the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,611
- 7,063
- Thread starter
-
- #201
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA AROBAINI NA NNE.
__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------
Mama kayoza na Mchungaji Wingo wakawa wameshika njia ya kwenda walipo wakina kayoza,
"Mungu wangu, awa watoto wapumbavu sana" Mama Kayoza alilalama baada ya kuona wanamdhalilisha mbele ya Mchungaji,
"Alafu hata yule binti waliekuwa nae ni mjinga, eneo la hospitali unavaaje vile kama huna wazazi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku wakiwa bado wanaelekea sehemu walipo wakina Kayoza.
Wakiwa wanazidi kuwasogelea na wamebakiza hata zisizo nyingi sana, Mara pasipo kutegemea, Mchungaji Wingo akatoa sauti ya mguno,
"mh!"
"vipi mchungaji?",Mama Kayoza akauliza..
***********ENDELEA*********
.."kuna fikra zimenijia",Mchungaji Wingo akajibu katika sauti iliyotulia,
"nishirikishe tu mchungaji",Mama kayoza, nae akaomba ubia,
"ujue katika mazingira kama yale waliopo vijana wako, sio vizuri sisi kufika pale, maana tunaweza kufanya wakose raha kabisa, hasa yule aliyekuwa na binti"
,Mchungaji Wingo alitoa busara zake,
"kwanini tusiende tu, wakituona ndio watapata funzo, hawatarudia tena kufanya uovu katika eneo la wazi kama hili",Mama Kayoza aliongea katika sura iliyojaa jazba,
"hapana mama, wewe waache tu, ila ukifika nyumbani uwaambie vyote ulivyoviona",Mchungaji alimwambia Mama Kayoza
"sawa mchungaji, ila hawa watoto wamenihaibisha jamani, loh!",Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko.
"ni ujana tu mama, ila itafika kipindi watajua kuwa wanachofanya ni ujinga",Mchungaji aliongea kwa upole.
"Yaani wanafanya ujinga uliokithiri, badala wakae hata wafunge wamuombee mjomba wao, wao wanazidi kujiongezea dhambi" Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko,
"Bado hawajawa na akili hizo, ila kama nilivyosema kuwa itafika muda watajitambua" Mchungaji Wingo alijibu,
"Alafu na yule binti sijui wa wapi?, ebu mchungaji niruhusu tu nikawaone nimtambue na yule binti" Mama Kayoza aliongea,
"Kwa jinsi alivyovaa vile, ukienda pale itakuwa kama anakudhalilisha tu mwanamke mwenzake. Sio uvaaji ule, mi mwanangu akivaa vile namchinjilia mbali" Mchungaji Wingo aliongea kwa hasira,
"Haya baba, tuondoke tu, nitaenda kupambana nao nyumbani" Mama Kayoza aliongea.
Wakabadili njia na kushika njia iendayo nje ya hospitali. Hakuna aliyekuwa anaongea tena, kila mtu alikuwa na wazo lake, ila Mama Kayoza alionekana ana hasira nyingi zilizochanganyikana na fedhea iliyotokana na kitendo kilichofanywa na watoto wake.
Hasira aliyokuwa nayo ilisababisha mpaka machozi yaanze kuchomozà katika ncha za macho yake,
"Mbona kama unalia mama?" Mchungaji Wingo alimuuliza mama Kayoza,
"Hapana, ni hasira tu. Yaani away watoto" Mama Kayoza alijibu Mchungaji Wingo,
"Hutakiwi kuwaza sana, utavuka mipaka na mwisho itakuwa dhambi, kuwa na moyo wa hekima mama" Mchungaji Wingo alimwambia Mama Kayoza,
"Sawa nimekusikia mchungaji" Mama Kayoza aliongea huku akijifuta machozi,
"mama unaelekea wapi sasa hivi?",Mchungaji alimuuliza mama Kayoza wakiwa nje ya geti la hospitali,
"nataka nipitie hapo sokoni nikachukue mahitaji ya nyumbani kidogo",Mama Kayoza alimjibu Mchungaji Wingo.
"ok, ni vizuri, maana hata mimi naelekea uko uko",Mchungaji Wingo aliongea huku akionekana kuvutiwa na jibu la mama Kayoza.
Kisha akawasha gari yake, na kuelekea maeneo ya sokoni.
*******************
Mkuu wa Polisi aliamua kuifatilia ile kesi kwa elimu yake yote aliyonayo, kwa mbinu zake zote alizokuwa nazo na kwa uzoefu wake wote aliokuwanao, ila hakutaka kumshirikisha askari yoyote, kwa maana alishakosa imani na askari wake.
Na kwa kuanza, aliamua kumfuatilia Omari kwanza. Aliamini kwa kiasi kikubwa, kuwa ile picha iliyotolewa katika magazeti, ni taswira ya Omari kabisa, ila alichokuwa anafuatilia ni ushaidi tu.
"Ukila na kipofu hutakiwi kumshika mkono" Mkuu wa polisi aliongea na kutabasamu mwenyewe.
"na nikipata ushaidi wa kutosha tu, nahakikisha Sajenti Minja nae anafunguliwa mashtaka, lakini kama atapona, kama akifa na yenyewe itakuwa sawa, kwa maana yeye ni msaliti. Anakaa na mtuhumiwa na hasemi, hata kama ni ndugu yake inatakiwa afuate sheria", Mkuu wa Polisi aliongea na nafsi yake, kisha akaendelea,.
"kesho nitamtafuta kijana mmoja wa mtaani, anisaidie kuchunguza taratibu hii kesi, siwezi kumpa askari hii kesi, bora nimtafute kijana achunguze taratibu nitamlipa pesa, tena itakuwa vzuri zaidi kama huyo kijana atakuwa anaishi mtaa ule ule wanaoishi wao".
Hayo ndiyo maamuzi aliyofikia mkuu wa polisi. Na uzuri wa huyu bwana ni kusimamia maneno yake, ni mtu aliyekuwa anasifika kutokana na utendaji kazi wake na pia kulikuwa na tetesi kuwa huyu ndiye atakuwa mkuu wa polisi wa nchi nzima mwaka unafuata.
******************
Wakina Omary walikuwa bado wanaendelea kula starehe zao na walikuwa hawana habari kama tayari mama yao alikuwa amewaona.
Hiyo siku Omary aliamua kujikumbushia maisha yake ya chuo, kukaa katika garden na mtoto wa kike kama vile huku wakila ice cream ndio ilikuwa maisha yake.
Kipindi chote hicho Kayoza alikuwa amekaa kimya ingawa alikuwa anataka kuondoka ila hakutaka kumwambia Omary kwa maana alihisi kama atamuharibia au atamkatishia starehe mwenzake, na alipofikiria kumtoroka pia aliwaza akifika nyumbani akiulizwa mwenzake yupo wapi? atajibu nini na walitoka pamoja?
Ikabidi akae kinyonge tu huku akicheza game katika simu yake alipochoka alikichukua kitabu chake cha riwaya kilichoitwa FAZA WA KANISA kilichoandikwa na mwandishi ALEX KILEO, akawa anakisoma.
"jamani eee, mi naona tuondoke sasa",Kayoza aliwaambia wenzake baada ya kusoma kurasa kadhaa za kile kitabu cha riwaya,
"dah!, kweli mzazi, maana tumeuza kichizi", Omari alijibu kwa lugha ya vijana, akiwa na maana ya kwamba, wamekaa sana,
"tunaenda kwa miguu au?",Kayoza akauliza,
"leo kwa kuwa niko na malkia wangu hapa, nitakodi taxi", Omari aliongea huku akimshika mkono Happy binti wa Mchungaji.
"Tutembeeni tu, kwani tunawahi wapi?" Happy binti Mchungaji aliuliza huku akitabasamu,
"Hatutaki uchafuke, mrembo kama wewe ukichafuka kisa umetembea kwa miguu itakuwa aibu kwetu" Kayoza aliongea kwa utani na kufanya wenzie wacheke,
"Mbona mi nimeshazoea jamani" Happy binti mchungaji aliongea huku akideka kwa Omary,
"Umezoea kwenu ila sio kwangu. K ita gari mwanangu tusepe" Omary alimuagiza Kayoza kwa nyodo na kumfanya Kayoza aondoke huku akitabasamu kutokana na mbwembwe za jamaa yake huyo.
Wakatafuta taxi, wakakubaliana bei na dereva taxi, kisha safari ya kurudi nyumbani ikaanza.
Kayoza alikaa kiti cha mbele na Omary na Happy binti mchungaji walikaa siti za nyuma kwa ajili ya kuwa huru kufanya mambo yao kama wapenzi.
Walipokaribia katika maeneo ambapo Sajenti Minja alipata ajali, wakamshauri dereva taxi apunguze mwendo kwa maana kulikuwa na kona mbaya na pia bado walikuwa na kumbukumbu ya tukio baya lililomkuta Sajenti Minja katika eneo hilo.
Wakakata kona ya kwanza vzuri tu, ile wanakata kona ya pili tu, dereva taxi akafunga breki kali sana, ila alichelewa, maana tayari alishaikwangua kwa nyuma gari iliyopo mbele yake, ilikuwa ni gari ya Mchungaji Wingo ambayo ndani pia alikuwepo mama Kayoza.
Katika gari waliyokuwamo wakina kayoza, Happy binti Mchungaji alikuwa kachanganyikiwa kabisa baada ya kugundua gari iliyopo mbele ni ya baba yake, na omary pia alikuwa katika hali hiyo ya kutokujielewa, maana aliamini kabisa leo ndio arobaini yake.
Mchungaji Wingo na Mama Kayoza wakatelemka katika gari ya Mchungaji, na Mchungaji akionekana mwenye hasira ya kukwanguliwa gari yake, akawa anaifuata taxi waliyokuwamo wakina Kayoza, Omari na Happy binti wa mchungaji, hapo ndipo hali za vijana hao zikawa mbaya zaidi kwa hofu.......
**********ITAENDELEA**********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA AROBAINI NA NNE.
__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------
Mama kayoza na Mchungaji Wingo wakawa wameshika njia ya kwenda walipo wakina kayoza,
"Mungu wangu, awa watoto wapumbavu sana" Mama Kayoza alilalama baada ya kuona wanamdhalilisha mbele ya Mchungaji,
"Alafu hata yule binti waliekuwa nae ni mjinga, eneo la hospitali unavaaje vile kama huna wazazi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku wakiwa bado wanaelekea sehemu walipo wakina Kayoza.
Wakiwa wanazidi kuwasogelea na wamebakiza hata zisizo nyingi sana, Mara pasipo kutegemea, Mchungaji Wingo akatoa sauti ya mguno,
"mh!"
"vipi mchungaji?",Mama Kayoza akauliza..
***********ENDELEA*********
.."kuna fikra zimenijia",Mchungaji Wingo akajibu katika sauti iliyotulia,
"nishirikishe tu mchungaji",Mama kayoza, nae akaomba ubia,
"ujue katika mazingira kama yale waliopo vijana wako, sio vizuri sisi kufika pale, maana tunaweza kufanya wakose raha kabisa, hasa yule aliyekuwa na binti"
,Mchungaji Wingo alitoa busara zake,
"kwanini tusiende tu, wakituona ndio watapata funzo, hawatarudia tena kufanya uovu katika eneo la wazi kama hili",Mama Kayoza aliongea katika sura iliyojaa jazba,
"hapana mama, wewe waache tu, ila ukifika nyumbani uwaambie vyote ulivyoviona",Mchungaji alimwambia Mama Kayoza
"sawa mchungaji, ila hawa watoto wamenihaibisha jamani, loh!",Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko.
"ni ujana tu mama, ila itafika kipindi watajua kuwa wanachofanya ni ujinga",Mchungaji aliongea kwa upole.
"Yaani wanafanya ujinga uliokithiri, badala wakae hata wafunge wamuombee mjomba wao, wao wanazidi kujiongezea dhambi" Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko,
"Bado hawajawa na akili hizo, ila kama nilivyosema kuwa itafika muda watajitambua" Mchungaji Wingo alijibu,
"Alafu na yule binti sijui wa wapi?, ebu mchungaji niruhusu tu nikawaone nimtambue na yule binti" Mama Kayoza aliongea,
"Kwa jinsi alivyovaa vile, ukienda pale itakuwa kama anakudhalilisha tu mwanamke mwenzake. Sio uvaaji ule, mi mwanangu akivaa vile namchinjilia mbali" Mchungaji Wingo aliongea kwa hasira,
"Haya baba, tuondoke tu, nitaenda kupambana nao nyumbani" Mama Kayoza aliongea.
Wakabadili njia na kushika njia iendayo nje ya hospitali. Hakuna aliyekuwa anaongea tena, kila mtu alikuwa na wazo lake, ila Mama Kayoza alionekana ana hasira nyingi zilizochanganyikana na fedhea iliyotokana na kitendo kilichofanywa na watoto wake.
Hasira aliyokuwa nayo ilisababisha mpaka machozi yaanze kuchomozà katika ncha za macho yake,
"Mbona kama unalia mama?" Mchungaji Wingo alimuuliza mama Kayoza,
"Hapana, ni hasira tu. Yaani away watoto" Mama Kayoza alijibu Mchungaji Wingo,
"Hutakiwi kuwaza sana, utavuka mipaka na mwisho itakuwa dhambi, kuwa na moyo wa hekima mama" Mchungaji Wingo alimwambia Mama Kayoza,
"Sawa nimekusikia mchungaji" Mama Kayoza aliongea huku akijifuta machozi,
"mama unaelekea wapi sasa hivi?",Mchungaji alimuuliza mama Kayoza wakiwa nje ya geti la hospitali,
"nataka nipitie hapo sokoni nikachukue mahitaji ya nyumbani kidogo",Mama Kayoza alimjibu Mchungaji Wingo.
"ok, ni vizuri, maana hata mimi naelekea uko uko",Mchungaji Wingo aliongea huku akionekana kuvutiwa na jibu la mama Kayoza.
Kisha akawasha gari yake, na kuelekea maeneo ya sokoni.
*******************
Mkuu wa Polisi aliamua kuifatilia ile kesi kwa elimu yake yote aliyonayo, kwa mbinu zake zote alizokuwa nazo na kwa uzoefu wake wote aliokuwanao, ila hakutaka kumshirikisha askari yoyote, kwa maana alishakosa imani na askari wake.
Na kwa kuanza, aliamua kumfuatilia Omari kwanza. Aliamini kwa kiasi kikubwa, kuwa ile picha iliyotolewa katika magazeti, ni taswira ya Omari kabisa, ila alichokuwa anafuatilia ni ushaidi tu.
"Ukila na kipofu hutakiwi kumshika mkono" Mkuu wa polisi aliongea na kutabasamu mwenyewe.
"na nikipata ushaidi wa kutosha tu, nahakikisha Sajenti Minja nae anafunguliwa mashtaka, lakini kama atapona, kama akifa na yenyewe itakuwa sawa, kwa maana yeye ni msaliti. Anakaa na mtuhumiwa na hasemi, hata kama ni ndugu yake inatakiwa afuate sheria", Mkuu wa Polisi aliongea na nafsi yake, kisha akaendelea,.
"kesho nitamtafuta kijana mmoja wa mtaani, anisaidie kuchunguza taratibu hii kesi, siwezi kumpa askari hii kesi, bora nimtafute kijana achunguze taratibu nitamlipa pesa, tena itakuwa vzuri zaidi kama huyo kijana atakuwa anaishi mtaa ule ule wanaoishi wao".
Hayo ndiyo maamuzi aliyofikia mkuu wa polisi. Na uzuri wa huyu bwana ni kusimamia maneno yake, ni mtu aliyekuwa anasifika kutokana na utendaji kazi wake na pia kulikuwa na tetesi kuwa huyu ndiye atakuwa mkuu wa polisi wa nchi nzima mwaka unafuata.
******************
Wakina Omary walikuwa bado wanaendelea kula starehe zao na walikuwa hawana habari kama tayari mama yao alikuwa amewaona.
Hiyo siku Omary aliamua kujikumbushia maisha yake ya chuo, kukaa katika garden na mtoto wa kike kama vile huku wakila ice cream ndio ilikuwa maisha yake.
Kipindi chote hicho Kayoza alikuwa amekaa kimya ingawa alikuwa anataka kuondoka ila hakutaka kumwambia Omary kwa maana alihisi kama atamuharibia au atamkatishia starehe mwenzake, na alipofikiria kumtoroka pia aliwaza akifika nyumbani akiulizwa mwenzake yupo wapi? atajibu nini na walitoka pamoja?
Ikabidi akae kinyonge tu huku akicheza game katika simu yake alipochoka alikichukua kitabu chake cha riwaya kilichoitwa FAZA WA KANISA kilichoandikwa na mwandishi ALEX KILEO, akawa anakisoma.
"jamani eee, mi naona tuondoke sasa",Kayoza aliwaambia wenzake baada ya kusoma kurasa kadhaa za kile kitabu cha riwaya,
"dah!, kweli mzazi, maana tumeuza kichizi", Omari alijibu kwa lugha ya vijana, akiwa na maana ya kwamba, wamekaa sana,
"tunaenda kwa miguu au?",Kayoza akauliza,
"leo kwa kuwa niko na malkia wangu hapa, nitakodi taxi", Omari aliongea huku akimshika mkono Happy binti wa Mchungaji.
"Tutembeeni tu, kwani tunawahi wapi?" Happy binti Mchungaji aliuliza huku akitabasamu,
"Hatutaki uchafuke, mrembo kama wewe ukichafuka kisa umetembea kwa miguu itakuwa aibu kwetu" Kayoza aliongea kwa utani na kufanya wenzie wacheke,
"Mbona mi nimeshazoea jamani" Happy binti mchungaji aliongea huku akideka kwa Omary,
"Umezoea kwenu ila sio kwangu. K ita gari mwanangu tusepe" Omary alimuagiza Kayoza kwa nyodo na kumfanya Kayoza aondoke huku akitabasamu kutokana na mbwembwe za jamaa yake huyo.
Wakatafuta taxi, wakakubaliana bei na dereva taxi, kisha safari ya kurudi nyumbani ikaanza.
Kayoza alikaa kiti cha mbele na Omary na Happy binti mchungaji walikaa siti za nyuma kwa ajili ya kuwa huru kufanya mambo yao kama wapenzi.
Walipokaribia katika maeneo ambapo Sajenti Minja alipata ajali, wakamshauri dereva taxi apunguze mwendo kwa maana kulikuwa na kona mbaya na pia bado walikuwa na kumbukumbu ya tukio baya lililomkuta Sajenti Minja katika eneo hilo.
Wakakata kona ya kwanza vzuri tu, ile wanakata kona ya pili tu, dereva taxi akafunga breki kali sana, ila alichelewa, maana tayari alishaikwangua kwa nyuma gari iliyopo mbele yake, ilikuwa ni gari ya Mchungaji Wingo ambayo ndani pia alikuwepo mama Kayoza.
Katika gari waliyokuwamo wakina kayoza, Happy binti Mchungaji alikuwa kachanganyikiwa kabisa baada ya kugundua gari iliyopo mbele ni ya baba yake, na omary pia alikuwa katika hali hiyo ya kutokujielewa, maana aliamini kabisa leo ndio arobaini yake.
Mchungaji Wingo na Mama Kayoza wakatelemka katika gari ya Mchungaji, na Mchungaji akionekana mwenye hasira ya kukwanguliwa gari yake, akawa anaifuata taxi waliyokuwamo wakina Kayoza, Omari na Happy binti wa mchungaji, hapo ndipo hali za vijana hao zikawa mbaya zaidi kwa hofu.......
**********ITAENDELEA**********
the Legend☆