the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,611
- 7,063
- Thread starter
-
- #261
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA HAMSINI NA HAMSINI NA MOJA.
----------------------
ILIPOISHIA....
-----------------------
Wakiwa bado wanaangaika kumuinua Kayoza, walishtushwa na gari iliyokuwa inakuja upande waliopo, ghafla hata kabla hawajaamua chochote, lile gari tayari lilikuwa mbele yao, likaenda kusimamama pale pale walipokuwepo.
wote walishtushwa baada ya kugundua kuwa lile gari ni la polisi...
---------------------
ENDELEA....
----------------------
...kuona hivyo, Mama Kayoza akatoka mbio kuelekea ndani, Omari nae kwa taharuki, ikambidi nae aingie ndani kwa spidi ya ajabu, wakamuacha Kayoza akiwa amelala pale pale chini huku hajitambui.
Baada ya dakika kadhaa, wakasikia mtu anagonga mlangoni,
Mama Kayoza na Omari wakaangaliana, huku wote wakiwa wamelowa jasho la hofu, na wakiulizana kwa macho ni nani amfungulie huyo mgongaji?,
"jamani nifungulieni, nina haraka",ilisikika sauti ya Sajenti Minja mlangoni na kuwafanya wapigwe na butwaa.
Mama Kayoza na Omari wakawa kama hawaamini vile,
"nani, Minja?",Mama Kayoza akauliza kwa wasiwasi huku akiwa haamini,
"ndio, fungua dada",Sajenti Minja alijibu kwa haraka,
Omari akiwa na hofu, alienda hadi mlangoni kisha akafungua mlango huku akitetemeka,
"ebu njoo tumuingize huyu ndani",Sajenti Minja alimwambia Omari wakati akiwa amemshika Kayoza,
Omari akaenda haraka, kisha wakamnyanyua Kayoza na kumpeleka chumbani kwake, kisha wote wakarudi sebuleni.
"shikamoo dada",Sajenti Minja alimsalimia Mama Kayoza,
"marhaba, vipi?",Mama Kayoza aliuliza,
"yaani kilichotokea nashindwa hata kuamini",Sajenti Minja aliongea huku akiwa ameinamia chini,
"ongea basi tukuelewe",Mama Kayoza alisema kwa jazba,
"yaani Kayoza hapa ametoka kumuua mtoto wa bosi",Sajenti Minja aliongea kwa huzuni,
"weeh, acha utani!",Mama Kayoza alishtuka,
"Martha au?" Omary nae aliuliza huku akiwa ameshika kichwa,
"yaani hapa nimechukua gari mara moja, nimewatoroka wenzangu wapo hospitali ili nije niwape taharifa, ila kwa bahati nzuri nimekuta Kayoza kashafika, maana nilikuwa na wasiwasi nae sana",Sajenti Minja aliongea kwa utulivu,
"duh!, hii kweli hatari, sasa?",Mama Kayoza alihoji,
"tutaongea zaidi kesho, wacha niwahi ili nijue ratiba za uko",Sajenti Minja aliongea huku akielekea katika mlango wa kutokea,
"haya baba, kukicha nitakuja msibani",Mama Kayoza aliongea huku akimtazama Sajenti Minja akipanda gari.
Sajenti Minja akawasha gari, alafu akaondoka.
Mama Kayoza akarudi ndani, wakajadiliana na Omari,
"Kwanza ilikuaje kuaje mpaka akamuua?" Mama Kayoza alimuuliza Omary,
"Sasa mama Mimi nitajuaje wakati Mimi na wewe tumeshinda wote hapa?" Omary alijibu mama Kayoza huku akimshangaa,
"Nyie vijana, labda kuna vitu mnaambianaga" Mama Kayoza aliongea,
"Kwa kweli Mimi sijui lolote" Omary alijibu,
"Sawa, nadhani ni muda wa kulala huu ingawa tumepitiliza sana leo, ila kesho kukicha ndio tutajua cha kufanya" Mama Kayoza aliongea huku akijiondoa eneo la sebuleni na kuelekea chumbani kwake,
"Sawa" Omary nae alijibu huku akiiendea swichi ya taa ya pale sebuleni, akazima na kuelekea chumbani kwao.
Hapo tayari walikubaliana wakalale mpaka asubuhi, ndio wajue cha kufanya.
***************
Baada ya msiba kuisha, Sajenti Minja aliomuomba Mkuu wa polisi kurudi nyumbani kwake, Mkuu wa Polisi akakubali kwa roho safi, Minja akahamia kwake rasmi.
Toka ahamie kwake, Sajenti Minja alikuwa amemaliza wiki sasa, siku moja akaamua aende kwa dada yake ili wakajadili mambo yanayomtokea Kayoza, akachukua gari yake mpaka kwa dada yake, akakaribishwa mpaka ndani.
Wakasalimiana na kwa pamoja wakasali na kumshukuru Mungu kwa kumsaidia Sajenti Minja kupona,
"Kazini umeshaanza kwenda?" Mama Kayoza alimuuluza Sajenti Minja,
"Hapana, Nina wiki mbili za kupumzika nyumbani, bado nimepewa muda wa kuiangalia afya yangu" Sajenti Minja alijibu,
"Afadhali upumzike, maana hakuna aliyedhani kama utakuwa hivi leo" Mama Kayoza aliongea huku akifurahi,
"Sidhani kama nahitaji kupumzika, huu muda niliopewa nipumzike nadhani nirudi kushughulika na Kayoza" Sajenti Minja aliongea,
"Utashughulika nae vipi?" Mama Kayoza aliuliza,
"Nafikiri safari ya Bukoba ni lazima itekelezeke, ila kabla hatujaenda huko ni lazima tumpate mganga mmoja wa mwisho hapa Shinyanga, labda anaweza kutusaidia" Sajenti Minja alitoa ushauri wake,
"Waganga wa hapa wameshashindwa, nadhani jibu lipo Bukoba" Kayoza aliongea,
"Bukoba tutaenda tu, ila tujaribu kwa Mara ya mwisho hapa, tukishindwa ndio twende uko Bukoba" Sajenti Minja alimuelewesha Kayoza,
"Mi nafikiri mjomba wako yupo sahihi, ebu jaribu kumuelewa" Mama Kayoza alimuambia mwanae....
***************
Yule kijana anayeitwa Ismail au Suma ambaye alipewa kazi na Mkuu wa Polisi, alipiga hatua kubwa sana katika upelelezi wake, aligundua kuwa mtu alijitambulisha kama Remmy kwa Mkuu wa Polisi, jina lake halisi ni Omari Hussein Mkwiji, na hana undugu wowote na wakina Sajenti Minja, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja(kayoza).
Ila yule kijana hakutaka kumwambia Mkuu wa Polisi mpaka ahakikishe kwa macho mauaji yakitokea mbele yake, ili awe na ushaidi, na alikuwa anatembea na kamera kila anapoenda, na popote alipo Omari na yeye alikuwepo ila wakina Omari hawakumgundua.
"Hii kazi imekuwa rahisi sana kama meli kuelea juu ya maji ya bahari" Suma aliongea huku akimtazama Omary ambaye alikuwa bize na mchezo wa Drafti, kisha Suma akatazama pembeni na kutabasamu.
****************
Baada ya kushauriana kifamilia, walikubaliana watafute Mganga wa mwisho pale Shinyanga, nae akishindwa basi wataenda Bukoba kijijini kwa bibi yake Kayoza.
Haikuchukua muda kumpata Mganga, walimpata Babu mmoja ambae alisifika kwa uganga wa kupiga ramli, wakajipanga.
wakatafuta siku wakaenda, kama kawaida walikuwa watatu, Sajenti Minja, Omari na Kayoza, ila pia kulikuwa na mtu wa nne ambaye wao hawakumtambua, na huyo sio mwingine ila ni kijana Suma.
Suma alikuwa anawafatilia kama kawaida bila wao kujua. Wao wakiwa katika gari ambayo ilikuwa inaendeshwa Sajenti Minja, yeye Suma alikuwa katika boda boda ambayo aliikodi kwa ajili ya kuifuatilia gari waliyokuwamo wakina Sajenti Minja.
Walifika salama kwa mganga, na wakapanga foleni kwa sababu walikuta kuna wateja nje wakisubiri zamu zao zifike.
Zamu yao ilipofika, wakaruhusiwa kuingia,
"karibuni vijana",Babu mmoja Mzee aliwakaribisha kwa sauti iliyokwaruza,
"asante, asante sana Babu",wakaitikia kwa pamoja,
"Habari za mtokato wajukuu zangu?" Babu aliwauliza,
"Uko kuna wema kabisa, ila kuna tatizo dogo kidogo" Sajenti Minja alijibu,
"Sasa mtapenda niwaambie shida yenu au mtanieleza wenyewe?",Babu aliwauliza huku akiwatazama na macho yake makavu yalikuwa na ranging nyekundu,
"Ningependa utuambie tu mzee",Sajenti Minja alijibu ili kupima uwezo wa huyo mganga,
Babu akatoka nje, baada ya dakika mbili akarudi ndani na sufuria yenye maji, akawaambia wote waingize mikono ya kushoto ndani ya sufuria,
walipotoa, akaweka dawa zake, kisha akachukua kikombe cha maji, akachota maji ya kwenye sufuria kisha akanywa, alipoyameza tu, akamgeukia Kayoza,
"ni tatizo kubwa sana",Mganga aliongea huku macho yake yakiwa kwa kayoza,
"ndio maana tumekuja ili utusaidie",Sajenti Minja aliingea,
"kuwasaidia naweza, ila huo msaada utagharimu na maisha ya huyu kijana",Mganga aliongea huku akimuoneshea kidole Kayoza,
"msaada gani huo?",Sajenti Minja aliuliza,
"Msaada uliopo ni kwamba mnachinja kondoo, alafu huyu kijana anawekwa kitanzi kama anataka kunyongwa, ile damu ya kondoo ikishamuingia haswa puani, lazima mzimu atampanda, hapo hapo mnamnyonga huyu kijana, mzimu atashindwa kutoka, kwa sababu huyu bwana mdogo atakosa pumzi na mzimu hutegemea hewa zaidi katika kutoka na kuingia",Mganga alimaliza kutoa maelekezo,
"hiyo ngumu, hamna zaidi ya hiyo?",Sajenti Minja aliuliza ya kufikiria kwa muda kidogo na kipindi chote hicho wakina Kayoza walikuwa wamekaa kimya,
"ipo",Mganga alijibu kwa kifupi,
"ipi hiyo?",Sajenti Minja akauliza,
"anatakiwa apelekwe kijijinii",Mganga aliongea,
"kijijini!?",Sajenti Minja aliuliza huku akishtuka,
"ndio, huyu apelekwe kijijini, tena KIJIJINI KWA BIBI yake mzaa baba, uko ndipo lilipo suluhisho la tatizo lake",Mganga aliongea alichomaanisha huku akiwa amefunga macho........
*********ITAENDELEA**********
KIJIJINI KWA BIBI--51
..."duh!, sawa babu, malipo ni kiasi gani",Sajenti Minja akamuuliza Mganga,
"weka kiasi chochote",Mganga aliongea huku akimuelekeza Sajenti Minja sehemu ya kuwekea hela,
Sajenti Minja akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu kumi, na kuiweka juu ya ungo wa Mganga,
"haya babu tunaenda",Sajenti Minja akaaga kwa niaba ya wenzake,
"haya karibuni tena, ila mnatakiwa muwahi kumpeleka, kwa sababu mkichelewa kidogo inaweza kuwagharimu zaidi",Mganga alitoa msisitizo huku akiwa awaangalii na badala yake alikuwa akizipanga panga vizuri dawa zake,
"hamna shida Babu, tutaenda wiki ijayo",Sajenti Minja alisema kwa sauti ya unyonge,
"Wiki ijayo?, Mimi ndio ningekuwa nyie, yaani ningeenda muda huu kupanda gari" Mganga aliendelea kuongea,
"Kwani mzee ni hatari sana tukienda wiki ijayo?" Sajenti Minja aliuliza huku akisimama kabisa, kwa maana mwanzo alikuwa anaongeo huku anatembea,
"Mwenyewe fikiria kwenye kchwa chako alafu utaamua uende wiki ijayo au uende haraka iwezekanavyo" Mganga alitoa jibu lililomfanya Sajenti Minja akae kimya na kutoka zake nje.
Baada ya hapo, wakina Sajenti Minja wakaondoka zao kurudi nyumbani.
Walipofika, wakamkuta Mama Kayoza yuko sebuleni anaangalia kwaya,
"karibuni jamani, za uko?",Mama Kayoza aliwakaribisha,
"uko ni yale yale tu",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyokata tamaa,
"yale yale yapi, ina maana na huyo Mganga ameshindwa?",Mama Kayoza aliongea kwa upole,
"ndio, ila nae amesema dawa ipo",Sajenti Minja akasema kiunyonge,
"si angewapa kama ipo",Mama Kayoza aliongea kwa mshangao,
"amesema ipo KIJIJINI KWA BIBI yake Kayoza",Sajenti Minja alijibu,
"mh, kweli ni yale yale",Mama Kayoza nae akawa mnyonge ghafla.
Ikawabidi wajipange, na mwisho wakakubaliana kuwa, Sajenti Minja achukue likizo fupi kwa ajili ya safari ya Bukoba.
*************************
Yule kijana aliyepewa kazi ya upelelezi alukuwa ni mpelelezi haswa, unaweza kujiuliza kwanini asingepewa kazi usalama wa utaifa?
Maana sio kufuatilia tu nyendo za Omary, ila mpaka baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wakina Omary alikuwa anayapata kwakutumia ujanja anaoujua yeye.
na hapa alikuwa ameyasikia maneno yanayohusu safari ya Bukoba, sasa alipoyasikia haya, akaenda hadi kwa Mkuu wa Polisi,
"vipi bwana mdogo, kuna mafanikio?",Mkuu wa Polisi alimuhoji yule Kijana,
"yapo mengi sana mkuu. Kwanza pole kwa msiba kwa maana kipindi kile nilikuja ila nilishindwa kuonana na wewe",Suma alijibu kwa kujiamini, na pia akatoa maneno ya pole,
"Siwezi kusema asante kwa maana uchungu bado ninao, tena mkubwa tu, na ukizingatie mtoto mwenyewe alikuwa mmoja tu" Mkuu wa polisi alijibu,
"Tatizo lilikuwa nini, maana Mimi nilisikia juu juu tu kuwa mlivamiwa?" Suma aliuliza,
"Ndiyo hayo hayo mambo ambayo nilikuagize uyafuatilie ndio yamenirudia nyumbani kwangu" Mkuu wa polisi aliongea kwa unyonge,
"Aisee pole sana. Sasa nimekuja hapa kukueleza nilipofikia" Kijana Suma aliongea huku akiweka note book yake mezani,
"ehe, niambie kijana wangu",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibadilisha mkao katika kochi,
"kwanza kabisa, yule kijana unayemtambua kama Remmy, jina lake halisi ni Omari Mkwiji, ni mwenyeji wa Tanga, pia mwanafunzi wa UDOM pale Dodoma, na pale hana undugu na yeyote kati ya wale, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja, ambae anaitwa Kayoza. Na mahali walipokutana nae ni Dodoma pale Chuo kikuu.
Huyu Kayoza ndio mwenye matatizo sasa, yeye ndio mnyonyaji wa damu, na Siku binti yako anafariki ni yeye ndio aliyemuua na hiyo habari niliisikia kwa Dada yake Sajenti Minja wakati wakiwa wanajadili kuumaliza ugonjwa wa Kayoza unaosababisha yeye kuwa katika hali ile ya kunyonya damu watu, na hapa ninavyokuambia ni kuwa Sajenti Minja atakuja kukuomba likizo ya muda kwa sababu walienda kwa mganga, wakaambiwa waende kijijini kwa bibi yake Kayoza ambapo ni Bukoba, uko ndipo waliambiwa kuwa kuna dawa ya kumponya Kayoza, kwa hiyo Sajenti Minja ataongozana na Kayoza na Omari kwa ajili ya Safari",yule Kijana alimaliza hivyo,
"kwa hiyo Minja anajua mchezo mzima, hata ile kesi kumbe ni ujanja ujanja tu!",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti yenye mawazo yaliyoificha hasira yake,
"mimi nafikiri kazi uliyonituma nimeshaimaliza",sauti ya yule Kijana ilimshtua Mkuu wa Polisi aliyekuwa kazama ndani ya kina kirefu cha mawazo,
"sawa, asante, ngoja nikuletee mzigo wako",Mkuu wa Polisi aliongea huku akinyanyuka na kuelekea ndani.
Baada ya dakika chache alitoka na bahasha kubwa ya kaki, akamkabidhi yule kijana, yule Kijana akazitoa pesa ndani ya bahasha, akazihesabu, kisha akaagana na Mkuu wa Polisi.
"Kijana uliniambia huna kazi?" Mkuu wa polisi alimuuliza Suma ambaye alikuwa ameshaanza kuondoka,
"Ndio Mkuu" Suma alijibu huku akisimama,
"Jiandae basi, maana nakuandalia barua itayokufanya uende moshi ukachukue mafunzo ya uaskari" Mkuu wa polisi alitoa maneno yalimfanya Suma amshukuru sana,
"Asante sana, nine lini?" Suma aliuliza,
"Nitaakutaharifu kupitia simu, we kaa tayari tu kwa maana itakuwa muda wowote kutoka sasa" Mkuu wa polisi alimjibu,
"nashukuru sana mzee wangu.
Ubaki salama", Suma aliongea na kuondoka sake na kumuacha Mkuu wa polisi akiwa sebuleni,
"Sajenti Minja, Joel Minja, Minja, Minja, lazima nikuue kwa mkono wangu, wewe ndio umesababisha mwanangu amekufa kifo cha aibu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo huku akiwa ameuma meno kwa hasira,
"Kwa hiyo Omary sio muuaji, Kayoza ndiyo kamuua binti yangu?, Minja unajua kila kitu ila umeficha mpaka mwanangu ameuwawa kinyama? Hakuna atakayesalimika kati yenu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha akagida kinywaji kikali chenye rangi ya maji kilichokuwa katika chupa kubwa kama ya waini (wine) ila chenyewe ubavuni kiliandikwa MAGIC MOMENT.
********************
Siku iliyofuata, Sajenti Minja alipanga akaombe likizo, akajitayarisha vizuri, na kuwa nadhifu kama kawaida yake. Akachukua gari yake na kwenda nayo moja kwa moja mpaka ofisini.
Ofisini aliingia saa nne asubuhi, alipokelewa na pole nyingi sana kutoka kwa askari wenzake, kwa sababu toka apate ajali ndio kwa mara ya kwanza alikuwa anaingia ofisini, baada ya salamu za hapa na pale, akawa anaelekea katika ofisi ya Mkuu wa Polisi, alipofika akagonga mlango,
Mkuu wa Polisi alikuwa ndani,
"nani?",Mkuu wa Polisi akauliza,
"Minja",Sajenti Minja akajibu kwa nje,
"leo ndio mwisho wako mshenzi na msaliti mkubwa wewe",Mkuu wa Polisi aliongea huku akijaza risasi katika bastola yake ndogo, alipomaliza, akamwambia Sajenti Minja aingie.......
********ITAENDELEA********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA HAMSINI NA HAMSINI NA MOJA.
----------------------
ILIPOISHIA....
-----------------------
Wakiwa bado wanaangaika kumuinua Kayoza, walishtushwa na gari iliyokuwa inakuja upande waliopo, ghafla hata kabla hawajaamua chochote, lile gari tayari lilikuwa mbele yao, likaenda kusimamama pale pale walipokuwepo.
wote walishtushwa baada ya kugundua kuwa lile gari ni la polisi...
---------------------
ENDELEA....
----------------------
...kuona hivyo, Mama Kayoza akatoka mbio kuelekea ndani, Omari nae kwa taharuki, ikambidi nae aingie ndani kwa spidi ya ajabu, wakamuacha Kayoza akiwa amelala pale pale chini huku hajitambui.
Baada ya dakika kadhaa, wakasikia mtu anagonga mlangoni,
Mama Kayoza na Omari wakaangaliana, huku wote wakiwa wamelowa jasho la hofu, na wakiulizana kwa macho ni nani amfungulie huyo mgongaji?,
"jamani nifungulieni, nina haraka",ilisikika sauti ya Sajenti Minja mlangoni na kuwafanya wapigwe na butwaa.
Mama Kayoza na Omari wakawa kama hawaamini vile,
"nani, Minja?",Mama Kayoza akauliza kwa wasiwasi huku akiwa haamini,
"ndio, fungua dada",Sajenti Minja alijibu kwa haraka,
Omari akiwa na hofu, alienda hadi mlangoni kisha akafungua mlango huku akitetemeka,
"ebu njoo tumuingize huyu ndani",Sajenti Minja alimwambia Omari wakati akiwa amemshika Kayoza,
Omari akaenda haraka, kisha wakamnyanyua Kayoza na kumpeleka chumbani kwake, kisha wote wakarudi sebuleni.
"shikamoo dada",Sajenti Minja alimsalimia Mama Kayoza,
"marhaba, vipi?",Mama Kayoza aliuliza,
"yaani kilichotokea nashindwa hata kuamini",Sajenti Minja aliongea huku akiwa ameinamia chini,
"ongea basi tukuelewe",Mama Kayoza alisema kwa jazba,
"yaani Kayoza hapa ametoka kumuua mtoto wa bosi",Sajenti Minja aliongea kwa huzuni,
"weeh, acha utani!",Mama Kayoza alishtuka,
"Martha au?" Omary nae aliuliza huku akiwa ameshika kichwa,
"yaani hapa nimechukua gari mara moja, nimewatoroka wenzangu wapo hospitali ili nije niwape taharifa, ila kwa bahati nzuri nimekuta Kayoza kashafika, maana nilikuwa na wasiwasi nae sana",Sajenti Minja aliongea kwa utulivu,
"duh!, hii kweli hatari, sasa?",Mama Kayoza alihoji,
"tutaongea zaidi kesho, wacha niwahi ili nijue ratiba za uko",Sajenti Minja aliongea huku akielekea katika mlango wa kutokea,
"haya baba, kukicha nitakuja msibani",Mama Kayoza aliongea huku akimtazama Sajenti Minja akipanda gari.
Sajenti Minja akawasha gari, alafu akaondoka.
Mama Kayoza akarudi ndani, wakajadiliana na Omari,
"Kwanza ilikuaje kuaje mpaka akamuua?" Mama Kayoza alimuuliza Omary,
"Sasa mama Mimi nitajuaje wakati Mimi na wewe tumeshinda wote hapa?" Omary alijibu mama Kayoza huku akimshangaa,
"Nyie vijana, labda kuna vitu mnaambianaga" Mama Kayoza aliongea,
"Kwa kweli Mimi sijui lolote" Omary alijibu,
"Sawa, nadhani ni muda wa kulala huu ingawa tumepitiliza sana leo, ila kesho kukicha ndio tutajua cha kufanya" Mama Kayoza aliongea huku akijiondoa eneo la sebuleni na kuelekea chumbani kwake,
"Sawa" Omary nae alijibu huku akiiendea swichi ya taa ya pale sebuleni, akazima na kuelekea chumbani kwao.
Hapo tayari walikubaliana wakalale mpaka asubuhi, ndio wajue cha kufanya.
***************
Baada ya msiba kuisha, Sajenti Minja aliomuomba Mkuu wa polisi kurudi nyumbani kwake, Mkuu wa Polisi akakubali kwa roho safi, Minja akahamia kwake rasmi.
Toka ahamie kwake, Sajenti Minja alikuwa amemaliza wiki sasa, siku moja akaamua aende kwa dada yake ili wakajadili mambo yanayomtokea Kayoza, akachukua gari yake mpaka kwa dada yake, akakaribishwa mpaka ndani.
Wakasalimiana na kwa pamoja wakasali na kumshukuru Mungu kwa kumsaidia Sajenti Minja kupona,
"Kazini umeshaanza kwenda?" Mama Kayoza alimuuluza Sajenti Minja,
"Hapana, Nina wiki mbili za kupumzika nyumbani, bado nimepewa muda wa kuiangalia afya yangu" Sajenti Minja alijibu,
"Afadhali upumzike, maana hakuna aliyedhani kama utakuwa hivi leo" Mama Kayoza aliongea huku akifurahi,
"Sidhani kama nahitaji kupumzika, huu muda niliopewa nipumzike nadhani nirudi kushughulika na Kayoza" Sajenti Minja aliongea,
"Utashughulika nae vipi?" Mama Kayoza aliuliza,
"Nafikiri safari ya Bukoba ni lazima itekelezeke, ila kabla hatujaenda huko ni lazima tumpate mganga mmoja wa mwisho hapa Shinyanga, labda anaweza kutusaidia" Sajenti Minja alitoa ushauri wake,
"Waganga wa hapa wameshashindwa, nadhani jibu lipo Bukoba" Kayoza aliongea,
"Bukoba tutaenda tu, ila tujaribu kwa Mara ya mwisho hapa, tukishindwa ndio twende uko Bukoba" Sajenti Minja alimuelewesha Kayoza,
"Mi nafikiri mjomba wako yupo sahihi, ebu jaribu kumuelewa" Mama Kayoza alimuambia mwanae....
***************
Yule kijana anayeitwa Ismail au Suma ambaye alipewa kazi na Mkuu wa Polisi, alipiga hatua kubwa sana katika upelelezi wake, aligundua kuwa mtu alijitambulisha kama Remmy kwa Mkuu wa Polisi, jina lake halisi ni Omari Hussein Mkwiji, na hana undugu wowote na wakina Sajenti Minja, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja(kayoza).
Ila yule kijana hakutaka kumwambia Mkuu wa Polisi mpaka ahakikishe kwa macho mauaji yakitokea mbele yake, ili awe na ushaidi, na alikuwa anatembea na kamera kila anapoenda, na popote alipo Omari na yeye alikuwepo ila wakina Omari hawakumgundua.
"Hii kazi imekuwa rahisi sana kama meli kuelea juu ya maji ya bahari" Suma aliongea huku akimtazama Omary ambaye alikuwa bize na mchezo wa Drafti, kisha Suma akatazama pembeni na kutabasamu.
****************
Baada ya kushauriana kifamilia, walikubaliana watafute Mganga wa mwisho pale Shinyanga, nae akishindwa basi wataenda Bukoba kijijini kwa bibi yake Kayoza.
Haikuchukua muda kumpata Mganga, walimpata Babu mmoja ambae alisifika kwa uganga wa kupiga ramli, wakajipanga.
wakatafuta siku wakaenda, kama kawaida walikuwa watatu, Sajenti Minja, Omari na Kayoza, ila pia kulikuwa na mtu wa nne ambaye wao hawakumtambua, na huyo sio mwingine ila ni kijana Suma.
Suma alikuwa anawafatilia kama kawaida bila wao kujua. Wao wakiwa katika gari ambayo ilikuwa inaendeshwa Sajenti Minja, yeye Suma alikuwa katika boda boda ambayo aliikodi kwa ajili ya kuifuatilia gari waliyokuwamo wakina Sajenti Minja.
Walifika salama kwa mganga, na wakapanga foleni kwa sababu walikuta kuna wateja nje wakisubiri zamu zao zifike.
Zamu yao ilipofika, wakaruhusiwa kuingia,
"karibuni vijana",Babu mmoja Mzee aliwakaribisha kwa sauti iliyokwaruza,
"asante, asante sana Babu",wakaitikia kwa pamoja,
"Habari za mtokato wajukuu zangu?" Babu aliwauliza,
"Uko kuna wema kabisa, ila kuna tatizo dogo kidogo" Sajenti Minja alijibu,
"Sasa mtapenda niwaambie shida yenu au mtanieleza wenyewe?",Babu aliwauliza huku akiwatazama na macho yake makavu yalikuwa na ranging nyekundu,
"Ningependa utuambie tu mzee",Sajenti Minja alijibu ili kupima uwezo wa huyo mganga,
Babu akatoka nje, baada ya dakika mbili akarudi ndani na sufuria yenye maji, akawaambia wote waingize mikono ya kushoto ndani ya sufuria,
walipotoa, akaweka dawa zake, kisha akachukua kikombe cha maji, akachota maji ya kwenye sufuria kisha akanywa, alipoyameza tu, akamgeukia Kayoza,
"ni tatizo kubwa sana",Mganga aliongea huku macho yake yakiwa kwa kayoza,
"ndio maana tumekuja ili utusaidie",Sajenti Minja aliingea,
"kuwasaidia naweza, ila huo msaada utagharimu na maisha ya huyu kijana",Mganga aliongea huku akimuoneshea kidole Kayoza,
"msaada gani huo?",Sajenti Minja aliuliza,
"Msaada uliopo ni kwamba mnachinja kondoo, alafu huyu kijana anawekwa kitanzi kama anataka kunyongwa, ile damu ya kondoo ikishamuingia haswa puani, lazima mzimu atampanda, hapo hapo mnamnyonga huyu kijana, mzimu atashindwa kutoka, kwa sababu huyu bwana mdogo atakosa pumzi na mzimu hutegemea hewa zaidi katika kutoka na kuingia",Mganga alimaliza kutoa maelekezo,
"hiyo ngumu, hamna zaidi ya hiyo?",Sajenti Minja aliuliza ya kufikiria kwa muda kidogo na kipindi chote hicho wakina Kayoza walikuwa wamekaa kimya,
"ipo",Mganga alijibu kwa kifupi,
"ipi hiyo?",Sajenti Minja akauliza,
"anatakiwa apelekwe kijijinii",Mganga aliongea,
"kijijini!?",Sajenti Minja aliuliza huku akishtuka,
"ndio, huyu apelekwe kijijini, tena KIJIJINI KWA BIBI yake mzaa baba, uko ndipo lilipo suluhisho la tatizo lake",Mganga aliongea alichomaanisha huku akiwa amefunga macho........
*********ITAENDELEA**********
KIJIJINI KWA BIBI--51
..."duh!, sawa babu, malipo ni kiasi gani",Sajenti Minja akamuuliza Mganga,
"weka kiasi chochote",Mganga aliongea huku akimuelekeza Sajenti Minja sehemu ya kuwekea hela,
Sajenti Minja akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu kumi, na kuiweka juu ya ungo wa Mganga,
"haya babu tunaenda",Sajenti Minja akaaga kwa niaba ya wenzake,
"haya karibuni tena, ila mnatakiwa muwahi kumpeleka, kwa sababu mkichelewa kidogo inaweza kuwagharimu zaidi",Mganga alitoa msisitizo huku akiwa awaangalii na badala yake alikuwa akizipanga panga vizuri dawa zake,
"hamna shida Babu, tutaenda wiki ijayo",Sajenti Minja alisema kwa sauti ya unyonge,
"Wiki ijayo?, Mimi ndio ningekuwa nyie, yaani ningeenda muda huu kupanda gari" Mganga aliendelea kuongea,
"Kwani mzee ni hatari sana tukienda wiki ijayo?" Sajenti Minja aliuliza huku akisimama kabisa, kwa maana mwanzo alikuwa anaongeo huku anatembea,
"Mwenyewe fikiria kwenye kchwa chako alafu utaamua uende wiki ijayo au uende haraka iwezekanavyo" Mganga alitoa jibu lililomfanya Sajenti Minja akae kimya na kutoka zake nje.
Baada ya hapo, wakina Sajenti Minja wakaondoka zao kurudi nyumbani.
Walipofika, wakamkuta Mama Kayoza yuko sebuleni anaangalia kwaya,
"karibuni jamani, za uko?",Mama Kayoza aliwakaribisha,
"uko ni yale yale tu",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyokata tamaa,
"yale yale yapi, ina maana na huyo Mganga ameshindwa?",Mama Kayoza aliongea kwa upole,
"ndio, ila nae amesema dawa ipo",Sajenti Minja akasema kiunyonge,
"si angewapa kama ipo",Mama Kayoza aliongea kwa mshangao,
"amesema ipo KIJIJINI KWA BIBI yake Kayoza",Sajenti Minja alijibu,
"mh, kweli ni yale yale",Mama Kayoza nae akawa mnyonge ghafla.
Ikawabidi wajipange, na mwisho wakakubaliana kuwa, Sajenti Minja achukue likizo fupi kwa ajili ya safari ya Bukoba.
*************************
Yule kijana aliyepewa kazi ya upelelezi alukuwa ni mpelelezi haswa, unaweza kujiuliza kwanini asingepewa kazi usalama wa utaifa?
Maana sio kufuatilia tu nyendo za Omary, ila mpaka baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wakina Omary alikuwa anayapata kwakutumia ujanja anaoujua yeye.
na hapa alikuwa ameyasikia maneno yanayohusu safari ya Bukoba, sasa alipoyasikia haya, akaenda hadi kwa Mkuu wa Polisi,
"vipi bwana mdogo, kuna mafanikio?",Mkuu wa Polisi alimuhoji yule Kijana,
"yapo mengi sana mkuu. Kwanza pole kwa msiba kwa maana kipindi kile nilikuja ila nilishindwa kuonana na wewe",Suma alijibu kwa kujiamini, na pia akatoa maneno ya pole,
"Siwezi kusema asante kwa maana uchungu bado ninao, tena mkubwa tu, na ukizingatie mtoto mwenyewe alikuwa mmoja tu" Mkuu wa polisi alijibu,
"Tatizo lilikuwa nini, maana Mimi nilisikia juu juu tu kuwa mlivamiwa?" Suma aliuliza,
"Ndiyo hayo hayo mambo ambayo nilikuagize uyafuatilie ndio yamenirudia nyumbani kwangu" Mkuu wa polisi aliongea kwa unyonge,
"Aisee pole sana. Sasa nimekuja hapa kukueleza nilipofikia" Kijana Suma aliongea huku akiweka note book yake mezani,
"ehe, niambie kijana wangu",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibadilisha mkao katika kochi,
"kwanza kabisa, yule kijana unayemtambua kama Remmy, jina lake halisi ni Omari Mkwiji, ni mwenyeji wa Tanga, pia mwanafunzi wa UDOM pale Dodoma, na pale hana undugu na yeyote kati ya wale, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja, ambae anaitwa Kayoza. Na mahali walipokutana nae ni Dodoma pale Chuo kikuu.
Huyu Kayoza ndio mwenye matatizo sasa, yeye ndio mnyonyaji wa damu, na Siku binti yako anafariki ni yeye ndio aliyemuua na hiyo habari niliisikia kwa Dada yake Sajenti Minja wakati wakiwa wanajadili kuumaliza ugonjwa wa Kayoza unaosababisha yeye kuwa katika hali ile ya kunyonya damu watu, na hapa ninavyokuambia ni kuwa Sajenti Minja atakuja kukuomba likizo ya muda kwa sababu walienda kwa mganga, wakaambiwa waende kijijini kwa bibi yake Kayoza ambapo ni Bukoba, uko ndipo waliambiwa kuwa kuna dawa ya kumponya Kayoza, kwa hiyo Sajenti Minja ataongozana na Kayoza na Omari kwa ajili ya Safari",yule Kijana alimaliza hivyo,
"kwa hiyo Minja anajua mchezo mzima, hata ile kesi kumbe ni ujanja ujanja tu!",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti yenye mawazo yaliyoificha hasira yake,
"mimi nafikiri kazi uliyonituma nimeshaimaliza",sauti ya yule Kijana ilimshtua Mkuu wa Polisi aliyekuwa kazama ndani ya kina kirefu cha mawazo,
"sawa, asante, ngoja nikuletee mzigo wako",Mkuu wa Polisi aliongea huku akinyanyuka na kuelekea ndani.
Baada ya dakika chache alitoka na bahasha kubwa ya kaki, akamkabidhi yule kijana, yule Kijana akazitoa pesa ndani ya bahasha, akazihesabu, kisha akaagana na Mkuu wa Polisi.
"Kijana uliniambia huna kazi?" Mkuu wa polisi alimuuliza Suma ambaye alikuwa ameshaanza kuondoka,
"Ndio Mkuu" Suma alijibu huku akisimama,
"Jiandae basi, maana nakuandalia barua itayokufanya uende moshi ukachukue mafunzo ya uaskari" Mkuu wa polisi alitoa maneno yalimfanya Suma amshukuru sana,
"Asante sana, nine lini?" Suma aliuliza,
"Nitaakutaharifu kupitia simu, we kaa tayari tu kwa maana itakuwa muda wowote kutoka sasa" Mkuu wa polisi alimjibu,
"nashukuru sana mzee wangu.
Ubaki salama", Suma aliongea na kuondoka sake na kumuacha Mkuu wa polisi akiwa sebuleni,
"Sajenti Minja, Joel Minja, Minja, Minja, lazima nikuue kwa mkono wangu, wewe ndio umesababisha mwanangu amekufa kifo cha aibu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo huku akiwa ameuma meno kwa hasira,
"Kwa hiyo Omary sio muuaji, Kayoza ndiyo kamuua binti yangu?, Minja unajua kila kitu ila umeficha mpaka mwanangu ameuwawa kinyama? Hakuna atakayesalimika kati yenu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha akagida kinywaji kikali chenye rangi ya maji kilichokuwa katika chupa kubwa kama ya waini (wine) ila chenyewe ubavuni kiliandikwa MAGIC MOMENT.
********************
Siku iliyofuata, Sajenti Minja alipanga akaombe likizo, akajitayarisha vizuri, na kuwa nadhifu kama kawaida yake. Akachukua gari yake na kwenda nayo moja kwa moja mpaka ofisini.
Ofisini aliingia saa nne asubuhi, alipokelewa na pole nyingi sana kutoka kwa askari wenzake, kwa sababu toka apate ajali ndio kwa mara ya kwanza alikuwa anaingia ofisini, baada ya salamu za hapa na pale, akawa anaelekea katika ofisi ya Mkuu wa Polisi, alipofika akagonga mlango,
Mkuu wa Polisi alikuwa ndani,
"nani?",Mkuu wa Polisi akauliza,
"Minja",Sajenti Minja akajibu kwa nje,
"leo ndio mwisho wako mshenzi na msaliti mkubwa wewe",Mkuu wa Polisi aliongea huku akijaza risasi katika bastola yake ndogo, alipomaliza, akamwambia Sajenti Minja aingie.......
********ITAENDELEA********
the Legend☆