Riwaya: Jina langu ni Pheady

ndio ndio
 
ao.
"Tutakutana tena wapi na saa ngapi?" Aliuliza Gilly.
"Tukutane saa tisa hapa kwangu kutafakari yatakayokuwa yamejiri, nafikiri wakati huo boss naye tutakuwa naw hapa. La maana ni kujitahifi katika mambo yenu mpate habari nzuri zinazowahusu hao watu au muwaue kabisa pale inapowezekana." Alimaliza kuongea Patrick huku wenzie wakiaga na kuondoka. Wakati huo ilikuwa ni saa mbili na robo asubuhi, walichelewa kuamka kutokana na usiku uliopita walikuwa na kazi nzito ya kwenda kutupa maiti ziwani na kujikuta wakiingia vitandani saa kumi na nusu.
Baada ya kuwa wameondoka wenzake, Patrick alifungua jokofu na kutoa chupa ya John Walker akaweka mezani. Ilikuwa ni asubuhi lakini kutokana na adha aliyokuwa nayo kichwani, sio ajabu kukata kinywaji kikali kwa wakati huo. Alikuwa amekunywa kama robo chupa hivi ndipo alipata wazo la kumpigia simu mpenzi wake wa zamani ambae ni muuguzi wa zahanati fulani.
"Halo, Patrick akiita kwenye simu baada ya kuwa amezungusha namba kadhaa.
"Nani mwenzangu?" Sauti toka upande wa pili iliuliza.
"Patrick hapa naomba, naomba kuongea na Norack," alisema.
"Subiri" alijibiwa. Kitambo kidogo sauti ikasikika kwenye simu. "Norack hapa, nani mwenzangu?"
"Inamaana aliyekuita akukuambia unaitwa na nani?" Lilimtoka Patrick swali badala ya jibu.
"Ohoo!! Patrick mpenzi umenikumbuka leo, sikuambiwa jina ila nimebaini sauti." Alisema Norack.
"Nimekumbuka mpenzi alafu vilevile nahitaji msaada wako." Alisema Patrick.
"Sema mpenzi mimi nipo wazi kwako" Alisema Norack.
"Nisingependa tuongee kwenye simu, kwa hiyo nikuoneje?"
" Mie nabadiri zamu saa tatu, kwa hiyo baada ya hapo nitakuwa nyumbani, unaweza kuja kuniona." Alisema Norack
"Kama unatoka saa tatu nisubiri hapo hapo kazini kwako nitakupitia tuongozane wote." Alisema Patrick.
"Sawa mie nitakusubiri lakini usiniweke kuchoma mahindi."
"Nitawahi mtoto, maana mie ndio mwenye shida"
"Okay, kwa heri." Alisema Norack na kuachia busu kwenye simu. Patrick alicheka na kurudisha hilo busu alafu akakata simu. Alichukua birauli iliyokuwa na pombe nusu na kuinywa yote alafu akabaki akitabasamu. Alikuwa akikumbuka jinsi Norack anavyompenda, lakini yeye hakuwa na mpango naye ki vile.
Ilipotimia saa tatu Patrick alishaegesha gari MAGAMBO zahanati akisubiri Norack atoke ili apate wasaa wa kumueleza shida yake.
Kama utakumbuka ni katika hiyohiyo zahanati ndipo alipolazwa Kikakika na Norack ni muuguzi wa hapo kwa muda mrefu. Kwani toka amalize mafunzo ya uuguzi hapo ndipo mahali pale pa kwanza kuanzia kazi kama miaka mitatu iliyopita.
Baada ya Norack kuwa ametoka na kupanda gari la Patrick waliondoka na kuongoza moja kwa moja mpaka kwa Norack. Patrick alimuambia akabadiri nguo za kazi yeye atamsubiri ndani ya gari. Kwani Patrick hakupenda kuingia ndani, siku zote walizokuwa wapenzi. Norack alifanya hivyo na baada ya muda kidogo alirudi akiwa amebadilika sio tena Norack muuguzi bali unaweza kumuita Norack wa maonyesho ya urmbo kwa jinsi alivyopendeza..
Patrick aliondoa gari moja kwa moja mpaka Nsimbo hotel, alipofika aliingia maegesho wakashuka na kwenda kukaa meza moja iliyokuwa kuwa nje kwenye bustani. Kwa kuwa ilikuwa asubuhi, kulikuwa hakuna watu hata kwenye meza za karibu yao, muhudumu alikuja akaagiza kifungua kinywa kwa akili ya Norack na yeye akaaagiza sharubati ya ndimu. Vyote vililetwa na wakaanza kutumia huku wakiongea maongezi ya kawaida. Baada ya kumaliza muhudumu alitoa vyombo na kuagizwa kuleta chupa nne za bia.
"Vipi? Mbona husemi shida yako uliyonayo, manake umeniweka roho juu kwa kusubiri kusikia kinachokusibu." Alisema Norack baada ya muhudumu kuleta bia na kuondoka.
"Sikiliza Norack, ninachokuomba kwanza nataka iwe Siri yako kwa ajiri ya heshima yako na yangu."
"Sema tu bwana,, Leo una wasiwasi na Mimi utafikiri hunijui. Wakati unaelewa nilivyo tayari hata kufa kwa ajiri yako." Alisema Norack wakati akimwangalia Patrick kwa macho ya udadisi..
"Kuna watu fulani ambao huwa tunafanya nao biashara za magendo wametuzurumu mali zetu na katika vurumai ya kugambea hiyo mali mmoja wao ameumia lakini walifanikiwa kutoroka nae. Kwa hiyo msaada wako niniohitaji ni kuniulizia kwa madaktari mnaofahamiana kama wamepokea mtu aliyejeruhiwa katika usiku wa kuamkia Leo. Mambo hayo nataka yafanywe kwa Siri hata unaowauliza wasielewe Kinachoendelea. Kumbuka tulikuwa kwenye biashara haramu hivyo haitakiwi mtu yeyote ajue. Iwapo utafanikiwa kunisaidia hilo suala kwa haraka nitafirahi sana. Na nakuahidi kukujengea nyumba maana utakuwa umesalimisha pesa zangu nyingi sana." Alimaliza kueleza Patrick.
"Norack alinyanyua birauli ya pombe na kuimimina mdomoni, alafu akarusha birauli tupu mezani na kuinama kidogo kufikiri.Alikuwa anakumbuka jinsi Kikakika alivyoletwa pale zahanati usiku, yeye ndie alikuwa zamu. Alitaka kumueleza Patrick lakini alisita. Ndipo alipoamua kumuambia kuwa atajitahidi kupata habari hiyo na pindi akipata fununu tu, atamtaarifu bila kuchelewa.
Kitu kilichofanya Norack asimueleze palepale ni kwamba alihofia asije akaikosa nyumba aliyoahidiwa. Kwani Kama angemueleza ingeonekana kuwa hajafanya kazi yoyote ya kustahili kujengewa nyumba..
Baada ya kuwa wamemaliza maongezi yao waliendelea na zile bia zao na walipomaliza kunywa waliondoka na kilichokuwa kimewapeleka pale kulikuwa kimeisha hicho kilichobaki ilikuwa kila mtu kuchakarika. Patrick alimpitiaha Norack nyumbani kwake na kumuavha pale yeye akaongoza kurudi kwake kujiandaa kuwapokea wageni wake. Walikuwa wameahidiana na Norack kuwasiliana saa kumi kwa njia ya simu. Patrick alimuambia Norack ampigie simu numbani kwake ifikapo saa hizo atakuwepo nyumbani.

9
Wakati tulipokuwa tumeishafika kwa dada huko Kilimahewa ndipo nikakumbuka kuwa nilikuwa na ahaadi na Mtuli saa saba mchana na mda ulikuwa umepita
"Halo Sonno nimekuwa mjinga sana Leo, unakumbuka wale wasichana tulikuwa nao kule Magnum tuliahidiana na yule mmoja wao kuwa tukutane saa saba River side. Na kama unavyoona sijaenda." Nilimueleza Sonno.
"Lakini sio mbaya sana,, kwani namba ya simu hakukupa?"alisema Sonno.
"Kanipa namba ya kazini na sasa hivi watakuwa wametoka kazini." Nilieleza.
"Pamoja na hayo, wewe si ulitaka watupe msaada wa kuweza kumpata Kikakika, na Kikakika mwenyewe tumeishampata. Sasa kinachokusimbua ni nini? Au unataka penzi nini?" Sono alisema katika hali ya utani.
"Unajua Sonno, mpaka sasa hivi hakuna haja ya kuniamini sana
 
daaaaaah kafupi sana boss
 
Nimekuwa busy sana ila nitajitahidi kesho nitupie ndefu kiasi.
 
KAZI IENDELEE


"Unajua Sonno, mpaka sasa hivi hakuna haja ya kujiamini sana maana hawa watu tunaopambana nao wanaonekana kuwa hatari kwetu hata zaidi ya polisi. Hivyo ningejenga uhusiano na yule msichana ingekuwa rahisi kwetu kupata habari zao." Nikisema.
"Wewe Pheady si useme tu, habari zao za nini wakati sisi tunawaacha kwenye mataa!?"Alisema Sonno
"Sikiliza Sonno, penzi nalitaka lakini na masuala ya kazi yamo katika hilo penzi."
"Ndio, kubali yaishe." Alisema Sonno alafu tukacheka wote kwa pamoja.
"Sasa kama ni hivyo mpigie simu kesho asubuhi uingee nae, huenda bwana yake akawa katika wale marehemu tuliowaua jana." Alisema Sonno.
"Ndio kitu kinachonisumbua akilini, lakini kesho sio mbali tutapata uhakika wa mambo." Nilisema.

Wakati tunaendelea na maongezi, aliingia mfangakazi wa dada akiwa na mfuko wa khaki pamoja na bahasha. Alifika na kuweka mwezani huku akisema mizigo yenu hii mliiacha kwenye gari. Tulikuwa tumemuachia fungua za gari afanye usafi. Mimi nilishangaa wakati Sonno alishituka na kutabasamu. Asante sana, tulikuwa tumesahau." Alisema Sonno wakati kijana alishatupa mgongo.
"Kuna nini humo?" Nilimuuliza Sonno aliyekuwa akigungua mfuko wa kaki.
"Sijui, huu mfuko na bahasha nilivichukua jana kwa Patrick. La ajabu sikukumbuki mpaka sasa ndio nashtuka." Alisema Sonno.
"Hata mimi nilikuona unatoka navyo lakini nilisahau kuuliza muda wote. Hii ni ajabu, hebu fungua tuone maajabu yake humo ndani."

Sonno alifungua tukakuta ndani kuna fulana tano za Blue. Tulipozichunguza tukang'amua ni fulana zisizopenyesha risasi. Na hiyo ni baada ya kujaribu kuzichoma moto lakini hazikuungua. Tulifurahi na kuziweka pembeni hapo tulifungua bahasha na ndani ya bahasha tulimkuta picha mbalimbali zikiwa na watu tofauti tofauti zingine ziliandikwa nyuma, tukaanza kuangalia moja baada ya moja kwani zilikuwa nyingi. Ghafla Sonno akanitupia moja ambayo niliiangalia na kuona ni picha yangu iliyopigwa nikiwa karibu na gari. Nilirudisha kumbukumbu na kukumbuka ile gari ilikuwa ya Mr Catto palepale nikajua ile picha ilipigwa nikiwa wapi. Niliiweka pembeni na kuendelea na uchambuzi, baada ya picha kama tatu hivi niliona picha ya mzungu mmoja hivi niliyemfahamu.

Ghafla akili yangu ilirudi nyuma yapata kama miaka mitatu hivi iliyopita na kujikuta nakumbuka mambo ya muda huo. Nilitoa sigara na kuwasha, nilikumbuja jinsi nilivyomuua huyo mzungu kinyama na kumtupa mto Rufiji huko tunduma. Hiyo ilikuwa ni baada ya kuwa nimepelekwa Afrika Kusini na rafiki yangu mmoja ambaye alikuwa ni jasusi. Na baada ya kufika huko ambapo nilijulikana kama mganda kutokana na maelezo nilipokuwa nimemuambia huyo rafiki yangu jasusi. Nilifanyiwa mpango wa kupata kazi katika shirika moja la kijasusi hapo Afrika Kusini, haikuchukua muda baada ya kuwa nimepewa kazi ya kuja Tanzania kulipua bomba la mafuta la Tanzania Zambia. Tulikuwa watu watatu tuliopewa hiyo kazi, miongoni mwa hao watu watatu mimi pekee ndio nilikuwa Muafrika. Tulipewa vifaa vyote ambavyo vingeweza kufanikisha hiyo hujuma, baada ya hapo iliamuliwa mimi na mzungu mmoja ambaye ndio yupo kwenye picha hapa tusafiri kwa gari pamoja na vifaa. Gari lilikuwa maalumu kwa kuchukua vitu vya hatari bila kujulikana katika kaguzi za mipakani. Mzungu mwingine ambaye ndie alikuwa kiongozi aondoke na ndege tutaonana nae Dar mji maarufu wa Tanzania.

Baada ya kuwa tumeanza safari, mawazo yaliniijia ya kuzuia hiyo hujuma kwa watanzania ambao ni ndugu zangu. Nilijisikia vibaya kuona nchi yangu ikifanyiwa unyama na baadae kuleta madhara kwa taifa na jamii kwa ujumla. Akilini nilipanga tufikapo Tanzania niwashtue askari wawakamate, lakini tulipofika Zambia nilibadili mawazo kwa kuhofia kuunganishwa nao ili kuisadia polisi. Maana polisi wa Tanzania hawaaminiki kwa kugeuza mambo ndio wenyewe. Unaweza shikwa kwa kosa la uzembe na uzurulaji lakini shitaka likaja la kukutwa na bangi. Kutokana na hofu hiyo niliamua niukate mzizi wa fitina mimi mwenyewe kwa kuwashindilia risasi hawa washenzi tuliokuwa tumetumwa nao.

Nikipiga akili namna ya kumuua huyu niliyenaye kwanza, alafu mwingine tutaonana nae huko Dar. Niliamua tufike Dar kwanza ndio nitamuua kirahisi maana kwa sasa siraha zote zilikuwa zimefungiwa sehemu maalumu kwa kuepuka upekuzi wa mipakani. Na kumuua kwa mikono ingekuwa tabu maana hata yeye alikuwa mzuri katika mapigano huenda akanizidi na kunitoa roho. Baada ya kuwa tumevuka mipaka ya Tanzania na Zambia niliona huo ndio ulikuwa mda muafaka wa kutekeleza mipango yangu iliyokichwani wakati huo tulikuwa Tunduma. Nilimshauri tupaki gari pembeni tutoe bastola kwa ajili ya kujilinda kwani tayari tulishafika na huku Tanzania hakuna upekuzi zaidi alafu njia tunayoiendea huwa Ina majambazi maana kuna pori kubwa kabla ya kuingia mji mwingine. Alidanganyika na uongo wangu akafungua ile sehemu na kutoa bastola mbili zenye kiwambo cha kuzuia sauti vilevile alitoa risasi kila mtu akaweka kwenye bastola yake. Kwa sababu tulishavuka mpaka na tulikuwa kwenye kipori kidogo niliona nisimcheleweshe, alipoichomeka bastola yake chini ya kitovu na kutaka kupanda ndani ya gari nilimlenga kichwa hakuwa na habari kwani alikuwa amenipa kisogo kwa wakati huo. Niliachia risasi moja ya kichwa na kumfanya aitwe marehemu wakati huohuo. Nilichukua blanket lililokiwa ndani ya gari na kumviringisha alafu nikamlaza kiti cha nyuma ya gari. Nilikamata gari na kuongoza kandokando ya mto Rufiji. Nilikuwa nazifahamu sehemu hizo, sikuwa mgeni wa mazingira hayo. Nilitafuta sehemu nzuri kusikokuwa na dalili za watu karibu. Nilipata na kusogeza gari karibu na ukingo wa mto, hapo nilitoa ile maiti ya yule mzungu na kuitupa mtoni.

Baada ya hapo nilikanya mafuta kuelekea Dar, baada ya kufika Dar yule mwingine hakunipa tabu. Tulipoonana tulipokuwa tumeahidiana nilimuambia mwenzetu amepatwa na flu na nimemuacha kwa daktari mmoja akiwa amepumzika. Aliomba twenda tukamuone, tuliondoka nikamleleka mpaka Tabata na kumshindilia risasi ambapo kesho yake maiti yake iliokotwa Tabata dampo. Hapo mie nilipotea katika uimwengu wa hao majasusi baada ya kuwa nimechukua siraha zote na kutelekeza gari.

"Vipi rafiki yangu mbona hivyo?" Sonno aliuliza baada ya kuona nimezubaa kwa mda mrefu.
"Unajua hii picha inanikumbusha mbali sana" nilimjibu.
 
PAMOJA BOSS IKO VZURI
 
Kiongozi salaam kama mtu Anataka hii story Ina bidinafanyaje ili aaipate
Kama unahitaji hard copy inabidi usubiri kidogo lakini kama ni soft copy tuwasiliane chemba unanitumia namba ya simu what's up na fedha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…