Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Riwaya: Kijijini kwa Bibi

RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA HAMSINI NA HAMSINI NA MOJA.

----------------------
ILIPOISHIA....
-----------------------

Wakiwa bado wanaangaika kumuinua Kayoza, walishtushwa na gari iliyokuwa inakuja upande waliopo, ghafla hata kabla hawajaamua chochote, lile gari tayari lilikuwa mbele yao, likaenda kusimamama pale pale walipokuwepo.

wote walishtushwa baada ya kugundua kuwa lile gari ni la polisi...

---------------------
ENDELEA....
----------------------

...kuona hivyo, Mama Kayoza akatoka mbio kuelekea ndani, Omari nae kwa taharuki, ikambidi nae aingie ndani kwa spidi ya ajabu, wakamuacha Kayoza akiwa amelala pale pale chini huku hajitambui.

Baada ya dakika kadhaa, wakasikia mtu anagonga mlangoni,

Mama Kayoza na Omari wakaangaliana, huku wote wakiwa wamelowa jasho la hofu, na wakiulizana kwa macho ni nani amfungulie huyo mgongaji?,

"jamani nifungulieni, nina haraka",ilisikika sauti ya Sajenti Minja mlangoni na kuwafanya wapigwe na butwaa.

Mama Kayoza na Omari wakawa kama hawaamini vile,

"nani, Minja?",Mama Kayoza akauliza kwa wasiwasi huku akiwa haamini,

"ndio, fungua dada",Sajenti Minja alijibu kwa haraka,

Omari akiwa na hofu, alienda hadi mlangoni kisha akafungua mlango huku akitetemeka,

"ebu njoo tumuingize huyu ndani",Sajenti Minja alimwambia Omari wakati akiwa amemshika Kayoza,

Omari akaenda haraka, kisha wakamnyanyua Kayoza na kumpeleka chumbani kwake, kisha wote wakarudi sebuleni.

"shikamoo dada",Sajenti Minja alimsalimia Mama Kayoza,

"marhaba, vipi?",Mama Kayoza aliuliza,

"yaani kilichotokea nashindwa hata kuamini",Sajenti Minja aliongea huku akiwa ameinamia chini,

"ongea basi tukuelewe",Mama Kayoza alisema kwa jazba,

"yaani Kayoza hapa ametoka kumuua mtoto wa bosi",Sajenti Minja aliongea kwa huzuni,

"weeh, acha utani!",Mama Kayoza alishtuka,

"Martha au?" Omary nae aliuliza huku akiwa ameshika kichwa,

"yaani hapa nimechukua gari mara moja, nimewatoroka wenzangu wapo hospitali ili nije niwape taharifa, ila kwa bahati nzuri nimekuta Kayoza kashafika, maana nilikuwa na wasiwasi nae sana",Sajenti Minja aliongea kwa utulivu,

"duh!, hii kweli hatari, sasa?",Mama Kayoza alihoji,

"tutaongea zaidi kesho, wacha niwahi ili nijue ratiba za uko",Sajenti Minja aliongea huku akielekea katika mlango wa kutokea,

"haya baba, kukicha nitakuja msibani",Mama Kayoza aliongea huku akimtazama Sajenti Minja akipanda gari.

Sajenti Minja akawasha gari, alafu akaondoka.

Mama Kayoza akarudi ndani, wakajadiliana na Omari,

"Kwanza ilikuaje kuaje mpaka akamuua?" Mama Kayoza alimuuliza Omary,

"Sasa mama Mimi nitajuaje wakati Mimi na wewe tumeshinda wote hapa?" Omary alijibu mama Kayoza huku akimshangaa,

"Nyie vijana, labda kuna vitu mnaambianaga" Mama Kayoza aliongea,

"Kwa kweli Mimi sijui lolote" Omary alijibu,

"Sawa, nadhani ni muda wa kulala huu ingawa tumepitiliza sana leo, ila kesho kukicha ndio tutajua cha kufanya" Mama Kayoza aliongea huku akijiondoa eneo la sebuleni na kuelekea chumbani kwake,

"Sawa" Omary nae alijibu huku akiiendea swichi ya taa ya pale sebuleni, akazima na kuelekea chumbani kwao.

Hapo tayari walikubaliana wakalale mpaka asubuhi, ndio wajue cha kufanya.

***************

Baada ya msiba kuisha, Sajenti Minja aliomuomba Mkuu wa polisi kurudi nyumbani kwake, Mkuu wa Polisi akakubali kwa roho safi, Minja akahamia kwake rasmi.

Toka ahamie kwake, Sajenti Minja alikuwa amemaliza wiki sasa, siku moja akaamua aende kwa dada yake ili wakajadili mambo yanayomtokea Kayoza, akachukua gari yake mpaka kwa dada yake, akakaribishwa mpaka ndani.

Wakasalimiana na kwa pamoja wakasali na kumshukuru Mungu kwa kumsaidia Sajenti Minja kupona,

"Kazini umeshaanza kwenda?" Mama Kayoza alimuuluza Sajenti Minja,

"Hapana, Nina wiki mbili za kupumzika nyumbani, bado nimepewa muda wa kuiangalia afya yangu" Sajenti Minja alijibu,

"Afadhali upumzike, maana hakuna aliyedhani kama utakuwa hivi leo" Mama Kayoza aliongea huku akifurahi,

"Sidhani kama nahitaji kupumzika, huu muda niliopewa nipumzike nadhani nirudi kushughulika na Kayoza" Sajenti Minja aliongea,

"Utashughulika nae vipi?" Mama Kayoza aliuliza,

"Nafikiri safari ya Bukoba ni lazima itekelezeke, ila kabla hatujaenda huko ni lazima tumpate mganga mmoja wa mwisho hapa Shinyanga, labda anaweza kutusaidia" Sajenti Minja alitoa ushauri wake,

"Waganga wa hapa wameshashindwa, nadhani jibu lipo Bukoba" Kayoza aliongea,

"Bukoba tutaenda tu, ila tujaribu kwa Mara ya mwisho hapa, tukishindwa ndio twende uko Bukoba" Sajenti Minja alimuelewesha Kayoza,

"Mi nafikiri mjomba wako yupo sahihi, ebu jaribu kumuelewa" Mama Kayoza alimuambia mwanae....

***************

Yule kijana anayeitwa Ismail au Suma ambaye alipewa kazi na Mkuu wa Polisi, alipiga hatua kubwa sana katika upelelezi wake, aligundua kuwa mtu alijitambulisha kama Remmy kwa Mkuu wa Polisi, jina lake halisi ni Omari Hussein Mkwiji, na hana undugu wowote na wakina Sajenti Minja, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja(kayoza).

Ila yule kijana hakutaka kumwambia Mkuu wa Polisi mpaka ahakikishe kwa macho mauaji yakitokea mbele yake, ili awe na ushaidi, na alikuwa anatembea na kamera kila anapoenda, na popote alipo Omari na yeye alikuwepo ila wakina Omari hawakumgundua.

"Hii kazi imekuwa rahisi sana kama meli kuelea juu ya maji ya bahari" Suma aliongea huku akimtazama Omary ambaye alikuwa bize na mchezo wa Drafti, kisha Suma akatazama pembeni na kutabasamu.

****************

Baada ya kushauriana kifamilia, walikubaliana watafute Mganga wa mwisho pale Shinyanga, nae akishindwa basi wataenda Bukoba kijijini kwa bibi yake Kayoza.

Haikuchukua muda kumpata Mganga, walimpata Babu mmoja ambae alisifika kwa uganga wa kupiga ramli, wakajipanga.

wakatafuta siku wakaenda, kama kawaida walikuwa watatu, Sajenti Minja, Omari na Kayoza, ila pia kulikuwa na mtu wa nne ambaye wao hawakumtambua, na huyo sio mwingine ila ni kijana Suma.

Suma alikuwa anawafatilia kama kawaida bila wao kujua. Wao wakiwa katika gari ambayo ilikuwa inaendeshwa Sajenti Minja, yeye Suma alikuwa katika boda boda ambayo aliikodi kwa ajili ya kuifuatilia gari waliyokuwamo wakina Sajenti Minja.

Walifika salama kwa mganga, na wakapanga foleni kwa sababu walikuta kuna wateja nje wakisubiri zamu zao zifike.

Zamu yao ilipofika, wakaruhusiwa kuingia,

"karibuni vijana",Babu mmoja Mzee aliwakaribisha kwa sauti iliyokwaruza,

"asante, asante sana Babu",wakaitikia kwa pamoja,

"Habari za mtokato wajukuu zangu?" Babu aliwauliza,

"Uko kuna wema kabisa, ila kuna tatizo dogo kidogo" Sajenti Minja alijibu,

"Sasa mtapenda niwaambie shida yenu au mtanieleza wenyewe?",Babu aliwauliza huku akiwatazama na macho yake makavu yalikuwa na ranging nyekundu,

"Ningependa utuambie tu mzee",Sajenti Minja alijibu ili kupima uwezo wa huyo mganga,

Babu akatoka nje, baada ya dakika mbili akarudi ndani na sufuria yenye maji, akawaambia wote waingize mikono ya kushoto ndani ya sufuria,

walipotoa, akaweka dawa zake, kisha akachukua kikombe cha maji, akachota maji ya kwenye sufuria kisha akanywa, alipoyameza tu, akamgeukia Kayoza,

"ni tatizo kubwa sana",Mganga aliongea huku macho yake yakiwa kwa kayoza,

"ndio maana tumekuja ili utusaidie",Sajenti Minja aliingea,

"kuwasaidia naweza, ila huo msaada utagharimu na maisha ya huyu kijana",Mganga aliongea huku akimuoneshea kidole Kayoza,

"msaada gani huo?",Sajenti Minja aliuliza,

"Msaada uliopo ni kwamba mnachinja kondoo, alafu huyu kijana anawekwa kitanzi kama anataka kunyongwa, ile damu ya kondoo ikishamuingia haswa puani, lazima mzimu atampanda, hapo hapo mnamnyonga huyu kijana, mzimu atashindwa kutoka, kwa sababu huyu bwana mdogo atakosa pumzi na mzimu hutegemea hewa zaidi katika kutoka na kuingia",Mganga alimaliza kutoa maelekezo,

"hiyo ngumu, hamna zaidi ya hiyo?",Sajenti Minja aliuliza ya kufikiria kwa muda kidogo na kipindi chote hicho wakina Kayoza walikuwa wamekaa kimya,

"ipo",Mganga alijibu kwa kifupi,

"ipi hiyo?",Sajenti Minja akauliza,

"anatakiwa apelekwe kijijinii",Mganga aliongea,

"kijijini!?",Sajenti Minja aliuliza huku akishtuka,

"ndio, huyu apelekwe kijijini, tena KIJIJINI KWA BIBI yake mzaa baba, uko ndipo lilipo suluhisho la tatizo lake",Mganga aliongea alichomaanisha huku akiwa amefunga macho........

*********ITAENDELEA**********

KIJIJINI KWA BIBI--51

..."duh!, sawa babu, malipo ni kiasi gani",Sajenti Minja akamuuliza Mganga,

"weka kiasi chochote",Mganga aliongea huku akimuelekeza Sajenti Minja sehemu ya kuwekea hela,

Sajenti Minja akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu kumi, na kuiweka juu ya ungo wa Mganga,

"haya babu tunaenda",Sajenti Minja akaaga kwa niaba ya wenzake,

"haya karibuni tena, ila mnatakiwa muwahi kumpeleka, kwa sababu mkichelewa kidogo inaweza kuwagharimu zaidi",Mganga alitoa msisitizo huku akiwa awaangalii na badala yake alikuwa akizipanga panga vizuri dawa zake,

"hamna shida Babu, tutaenda wiki ijayo",Sajenti Minja alisema kwa sauti ya unyonge,

"Wiki ijayo?, Mimi ndio ningekuwa nyie, yaani ningeenda muda huu kupanda gari" Mganga aliendelea kuongea,

"Kwani mzee ni hatari sana tukienda wiki ijayo?" Sajenti Minja aliuliza huku akisimama kabisa, kwa maana mwanzo alikuwa anaongeo huku anatembea,

"Mwenyewe fikiria kwenye kchwa chako alafu utaamua uende wiki ijayo au uende haraka iwezekanavyo" Mganga alitoa jibu lililomfanya Sajenti Minja akae kimya na kutoka zake nje.

Baada ya hapo, wakina Sajenti Minja wakaondoka zao kurudi nyumbani.

Walipofika, wakamkuta Mama Kayoza yuko sebuleni anaangalia kwaya,

"karibuni jamani, za uko?",Mama Kayoza aliwakaribisha,

"uko ni yale yale tu",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyokata tamaa,

"yale yale yapi, ina maana na huyo Mganga ameshindwa?",Mama Kayoza aliongea kwa upole,

"ndio, ila nae amesema dawa ipo",Sajenti Minja akasema kiunyonge,

"si angewapa kama ipo",Mama Kayoza aliongea kwa mshangao,

"amesema ipo KIJIJINI KWA BIBI yake Kayoza",Sajenti Minja alijibu,

"mh, kweli ni yale yale",Mama Kayoza nae akawa mnyonge ghafla.

Ikawabidi wajipange, na mwisho wakakubaliana kuwa, Sajenti Minja achukue likizo fupi kwa ajili ya safari ya Bukoba.

*************************

Yule kijana aliyepewa kazi ya upelelezi alukuwa ni mpelelezi haswa, unaweza kujiuliza kwanini asingepewa kazi usalama wa utaifa?

Maana sio kufuatilia tu nyendo za Omary, ila mpaka baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wakina Omary alikuwa anayapata kwakutumia ujanja anaoujua yeye.

na hapa alikuwa ameyasikia maneno yanayohusu safari ya Bukoba, sasa alipoyasikia haya, akaenda hadi kwa Mkuu wa Polisi,

"vipi bwana mdogo, kuna mafanikio?",Mkuu wa Polisi alimuhoji yule Kijana,

"yapo mengi sana mkuu. Kwanza pole kwa msiba kwa maana kipindi kile nilikuja ila nilishindwa kuonana na wewe",Suma alijibu kwa kujiamini, na pia akatoa maneno ya pole,

"Siwezi kusema asante kwa maana uchungu bado ninao, tena mkubwa tu, na ukizingatie mtoto mwenyewe alikuwa mmoja tu" Mkuu wa polisi alijibu,

"Tatizo lilikuwa nini, maana Mimi nilisikia juu juu tu kuwa mlivamiwa?" Suma aliuliza,

"Ndiyo hayo hayo mambo ambayo nilikuagize uyafuatilie ndio yamenirudia nyumbani kwangu" Mkuu wa polisi aliongea kwa unyonge,

"Aisee pole sana. Sasa nimekuja hapa kukueleza nilipofikia" Kijana Suma aliongea huku akiweka note book yake mezani,

"ehe, niambie kijana wangu",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibadilisha mkao katika kochi,

"kwanza kabisa, yule kijana unayemtambua kama Remmy, jina lake halisi ni Omari Mkwiji, ni mwenyeji wa Tanga, pia mwanafunzi wa UDOM pale Dodoma, na pale hana undugu na yeyote kati ya wale, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja, ambae anaitwa Kayoza. Na mahali walipokutana nae ni Dodoma pale Chuo kikuu.

Huyu Kayoza ndio mwenye matatizo sasa, yeye ndio mnyonyaji wa damu, na Siku binti yako anafariki ni yeye ndio aliyemuua na hiyo habari niliisikia kwa Dada yake Sajenti Minja wakati wakiwa wanajadili kuumaliza ugonjwa wa Kayoza unaosababisha yeye kuwa katika hali ile ya kunyonya damu watu, na hapa ninavyokuambia ni kuwa Sajenti Minja atakuja kukuomba likizo ya muda kwa sababu walienda kwa mganga, wakaambiwa waende kijijini kwa bibi yake Kayoza ambapo ni Bukoba, uko ndipo waliambiwa kuwa kuna dawa ya kumponya Kayoza, kwa hiyo Sajenti Minja ataongozana na Kayoza na Omari kwa ajili ya Safari",yule Kijana alimaliza hivyo,

"kwa hiyo Minja anajua mchezo mzima, hata ile kesi kumbe ni ujanja ujanja tu!",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti yenye mawazo yaliyoificha hasira yake,

"mimi nafikiri kazi uliyonituma nimeshaimaliza",sauti ya yule Kijana ilimshtua Mkuu wa Polisi aliyekuwa kazama ndani ya kina kirefu cha mawazo,

"sawa, asante, ngoja nikuletee mzigo wako",Mkuu wa Polisi aliongea huku akinyanyuka na kuelekea ndani.

Baada ya dakika chache alitoka na bahasha kubwa ya kaki, akamkabidhi yule kijana, yule Kijana akazitoa pesa ndani ya bahasha, akazihesabu, kisha akaagana na Mkuu wa Polisi.

"Kijana uliniambia huna kazi?" Mkuu wa polisi alimuuliza Suma ambaye alikuwa ameshaanza kuondoka,

"Ndio Mkuu" Suma alijibu huku akisimama,

"Jiandae basi, maana nakuandalia barua itayokufanya uende moshi ukachukue mafunzo ya uaskari" Mkuu wa polisi alitoa maneno yalimfanya Suma amshukuru sana,

"Asante sana, nine lini?" Suma aliuliza,

"Nitaakutaharifu kupitia simu, we kaa tayari tu kwa maana itakuwa muda wowote kutoka sasa" Mkuu wa polisi alimjibu,

"nashukuru sana mzee wangu.
Ubaki salama", Suma aliongea na kuondoka sake na kumuacha Mkuu wa polisi akiwa sebuleni,



"Sajenti Minja, Joel Minja, Minja, Minja, lazima nikuue kwa mkono wangu, wewe ndio umesababisha mwanangu amekufa kifo cha aibu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo huku akiwa ameuma meno kwa hasira,

"Kwa hiyo Omary sio muuaji, Kayoza ndiyo kamuua binti yangu?, Minja unajua kila kitu ila umeficha mpaka mwanangu ameuwawa kinyama? Hakuna atakayesalimika kati yenu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha akagida kinywaji kikali chenye rangi ya maji kilichokuwa katika chupa kubwa kama ya waini (wine) ila chenyewe ubavuni kiliandikwa MAGIC MOMENT.

********************

Siku iliyofuata, Sajenti Minja alipanga akaombe likizo, akajitayarisha vizuri, na kuwa nadhifu kama kawaida yake. Akachukua gari yake na kwenda nayo moja kwa moja mpaka ofisini.

Ofisini aliingia saa nne asubuhi, alipokelewa na pole nyingi sana kutoka kwa askari wenzake, kwa sababu toka apate ajali ndio kwa mara ya kwanza alikuwa anaingia ofisini, baada ya salamu za hapa na pale, akawa anaelekea katika ofisi ya Mkuu wa Polisi, alipofika akagonga mlango,

Mkuu wa Polisi alikuwa ndani,
"nani?",Mkuu wa Polisi akauliza,

"Minja",Sajenti Minja akajibu kwa nje,

"leo ndio mwisho wako mshenzi na msaliti mkubwa wewe",Mkuu wa Polisi aliongea huku akijaza risasi katika bastola yake ndogo, alipomaliza, akamwambia Sajenti Minja aingie.......

********ITAENDELEA********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI--52

...Sajenti Minja akaingia ndani,

"vipi tena mkuu, mbona kifaa umekiweka mezani?",Sajenti Minja aliuliza baada ya kuiona bastola iko juu ya meza ya Mkuu wa Polisi,

"nilikuwa naisafisha, karibu Minja",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibasamu kwa tabasamu batili,

"Tunatishana bwana, hivyo vyombo vya moto vinafichwagwa bwana" Sajenti Minja aliongea huku nae akitabasamu,

"Kweli kabisa.. Vipi mbona umekuja leo kabla likizo yako haijaisha? Au uliwamisi wenzako?" Mkuu wa polisi alimuuliza Sajenti Minja,

"Hata hiyo ni sababu pia, ila sababu juu iliyonileta ni kuja kuomba kuongezewa likizo" Sajenti Minja aliongea kauli ambayo mkuu wa polisi aliitegemea,

"Haina shida Minja, je ungetaka likizo ya muda gani?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Ningepata kama wiki mbili nyingune, ingekuwa safi sana" Sajenti Minja aliongea,

"Mi nitakupa likizo ya mwezi mzima, najua hali yako haijatengemaa vizuri" Mkuu wa polisi aliongea,

"Nashukuru sana, sasa ngoja nikaandae barua ili niiwasilishe baadae" Sajenti Minja aliongea,

"Hapana, hakuna haja ya barua, we nenda tu Minja" Mkuu wa polisi alimzuia Sajenti Minja kuandika barua,

"Haiwezi kuleta matatizo baadae?" Sajenti Minja alimuuliza mkuu wake,

"Hakuna Shida Minja, Mimi ndiyo nimekuruhusu, usiwe na wasiwasi" Mkuu wa polisi alimwambia Sajenti Minja.

Baada ya Sajenti Minja kuongea kilichompeleka, haikuwa ngumu kukubaliwa, alipewa likizo ya mwezi mzima,

"utakuwa hapa hapa au utarudi Dodoma?",Mkuu wa Polisi alimuuliza Sajenti Minja,

"hapa hapana, nitaenda Moshi kwa wazazi, alafu wiki mbili za mwisho nitazimalizia Dodoma",Sajenti Minja alijibu,

"haya bwana Minja, mi nakutakia likizo njema, na safari njema pia",Mkuu wa Polisi alihongea kwa sura aliyoibandika huzuni wa bandia,

"shukrani sana Mkuu, tukijaaliwa",Sajenti Minja alisema wakati ananyanyuka kutoka kwenye kiti,

Kisha akauendea mlango na kwenda zake.

Mkuu wa polisi alisitisha zoezi la kumuua Sajenti Minja ofisini kwa sababu angekamatwa na kufungwa kwa sababu ushaidi ungekuwepo wa kutosha, aliamua kwenda kumuua Sajenti Minja huko huko Bukoba, Mkuu wa Polisi na yeye akajipa likizo.

Likizo iliyokuwa maalum kwa ajili ya kisasi, likizo ambayo aliibatiza jina na kuiita LIKIZO YA MALIPO YA KIFO.

*****************

Siku ya safari ilipofika, Mama Kayoza aliwasindikiza mpaka stendi kuu ya mkoa, walipofika, wakafanikiwa kupata usafiri wa haraka haraka,

"Jamani safari njema" Mama aliwaambia,

"Lakini Dada kumbuka sisi tunaenda sehemu ambayo hatuhijui, kama una namba za wenyeji wetu ni bora uwape taharifa juu ya safari yetu" Sajenti Minja alimuambia Dada yake,

"Kayoza anapajua huyo, au na wewe umepasahau?" Mama Kayoza aliongea huku akimuangalia Kayoza,

"Mama ni muda sana, hata kumbukumbu sina vizuri" Kayoza alijibu,

"Mimi na wewe ni nani ambae ametoka muda mrefu kule? Mbona mimi bado napakumbuka?" Mama Kayoza alimuuliza mwanae,

"Tatizo sio kila sehemu naikumbuka, kuna njia sizikumbuki kabisa" Kayoza alijibu Mama yake,

"Bwana nyie wanaume, mtafika tu, maana Mimi sina mawasiliano na mtu yoyote wa uko" Mama Kayoza aliongea,

"Tutafika tu" Omary aliongea na kufanya wenzake wamuangalie,

"Unavyoongea utasema unapajua, au umeshawahi kufika?" Sajenti Minja alimuuliza Omary,

"Tuwe na imani tutafika tu" Omary alijibu na kufanya wenzake wacheke,

"Achana na huyu mwendawazimu, ebu nichoree ramani kwenye karatasi" Sajenti Minja alimwambia Dada yake,

"Nipe hiyo karatasi na kalamu" Mama Kayoza akaongea na kumfanya Sajenti Minja ajisachi na kutoa kalamu na kitabu chake kidogo cha diary na kumpatia Mama Kayoza kisha akaanza kuwachorea ramani huku pia akiwaelekeza, alipomaliza akawaachia ile karatasi yenye mchoro.

Wakaendelea kuongea na maongezi mengine mpaka muda wa kuondoka basi ulipofika ndipo mama Kayoza akaagana na wenzake hao na kuachana hapo huku wakipungiana mikono kipindi basi inaacha eneo la kituo kikuu cha mabasi ya mikoani.

Baada ya gari kupotea machoni pake, Mama Kayoza aliondoka zake eneo hill huku akiamini Wakina Sajenti Minja watakaa wiki tu kisha watarudi.

*****************

Mkuu wa Polisi nae alipanda basi hilo hilo walilopanda wakina Sajenti Minja, ila yeye alipata nafasi siti ya mbele kabisa kwa dereva, wakati wakina Sajenti Minja wao walipata siti jirani na za nyuma. Na kingine ni kwamba mkuu wa polisi ilikuwa ngumu sana kumtambua kwa maana alivaa kama mzee wa kijijini kabisa.

Kwa hiyo ndani ya basi kukawa na makundi mawili, moja la Sajenti Minja na lingine ni la mkuu wa polisi ila tofauti ni kwamba kundi moja lilikuwa la mtu mmoja na tayari alishawajua adui zake, na kundi la pili ni la Sajenti Minja ambalo walikaa bila kujua kama wanafuatiliwa na mkuu wa polisi.

Bukoba waliingia saa kumi na moja jioni, wakatafuta usafiri wa kuwapeleka Vanga, kijijini kwa bibi yake Kayoza.

Vanga waliingia saa moja kasoro robo, hawakupata shida kufika katika nyumba ya Bibi yake Kayoza, kwani ni ukoo wa kichifu, kwa hiyo ukoo wao ulikuwa maarufu sana pale kijijini.

Na hata usiku ulipokuwa mwingi walitaka kuondoka ili wakatafute lodge ila walikataliwa na kuambiwa ni lazima walale pale kwa maana kuna nafasi za kutosha na hakuna haja ya kwenda kutafuta Guest.

Kumbuka chote hicho Mkuu wa Polisi nae alikuwa akiwafuatilia kwa kila hatua na alitumia akili nyingi kuwafuatilia bila ya wao kujua.

Mkuu wa Polisi alipojiaminisha nyumba waliyofikia wakina Sajenti Minja, na yeye akaamua kutafuta Guest iliyopo jirani na nyumba hiyo, alifanikiwa kupata Guest jirani na nyumba waliyofikia wakina Sajenti Minja.

Wakina sajenti Minja walipokewa kama watu wa kawaida sana, ila baada ya kujitambulisha, vigelegele vilipigwa na shangazi zake Kayoza, usiku huo huo ndugu wa mbali walipigiwa simu kufahamishwa ujio wa Kayoza, Kayoza akaomba aonane na bibi yake, ila Baba zake wadogo wakamzuia, wakidai bibi yake ni mgonjwa sana, kama kuonana labda kesho ila kwa usiku ule isingewezekana.

Asubuhi kulipokucha, Sajenti Minja na Omari waliamshwa mapema sana, kisha wakatayarishiwa ndizi zilizokorogwa kama uji, hicho ni chakula cha heshima katika kabila lao.

Walipomaliza kula, wenyeji wakawa wanawatembeza katika mali ziliachwa na Baba yake Kayoza, na moja ya hizo mali pale kijijini ni ile Guest aliyofikia mkuu wa Polisi.

Wakaenda pale Guest, wakawa wanaoneshwa eneo la Guest yote, mara Sajenti Minja akaomba aelekezwe Choo kilipo, akaelekezwa na kisha akawa anaelekea katika mlango wa chooni sasa ambao ulitazamana na mlango wa chumba alichofikia Mkuu wa Polisi.

Mkuu wa polisi alikuwa anatoka ili aelekee kutafuta kifungua kinywa, aliupa mlango wa chooni mgongo wakati anafunga na ufunguo mlango wa chumbani kwake, na wakati huo huo Sajenti Minja nae alikuwa anatoka chooni, anaelekea pale alipo mkuu wa Polisi maana pale ndipo kulipokuwa na njia ya moja kwa moja mpaka nje...

"JESUS!",Sajenti Minja akashtuka alipomtazama mgongoni Mkuu wa polisi..

*********INAENDELEA*******

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI--53

...ila sauti yake haikumfikia Mkuu wa Polisi, Sajenti Minja akarudi ndani ya choo, kisha akafunga mlango, akawa anachungulia kupitia tundu la ufunguo, akamshuhudia Mkuu wa Polisi akielekea nje.

"Amekuja kufanya nini huku? Au amejipa likizo na yeye kutokana na kifo cha mwanae? Au anatufuatilia?" Sajenti Minja alikuwa anajiuliza mwenyewe huku akiwa bado yupo ndani ya choo.

Baada ya dakika tano, Sajenti Minja alitoka chooni na kuelekea walipo wakina Kayoza,

"vipi anko, mbona umekaa muda mrefu sana?",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,

"tumbo limenishika si mchezo, mimi naona nirudi nikapumzike, nyie endeleeni na ziara",Sajenti Minja hakutaka kusema ukweli, ingawa mshtuko wa kumuona Mkuu wa Polisi ulimfanye achoke ila hakuwa na sababu ya kuwaambia wenzake ukweli kutokana na yeye kutokuwa na jibu haswa juu ya uwepo wa Mkuu wa polisi katika eneo lile,

"sisi tumeshamaliza, tulikuwa tunakusubiri wewe tu",Kayoza alimwambia Sajenti Minja,

"haya bwana, mimi naelekea mjini, nyie nendeni tu nyumbani, njia si mnaikumbuka?",Mwenyeji wao aliwauliza,

"tunaikumbuka bwana mkubwa",Sajenti Minja alijibu huku akijilazimisha kutabasamu,

Kisha wakaagana na mwenyeji wao, na wao wakashika njia ya kurudi nyumbani.

Sajenti Minja akaona huo ndio muda mzuri wa kuwaambia alichokiona, ingawa alitaka kuwaficha ila akaona haitakuwa vyema kuwaficha kwa kuwa wao ni wamoja na wamefika mkoa ule kwa lengo moja.

"jamani nimemuoona Mkuu wa Polisi pale hotelini",Sajenti Minja aliongea kisha akawa anasubiri swali,

"Mara hii umeshaonana na mkuu wa polisi wa mkoa huu, kweli nyie maaskari mnajuana sana" Omary aliongea huku akishangaa,

"Sio wa mkoa huu, yule wa Shinyanga" Sajenti Minja alitoa Maelezo yaliyowafanya wenzake washtuke,

"itakuwa umemfananisha",Omari aliongea huku akiwa bado anamshangaa Sajenti Minja,

"nimemfananisha vipi?, wakati namfahamu fika",Sajenti Minja aliongea kwa kupaniki,

"sasa huku kafuata nini?",Omari akamuuliza,

"huwezi jua bwana, yule ni polisi, inawezekana anatufatilia sisi",Sajenti Minja aliongea kwa uhakika,

"duniani wawili wawili mjomba",Kayoza aliongea baada ya kuwa kimya muda mrefu,

"ok, mmeshinda, ila mtaniambia wenyewe",Sajenti Minja alimaliza, kisha wakaendelea na stori nyingine, huku Sajenti Minja akiwa hana amani kabisa katika moyo wake.

Walipofika nyumbani, wakapelekwa moja kwa moja hadi kwenye chumba cha Bibi yake Kayoza, wakamsalimia, kisha wakatambulishwa, Bibi Kayoza alifurahi sana, alipomuona Kayoza, waliongea sana,

"ila bibi pamoja na kukusalimia, kuna jingine lililonileta huku",Kayoza alimwambia Bibi yake,

"hata usiniambie mume wangu, najua lililokuleta",Bibi yake Kayoza alimkatisha Kayoza,

"nateseka sana bibi, naishi maisha ya kutafutwa na askari kama jambazi",Kayoza aliongea kwa majonzi,

"ilikua lazima upitie hiyo hali mume wangu",Bibi yake Kayoza alisema na kumfanya Kayoza avute kamasi kwanza,

"kivipi bibi?",Kayoza alihoji huku akifuta machozi,

"bila ubishi wa baba yako na kiburi cha mama yako, yote yasingekukuta hayo",Bibi Kayoza alisema, kisha akawapa hadithi ile ile waliyopigiwa na Mama Kayoza.

"yote hayo yamepita, kilichonileta huku ni dawa ya kuniachanisha na hili dudu",Kayoza aliongea kwa upole,

"Futa kauli yako, usiseme hili dudu, kusema hivyo ni kosa kama mwananchi kumtukana rais wake" Bibi Kayoza alimwambia mjukuu wake tena hata sura yake ilionesha hakufurahishwa na kauli ya Kayoza,

"Sasa ni jina lipi unaona linafaa kuitwa?" Kayoza aliuliza na yeye alipaniki baada ya kuna Bibi yake akikitetea kile kiumbe kinachomnyima yeye Furaha ya maisha,

"Heshimu mazingira kama unataka kupona, kinyume na hapo hakuna kitakachowezekana" Bibi Kayoza aliongea maneno ambayo yalieleweka vizuri kwa Kayoza,

"Sawa nimekuelewa bibi, sasa hapa nimekuja kufuata dawa" Kayoza alimwambia bibi yake,

"dawa ipo, ila nitakupa usiku",Bibi yake kayoza alimwambia mjukuu wake,

"kwani ni dawa gani bibi?",Kayoza aliuliza,

"utaijua usiku huo huo",Bibi yake Kayoza alijibu,

"Na kwanini iwe usiku bibi?" Kayoza aliendelea na udadisi wake,

"Usiku kwa sababu ya kuwa watu wote wa hapa walioenda kazini watakuwa wamerudi nyumbani" Bibi Kayoza alijibu,

"Kwani ni lazima wawepo?" Kayoza aliendelea kuuliza,

"Ndio ni lazima wawepo, kwa sababu haya mambo yamekaa kimila, kwa hiyo basi ni lazima wanaukoo wote washiriki" Bibi Kayoza alijibu na kisha wakaendelea na hadithi zao binafsi kwa kushirikiana na Sajenti Minja na Omary ambao muda wote walikaa kimya ili kumuachia Kayoza uwanja mpana wa kuuliza maswali yake.

**************

Mkuu wa Polisi alifanikiwa sio kupajua tu mahali walipofikia wakina Sajenti Minja, alipajua mpaka Mahalia wanapolala yaani chumba walichokuwa wanakitumia wakina Sajenti Minja.

Mkuu wa polisi akapanga kuwa usiku huo ndio itakuwa mwisho wao kuvuta hewa safi ya duniani.

********************

Usiku ulipoingia, wakakusanyika wanaukoo wote, kisha wakatangaza lengo la kuitwa pale, ambalo lilikuwa ni kumuamisha mzimu kutoka kwa Kayoza na kwenda kwa Baba yake mdogo. Watu wasiokuwa wa ukoo ule hawakuhusika kujumuika pale, kwa hiyo Sajenti Minja na Omari waliambiwa wakae vyumba vya uwani. Wakina Sajenti Minja wakaondoka na kuelekea uko uwani.

Shughuli ikaanza ya kuuhamisha mzimu, yakaletwa maji masafi, mbuzi jike mwenye mimba na majani ya mitishamba ambayo waliyajua wao wenyewe.

Kayoza akalazwa chini, na pembeni yake alikuwa baba yake mdogo, bibi akaanza vitu vyake.

Muda wote huo, mkuu wa Polisi alikuwa anafuatilia kila kitu, mpaka kile kitendo cha wakina Sajenti Minja kuenda vyumba vya uwani alikiona, akawa anavuta muda ili akakamilishe azma yake, muda wake alioupanga ulipofika, akawa anaelekea kwenye chumba walichokuwepo Sajenti Minja na Omari, alipofika akagonga, bila ya kufikiria kuuliza mgongaji nani?, Omari akaundea mlango kisha akafungua, hakuamini macho yake alipomuona mkuu wa Polisi amesimama mlangoni huku kashika bastola, Omari kabla hajafanya chochote, alipigwa risasi kama nne hivi za kifuani, na kuanguka chini kwa kishindo mithili ya embe kubwa ambayo halijakomaa lililopopolewa mtini.

Na kule nje kwenye tambiko, wakati bibi anaendelea na tambiko, ulisikika mlio wa risasi ulisababisha mstuko na kumpelekea bibi kuanguka na kufa kwa presha iliyotokana na mshtuko wa ulisababishwa na mlio wa risasi, Bibi akawa amekufa bila hata kufanikisha zoezi la kuuhamisha mzimu.

Baada ya mlio wa risasi kusikika na bibi kuanguka chini kama mzigo, watu wote katika eneo lile walikurupuka, wingine wakiundea mwili wa bibi na wengine walikimbilia eneo ambalo mlio wa risasi ulitokea, wakakuta mtu akitokomea gizani kwa mbele yao mlangoni alikuwa Omary aliyekuwa amelala chini huku damu zikiwa zimemtapakaa,

Sajenti Minja akamsogelea na kukaa chini huku machozi yakimtoka na kuchukua kchwa cha kayoza na kukiweza mapajani mwake, akawa anamuangalia Omary aliyekuwa anatabasamu huku kila akitoa funda la pumzi lilikuwa likitoka huku limeambatana na damu.

Wenyeji wa pale walikuwa wanashangaa na wasijue la kufanya.

Omary akafumbua macho na kumuangalia Sajenti Minja aliyekuwa analia, kisha Omary akaongea maneno machache tu,

"Mk....uu ...wa...pol...isi" Omary aliongea kauli ambayo watu wengine hawakuielewa isipokuwa Sajenti Minja pekee.

Omary baada ya kutamka maneno hayo, shingo yake ililegea na kuanguka, huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya Omary, roho yake ikatengana na mwili akiwa ugenini, kauli ya babu yake ikatimia.....

********ITAENDELEA**"****"***

the Legend☆
 
jaman minja wangu weee
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA HAMSINI NA HAMSINI NA MOJA.

----------------------
ILIPOISHIA....
-----------------------

Wakiwa bado wanaangaika kumuinua Kayoza, walishtushwa na gari iliyokuwa inakuja upande waliopo, ghafla hata kabla hawajaamua chochote, lile gari tayari lilikuwa mbele yao, likaenda kusimamama pale pale walipokuwepo.

wote walishtushwa baada ya kugundua kuwa lile gari ni la polisi...

---------------------
ENDELEA....
----------------------

...kuona hivyo, Mama Kayoza akatoka mbio kuelekea ndani, Omari nae kwa taharuki, ikambidi nae aingie ndani kwa spidi ya ajabu, wakamuacha Kayoza akiwa amelala pale pale chini huku hajitambui.

Baada ya dakika kadhaa, wakasikia mtu anagonga mlangoni,

Mama Kayoza na Omari wakaangaliana, huku wote wakiwa wamelowa jasho la hofu, na wakiulizana kwa macho ni nani amfungulie huyo mgongaji?,

"jamani nifungulieni, nina haraka",ilisikika sauti ya Sajenti Minja mlangoni na kuwafanya wapigwe na butwaa.

Mama Kayoza na Omari wakawa kama hawaamini vile,

"nani, Minja?",Mama Kayoza akauliza kwa wasiwasi huku akiwa haamini,

"ndio, fungua dada",Sajenti Minja alijibu kwa haraka,

Omari akiwa na hofu, alienda hadi mlangoni kisha akafungua mlango huku akitetemeka,

"ebu njoo tumuingize huyu ndani",Sajenti Minja alimwambia Omari wakati akiwa amemshika Kayoza,

Omari akaenda haraka, kisha wakamnyanyua Kayoza na kumpeleka chumbani kwake, kisha wote wakarudi sebuleni.

"shikamoo dada",Sajenti Minja alimsalimia Mama Kayoza,

"marhaba, vipi?",Mama Kayoza aliuliza,

"yaani kilichotokea nashindwa hata kuamini",Sajenti Minja aliongea huku akiwa ameinamia chini,

"ongea basi tukuelewe",Mama Kayoza alisema kwa jazba,

"yaani Kayoza hapa ametoka kumuua mtoto wa bosi",Sajenti Minja aliongea kwa huzuni,

"weeh, acha utani!",Mama Kayoza alishtuka,

"Martha au?" Omary nae aliuliza huku akiwa ameshika kichwa,

"yaani hapa nimechukua gari mara moja, nimewatoroka wenzangu wapo hospitali ili nije niwape taharifa, ila kwa bahati nzuri nimekuta Kayoza kashafika, maana nilikuwa na wasiwasi nae sana",Sajenti Minja aliongea kwa utulivu,

"duh!, hii kweli hatari, sasa?",Mama Kayoza alihoji,

"tutaongea zaidi kesho, wacha niwahi ili nijue ratiba za uko",Sajenti Minja aliongea huku akielekea katika mlango wa kutokea,

"haya baba, kukicha nitakuja msibani",Mama Kayoza aliongea huku akimtazama Sajenti Minja akipanda gari.

Sajenti Minja akawasha gari, alafu akaondoka.

Mama Kayoza akarudi ndani, wakajadiliana na Omari,

"Kwanza ilikuaje kuaje mpaka akamuua?" Mama Kayoza alimuuliza Omary,

"Sasa mama Mimi nitajuaje wakati Mimi na wewe tumeshinda wote hapa?" Omary alijibu mama Kayoza huku akimshangaa,

"Nyie vijana, labda kuna vitu mnaambianaga" Mama Kayoza aliongea,

"Kwa kweli Mimi sijui lolote" Omary alijibu,

"Sawa, nadhani ni muda wa kulala huu ingawa tumepitiliza sana leo, ila kesho kukicha ndio tutajua cha kufanya" Mama Kayoza aliongea huku akijiondoa eneo la sebuleni na kuelekea chumbani kwake,

"Sawa" Omary nae alijibu huku akiiendea swichi ya taa ya pale sebuleni, akazima na kuelekea chumbani kwao.

Hapo tayari walikubaliana wakalale mpaka asubuhi, ndio wajue cha kufanya.

***************

Baada ya msiba kuisha, Sajenti Minja aliomuomba Mkuu wa polisi kurudi nyumbani kwake, Mkuu wa Polisi akakubali kwa roho safi, Minja akahamia kwake rasmi.

Toka ahamie kwake, Sajenti Minja alikuwa amemaliza wiki sasa, siku moja akaamua aende kwa dada yake ili wakajadili mambo yanayomtokea Kayoza, akachukua gari yake mpaka kwa dada yake, akakaribishwa mpaka ndani.

Wakasalimiana na kwa pamoja wakasali na kumshukuru Mungu kwa kumsaidia Sajenti Minja kupona,

"Kazini umeshaanza kwenda?" Mama Kayoza alimuuluza Sajenti Minja,

"Hapana, Nina wiki mbili za kupumzika nyumbani, bado nimepewa muda wa kuiangalia afya yangu" Sajenti Minja alijibu,

"Afadhali upumzike, maana hakuna aliyedhani kama utakuwa hivi leo" Mama Kayoza aliongea huku akifurahi,

"Sidhani kama nahitaji kupumzika, huu muda niliopewa nipumzike nadhani nirudi kushughulika na Kayoza" Sajenti Minja aliongea,

"Utashughulika nae vipi?" Mama Kayoza aliuliza,

"Nafikiri safari ya Bukoba ni lazima itekelezeke, ila kabla hatujaenda huko ni lazima tumpate mganga mmoja wa mwisho hapa Shinyanga, labda anaweza kutusaidia" Sajenti Minja alitoa ushauri wake,

"Waganga wa hapa wameshashindwa, nadhani jibu lipo Bukoba" Kayoza aliongea,

"Bukoba tutaenda tu, ila tujaribu kwa Mara ya mwisho hapa, tukishindwa ndio twende uko Bukoba" Sajenti Minja alimuelewesha Kayoza,

"Mi nafikiri mjomba wako yupo sahihi, ebu jaribu kumuelewa" Mama Kayoza alimuambia mwanae....

***************

Yule kijana anayeitwa Ismail au Suma ambaye alipewa kazi na Mkuu wa Polisi, alipiga hatua kubwa sana katika upelelezi wake, aligundua kuwa mtu alijitambulisha kama Remmy kwa Mkuu wa Polisi, jina lake halisi ni Omari Hussein Mkwiji, na hana undugu wowote na wakina Sajenti Minja, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja(kayoza).

Ila yule kijana hakutaka kumwambia Mkuu wa Polisi mpaka ahakikishe kwa macho mauaji yakitokea mbele yake, ili awe na ushaidi, na alikuwa anatembea na kamera kila anapoenda, na popote alipo Omari na yeye alikuwepo ila wakina Omari hawakumgundua.

"Hii kazi imekuwa rahisi sana kama meli kuelea juu ya maji ya bahari" Suma aliongea huku akimtazama Omary ambaye alikuwa bize na mchezo wa Drafti, kisha Suma akatazama pembeni na kutabasamu.

****************

Baada ya kushauriana kifamilia, walikubaliana watafute Mganga wa mwisho pale Shinyanga, nae akishindwa basi wataenda Bukoba kijijini kwa bibi yake Kayoza.

Haikuchukua muda kumpata Mganga, walimpata Babu mmoja ambae alisifika kwa uganga wa kupiga ramli, wakajipanga.

wakatafuta siku wakaenda, kama kawaida walikuwa watatu, Sajenti Minja, Omari na Kayoza, ila pia kulikuwa na mtu wa nne ambaye wao hawakumtambua, na huyo sio mwingine ila ni kijana Suma.

Suma alikuwa anawafatilia kama kawaida bila wao kujua. Wao wakiwa katika gari ambayo ilikuwa inaendeshwa Sajenti Minja, yeye Suma alikuwa katika boda boda ambayo aliikodi kwa ajili ya kuifuatilia gari waliyokuwamo wakina Sajenti Minja.

Walifika salama kwa mganga, na wakapanga foleni kwa sababu walikuta kuna wateja nje wakisubiri zamu zao zifike.

Zamu yao ilipofika, wakaruhusiwa kuingia,

"karibuni vijana",Babu mmoja Mzee aliwakaribisha kwa sauti iliyokwaruza,

"asante, asante sana Babu",wakaitikia kwa pamoja,

"Habari za mtokato wajukuu zangu?" Babu aliwauliza,

"Uko kuna wema kabisa, ila kuna tatizo dogo kidogo" Sajenti Minja alijibu,

"Sasa mtapenda niwaambie shida yenu au mtanieleza wenyewe?",Babu aliwauliza huku akiwatazama na macho yake makavu yalikuwa na ranging nyekundu,

"Ningependa utuambie tu mzee",Sajenti Minja alijibu ili kupima uwezo wa huyo mganga,

Babu akatoka nje, baada ya dakika mbili akarudi ndani na sufuria yenye maji, akawaambia wote waingize mikono ya kushoto ndani ya sufuria,

walipotoa, akaweka dawa zake, kisha akachukua kikombe cha maji, akachota maji ya kwenye sufuria kisha akanywa, alipoyameza tu, akamgeukia Kayoza,

"ni tatizo kubwa sana",Mganga aliongea huku macho yake yakiwa kwa kayoza,

"ndio maana tumekuja ili utusaidie",Sajenti Minja aliingea,

"kuwasaidia naweza, ila huo msaada utagharimu na maisha ya huyu kijana",Mganga aliongea huku akimuoneshea kidole Kayoza,

"msaada gani huo?",Sajenti Minja aliuliza,

"Msaada uliopo ni kwamba mnachinja kondoo, alafu huyu kijana anawekwa kitanzi kama anataka kunyongwa, ile damu ya kondoo ikishamuingia haswa puani, lazima mzimu atampanda, hapo hapo mnamnyonga huyu kijana, mzimu atashindwa kutoka, kwa sababu huyu bwana mdogo atakosa pumzi na mzimu hutegemea hewa zaidi katika kutoka na kuingia",Mganga alimaliza kutoa maelekezo,

"hiyo ngumu, hamna zaidi ya hiyo?",Sajenti Minja aliuliza ya kufikiria kwa muda kidogo na kipindi chote hicho wakina Kayoza walikuwa wamekaa kimya,

"ipo",Mganga alijibu kwa kifupi,

"ipi hiyo?",Sajenti Minja akauliza,

"anatakiwa apelekwe kijijinii",Mganga aliongea,

"kijijini!?",Sajenti Minja aliuliza huku akishtuka,

"ndio, huyu apelekwe kijijini, tena KIJIJINI KWA BIBI yake mzaa baba, uko ndipo lilipo suluhisho la tatizo lake",Mganga aliongea alichomaanisha huku akiwa amefunga macho........

*********ITAENDELEA**********

KIJIJINI KWA BIBI--51

..."duh!, sawa babu, malipo ni kiasi gani",Sajenti Minja akamuuliza Mganga,

"weka kiasi chochote",Mganga aliongea huku akimuelekeza Sajenti Minja sehemu ya kuwekea hela,

Sajenti Minja akaingiza mkono mfukoni na kutoa shilingi elfu kumi, na kuiweka juu ya ungo wa Mganga,

"haya babu tunaenda",Sajenti Minja akaaga kwa niaba ya wenzake,

"haya karibuni tena, ila mnatakiwa muwahi kumpeleka, kwa sababu mkichelewa kidogo inaweza kuwagharimu zaidi",Mganga alitoa msisitizo huku akiwa awaangalii na badala yake alikuwa akizipanga panga vizuri dawa zake,

"hamna shida Babu, tutaenda wiki ijayo",Sajenti Minja alisema kwa sauti ya unyonge,

"Wiki ijayo?, Mimi ndio ningekuwa nyie, yaani ningeenda muda huu kupanda gari" Mganga aliendelea kuongea,

"Kwani mzee ni hatari sana tukienda wiki ijayo?" Sajenti Minja aliuliza huku akisimama kabisa, kwa maana mwanzo alikuwa anaongeo huku anatembea,

"Mwenyewe fikiria kwenye kchwa chako alafu utaamua uende wiki ijayo au uende haraka iwezekanavyo" Mganga alitoa jibu lililomfanya Sajenti Minja akae kimya na kutoka zake nje.

Baada ya hapo, wakina Sajenti Minja wakaondoka zao kurudi nyumbani.

Walipofika, wakamkuta Mama Kayoza yuko sebuleni anaangalia kwaya,

"karibuni jamani, za uko?",Mama Kayoza aliwakaribisha,

"uko ni yale yale tu",Sajenti Minja alijibu katika sauti iliyokata tamaa,

"yale yale yapi, ina maana na huyo Mganga ameshindwa?",Mama Kayoza aliongea kwa upole,

"ndio, ila nae amesema dawa ipo",Sajenti Minja akasema kiunyonge,

"si angewapa kama ipo",Mama Kayoza aliongea kwa mshangao,

"amesema ipo KIJIJINI KWA BIBI yake Kayoza",Sajenti Minja alijibu,

"mh, kweli ni yale yale",Mama Kayoza nae akawa mnyonge ghafla.

Ikawabidi wajipange, na mwisho wakakubaliana kuwa, Sajenti Minja achukue likizo fupi kwa ajili ya safari ya Bukoba.

*************************

Yule kijana aliyepewa kazi ya upelelezi alukuwa ni mpelelezi haswa, unaweza kujiuliza kwanini asingepewa kazi usalama wa utaifa?

Maana sio kufuatilia tu nyendo za Omary, ila mpaka baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wakina Omary alikuwa anayapata kwakutumia ujanja anaoujua yeye.

na hapa alikuwa ameyasikia maneno yanayohusu safari ya Bukoba, sasa alipoyasikia haya, akaenda hadi kwa Mkuu wa Polisi,

"vipi bwana mdogo, kuna mafanikio?",Mkuu wa Polisi alimuhoji yule Kijana,

"yapo mengi sana mkuu. Kwanza pole kwa msiba kwa maana kipindi kile nilikuja ila nilishindwa kuonana na wewe",Suma alijibu kwa kujiamini, na pia akatoa maneno ya pole,

"Siwezi kusema asante kwa maana uchungu bado ninao, tena mkubwa tu, na ukizingatie mtoto mwenyewe alikuwa mmoja tu" Mkuu wa polisi alijibu,

"Tatizo lilikuwa nini, maana Mimi nilisikia juu juu tu kuwa mlivamiwa?" Suma aliuliza,

"Ndiyo hayo hayo mambo ambayo nilikuagize uyafuatilie ndio yamenirudia nyumbani kwangu" Mkuu wa polisi aliongea kwa unyonge,

"Aisee pole sana. Sasa nimekuja hapa kukueleza nilipofikia" Kijana Suma aliongea huku akiweka note book yake mezani,

"ehe, niambie kijana wangu",Mkuu wa Polisi aliongea huku akibadilisha mkao katika kochi,

"kwanza kabisa, yule kijana unayemtambua kama Remmy, jina lake halisi ni Omari Mkwiji, ni mwenyeji wa Tanga, pia mwanafunzi wa UDOM pale Dodoma, na pale hana undugu na yeyote kati ya wale, ila anaishi pale kama rafiki wa mjomba wake Sajenti Minja, ambae anaitwa Kayoza. Na mahali walipokutana nae ni Dodoma pale Chuo kikuu.

Huyu Kayoza ndio mwenye matatizo sasa, yeye ndio mnyonyaji wa damu, na Siku binti yako anafariki ni yeye ndio aliyemuua na hiyo habari niliisikia kwa Dada yake Sajenti Minja wakati wakiwa wanajadili kuumaliza ugonjwa wa Kayoza unaosababisha yeye kuwa katika hali ile ya kunyonya damu watu, na hapa ninavyokuambia ni kuwa Sajenti Minja atakuja kukuomba likizo ya muda kwa sababu walienda kwa mganga, wakaambiwa waende kijijini kwa bibi yake Kayoza ambapo ni Bukoba, uko ndipo waliambiwa kuwa kuna dawa ya kumponya Kayoza, kwa hiyo Sajenti Minja ataongozana na Kayoza na Omari kwa ajili ya Safari",yule Kijana alimaliza hivyo,

"kwa hiyo Minja anajua mchezo mzima, hata ile kesi kumbe ni ujanja ujanja tu!",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti yenye mawazo yaliyoificha hasira yake,

"mimi nafikiri kazi uliyonituma nimeshaimaliza",sauti ya yule Kijana ilimshtua Mkuu wa Polisi aliyekuwa kazama ndani ya kina kirefu cha mawazo,

"sawa, asante, ngoja nikuletee mzigo wako",Mkuu wa Polisi aliongea huku akinyanyuka na kuelekea ndani.

Baada ya dakika chache alitoka na bahasha kubwa ya kaki, akamkabidhi yule kijana, yule Kijana akazitoa pesa ndani ya bahasha, akazihesabu, kisha akaagana na Mkuu wa Polisi.

"Kijana uliniambia huna kazi?" Mkuu wa polisi alimuuliza Suma ambaye alikuwa ameshaanza kuondoka,

"Ndio Mkuu" Suma alijibu huku akisimama,

"Jiandae basi, maana nakuandalia barua itayokufanya uende moshi ukachukue mafunzo ya uaskari" Mkuu wa polisi alitoa maneno yalimfanya Suma amshukuru sana,

"Asante sana, nine lini?" Suma aliuliza,

"Nitaakutaharifu kupitia simu, we kaa tayari tu kwa maana itakuwa muda wowote kutoka sasa" Mkuu wa polisi alimjibu,

"nashukuru sana mzee wangu.
Ubaki salama", Suma aliongea na kuondoka sake na kumuacha Mkuu wa polisi akiwa sebuleni,



"Sajenti Minja, Joel Minja, Minja, Minja, lazima nikuue kwa mkono wangu, wewe ndio umesababisha mwanangu amekufa kifo cha aibu",Mkuu wa Polisi aliongea kwa sauti ndogo huku akiwa ameuma meno kwa hasira,

"Kwa hiyo Omary sio muuaji, Kayoza ndiyo kamuua binti yangu?, Minja unajua kila kitu ila umeficha mpaka mwanangu ameuwawa kinyama? Hakuna atakayesalimika kati yenu" Mkuu wa polisi aliongea na kisha akagida kinywaji kikali chenye rangi ya maji kilichokuwa katika chupa kubwa kama ya waini (wine) ila chenyewe ubavuni kiliandikwa MAGIC MOMENT.

********************

Siku iliyofuata, Sajenti Minja alipanga akaombe likizo, akajitayarisha vizuri, na kuwa nadhifu kama kawaida yake. Akachukua gari yake na kwenda nayo moja kwa moja mpaka ofisini.

Ofisini aliingia saa nne asubuhi, alipokelewa na pole nyingi sana kutoka kwa askari wenzake, kwa sababu toka apate ajali ndio kwa mara ya kwanza alikuwa anaingia ofisini, baada ya salamu za hapa na pale, akawa anaelekea katika ofisi ya Mkuu wa Polisi, alipofika akagonga mlango,

Mkuu wa Polisi alikuwa ndani,
"nani?",Mkuu wa Polisi akauliza,

"Minja",Sajenti Minja akajibu kwa nje,

"leo ndio mwisho wako mshenzi na msaliti mkubwa wewe",Mkuu wa Polisi aliongea huku akijaza risasi katika bastola yake ndogo, alipomaliza, akamwambia Sajenti Minja aingie.......

********ITAENDELEA********

the Legend☆

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KIJIJINI KWA BIBI--53

...ila sauti yake haikumfikia Mkuu wa Polisi, Sajenti Minja akarudi ndani ya choo, kisha akafunga mlango, akawa anachungulia kupitia tundu la ufunguo, akamshuhudia Mkuu wa Polisi akielekea nje.

"Amekuja kufanya nini huku? Au amejipa likizo na yeye kutokana na kifo cha mwanae? Au anatufuatilia?" Sajenti Minja alikuwa anajiuliza mwenyewe huku akiwa bado yupo ndani ya choo.

Baada ya dakika tano, Sajenti Minja alitoka chooni na kuelekea walipo wakina Kayoza,

"vipi anko, mbona umekaa muda mrefu sana?",Kayoza alimuuliza Sajenti Minja,

"tumbo limenishika si mchezo, mimi naona nirudi nikapumzike, nyie endeleeni na ziara",Sajenti Minja hakutaka kusema ukweli, ingawa mshtuko wa kumuona Mkuu wa Polisi ulimfanye achoke ila hakuwa na sababu ya kuwaambia wenzake ukweli kutokana na yeye kutokuwa na jibu haswa juu ya uwepo wa Mkuu wa polisi katika eneo lile,

"sisi tumeshamaliza, tulikuwa tunakusubiri wewe tu",Kayoza alimwambia Sajenti Minja,

"haya bwana, mimi naelekea mjini, nyie nendeni tu nyumbani, njia si mnaikumbuka?",Mwenyeji wao aliwauliza,

"tunaikumbuka bwana mkubwa",Sajenti Minja alijibu huku akijilazimisha kutabasamu,

Kisha wakaagana na mwenyeji wao, na wao wakashika njia ya kurudi nyumbani.

Sajenti Minja akaona huo ndio muda mzuri wa kuwaambia alichokiona, ingawa alitaka kuwaficha ila akaona haitakuwa vyema kuwaficha kwa kuwa wao ni wamoja na wamefika mkoa ule kwa lengo moja.

"jamani nimemuoona Mkuu wa Polisi pale hotelini",Sajenti Minja aliongea kisha akawa anasubiri swali,

"Mara hii umeshaonana na mkuu wa polisi wa mkoa huu, kweli nyie maaskari mnajuana sana" Omary aliongea huku akishangaa,

"Sio wa mkoa huu, yule wa Shinyanga" Sajenti Minja alitoa Maelezo yaliyowafanya wenzake washtuke,

"itakuwa umemfananisha",Omari aliongea huku akiwa bado anamshangaa Sajenti Minja,

"nimemfananisha vipi?, wakati namfahamu fika",Sajenti Minja aliongea kwa kupaniki,

"sasa huku kafuata nini?",Omari akamuuliza,

"huwezi jua bwana, yule ni polisi, inawezekana anatufatilia sisi",Sajenti Minja aliongea kwa uhakika,

"duniani wawili wawili mjomba",Kayoza aliongea baada ya kuwa kimya muda mrefu,

"ok, mmeshinda, ila mtaniambia wenyewe",Sajenti Minja alimaliza, kisha wakaendelea na stori nyingine, huku Sajenti Minja akiwa hana amani kabisa katika moyo wake.

Walipofika nyumbani, wakapelekwa moja kwa moja hadi kwenye chumba cha Bibi yake Kayoza, wakamsalimia, kisha wakatambulishwa, Bibi Kayoza alifurahi sana, alipomuona Kayoza, waliongea sana,

"ila bibi pamoja na kukusalimia, kuna jingine lililonileta huku",Kayoza alimwambia Bibi yake,

"hata usiniambie mume wangu, najua lililokuleta",Bibi yake Kayoza alimkatisha Kayoza,

"nateseka sana bibi, naishi maisha ya kutafutwa na askari kama jambazi",Kayoza aliongea kwa majonzi,

"ilikua lazima upitie hiyo hali mume wangu",Bibi yake Kayoza alisema na kumfanya Kayoza avute kamasi kwanza,

"kivipi bibi?",Kayoza alihoji huku akifuta machozi,

"bila ubishi wa baba yako na kiburi cha mama yako, yote yasingekukuta hayo",Bibi Kayoza alisema, kisha akawapa hadithi ile ile waliyopigiwa na Mama Kayoza.

"yote hayo yamepita, kilichonileta huku ni dawa ya kuniachanisha na hili dudu",Kayoza aliongea kwa upole,

"Futa kauli yako, usiseme hili dudu, kusema hivyo ni kosa kama mwananchi kumtukana rais wake" Bibi Kayoza alimwambia mjukuu wake tena hata sura yake ilionesha hakufurahishwa na kauli ya Kayoza,

"Sasa ni jina lipi unaona linafaa kuitwa?" Kayoza aliuliza na yeye alipaniki baada ya kuna Bibi yake akikitetea kile kiumbe kinachomnyima yeye Furaha ya maisha,

"Heshimu mazingira kama unataka kupona, kinyume na hapo hakuna kitakachowezekana" Bibi Kayoza aliongea maneno ambayo yalieleweka vizuri kwa Kayoza,

"Sawa nimekuelewa bibi, sasa hapa nimekuja kufuata dawa" Kayoza alimwambia bibi yake,

"dawa ipo, ila nitakupa usiku",Bibi yake kayoza alimwambia mjukuu wake,

"kwani ni dawa gani bibi?",Kayoza aliuliza,

"utaijua usiku huo huo",Bibi yake Kayoza alijibu,

"Na kwanini iwe usiku bibi?" Kayoza aliendelea na udadisi wake,

"Usiku kwa sababu ya kuwa watu wote wa hapa walioenda kazini watakuwa wamerudi nyumbani" Bibi Kayoza alijibu,

"Kwani ni lazima wawepo?" Kayoza aliendelea kuuliza,

"Ndio ni lazima wawepo, kwa sababu haya mambo yamekaa kimila, kwa hiyo basi ni lazima wanaukoo wote washiriki" Bibi Kayoza alijibu na kisha wakaendelea na hadithi zao binafsi kwa kushirikiana na Sajenti Minja na Omary ambao muda wote walikaa kimya ili kumuachia Kayoza uwanja mpana wa kuuliza maswali yake.

**************

Mkuu wa Polisi alifanikiwa sio kupajua tu mahali walipofikia wakina Sajenti Minja, alipajua mpaka Mahalia wanapolala yaani chumba walichokuwa wanakitumia wakina Sajenti Minja.

Mkuu wa polisi akapanga kuwa usiku huo ndio itakuwa mwisho wao kuvuta hewa safi ya duniani.

********************

Usiku ulipoingia, wakakusanyika wanaukoo wote, kisha wakatangaza lengo la kuitwa pale, ambalo lilikuwa ni kumuamisha mzimu kutoka kwa Kayoza na kwenda kwa Baba yake mdogo. Watu wasiokuwa wa ukoo ule hawakuhusika kujumuika pale, kwa hiyo Sajenti Minja na Omari waliambiwa wakae vyumba vya uwani. Wakina Sajenti Minja wakaondoka na kuelekea uko uwani.

Shughuli ikaanza ya kuuhamisha mzimu, yakaletwa maji masafi, mbuzi jike mwenye mimba na majani ya mitishamba ambayo waliyajua wao wenyewe.

Kayoza akalazwa chini, na pembeni yake alikuwa baba yake mdogo, bibi akaanza vitu vyake.

Muda wote huo, mkuu wa Polisi alikuwa anafuatilia kila kitu, mpaka kile kitendo cha wakina Sajenti Minja kuenda vyumba vya uwani alikiona, akawa anavuta muda ili akakamilishe azma yake, muda wake alioupanga ulipofika, akawa anaelekea kwenye chumba walichokuwepo Sajenti Minja na Omari, alipofika akagonga, bila ya kufikiria kuuliza mgongaji nani?, Omari akaundea mlango kisha akafungua, hakuamini macho yake alipomuona mkuu wa Polisi amesimama mlangoni huku kashika bastola, Omari kabla hajafanya chochote, alipigwa risasi kama nne hivi za kifuani, na kuanguka chini kwa kishindo mithili ya embe kubwa ambayo halijakomaa lililopopolewa mtini.

Na kule nje kwenye tambiko, wakati bibi anaendelea na tambiko, ulisikika mlio wa risasi ulisababisha mstuko na kumpelekea bibi kuanguka na kufa kwa presha iliyotokana na mshtuko wa ulisababishwa na mlio wa risasi, Bibi akawa amekufa bila hata kufanikisha zoezi la kuuhamisha mzimu.

Baada ya mlio wa risasi kusikika na bibi kuanguka chini kama mzigo, watu wote katika eneo lile walikurupuka, wingine wakiundea mwili wa bibi na wengine walikimbilia eneo ambalo mlio wa risasi ulitokea, wakakuta mtu akitokomea gizani kwa mbele yao mlangoni alikuwa Omary aliyekuwa amelala chini huku damu zikiwa zimemtapakaa,

Sajenti Minja akamsogelea na kukaa chini huku machozi yakimtoka na kuchukua kchwa cha kayoza na kukiweza mapajani mwake, akawa anamuangalia Omary aliyekuwa anatabasamu huku kila akitoa funda la pumzi lilikuwa likitoka huku limeambatana na damu.

Wenyeji wa pale walikuwa wanashangaa na wasijue la kufanya.

Omary akafumbua macho na kumuangalia Sajenti Minja aliyekuwa analia, kisha Omary akaongea maneno machache tu,

"Mk....uu ...wa...pol...isi" Omary aliongea kauli ambayo watu wengine hawakuielewa isipokuwa Sajenti Minja pekee.

Omary baada ya kutamka maneno hayo, shingo yake ililegea na kuanguka, huo ndio ukawa mwisho wa maisha ya Omary, roho yake ikatengana na mwili akiwa ugenini, kauli ya babu yake ikatimia.....

********ITAENDELEA**"****"***

the Legend☆
maskini omary wangu mimi,mkuu wa polisi nakuchukia mimi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom