarufu wako
unapotea.This is your last chacne
to make your dream come true.Ni wakati wako wa kuitengeneza njia
ya kuingia katika lile jumba
jeupe.” Frank akanyamaza
akamtazama Daudi Sichoma
aliyekuwa kimya akimsikiliza
halafu akawageukia wajumbe
wengine
“Nyote niliowaita hapa
nafahamu ni wenye kuhitaji sana
nafasi za uongozi na mpango huu
wa kuiangusha serikali ndio
mpango pekee utakaowawezesha
na kuwahakikishia nafasi za
uongozi.Kuiangusha serikali
iliyoko madarakani ni jambo zito
ambalo haliwezi kufanywa na sisi
pekee yetuliomo humu chumbani
.Huu ni mchakato mrefu na
jumuishi nikimaanisha kwamba ni
mchakato unaohusisha watu
wengi lakini wenye lengo na nia moja.Sisi sote tulioko hapa ndio
tutakaoratibu mchakato mzima wa
mapinduzi haya.Naombeni ndugu
zangu msikate tamaa.Tunaweza
kulifanya jambo hili.Mkumbuke
pia tunayo sapoti ya kutosha toka
kwa washirika wetu katika suala
hili.Tayari zimekwisha tengwa
shilingi Trilioni sita kwa ajili tu ya
kufanikisha jambo hili.Pamoja na
fedha lakini washirika wetu
watatusaidia pia katika ila kitu
tunachokihitaji”akasema Frank na
kunyamaza tena akawatazama
wajumbe wale.daudi sichoma
akakohoa kidogo na kusema
“ Kidogo sasa ninaanza
kukuelewa Frank.Mpango huu si
mbaya kama nilivyokuwa
ninaufukiria isipokuwa ni mpango
mzito wenye kuhitaji mikakati mizito pia .Lazima tuvihusishe
vyombo vya ulinzi na usalama
hususani jeshi na idara ya
usalama wa taifa,wanasiasa na
wadau wengine watakaoonekana
kuhitajika.Mimi niko tayari
kushirikiana nanyi katika mpango
huu lakini kwa makubaliano
maalum” akasema Daudi Sichoma
“ Ahsante sana Daud kwa
maamuzi yako .Kwa kuwa bado
tuna mchakato mrefu mbele yetu
nina imani kwamba tutafikia
makubaliano unayohitaji”
akasema Frank na kuwageukia
wajumbe wengine
“ Ndugu zangu kati yenu
kuna yeyote mwenye mawazo
tofauti? Kuna yeyote mwenye
duku duku au maoni yoyote
kuhusiana na mpango huu? Akauliza Frank.Kabla mtu yeyote
hajajibu,simu ya Frank
ikaita,akastuka baada ya kuona
watu wote wanamtazama
“ Samahani ndugu zangu
kwa kutoizima simu yangu katika
kikao kizito kama hiki” akasema
Frank huku akitoa simu yake kwa
lengo la kuizima lakini mara tu
alipotazama jina la mpigaji
akastuka.Jina lilisomeka kama
hospitali Graca
“ Samahani jamani naomba
niipokee simu hii ni muhimu
sana” akasema Frank na kutoka
nje ya kile chumba
“Hallow” akasema Frank
“ Hallow Frank habari za Dar
es salaam? Ikasema sauti ya
upande wa pili
 
Good job bro [emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 23

wapi ilipo kompyuta yake.Elvis
naomba usiniache hapa.take me
anywhere safe.Ni mara yanguya
kwanza kukuona lakini I feel safe
around.macho yako yananifanya
nikuamini” akasema Graca huku
macho yake yakilengwa na
machozi
“ Nitakusaidia
Graca.Nitakuondoa hapa na
kukupeleka sehemu salama
kabisa ambako si baba yako wala
yeyote anayekutafuta
atakupata.Lakini kabla ya kufanya
hivyo kuna jambo nataka
kulifahamu toka kwako.Nataka
kufahamu ndani ya hilo begi
kulikuwa na kitu gani cha
muhimu kiasi cha kupelekea
baba yako kufanya haya yote
aliyoyafanya?Kompyuta hiyo uliyoichukua ilikuwa na jambo
gani na iko wapi kwa sasa?
Graca akamtazama Elvis na
kusema
“Siwezi kukueleza chochote
kwa sasa hivi hadi hapo
nitakapohakikisha kwamba niko
sehemu salama.Take me
somewhere safe and I will tell you
everythingI know na nitakueleza
kompyuta hiyo iko wapi” akasema
Graca
“ Graca ninaelewa hofu yako
lakini naomba uniamini na
uniambie kuhusiana na
ulichokigunuda kwa baba
yako.Tafadhali naomba
ushirikiane nani.Usiniogope mimi
si mtu mbaya” akasema Elvis
“ Elvis najua umefunga safari
ndefu kuja huku kuonana na mimi kwa nia njema kabisa na
kama nilivyokueleza awali kwamba
ninakuamini na niko tayari
kukueleza kila kitu lakini kwa
sasa siwezi kukueleza jambo lolote
ninalolifahamu hadi hapo
nitakapohakikisha kwamba niko
salama.Mkoba ule na kilichomo
ndani yake ndiyo kinga yangu kwa
sasa kwa hiyo fanya
nilivyokuelekeza na nitakueleza
kila unachokitaka” akasema Graca
“ Graca !!... Elvis akataka
kusema kitu lakini Graca
akamzuia
“ Elvis hakuna chochote
utakachoniambia kitakachoweza
kuubadili msimamo wangu.Ninazo
taarifa nyeti sana ambazo
ninaamini zitakuwa ni za msaada
mkubwa sana kwako lakini siwezi kukueleza hadi hapo
nitakapohakikisha kwamba niko
salama” akasemaGraca.Elvis
akamtazama kwa makini usoni na
kuamini kile alichokisema Graca
“ She’s telling the
truth.hawezi kunieleza chochote
bila kufanya anavyotaka” akawaza
Elvis na kusema
“Nimekuelewa
Graca.Naomba unipe muda
kidogo niangalie namna ya
kufanya.I promise you I’ll get
you out of here.”akasema
Elvis.Bila kusema chochote
Graca akainuka na kutembea
taratibu kuelekea ndani.Elvis
akamtazama namna
alivyokuwa akitembea kwa
unyonge akamuonea huruma
sana lazima nimsaidie.Siwezi
kumuacha hapa akiendelea
kuteseka.Akawaza Elvis
halafu akaelekea katika meza
waliyokuwa wamekaa Bongan
na Dr Susan
“ Tayari mmekwisha
ongea? Umefanikiwa kupata
ulichokuwa unakihitaji? Akauliza
Bongani
“ Bongani mambo si rahisi
kama nilivyitegemea" akasema
Elvis
“ Nini kimetokea Elvis,Graca
hajakupa ushirikiano? ” akauliza
Bongani.Elvis akamvuta pembeni
kidogo ili waongee.Akamweleza
kila kitu alichoongea na Graca
“kwa hiyo mambo yako
namna hiyo Bongani.Graca kuna
jambo kubwa analifahamu kuhusiana na baba yake lakini
hayuko tayari kuliweka wazi bila
kwanza kuwa na uhakika wa
usalama wa maisha yake”
akasemaElvis
“ kwa hiyo tutafanya nini
Elvis ili tuweze kuzipata taarifa
hizo toka kwa Graca?akauliza
Bongani
“hakuna njia nyingine ya
kufanya zaidi ya kufanya vile
anavyotaka yaani kumpeleka
sehemu salama.Bongani naomba
unisaidie katika hili ili niweze
kumuondoa Graca hapa
hospitali.Pamoja na kuwa na kitu
cha muhimu ninachokihitaji lakini
nimeguswa sana na mateso ya
binti huyu,ameteseka kiasi cha
kutosha na siko tayari kumuacha akiendelea kuteseka
hapa.Tafadhali naomba unisaidie”
Bongani akafikiri kwa muda
na kusema
“ Hata mimi nimeguswa sana
na histora ya huyu binti na
nitakusaidia ili tuweze kumtoa
hapa.Ninachotaka kufahamu ni
kuhusu usalama wa maisha yake
endapo tutafanikiwa kumuondoa
hapa.Una hakika atakuwa
salama?akauliza Bongani.Elvis
akawaza kidogo na kusema
“Bongani suala la usalama wa
Graca lina changamoto nyingi
lakini hilo ni jukumu langu
ambalo sina budi kulibeba na
nitahakikisha kwamba anakuwa
salama.Nitamlinda dhidi ya yeyote
mwenye nia ya kumdhuru” “Bongani akainama akafikri
kidogo na kusema
“ sawa Elvis
.Nitakusaidia,naomba unipe muda
wa dakika kama kumi nikaongee
na Dr Susan nione kama anaweza
akatusaidia”
“ una hakika atatusaidia?
Akauliza Elvis
“ Nina uhakika lakini hatuna
budi kujaribu.Nina mahusiano
naye mazuri.Tuliwahi kuwa katika
mahusiano ya kimapenzi wakati
tukiwa chuo kikuu na mpaka sasa
bado tuna mahusiano mazuri”
akasema Bongani na kuelekea
katika ofisi ya Dr Susan
“Nahisi kuna suala zito sana
ambalo liko nyuma ya pazia kiasi
kwamba Frank alikuwa tayari hata
kutaka kumuua mwanae kwa ajili ya kulificha.Lazima nilifahamu
suala hilo .Nitamsaidia Graca kwa
namna yoyote ile nitakayoweza na
nitamuondoa hapa.Nitamlinda
dhidi ya yeyote yule anayetishia
maisha yake.”akawaza Elvis
Bongani alitumia zaidi ya
dakika kumi na tano kuongea na
Dr Susan kumuelezea kuhusiana
na tatizo la Graca.Hadi anamaliza
kumueleza Dr Susan alikuwa
anahisi baridi.Alionekana kuzama
katika mawazo mengi
“ Siku zote nilijua lazima
kuna jambo haliko sawa kwa
Graca.Sikutaka kuharakisha
kumuuliza nini kilichokuwa
kinamsumbua na ndiyo maana
nikajenga ukaribu mkubwa kati
yangu naye ili siku moja aweze
kunieleza tatizo lake.Namuoenea huruma sana binti huyu kwa
mateso makubwa aliyonayo.Huu
ni mtihani mkubwa kwangu lakini
lazim animsaidie” Dr Susan akiwa
katika mawazo mengi mara
akastuliwa na Bongani
“ Dr Susan !!...
Akainua kichwa na kumtazama
Bongani
“Unasemaje Bongan? Akauliza
“ natumani umenisikia na
kunielewa.Nini mawazo yako?
Akaulizia Bongani .Dr Susan
akavuta pumzi ndefu na kusema
“Bongani nashindwa niseme
nini lakini naomba nikiri kwamba
nimegswa mno na historia nzima
ya Graca.Siku zote nilikuwa
nikifahamu kwamba Graca ana
tatizo kubwa linalomsumbua
tofauti na ugonjwa wa akili lakini sikuweza kumshawishi anieleze
tatizo lake.Maelezo uliyonipa
yamenistua mno”akasema Dr
Susan
“ Dr Susna sote tumeguswa
na tatizo la Graca na ndiyo maana
tunatafuta namna ya kumsaidia
na mtu pekee ambaye
tunamtegemea kwa sasa ni wewe”
akasema Bongani .Dr Susan
akaonekana kuzama mawazoni
halafu akakohoa kidogo na
kusema
“ Una hakika kwamba Elvis
ana nia ya dhati kumsaidia Graca
na si mmoja wa watu wa baba
yake ambaye anataka kumchukua
na kwenda kumdhuru?
Bongani akatabasamu na
kusemaElvis anafanya kazi kama
ninayofanya mimi na lengo lake ni
kumsaidia Graca hivyo nakuomba
usiwe na hofu naye hata kdogo”
akasema Bongani.Dr Susan
akaegemea kti chake akatazama
juu kwa sekunde kadhaa na
kusema
“ Nitamsaidia.Ninakuamini
sana na nina hakika baada ya
kutoka hapa Graca atakuwa
katika mikono salama”
“ Ahsante sana Dr Susan
.Ahsante sana kwa msaada wako”
akasema Bongani kwa furaha.
“Tutafanya hivi.Graca
nitaondoka naye mimi katika gari
langu.Hataondoka na kitu
chochote hapa kila kitu chake
atakiacha hapa ili kutoleta udadisi
pindi itakapobainika kwambaametoweka.Baada ya kama dakika
kumi nitakapoondoka ninyi
mtafuata kwa nyuma.Nitawasubiri
pale kwa Pamela
Thambo”akasemaDr Susna
naBongani akatoka mle ofisini kwa
Dr Susan akamfuata Elvis
“ What happened? amekubali
kutusuaidia?akauliza Elvis kwa
wai wasi mara tu alipomuona
Bongani
“ Ndiyo! Amekubali
kutusaidia” akasema Bongani
“ Thank you Lord! Akasema
Elvis huku akiinua mikono
kumshukuru Mungu.Bongani
akamueleza Elvis namna mpango
utakavyokuwa kisha wakaelekea
katika kantini ya hospitali hapo
wakaagiza vinywaji baridi.Wakati
wakiendelea na vinwyaji mara ikapita gari ya Dr Susan
ikafunguliwa geti na kutoka bila
kukaguliwa . Dakika kumi baada
ya Dr Susan kutoka Bongani na
Elvis nao wakaelekea lilipo gari
lao,wakaingia na kuondoka.Katika
lango kuu walikaguliwa na
kuruhusiwa kupita wakaondoka.
******************
Katika nyumba kubwa
iliyokuwa na utulivu
mkubwa,Bongani ,Elvis na Graca
walikuwa wamekaa wakijaribu
kuangalia ni kwa namna gani
Elvis na Graca watakavyoweza
kurejea Tanzania salama.Graca
alionekana mchovu sana hali
iliyomlazimu alale sofani na kuwaacha Bongani na Elvis
wakiendelea kujadiliana
“ Kuna njia nyingi za kuweza
kuwaondoa hapa na kuwarudisha
Tanzania lakini tunahitaji kupata
usafiri wa haraka wa kuweza
kuwaondoa hapa leo hii
.Hamtakiwi kulala hapa leo”
akasema Bongani
“ Hilo ni jambo la msingi sana
.Kwa hali ilivyo hatutakiwi kulala
hapa leo.Tutawezaje basi kupata
usafiri wa haraka wa kutuondoa
hapa? “ akauliza Elvis .Bongani
akainama akafikiri kidogo na
kusema
“ Usihofu kuhusu suala hilo
Elvis.Ni jukumu langu
kuhakikisha kwamba unapata
usafiri na unaondoka hapa
salama.Ngoja kwanza niwasiliane na washirika wangu kadhaa nione
namna watakavyoweza kunisaidia”
akasema Bongani kisha akainuka
na kuelekea chumbani .Elvis
akamtazama Graca aliyekuwa
amelala sofani .Graca akageuza
shingo na kugonganisha macho na
Elvis ,akatabasamu kidogo na kwa
sauti ndogo akauliza
“ Mbona unanitazama hivyo?
Elvis akainuka na kwenda kukaa
katika sofa lililokuwa pembeni ya
Graca
“ Unajisikiaje Graca?
Akauliza
“ Ninajisikia vizuri tu.Ni yale
madawa waliyokuwa wakinichoma
ndiyo yanayonifanya nionekane
naumwa sana lakini mimi siumwi”
akasema Pole sana Graca.Kuna kitu
chochote unahitaji kwa sasa?
“Elvis Kwa sasa Ninachohitaji
ni kwenda sehemu salama”
“ Usihofu Graca.Nimeibeba
dhamana hiyo ya usalama wako
na nitahakikisha unakuwa salama
na hakuna atakayekudhuru”
“ Nitashukuru sana kwa hilo
Elvis….” Akasema Graca na mara
Bongani akaingia pale sebuleni
“ Vipi kuna mafanikio yoyote ?
akauliza Elvis
“ Ndiyo.Kunaweza kuwa na
uwezekano.Nimewasiliana na
mmoja wa rafiki zangu
amenidokeza kwamba kuna ndege
ya jeshi inaondoka usiku wa leo
kuelekea Zambia.Nimewasiliana
na mmoja wa makamanda wa
jeshi amenitaka nionane naye sasa hivi.Ngoja nikaonane naye
nimsikilize ni mtu ambaye nina
hakika anaweza akanisaidia”
akasema Bongani
“ Ahsante sana Bongani kwa
msaada wako huu
mkubwa.Ninaomba Mungu
ufanikiwe ili tuweze kuondoka
hapa” akasema Elvis
“ Usihofu Elvis.Ngoja
nikaonane na huyu mkuu
nitarejea baada ya muda mfupi”
akasema Bongani na kutoka.
“ Huyu rafiki yako ana roho
nzuri sana.Ni nadra sana katika
dunia ya sasa kumpata mtu
ambaye anaweza akakuhangaikia
kama huyu.” Akasema Graca
baada ya Bongani kuondoka.Elvis
akatabasamu na kusema Anaitwa Bongani.Naye
anafanya kazi kama ninayoifanya
mimi na vile vile ni rafiki yangu
sana.Ni jadi yetu kusaidiana
tunapokuwa na matatizo na hata
yeye akija Tanzania na akiwa na
tatizo ni jukumu langu
kuhakiksha kwamba nimemsaidia
kwa kila namna.Hivyo ndivyo
tunavyofanya kazi” akasema Elvis
“ Natamani na mimi siku
moja ningefanya kazi kama yako”
akasema Graca
“ Unaipenda kazi hii?
Akauliza Elvis
“ Ndiyo nimetokea kuipenda
sana” akasema Graca
“ Kwa nini unaipenda kazi
hii?
“ Mambo yaliyonikuta ndiyo
yananifanya niipende na na nitake kufanya kazi kama yako.Nataka
nipambane na watu makatili wasio
na hata chembe ya huruma kwa
binadamu wenzao.Vile vile nataka
nilipe kisasi kwa baba yangu
pamoja na washirika wake kwa
kusababisha maisha yangu yawe
namna hii.Unawezaje kunisaidia ili
niweze kuifanya kazi hii? akauliza
Graca
Elvis akavuta pumzi ndefu
akamtazama Graca ambaye
hakuonyesha kama alikua
akitania
“ Graca naomba unisikilize
mdogo wangu .Kwanza kabisa
naomba ufahamu kwamba kuna
maisha mazuri zaidi
yanayokusubiri pale utakapokuwa
huru na unastahili maisha
mazuri.Umri wako bado unaruhusu wewe kuendelea na
masomo na baadae ukaishi
maisha yale ambayo umekuwa
ukiyaota kwa siku nyingi hivyo
naomba uondoe kabisa kichwani
mwako wazo la kutaka kufanya
kazi kama hii.Kazi hii ni ngumu
mno na ina mambo mazito ndani
yake .Inahitaji mtu mwenye roho
ngumu kama ya paka.Mara tu
uingiapo katika kazi hii hutakuwa
na maisha ya kawaida tena kwani
muda wote unakuwa
umezungukwa na maadui ambao
dhamira zao si njema hata kidogo
na walio tayari kuua muda wowote
.Kazi hii inakuweka katika hatari
muda wote.Wengi wetu tumeingia
katika kazi hii bila kufahamu
tunakwenda kukutana na mambo
gani na kwa sasa tumekwisha zoea na kuiona ni ya kawaida lakini
naomba nikuhakikishie kwamba
hii si kazi rahisi kuifanya na wala
usiitamani.Niko tayati kukusaidia
kwa kila namna niwezavyo
kuyajenga maisha yao lakini si
kukusaidia ili uingie katika kazi
hii.Umenielewa Graca? Akaulizia
Elvis
“ Nimekuelewa Elvis japokuwa
bado moyo wangu unataka sana
kuifanya kazi hii ili niweze
kuufutilia mbali mtandao wote wa
baba” akasema Graca na kuzidi
kumvutia zaidi Elvis
“ Mtandao upi Graca? Baba
yako ana mtandao
unaoshughulika na nini? Akauliza
Elvis
“ Usiwe na haraka
Elvis.Utafahamu kila kitu ila naomba ufuate makubaliano yetu
.Nipeleke sehemu salama na
nitakueleza kila kitu
ninachokifahamu” akasema Graca
“ Sawa nitahakikisha
unakuwa salama.Ninahitaji sana
taarifa zako”
“ Usijali Elvis,nitakueleza kila
kitu,” akasema Graca halafu
ghafla akaonekana kama kuna
kitu anakiwaza
“ Elvis kuna kitu ambacho
nilisahau kukwambia”
“ Kitu gani Graca?
“ Kuna watu wawili pale
hospitali wamekuwa
wakinichunguza.Kuna mpishi
mmoja pamoja na mlinzi.Watu
hawa wamekuwa wakinifuatilia
sana na nina hakika watakuwa
wanalipwa na baba ili wanichunguze nyendo
zangu.Japokuwa sina hakika sana
lakini kwa namna walivyokuwa
wakinifuatilia nina hisi lazima
watakuwa wamepewa kazi ya
kunichunguza” akasema Graca
“ Usijali kuhusu hao
watu.Hata kama wamewekwa na
baba yako kukuchunguza hawana
uwezo wa kupambana na
mimi.Usihofu kitu ukiwa na mimi”
akasema Elvis
“ Ahsante sana Elvis”
akasema Graca na kimya kifupi
kikapita
Ilipita saa moja na dakika ishirini
Bongani akarejea
“ Hallow Elvis.Mko salama
wote?
“ Tuko salama.Mambo
yamekwendaje huko? Mambo yamekwenda vizuri
sana .Kuna ndege ya jeshi
inayowapeleka wanajeshi kwenye
mazoezi nchini Zambia na tayari
nimekwisha ongea na kiongozi wa
kikosi hicho na amenikubalia
kuwachukua na ninyi.Hakukuwa
na ugumu wowote kwani wakuu
wengi wa jeshi ni marafiki
zangu.Pale Lusaka nimekwisha
wasiliana na mtu mmoja anaitwa
Stanley Chiteta.Huyu ni rafiki
yangu mkubwa na ni mfanyakazi
wa idara ya usalama wa taifa ya
Zambia.Yeye ndiye
atakayewapeleka hadi katika
mpaka wa Tanzania na Zambia
katika mji wa Tunduma na tokea
pale hamtakuwa na wasi wasi tena
mtakuwa mmekwisha ingia nchini
kwenu na mtatafuta usafiri wa kuelekea Dar es salaam.Stanley ni
mzoefu na nina hakika atakuwa ni
msaada mkubwa kwenu” akasema
Bongani
“ Bongani sina namna ya
kukushukuru kwa msaada wako
huu mkubwa uliotusaidia.”
Akasema Elvis .Bongani
akatabasamu na kusema
“ Usijali Elvis ni jukumu
langu kukusaidia na nimefanya
kile ninachopaswa kukifanya .Kwa
kuwa hatuna muda wa kutosha ni
wakati sasa wa kujiandaa kwa
safari.” Akasema Bongani na
kumpatia Graca mfuko uliokuwa
na nguo na vitu vingine mbali
mbali alivyomnunulia.Graca
akaingia chumbani kujiandaa na
baada ya kuwa tayari safari ya kuelekea uwaja wa ndege wa jeshi
ikaanza
DAR ES SALAAM – TANZANIA
Ni saa moja za jioni ,kiza
tayari kimetanda angani,Patricia
na Doreen rafiki yake wamekaa
katika kibaraza nyumbani kwa
Doreen wakiongea.Walionekana
kuzama katika maongezi mazito
“ Kwa hiyo Doreen maisha
yangu yanazidi kuwa magumu
siku hadi siku.Umeona wewe
mwenyewe ujumbe ninaotumiwa
katika simu na ndugu za
Elvis.Wanayafanya maisha yangu
yawe magumu sana.Hakuna mtu
anayejali upendo mkubwa uliopo
kati yangu na Elvis.Wao
wanachotaka ni mtoto tu” akasema Patricia kwa
uchungu.Doreen akamtazama
akamuonea huruma rafiki yake
“ Pole sana Patricia
.Ninafahamu ni kiasi gani
unaumizwa na suala hili na kama
nilivyokueleza toka awali kwamba
niko tayari kukusaidia katika
jambo hili.Sipendi kukuona
ukiumia namna hii” Akasema
Doreen
“ Doreen nashukuru sana
kwa kukubali kunisaidia ingawa
najua haikuwa rahisi kukubali
kufanya jambo kama hili lakini
tutafanya nini tena wakati mpango
wetu ulishindikana? Akasema
Patricia .Kimya kikatanda kila
mmoja alikuwa anawaza lake.Ni
Doreen ndiye aliyeuvunja ukimya Patricia naomba usikate
tamaa ndugu yangu. Ni kweli
tulijaribu ikashindikana lakini
hatupaswi kukata tamaa
.Tunapaswa kufikiri namna
nyingine tutakayoweza kufanya ili
kumfanya Elvis akubaliane na
wazo letu” akasema Doreen
“ Doreen unionavyo hapa
tayari nimekwisha fikiri sana na
ninatumai akili yangu imefikia
kiwango chake cha mwisho cha
kufikiri na bado sijapata jibu”
akasema kwa uchungu
Patricia.Doreen akamshika bega
na kumwambia
“ Patricia its too early to give
up.Nina hakika lazima tutapata
njia ya kufanya .Kitu cha msingi
ni kujaribu kutuliza akili na kuja na mpango mpya.Nina hakika
tutafanikiwa “ akasema Doreen
“ Doreen sina shaka nawe
hata kidogo najua uko tayari
kunisadia lakini tatizo liko kwa
Elvis.Ananipenda kupindukia na
hayuko tayari kufanya jambo
kama hili tunalolipanga.Suala la
kumuomba azae na mwanamke
mwingine kwake yeye ni sawa na
usaliti kwangu kwa hiyo hataki
kabisa
kulisikia.Nimechanganyikiwa
Doreen na sijui tutafanya nini na
ndugu za Elvis ndo hao wanadai
mtoto kila leo” akasema Patricia
“ Unaonaje endapo tutakaa
naye na kuongea naye kwa pamoja
kuhusiana na suala hili pengine
anaweza akatuelewa” Akasema
Doreen Elvis ni mtu mwenye
msimamo mkali sana na akisema
hapana katika jambo Fulani basi
huwa ni vigumu sana
kumbadili.Sina hakika kama hata
tukimueleza ukweli anaweza
akatuelewa.Mpango ule
ulioshindikana ulikuwa mzuri
sana” akasema Patricia
“ Pamoja na hayo Patricia ni
mapema mno kukata tamaa.Bado
kuna njia nyingi tu tunaweza
kufanya ili kumfanya Elvis
akubaliane nasi” Akasema Doreen
Patricia akamtazama na
kuonyesha wasi wasi
“ Unazungumzia njia gani
Doreen? Kama unazungumzia
masuala ya waganga mimi siko
tayari kwa hilo.Ni bora niendelee kuteseka kuliko kwenda kwa
waganga”
Doreen akacheka na kusema
“ Hapana Patricia.Mimi si
muumini wa masuala hayo na
tangu utoto wangu siamini kabisa
katika mambo hayo ya
waganga.Nilikuwa namaanisha
kutafuta njia nyingine za kuweza
kulifanikisha jambo hili hata kama
Elvis hataki kuliko kukata tamaa”
akasema Doreen
“ Hilo ndilo jambo la msingi
ambao tunapaswa kulifanya kwa
sasa.Ngoja kwanza niende
nikapumzishe kichwa ili nije na
wazo jipya.” Akasema Patricia
huku akinyanyua mkoba wake na
kupiga hatua kuelekea lilipo gari
lake Sikuwahi kuota kama siku
moja nitakuwa na wakati mgumu
kama nilionao hivi sasa. Kuna
wakati ninajuta hata kuolewa
.Ningekuwa peke yangu haya yote
yasingenitokea.Anyaway
ninampenda Elvis na nitalipigania
penzi letu kwa gharama zozote
zile” akawaza Patricia
********************
Ni shamba lenye ekari zaidi ya
kumi lililoko njekidogo ya jiji la dar
es salaam.Ndani ya shamba hilo
lililosheheni mazao mbalimbali
kulikuwa pia na mifugo kama vile
kuku,ng’ombe n.k.Kati kati ya
shamba lile kuwa kulikuwa na
jumba kubwa la kifahari la ghorofa
tatu.Hili ni shamba linalomilikiwa na Brigedia jenerali Frank
kwaju.Jioni hii ukimya mzito
ulitawala kulizunguka jumba
hili.Ni milio ya mifugo tu ndiyo
iliyokuwa ikisikika .Hakukuwa na
zile pita pita za kila siku za
wafanyakazi
Saa mbili na dakika tatu za
usiku,gari tatu zikawasili katika
geti la kuingilia shambani
hapo.Geti kubwa likafunguliwa na
walinzi na kisha gari zile
zikaikamata barabara iliyokuwa
inaelekea moja kwa moja katikati
ya shamba liliko jumba lile kubwa
lililozungukwa na ukuta mkubwa
na nyaya za umeme juu yake.Geti
likafunguliwa na gari zikaingia
Watu kumi wakashuka toka
katika zile gari wakiongozwa na
Brigedia jenereli Frank halafu wakalekea ndani katika ukumhi
wa siri wa mikutano ulioko ndani
ya jumba lile.Ukumbi tayari
ulikwisha andaliwa maalum kwa
ajili ya kikao hiki kizito
kinachotaratiwa kufanyika usiku
huu.Baada ya kama dakika
ishirini toka akina Frank wawasili
pale numbani,zikawasili gari mbili
na akashuka waziri mkuu mstaafu
Daud Sichoma akiwa
ameongozana na watu wengine
watano wakapokelewa na Brigedia
Frank na kupelekwa katika
ukumbi wa mikutano ambako
wajumbe wote waliokuwa
wakitakiwa katika kikao kile
walikwisha wasili na aliyekuwa
akisubiriwa ni Mheshimiwa Daudi
Sichoma na ujumbe wake.Mara tu
walipoingia katika chumba cha mikutano,watu wote wakasimama
kuonyesha heshima kwa wgeni
waliowasili.Daudi na ujumbe wake
wakaonyeshwa viti wakaketi na
bila kupoteza wakati mwenyekiti
wa kikao kile brigedia Frank
akafungua kikao.Kwanza alianza
kwa kufanya utambulisho.Baada
ya wajumbe kufahamiana kwa
majina na sehemu watokako
Frank akaendelea
“ Ndugu wajumbe nadhani ni
wakati sasa wa kuwatambulisha
wageni wetu wakuu waliotufanya
tukusanyike hapa usiki
huu.Wageni wetu watasimama na
kujitambulisha wao ni akina nani
na kisha tutaendelea na kile
kilichotuleta” akasema Frank na
kuwaomba wageni wale wawili wasimame mmoja mmoja na
kujitambulisha
“ naitwa Mustapha Al
jamal”akaanza kujitambulisha
mgeni wa kwanza
“ Mimi ni raia wa Iran na ni
mmiliki wa wa kampuni moja
kubwa ya mafuta katika
mashariki ya kati.Kwa sababu za
kiusalaam naomba nisiitaje
kampuni yangu hadi hapo
mbeleni” akamaliza
kujitambulisha ndugu Mustapha
na kumpa nafasi mwenzake
aliyeambatana naye
“ Mimi naitwa Alhafidh
Sadiq.Na mimi kama mwenzangu
aliyetangulia ni mmiliki wa
kampuni kadhaa kubwa za mafuta
katika eneo la mashariki ya
kati.Vile vile kama alivyofanya mwenzangu nisingependa na mimi
kuziweka wazi kampuni zangu”
akasema Alhafidh
“ Ahsanteni sana wageni wetu
kwa kujitambulisha.Sisi ni
wenzenu na tumefurahi sana
kuwa nanyi hapa kwa usiku
huu”akasema Frank akameza
mate na kuendelea
“ Ndugu wajumbe baada ya
kuwafahamu wagheni wetu
naomba sasa tuendelee na kikao
chetu.” Akanyamaza kidogo halafu
akaendelea
“ Wageni wetu hawa
wamekuja na jambo zito sana
ambalo utekelezaji wake
unatuhitaji sana sisi.Endapo
jambo hili likifanikiwa basi sisi
sote pamoja wao tutafaidika
sana.Kwa hiyo basi sitaki kuchukua muda mwingi kwani
muongeaji mkuu yupo na ndiye
atakayetueleza kila kitu.Karibu
ndugu Alhafidh ili uweze kutueleza
nini hasa kilichowaleta hapa
Tanzania” akasema Frank.Alhafidh
akaweka sawa koo lake akafungua
faili lililokuwa mbele yake
akaisoma karatasi ya kwanza kana
kwamba kuna mambo
anajikumbusha halafu akasema
“ Ndugu zangu ni furaha
kubwa kwetu kukutana nanyi
usiku huu.Kwa niaba ya
mwenzangu napenda kuchukua
nafasi hii kuwashukuru nyote kwa
kuacha shughuli zenu na kuja
kutusikiliza.Napenda
kuwahakikishia kwamba
hamtajutia kufika kwenu hapa
usiku huu kwani suala tulilowaitia hapa ni lenye manufaa makubwa
kwenu na kwetu pia.Brigedia
jeneral Frank ni rafiki yangu sana
wa muda mrefu.Tumefahamiana
katika shughuli zetu za kibiashara
na ninyi nyote aliowachagua
kuhuddhuria kikao hiki nina
imani ni watu makini na
anaowaakini hivyo natumaini
mazungumzo yetu yatakwenda
vizuri” Alhafidh akanyamza kidogo
akameza mate na kuendelea
“ Nadhani ninyi nyote hapa
mnafahamu hali halisi ya eneo
zima la masharaiki ya kati
inavyoendelea hivi sasa.Katika kila
taarifa ya habari inayotangazwa
duniani hakukosekani taarifa
kuhusiana na mashariki ya
kati.Lakini nini hasa kiini cha
machafuko yote katika eneo hili la mashariki ya kati?.Chanzo chote
cha machafuko ni nchi za
Marekani na washirika wake.Nchi
hizi za magharibi zimekuwa
zikiendesha chochoko dhidi ya
serikali za mashariki ya kati na
hivyo kusababisha machafuko
kusambaa katika eneo zima la
masharikiya kati.Lakini naomba
nyote mjiulize kwa nini mashariki
ya kati? Kwa nini nchi za
magharibi zinachochea migogoro
na mifarakano mashariki ya kati?
Jibu hapa ni jepesi sana.Ni kwa
sababu ya utajiri mkubwa wa
mafuta ulioko katika eneo
hili.Migogoro hii inapotokea
wanaofaidika ni Marekani na
washirika wake kwani hujitokeza
na kuingilia kati huku wakibeba
na kujiwekea akiba kubwa ya mafuta katika nchi zao huku
wakiwaacha maelfu ya watu wasio
na hatia wakiuana.Suala hili
limeamsha hasira na chuki kubwa
dhidi ya marekani na washirika
wake na ndiyo maana mnasikia
kila mara vinaibuka vikundi
mbalimbali vya kigaidi ambavo
vingi adui yake mkubwa ni
Marekani na washirika wake.Hii ni
sababu kubwa iliyopeleka
Marekani kuanza kujitoa taratibu
katika siasa za mashariki ya kati
na kuanza kupunguza utegemezi
wa mafuta toka mashariki ya kati
.Kwa hivi sasa marekani
imeongeza juhudi katika kuzalisha
mafuta ya ndani ikiwemo mafuta
yatokanayo na mimea
.Wamewekeza katika teknolojia
mpya ili watengeneze magari na mitambo visivyohitaji mafuta
mengi.” Alhafidh akanyamaza
kidogo halafu akaendelea.
“ Baada ya utafiti wa miaka
mingi kuhusiana na uwepo wa
mafuta na gesi katika bahari kuu
nchini Tanzania na kulitolewa
taarifa iliyoushangaza
ulimwengu.Kumegunduliwa kiasi
kikubwa cha mafuta nchini
Tanzania ambacho kinasemekena
ni kikubwa kuliko hata
kilekinachoweza kupatikaana eneo
zima la mashariki ya kati.Huu ni
ugunduzi mkubwa sana kuwahi
kufanyika katika miaka ya hivi
karibuni.Ugunduzi huu unaifanya
Tanzania kuingia katika
ulimwengu mpya kwani mataifa
yote makubwa hivi sasa
yameelekeza macho yao nchini Tanzania.Uchumi wa Tanzania
utapaa kwa kasi kubwa na ndani
ya muda mfupi ujao nchi yenu
itaingia katika nchi tajiri duniani”
Alhafidh akatulia na kuwatazama
wajumbe ambao wote walikuwa
wakitabasamu kutokana na taarifa
ile
“ Rais wa marekani
amemaliza ziara ya siku nne
nchini Tanzania ikiwa ni ziara
ndefu kuwahi kufanywa na rais
wa marekani katika taifa moja
husan haya ya bara la
Afrika.Ninathubutu kusema
kwamba hii imekua ni ziara yenye
mafanikio makubwa sana kwa
marekani.Mambomengi mazuri
yamefanyika katika ziara hiyo
ikiwa ni pamoja na kuzindua
miradi mikubwa ya nishati ,reli na maji,Pamoja na mambo hayo
makubwa huku watanzania walio
wengi wanaamni ni neema kubwa
wameipata lakini nataka mjiulize
kwa nini iwe sasa? Kwanini rais
wa marekani aitembelee Tanzania
sasa tena ikiwa ni ziara ndefu
kuwahi kufanywa na kiongozi
yoyote wa taifa la marekani katika
nchi yoyote ya afrika? Jibu hapa
ni rahisi tu.Nikwa sababu ya
neema kubwa ya mafuta na gesi
iliyogunduliwa Tanzania..Sababu
ya pili ni kujiimarisha kijeshi kwa
kujenga kambi yake hapa
Tanzania ili kuendeleza
mapambano dhidi ya wale wote
wenye kupambana na taifa hili
bila kuchoka na hasa vikundo vya
kigaidi kama vile
Alqaeda,alshabaab,Boko haram, n.k ambavyo vimekuwa
vikijimarisha sana kwa siku za
karibuni” Alhafish akanyamaza
kidogo na kuwatazama wajumbe
wa kikao kile ambao wote
walikuwa kimya kabisa
wakimsikiliza kisha akaendelea
“ Kama nilivyowafahamisha
kwamba ziara hii ya rais wa
Marekani nchini Tanzania ilikuwa
ni kwa sababu maalum zenye
manufaa kwa taifa hilo.Ukiacha
sababu za kiusalama ,kubwa
lililomleta hapa ni suala la mafuta
na gesi.Mtakumbuka awali
niliwaeleza kwamba kwa sasa
Marekani wanapunguza utegemezi
wa mafuta ya mashariki ya kati na
na kuifanya itegemee mafuta yake
ya ndani.Ugunduzi huu wa
kiwango kikubwa cha mafuta na gesi nchini Tanzania umeifanya
Marekani ianze kitolea macho
tanzania nchi ambayo imekuwa
ikipokea misaada mingi toka
Marekani.Katika ziara hii ya rais
wa Marekani kumesainiwa
mikataba kadhaa mikubwa baina
ya serikali ya tanzania na
wawekezaji wakubwa wa mafuta
na gesi toka Marekani.Katika
mikataba hiyo Serikali ya
Tanzania imeyaruhusu
makampuni makubwa ya
marekani kufanya uwekezaji
mkubwa katka sekta ya mafuta
na gesi Tanzania.Hii ina maana
moja kubwa kwamba makampuni
ya kimarekani ndiyo
yatakayoliongoza soko la mafuta
duniani .Marekani haitakuwa tena
na tatizo la mafuta na haitahitaji tena mafuta toka mashariki ya
kati.Washirika wa Marekani pia au
nchi zile kubwa zinazoongoza kwa
viwanda duniani hazitakuwwa
tena na wasi wasi kuhusiana na
suala la mafuta na gesi
,watahamia katika mafuta
yatokayo Tanzania.Bei ya mafuta
duniani itaporomoka na hali hii
itayalazimisha makampuni ya
mafuta ya mashariki ya kati
kupunguza bei ya mafuta ili
kuendana na bei itakayokuwepo
katika soko la dunia.Kushuka kwa
bei ya mafuta kwa nchi za
mashariki ya kati inamaanisha
kwamba hata uchumi wa nchi hizi
lazima utaporomoka kwa sababu
uchumi wao unategemea sana
biashara ya mafuta.Lengo kuu la
Marekani ni kuhakikisha kwamba uchumi wa nchi za mashariki ya
kati unazorota kutokana na
kudorora kwa biashara ya mafuta”
akanyamaza akanywa maji kidogo
kisha akaendelea.
“Nadhani hadi hivi sasa kuna
picha ambayo tayari mmekwisha
ipata kuhusiana na ziara ya rais
wa Mareani” akasema Alhafidhi na
wajumbe wote wakatikisa vichwa
ishara kwamba wanakubaliana
naye.Akatabasamu halafu
akaendelea
“ Suala hili limekuwa
likiumiza vichwa sana
makampuni makubwa ya mafuta
ya masharki ya Kati na hata
serikali zao kwa ujumla.Ni suala
linalohusu maslahi mapana ya
mataifa haya ambayo uchumi
wake unategemea mafuta.Hatutaki makampuni yetu yatetereke
kutokana na kuyumba kwa bei ya
mafuta katika soko la
dunia.Hatutaki uchumi wa
mataifa yetu uzorote kutokana na
kuyumba kwa bei ya mafuta .Vita
vya wenyewe kwa wenyewe katika
eneo zima la mashariki ya kati
vimesababisha chumi za mataifa
haya zilizokuwa zikikua kwa kasi
kuzozorota .Endapo litaatokea
tena baa hilo la kuporomoka kwa
bei ya mafuta mataifa haya
yatakuwa yakichungulia katika
lindi kubwa la umasikini kwani
chumi zao hazitaweza kustawi
kamwe.Ni kutokana na hali hiyo
kumekuwa na mazungumzo ya
kina kati ya serikali za mashariki
ya kati na makampuni makubwa
ya mafuta ya wazawa wa mashiriki ya kati.katika mazungumzo hayo
yote suala la Marekani kuendesha
sekta ya mafuta ya Tanzania
limepingwa vikali.Hatuko tayati na
hatutakuwa tayari kuiacha
Marekani itawale sekta hii nyeti
sana ambayo ndiyo hasa uchumi
wetu sisi watu wa mashariki ya
kati.Narudia tena kwamba hatuko
tayari na wala hatuwakuwa tayari
kuiacha Marekani itawale sekta ya
mafuta ya dunia.Kwa maana hiyo
basi tumefikia uamuzi wa
kuusimamisha na kuuzima kabisa
mpango wa marekani wa
kuidhibiti sekta ya mafuta
duniani.” Alhafidh akatoa
kitambaa na kujifuta jasho halafu
akanywa maji kidogona kuendelea.
“ Serikali ya Tanzania tayari
imekwisha sainiana mikataba mikubwa na makampuni ya
kimarekani na hivyoo suala hilo
kwa sasa lipo kisheria .Hakuna
namna tunayoweza kufanya ili
kutengua mikataba hiyo mikubwa
sana.Kuna njia moja tu ambayo
tunaweza kuifanya ili kulimaliza
suala hili” Alhafidh akanyamaza
na kuziangalia nyuso za wajumbe
waliokuwa kimya
wakimsikiliza.Akanyanyua glasi ya
maji na kupiga funda moja
akaiweka chini akatoa kitambaa
na kujifuta jasho lililokuwa
likimtoka usoni licha ya ukumbi
ule mdogo kuwa na kiyoyozi.Hii
ilitokaa na uzito wa suala
walilokuwa wakiliongelea
“ Ndugu wajumbe njia pekee
ya kuweza kulipatia ufumbuzi suala hili ni kwa kuiangusha
serikali iliyoko madarakani”
Kimya kizito kikatanda mle
ndani.Sura za wajumbe
zilionyesha mabadiliko ya
ghafla.Minong’ono ya chini kwa
chini ikasikika.Mara Daudi
Sichoma akasimama na
kumuelekezea macho Brigedia
Frank huku midomo yake
ikitetemeka
“ What is this Frank? Hiki
ndicho kitu cha muhimu
ulichoniitia? I cant believe this
!!!....akasema Daudi kwa ukali
.wajumbe wengine wanne
wakasimama wakionyesha
kustushwa na kauli ile.Hali
ilibadikika mle chumbani
ikamlazimu Brigedia Frank
asimame. Please calm down
guys.Nawaombeni mtulie na
tusikilizane.Mr David tafadhali
naomba ukae chini na
tusikilizane”akasema Frank na
wale wajumbe waliokuwa
wamesimama wakiongozwa na
Daudi Sichoma wakaketi na
ukimya ukatawala mle ndani
.Frank alipohakikisha wajumbe
wote wametulia kaendelea
“ Ninauona mstuko mkubwa
katika nyuso zenu.Nilitegemea
kitu kama hiki kutokea.Hii si
taarifa nyepesi hata kidogo.Ni
taarifa nzito na yenye kustusha
lakini nyote niliowachagua
kuhudhuria kikao hiki
ninauhakika mkubwa kwamba
hizi ni taarifa njema sana
kwenu.Naomba msiwe na jazba na twende taratibu tutaelewana”
akasema Frank
“Frank kuiangusha serikali si
suala rahisi hata kidogo kama
unavyodhani” akasema David
Sichoma .Frak akatabasamu na
kusema
“ Ninafahamu
unachokimaanisha David lakini
nina uhakika mkubwa hakuna
kitakacho
shindikana.Nime………”kabla
Frank hajaendelea zaidi Daudi
Sichoma akamkatisha
“Frank you know nothing
.Suala ulilolileta ni suala
lisilowezekana kabisa” akasema
Daudi
“ Unaweza kuwa sahihi David
kwamba sijawahi kuwa katika
serikali lakini ninafahamu kila kinachoendelea
serikalini.Ninawafahamu viongozi
wakubwa serikalini.Ninaifahamu
seriali nje na ndani.Daudi
Sichoma ninakufahamu vyema
umewahi kushika nyadhifa
mbalimbali za uongozi serikalini
na hatimaye ukafanikiwa kwa
waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania.Nafahamu
ndoto yako kubwa ilikuwa ni kuwa
rais wa Tanzania lakini kwa bahati
mbaya ndoto yako hiyo
haikuwezekana kutimia kwa
sababu watu ndani ya serikali
waliligundua hilo na hawakuwa
tayari kukuona ukishika nafasi ya
urais na ndiyo maana walianza
kukuandama kwa mambo mengi
na hatimaye kukuzushia kashfa
kubwa na ukaondolewa katika nafasi yako ya uwaziri
mkuu.Ninafahamu madai yale
yaliyotolewa dhidi yako kuhusiana
na kashfa ile hayakuwa ya kweli
na zilikuwa ni njama za kisisasa
na kuhakikisha unapotea kabisa
katika ulingo wa siasa.Lengo lao
limefanikiwa kwani wamefanikiwa
kabisa kukuondoa katika ulingo
wa siasa.Hausikiki tena viywani
mwa watu.Umekwisha sahaulika
kabisa na ndoto yako ya urais
imepotea.Najua unajitahidi sana
kutaka kujirudisha katika medani
za siasa lakini wabaya wako
hawataki kukupa tena
nafasi.Vikwazo vimekuwa vingi na
wamepambana hadi kuhakikisha
kwamba umaarufu wako
unapotea.This is your last chacne
to make your dream come true.Ni wakati wako wa kuitengeneza njia
ya kuingia katika lile jumba
jeupe.” Frank akanyamaza
akamtazama Daudi Sichoma
aliyekuwa kimya akimsikiliza
halafu akawageukia wajumbe
wengine
“Nyote niliowaita hapa
nafahamu ni wenye kuhitaji sana
nafasi za uongozi na mpango huu
wa kuiangusha serikali ndio
mpango pekee utakaowawezesha
na kuwahakikishia nafasi za
uongozi.Kuiangusha serikali
iliyoko madarakani ni jambo zito
ambalo haliwezi kufanywa na sisi
pekee yetuliomo humu chumbani
.Huu ni mchakato mrefu na
jumuishi nikimaanisha kwamba ni
mchakato unaohusisha watu
wengi lakini wenye lengo na nia moja.Sisi sote tulioko hapa ndio
tutakaoratibu mchakato mzima wa
mapinduzi haya.Naombeni ndugu
zangu msikate tamaa.Tunaweza
kulifanya jambo hili.Mkumbuke
pia tunayo sapoti ya kutosha toka
kwa washirika wetu katika suala
hili.Tayari zimekwisha tengwa
shilingi Trilioni sita kwa ajili tu ya
kufanikisha jambo hili.Pamoja na
fedha lakini washirika wetu
watatusaidia pia katika ila kitu
tunachokihitaji”akasema Frank na
kunyamaza tena akawatazama
wajumbe wale.daudi sichoma
akakohoa kidogo na kusema
“ Kidogo sasa ninaanza
kukuelewa Frank.Mpango huu si
mbaya kama nilivyokuwa
ninaufukiria isipokuwa ni mpango
mzito wenye kuhitaji mikakati mizito pia .Lazima tuvihusishe
vyombo vya ulinzi na usalama
hususani jeshi na idara ya
usalama wa taifa,wanasiasa na
wadau wengine watakaoonekana
kuhitajika.Mimi niko tayari
kushirikiana nanyi katika mpango
huu lakini kwa makubaliano
maalum” akasema Daudi Sichoma
“ Ahsante sana Daud kwa
maamuzi yako .Kwa kuwa bado
tuna mchakato mrefu mbele yetu
nina imani kwamba tutafikia
makubaliano unayohitaji”
akasema Frank na kuwageukia
wajumbe wengine
“ Ndugu zangu kati yenu
kuna yeyote mwenye mawazo
tofauti? Kuna yeyote mwenye
duku duku au maoni yoyote
kuhusiana na mpango huu? Akauliza Frank.Kabla mtu yeyote
hajajibu,simu ya Frank
ikaita,akastuka baada ya kuona
watu wote wanamtazama
“ Samahani ndugu zangu
kwa kutoizima simu yangu katika
kikao kizito kama hiki” akasema
Frank huku akitoa simu yake kwa
lengo la kuizima lakini mara tu
alipotazama jina la mpigaji
akastuka.Jina lilisomeka kama
hospitali Graca
“ Samahani jamani naomba
niipokee simu hii ni muhimu
sana” akasema Frank na kutoka
nje ya kile chumba
“Hallow” akasema Frank
“ Hallow Frank habari za Dar
es salaam? Ikasema sauti ya
upande wa pili
Hili dude nalisoma sichoki kabisa....good job bro. Lete madude tupungeze mawazo ya hapa na pale
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 24

Habari ni nzuri nani
mwenzangu? Akauliza Frank
“Ninaitwa Dr Susan napiga
simu toka katika hospitali na
magonjwa ya akili anakotibiwa
mwanao Graca.”
“ Oh! Dr Susan.Nimestushwa
sana na simu yako usiku
huu.Kwema huko? Akauliza
“ Huku si kwema.Kuna jambo
limetokea mchana wa leo”akasema
Dr Susan na kuzidi kumtia hofu
Frank
“ Jambo gani limetokea?
Mbona unanipa hofu namna
hiyo?akauliza Frank
“ Graca amepotea na mpaka
sasa hivi hatujui yuko wapi”
“ What ?!!...Frank akahamaki
“ Nakutaarifu kwamba
mwanao Graca ametoweka mchana wa leo na mpaka muda
huu hajaonekana.Juhudi za
kumtafuta zinaendelea
tukishirikiana na vyombo vya
usalama”
“ Dr Susan jambo hili
limetokeaje?hakukuwa na ulinzi
hapo hospitali hadi mwanangu
akatoroka? Akauliza Frank
“ Badohakuna anayefahamu
nini kilitokea hadi Graca
akatoweka.Tumewachia jukumu
hili vyombo vya usalama
vichunguze .Usiwe na hofu
tunalishughulikia suala hili kwa
karibu sana na tunaamini Graca
hatakuwa mbali na hapa”
“ Dr Susan bado maelezo
yako hayajitoshelezi? Nieleze kwa
ufasaha mwanagu amepoteaje
wakati hapo hospitali kuna ulinzi na wagonjwa wote wanakuwa
chini ya uangalizi maalum?
Akauliza Frank kwa ukali
“ Tukio hili hata sisi
limetustua sana.Awali tulidhani
yuko katika maeneo ya hapa
hospitali lakini saa moja za jioni
wakati tunapitia wagonjwa wote ili
kuhakikisha wako wote Graca
pekee ambaye
hakuonekana.Tulianza juhudi za
kumsaka kila kona ya hospitali
lakini hakuonekana ikatulazimu
kutoa taarifa kwa vyombo vya
usalama na tayari wamekwisha
fika na wanaendelea na zoezi la
kumtafuta.Nitawasiliana nawe kila
mara nitakapopata ripoti toka
kwao.Nakuhakikishia kwamba
tunafanya kila linalowzekana
kuhakikisha Graca anapatikana kwani ni mgonjwa na anahitaji
matibabu.Picha yake itasambazwa
katika kila kona na watu
watatusaidia kumtafuta.Tahadhari
imekwisha tolewa pia kwa wote
wanaoishi jirani na hospitali
kwamba kuna mgonjwa
ametoweka hospitali kwa hiyo
watakapomuona watoe taarifa
haraka sana hapa hospitali au
katika kituo chochote cha
polisi.Ninahakika mpaka kesho
asubuhi tutakuwa na taarifa nzuri
zenye kutia matumaini” akasema
Dr Susan
“ Ok ! Ahsante sana Dr Susan
kwa taarifa japokuwa ni taarifa
zenye kustusha sana.Naomba
unipe taarifa kila hatua
inayofikiwa” akasema Frank usijali Frank.Nitawasiliana
nawe kila mara kukupa taarifa”
akasema Dr Susan na kukata
simu.BadoFrank aliendeelea
kutazama juu akiwa na mawazo
mengi
“ Hii imetokeaje?Graca
amepoteaje? Amewezaje kutoroka
pale hospitali wakati kuna ulinzi
mkali? Akajiuliza Frank halafu
akachukua simu yake na
kuzitafuta namba Fulani akapiga
“hallow Bonny.” akasema
Frank baada ya simu kupokelewa
“Hallow Frank”ikajibu sauti
ya upande wa pili
“Bonny hebu nieleze nini
kimetokea? Ninakulipa fedha
nyingi kila mwezi wewe na
mwenzako kwa ajili ya kumlinda
mwanangu imekuaje leo ninapokea taarifa kwamba
amepotea? Akauliza Frank kwa
ukali
“ Frank utaniwia radhi lakini
nilikuwa katika hatua za
kukutaarifu kilichotokea.Ni kweli
Graca ametoweka na sote
tumeshirikiana kumtafuta bila
mafanikio.Kuna kitu kilitokea
ambacho nakiunganisha na tukio
hili la kutoweka kwa Graca”
“ Nini kilitokea ? akauliza
Frank
“ Mchana wa leo kuna watu
wawili walifika hapa na mmoja
wao akawa akiongea na Graca
bustanini.Nilifanikwia kupata
picha yake toka kwa mbali
nitakutumia muda si mrefu ili
uweze kumuona mtu huyo ni nani
na kama unamfahamu ama vipi.Baadae watu hao waliondoka
na walifanyiwa ukaguzi getini ila
hawakuwa na kitu chochote
.Tunachoshindwa kuelewa ni
kwamba Graca ametoweka vipi?
Kuna uzio mkubwa na hawezi
kuruka.Kama ni hivyo amewezaje
kutoweka? Lakini wasiwasi wangu
upo kwa wale jamaa wawili.Lazima
kuna kitu wanakifahamu kuhusu
kupotea kwa Graca”akasema Bony
“Nitume picha za watu hao
haraka”akasema Frank na baada
ya dakika moja picha
zikaingia.Akaziangalia picha zile
na kuhsi kwa mbali kijashi
kinamtoka.
“Mungu wangu
…..Elvis!!..akasema Frank kwa
sauti ndogo ya mshangao.Kwa
dakika mbili alibaki anaziangalia picha zile katika simu yake na
mara akakumbuka kwamba kuna
kikao kinachoendelea
akakurupuka na kurejea kikaoni
Kikao kiliendelea hadi
ilipotimu saa tisa za usiku ndipo
kilipomalizika kwa makubaliano
kwamba siku itakayofuata
wakutane tena nyumbani kwa
Daudi Sichoma kwa ajili ya
mikakati zaidi.Wajumbe
wakaagana na kutawanyika.Frank
na Pascal Situmwa
wakawapeleleka akina Alhafidh
hotelini walikofikia kisha
wakaagana nao kwa miadi ya
kuonana tena asubuhi kabla
hawajaelekea uwanja wa ndege
kwa ajili ya kuondoka nchini
“Pascal we need to talk”
akasema Frank wakati wakishuka ngazi za hoteli kuelekea katika
maegesho ya magari.Pascal
akaonekana kustuka kidogo
akageuka na kumtazama Frank
akagundua kuna kitu hakikuwa
sawa.
“ Frank are you ok?akauliza
Pascal
“ No ! I’m not ok”akajibu
Frank
“ Nini kimetokea Frank? Toka
ulipotoka mle kikaoni ukaenda
kuongea na simu kuna kitu
nilikigundua.Haukuwa sawa
kabisa.Whats wrong? Akauliza
Pascal
“ Pascal tuna tatizo” akasema
taratibu Frank huku akiufungua
mlango wa gari akaliwasha
wakaondoka.Mara tu walipotoka katika geti la hoteli Pascal
akauliza
“ Frank kuna tatizo gani?
Fran akavuta pumzi ndefu na
kusema
“ Graca ametoroka hospitali
na hajulikani alipo”
“ Graca !! ametoweka
vipi?Hospitali hiyo haina ulinzi?
Akauliza pascal
“ Ulinzi upo tena mkali sana”
“ sasa ametoroka vipi kama
kuna ulinzi?.akauliza
pascal.Frank akapunguza mwendo
wa gari akachukua simu yake na
kumuonyesha Pascal
“ Elvis Tarimo” akasema
Frank
“ Elvis !!!!!..Pascal akastuka
“ Unamfahamu vizuri Elvis? “Ndiyo ninamfahamu vizuri.Ni
mfanyakazi wa idara ya ujasusi ya
taifa.Inasmekana ni mmoja kati ya
watu tegemeo sana katika idara
yake.Elvis anahusiana nini na
kupotea kwa Graca?akauliza
Pascal
“ Elvis alionekana akiongea
na Graca na baadae jioni Graca
hakuonekana tena”
Sura ya pascal ikaonyesha
uoga mkubwa.Safari ikaendelea
kimya kimya.Pascal alionekana
kuwa na mawazo mengi sana
“ Pascal unawaza nini?
Akauliza Frank baada ya
kumuona Pascal akiwa amezama
katika lindi la mawazo
“ Frank we have a problem”
akasema Pascal “ yes I know that we have a
problem” Akasema Pascal
“ Ninavyomfahamu Elvis
mpaka afikie hatua ya kwenda
kuonana na Graca basi lazima
kuna jambo amekwisha
linusa.Something is not right ”
akasema Pascal
“ Ninachojiuliza ni kwamba
kwa nini akaongee na Graca ?Nina
wasi was kuna jambo
ameligundua kuhusiana na
nyaraka zile zilizokuwamo katika
komputa ile aliyoiba Graca na
mama yake.Graca ni mtoto wangu
lakini nilifanya kosa kubwa sana
kumuacha hai mpaka sasa hivi”
akasema Frank
“Una hakika Elvis anaweza
kuwa amezipata nyaraka hizo?
Akauliza Pascal Sina hakika kama atakuwa
amezipata kwa sababu kama
tayari angekuwa nazo basi
asingesumbuka kwenda kuonana
na Graca.Ninachohisi mimi ni
kwamba kuna kitu atakuwa
anakihisi au kuna fununu fulani
anazo na ndiyo maana anafanya
uchunguzi.Kama nyaraka zile
angekuwa nazo mikononi toka
zilipopotea basi tungekuwa
tunaongea mambo mengine hivi
sasa”akasema Frank
“So what are we going to do?
Akauliza Pascal
“ Tunatakiwa tukabiliane na
suala hili haraka sana.Kwanza
tunatakiwa kuhakikisha kwamba
Graca anapatikana na vile vile
tunatakiwia kumdhibiti
Elvis.Tunatakiwa tufahamu ni kitu gani anakijua kuhusiana na sisi”
akasema Frank.Pascal akazama
tena mawazoni
“ Frank unakumbuka niliwahi
kukwambia kwamba pochi yangu
ndogo iliyokuwa na kumbu kumbu
zangu muhimu iliwahi kupotea
pale nyumani kwangu?
“Ndiyo nakumbuka.Nadhani
msichana yulealiyeiiba aliuawa”
“Ndiyo .Niliwatuma vijana
wangu wamzimishe kabisa kwani
niliamini lazima kuna mtu
alimtuma aniibie pochi ile.Kuna
jambo ambalo nimelikumbuka
sasa hivi”
“Jambo gani Pascal?
“Ni hivi majuzi tu kuna mtu
alingia pale nyumbani kwangu
lakini hakuiba kitu
chochote.Alionekana wakati akitoka kwa hiyo vijana
hawakuweza kumjua ni
nani.Ninaanza kuhisi kwamba
huenda mtu huyu naye alitumwa
kuja kuchunguza kitu pale
kwangu.Nina wasiwasi kwamba
huenda tukawa tumejulikana
mambo yetu na hivyo wanaendelea
kutuchunguza na kukusanya
ushahidi wakutosha.Nadhani hata
Elvis kwenda kuonana na Graca ni
sehemu ya uchunguzi
unaoendelea.Elvis anataka kupata
taarifa toka kwa Graca.Endapo
kuna mambo ambayo Graca
anayafahamu kuhusu sisi hatasita
kumweleza Elvis.Kwa sasa nina
uhakika mkubwa kwamba ni Elvis
ndiye aliyemtorosha Graca.Swali la
kujiuliza ni je wako wapi?
Akasema Pascal. Yule mtoto nina hakika
tayari atakuwa anafahamu mambo
mengi kuhusiana na sisi na
ninahisihatasita kumweleza Elvis
kila kitu
anachokifahamu.Kumuacha hai
lilikuwa kosa kubwa
sana”akasema Frank
“Pascal una hakika yule
msichana alikufa? Pascal
akastuka kwa swali lile.hakuwa
amelitegemea
“ Ndiyo nina hakika .kwani
vipi?
“ I’m just Curious”
“Vijana niliowatuma waifanye
kazi ile walinihakikishia kwamba
wamemuua na kumtupa bonde la
mpunga”
“ Ulifanya kosa kuwaamini na
kuwaacha wakaifanya kazi ile peke yao.Ulitakiwa uwepo na
uhakikishe kwamba ni kweli
amekata pumzi”
“ Mbona unaonyesha wasi
wasi Frank?
“ Kuna kitu
ninakihisi.Naomba kesho ulifanyie
uchunguzi suala hili kama ni kweli
alikufa ama vipi” akasema Frank
“ Vijana walinihakikshia
kwamba yule binti amefariki na
wakamtupa lakini ushauri wako si
mbaya.Ninafahamiana na wakuu
wa polisi wa vituo karibu vyote
hapa jijini.Nitawasiliana nao ili
nijue kama katika tarehe ile kuna
maiti yoyote iliokotwa.Mpaka
kesho saa nne tayari tutakuwa na
jibu”
“Good”akasema Frank na
kukanyaga pedeli ya mafuta gari ikaongeza mwendo kuelekea
nyumbani kwa Pascal
“ Pascal kesho asubuhi kitu
cha kwanza unachotakiwa
kukifuatilia ni iwapo Elvis yupo
hapa nchini au hayupo.Kama
hayupo tutapata uhakika kwamba
ni kweli alikwenda afrika ya kusini
kuonana na Graca.Baada ya hapo
tunatakiwa tufahamu pia kama
alitumwa afrika ya kusini kikazi
.Kama alitumwa kikazi alitumwa
kazi gani?Lazima tuchukue
tahadhali za mapema na hasa
katika wakati huu mbao
tunakabiliwa na mpango mzito
mbele yetu.Elvis mtu yeyote
hatakiwi kuwa kizingiti
kwetu.Yeyote yule ambaye
ataonekana kama hatari kwetu tutamuondoa haraka sana”
akasema Frank
“ Kesho ni siku yetu ngumu
sana.Tuna mambo mengi ya
kufanya .Kesho ni mwanzo wa
harakati mpya”akasema Pascal
huku akishuka garini wakaagana
Frank akaendelea na safari
kuelekea kwake
“ Elvis tarimo !!.. akasema
Frank kwa sauti ndogo
“ Huyu kijana bado
hajanifahamu mimi ni nani.I
swear nitamkata kauli sekunde
chache nikigundua kwamba
amekuwa akinifuatilia mambo
yangu.Safari hii ameingia sehemu
mbaya sana” akawaza Frank
akiwa njiani kuelekea kwake.
******************** Saa tatu za usiku ndege ye
jeshi la afrika kusini iliyokua
ikiwapeleka wanajeshi wa afriak
kusini katika mazoezi ya pamoja
ya kijeshi nchini Zambia ikatua
katika uwanja wa ndege wa kijeshi
uliopo nje kidogo ya jiji la
Lusaka.Ndani ya ndege hiyo
walikuwamo pia Elvis na
Graca.Ilikuwa ni safari ngumu
kwa Graca kwani hakuwahi
kusafiri na ndege za kijeshi ila kwa
Elvis ilikuwa ni moja ya safari
zake za kawaida
Ndege ilisimama lango
likafunguliwa na wanajeshi
wakashuka.Kiongozi wa msafara
ule Meja Tsemaleke Suso
akawaongoza Elvis na Graca hadi
katika gari dogo la jeshi
wakapanda.Wanajeshi wengine
wakaingia katika katika gari kubwa na safari ya kuelekea
katika kambi ya kijeshi
ikaanza.Baada ya kukatisha mitaa
kadhaa ya mji wa Lusaka
hatimaye Meja Tsemaleke
akamuamuru dereva wa lile gari
walilopanda akina Elvis
asimamishe gari katika mtaa
Fulani wenye maduka mengi
akashuka na kuwaomba akina
Elvis nao washuke
“ kwa mujibu wa maelekezo
niliyopewa na Bongani ni kwamba
niwafikishe hapa na toka hapa
kuna mtu ambaye atawachukua
na kuendelea na safari yenu”
akasema Meja Tsemaleke
“ Ahsante sana Meja kwa
msaada wako huu mkubwa”
akasema Elvis huku akipeana
mkono na MejaTsemaleke
wakaagana akarejea garini
wakaendelea na safari yao
Elvis na Graca walisimama pale mahala waliposhuswa nje ya duka
moja lililokuwalimefungwa.Huu ni
mtaa wa maduka na bado maduka
kadhaa pamoja na sehemu za
kuuzia vyakula na vinywaji
yalikuwa wazi.Graca alionekana
kuwa na wawi wasi mwingi
“ Nini kinaendelea baada ya
hapa? Akauliza
“ Usiwe na wasi wasi Graca
tutafika tu Tanzania” akasema
Elvis na baada ya kama dakika
tano mlango wa gari lililokuwa
limeegeshwa mita chache toka
pale walipokuwa wamesimama
akashuka mtu mmoja aliyekuwa
amevaa kofia nyeusi ya duara na
koti refu jeusi.Mtu yule alisimama
nje ya gari lake akaangaza angaza
pande zote kisha akaanza
kutembea taratibu kuwafuata
akina Elvis
“ Hallow” akawasalimu
“ Hallo” akajibu Elvis Elvis? Yule jamaa akauliza
“ Stanley? Elvis naye
akauliza.Yule jamaa akaitika kwa
kichwa kisha wakashikana mikono
wakasalimiana halafu
akawaongoza hadi katika gari lake
wakaingia lakini kabla
hawajaondoka akamgeukia Elvis
“ Elvis Maelekezo niliyopewa
ni kuwafikisha mpakani mwa
Tanzania na Zambia na
kuhakikisha mnafika salama
nchini kwenu.Niko sahihi?”
akasema Stanley
“ Uko sahihi Stanley.Hilo
ndilo hitaji letu kubwa” akajibu
Elvis na Stanley ambaye
alionekana ni mtu asiyependa
maongezi mengi akawasha gari na
kuondoka
“ Stanley samahani naweza
kutumia simu yako kupiga
Tanzania? Akasema Elvis .Bila
kujibu kitu Stanley akampatia Elvis simu yake.Elvis akaandika
namba alizotaka kupiga na
kubonyeza kitufe cha kupigia simu
ikaanza kuita na baada ya muda
ikapokelewa
“ Hallo “ ikajibu sauti tamu ya
kike upande wa pili
“ Hallow Doreen..” akasema
Elvis
“ Elvis !! Doreen akastuka
“ Ndiyo Doreen” akasema
Elvis na kumsikia Doreen
akishusha pumzi
“ Patricia aliniambia kwamba
umesafiri kwenda afrika ya kusini
mbona unanipigia na namba ya
simu ya Zambia? Akauliza Doreen
“ Ndiyo nilikwenda afrika ya
kusini lakini kwa sasa niko
Zambia” akajibu Elvis na kimya
kifupi kikapita
“ Doreen are you there?
Akauliza Elvis
“ I’m here Elvis” Good.Doreen unakumbuka
uliniambia kwamba uko tayari
kunisaidia kwa jambo lolote ?
“ Ndiyo nakumbuka Elvis
.Unataka nikusaidie kwa jambo
gani? Sema chochote niko tayari”
akasema Doreen
“ Naomba kesho alfajiri na
mapema uchukue gari lako lile
jipya na uanze safari ya kuelekea
jijini Mbeya.Nitakupigia simu
nikiwa Mbeya na kukujulisha
mahala nilipo” akasema Elvis
.Doreen akabaki kimya
“ Doreen are you there?
Akauliza Elvis
“ I’m here Elvis” akajibu
Doreen
“ Umenielewa nilichokuomba?
I real need your help right now”
akasema Elvis Baada ya kimya
cha sekunde kadhaa Doreen
akasema
“ Ok Elvis nitakusaidia.Kwako sina uwezo wa kusema hapana”
akajibu Doreen.Uso wa Elvis
ukapambwa na tabasamu baada
ya jibu lile la Doreen.
“ Ahsante sana
Doreen.Ahsante sana.Tafadhali
naomba usimweleze chochote
Patricia.Nitakupigia simu kesho
nikiwa Mbeya na kukupa
maelekezo mahala nitakapokuwa”
akasema Elvis
“ Usijali Elvis japokuwa
umenistukiza sana lakini
nitajitahidi kufanya kama
ulivyoniomba.Ila tafadhali naomba
unihakikishie kwamba uko salama
na hakuna tatizo lolote” akasema
Doreen
“ Niko salama Doreen usihofu
chochote” akasema Elvis na
kukata simu akamrudishia
Stanley simu yake.Hawakuongea
kitu chochote safari ikaendelea
kwa kasi kuelekea Tunduma mji uliopo mpakani mwa Tanzania na
Zambia
***********************
Ilikuwa ni safari ndefu
kutokana na umbali mrefu uliopo
kati ya Lusaka na Tunduma
.Kutoka Lusaka hadi Tunduma ni
umbali wa kilometa 1022.Stanley
ambaye alionekana kwa mahiri
mno katika usukani aliendesha
gari kwa kasi na umakini
mkubwa.Graca kutokana na
uchovu aliokuwa nao kwa safari
ndefu ilimlazimu alale katika kiti
cha nyuma
Saa mbili za asubuhi
walikaribia mji wa
Tunduma.Stanley akaachana na
barabara kuu akachepuka katika
barabara ya vumbi ambayo
ilionyesha haikuwa ikipitwa sana
ma magari.Aliendesha taratibu kutokana na barabara ile kujaa
mashimo mengi.Baada ya mwendo
wa kama dakika ishirini katika
barabara ile akasimamisha gari na
kutoa simu akampigia mtu Fulani
wakaongea halafu safari
ikaendelea.Dakika kama kumi hivi
akasimisha gari chini ya mti
mmoja mkubwa akashuka na
kutoa simu yake akawasiliana na
mtu na baada ya kama dakika
tano hivi wakatokea watu wawili
wakiwa na piki piki.Stanley
akasalimiana nao wakaongea
kidogo halafu akatoa fedha katika
pochi yake na kuwahesabia na
kurejea garini alikowaacha akina
Elvis
“ Elvis hawa jamaa wa piki
piki ndio watakaowaingiza
Tanzania ,Ni wazozefu sana wa
njia hizi za vichochoroni kwa hiyo
msiwe na wasi wasi hata
kidogo.Kitu ninawachowaomba ni kwamba msiwaulize chochote na
wala msitake kufahamu chochote
toka kwao.Watawapeleka sehemu
mnakotaka kwenda na baada ya
hapo mtatafuta usafiri wa
kuwafikisha Dar es salaam.Poleni
sana kwa safari ndefu” akasema
Stanley
“ Stanley sina neno kubwa la
kuweza kukushukuru kwa
msaada huu ya kusema ahsante
sana. Tunashukuru umetufikisha
hapa salama na ninakutakia safari
njema ya kurejea Lusaka “
akasema Elvis huku akimpa
mkono wakaagana na kuelekea
katika piki piki wakapanda na
safari ya kuelekea Tunduma
ikaanza.
Dakika thelathini baadae
waliwasili katika mji wa Tunduma
mji wenye pilika pilika nyingi sana
za kibiashara.Elvis akawaomba
wale vijana wawapeleke katika stendi ya magari yaendayo mjini
Mbeya na kuagana na vijana wale
.Pale stendi kulikuwa na watu
wengi na Elvis hakutaka wapande
gari lenye watu wengi hivyo
akakodisha gari ndogo aina ya
Noah ili iwapeleke Mbeya.
Saa saba za mchana wakawasili
jijini Mbeya, jiji zuri na lenye
kuvutia sana.Dereva wa lile gari
walilokodi alilifahamu vyema sana
jiji la Mbeya hivyo akawapeleka
katika hoteli nzuri ambako
walichukua vyumba viwili .Kwa
kutumia simu ya pale hotelini
Elvis akawasiliana na Doreen
aliyekuwa safarini kuelekea Mbeya
na kumfahamisha mahala
walikofikia.
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 25

****************
Pamoja na kurejea nyumbani
saa kumi alfajiri lakini Pascal
alishindwa kabisa kupata usingizi
.Kichwa chake kilikuwa na
mawazo mengi sana lakini mawili
makubwa yaliyokuwa
yakimsumbua kichwa ni mpango
ule wa kuiangusha serikali na pili
ni taarifa za kuonekana kwa Elvis
akiwa na Graca nchini afrika ya
kusini.Hizi ni taarifa zilizomstua
sana kwani anafahamu vizuri Elvis
mpaka akaonane na Graca lazima
kuna kitu ambacho alikuwa
anakifuatilia
“ Damn !! akasema Pascal
kwa hasira na kuinua glasi ya
mvinyo akanywa
Hadi kunapambazuka bado
alikuwa macho.Akaoga na
kuelekea kazini.Akiwa njiani
aliwasiliana na Arafa mmoja wa wafanyakazi wa idara ya ujasusi
anakofanya kazi Elvis
“ Hallow Pascal” akasema
Arafa baada ya kupokea simu
“ hallow Arafa uko wapi sasa
hivi? Akauliza Pascal
“ Ninaelekea kazini
Pascal.wewe uko wapi?
“ Hata mimi ninaeleka kazini.”
“ Kulikoni Pascal leo
umenipigia simu asubuhi namna
hii? Akauliza Arafa
“ Nilitaka kuja ofisini kwenu
leo hii lakini sintaweza kwa hiyo
ninahitaji msaada wako”
“ Msaada gani Pascal?
“ Ninahitaji kuonana na
Elvis.Kuna taarifa ninataka
kumpa lakini kuna mtu aliniambia
kwamba Elvis hayupo.Sina uhaika
sana na jibu hilo kwa hiyo naomba
unisaidie kuthibitha kama ni kweli
hayupo.Kama yupo usimweleze
chochote nitaarifu nitamtafuta mimi mwenyewe kwa wakati
wangu” akadanganya Pascal
“Hauna mawasiliano na Elvis?
Akauliza Arafa
“ Hapana sina .Elvis ni mtu
ambaye sijazoeana naye kiasi cha
kuwa na mawasilino naye
japokuwa tunafahamiana.”
Akasema Pascal .Arafa akafikiri
kidogo kisha akasema
“ OK nitakutaarifu nikifika
ofisini” akasema Arafa na kukata
simu
“ Leo lazima nipate uhakika
kuhusu Elvis kuonekana afrika ya
kusini.Huyu mtu ananiweka
tumbo joto sana.Elvis ni mtu
hatari na lazima tumdhibiti
mapema” akawaza Pascal
Alifika ofisini kwao na
alionekana ni mwenye mawazo
mengi .Aliendelea na kazi na saa
tatu na robo Arafa akampigia simu
“ Halow Arafa” akasema Pascal
“ Pascal ni kweli Elvis hayupo
yuko nje ya mkoa kikazi”
“ Amekwenda mkoa gani na
atarudi lini?
“ Siwezi kujua yuko wapi na
anafanya nini na atarudi lini
kwani kiwango change si cha
kufahamu mambo kama
hayo.Atakaporejea
nitakufahamisha mara moja”
“Ahsante sana Arafa .Naomba
unitaarifu atakaporejea ila
tafadhali naomba usimfahamishe
chochote kama nilikuwa
namtafuta”
“ usijali Pascal” akajibu Arafa
na kukata simu
“ Kwa sasa nina uhakika
kwamba Elvis amekwenda nchini
Afrika ya kusini na si nje ya mkoa
kama alivyoniambia Arafa.Lakini
kwa nini akaenda kuonana na
Graca? Hili ndilo swali la kutafutiamajibu haraka sana” akawaza
Pascal na kutoka nje ya jengo
akampigia simu Brigedia Frank
“ hallow Pascal “ akasema
Frank
“ Frank tayari nimepata
uhakika kwamba Elvis ana safari
ya kikazi lakini mtu aliyenipa
taarifa hizo hakuweza kunieleza
amekwenda wapi na ni kazi gani
amekwenda kufanya.Mpaka hapa
hakuna shaka kwamba ni kweli
Elvis alikwenda Afrika ya kusini.”
Akasema Pascal halafu kimya
kifupi kikapita Frank akasema
“Kinachoniumiza kichwa ni
kwamba kwa nini alikwenda
kuonana na Graca? Nina hakika
kuna kitu anakitafuta.Ni kitu gani
basi alikuwa anakitafuta kwa
Graca?Amempeleka wapi Graca?
Mpaka hivi sasa sijapokea taarifa
zozote kuhusiana na zoezi la
kumtafuta mwanangu” Frank hata mimi jambo hilo
limekuwa linaniumiza sana
kichwa changu.Tunatakiwa
tutafute jibu la haraka sana la
swali hili” akasema Pascal
“ OK vizuri.Bado uko ofsini?
Akauliza Frank
“ Ninajiandaa kuondoka ili
kuwahi kikao cha leo mchana
“ Good.Kikao cha leo mchana
ni muhimu sana kwani ndicho
kitakachotupa muelekeo mzima
wa mkakati wetu .Wageni wetu
tayari nimewasindikiza
wameondoka .Utanipitia hapa
nyumbani ili tuongozane wote
kuelekea kikaoni” akasema Frank
“ Ok Frank nakuja sasa hivi”
akasema Pascal
***************** Jumba la kifahari la aliyewahi
kuwa waziri mkuu wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Daudi
sichoma lilizungukwa na bustani
iliyotengenezwa kwa ustadi
mkubwa,iliyosheheni miti mizuri
na maua ya kupendeza. Ndege
wazuri wa kila rangi waliruka
katika miti yenye maua mazuri na
kuzidi kuifanya bustani ile iwe na
mandhari ya kipekee sana.Daudi
Sichoma ni mmoja kati ya viongozi
wanaosemekana kujilimbikizia
utajiri mkubwa sana ndani na nje
ya nchi.Alimiliki mahoteli
makubwa ndani na nje ya nchi,pia
anamiliki shirika la ndege na vile
vile ana hisa nyingi katika
makampuni mengi makubwa ya
ndani na nje ya nchi.Kiwango cha
utajiri wake kimebaki kuwa siri
kutokana na kumiliki miradi
mingine mingi kwa siri
Eneo litakalotumika kwa ajili ya kikao liliandaliwa vizuri sana
katikati ya bustani hii nzuri.Kabla
ya kukaa katika meza ya kikao
kulikuwa na sehemu iliyoandaliwa
maalum kwa ajili ya wajumbe
kupata chakula kabla ya kuanza
kwa kikao.
Mpaka saa saba mchana
karibu wajumbe wote waliotakiwa
kuhudhuria kikao kile tayari
walikwisha wasili.Daudi
akawaongoza wajumbe wale hadi
katika sehemu kulikoandaliwa
chakula na wajumbe wakaanza
kujipatia mlo wa mchana.Kilikuwa
ni chakula kizuri kilichoandaliwa
na wapishi mahiri waliotoka
katika mojawapo ya hoteli
anayomiliki Daudi.Baada ya
chakula wajumbe wakaelekea
sehemu kulikokuwa
kumeandaliwa kwa ajili ya
kikao.Eneo lote lilikuwa kimya
sana. Ni milio tu ya ndege iliyokuwa ikisikika katika bustani
ile.Brigedia Frank ambaye ndiye
aliyekuwa mwenyekiti wa kikao
kile akafungua kikao kwa
kuwashuku wajumbekwa kufika
kwao
“ napenda niwataarifu
kwamba wale wageni wetu
tuliokuwa nao jana wameondoka
leo asubuhi kurejea makwao na
majukumu yote ya ule mpango
yako juu yetu kwa hiyo hatuna
muda wa kupoteza tunatakiwa
tuanze mara moja mikakati ya
kutekeleza mpango huu
mkubwa.wao tutakuwa
tukiwatumia mihutasari ya kila
kikao tunachokifanya na
utekelezaji wa kila jambo.Fedha
zitawekwa katika akaunti maalum
na kila pale tutakapokuwa
tukihitaji fedha hatutakuwa na
upungufu wowote.Ndugu zangu
hiki ni kikao cha chetu cha kwanza cha kuweka mikakati ya
kuelekea Tanzania
mpya.Mnakaribishwa kwa mawazo
tukianza na mheshimiwa Daudi
ambaye ana uzoefu mkubwa wa
kuwepo serikalini na atatusaidia
sana kimawazo” akasema Brigedia
Frank .Daudi sichoma
akatabasamu na kukohoa kidogo
akasema
“ Awali ya yote napenda
kuwashukuru nyote kwa kufika
kwenu.Namshukuru sana Frank
kwa uamuzi wake wa
kunishirikisha katika mpango huu
muhimu.Nasema ni mpango
muhimu kwa taifa letu kwani
endapo utafanikiwa basi utaleta
neema kwa watanzania na maisha
yao yataboreka tofauti na hali
ilivyo sasa.Sote tuliwasikia akina
Alhafidh na maelezo waliyotupatia
.Ukiyachambua kwa undani
maelezo yale utagundua kwamba kuna kila ulazima wa kuiondoa
kwa lazima serikali iliyopo
madarakani.Hatuwezi kuiondoa
kwa njia za kdemokrasia bali kwa
kufanya mapinduzi.” Akasema
Daudi na kunyamaza kidogo kisha
akaendelea
“ Tukirejea maelezo ya
Alhafidh tunagundua kwamba
mipango yote inayofanyika hivi
sasa kuhusiana na uwekezaji
mkubwa katika sekta ya mafuta
na gesi inalenga katika
kuwanufaisha viongozi walioko
madarakani.Hakuna hata mpango
mmoja utakaowanufaisha
wananchi wa hali ya chini.Kitu
cha pili ni kwamba viongozi hawa
wanataka kuipeleka Tanzania
katika machafuko kwa sababu
endapo marekani watajenga kituo
chao cha kijeshi hapa nchini basi
Tanzania itakuwa ni moja ya
shabaha za magaidi.Nchi haitakuwa salama
tena.Tunatakiwa tuhakikishe
kwamba hilo halitokei kwa kuja na
mikakati mizito sana ambayo
itakuwa na faida kwa watanzania
na hata tutakapofanikiwa
kuiangusha serikali basi
watanzania watuamini kwamba
tuna nia ya dhati ya kufanya
mageuzi makubwa ya maisha
yao.Endapo kila mtanzania
ataiona na kufurahia faida ya
kuwa na gesi na mafuta nchini
Tanzania basi mapinduzi
tutakayoyafanya yatakuwa na
manufaa na watanzania
watatupenda na kutuunga
mkono.Makampuni ya kiarabu
tutayapa udhibiti wa biashara ya
mafuta na yatatuletea faida kubwa
sana na tutahakikisha kila
mwananchi wa nchi hii mkubwa
kwa mdogo wanafaidika
nayo.Tutakuza uchumi tutaboresha maisha ya
mwananchi mmoja moja na kila
raia wanchi hii atakuwa na uso
wenye tabasamu.Hiyo ndiyo ndoto
yangu ya muda mrefu sana ya
kumfanya Mtanzania afurahi
kuwapo Tanzania” akasema Daudi
na wajumbe wote wakampigia
makofi kumuunga mkono David
akaendelea
“ Ndoto yangu ya miaka mingi
ni kuwa rais wa nchi hii.Lengo si
kutaka kutafuta utajiri au
umaarufu au kuabudiwa lakini
lengo langu kubwa ni kutaka
kumfanya kila raia wa nchi hii awe
na furaha ,ayamudu maisha yake
,watoto wetu wasome na ajira
zipatikane.Hayo yote
yanawezekana tu kwa kuwa na
koongozi jasiri kama mimi.Nyote
mnafahamu mambo niliyoyafanya
na kuleta mabadiliko katika jamii
.Ni mambo hayo niliyoyafanya ndiyo yanayofanya nikawa na
maadui wengi kisiasa na
nikaondolewa madarakani.Pamoja
na kuondolewa katika nafasi
yangu ya uwaziri mkuu bado
wameendelea kunifuata fata na
kuhakikisha kwamba wananizika
kabisa na kwa hilo naweza
kusema kwamba wamefanikiwa
kwani sionekani tena katika
medani za siasa.Ninamshukuru
Frak kwa kunishirikisha tena
kaika mpango huu ambao nina
hakika lazima utafanikiwa.”
Wajumbe wakapiga makofi
halafu akaendelea
“ Naomba niweke wazi kwenu
kwamba kama ilivyo ndoto yangu
ya muda mrefu na endapo mpango
huu utafanikiwa basi naombeni
mimi niwe rais.Naomba
tukubaliane toka awali kwamba
tukifakiwa mimi ndiye
nitakayekuwa rais” Daudi akasema na kuwatazama
wajumbe .Kimya kifupi kikapita
Frank akasema
“ Mimi sina kipingamizi na
hilo.Nafahamu wananchi wengi
bado wanakuhitaji sana ili
uwaongoze.wewe ndiye
utakayekuwa rais wetu”
Wajumbe wengine nao
wakaungana na Frank na wote
wakakubaliana kwamba endapo
mapinduzi yatafanyka basi Daudi
awe ndiye rais
“ Ahsanteni sana ndugu
zangu kwa kunikubalia ombi
langu.Kwa sasa nitatoa
ushirikiano wa kila namna ili
kufanikisha mpango huu”akasema
Daudi huku akitabasamu na
wajumbe wakampigia makofi
“ Ndugu zangu kuiangusha
serikalini ni mpango mpana sana
na wa siri kubwa.Ili tufanikiwe
kuna watu ambao lazima uwe nishirikishi .kwanza kabisa lazima
tutafute uungwaji mkono toka kwa
makamanda wa vikosi vya jeshi
ambao watatengeneza mtandao wa
askari watakaofanya uasi.Jeshi
litaipindua serikali na kukabidhi
madaraka kwa mtandao wetu kwa
maana hiyo lazaima tupate
makamanda wa jeshi ambao
watakuwa tayari kushirikiana
nasi.Pili tunatakiwa kuchochea
uhasama mkubwa na chuki kwa
raia dhidi ya serikali
yao.Tunatakiwa tulete aina Fulani
ya machafuko ambapo jeshi la
polisi litalazimika kutumia nguvu
kubwa katika kuyatuliza na
kusababisha vifo na katika
machafuko hayo sisi yatakuwa na
faida kwetu .Serikali itaonekana
imeshindwa kuwalinda raia wake
na inakiuka haki za binadamu na
hivyo wananchi hawatakuwa na
imani nayo tena.Tanzaniaitachafuka katika jumuia ya
kimataifa na hiyo itakuwa ni
sababu nyingine ya kutosha
kabisa kwa sisi kufanya
mapinduzi.Tutakapoingia
madarakani ndani ya kipindi
kifupi tutarejesha halali ya amani
na hivyo wananchi watakuwa na
imani na matumaini makubwa na
sisi.Katika kipengele hiki
tutawatumia wanasiasa wa vyama
vya upinzani.Hawa watapandikiza
chuki kwa katika jamii kwamba
serikali imewazuia mafuta wa
marekani na hivyo kuongoza
maandamano na migomo isiyo na
kikomo kuishinikiza serikali
iliyoko madarakani kuachia
ngazi.Migomo na maandamano
hayo yataandamana na vurugu na
hivyo kuilazimisha serikali
kutumia nguvu
kubwa.Tutawawezesha wanasiasa
hawa kifedha na watazunguka nchi nzima kuifanya kampeni
hii”David akanyamaza wajumbe
wakampigia makofi kwa mawazo
yake mazuri. Kisha wakaendelea
“ wanasiana hawa
wanachokipigania wa watanzania
bali maslahi yao binafsi kwa hiyo
kwa kutumia ushawishi wa fedha
tutaviunganisha vyama vyote vya
upinzani hiyo itaturahishishia
kutimiza lengo letu.Mimi nitawaita
viongozi hao wa vyama vya siasa
vya upinzani na kufanya nao
mkutano wa siri.Nitawashawishi
na watakubaliana
nami.Sintawaeleza kuhusiana na
mpango wetu wa kuiangusha
serkali lakini nitawahakikishia
kwamba endapo watafanya
kampeni hiyo na serikali iliyoko
madarakani ikaondolewa basi
mimi nitagombea urais kupitia
muungano wa vyama vya
upinzani.Baada ya mapinduzi viongozi hawa wa vyama vya siasa
tutawapatia nyadhifa mbalimbali
katika serikali ikiwa ni njia ya
kuwafunga midomo”akanyamaza
akainua glasi yake ya maji
akanywa na kuendelea
“ Kipengele cha tatu ambacho
tunatakiwa kukifanya ni
kuwashirikisha baadhi ya
viongozi kadhaa kutoka serikali
kuu,idara ya usalama wa
taifa.Jeshi la polisi na sehemu
yoyote ambayo tutayaona ina
manufaa.kwa upande wa serikali
kuu kuna mtu ambaye tunaweza
kumtumia.Makamu wa rais ndugu
Shafi Abdulkhareem Omari.Mzee
huyu hana maelewano mazuri na
rais na si mara moja kumetokea
mikwaruzano.Mzee huyu atatufaa
sana na atatusaidia katika mambo
mengi.Baada ya mapinduzi mzee
huyu ataendelea na wadhifa wake
wa makamu wa rais” akanyamaza tena na kuwatazama wajumbe
halafu akaendelea
“ hayo ndiyo mambo matatu
makubwa ambayo tunatakiwa
kuyafanya iwapo tunataka
mpango wetu ufanikiwe,Jeshi,
wanasiana na viongozi wachache
wa serikali na idara za usalama
.Tukifanikiwa kuzidhibiti sehemu
hizo basi tujue kwamba mpango
wetu utafanikiwa asilimia mia
moja .Kwa upande wangu mimi
nitashughulika na viongozi wa
vyama vya siasa na kuwaweka
chini na
watanisikiliza.Nitashughulika pia
na makamu wa rais pamoja na
vongozi wengine.Wote hawa nina
hakika ya kuwashawishi na
wakajiunga nasi.Upande wa jeshi
na sehemu nyingine
itakayoonekana kuwa na
umuhimu zitashughulikuwa na
watu wengine” akamaliza kutoa maoni yake Daudi .wajumbe
wakampigia makofi
“ Ahsnte sana mheshimwa
rais” akasema Frank na wote
wakacheka
“ tafadhali msicheke.Huyu
ndiye rais wetu mtarajiwa kwa
maana hiyo hakuna haja ya
kusubiri hadi mapinduzi yafanyike
ndipo tuanze kumuita rais.Mambo
yanaanza sasa kwani uhakika wa
kuchukua serikalini ni mkubwa
sana” akasema Frank
“ Nadhani nyote mmesikia
mheshimiwa David yeye ana
uzoefu mkubwa katika serikali na
ametupa mwangaza mkubwa sana
na muelekeo mkubwa.Bado
tunaendelea kuchukua maoni na
mitazamo ya kila mmoja wetu
hapa.Kabla sijaendelea zaidi
naomba na mimi niweke wazi
mbele yenu kwamba
nitashghulikia suala la jeshi.Nina ushawishi mkubwa kwa
makamanda wa vikosi mbalimbali
vya jeshi kwa hiyo naomba suala
hili niachiwe mimi na nitaliweka
sawa.Licha ya nguvu ya ushawishi
lakini mkumbuke pia kwamba
tuna fedha nyingi sana kwa ajili ya
kazi hii.kwa hiyo lazima fedha
itumike na panapo fedha hakuna
kinachoharibika” akasema Frank
na kisha wakaendelea na mjadala
******************
Kengele ya mlango wa
chumba cha Elvis ikalia na
kumuamsha toka usingizini.Toka
walipopata chakula cha mchana
alikuwa amelala kutokana uchovu
wa safari ndefu.Akajiinua kwa
uchovu na kutazama saa yake
.Ilipata saa kumi na mbili za
jioni.Akainuka akavaa shati na
kuelekea mlangoni.Akaufunguamlango na kukutana na
muhudumu
“ samahani kaka yule mgeni
wako uliyesema tumuandalie
chumba tayari amewasili”
akasema muhudmu
“ Doreen ?!!
“ Ndiyo kaka.Yupo mapokezi
anakusibiri”
“ Ok ahsante sana nakuja
sasa hivi”akasema Elvis na kuvaa
viatu vya wazi vilivyokuwamo mle
chumbani akatoka na kuelekea
mapokezi.Doreen alikuwa amekaa
katika sofa jeusi la pale mapokezi
na mara tu alimpomuona Elvis
akasimama na kumkumbatia
“ Elvis !! akasema Doreen
huku akiendelea kumkumbatia
Elvis kwa nguvu
“ Ahsante sana Doreen kwa
kuja.Karibu sana mbeya”
“Ahsante sana Elvis
.Ninashukuru nimefika salama.Njia nzima nilikuwa na
mawazo mengi sana kama uko
salama.”
“ Niko salama
Doreen.Hukupatwa na tatizo lolote
njiani?
“ Hapana sikupata tatizo
lolote .Gari hili bado jipya kabisa”
akasema Doreen
“ Patricia anaendeleaje?
Ulimweleza chochote kuhusiana
na safari hii?
“ Patricia anaendelea vizuri na
sikumweleza chochote kuhusiana
na safari hii na wala hajui kama
nimesafiri” akasema Doreen
“ Ahsante sana Doreen.Kwa
sasa naomba ujimwagie maji
halafu tupumzike kidogo kisha
tutapata chakula cha usiku.Tuna
maongezi marefu kidogo baada ya
chakula,” akasema Elvis na
kumpeleka Doreen katika chumba
alichokuwa amemuandalia Ouh jamani ! kwa nini
linapokuja suala la Elvis najikuta
siwezi kumkatalia kitu chochote ?
Nimeendesha gari toka Dar hadi
huku bila kujua nini
ananiitia”akawaza Doreen baada
ya Elvis kutoka mle
chumbani.Akavua koti na kulitupa
kitandani kisha akavua gauni lake
na kubakiwa na nguo ya ndani
“ Its cold like hell .Baridi
sana huku mbeya.Natamani kama
ningepata nafasi ya kulala na Elvis
leo..” Akawza Doreen akajifunga
taulo na kuingia bafuni akafungua
maji ya moto na kuoga
“ Kitendo cha patricia
kunitaka nizae na mume wake
Elvis kimeniweka katika wakati
mgumu sana .Kuna hisia za
tofauti nimeanza kuzipata kuhusu
elvis.Toka nilipolala naye siku ile
na kuyashika maungo yake nyeti
kila nikimuona mwili wote hunisisimka” akawaza Doreen
huku akiendelea kuoga.Picha ya
usiku ule akiwa mtupu amelala
kitandani kwa Elvis ikamjia
kichwani akatabasamu
“ Natamani usiku kama ule
ujirudie leo hii tena tukiwa huku
mbali ambako hakuna mtu wa
kumuogopa.” Akaendelea kuwaza
Doreen huku akijifuta maji
akarejea chumbani na kujilaza
kitandani akajifunika blanketi
kulikuwa na baridi kali na
taratibu kijiusingizi kikamchukua.
**************
Akiwa usingizini kwa mbali
alisikia kama mlango wa chumba
chake unagongwa.Mwanzoni
alidhani labda anaota lakini
mlango ulipoendelea kugongwa
akafumbua macho.Ni kweli kunamtu alikuwa anagonga
mlango.Akainuka na kuelekea
mlangoni akaufungua na
kukutana na sura yenye
tabasamu ya Elvis.Kwa muda wa
sekunde kadhaa Elvis alibaki
anakodolea macho kifua cha
Doreen .Kuna kitu kilimvutia pale
kifuani.Doreen aligundua kwamba
Elvis alikuwa amevutika na
sehemu ile ya kifua naye akabaki
amesimama na kumuacha Elvis
aendee kukisaili kifua chake.Elvis
akakohoa kidogo na kusema
“ Pole sana na uchovu Doreen
na samahani kwa kukuamsha”
“ Ahsante sana Elvis.Kuna
baridi sana huku na ndiyo maana
nikapitiwa na kijiusingizi.Karibu
ndani”
“ Doreen nimekuja kukutaarifu kwamba ni muda wa
kupata chakula cha usiku sasa.”
“ Ahsante sana Elvis.Nilikuwa
nimejisahau kabisa kuhusu
chakula.Karibu ndani Elvis na
mimi nijiandae twende “
“ Ahsante sana Doreen .Mimi
natangulia hotelini utanikuta
kule”
“ No Elvis.tafadhali nisubiri
tuongozane wote.karibu ingia
ndani”
“ Ok Doreen niko hapa nje
ninakusubiri”
“ Ingia ndani Elvis.Are you
afraid of me? C’mon I’m not a
ghost.Please come in” akasema
Doreen
“ ahsante Doreen.Badilisha
nguo na utanikuta hapa nje”
“ Ok Mr shy guy.Just wait for me here .I wont take long”
akasema Doreen na kuufunga
mlango akamuacha Elvis
amesimama pale nje
akimsubiri.Baada ya dakika tano
akatoka akiwa amevaa nguo nzito
za baridi wakaongozana hadi
sehemu ya chakula .Hakukuwa na
watu wengi zaidi ya raia wachache
wa kigeni .Elvis akamuongoza
Doreen hadi katika meaza moja
iliyokuwa pembeni ambayo
msichana mmoja mwenye umbo
dogo alikuwa amekaa
“ karibu Doreen” akasema
Elvis na kumvutia Doreen kiti
akaketi.Doreen na Graca
wakatazamana .Elvis akatabsamu
na kusema
“ Doreen samahani
sikukutaarifu toka mwanzo lakini katika safari yangu hii
nimeambatana na mtu
mwingine.Tafdhali kutanana
Graca Frank,Ni mtanzania
aliyekuwa nchini afrika ya kusini
na kwa sasa anaelekea Dar es
salaama” akasema Elvis halafu
akamgeukia Graca
“ Graca kutana na Doreen.Ni
mmoja kati ya marafiki zangu
wakubwa”
Doreen na Graca
wakasalimina na kisha
wakaendelea kupata mlo wa
usiku.Ni Elvis na Doreen pekee
waliokuwa wazungungumzaji pale
mezani.Graca alikuwa
kimya.Pengine ni kwa sababu ya
kutokuwa na mazoea nao ya
karibu
Baada ya kumaliza chakula Elvis akamsindikiza Graca hadi
chumbani kwake
“ kesho alfajiri na mapema
tunaanza safari ya kuelekea Dar
es salaam.Doreen amekuja na gari
ambalo ndilo tutalitumia.Sikutaka
tupande magari makubwa ya
abiria kwani sitaki uonekanae.
Kwa hiyo nitakuamsha alfajiri na
mapema kwa ajiili ya kuanza
safari.
“ Ahsante sana Elvis kwa
msaada wako .Sikujua kama una
moyo wa huruma namna
hii.Nakuahidi nikifika sehemu
salama nitakueleza kila kitu
ninachokifahamu”
“ Usihofu Graca.Uko salama
na utaendelea kuwa
salama.Nitakulinda siku zote na
hakuna mtu yeyote atakayekudhuru.Kwa sasa endelea
kupumzika” akasema Elvis na
kugeuka akaanza kuondoka.
“ is she yur girlfriend?
Akauliza Graca .Elvis ambaye
tayari alikwisha ushika mlango
akageuka
“ Unasemaje Graca? Akauliza
“ Doreen.Is she your
girlfriend? Akauliza tena Graca
“ We’re friends.Good friends”
akajibu Elvis
“ You look good together.Ok
Good night Elvis” akasema Graca
“ Good night” akasema Elvis
huku akitabasamu akaufunga
mlango na moja kwa moja
wakaelekea chumbani kwa Doreen
akagonga mlango Doreen
akaufungua .Elvis akaingia ndani
na kwenda kuketi sofaniKuna baridi sana
Elvis.Ninahisi nahitaji kupata
mvinyo” akasema Doreen akapiga
simu hotelini wamletee
mvinyo.Baada ya dakika mbili
muhudumu akawasili akiwa na
chupa ya mvinyo na glasi
mbili.Doreen akamimina mvinyo
ule katika glasi na kumpatia Elvis
glasi moja.
“Ni mara yangu ya kwanza
kufika Mbeya.Sikujua kama kuna
baridi kiasi hiki”akasema Doreen
huku naye akiketi sofani karibu
na Elvis
“ Mbeya ni mkoa wenye
baridi kali sana.Nimewahi kufika
mara kadhaa kwa hiyo
ninapafahamu vyema na ndiyo
maana nikakusisitiza usisahau
nguo za baridi” “Ahsante sana kwa
kunikumbsha.Bila hivyo sijui
ningefanya nini japokuwa hata
hivi sasa bado naisikia baridi kali
sana.” Akasema Doreen
“ Ok tuachane na hayo.Pole
sana na uchovu wa safari ndefu”
akasema David
“Ni safari ndefu
sana.Nashukuru nimefika salama
na sikupatwa na tatizo lolote
njiani”
Hongera kwa kuendesha gari kwa
umahiri mkubwa,wanawake wengi
hawawezi kuendesha gari kwa
umbali mrefu namna hii”
“Mimi nimekwisha zoea
kuendesha gari umbali
mrefu.Huwa ninaendesha gari
hadi Nairobi hadi Kampala bila
matatizo.” Akasema Doreen halafu kimya kikapita
“ Patricia aliniambai kwamba
umekwenda afrika ya kusini
lakini nikastuka uliponipigia na
namba za Zambia.Uliamua kurudi
kwa kutumia njia ya gari?akauliza
Doreen
“ Nlilazimika kutumia njia ya
gari badala ya ndege.Hii ni kwa
sababu ya Graca”
“Graca?! Doreen akashangaa
“ Graca amefanya nini?
“ Kilichonipeleka afrika ya
kusini ilkuwa ni kumfuata binti
huyu.”
“ Kwani Graca ni nani?
Kafanya nini? Akauliza Doreen
“ Siwezi kukueleza kwa
undani sana kuhusu yeye kwa
sababu ni mambo ya ndani sana
ya kikazi lakini kwa ufupi ni kwamba Graca ana taarifa
muhimu sana na maisha yake
yako hatarini na ndiyo maana
imenilazimu kumuondoa kule
afrika ya kusini”
“ wanataka kumuua ? !
Doreen akashangaa
“ Kwa miaka kadhaa sasa
amekuwa akiishi kwa mateso
makubwa na kwa taarifa alizonazo
lazima nichukue dhamana ya
kumlinda.”
“ Ouh Elvis pole sana”
“ Ahsante sana Doreen.lakini
hii ni mojawapo ya kazi
zangu.Nimekwisha zoea mambo
kama haya”
“ hao wanaotaka kumuua
wako wapi? Unawafahamu?
Akaulizia Doreen
“ wako afrika ya kusini na wengine wako hapa nchini na
ndiyo maana sikutaka kutumia
usafiri wa kawaida wa abiria kwa
nia ya kumficha.Toka afrika ya
kusini nimepita naye katika njia
za uficho ili asionekane.Baada ya
kufika hapa nimeona nitafute mtu
ambaye ninamuanini wa
kunisaidia na nimekuchagua
wewe.Ninakuamini sana Doreen
and please don’t let me down”
Doreen akatabasamu na
kusema
“ Elvis ahsante sana kwa
kuniamini.Naomba kuahidi
kwamba katu siko tayari
kukuangusha .Sijawahi na
sintofanya hivyo kamwe.Chochote
utakachokitaka toka kwangu
nitakupatia na ndiyo maana niko
hapa muda huu kwa sababu ulinitaka nije hapa.Feel free to tell
me anything,I mean anything”
akasema Doreen na uso wa Elvis
ukajenga tabasamu
“ nashukuru kwa maneno
yako mazito.Nitaendelea
kukuamini kwa siku zote za uhai
wangu.Kitu kikubwa nilichokuitia
hapa ni kwamba Graca anahitaji
msaada.kwanza kusafirishwa kwa
siri hadi Dar e s salaam na pili
kuhifadhiwa sehemu salama.Mtu
anayetishia maisha yake ni baba
yake mzazi ambaye ni afisa
mkubwa jeshini .Kuna mambo ya
siri anayoyafahamu Graca
kuhusiana na baba yake na
tumekubaliana kwamba ili
anieleze mambo hayo lazima
nihakikishe anakuwa
salama.Akisha nieleza nitamfanyia mpango wa kumuhamisha nchi na
kumtafutia makazi nchi nyingine
akaendelee na maisha yake .Kwa
mambo hayo mawili ninahitaji mtu
ambaye nina muamini sana”
akasema Elvis
Doreen akamtazama Elvis
usoni.Macho yalionyesha uoga
Fulani
“ Mbona unaogopa Doreen”
akauliza Elvis
“ Elvis I’m so scared” akasema
Doreen.Elvis akamsogelea
akamshika mkono na kumtazama
usoni
“ Do you trust me Doreen?
Akauliza
“ Ofcourse I do. I trust you”
akasema Doreen.
“ Thank you .That the only
thing I wanted to hear from you.So don’t be scared.You are
more than safe around me”
akasema Elvis na kumfanya
Doreen atabasamu
“ Tell me Elvis.What do
yuwant me to do?
“ kesho tutarejea dar es
salaam.Nataka sehemu ya
kumficha Graca,sehemu ambayo
hakuna watu wengi wanaingia
.Ninataka Graca akae nyumbani
kwako kwa muda wakati
ninamtafutia makazi mazuri”
“ Ahsante sana Elvis kwa
kuniamini na kuchagua Graca
akae kwangu.Sipingani na
mawazo yako lakini ninadhani
unahitaji kutafuta sehemu
ambayo ni salama zaidi .Pale
kwangu ni sehemu salama lakini
watu wengi huingia .Mimi ni mtu mwenye mazoea na watu wengi
kwa hiyo kuwazuia watu ghafla
wasifike nyumbani kwangu
kunaweza kuleta udadisi kidogo
na wakataka kujua kulikoni.Lakini
kuna wazo nimelipata”
“ wazo gani? Akauliza Elvis
“ Kuna rafiki yangu mmoja
ameolewa na mzungu na kwa sasa
mzungu huyo anarejea kwao.Kwa
kuwa anaondoka na mke wake
wameamua wauze kila kitu chao
hapa Tanzania .Nyumba yao ni
nzuri sana na yenye usalama wa
kutosha.Ina uzio mkubwa na ina
kila kitu ndani hadi bwawa la
kuogelea.Kama tukiona inafaa
tuinunue nyumba ile hata kwa
kulipa pesa nusu na baadae
tutamaliza deni taratibu.Nadhani
hii itakuwa ni sehemu nzuri sana kumuhifadhi Graca”akasema
Doreen na Elvis akatabasamu
“Hilo ni wazo zuri sana na
nyumba kama hiy ndiyo ambayo
ninaitafuta.Inauzwa shilingi ngapi
hiyo nyumba?
“ Mimi aliniambia kwamba
endapo ningempatia milioni
themanini basi angeweza
kunipatia nyumba hiyo kwa
sababu ni rafiki yangu lakini
thamni yake ni zaidi ya milioni
mia moja na hamsini.Ni rafiki
yangu mkubwa na tunaelewana
sana .Ninaweza kuongea naye na
bei ikashuka hata zaidi ya hapo na
tnaweza hata kumlipa kwa
awamu.”
“ kama ni hivyo hakuna haja
ya kusubiri zaidi .Ongea naye sasa
hivi na mwambie kwamba tutampaia shilingi milioni ishirini
za kuanzia na zitakazobaki
tutamlipa taratibu” akasema
Elvis.Doreen akachukua simu
yake na kumpigia huyo rafiki
yake wakaongea kwa zaidi ya robo
saa
“ Imekuwa bahati sana kwani
mpaka sasa hivi bado hajaiuza na
kesho wanaondoka kuelekea
Denmark.Amekubali kuchukua
kiasi hicho kilichopo cha fedha na
kilichobaki tutamlipa kwa kuwa
anaondoka kesho asubuhi sana
amesema kwamba funguo
nitaikuta katika kampuni ya ulinzi
ambayo wana mkataba wa
kumlindia.Kila kitu amekiacha
pale ndani hadi gari.
“ wow ! that’s great
news”akasema Elvis Naomba unipatie kompyuta
yako .Amekupa namba za akaunti
yake ya benki?
“ Amesema atanitumia muda
si mrefu”akasema Doreen huku
akilifungua begi lake na kutoa
kompyuta yake ndogo na muda
huo huo ujumbe mfupi ukaingia
katika simu yake
“ Tayari amenitumia akaunti
yake” akasema Doreen huku
akiziandika namba zile na
kumpatia Elvis ambaye alianza
mara moja zoezi la kuhamisha
pesa toka katika akaunti yake na
kuzipeleka katika katika akaunti
ya rafiki yake Doreen aitwaye
Amanda.Alihamisha kiasi cha
shilingi million ishirini na baada
ya dakika kumi Amanda akapiga
simu na kuthibitisha kwamba kiasi kile cha fedha tayari
kimeingia katika akaunti yake
“ Huu ndio uzuri wa
teknolojia.Imerahisisha sana
ufanyaji wa biashara.Ingekuwa ni
zamani ingenilazimu mpaka
kwenda benki na kuchukua kiasi
hicho kikubwa cha fedha.Ahsante
sana Doreen kwa msaada
wako.Umenisaidia kitu kikubwa
sana”akasema Elvis.Doreen
akatabasamu ,kikapita kimya
kifupi Doreen akasema
“ Arent you going to involve
Patricia in this ? akauliza
Doreen.Elvis akainama akafikiri
na kusema
“ Nitamfahamisha lakini si
sasa”
“ kwa nini hutaki
kumshirikisha katika suala hili? Don’t you trust her? Akauliza
Doreen
“ I trust her lakini kwa sasa
sitaki kumuhusisha katika suala
hili sitaki kumuongezea
matatizo.Ana mzigo mzito
unaomuelemea hivi sasa,sitaki
kumbebesha mzigo zaidi.Alionao
sasa unamtosha sana” akasema
Elvis kwa uchungu
“ Nakubaliana nawe Elvis
.matatizo aliyonayo Patricia ni
makubwa na hahitaji kuongezewa
matatizo zaidi” akasema Doreen
kimya kikapita
“ Unafikiria nini Elvis
kuhusiana na suala hili?
“ Suala gani Doreen?
“ Suala la Patricia”
“ Doreen suala la Patricia
kukosa mtoto sina namna ya kulitafutia ufumbuzi na hakuna
namna ya kufanya ili aweze
kupata mtoto.Patricia ni rafiki
yako mkubwa na nina imani
amekwishakueleza tatizo lake
kwamba hawezi kubeba
mimba.Kizazi chake kilikwisha
ondolewa.I was there when it
happened.Hakuna wa kumlaumu
kwa kilichotokea kwani bila
kufanya vile angepoteza
maisha.Ninampenda Patricia na
nilimpenda huku nikiyafahamu
matatizo yake na nilipomuoa
nilikwisha jiandaa kisaikolojia
kwamba sintakuwa na mtoto
maishani kwa sababu mke wangu
hana uwezo wa kunizalia
mtoto.Suala hili mimi haliniumizi
kichwa hata kidogo
.Kinachomsumbua Patricia kwa sasa ni maneno ambayo yameanza
kujitokeza toka kwa ndugu zangu
wakidai kwamba tumechukua
muda mrefu toka tulipooana bila
ya kuwa na mtoto.Ndugu zangu
wanadai mtoto .Haya ni matatizo
ya kawaida na ambayo
ninauhakika baada ya suala hili
kumalizika nitayaweka
sawa.Sintampa nafasi ndugu
yeyote kuingilia ndoa yangu.Huu
ni upepo tu naamini utapita na
mimi na mke wangu tutabaki
salama” akasema Elvis
“ yah ! hata mimi naomba iwe
hivyo.Patricia anateseka sana.”
“ usijali suala hili litakwisha
tu”akasema Elvis ingawa
ilionekana wazi kwamba alikuwa
akiumia sana moyoni.Doreen
akasema Elvis nafahamu unampenda
sana patricia na kwa hilo siwezi
kupingana nawe.Pamoja na hayo
naomba uwe muwazi kwangu ni
kweli hautaki kuwa na mtoto
katika maisha yako?Hautaki
kuitwa baba katika maisha yako?
Hautaki kumpata mrithi wa mali
zako? Please be honest with me”
Elvis akaninama na
kuonekana kuzama katika
mawazo.Suala aliloulizwa na
Doreen lilionekana kumchanganya
sana
“ Answer me Elvis” akasema
Doreen baada ya ukimya kutawala
mle chumbani.Elvis akainuka na
kwenda dirishani akafunua pazia
na kutazama nje halafu akageuka
na kwenda kuchukua glasi yake
na mvinyo akanywa kidogo. “ Doreen swali uliloniuliza ni
gumu sana na sijui nikujibu nini”
" Just be Honest with me”
akasema Doreen.Elvis akafikiria
tena kidogo na kusema
“ Ukweli ni kwamba hakuna
mwanandoa ambaye hapendi
kuwa na mtoto.Kila mmoja
angependa apate mtoto tena hata
zaidi ya mmoja.Kuna nyakati
huwa najitazama namna
ninavyoishi na mke wangu na
ninaona furaha yetu ingekuwa
maradufu endapo tungepata
mtoto.Kwa wazazi wangu mimi ni
mtoto wao wa pekee na hawana
mtoto mwingine.Kabla hajafariki
baba yangu alituachia mali nyingi
na mrithi pekee ni
mimi.Ningependelea kuwa na
mtoto ambaye angerithi mali hizi zote lakini uwezo huo haupo.Mke
wangu wa ndoa hana uwezo wa
kupata mtoto.Hili si suala dogo
hata kidogo ni suala zito lakini
ninamshukuru Mungu kwa
kunipa nguvu na uwezo wa
kulikabili suala hili.Toka awali
nilikwisha jitayarisha kisaikolojia
kwamba sintakuwa na mtoto
ingawa kuna nyakati huwa
ninatamani sana mtoto lakini
uwezo huo haupo tena:” akasema
Elvis .Doreen aliyekuwa kimya
akimtazama akainua Glasi yake ya
mvinyo akanywa na kusema
“ Pole sana Elvis.Ahsante pia
kwa kuwa muwazi kwangu.Najua
ni suala gumu lakini bado
unaweza kulipatia ufumbuzi”
“Ufumbuzi gani Doreen?
“Patricia anakupenda sana na amekwisha usoma moyo wako na
akafahamu kabisa kwamba
unatamani kuwa na mtoto na
ndiyo maana akakupa ruhusa ya
kutafuta mwanamke uzae naye
mtoto.Huu si uamuzi mwepesi
lakini ameweza kuufanya ili
maisha yenu yaweze kuwa na
nuru na furaha,”
“ I cant do that Doreen,I
swear I cant” akasema Elvis
“ kama mkeo tayari
amekwisha kuruhusu unashindwa
nini? Kwa nini uendelee kumtesa
mkeo?
“ Siwezi kufanya hivyo kwa
sasa nafahamu atateseka zaidi
pale nitakapozaa nje ya
ndoa.Niliapa mbele ya altare
kwamba nitampenda Patricia
katika shida na raha .Tuko katika wakati wa shida hivyo lazima
niishi kiapo change cha kumpenda
zaidi hasa wakati wa
shida”akasema Elvis
“ Patricia hawezi kuteseka
kwani tayari amekwisha jiandaa
kwa hilo na kizuri zaidi
amekwambia kwamba
atakutafutia mwanamke
anayemuamini na akanichagua
mimi.Hata hapo bado
haiwezekani?
“Doreen nimekwisha kwambia
kwamba siwezi kufanya hivyo hata
awe nani na hakuna
atakayenishawishi nifanye hivyo”
Doreen akamtazama kidogo na
kuulzia
“ Elvis be honest with
me.Kinachokufanya ulipinge suala
hili kwa nguvu zote ni kwa sababu ya upendo wako kwa Patricia au
there is something else?
“What ?! akauliza Elvis
“ Ina maana hujanisikia?
Nimekuuliza kwamba
kinachokufanya ulipinge suala hili
la kutafuta mtoto nje ya ndoa
wakati mkeo amekwisha kupa
ruhusa hiyo ni upendo wako kwa
Patricia au kuna sababu nyingine?
“ Kwa nini unaniuliza hivyo
Doreen wakati jibu unalifahamu
kwamba nilimpenda Patricia kwa
namna alivyo na ndiyo maana
siwezi kufanya kitendo kama
hicho anachonitaka nifanye.Siwezi
kufanya jambo lolote kinyume na
kiapo cha kanisani”
“ Elvis you are my friend
.Please be honest with me”
“Be honest with you? yes be honest with me .Is
everything ok with you?
“Doreen sikuelewi
unamaanisha nini kuniuliza
hivyo?
“ Namaanisha kuhusu uwezo
wako wa kumpa mimba
mwanamke.Una hakika uko sawa?
“ I am ok.Una wasi wasi naweza
kuwa na kasoro ndiyo maana
ninalipinga wazo la kuzaa nje ya
ndoa? Ondoa shaka kuhusu
hilo.Hata kama ingekuwa ni kweli
basi ingebaki kuwa ni siri yangu
na mke wangu lakini kukujibu
swali lako ni kwamba mimi sina
kasoro ni rijali kama wengine na
uwezo wangu siutilii mashaka
hata kidogo” akasema Elvis
“ Mhhh ! I nina mashaka”
akasema Doreen “ Kwa nini unakuwa na
mashaka Doreen?
Doreen akanywa kidogo kinywaji
na kusema
“ Nina wasi wasi kwa nini
hutaki mtoto wakati mke wako
amekwisha kupa ruhusa ya
kutafuta mtoto nje ya ndoa. Kama
ungekuwa huna kasoro
usingekataa”
“ Doreen mbona unasisitiza
sana kwamba nina matatizo? Sina
tatizo lolote .Mimi ni mzima
kabisa”
“ Can you prove that to me?
“ Prove what ? akauliza Elvis
“ That you are ok”
“ kwa nini nidhihirishe
kwako? Wewe hupaswi kufahamu
masuala kama hayo na hata kama
nikiwa na tatizo ni suala langu la ndani na hapaswi mtu mwingine
kufahamu”
“ Mhh ! I’m curious” akasema
Doreen na kumsogelea Elvis
“ Usiogope Elvis.Please come
closer” Akasema Doreen
“ Unataka kufanya nini
Doreen? Akauliza Elvis lakini
tayari Doreen alikwisha upeleka
mkono wake kunako ikulu na
muda ule ule ikulu
kukachachamaa
“ stop that Doreen.what are
you dong?akasema Elvis kwa sauti
ya juu.Doreen akatabasamu na
kusema
“ relax Elvis.Nilitaka tu
kuhakikisha mambo yako
sawa.Nimeamini uko sawa.”
Elvis akamtazama Doreen
usoni na kusema Doreen kwa nini
unaf…………” kabla hajamalizia
sentensi yake Doreen akasema
“ Relax Elvis,relax.Hakuna
tatizo kila kitu kiko ok” akasema
Doreen.
Bado Elvis aliendelea
kumtazam Doreen usoni kwa
macho makali.Hakuamini kama
angeweza kufanya kitendo kama
kile cha kumshika maeneo nyeti
“ Ok Elvis,let us get back to
our serious business” akasema
Doreen
“ Subiri kwanza.Doreen kwa
nini umefanya kitendo kile?
Akauliza Elvis.Doreen akainua
glasi yake akanywa na kusema
“ Ok Elvis ,unataka kufahamu
ni kwa nini nimefanya vile? Huu
hapa ni ukweli.Ukotayati kuufahamu? Akauliza
“ Ndiyo.Niambie kwa nini
umefanya kitendo kile ?
“ Ukweli ni kwamba nilihitaji
kuwa na uhakika kama kila kitu
kiko vizuri na hauna kasoro
yoyote.Ninahitaji ukubali kuzaa na
mimi mtoto kwa ajili ya
Patricia.Anateseka sana kwa
jambo hili.Sielewi ni kwa nini
unakuwa mgumu sana
kukubaliana na mke wako kuhusu
suala hili.Mimi nimekwishakubali
kumsaidia Patricia na niko tayari
muda wowote kuzaa na wewe
lakini kwako limekuwa ni suala
gumu .Kwa nini Elvis? Akauliza
Doreen
Elvis akavuta pumzi ndefu na
kusema
“ How much she paid you? Elvis namba usinielewe
vibaya .Nilikubali kwa moyo
mweupe kumsaidia Patricia na
wewe pia kumpata mtoto na si
kwa sababu ya pesa.I have my
own money,I have millions of
money na sina shida ya
pesa.Nimejitolea tu kumsadia
rafiki yangu anayeteseka sana na
wala usione ninakulazimisha
ukadhani labda nina mapungufu
ama ninataka kuwa mke wako wa
pili la hasha .Sina lengo hilo bali
nia yangu ni kuwasaidia ninyi
,wewe na mkeo kupata mtoto ili
ndoa yenu iwe na furaha.Mkeo
yuko tayari kwa jambo hilo wewe
ndiye unayekwamisha“ akasema
Doreen.Chumba kikawa kimya
kabisa.Kila mmoja alikuwa
akiwaza lake.Elvis akasema I don’t know what to say
Doreenm,wewe na Patricia
mmeniweka katika wakati mgumu
sana”akasema Elvis
“ You don’t have to say
anything Elvis.Unachotakiwa
kufanya ni maamuzi tu.Ingia
katika moyo wa Patricia na
uangalie ni namna gani anateseka
kwa kukosa mtoto.Kwa taarifa
yako hakuna kitu kinachomtesa
mwanamke kama kukosa
mtoto.Think carefully about this”
akasema Doreen
“ I don’t know Doreen.I real
don’t know what t do right now.I’m
so confused” akasema
Elvis.Doreen akamshika bega na
kusema
“ Elvis suala ni gumu na
linahitaji maamuzi magumu so think like a man and make
decision like a man.I’m not forcing
you to do it but promise me that
you’ll think about this” akasema
Doreen
Elvis akaniama akafikiri kidogo
na kusema
“ Ok Doreen.I’ll think about
that” akasema Elvis
“ Ahsante sana Elvis.Sasa
naomba ukapumzike kwani kesho
tuna safari ndefu ya kurejea Dar ”
akasema Doreen .Elvis akainuka
“ Ahsante sana Doreen .Ngoja
nikapumzike.Nitakuamsha kesho
alfajiri na mapema kwa ajili ya
safari” akasema Elvis huku
akianza kupiga hatua kuelekea
mlangoni.Akaufungua mlango na
kabla hajatoka Doreen akamuita
“ Elvis !! .Elvis akageuka Sweet dreams” akasema Doreen
“ Goodnight Doreen’ akasema
Elvis na kuufunga
mlango.Taratibu akatembea
kueleka katka chumba chake
akaingia na kujtupa kitandani
“Najua Patricia anaumia sana
na suala hili lakini sina namna ya
kufanya.Siwezi kuzaa nje ya ndoa
hata kama yeye ameridhia nifanye
hivyo.Sijui ni kitu gani
kimemuingia Patrcia na kumfanya
awaze mambo haya na kunitaka
nizae na rafiki yake Doreen.Lakini
ngoja kwanza niliweke pembeni
suala hili nishughulike na suala
zito lililoko mbele yangu la
Graca.Nitakaa na patricia na
kuongea naye kwa kina kuhusiana
na suala hili na nitamuelewesha
athari zake.Hata mimi sipendi kumuona akiumia lakini huu ni
msalaba wetu lazima tuubebe
wote” akawaza Elvis na kulala
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 24

Habari ni nzuri nani
mwenzangu? Akauliza Frank
“Ninaitwa Dr Susan napiga
simu toka katika hospitali na
magonjwa ya akili anakotibiwa
mwanao Graca.”
“ Oh! Dr Susan.Nimestushwa
sana na simu yako usiku
huu.Kwema huko? Akauliza
“ Huku si kwema.Kuna jambo
limetokea mchana wa leo”akasema
Dr Susan na kuzidi kumtia hofu
Frank
“ Jambo gani limetokea?
Mbona unanipa hofu namna
hiyo?akauliza Frank
“ Graca amepotea na mpaka
sasa hivi hatujui yuko wapi”
“ What ?!!...Frank akahamaki
“ Nakutaarifu kwamba
mwanao Graca ametoweka mchana wa leo na mpaka muda
huu hajaonekana.Juhudi za
kumtafuta zinaendelea
tukishirikiana na vyombo vya
usalama”
“ Dr Susan jambo hili
limetokeaje?hakukuwa na ulinzi
hapo hospitali hadi mwanangu
akatoroka? Akauliza Frank
“ Badohakuna anayefahamu
nini kilitokea hadi Graca
akatoweka.Tumewachia jukumu
hili vyombo vya usalama
vichunguze .Usiwe na hofu
tunalishughulikia suala hili kwa
karibu sana na tunaamini Graca
hatakuwa mbali na hapa”
“ Dr Susan bado maelezo
yako hayajitoshelezi? Nieleze kwa
ufasaha mwanagu amepoteaje
wakati hapo hospitali kuna ulinzi na wagonjwa wote wanakuwa
chini ya uangalizi maalum?
Akauliza Frank kwa ukali
“ Tukio hili hata sisi
limetustua sana.Awali tulidhani
yuko katika maeneo ya hapa
hospitali lakini saa moja za jioni
wakati tunapitia wagonjwa wote ili
kuhakikisha wako wote Graca
pekee ambaye
hakuonekana.Tulianza juhudi za
kumsaka kila kona ya hospitali
lakini hakuonekana ikatulazimu
kutoa taarifa kwa vyombo vya
usalama na tayari wamekwisha
fika na wanaendelea na zoezi la
kumtafuta.Nitawasiliana nawe kila
mara nitakapopata ripoti toka
kwao.Nakuhakikishia kwamba
tunafanya kila linalowzekana
kuhakikisha Graca anapatikana kwani ni mgonjwa na anahitaji
matibabu.Picha yake itasambazwa
katika kila kona na watu
watatusaidia kumtafuta.Tahadhari
imekwisha tolewa pia kwa wote
wanaoishi jirani na hospitali
kwamba kuna mgonjwa
ametoweka hospitali kwa hiyo
watakapomuona watoe taarifa
haraka sana hapa hospitali au
katika kituo chochote cha
polisi.Ninahakika mpaka kesho
asubuhi tutakuwa na taarifa nzuri
zenye kutia matumaini” akasema
Dr Susan
“ Ok ! Ahsante sana Dr Susan
kwa taarifa japokuwa ni taarifa
zenye kustusha sana.Naomba
unipe taarifa kila hatua
inayofikiwa” akasema Frank usijali Frank.Nitawasiliana
nawe kila mara kukupa taarifa”
akasema Dr Susan na kukata
simu.BadoFrank aliendeelea
kutazama juu akiwa na mawazo
mengi
“ Hii imetokeaje?Graca
amepoteaje? Amewezaje kutoroka
pale hospitali wakati kuna ulinzi
mkali? Akajiuliza Frank halafu
akachukua simu yake na
kuzitafuta namba Fulani akapiga
“hallow Bonny.” akasema
Frank baada ya simu kupokelewa
“Hallow Frank”ikajibu sauti
ya upande wa pili
“Bonny hebu nieleze nini
kimetokea? Ninakulipa fedha
nyingi kila mwezi wewe na
mwenzako kwa ajili ya kumlinda
mwanangu imekuaje leo ninapokea taarifa kwamba
amepotea? Akauliza Frank kwa
ukali
“ Frank utaniwia radhi lakini
nilikuwa katika hatua za
kukutaarifu kilichotokea.Ni kweli
Graca ametoweka na sote
tumeshirikiana kumtafuta bila
mafanikio.Kuna kitu kilitokea
ambacho nakiunganisha na tukio
hili la kutoweka kwa Graca”
“ Nini kilitokea ? akauliza
Frank
“ Mchana wa leo kuna watu
wawili walifika hapa na mmoja
wao akawa akiongea na Graca
bustanini.Nilifanikwia kupata
picha yake toka kwa mbali
nitakutumia muda si mrefu ili
uweze kumuona mtu huyo ni nani
na kama unamfahamu ama vipi.Baadae watu hao waliondoka
na walifanyiwa ukaguzi getini ila
hawakuwa na kitu chochote
.Tunachoshindwa kuelewa ni
kwamba Graca ametoweka vipi?
Kuna uzio mkubwa na hawezi
kuruka.Kama ni hivyo amewezaje
kutoweka? Lakini wasiwasi wangu
upo kwa wale jamaa wawili.Lazima
kuna kitu wanakifahamu kuhusu
kupotea kwa Graca”akasema Bony
“Nitume picha za watu hao
haraka”akasema Frank na baada
ya dakika moja picha
zikaingia.Akaziangalia picha zile
na kuhsi kwa mbali kijashi
kinamtoka.
“Mungu wangu
…..Elvis!!..akasema Frank kwa
sauti ndogo ya mshangao.Kwa
dakika mbili alibaki anaziangalia picha zile katika simu yake na
mara akakumbuka kwamba kuna
kikao kinachoendelea
akakurupuka na kurejea kikaoni
Kikao kiliendelea hadi
ilipotimu saa tisa za usiku ndipo
kilipomalizika kwa makubaliano
kwamba siku itakayofuata
wakutane tena nyumbani kwa
Daudi Sichoma kwa ajili ya
mikakati zaidi.Wajumbe
wakaagana na kutawanyika.Frank
na Pascal Situmwa
wakawapeleleka akina Alhafidh
hotelini walikofikia kisha
wakaagana nao kwa miadi ya
kuonana tena asubuhi kabla
hawajaelekea uwanja wa ndege
kwa ajili ya kuondoka nchini
“Pascal we need to talk”
akasema Frank wakati wakishuka ngazi za hoteli kuelekea katika
maegesho ya magari.Pascal
akaonekana kustuka kidogo
akageuka na kumtazama Frank
akagundua kuna kitu hakikuwa
sawa.
“ Frank are you ok?akauliza
Pascal
“ No ! I’m not ok”akajibu
Frank
“ Nini kimetokea Frank? Toka
ulipotoka mle kikaoni ukaenda
kuongea na simu kuna kitu
nilikigundua.Haukuwa sawa
kabisa.Whats wrong? Akauliza
Pascal
“ Pascal tuna tatizo” akasema
taratibu Frank huku akiufungua
mlango wa gari akaliwasha
wakaondoka.Mara tu walipotoka katika geti la hoteli Pascal
akauliza
“ Frank kuna tatizo gani?
Fran akavuta pumzi ndefu na
kusema
“ Graca ametoroka hospitali
na hajulikani alipo”
“ Graca !! ametoweka
vipi?Hospitali hiyo haina ulinzi?
Akauliza pascal
“ Ulinzi upo tena mkali sana”
“ sasa ametoroka vipi kama
kuna ulinzi?.akauliza
pascal.Frank akapunguza mwendo
wa gari akachukua simu yake na
kumuonyesha Pascal
“ Elvis Tarimo” akasema
Frank
“ Elvis !!!!!..Pascal akastuka
“ Unamfahamu vizuri Elvis? “Ndiyo ninamfahamu vizuri.Ni
mfanyakazi wa idara ya ujasusi ya
taifa.Inasmekana ni mmoja kati ya
watu tegemeo sana katika idara
yake.Elvis anahusiana nini na
kupotea kwa Graca?akauliza
Pascal
“ Elvis alionekana akiongea
na Graca na baadae jioni Graca
hakuonekana tena”
Sura ya pascal ikaonyesha
uoga mkubwa.Safari ikaendelea
kimya kimya.Pascal alionekana
kuwa na mawazo mengi sana
“ Pascal unawaza nini?
Akauliza Frank baada ya
kumuona Pascal akiwa amezama
katika lindi la mawazo
“ Frank we have a problem”
akasema Pascal “ yes I know that we have a
problem” Akasema Pascal
“ Ninavyomfahamu Elvis
mpaka afikie hatua ya kwenda
kuonana na Graca basi lazima
kuna jambo amekwisha
linusa.Something is not right ”
akasema Pascal
“ Ninachojiuliza ni kwamba
kwa nini akaongee na Graca ?Nina
wasi was kuna jambo
ameligundua kuhusiana na
nyaraka zile zilizokuwamo katika
komputa ile aliyoiba Graca na
mama yake.Graca ni mtoto wangu
lakini nilifanya kosa kubwa sana
kumuacha hai mpaka sasa hivi”
akasema Frank
“Una hakika Elvis anaweza
kuwa amezipata nyaraka hizo?
Akauliza Pascal Sina hakika kama atakuwa
amezipata kwa sababu kama
tayari angekuwa nazo basi
asingesumbuka kwenda kuonana
na Graca.Ninachohisi mimi ni
kwamba kuna kitu atakuwa
anakihisi au kuna fununu fulani
anazo na ndiyo maana anafanya
uchunguzi.Kama nyaraka zile
angekuwa nazo mikononi toka
zilipopotea basi tungekuwa
tunaongea mambo mengine hivi
sasa”akasema Frank
“So what are we going to do?
Akauliza Pascal
“ Tunatakiwa tukabiliane na
suala hili haraka sana.Kwanza
tunatakiwa kuhakikisha kwamba
Graca anapatikana na vile vile
tunatakiwia kumdhibiti
Elvis.Tunatakiwa tufahamu ni kitu gani anakijua kuhusiana na sisi”
akasema Frank.Pascal akazama
tena mawazoni
“ Frank unakumbuka niliwahi
kukwambia kwamba pochi yangu
ndogo iliyokuwa na kumbu kumbu
zangu muhimu iliwahi kupotea
pale nyumani kwangu?
“Ndiyo nakumbuka.Nadhani
msichana yulealiyeiiba aliuawa”
“Ndiyo .Niliwatuma vijana
wangu wamzimishe kabisa kwani
niliamini lazima kuna mtu
alimtuma aniibie pochi ile.Kuna
jambo ambalo nimelikumbuka
sasa hivi”
“Jambo gani Pascal?
“Ni hivi majuzi tu kuna mtu
alingia pale nyumbani kwangu
lakini hakuiba kitu
chochote.Alionekana wakati akitoka kwa hiyo vijana
hawakuweza kumjua ni
nani.Ninaanza kuhisi kwamba
huenda mtu huyu naye alitumwa
kuja kuchunguza kitu pale
kwangu.Nina wasiwasi kwamba
huenda tukawa tumejulikana
mambo yetu na hivyo wanaendelea
kutuchunguza na kukusanya
ushahidi wakutosha.Nadhani hata
Elvis kwenda kuonana na Graca ni
sehemu ya uchunguzi
unaoendelea.Elvis anataka kupata
taarifa toka kwa Graca.Endapo
kuna mambo ambayo Graca
anayafahamu kuhusu sisi hatasita
kumweleza Elvis.Kwa sasa nina
uhakika mkubwa kwamba ni Elvis
ndiye aliyemtorosha Graca.Swali la
kujiuliza ni je wako wapi?
Akasema Pascal. Yule mtoto nina hakika
tayari atakuwa anafahamu mambo
mengi kuhusiana na sisi na
ninahisihatasita kumweleza Elvis
kila kitu
anachokifahamu.Kumuacha hai
lilikuwa kosa kubwa
sana”akasema Frank
“Pascal una hakika yule
msichana alikufa? Pascal
akastuka kwa swali lile.hakuwa
amelitegemea
“ Ndiyo nina hakika .kwani
vipi?
“ I’m just Curious”
“Vijana niliowatuma waifanye
kazi ile walinihakikishia kwamba
wamemuua na kumtupa bonde la
mpunga”
“ Ulifanya kosa kuwaamini na
kuwaacha wakaifanya kazi ile peke yao.Ulitakiwa uwepo na
uhakikishe kwamba ni kweli
amekata pumzi”
“ Mbona unaonyesha wasi
wasi Frank?
“ Kuna kitu
ninakihisi.Naomba kesho ulifanyie
uchunguzi suala hili kama ni kweli
alikufa ama vipi” akasema Frank
“ Vijana walinihakikshia
kwamba yule binti amefariki na
wakamtupa lakini ushauri wako si
mbaya.Ninafahamiana na wakuu
wa polisi wa vituo karibu vyote
hapa jijini.Nitawasiliana nao ili
nijue kama katika tarehe ile kuna
maiti yoyote iliokotwa.Mpaka
kesho saa nne tayari tutakuwa na
jibu”
“Good”akasema Frank na
kukanyaga pedeli ya mafuta gari ikaongeza mwendo kuelekea
nyumbani kwa Pascal
“ Pascal kesho asubuhi kitu
cha kwanza unachotakiwa
kukifuatilia ni iwapo Elvis yupo
hapa nchini au hayupo.Kama
hayupo tutapata uhakika kwamba
ni kweli alikwenda afrika ya kusini
kuonana na Graca.Baada ya hapo
tunatakiwa tufahamu pia kama
alitumwa afrika ya kusini kikazi
.Kama alitumwa kikazi alitumwa
kazi gani?Lazima tuchukue
tahadhali za mapema na hasa
katika wakati huu mbao
tunakabiliwa na mpango mzito
mbele yetu.Elvis mtu yeyote
hatakiwi kuwa kizingiti
kwetu.Yeyote yule ambaye
ataonekana kama hatari kwetu tutamuondoa haraka sana”
akasema Frank
“ Kesho ni siku yetu ngumu
sana.Tuna mambo mengi ya
kufanya .Kesho ni mwanzo wa
harakati mpya”akasema Pascal
huku akishuka garini wakaagana
Frank akaendelea na safari
kuelekea kwake
“ Elvis tarimo !!.. akasema
Frank kwa sauti ndogo
“ Huyu kijana bado
hajanifahamu mimi ni nani.I
swear nitamkata kauli sekunde
chache nikigundua kwamba
amekuwa akinifuatilia mambo
yangu.Safari hii ameingia sehemu
mbaya sana” akawaza Frank
akiwa njiani kuelekea kwake.
******************** Saa tatu za usiku ndege ye
jeshi la afrika kusini iliyokua
ikiwapeleka wanajeshi wa afriak
kusini katika mazoezi ya pamoja
ya kijeshi nchini Zambia ikatua
katika uwanja wa ndege wa kijeshi
uliopo nje kidogo ya jiji la
Lusaka.Ndani ya ndege hiyo
walikuwamo pia Elvis na
Graca.Ilikuwa ni safari ngumu
kwa Graca kwani hakuwahi
kusafiri na ndege za kijeshi ila kwa
Elvis ilikuwa ni moja ya safari
zake za kawaida
Ndege ilisimama lango
likafunguliwa na wanajeshi
wakashuka.Kiongozi wa msafara
ule Meja Tsemaleke Suso
akawaongoza Elvis na Graca hadi
katika gari dogo la jeshi
wakapanda.Wanajeshi wengine
wakaingia katika katika gari kubwa na safari ya kuelekea
katika kambi ya kijeshi
ikaanza.Baada ya kukatisha mitaa
kadhaa ya mji wa Lusaka
hatimaye Meja Tsemaleke
akamuamuru dereva wa lile gari
walilopanda akina Elvis
asimamishe gari katika mtaa
Fulani wenye maduka mengi
akashuka na kuwaomba akina
Elvis nao washuke
“ kwa mujibu wa maelekezo
niliyopewa na Bongani ni kwamba
niwafikishe hapa na toka hapa
kuna mtu ambaye atawachukua
na kuendelea na safari yenu”
akasema Meja Tsemaleke
“ Ahsante sana Meja kwa
msaada wako huu mkubwa”
akasema Elvis huku akipeana
mkono na MejaTsemaleke
wakaagana akarejea garini
wakaendelea na safari yao
Elvis na Graca walisimama pale mahala waliposhuswa nje ya duka
moja lililokuwalimefungwa.Huu ni
mtaa wa maduka na bado maduka
kadhaa pamoja na sehemu za
kuuzia vyakula na vinywaji
yalikuwa wazi.Graca alionekana
kuwa na wawi wasi mwingi
“ Nini kinaendelea baada ya
hapa? Akauliza
“ Usiwe na wasi wasi Graca
tutafika tu Tanzania” akasema
Elvis na baada ya kama dakika
tano mlango wa gari lililokuwa
limeegeshwa mita chache toka
pale walipokuwa wamesimama
akashuka mtu mmoja aliyekuwa
amevaa kofia nyeusi ya duara na
koti refu jeusi.Mtu yule alisimama
nje ya gari lake akaangaza angaza
pande zote kisha akaanza
kutembea taratibu kuwafuata
akina Elvis
“ Hallow” akawasalimu
“ Hallo” akajibu Elvis Elvis? Yule jamaa akauliza
“ Stanley? Elvis naye
akauliza.Yule jamaa akaitika kwa
kichwa kisha wakashikana mikono
wakasalimiana halafu
akawaongoza hadi katika gari lake
wakaingia lakini kabla
hawajaondoka akamgeukia Elvis
“ Elvis Maelekezo niliyopewa
ni kuwafikisha mpakani mwa
Tanzania na Zambia na
kuhakikisha mnafika salama
nchini kwenu.Niko sahihi?”
akasema Stanley
“ Uko sahihi Stanley.Hilo
ndilo hitaji letu kubwa” akajibu
Elvis na Stanley ambaye
alionekana ni mtu asiyependa
maongezi mengi akawasha gari na
kuondoka
“ Stanley samahani naweza
kutumia simu yako kupiga
Tanzania? Akasema Elvis .Bila
kujibu kitu Stanley akampatia Elvis simu yake.Elvis akaandika
namba alizotaka kupiga na
kubonyeza kitufe cha kupigia simu
ikaanza kuita na baada ya muda
ikapokelewa
“ Hallo “ ikajibu sauti tamu ya
kike upande wa pili
“ Hallow Doreen..” akasema
Elvis
“ Elvis !! Doreen akastuka
“ Ndiyo Doreen” akasema
Elvis na kumsikia Doreen
akishusha pumzi
“ Patricia aliniambia kwamba
umesafiri kwenda afrika ya kusini
mbona unanipigia na namba ya
simu ya Zambia? Akauliza Doreen
“ Ndiyo nilikwenda afrika ya
kusini lakini kwa sasa niko
Zambia” akajibu Elvis na kimya
kifupi kikapita
“ Doreen are you there?
Akauliza Elvis
“ I’m here Elvis” Good.Doreen unakumbuka
uliniambia kwamba uko tayari
kunisaidia kwa jambo lolote ?
“ Ndiyo nakumbuka Elvis
.Unataka nikusaidie kwa jambo
gani? Sema chochote niko tayari”
akasema Doreen
“ Naomba kesho alfajiri na
mapema uchukue gari lako lile
jipya na uanze safari ya kuelekea
jijini Mbeya.Nitakupigia simu
nikiwa Mbeya na kukujulisha
mahala nilipo” akasema Elvis
.Doreen akabaki kimya
“ Doreen are you there?
Akauliza Elvis
“ I’m here Elvis” akajibu
Doreen
“ Umenielewa nilichokuomba?
I real need your help right now”
akasema Elvis Baada ya kimya
cha sekunde kadhaa Doreen
akasema
“ Ok Elvis nitakusaidia.Kwako sina uwezo wa kusema hapana”
akajibu Doreen.Uso wa Elvis
ukapambwa na tabasamu baada
ya jibu lile la Doreen.
“ Ahsante sana
Doreen.Ahsante sana.Tafadhali
naomba usimweleze chochote
Patricia.Nitakupigia simu kesho
nikiwa Mbeya na kukupa
maelekezo mahala nitakapokuwa”
akasema Elvis
“ Usijali Elvis japokuwa
umenistukiza sana lakini
nitajitahidi kufanya kama
ulivyoniomba.Ila tafadhali naomba
unihakikishie kwamba uko salama
na hakuna tatizo lolote” akasema
Doreen
“ Niko salama Doreen usihofu
chochote” akasema Elvis na
kukata simu akamrudishia
Stanley simu yake.Hawakuongea
kitu chochote safari ikaendelea
kwa kasi kuelekea Tunduma mji uliopo mpakani mwa Tanzania na
Zambia
***********************
Ilikuwa ni safari ndefu
kutokana na umbali mrefu uliopo
kati ya Lusaka na Tunduma
.Kutoka Lusaka hadi Tunduma ni
umbali wa kilometa 1022.Stanley
ambaye alionekana kwa mahiri
mno katika usukani aliendesha
gari kwa kasi na umakini
mkubwa.Graca kutokana na
uchovu aliokuwa nao kwa safari
ndefu ilimlazimu alale katika kiti
cha nyuma
Saa mbili za asubuhi
walikaribia mji wa
Tunduma.Stanley akaachana na
barabara kuu akachepuka katika
barabara ya vumbi ambayo
ilionyesha haikuwa ikipitwa sana
ma magari.Aliendesha taratibu kutokana na barabara ile kujaa
mashimo mengi.Baada ya mwendo
wa kama dakika ishirini katika
barabara ile akasimamisha gari na
kutoa simu akampigia mtu Fulani
wakaongea halafu safari
ikaendelea.Dakika kama kumi hivi
akasimisha gari chini ya mti
mmoja mkubwa akashuka na
kutoa simu yake akawasiliana na
mtu na baada ya kama dakika
tano hivi wakatokea watu wawili
wakiwa na piki piki.Stanley
akasalimiana nao wakaongea
kidogo halafu akatoa fedha katika
pochi yake na kuwahesabia na
kurejea garini alikowaacha akina
Elvis
“ Elvis hawa jamaa wa piki
piki ndio watakaowaingiza
Tanzania ,Ni wazozefu sana wa
njia hizi za vichochoroni kwa hiyo
msiwe na wasi wasi hata
kidogo.Kitu ninawachowaomba ni kwamba msiwaulize chochote na
wala msitake kufahamu chochote
toka kwao.Watawapeleka sehemu
mnakotaka kwenda na baada ya
hapo mtatafuta usafiri wa
kuwafikisha Dar es salaam.Poleni
sana kwa safari ndefu” akasema
Stanley
“ Stanley sina neno kubwa la
kuweza kukushukuru kwa
msaada huu ya kusema ahsante
sana. Tunashukuru umetufikisha
hapa salama na ninakutakia safari
njema ya kurejea Lusaka “
akasema Elvis huku akimpa
mkono wakaagana na kuelekea
katika piki piki wakapanda na
safari ya kuelekea Tunduma
ikaanza.
Dakika thelathini baadae
waliwasili katika mji wa Tunduma
mji wenye pilika pilika nyingi sana
za kibiashara.Elvis akawaomba
wale vijana wawapeleke katika stendi ya magari yaendayo mjini
Mbeya na kuagana na vijana wale
.Pale stendi kulikuwa na watu
wengi na Elvis hakutaka wapande
gari lenye watu wengi hivyo
akakodisha gari ndogo aina ya
Noah ili iwapeleke Mbeya.
Saa saba za mchana wakawasili
jijini Mbeya, jiji zuri na lenye
kuvutia sana.Dereva wa lile gari
walilokodi alilifahamu vyema sana
jiji la Mbeya hivyo akawapeleka
katika hoteli nzuri ambako
walichukua vyumba viwili .Kwa
kutumia simu ya pale hotelini
Elvis akawasiliana na Doreen
aliyekuwa safarini kuelekea Mbeya
na kumfahamisha mahala
walikofikia.
Big salute kulubule.
 
Back
Top Bottom