Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Riwaya: Kijijini kwa Bibi

RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA NNE.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

Mama kayoza na Mchungaji Wingo wakawa wameshika njia ya kwenda walipo wakina kayoza,

"Mungu wangu, awa watoto wapumbavu sana" Mama Kayoza alilalama baada ya kuona wanamdhalilisha mbele ya Mchungaji,

"Alafu hata yule binti waliekuwa nae ni mjinga, eneo la hospitali unavaaje vile kama huna wazazi?" Mchungaji Wingo aliuliza huku wakiwa bado wanaelekea sehemu walipo wakina Kayoza.

Wakiwa wanazidi kuwasogelea na wamebakiza hata zisizo nyingi sana, Mara pasipo kutegemea, Mchungaji Wingo akatoa sauti ya mguno,

"mh!"

"vipi mchungaji?",Mama Kayoza akauliza..

***********ENDELEA*********

.."kuna fikra zimenijia",Mchungaji Wingo akajibu katika sauti iliyotulia,

"nishirikishe tu mchungaji",Mama kayoza, nae akaomba ubia,

"ujue katika mazingira kama yale waliopo vijana wako, sio vizuri sisi kufika pale, maana tunaweza kufanya wakose raha kabisa, hasa yule aliyekuwa na binti"
,Mchungaji Wingo alitoa busara zake,

"kwanini tusiende tu, wakituona ndio watapata funzo, hawatarudia tena kufanya uovu katika eneo la wazi kama hili",Mama Kayoza aliongea katika sura iliyojaa jazba,

"hapana mama, wewe waache tu, ila ukifika nyumbani uwaambie vyote ulivyoviona",Mchungaji alimwambia Mama Kayoza

"sawa mchungaji, ila hawa watoto wamenihaibisha jamani, loh!",Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko.

"ni ujana tu mama, ila itafika kipindi watajua kuwa wanachofanya ni ujinga",Mchungaji aliongea kwa upole.

"Yaani wanafanya ujinga uliokithiri, badala wakae hata wafunge wamuombee mjomba wao, wao wanazidi kujiongezea dhambi" Mama Kayoza aliongea kwa masikitiko,

"Bado hawajawa na akili hizo, ila kama nilivyosema kuwa itafika muda watajitambua" Mchungaji Wingo alijibu,

"Alafu na yule binti sijui wa wapi?, ebu mchungaji niruhusu tu nikawaone nimtambue na yule binti" Mama Kayoza aliongea,

"Kwa jinsi alivyovaa vile, ukienda pale itakuwa kama anakudhalilisha tu mwanamke mwenzake. Sio uvaaji ule, mi mwanangu akivaa vile namchinjilia mbali" Mchungaji Wingo aliongea kwa hasira,

"Haya baba, tuondoke tu, nitaenda kupambana nao nyumbani" Mama Kayoza aliongea.

Wakabadili njia na kushika njia iendayo nje ya hospitali. Hakuna aliyekuwa anaongea tena, kila mtu alikuwa na wazo lake, ila Mama Kayoza alionekana ana hasira nyingi zilizochanganyikana na fedhea iliyotokana na kitendo kilichofanywa na watoto wake.

Hasira aliyokuwa nayo ilisababisha mpaka machozi yaanze kuchomozà katika ncha za macho yake,

"Mbona kama unalia mama?" Mchungaji Wingo alimuuliza mama Kayoza,

"Hapana, ni hasira tu. Yaani away watoto" Mama Kayoza alijibu Mchungaji Wingo,

"Hutakiwi kuwaza sana, utavuka mipaka na mwisho itakuwa dhambi, kuwa na moyo wa hekima mama" Mchungaji Wingo alimwambia Mama Kayoza,

"Sawa nimekusikia mchungaji" Mama Kayoza aliongea huku akijifuta machozi,

"mama unaelekea wapi sasa hivi?",Mchungaji alimuuliza mama Kayoza wakiwa nje ya geti la hospitali,

"nataka nipitie hapo sokoni nikachukue mahitaji ya nyumbani kidogo",Mama Kayoza alimjibu Mchungaji Wingo.

"ok, ni vizuri, maana hata mimi naelekea uko uko",Mchungaji Wingo aliongea huku akionekana kuvutiwa na jibu la mama Kayoza.

Kisha akawasha gari yake, na kuelekea maeneo ya sokoni.

*******************

Mkuu wa Polisi aliamua kuifatilia ile kesi kwa elimu yake yote aliyonayo, kwa mbinu zake zote alizokuwa nazo na kwa uzoefu wake wote aliokuwanao, ila hakutaka kumshirikisha askari yoyote, kwa maana alishakosa imani na askari wake.

Na kwa kuanza, aliamua kumfuatilia Omari kwanza. Aliamini kwa kiasi kikubwa, kuwa ile picha iliyotolewa katika magazeti, ni taswira ya Omari kabisa, ila alichokuwa anafuatilia ni ushaidi tu.

"Ukila na kipofu hutakiwi kumshika mkono" Mkuu wa polisi aliongea na kutabasamu mwenyewe.

"na nikipata ushaidi wa kutosha tu, nahakikisha Sajenti Minja nae anafunguliwa mashtaka, lakini kama atapona, kama akifa na yenyewe itakuwa sawa, kwa maana yeye ni msaliti. Anakaa na mtuhumiwa na hasemi, hata kama ni ndugu yake inatakiwa afuate sheria", Mkuu wa Polisi aliongea na nafsi yake, kisha akaendelea,.

"kesho nitamtafuta kijana mmoja wa mtaani, anisaidie kuchunguza taratibu hii kesi, siwezi kumpa askari hii kesi, bora nimtafute kijana achunguze taratibu nitamlipa pesa, tena itakuwa vzuri zaidi kama huyo kijana atakuwa anaishi mtaa ule ule wanaoishi wao".

Hayo ndiyo maamuzi aliyofikia mkuu wa polisi. Na uzuri wa huyu bwana ni kusimamia maneno yake, ni mtu aliyekuwa anasifika kutokana na utendaji kazi wake na pia kulikuwa na tetesi kuwa huyu ndiye atakuwa mkuu wa polisi wa nchi nzima mwaka unafuata.

******************
Wakina Omary walikuwa bado wanaendelea kula starehe zao na walikuwa hawana habari kama tayari mama yao alikuwa amewaona.

Hiyo siku Omary aliamua kujikumbushia maisha yake ya chuo, kukaa katika garden na mtoto wa kike kama vile huku wakila ice cream ndio ilikuwa maisha yake.

Kipindi chote hicho Kayoza alikuwa amekaa kimya ingawa alikuwa anataka kuondoka ila hakutaka kumwambia Omary kwa maana alihisi kama atamuharibia au atamkatishia starehe mwenzake, na alipofikiria kumtoroka pia aliwaza akifika nyumbani akiulizwa mwenzake yupo wapi? atajibu nini na walitoka pamoja?
Ikabidi akae kinyonge tu huku akicheza game katika simu yake alipochoka alikichukua kitabu chake cha riwaya kilichoitwa FAZA WA KANISA kilichoandikwa na mwandishi ALEX KILEO, akawa anakisoma.

"jamani eee, mi naona tuondoke sasa",Kayoza aliwaambia wenzake baada ya kusoma kurasa kadhaa za kile kitabu cha riwaya,

"dah!, kweli mzazi, maana tumeuza kichizi", Omari alijibu kwa lugha ya vijana, akiwa na maana ya kwamba, wamekaa sana,

"tunaenda kwa miguu au?",Kayoza akauliza,

"leo kwa kuwa niko na malkia wangu hapa, nitakodi taxi", Omari aliongea huku akimshika mkono Happy binti wa Mchungaji.

"Tutembeeni tu, kwani tunawahi wapi?" Happy binti Mchungaji aliuliza huku akitabasamu,

"Hatutaki uchafuke, mrembo kama wewe ukichafuka kisa umetembea kwa miguu itakuwa aibu kwetu" Kayoza aliongea kwa utani na kufanya wenzie wacheke,

"Mbona mi nimeshazoea jamani" Happy binti mchungaji aliongea huku akideka kwa Omary,

"Umezoea kwenu ila sio kwangu. K ita gari mwanangu tusepe" Omary alimuagiza Kayoza kwa nyodo na kumfanya Kayoza aondoke huku akitabasamu kutokana na mbwembwe za jamaa yake huyo.

Wakatafuta taxi, wakakubaliana bei na dereva taxi, kisha safari ya kurudi nyumbani ikaanza.

Kayoza alikaa kiti cha mbele na Omary na Happy binti mchungaji walikaa siti za nyuma kwa ajili ya kuwa huru kufanya mambo yao kama wapenzi.

Walipokaribia katika maeneo ambapo Sajenti Minja alipata ajali, wakamshauri dereva taxi apunguze mwendo kwa maana kulikuwa na kona mbaya na pia bado walikuwa na kumbukumbu ya tukio baya lililomkuta Sajenti Minja katika eneo hilo.

Wakakata kona ya kwanza vzuri tu, ile wanakata kona ya pili tu, dereva taxi akafunga breki kali sana, ila alichelewa, maana tayari alishaikwangua kwa nyuma gari iliyopo mbele yake, ilikuwa ni gari ya Mchungaji Wingo ambayo ndani pia alikuwepo mama Kayoza.

Katika gari waliyokuwamo wakina kayoza, Happy binti Mchungaji alikuwa kachanganyikiwa kabisa baada ya kugundua gari iliyopo mbele ni ya baba yake, na omary pia alikuwa katika hali hiyo ya kutokujielewa, maana aliamini kabisa leo ndio arobaini yake.

Mchungaji Wingo na Mama Kayoza wakatelemka katika gari ya Mchungaji, na Mchungaji akionekana mwenye hasira ya kukwanguliwa gari yake, akawa anaifuata taxi waliyokuwamo wakina Kayoza, Omari na Happy binti wa mchungaji, hapo ndipo hali za vijana hao zikawa mbaya zaidi kwa hofu.......

**********ITAENDELEA**********


the Legend☆
 
Wakuu kuna episodes 4 za hii riwaya nimejaribu kuzitafuta leo bila mafanikio, hiyo ndio sababu iliyofanya nichelewe kupost mpaka muda huu. Nazo ni episode ya 35-38. Nyingine zote zipo. So tutaendelea na episode ya 39. Samahanini kwa usumbufu utakaojitokeza

the Legend☆
Hatuna jinsi inabidi tukubaliane na hali
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA TANO.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

Mchungaji Wingo na Mama Kayoza wakatelemka katika gari ya Mchungaji, na Mchungaji akionekana mwenye hasira ya kukwanguliwa gari yake, akawa anaifuata taxi waliyokuwamo wakina Kayoza, Omari na Happy binti wa mchungaji, hapo ndipo hali za vijana hao zikawa mbaya zaidi kwa hofu.......

_______________
ENDELEA........
________________

...Dereva taxi baada ya kuona yule dereva wa gari aliyoigonga anakuja, kwa haraka sana happy alimwambia taxi atelemke kwa maana yule anaekuja ni baba yake na yeye hataki ajue kama yupo ndani, Dereva taxi nae akaamua kutelemka, ili akabiliane na Mchungaji Wingo,

"kijana leseni yako umekatiwa na serikali au umeipata mitaani?", ndio swali la kwanza kuuliza Mchungaji baada ya Dereva taxi kushuka, Mchungaji Wingo alikuwa na hasira sana na hilo lilionekana wakati anaongea maana sauti yake ilikuwa inatoka na mitetemo ya hasira,

"nisamehe mzee wangu",Dereva taxi alikimbilia kujitetea badala ya kujibu swali, pia dereva taxi alishapata yoga kutokana na hasira alizokuwa nazo,

"inaonesha hata shule hukuenda, maana nimekuuliza swali jingine, we unaniambia vitu vingine",Mchungaji aliendelea kumshambulia Dereva taxi ambae aliamua akae kimya.

"Leseni nimepata veta, nilisomea pale" Dereva taxi alijibu huku akitetemeka,

"Angalia sasa ulivyo mjinga, jibu la swali la kwanza unaweka katika swali la pili" Mchungaji Wingo aliongea huku akitoa tabasamu lisilo la furaha, lilikuwa tabasamu la karaha.

Wakiwa bado wanaangaliana, Dereva taxi akiwa hana la kuongea kutokana na maneno ya Mchungaji Wingo, na Mchungaji Wingo akiwa anasubiri Dereva taxi aongee ili aendelee kumshambulia.

Mlango wa mbele wa taxi ukafunguliwa, akatetelemka Kayoza,

"shikamoo Mchungaji",Kayoza akasalimia kwa mashaka huku akimtazama mama yake aliyekuwa anamuangalia kwa jicho Kali mpaka Kayoza akawa anajiuliza ni kosa gani amefanya mpaka mama yake amuangalie kwa jicho Kali vile,

"marhaba, kumbe wewe ndio umemkodi huyu?",Mchungaji alimuuliza kayoza huku kidole chake cha shahada kikimuelekea Dereva taxi,

"ndio mchungaji",Kayoza akajibu kwa unyenyekevu,

"alichokifanya hapa unakubaliana nacho?",Mchungaji alimtumpia swali jingine Kayoza,

"hapana, ni bahati mbaya",Kayoza alimtetea Dereva taxi,

"angaliaga vitu vya kutetea kijana, uwaga nakuona una busara sana",Mchungaji alimwambia Kayoza,

Kayoza akaamua kukaa kimya,

"ee, nijibu kijana, kwa hiyo angetugonga tukafa bado ungeng'ang'ania bahati mbaya?",Mchungaji aliendelea kung'aka kwa sauti ya upole iliyojaa hasira,

"naomba unisamehe mzee wangu, nitakulipa pesa ya kupaka rangi katika eneo nililolichubua",Dereva taxi alidakia pasipo kuhusishwa, maana aliona ili kujiepusha na ile habari pale basi ni lazima akubali kulipa gharama za uharibifu wa gari ya Mchungaji,

"acha uhuni bwana mdogo, nani kakwambia anahitaji pesa yako?"Mchungaji aliongea kwa ukali,

"nakubali nimefanya kosa mzee, naomba unisamehe",Dereva taxi aliongea kwa huruma kiasi kwamba machozi yalikuwa yanataka kumtoka,

"Imeandikwa Samehe saba Mara sabini" Kayoza aliongea huku akitupa jicho lake pembeni lisikutane na jicho la mchungaji na kufanya mchungaji atoe tabasamu huku akimuangalia Kayoza,

"Imeandikwa na nani, sura ya ngapi na mstari wa ngapi?" Mchungaji alimuuliza Kayoza ambaye alikuwa hana jibu akabaki tu kuangalia chini,

"Ni neno la Mungu liko kwenye biblia" Kayoza alijibu na kumfanya Mchungaji acheke kabisa, kwa maana maneno anayoongea Kayoza yalikuwa yanamtoka tu bila kutarajia,

"Dereva we nenda bwana, mimi sina neno na wewe ila nilitaka nikufundishe ili usirudie kwa watu wengine",Mchungaji alimwambia Dereva taxi,

"asante sana mzee wangu",Dereva taxi alishukuru

"Usinishukuru Mimi, mshukuru huyu Mteja wako alietoa neno la Mungu" Mchungaji Wingo aliongea huku akiondoka eneo alilokuwepo Kayoza na Dereva taxi,

"Man turudi katika gari tuendelee na safari" Dereva taxi alimwambia Kayoza,

"Wapeleke hao, Mimi itabidi niondoke na hao wazee" Kayoza alijibu na kumfanya Dereva taxi ageuke na kwenda kupanda katika gari yake na kuliondoa kwa mwendo wa kistaharabu.

"we Kayoza mwenzako yuko wapi?",Mama Kayoza alimuuliza mwanae wakati anaingia katika gari ya Mchungaji Wingo,

"khe!, bi mkubwa hata sijakaa vizuri umeanza na maswali, ngoja nitulie kwanza",Kayoza alishangaa mama yake kuanza kumshambulia ndani ya gari,

"nijibu bwana",Mama alisisitiza tena kwa hasira,

"Alafu mbona unaonekana una hasira sana na Mimi, nimekukosea nini leo?" Kayoza aliuliza huku akimuangalia mama yake,

"Wewe usiniletee ujinga ujue, si nimekuuliza hapa? Badala unijibu na wewe unauliza, ndio ulivyofunzwa hivyo na shangazi zako" Mama Kayoza aliuliza huku macho yake yakiwa mekundu kwa ajili ya hasira aliyokuwa nayo,

"Umeuliza nini kwani?" Kayoza aliuliza tena na kumfanya Mama yake azidishe hasira,

"Mpumbavu mwenzako yupo wapi?" Mama Kayoza aliuliza kwa sauti ya juu mpaka Mchungaji akatabasamu kwa namna Mama Kayoza alivyopaniki,

"Atakuwa yuko nyumbani",Kayoza alijibu bila ya uhakika kwa maana hakujua kama Omary ataenda nyumbani au atakuwa bado anatanua na Happy binti Mchungaji,

"nyie hospitali si mlikuwa pamoja, sasa imekuaje mnarudi kwa mafungu?",Mama kayoza akaongeza swali lingine lililomshtua Kayoza, ila akajifanya yupo sawa tu,

"we umejuaje tulikuwa hospitali wakati hatukukuaga?",Kayoza nae akamtupia swali mama yake,

"sisi ndo tumetoka huko na tuliwaona",Mama Kayoza akamjibu mwanae

"mlikuwa upande gani, mbona hukuja eneo tulilokuwepo?",Kayoza akaendelea kuhoji,

"ningekuja vipi wakati mlikuwa na mkwe pale, si ndio kilichowaleta huku shinyanga, kutafuta wanawake tu wanaovaa hivyo hovyo",Mama kayoza alimjibu mwanae wakati anatelemka katika gari kuashiria wamefika, hill jibu lilimshtua Kayoza kwa maana aliamini kabisa Mchungaji atakuwa amewaona wakati Wapi na Happy.

Mama Kayoza na Mwanae baada ya kutelemka katika gari ya Mchungaji Wingo, wakamuaga mchungaji,

"Kijana kuweni makini sana na mabinti wa watu, huku shinyanga ni kubaya sana" Mchungaji Wingo alimwambia Kayoza kisha hakutaka kusubiri neno lolote kutoka kwa Kayoza, Mchungaji akaondoa gari yake kwa mwendo wa taratibu na kumuacha Kayoza akiwa anaitafakari ile kauli ya mchungaji Wingo ya kuwa makini na mabinti za watu,

"We Kayoza twende ndani, mbona umeganda kama kichuguu?" Mama Kayoza alimgutusha mwanae kutoka katika tafakari na kumfanya Kayoza atabasamu ili mama yake amuone yuko sawa.

Wkuingia ndani, ambapo walimkuta Omari anaangalia Runinga, Omari akamsalimia mama Kayoza.

"mkwe umemuacha wapi?",Mama Kayoza akamuuliza Omari huku akiwa bado na hasira zake,

"yupi tena huyo mama?",Omari akauliza huku anacheka kinafki, lakini nae tayari kengele ya hatari ilikuwa imeshagonga kichwani mwake, alidhani tayari picha yake na Happy Binti Mchungaji ilikuwa imeungua kumbe masikini ya Mungu hakuna kati ya Mama Kayoza wala Mchungaji Wingo aliyegundua kuwa yule binti waliyekuwa nae ni Happy binti Mchungaji.

"jifanye tu humjui, kumbukeni mna matatizo, msitake kujiongezea mengine",Mama Kayoza alimaliza huku akielekea chumbani kwake na kuwaacha vijana wake wakitazamana.

"vipi, kashtukia nini?",Omari alimuuliza Kayoza,

"anadai alituona hospital, ila sijajua kama wamegundua yule demu tuliekuwa nae ni happy, maana kauli zao sizielewi elewi zimekaa kimafumbo mafumbo ",Kayoza alimjibu Omari,

"He hii hatari, na mchungaji nae anasemaje?" Omary alimuuliza Kayoza huku wasiwasi ukianza kuchukua nafasi yake,

"Huyo hakuongea kitu kabisa, ila wakati ametushusha hapo nje, ameniacha na kauli tata sana, amesema tuwe makini na mabinti za watu" Kayoza alimwambia Omary,

"Itakuwa wamegundua nini?" Omary aliuliza kwa wasiwasi,

"Ila kama wangemgundua yule binti ni Happy wangetuambia tu, hakuna mzazi anaeweza kuvumilia mwanae kujiingiza katika mapenzi kabla ya ndoa, tena ukizingatia Baba mwenyewe ni mchungaji" Kayoza aliongea kwa kujipa moyo,

"Ila kweli man" Omary alimsapoti mwenzake,

"Nilivyoshuka katika taxi, mbona sikuwaona tena ndani ya
taxi? Maana kila nikijitahidi kuangalia sioni mtu", Kayoza aliuliza huku akicheka,

"tuliinama nyuma ya siti mwanangu", Omari alijibu kwa hali ya ushindi,

"mimi nilijua ndio tumekwisha",Kayoza nae akachomekea,

"we acha tu mwanangu, nilivyoona dereva kaingia ndani, nilimwambia awai, alivyonishusha tu, nikampatia mpunga wake kisha nikamwambia amuwaishe wife",Omari aliongea kwa kujiamini,

"ila mjomba, una zali",Kayoza alimfagilia Omari,

"mi bad number kaka, na nilipofika, nikamnyonya mate Happy hapo nje",Omari aliendelea kujinadi, lakini Kayoza hakuonekana kumsapoti tena na badala yake alikodolea macho nyuma ya Omari, ikambidi Omari ageuka aangalie anachoangalia Kayoza, hapo sasa ndio akakutanisha Macho yake na Macho ya Mama Kayoza ambaye alikua kasimama nyuma ya kiti alichokaa Omary huku akiwaangalia kwa jicho la hasira, hasira zaidi ya hasira alizokuwa nazo mwanzo........

*********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA SITA.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

"Nilivyoshuka katika taxi, mbona sikuwaona tena ndani ya taxi? Maana kila nikijitahidi kuangalia sioni mtu", Kayoza aliuliza huku akicheka,

"tuliinama nyuma ya siti mwanangu", Omari alijibu kwa hali ya ushindi,

"mimi nilijua ndio tumekwisha",Kayoza nae akachomekea,

"we acha tu mwanangu, nilivyoona dereva kaingia ndani, nilimwambia awai, alivyonishusha tu, nikampatia mpunga wake kisha nikamwambia amuwaishe wife",Omari aliongea kwa kujiamini,

"ila mjomba, una zali",Kayoza alimfagilia Omari,

"mi bad number kaka, na nilipofika, nikamnyonya mate Happy hapo nje",Omari aliendelea kujinadi, lakini Kayoza hakuonekana kumsapoti tena na badala yake alikodolea macho nyuma ya Omari, ikambidi Omari ageuka aangalie anachoangalia Kayoza, hapo sasa ndio akakutanisha Macho yake na Macho ya Mama Kayoza ambaye alikua kasimama nyuma ya kiti alichokaa Omary huku akiwaangalia kwa jicho la hasira, hasira zaidi ya hasira alizokuwa nazo mwanzo........

************ENDELEA************

..."nyie watoto mjue ni wapumbavu sana?",mama Kayoza aliongea kwa jazba, wakina Kayoza walitulia kimya, kisha akaendelea,

"mi nilifikiri kwa elimu ya chuo kikuu mliokuwa nayo mnaweza mkawa mnafikiri vitu vya maana, kumbe muda wote mnafikiria upumbavu tu, naishi na wajinga tu humu ndani tena mtanipa ugonjwa wa moyo bure, mi namfikiria kaka yangu, nyie mnafikiria mapenzi, hivi mnataka mimi nifanyaje?",Mama Kayoza aliuliza akitegemea kujibiwa, ila hakuna hata aliemjibu,
"eti Kayoza, si nawauliza nyie, ee?",Mama Kayoza aliongea huku akimuangalia mwanae,
"sasa mama unataka nikujibu nini",Kayoza aliongea katika sauti ya kupaniki",
"unamjibu nani hivyo?",Mama Kayoza alipamba moto, tena wa gesi, Kayoza akanyanyuka alipokaa na kuelekea chumbani kwao,
"endelea tu na kiburi chako, ila kina mwisho wake, na nina uhakika Kayoza utakuja kuniua na ugonjwa wa moyo", Mama Kayoza alimwambia mwanae wakati anaondoka, kisha akamgeukia Omari,
"Omari mimi sikujui ila nakulea kama mwanangu, hata siku moja sikuwai kufikiria kama utafanya kitendo kama nilichokiona leo, tena hadharani, alafu unakuja hapa unaanza kujisifu kwa ujinga uliokuwa unaufanya!?, wewe unafikiri heshima ninayokupa itakuwa katika kiwango gani?, ee!, nijibu Omari" ,Mama Kayoza alikuwa kama mbogo aliyejeruhiwa na risasi,

"mama naomba sana msamaha, ila haya ni mapito ya ujana mama yangu",Omari aliongea kwa hekima,

"mbadilike, nyie ni wasomi bwana, nawashangaa mnavyofanya ujinga",Mama Kayoza alimwaga sera zake,

"nakuahidi mama, haitokaa itokee tena, naomba uniamini mama yangu",Omari aliongea katika sura ya majuto na upole sana,

"shauri yenu bwana, kamuite mwenzio, muende mkaninunulie maziwa mie",Mama Kayoza aliongea huku anaelekea jikoni.

Omary akatoka sebuleni na kuelekea chumbani ambapo ndipo Kayoza alikuwepo,

"Twende tukanunue maziwa, mama ametutuma" Omary alimwambia Kayoza,

"Bado anawaka au amepoa kidogo?" Kayoza alimuuliza mwenzake,

"Amepoa, ila dah..inawezekana ni kweli tumefanya kitendo cha kipuuzi" omary aliongea kwa majuto kuonesha kuwa amekosa,

"Uwa inatokeaga, ila kumbuka kuwa hata katika kipindi cha huzuni uwa kuna muda mchache wa furaha" Kayoza aliongea huku akivaa fulana yake,

"Kweli ila sio kwa kiwango kile tulichofikia, tulipitiliza" Omary aliongea huku akitoka nje kumfuata mwenzake.

"Kawaida tu bwana, haina haja ya kujuta wala kusikitika" Kayoza aliongea huku nae akitoka,

******************

BAADA YA MIEZI MIWILI

wakina Kayoza na Mkuu wa polisi wakiwa katika eneo la hospitali, Mkuu wa polisi alitaka kuwatega tena, safari hii alitaka kujua kama awa vijana wameshawahi kuishi mkoani Dodoma.

"Nyie mmezaliwa mkoa huu huu?" Mkuu wa polisi aliwauliza,

"Mimi nimezaliwa bukoba" Kayoza alijibu kwa ufasaha huku akitabasama,

"Na remmy wewe ulizaliwa wapi rafiki yangu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimfunga Omary kifungo cha juu cha shati,

"Mimi kwetu Tanga na ndipo nilipozaliwa?" Omary alijibu huku nae akitabasamu,

"Elimu zenu zopoje, yaani mmesoma mpaka kidato cha ngapi?, maana nyie ni ndugu zangu sasa, nataka nijue elimu yenu ili niwaangalizie hajira" Mkuu wa polisi aliuliza swali kwa kutumia akili nyingi ili aweze kuwataka hisia wakina Kayoza na atimize upelelezi wake,

"Sisi tuna elimu ya chuo, chuo kikuu" Kayoza alijibu huku akidhani ni sifa kubwa kusema ana elimu ya chuo, hajui kuwa kama anapelelezwa,

"Chuo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akitabasamu,

"Chuo kikuu cha Dodoma, UDOM" omary alitoa jibu lililoanza kumpa mwanga mkuu wa polisi,

"Mlisomea nini pale?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Public relation, yaan mahusiano ya kijamii" Kayoza alijibu kwa kujiamini,

"Mmemaliza mwaka gani" Mkuu wa polisi aliendelea kuuliza,

"Mwaka jana, mwezi wa sita" Omary alitoa jibu lililomfanya Mkuu wa polisi aridhike kuwa ni kweli uenda awa vijana ndio wahusika wa mauaji, maana hata taarifa aliyokuwa nayo ulikuwa inasema ni wahitimu wa chuo, ila hawajarudi tena kuchukua vyeti vyao kutokana na kutafutwa na polisi baada ya kugundulika kuwa waliwaua wanafunzi wenzao wawili wa kike,

"Mna vyeti vyenu ili mniletee copy kesho na barua ya kuomba kazi, maana kuna kampuni ya jamaa yangu ya uchimbaji madini hapo kahama" Mkuu wa Polisi aliuliza sasa kupata uhakika wa vyeti,

"Vyeti hatuna, hatukwenda kuvifuata" Kayoza alijibu huku akijiuliza itakuwaje kama mkuu wa polisi atauliza sababu ya wao kutokwenda kuvifuata vyeti vyao, na kipindi hicho mkuu wa polisi alishaamini tayari hisia sake kuhusu Hawa vijana kuwa ndio wauaji wenyewe,

"Kwanini hamjavichukua sasa?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Matatizo ya ada, hali ya kiuchumi nyumbani ilikuwa ngumu kweli" Omary alijibu baada ya kumuona Kayoza akibabaika,

"Hata mjomba wenu hakuwasaidia?" Mkuu wa polisi aliwatupia swali jingine, ila kabla hawajajibu walimuona Daktari akiwafuata mbio mbio huku akihema juu juu, naona kwa ajili ya kukimbia sana na hata uso wake ulikuwa na furaha sana Siku hiyo tofauti na furaha anayokuwaga nayo siku nyingine,

"vipi Dokta, mbona hivyo?",Mkuu wa polisi alimuhoji Daktari,

"Taratibu mkuu, usiwe na papara na maswali yako ya kipolisi" Daktari aliongea kwa pupa huku furaha yake ikiwa bado ipo nae,

"Na wewe nawe uwa huishiwagi vituko? Sasa unavyokuja unakimbia hivyo alafu unapigia breki kwetu, ntaacha vipi kukuuliza?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akionekana hajapendezwa na kile kitendo cha daktari,

"OK, nisamehe mkuu, ila sikukusudia kukukera, nipo hapa mbele yako kwa sababu maalum" Daktari aliongea huku ile hali ya mzaha aliyokuwa nayo mwanzo ikiwa haipo tena,

"Sasa si ndio utuambie hiyo habari, wewe bwana vipi bwana" Mkuu wa polisi aliongea kwa sauti ya ukali kidogo,

"mgonjwa wenu kafumbua macho",Daktari aliwaletea habari ile ambayo ilikua kama uokovu kwao maana hata hasira zao zilikuwa zimeyeyuka ghafla kutokana na hizo habari,

"vipi, anaongea?",Mkuu wa Polisi aliuliza swali huku akiwa amemtolea macho daktari,

"sijajua bado, maana nilipomkuta katika hali hiyo nilimuacha na Daktari wa zamu na kuamua kuwafuata nyie",yule Daktari alijibu,

"Si tunaweza kwenda kumuona?" Kayoza alimuuliza daktari baada ya muda mrefu wa ukimya,

"Twendeni" Daktari alijibu huku akiondoka na kufanya wote waanze safari ya kuitafuta wodi ambayo kalazwa Sajenti Joel Minja.

Walipoenda wodi ya wagonjwa mahututi ambayo alilazwa Sajenti Minja hapo hawali, walikuta kitanda alicholala Sajenti Minja kitupu, ikambidi Daktari aliefuatana na wakina Kayoza amtafute Daktari wa zamu ili kujua mgonjwa amehamishiwa wapi. Alichukua simu yake na kumpigia mwenzake ili amuulize ni Wapi Sajenti Minja amehamishiwa,

"twendeni grade C",Daktari aliwaambia baada ya kukata simu, walipofika huko grade C, walimkuta Daktari wa zamu anamalizia kumpima Sajenti Minja, wakasubiri kwa muda kidogo, kisha wakaruhusiwa kuingia, walipofika katika kitanda alicholala Sajenti Minja, wote watatu wakajenga tabasamu katika nyuso zao, lakini Sajenti Minja alikuwa tofauti kidogo, hakuonesha kuwakumbuka kabisa,

"bado kumbukumbu hazijamrudia vizuri",Daktari wa zamu alimuambia Mkuu wa Polisi,

"itachukua muda gani kurejea katika hali yake?",Mkuu wa Polisi aliuliza,

"itategemea na nyinyi wenyewe, maana anapomuona mtu mara kwa mara ndio anapata kumbukumbu",Daktari alimjibu Mkuu wa Polisi, kisha wote wakawa wanamuangalia Sajenti Minja ambae alikuwa amelala uku macho yake yakiwa wazi yakipepesa pepesa,

"Amekonda aisee" Mkuu wa Polisi aliongea huku akiwa bado anamuangalia Sajenti Minja,

"Kukonda lazima, maana alikuwa anakula kwa mipira na dripu pekee" Daktari wa zamu alijibu huku akiuweka vizuri mkono wa Sajenti Minja,

"Sasa mpaka atengemae kabisa itachukua muda gani?" Mkuu wa polisi alimuuliza Daktari wa zamu,

"Hatuwezi kujua, ila kama atakuwa anakula vizuri na kunywa maji ya kutosha, anaweza kurudi kama hawali" Daktari alijibu,

"Ila hata hii hatua aliyofikia, ni hatua ya kumshukuru sana Mungu" Kayoza aliongea huku machozi ya furaha yakimtoka, alishindwa kuzuia hisia zake, aliamini mpigania ubinadamu wake amepona kwa hiyo ana uhakika wa kupona kwa maana Sajenti Minja ndiye mtu pekee aliyekuwa anaangaika nae kwa vitendo na maneno.

Wakati wakiwa bado wanaongea pembeni ya kitanda ambacho amelala Sajenti Minja, ndipo Sajenti Minja akamtolea macho mkuu wake wa Polisi huku akiwa kama anajitahidi kuvuta kumbukumbu juu ya mtu huyo,

"vipi Minja mbona unaniangalia sana, unanikumbuka?",Mkuu wa polisi akamuuliza swali Sajenti Joel Minja,

"ndio nimekukumbuka vizuri sana, ni mkuu wangu wa kazi",Sajenti alijibu kwa ufasaha kwa sauti iliyochoka sana kutokana na kulala kwa wiki nyingi sana.

lakini jibu la Sajenti Minja likampa njia Mkuu wa Polisi, akaona huo ndio wa wakati halisi wa kumjua na kumuumbua mtu anayejiita Remmy, na muda huo ndio alitaka ahakikishe kuwa yule kijana ambae anamtilia mashaka ni yeye haswa,

"huyu nae unamkumbuka?",Mkuu wa Polisi aliongea huku akimshika bega Kayoza, alikuwa na maana yake kuanza na Kayoza,

"huyo ni mtoto wa dada, anaitwa Kayoza",Sajenti Minja alijibu tena kuashiria kumbukumbu zimemrejea.

Omari na Kayoza waligundua mchezo anaocheza Mkuu wa Polisi, na wote walinyong'onyea kwa kujua kwamba wameumbuka, kwa maana anaefuata kutambulishwa ni Omari.

"huyu nae anaitwa nani?, taja majina yake yote matatu, ili nijue kumbukumbu yako imerudi",Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja huku akimsogeza Omary mbele ya macho ya Sajenti Minja....

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
Asante sana mkuu
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA AROBAINI NA SITA.

__________________
ILIPOISHIA....
-----------------------------

"Nilivyoshuka katika taxi, mbona sikuwaona tena ndani ya taxi? Maana kila nikijitahidi kuangalia sioni mtu", Kayoza aliuliza huku akicheka,

"tuliinama nyuma ya siti mwanangu", Omari alijibu kwa hali ya ushindi,

"mimi nilijua ndio tumekwisha",Kayoza nae akachomekea,

"we acha tu mwanangu, nilivyoona dereva kaingia ndani, nilimwambia awai, alivyonishusha tu, nikampatia mpunga wake kisha nikamwambia amuwaishe wife",Omari aliongea kwa kujiamini,

"ila mjomba, una zali",Kayoza alimfagilia Omari,

"mi bad number kaka, na nilipofika, nikamnyonya mate Happy hapo nje",Omari aliendelea kujinadi, lakini Kayoza hakuonekana kumsapoti tena na badala yake alikodolea macho nyuma ya Omari, ikambidi Omari ageuka aangalie anachoangalia Kayoza, hapo sasa ndio akakutanisha Macho yake na Macho ya Mama Kayoza ambaye alikua kasimama nyuma ya kiti alichokaa Omary huku akiwaangalia kwa jicho la hasira, hasira zaidi ya hasira alizokuwa nazo mwanzo........

************ENDELEA************

..."nyie watoto mjue ni wapumbavu sana?",mama Kayoza aliongea kwa jazba, wakina Kayoza walitulia kimya, kisha akaendelea,

"mi nilifikiri kwa elimu ya chuo kikuu mliokuwa nayo mnaweza mkawa mnafikiri vitu vya maana, kumbe muda wote mnafikiria upumbavu tu, naishi na wajinga tu humu ndani tena mtanipa ugonjwa wa moyo bure, mi namfikiria kaka yangu, nyie mnafikiria mapenzi, hivi mnataka mimi nifanyaje?",Mama Kayoza aliuliza akitegemea kujibiwa, ila hakuna hata aliemjibu,
"eti Kayoza, si nawauliza nyie, ee?",Mama Kayoza aliongea huku akimuangalia mwanae,
"sasa mama unataka nikujibu nini",Kayoza aliongea katika sauti ya kupaniki",
"unamjibu nani hivyo?",Mama Kayoza alipamba moto, tena wa gesi, Kayoza akanyanyuka alipokaa na kuelekea chumbani kwao,
"endelea tu na kiburi chako, ila kina mwisho wake, na nina uhakika Kayoza utakuja kuniua na ugonjwa wa moyo", Mama Kayoza alimwambia mwanae wakati anaondoka, kisha akamgeukia Omari,
"Omari mimi sikujui ila nakulea kama mwanangu, hata siku moja sikuwai kufikiria kama utafanya kitendo kama nilichokiona leo, tena hadharani, alafu unakuja hapa unaanza kujisifu kwa ujinga uliokuwa unaufanya!?, wewe unafikiri heshima ninayokupa itakuwa katika kiwango gani?, ee!, nijibu Omari" ,Mama Kayoza alikuwa kama mbogo aliyejeruhiwa na risasi,

"mama naomba sana msamaha, ila haya ni mapito ya ujana mama yangu",Omari aliongea kwa hekima,

"mbadilike, nyie ni wasomi bwana, nawashangaa mnavyofanya ujinga",Mama Kayoza alimwaga sera zake,

"nakuahidi mama, haitokaa itokee tena, naomba uniamini mama yangu",Omari aliongea katika sura ya majuto na upole sana,

"shauri yenu bwana, kamuite mwenzio, muende mkaninunulie maziwa mie",Mama Kayoza aliongea huku anaelekea jikoni.

Omary akatoka sebuleni na kuelekea chumbani ambapo ndipo Kayoza alikuwepo,

"Twende tukanunue maziwa, mama ametutuma" Omary alimwambia Kayoza,

"Bado anawaka au amepoa kidogo?" Kayoza alimuuliza mwenzake,

"Amepoa, ila dah..inawezekana ni kweli tumefanya kitendo cha kipuuzi" omary aliongea kwa majuto kuonesha kuwa amekosa,

"Uwa inatokeaga, ila kumbuka kuwa hata katika kipindi cha huzuni uwa kuna muda mchache wa furaha" Kayoza aliongea huku akivaa fulana yake,

"Kweli ila sio kwa kiwango kile tulichofikia, tulipitiliza" Omary aliongea huku akitoka nje kumfuata mwenzake.

"Kawaida tu bwana, haina haja ya kujuta wala kusikitika" Kayoza aliongea huku nae akitoka,

******************

BAADA YA MIEZI MIWILI

wakina Kayoza na Mkuu wa polisi wakiwa katika eneo la hospitali, Mkuu wa polisi alitaka kuwatega tena, safari hii alitaka kujua kama awa vijana wameshawahi kuishi mkoani Dodoma.

"Nyie mmezaliwa mkoa huu huu?" Mkuu wa polisi aliwauliza,

"Mimi nimezaliwa bukoba" Kayoza alijibu kwa ufasaha huku akitabasama,

"Na remmy wewe ulizaliwa wapi rafiki yangu?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akimfunga Omary kifungo cha juu cha shati,

"Mimi kwetu Tanga na ndipo nilipozaliwa?" Omary alijibu huku nae akitabasamu,

"Elimu zenu zopoje, yaani mmesoma mpaka kidato cha ngapi?, maana nyie ni ndugu zangu sasa, nataka nijue elimu yenu ili niwaangalizie hajira" Mkuu wa polisi aliuliza swali kwa kutumia akili nyingi ili aweze kuwataka hisia wakina Kayoza na atimize upelelezi wake,

"Sisi tuna elimu ya chuo, chuo kikuu" Kayoza alijibu huku akidhani ni sifa kubwa kusema ana elimu ya chuo, hajui kuwa kama anapelelezwa,

"Chuo gani?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akitabasamu,

"Chuo kikuu cha Dodoma, UDOM" omary alitoa jibu lililoanza kumpa mwanga mkuu wa polisi,

"Mlisomea nini pale?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Public relation, yaan mahusiano ya kijamii" Kayoza alijibu kwa kujiamini,

"Mmemaliza mwaka gani" Mkuu wa polisi aliendelea kuuliza,

"Mwaka jana, mwezi wa sita" Omary alitoa jibu lililomfanya Mkuu wa polisi aridhike kuwa ni kweli uenda awa vijana ndio wahusika wa mauaji, maana hata taarifa aliyokuwa nayo ulikuwa inasema ni wahitimu wa chuo, ila hawajarudi tena kuchukua vyeti vyao kutokana na kutafutwa na polisi baada ya kugundulika kuwa waliwaua wanafunzi wenzao wawili wa kike,

"Mna vyeti vyenu ili mniletee copy kesho na barua ya kuomba kazi, maana kuna kampuni ya jamaa yangu ya uchimbaji madini hapo kahama" Mkuu wa Polisi aliuliza sasa kupata uhakika wa vyeti,

"Vyeti hatuna, hatukwenda kuvifuata" Kayoza alijibu huku akijiuliza itakuwaje kama mkuu wa polisi atauliza sababu ya wao kutokwenda kuvifuata vyeti vyao, na kipindi hicho mkuu wa polisi alishaamini tayari hisia sake kuhusu Hawa vijana kuwa ndio wauaji wenyewe,

"Kwanini hamjavichukua sasa?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Matatizo ya ada, hali ya kiuchumi nyumbani ilikuwa ngumu kweli" Omary alijibu baada ya kumuona Kayoza akibabaika,

"Hata mjomba wenu hakuwasaidia?" Mkuu wa polisi aliwatupia swali jingine, ila kabla hawajajibu walimuona Daktari akiwafuata mbio mbio huku akihema juu juu, naona kwa ajili ya kukimbia sana na hata uso wake ulikuwa na furaha sana Siku hiyo tofauti na furaha anayokuwaga nayo siku nyingine,

"vipi Dokta, mbona hivyo?",Mkuu wa polisi alimuhoji Daktari,

"Taratibu mkuu, usiwe na papara na maswali yako ya kipolisi" Daktari aliongea kwa pupa huku furaha yake ikiwa bado ipo nae,

"Na wewe nawe uwa huishiwagi vituko? Sasa unavyokuja unakimbia hivyo alafu unapigia breki kwetu, ntaacha vipi kukuuliza?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akionekana hajapendezwa na kile kitendo cha daktari,

"OK, nisamehe mkuu, ila sikukusudia kukukera, nipo hapa mbele yako kwa sababu maalum" Daktari aliongea huku ile hali ya mzaha aliyokuwa nayo mwanzo ikiwa haipo tena,

"Sasa si ndio utuambie hiyo habari, wewe bwana vipi bwana" Mkuu wa polisi aliongea kwa sauti ya ukali kidogo,

"mgonjwa wenu kafumbua macho",Daktari aliwaletea habari ile ambayo ilikua kama uokovu kwao maana hata hasira zao zilikuwa zimeyeyuka ghafla kutokana na hizo habari,

"vipi, anaongea?",Mkuu wa Polisi aliuliza swali huku akiwa amemtolea macho daktari,

"sijajua bado, maana nilipomkuta katika hali hiyo nilimuacha na Daktari wa zamu na kuamua kuwafuata nyie",yule Daktari alijibu,

"Si tunaweza kwenda kumuona?" Kayoza alimuuliza daktari baada ya muda mrefu wa ukimya,

"Twendeni" Daktari alijibu huku akiondoka na kufanya wote waanze safari ya kuitafuta wodi ambayo kalazwa Sajenti Joel Minja.

Walipoenda wodi ya wagonjwa mahututi ambayo alilazwa Sajenti Minja hapo hawali, walikuta kitanda alicholala Sajenti Minja kitupu, ikambidi Daktari aliefuatana na wakina Kayoza amtafute Daktari wa zamu ili kujua mgonjwa amehamishiwa wapi. Alichukua simu yake na kumpigia mwenzake ili amuulize ni Wapi Sajenti Minja amehamishiwa,

"twendeni grade C",Daktari aliwaambia baada ya kukata simu, walipofika huko grade C, walimkuta Daktari wa zamu anamalizia kumpima Sajenti Minja, wakasubiri kwa muda kidogo, kisha wakaruhusiwa kuingia, walipofika katika kitanda alicholala Sajenti Minja, wote watatu wakajenga tabasamu katika nyuso zao, lakini Sajenti Minja alikuwa tofauti kidogo, hakuonesha kuwakumbuka kabisa,

"bado kumbukumbu hazijamrudia vizuri",Daktari wa zamu alimuambia Mkuu wa Polisi,

"itachukua muda gani kurejea katika hali yake?",Mkuu wa Polisi aliuliza,

"itategemea na nyinyi wenyewe, maana anapomuona mtu mara kwa mara ndio anapata kumbukumbu",Daktari alimjibu Mkuu wa Polisi, kisha wote wakawa wanamuangalia Sajenti Minja ambae alikuwa amelala uku macho yake yakiwa wazi yakipepesa pepesa,

"Amekonda aisee" Mkuu wa Polisi aliongea huku akiwa bado anamuangalia Sajenti Minja,

"Kukonda lazima, maana alikuwa anakula kwa mipira na dripu pekee" Daktari wa zamu alijibu huku akiuweka vizuri mkono wa Sajenti Minja,

"Sasa mpaka atengemae kabisa itachukua muda gani?" Mkuu wa polisi alimuuliza Daktari wa zamu,

"Hatuwezi kujua, ila kama atakuwa anakula vizuri na kunywa maji ya kutosha, anaweza kurudi kama hawali" Daktari alijibu,

"Ila hata hii hatua aliyofikia, ni hatua ya kumshukuru sana Mungu" Kayoza aliongea huku machozi ya furaha yakimtoka, alishindwa kuzuia hisia zake, aliamini mpigania ubinadamu wake amepona kwa hiyo ana uhakika wa kupona kwa maana Sajenti Minja ndiye mtu pekee aliyekuwa anaangaika nae kwa vitendo na maneno.

Wakati wakiwa bado wanaongea pembeni ya kitanda ambacho amelala Sajenti Minja, ndipo Sajenti Minja akamtolea macho mkuu wake wa Polisi huku akiwa kama anajitahidi kuvuta kumbukumbu juu ya mtu huyo,

"vipi Minja mbona unaniangalia sana, unanikumbuka?",Mkuu wa polisi akamuuliza swali Sajenti Joel Minja,

"ndio nimekukumbuka vizuri sana, ni mkuu wangu wa kazi",Sajenti alijibu kwa ufasaha kwa sauti iliyochoka sana kutokana na kulala kwa wiki nyingi sana.

lakini jibu la Sajenti Minja likampa njia Mkuu wa Polisi, akaona huo ndio wa wakati halisi wa kumjua na kumuumbua mtu anayejiita Remmy, na muda huo ndio alitaka ahakikishe kuwa yule kijana ambae anamtilia mashaka ni yeye haswa,

"huyu nae unamkumbuka?",Mkuu wa Polisi aliongea huku akimshika bega Kayoza, alikuwa na maana yake kuanza na Kayoza,

"huyo ni mtoto wa dada, anaitwa Kayoza",Sajenti Minja alijibu tena kuashiria kumbukumbu zimemrejea.

Omari na Kayoza waligundua mchezo anaocheza Mkuu wa Polisi, na wote walinyong'onyea kwa kujua kwamba wameumbuka, kwa maana anaefuata kutambulishwa ni Omari.

"huyu nae anaitwa nani?, taja majina yake yote matatu, ili nijue kumbukumbu yako imerudi",Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja huku akimsogeza Omary mbele ya macho ya Sajenti Minja....

**********ITAENDELEA**********

the Legend☆

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu kuna episodes 4 za hii riwaya nimejaribu kuzitafuta leo bila mafanikio, hiyo ndio sababu iliyofanya nichelewe kupost mpaka muda huu. Nazo ni episode ya 35-38. Nyingine zote zipo. So tutaendelea na episode ya 39. Samahanini kwa usumbufu utakaojitokeza

the Legend☆
Aisee..
Hiluka Prison of hope..wanakuvuruga hadi huoni!
Dah!
Wanawake muwe na huruma basi japo kidogo... "eti "Shuu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nmeipenda sana hii simulizi aisee ni nzur mno na inakupa hamu ya kuendlelea kuisoma
 
Back
Top Bottom