Riwaya: Kasri ya Mwinyi Fuad

Riwaya: Kasri ya Mwinyi Fuad

Mkuu ni hadithi nzuri ya kizalendo, kubwa kabisa nikupe sifa kubwa umekuwa unapost bila maringo mwanzo mwisho. Endelea na moyo huo huo
 
SEHEMU YA 80 ..................... MWISHO



“Ndiyo.”

Vuai alimpa mkono Kijakazi kwa furaha na kumwuliza “Unaweza kunitambua?”

“Naweza.”

“Wapi?”

“Mimi najua vizuri lakini siku nyingi tumepoteana. Wewe si Vuai tuliyekuwa tukifanya kazi pamoja kwa Puad?” Kijakazi aliuliza.

“Khassa!” Vuai alijibu “Sasa kumezidi nini tena, Kijakazi? Jua karibu litakuchwa na wewe uko hapa. Je, umekuja kutueleza habari za Fuad?” Vuai aliendelea.

“Kama ulivyoweza kukisia,” Kijakazi alijibu mbiyo mbiyo, “hayo ndiye yaliyonileta hapa.”

“Kwani wewe bado uko kwa Fuad tu?” Vuai aliuliza.

“Hivi sasa natokea kwake lakini sidhani kama nitarejea tena.”

Vuai ambaye alikuwa amesimama wakati wote aliokuwa akizungumza na Kijakazi alikaa pale juu ya bao na kuanza kumhoji Kijakazi.

“Ehe! Nini anasema Fuad? Amekutuma cho chote kwetu?”

Kijakazi alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kumwelezea Vuai habari zote za Fuad na hamu hiyo ilimfanya kubabaika katika aliyotaka kuyasema. Hakujua aanzie wapi na mara alianza kupiga makelele, “Mbaya! Mbaya sanal”

“Mimi najua,” Vuai alimjibu Kijakazi huku akimpigapiga bega.

“Wewe Vuai unavielewa vizuri vitimbwi vya mtoto yule na juu ya hivyo nyinyi, m’mekwenda kumpa ukubwa katika shamba lenu! Unajua vizuri kama Fuad anatuma kitumwa na anapokupa amri lazima uitekeleze hapo hapo! Anapotaka jambo lazima liwe kama kudra na mwanadamu! Akisema umvue viatu basi lazima umvue hapo hapo na ukichelewa kidogo tu basi mara anakupopoa kwa mateke! Yeye hakupendeni, anakuchukieni na kukudharauni! Anasema hamjui kitu! Wajinga, wapumbavul”

Kijakazi alitoa hadithi ndefu kuhusu ubaya wa Fuad. Alisahau kabisa kama Vuai alikuwa ni mmoja katika wale wal’oteswa kitumwa na Fuad wakati alipokuwa akifanyakazi shambani kwake. Mara alihadithia siku alizovulishwa viatu, mara alihadithia siku alizofukuzwa chumbani... almuradi hakuna alilolibakisha.

Vuai alinyamaza kimya buku akimsikiliza Kijakazi kwani alielewa vizuri kwamba Kijakazi alikuwa na joto la moyo na alikuwa na mengi ya kusema kuhusu mateso ya Fuad. Aliona ni jambo la busara kumwacha Kijakazi atoe joto la roho alilokuwa nalo ijapokuwa yeye Vuai mwenyewe alimwelewa vizuri Fuad.

Vuai alimkamata bega Kijakazi taratibu huku akitikisa kichwa na kusema “Kwanza nani aliyekwambia kama Fuad ndiye mkubwa hapa?”

“Ameniambia mwenyewel” Kwa makelele Kijakazi alijibu.

“Hayo si kweli, alikuwa anakudanganya tu labda kwa madhumuni ya kutaka kukutisha.”

“Hivyo yeye si mkubwa hapa? Hivyo alikuwa anajigamba tu?” Kijakazi aliuliza.

Kijakazi alipigwa na mshangao na alitulia kimya huku amemkodolea macho Vuai. Vuai naye alinyamaza kimya vile vile na palikuwa na kimya cha muda mfupi baina yao mpaka Vuai alipokivunja kimya hicho.

“Wacha ukubwa, bata akitaka kuwa mwanachama wa kawaida tu shambani hapa basi hatutomruhusu Fuad kufanya hivyo kwani yeye alivyokuwa na fikra za kibwana shamba hataweza kufanya kazi hapa kwa moyo thabiti. lazima atataka kupitisha vitendo vya uharibifu.”

“Kweli, kweli tupu hayo unayoyasema!” Alisema Kijakazi.

Vuai alikaa kimya buku akimtazama Kijakazi usoni. Zilimjia huruma za dhati kwa namna alivyomwona Kijakazi amechakazwa kwa kazi ya kitumwa ya muda mrefu. Wakati Vuai alipokuwa akimtazama Kijakazi fikra zake zilipotea na alianza kuwaza siku ambazo yeye mwenyewe alifanya kazi shambani kwa Fuad. Aliyakumbuka mateso waliyokuwa wakiteswa, jinsi walivyokuwa wakitukanwa. Na mara akakumbuka siku ile Fuad aliyotaka kumkamata Mkongwe kwa nguvu na kumwingilia kibandani kwake. Mara fikra bizi zilimpotea na kumjia fikra za siku ile ambayo Fuad alimkuta njiani anarejea mkutanoni huko Kijangwani... Alipokuwa katika fikra akizikumbuka siku za mateso, alisahau kabisa kama pale alipo alikuwa amekaa na mtu aliyekuwa akizungumza naye lakini kwa ghafla alishtuka kama mtu aliyezindukana usingizi na mara lilimtoka swali, “Sasa Kijakazi siku zote hizi zilizopita nini kilichokuzuia usije kujiunga na sisi hapa?”

“Ujinga wangu,” bila ya kufikiri Kijakazi alijibu.

“Sasa ukitoka hapa unarejea kwa Fuad?” Vuai aliulizatena.

“Lo, Mungu apishe mbali! Nitatokomea po pote pale lakini sitarudi tena kwa yule mwizi wa fadhila asiyejua wema wala hisani.”

“Sasa sikiliza Kijakazi,” Vuai alianza kusema “sisi sote tunaoishi hapa ni sawa sawa na wanao. Yaliyokufika wewe na sisi yametufika vile vile ila wewe mwenzetu umetuzidi. Lakini ndyo ulimwengu, kwani mambo huzidiana. Sasa Kijakazi mimi nakushauri bora uje hapa ili ujiunge na sisi watoto wako tushirikiane kufanya kazi pamoja na wewe utakuwa mwanachama kamili wa shamba hili la ushirika na utapata haki sawa sawa kama mwanachama yo yote yule; au una shauri gani?”

Kijakazi al’ogopa kujibu kitu cho chote kile, lakini mara alisema, “Ah! Nadhani hamtakuwa na haja ya mwanachama mtu mzima kama mimi. Mimi sina nguvu tena za kufanya kazi yo yote; mimi nimekwisha kabisa na pahala kama hapa panahitaji mtu mwenye nguvu anayeweza kufanya kazi.”

“Basi umekuja hapa kutuhadithia habari za Fuad tu?” Vuai alimwuliza Kijakazi kwa masihara huku akitabasamu. Mara Vuai aliendelea na kusema, “Kijakazi juu ya utu uzima uliokuwa nao sisi tutakuchukua katika shamba letu. Utakuwepo hapa kwa muda na serikali ya kimapinduzi ya ASP ina mipango madhubuti kuhusu watu wazima kama nyinyi. Zipo nyumba maalum zinajengwa kwa ajili yenu huko Sebulen, usitie wasiwasi wo wote. Kama nilivyokwambia sisi sote hapa ni kama watoto wako na sisi tutakuenzi wewe kama mzee wetu. Wewe Kijakazi una maarifa ya s’ku nyingi katika kazi za ufugaji na tutafurahi pindi ukiweza kuwapa vijana wetu maarifa yako katika kazi hiyo. Wao watakuwa tayari wakati wo wote kujifunza kutoka kwako. Sisi tulitumaini kwamba utakuja kujiunga na sisi zamani lakini ulichelewa. Njoo, Kijakazi, uishi na sisi hapa.”

Kijakazi aliruka kwa furaha na mara aliukamata mkono wa Vuai na kutaka kuubusu lakini Vuai aliurusha mkono wake na kusema. “Kijakazi tabia hiyo itakubidi uiache hapa. Sisi hapa sote m wanachama sawa sawa vva shamba hili la ushirika na hapana mtukufu miongoni mwetu ambaye anataka kubusiwa mikono. Wewe Kijakazi utakuwa pamoja na sisi hapa lakini kwanza itakubidi ukapumzike na upate matibabu huko hospitalini. Sasa itakubidi urejee kwa Fuad ili ukachukue vitu vyako na halafu urejee hapa.”

“Nani? Mimi? Mimi sina cho chote huko kwa Fuad, vitu vyangu vyote nilivyonavyo ni haya magwanda niliyovaa,” Kijakaz’ alisema huku akishusha pumzi kama mtu aliyetuliwa mzigo mz’to.

Kijakazi alishtuka kwa sauti ya mvumo mkubwa aliousikia, masikio yakamziba. Alitaka kufanya kama kukimbia lakini mara aliona makundi ya watu wakitoka kutoka kwenye mabanda mbali mbali. Ilikuwa ni saa kumi na mbili magharibi na sauti ile ilikuwa ni sauti ya king’ora iliyotowa ishara ya kumalizika kwa saa za kazi.

Kwa mbali Kijakazi aliliona kundi la wanawake waliokazana miongoni mwao akiwamo Mkongwe. Kijakazi alimfuatia Mkongwe mbiyo huku akimpigia makelele na alipokutana naye alimkumbatia huku machozi yakimtoka.

“Kweli, mwanangu! Yote uliyokuwa ukiniambia ni kweli tupu” Kijakazi alimwambia Mkongwe huku akisugua uso wake juu ya mabega ya Mkongwe.

Mkongwe hakumjibu kitu. Kundi la watu waliokuwa wakitoka makazini mwao walimzongea Kijakazi ambaye al’kuwa bado amemkumbatia Mkongwe huku machozi yakimmiminika. Wote waliingiwa na hamu ya kumwona Kijakazi kwani siku nyingi walikwisha kusikia hadithi zake.

“Nyamaza shoga, nyamaza shoga yangu, usilie; hapa umefika kwenu na sote tukikungojea kwa hamu kubwa. Twende zetu.” Mkongwe alimshika mkono Kijakazi na kumwongoza chumbani kwake.

Mara Vuai alinyanyua sauti yake na kumwuliza Mkongwe, “Unafikiri Kijakazi leo atalala wapi?”

“Haidhuru mimi niko tayari kulala po pote pale!” Kijakazi alisema kwa ghafla huku ak’jipangusa machozi.

“Atalala na mimi: yeye atalala juu ya kitanda na mimi nitatandika mkeka chini nakulala hapo. Karibu pamoja na sisi shoga yangu,” alisema Mkongwe.

“Ahsante, shoga yangu, ahsante!”

Mkongwe alimwongoza Kijakazi mpaka chumbani kwake ambako walilala pamoja siku ile.

Fuad alibakia peke yake, mambo yalimbadilikia, na hatimaye hakuweza tena kuisbi Unguja. Aliondoka kwa njia ya magendo, labda kwa kutumia n’galawa au mashua. na bapana aliyejua alitokomea wapi.

MWISHO


cc Great God
Asante sana nimeisoma mpaka mwisho imenikumbusha mbali sana🙏👍
 
Naam huo ndio mwisho wa Riwaya ya KASRI YA MWINYI FUAD Iliyoandikwa na Mwandishi ADAM SHAFI ADAM Na Imeletwa kwenu na PSEUDEPIGRAPHAS

Asante kwa kusoma Riwaya hii toka mwanzo hadi mwisho.

Weka maoni yako, tujue kama tulikuwa pamoja !!!!... Usipite kimyakimya
Shukrani sana tulikuwa pamoja mpaka mwisho
 
Simulizi Zinazorushwa na BURE SERIES

1. Simulizi: Kurudi Kwa Moza
Bonyeza hapa chini kusoma
Simulizi: Kurudi Kwa Moza

2. Riwaya: Kasri ya Mwinyi Fuad
Bonyeza hapa chini kusoma
Riwaya: Kasri ya Mwinyi Fuad

3.Simulizi: Nini maana ya mapenzi
Bonyeza hapa chini kusoma
Simulizi: Nini maana ya mapenzi

4. Simulizi : Nguvu Ya Mapenzi
Bonyeza hapa chini kusoma
Simulizi : Nguvu Ya Mapenzi

5. Mkuki Kwa Nguruwe (Kisa Cha Kweli)
Bonyeza hapa chini kusoma
Mkuki Kwa Nguruwe (Kisa Cha Kweli)

6. RIWAYA: Sauti Yake Masikioni Mwangu
Bonyeza hapa chini kusoma
RIWAYA: Sauti Yake Masikioni Mwangu

7. NDOA ILIVYOTETERESHA IMANI YANGU (Kisa Cha Kweli)
Bonyeza hapa chini kusoma
NDOA ILIVYOTETERESHA IMANI YANGU (Kisa Cha Kweli)



kitonsa
 
SEHEMU YA 80 ..................... MWISHO



“Ndiyo.”

Vuai alimpa mkono Kijakazi kwa furaha na kumwuliza “Unaweza kunitambua?”

“Naweza.”

“Wapi?”

“Mimi najua vizuri lakini siku nyingi tumepoteana. Wewe si Vuai tuliyekuwa tukifanya kazi pamoja kwa Puad?” Kijakazi aliuliza.

“Khassa!” Vuai alijibu “Sasa kumezidi nini tena, Kijakazi? Jua karibu litakuchwa na wewe uko hapa. Je, umekuja kutueleza habari za Fuad?” Vuai aliendelea.

“Kama ulivyoweza kukisia,” Kijakazi alijibu mbiyo mbiyo, “hayo ndiye yaliyonileta hapa.”

“Kwani wewe bado uko kwa Fuad tu?” Vuai aliuliza.

“Hivi sasa natokea kwake lakini sidhani kama nitarejea tena.”

Vuai ambaye alikuwa amesimama wakati wote aliokuwa akizungumza na Kijakazi alikaa pale juu ya bao na kuanza kumhoji Kijakazi.

“Ehe! Nini anasema Fuad? Amekutuma cho chote kwetu?”

Kijakazi alikuwa na hamu kubwa ya kutaka kumwelezea Vuai habari zote za Fuad na hamu hiyo ilimfanya kubabaika katika aliyotaka kuyasema. Hakujua aanzie wapi na mara alianza kupiga makelele, “Mbaya! Mbaya sanal”

“Mimi najua,” Vuai alimjibu Kijakazi huku akimpigapiga bega.

“Wewe Vuai unavielewa vizuri vitimbwi vya mtoto yule na juu ya hivyo nyinyi, m’mekwenda kumpa ukubwa katika shamba lenu! Unajua vizuri kama Fuad anatuma kitumwa na anapokupa amri lazima uitekeleze hapo hapo! Anapotaka jambo lazima liwe kama kudra na mwanadamu! Akisema umvue viatu basi lazima umvue hapo hapo na ukichelewa kidogo tu basi mara anakupopoa kwa mateke! Yeye hakupendeni, anakuchukieni na kukudharauni! Anasema hamjui kitu! Wajinga, wapumbavul”

Kijakazi alitoa hadithi ndefu kuhusu ubaya wa Fuad. Alisahau kabisa kama Vuai alikuwa ni mmoja katika wale wal’oteswa kitumwa na Fuad wakati alipokuwa akifanyakazi shambani kwake. Mara alihadithia siku alizovulishwa viatu, mara alihadithia siku alizofukuzwa chumbani... almuradi hakuna alilolibakisha.

Vuai alinyamaza kimya buku akimsikiliza Kijakazi kwani alielewa vizuri kwamba Kijakazi alikuwa na joto la moyo na alikuwa na mengi ya kusema kuhusu mateso ya Fuad. Aliona ni jambo la busara kumwacha Kijakazi atoe joto la roho alilokuwa nalo ijapokuwa yeye Vuai mwenyewe alimwelewa vizuri Fuad.

Vuai alimkamata bega Kijakazi taratibu huku akitikisa kichwa na kusema “Kwanza nani aliyekwambia kama Fuad ndiye mkubwa hapa?”

“Ameniambia mwenyewel” Kwa makelele Kijakazi alijibu.

“Hayo si kweli, alikuwa anakudanganya tu labda kwa madhumuni ya kutaka kukutisha.”

“Hivyo yeye si mkubwa hapa? Hivyo alikuwa anajigamba tu?” Kijakazi aliuliza.

Kijakazi alipigwa na mshangao na alitulia kimya huku amemkodolea macho Vuai. Vuai naye alinyamaza kimya vile vile na palikuwa na kimya cha muda mfupi baina yao mpaka Vuai alipokivunja kimya hicho.

“Wacha ukubwa, bata akitaka kuwa mwanachama wa kawaida tu shambani hapa basi hatutomruhusu Fuad kufanya hivyo kwani yeye alivyokuwa na fikra za kibwana shamba hataweza kufanya kazi hapa kwa moyo thabiti. lazima atataka kupitisha vitendo vya uharibifu.”

“Kweli, kweli tupu hayo unayoyasema!” Alisema Kijakazi.

Vuai alikaa kimya buku akimtazama Kijakazi usoni. Zilimjia huruma za dhati kwa namna alivyomwona Kijakazi amechakazwa kwa kazi ya kitumwa ya muda mrefu. Wakati Vuai alipokuwa akimtazama Kijakazi fikra zake zilipotea na alianza kuwaza siku ambazo yeye mwenyewe alifanya kazi shambani kwa Fuad. Aliyakumbuka mateso waliyokuwa wakiteswa, jinsi walivyokuwa wakitukanwa. Na mara akakumbuka siku ile Fuad aliyotaka kumkamata Mkongwe kwa nguvu na kumwingilia kibandani kwake. Mara fikra bizi zilimpotea na kumjia fikra za siku ile ambayo Fuad alimkuta njiani anarejea mkutanoni huko Kijangwani... Alipokuwa katika fikra akizikumbuka siku za mateso, alisahau kabisa kama pale alipo alikuwa amekaa na mtu aliyekuwa akizungumza naye lakini kwa ghafla alishtuka kama mtu aliyezindukana usingizi na mara lilimtoka swali, “Sasa Kijakazi siku zote hizi zilizopita nini kilichokuzuia usije kujiunga na sisi hapa?”

“Ujinga wangu,” bila ya kufikiri Kijakazi alijibu.

“Sasa ukitoka hapa unarejea kwa Fuad?” Vuai aliulizatena.

“Lo, Mungu apishe mbali! Nitatokomea po pote pale lakini sitarudi tena kwa yule mwizi wa fadhila asiyejua wema wala hisani.”

“Sasa sikiliza Kijakazi,” Vuai alianza kusema “sisi sote tunaoishi hapa ni sawa sawa na wanao. Yaliyokufika wewe na sisi yametufika vile vile ila wewe mwenzetu umetuzidi. Lakini ndyo ulimwengu, kwani mambo huzidiana. Sasa Kijakazi mimi nakushauri bora uje hapa ili ujiunge na sisi watoto wako tushirikiane kufanya kazi pamoja na wewe utakuwa mwanachama kamili wa shamba hili la ushirika na utapata haki sawa sawa kama mwanachama yo yote yule; au una shauri gani?”

Kijakazi al’ogopa kujibu kitu cho chote kile, lakini mara alisema, “Ah! Nadhani hamtakuwa na haja ya mwanachama mtu mzima kama mimi. Mimi sina nguvu tena za kufanya kazi yo yote; mimi nimekwisha kabisa na pahala kama hapa panahitaji mtu mwenye nguvu anayeweza kufanya kazi.”

“Basi umekuja hapa kutuhadithia habari za Fuad tu?” Vuai alimwuliza Kijakazi kwa masihara huku akitabasamu. Mara Vuai aliendelea na kusema, “Kijakazi juu ya utu uzima uliokuwa nao sisi tutakuchukua katika shamba letu. Utakuwepo hapa kwa muda na serikali ya kimapinduzi ya ASP ina mipango madhubuti kuhusu watu wazima kama nyinyi. Zipo nyumba maalum zinajengwa kwa ajili yenu huko Sebulen, usitie wasiwasi wo wote. Kama nilivyokwambia sisi sote hapa ni kama watoto wako na sisi tutakuenzi wewe kama mzee wetu. Wewe Kijakazi una maarifa ya s’ku nyingi katika kazi za ufugaji na tutafurahi pindi ukiweza kuwapa vijana wetu maarifa yako katika kazi hiyo. Wao watakuwa tayari wakati wo wote kujifunza kutoka kwako. Sisi tulitumaini kwamba utakuja kujiunga na sisi zamani lakini ulichelewa. Njoo, Kijakazi, uishi na sisi hapa.”

Kijakazi aliruka kwa furaha na mara aliukamata mkono wa Vuai na kutaka kuubusu lakini Vuai aliurusha mkono wake na kusema. “Kijakazi tabia hiyo itakubidi uiache hapa. Sisi hapa sote m wanachama sawa sawa vva shamba hili la ushirika na hapana mtukufu miongoni mwetu ambaye anataka kubusiwa mikono. Wewe Kijakazi utakuwa pamoja na sisi hapa lakini kwanza itakubidi ukapumzike na upate matibabu huko hospitalini. Sasa itakubidi urejee kwa Fuad ili ukachukue vitu vyako na halafu urejee hapa.”

“Nani? Mimi? Mimi sina cho chote huko kwa Fuad, vitu vyangu vyote nilivyonavyo ni haya magwanda niliyovaa,” Kijakaz’ alisema huku akishusha pumzi kama mtu aliyetuliwa mzigo mz’to.

Kijakazi alishtuka kwa sauti ya mvumo mkubwa aliousikia, masikio yakamziba. Alitaka kufanya kama kukimbia lakini mara aliona makundi ya watu wakitoka kutoka kwenye mabanda mbali mbali. Ilikuwa ni saa kumi na mbili magharibi na sauti ile ilikuwa ni sauti ya king’ora iliyotowa ishara ya kumalizika kwa saa za kazi.

Kwa mbali Kijakazi aliliona kundi la wanawake waliokazana miongoni mwao akiwamo Mkongwe. Kijakazi alimfuatia Mkongwe mbiyo huku akimpigia makelele na alipokutana naye alimkumbatia huku machozi yakimtoka.

“Kweli, mwanangu! Yote uliyokuwa ukiniambia ni kweli tupu” Kijakazi alimwambia Mkongwe huku akisugua uso wake juu ya mabega ya Mkongwe.

Mkongwe hakumjibu kitu. Kundi la watu waliokuwa wakitoka makazini mwao walimzongea Kijakazi ambaye al’kuwa bado amemkumbatia Mkongwe huku machozi yakimmiminika. Wote waliingiwa na hamu ya kumwona Kijakazi kwani siku nyingi walikwisha kusikia hadithi zake.

“Nyamaza shoga, nyamaza shoga yangu, usilie; hapa umefika kwenu na sote tukikungojea kwa hamu kubwa. Twende zetu.” Mkongwe alimshika mkono Kijakazi na kumwongoza chumbani kwake.

Mara Vuai alinyanyua sauti yake na kumwuliza Mkongwe, “Unafikiri Kijakazi leo atalala wapi?”

“Haidhuru mimi niko tayari kulala po pote pale!” Kijakazi alisema kwa ghafla huku ak’jipangusa machozi.

“Atalala na mimi: yeye atalala juu ya kitanda na mimi nitatandika mkeka chini nakulala hapo. Karibu pamoja na sisi shoga yangu,” alisema Mkongwe.

“Ahsante, shoga yangu, ahsante!”

Mkongwe alimwongoza Kijakazi mpaka chumbani kwake ambako walilala pamoja siku ile.

Fuad alibakia peke yake, mambo yalimbadilikia, na hatimaye hakuweza tena kuisbi Unguja. Aliondoka kwa njia ya magendo, labda kwa kutumia n’galawa au mashua. na bapana aliyejua alitokomea wapi.

MWISHO


cc Great God

Safi sana... Bonge la story...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom