Riwaya: Kijijini kwa Bibi

Riwaya: Kijijini kwa Bibi

KIJIJINI KWA BIBI--59

...jinsi walivyozidi kusogeleana ndio machozi katika macho yao yalizidi kuongezeka, walikumbatiana kwa furaha iliyoambatana na uchungu wa kumbukumbu mbaya za nyuma, kwa dakika nzima hakuna aliyemsemesha mwenzake,

"pole mwanangu, hiyo yote ni mitihani ya dunia", ndivyo mama Kayoza alianza kuongea maneno hayo ambayo aliamini yatamfariji mtoto wake,

"kwanini mimi tu mama, kila uchungu unapita katika njia ya moyo wangu, kwanini mimi, nimemkosea nini Mungu?", Kayoza aliongea huku akilia,

"yanapita hayo mwanangu, vumilia na uamini mungu yuko pamoja na wewe", Mama kayoza aliendelea kumfariji mwanae, kisha akaendelea,

"hata mimi mjomba wako aliponipigia simu na kunieleza kifo cha Omary na bibi yako, nilisikitika sana na mbaya zaidi aliniambia kuwa bibi yako alikufa wakati anajiandaa kukutoa hilo dubwana linalokusumbua", Mama Kayoza alipofika hapo akanyamaza baada ya kuona Kayoza analia kwa uchungu sana.

"mjomba wako yuko ndani?", Mama Kayoza aliuliza swali lililozidisha kilio kwa mwanae,

"ina maana mama hujui?", Kayoza akajikuta anamtupia swali mama yake,

"sijui nini?, mbona unanipa wasiwasi tena!", Mama Kayoza aliuliza kwa mshangao,

"habari za mjomba Minja", Kayoza akaendelea kumfafanulia mama yake,

"ehe, kaka yangu kafanyaje tena", Mama Kayoza akaendelea kuuliza huku tayari akiwa amejaa wasiwasi sana, kwa maana kauli za Kayoza zilianza kumtisha,

"Mjomba minja alipigwa risasi, ila hakufa na jana kavamiwa na mtu asiejulikana na akamchoma kisu cha...", Kayoza alishindwa kumalizia baada ya mama yake kuanguka chini na kupoteza fahamu.

Ikambidi Kayoza awaite ndugu zake wamsaidie, dakika tano zikapita bila Mama Kayoza kuzinduka.

"Umemfanyaje mama yako?" Baba ake mdogo Kayoza alimuuliza Kayoza,

"Sijamfanya kitu" Kayoza alijibu,

"Amekuja saa ngapi?" Baba mdogo aliendelea na Maswali,

"Ameingia muda si mrefu" Kayoza alijibu,

"Mbona hajasema kama anakuja, au wewe alikupa taharifa?" Baba mdogo aliuliza,

"Na wewe nawe punguza maswali yako bwana, si umsubiri azinduke ndio umuulize yeye mwenyewe hayo maswali" Kayoza aliongea kwa hasira baada ya kuona maswali yamekuwa mengi kuliko vitendo,

"We unamjibu nani hivyo?" Baba mdogo aliuliza kwa hasira,

"Kwani naongea na nani, au naongea na nyani?" Kayoza nae aliongea kwa hasira, na kufanya baba yake mdogo atake kumvaa ila ndugu wengine waliingilia kati na kumzuia baba yake mdogo apunguze hasira,

"Kwanza tokea mmekuja hapa ndio matatizo nayo yamekuja, mna mikosi tele imewajaa" Baba mdogo aliongea kwa hasira,

"Na bado mkosi mwingine unakuja" Kayoza alijibu huku akimpepea mama yake aliyekuwa bado amepoteza fahamu,

"Tusijibishane Kayoza ujue nitakupiga" Baba mdogo aliongea huku akimnyooshea kidole,

"Kunipiga huwezi, na sitaki tena malumbano na wewe, vinginevyo nitafanya kitu ambacho hutokaa unisahau" Kayoza aliongea huku akimuangalia baba yake mdogo kwa jicho Kali sana,

"Utafanya nini sasa wewe?, we si Mbwa tu" Baba mdogo aliongea kwa hasira na kufanya watu wamtoe eneo lile kwa maana waliona hakukuwa na umuhimu tena watu hao kukaa pamoja muda huo.

Baada ya baba mdogo kutolewa kidogo amani ilirejea katika eneo lile,

"Mimi naona hawezi kuamka, ni bora tumpeleke hospitali" Ndugu mmoja aliongea huku akimuangalia Kayoza,

"Hata mimi nilikuwa na wazo kama hilo" Ndugu mwingine aliongezea,

"Twendeni tu, Hamna jinsi" Kayoza aliongea.

Uhamuzi uliopitishwa ni kumpeleka hospitali, wakakodi gari la abiria, wakampakia mama Kayoza, huku Kayoza na Shangazi yake wakichukua jukumu la kumsindikiza.

Walipokaribia eneo la hospitali, mama Kayoza alirejewa na fahamu zake,

"unajisikiaje wifi?", Shangazi yake Kayoza alimuuliza Mama Kayoza,

"safi, tunaelekea wapi?", mama Kayoza aliuliza,

"hospitali", Kayoza alimjibu mama yake,

Mama kayoza baada ya kusikia neno "hospitali", kumbukumbu zikamrudia, akaanza kuangua kilio ndani ya gari huku akitaja jina la Sajenti Minja.

"Mama na wewe bwana, kwani amekufa?" Kayoza aliuliza kwa jazba,

"Muache alie ili apunguze uchungu" Shangazi yake alijibu,

"Sasa inakuwa ni Makelele tu kama tunamsiba bwana" Kayoza aliongea kwa kulalamika,

"Siku hizi umekuwaje wewe, hivi hata hujioni kuwa upo tofauti?" Shangazi yake aliuliza huku akiwa amemkazia macho Kayoza na kufanya Kayoza akae kimya tu.

Walipofika hospitali, Kayoza akaenda katika chumba cha Daktari. Maana alishakariri kila sehemu ya hospital na karibu madaktari wote wa ile hospitali walikuwa wanamjua Kayoza kutokana na kushinda sana eneo la Hospitali.

"ooh, afadhali dogo umekuja, maana tulikuwa tunakusubiri wewe", Daktari alikua akimwambia Kayoza maneno hayo,

"vipi hali ya mgonjwa wangu?",Kayoza alimtupia swali Daktari,

"mgonjwa wako bwana,...tayari tumeshamfanyia upasuaji, na tumefanikiwa kulitoa jicho lake la kushoto, ila tumemuwekea jicho la kondoo", Daktari alijibu kwa ufasaha swali la Kayoza,

"kwa hiyo gharama zote ni kiasi gani?", Kayoza aliuliza,

"ni milioni mbili na laki tatu, kwa sababu hata hilo jicho la kondoo tumelinunua kwa pesa nyingi kidogo", Daktari alimuelewesha Kayoza,

"Ila dokta si ulisema ni laki tatu tu?" Kayoza alimuuliza daktari huku akimshangaa,

"Ila si nimekwambia hilo jicho la kondoo tumelinunua" Daktari aliongea huku akitabasamu,.

"Sasa hicho la kondoo ndio milioni moja?, si ungeniambia mimi nilete, ningekuja nalo tu kwa maana nyumbani tuna kondoo wengi tu" Kayoza aliongea huku akimshangaa daktari,

"Ninaposema jicho la kondoo simaanishi ni jicho la kondoo mnyama, ninachomaanisha ni jicho la bandia" Daktari aliongea huku akitabasamu,

"Ila milioni mbili na laki tatu ni nyingi sana, siwezi kuzimudu" Kayoza aliongea kwa sauti ya unyonge.

"Wewe una shilingi ngapi?" Daktari alimuuluiza,

"Mimi nilijiandaa na hiyo laki tatu, ila itanibidi niongeze na laki mbili, kwani ndio niliyonayo" Kayoza alizungumza,

"Sawa nipe hiyo, ila mwenzangu yoyote akikuuliza useme umenipa laki tatu" Daktari aliongea huku akimtazama Kayoza,

"Ila hapa sina" Kayoza alijibu,

"Aaaagh dogo, zikwapi sasa?" Daktari aliuliza huku akionekana hajafurahishwa na kauli ya Kayoza,

"Nitakuletea kesho asubuhi" Kayoza alimuelewesha Daktari,

"Zamu yangu inaisha leo ila itanibidi nikusubiri mpaka kesho utakapoleta, na ulete kweli kesho" Daktari aliongea kwa mkazo,

"sawa dokta, nitazileta kesho hasubui", Kayoza alijibu.

Baada ya hapo, Daktari akatoka na Kayoza na kwenda katika wodi aliyolazwa Sajenti Minja, huku wakiambatana na Mama na Shangazi wa Kayoza.

**********************

BAADA YA MWEZI

Jumamosi asubuhi ndiyo siku ambayo Sajenti Minja aliruhusiwa kurudi nyumbani huku akiwa na ulemavu wa maisha. Kayoza na Mama yake ndio walikwenda kumchukua hospitali.

Walipofika nyumbani, walipokelewa kwa furaha sana,

"itabidi leo tufanye sherehe ya kumshukuru Mungu kwa maajabu aliyoyaonesha kwa bwana Minja", Baba yake mdogo Kayoza alitoa wazo,

"hapana baba, sherehe iwe kesho",Kayoza aliongea huku akiwa na sura ya furaha,

"kwanini unataka iwe kesho mwanangu?", Baba yake mdogo alimuuliza Kayoza,

"kwa sababu kesho nataka kufanya kitu ambacho kitakua kama historia ya kumbukumbu nzuri ya ushujaa kwangu", kama kawaida yake, Kayoza aliongea huku akiwa na tabasamu,

"mh! kitu gani hicho?", Mama Kayoza alimuuliza mtoto wake,

"hampaswi kuwa na haraka, nyie ngojeni nataka iwe kama tukio la kushtukiza kwenu", Kayoza alimjibu mama yake,

"haya bwana, sisi tunasubiri kwa hamu.

******************

Kesho yake ambayo ilikua jumapili, mida ya saa nne asubuhi, Kayoza akaondoka kwao bila ya kuaga na kuelekea katika ile guest aliyopanga Mkuu wa Polisi, alipofika mapokezi, alimuuliza yule muhudumu kama mtu aliyemfuata yupo, akajibiwa yupo tena amelewa sana, Kayoza akaenda mpaka katika mlango wa chumba cha Mkuu wa Polisi, aliingiza mkono katika mfuko wa suruali na kutoa kitambaa ambacho alifunga puani, kama mtu anayezuia harufu fulani.

kisha akagonga mlango huku akiwa kashika chupa tupu ya soda mkononi, mkuu wa Polisi akauendea mlango, kisha akaufungua, alipofungua tu, alikutana na chupa ya kichwa iliyompeleka moja kwa moja sakafuni, Kayoza akatumia vizuri nafasi ya kumshambulia mfululizo mpaka Mkuu wa Polisi akawa hatamaniki kwa jinsi alivyokuwa anavuja damu kichwani, ghafla Mkuu wa Polisi akampiga teke Kayoza na kusababisha chupa imponyoke Kayoza, Mkuu wa Polisi kwa kasi ya mshale, akakimbilia katika kitanda chake, akaunyanyua mto, kisha akachukua bastola yake na kumuelekezea Kayoza,

"mwanaharamu mkubwa wewe, kwa kitendo ulichonifanyia, sio rahisi nikikuacha hai", Mkuu wa Polisi aliongea huku akikoti risasi katika bastola yake, Kayoza alitawaliwa na hofu na kukata tamaa. Aliamini hapo ndipo mbio za kupambana na Mkuu wa polisi zake zilipoishia.

Mkuu wa polisi akaweka target katika paji la uso wa Kayoza, Kayoza akafumba macho kuashiria kukata tamaa, Kisha Mkuu wa Polisi akafyatua risasi..

**********ITAENDELEA*********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI--60

SEHEMU YA MWISHO.

....lakini risasi haikutoka, Mkuu wa polisi akajaribu tena, lakini hali ikawa ile ile, bastola ilikua haina risasi, Mkuu wa Polisi akaruka mpaka kwenye kabati, akachukua mfuko wa risasi, Kayoza kuona hivyo, akaikimbilia chupa ya soda aliyokuja nayo, ambayo ilikuwa karibu na mlango, ile kuikota ili amuwai akakuta tayari Mkuu wa Polisi anaikoki bastola, Kayoza akamuwai, akarusha ile chupa ambayo iliupiga mkono wa Mkuu wa Polisi ambao ulikua umeshika ile bastola na kufanya ile bastola iende chini, Kayoza akaruka juu na kumpiga teke Mkuu wa Polisi, Mkuu wa Polisi akadondoka chini, Kayoza akaiokota ile bastola na kumfyatulia Mkuu wa Polisi risasi zisizo na idadi mpaka akafa. Kisha hapo ndipo akakiri kuwa ana kosa sasa la mauaji, kwa maana ameua kwa kukusudia tofauti na anavyoua kipindi mzimu unapompanda.

Kayoza akaenda katika kabati na kuvunja kioo, akachukua kipande cha kioo, kisha akachukua ndoo iliyo mule ndani na kwenda sehemu ulipo mwili wa Mkuu wa Polisi, akaanza kuuchinja huku akikinga damu kwa kutumia ile ndoo, mpaka aliporidhika. Na kumbuka kipindi chote hicho alikuwa na kitambaa puani ambacho alikipulizia pafyumu kwa ajili ya kuzuia harufu ya damu ya aina yoyote ile.

Baada ya kufanya ukatili huo ambayo hakutaka kabisa kuujutia, Kayoza alicheka mwenyewe ndani ya chumba ambacho alifanyia mauaji na kisha Kazi kubwa ambayo ilimkabiri kwa wakati huo ikawa ni kutoka nje, maana watu walishajaa nje.

Akachukua kichwa cha Mkuu wa Polisi akakiweka ndani ya ndoo, kisha akaifunika ndoo, safari ya kwenda nje ikaanza, alipofungua mlango watu wote wakatawanyika, kwa maana waliamini Kayoza sio mtu wa kawaida kabisa, na ili kuwatisha zaidi, Kayoza akapiga risasi hewani, watu wakakaa nae mbali kabisa, nguo zote alizozivaa zilikuwa zimetapakaa damu, ila yeye hakuweza kuisikia harufu ya damu kutokana na kitambaa alichojifunga puani kwa ajili ya kuhofia mzimu kumpanda endapo harufu ya damu itapenya puani mwake.

Akatoka na ndoo yake mpaka kwao, huku akifuatwa na kundi la watu na waandishi wa habari walikuwepo, tena wengi walikuwa na furaha kwa sababu ya kupata habari itakayouza magazeti yao.

Njia nzima alikuwa akitembea huku kundi kubwa sana la watu likimfuata na kila mmoja akisema lake kutokana na ukatili ule waliokuwa wanaushuhudia mubashara, kwa maana vitu kama vile walishazoea kuviona katika filamu za watu wa mashariki mpwa dunia au kukutana navyo katika simulizi za wakina ALEX KILEO.

Alipofika kwao, akatoa onyo kuwa, mtu yeyote asimsogelee, na mtu ataekaidi amri, atampiga risasi. na kweli walimuogopa kwa maana Kayoza wa siku hiyo hakuwa na chembe za ubinadamu kabisa, hata sura yake ilidhihirisha hiyo kwa maana zile damu zilizomtapakaa mwili mzima na macho yake yalivyokuwa mekundu yalionesha hakuna hatari anayoiona mbele yake. Tayari alishaamua kuwa mnyama na aliona hiyo ndiyo bora ya kufanya kwa wakati huo.

Baada ya kufika kwao, Kayoza akaingia katika chumba chake akajifungia mlango kwa ndani, hapo ndipo alipodhamilia kufanya kama Maelezo ya mganga wa mwisho kumtembelea yalivyosema, akakumbuka kuwa mganga alisema kuwa njia ya kuundoa huo mzimu inaweza kugharimu na maisha yake, yaani maisha ya Kayoza, hata Sajenti Minja alipouliza ni njia gani hiyo? Mganga alijibu kuwa itabidi achinjwe kondoo alafu Kayoza awekwe katika kitanzi ili harufu ya damu itakapoingia puani kwa Kayoza ni lazima mzimu umpande, na hapo ndipo ile kamba ya kitanzi ivutwe na imnyonge kayoza, ni lazima kayoza ni lazima afe na mzimu ufe kwa maana mzimu hutegemea pumzi katika kutoka na kuingia katika mwili wa Kayoza.

Baada ya Kayoza kuyakumbuka maneno hayo, alijikuta akitabasamu, tabasamu la umauti lililokuwa linatoka pasipokuwa na furaha ila hasira zilizotokana na kukata tamaa ya kupata suluhisho la matatizo yake.

kisha akachukua kamba akaitundika juu na kuweka kitanzi, kisha akaweka stuli na kupanda juu, alafu akaifunua ile ndoo ambayo aliiwekea damu ya Mkuu wa Polisi, akakitoa kile kichwa na kukitupia chini ya kitanda, kisha akajifungua kile kitambaa puani, harufu ya damu ikampenya sawa sawa katika matundu ya pua yake, alivyoanza kuhisi dalili ya kupandwa na mzimu akaitupa ile ndoo, na kuitegua stuli, mzimu ukawa tayari umeshampanda, na kitanzi kikambana sawa sawa, Kayoza na mzimu wake, akaanza kupiga kelele kwa sauti ya ajabu, hali iliyofanya watu waliokuwa nje ya nyumba watawanyike.

Nje, kwanza ilipiga radi kubwa sana, huku ikifuatiwa na upepo mkali sana, mpaka nyumba zenye udhaifu zilianguka, alafu ikanyesha mvua kubwa sana ikiambatana na jua kali sana.

Kayoza ilimchukua kama dakika thelathini kuangaika juu ya kitanzi, mwishowe alitulia kimya kabisa, na ukawa ndio mwisho wa maisha yake na mzimu wake.

Polisi ndio walikuja kuvunja mlango na kuukuta mwili wa Kayoza unatoa moshi na ulikuwa mweusi sana kuashiria alikuwa anaungua, macho na masikio yalikuwa yametoboka, hakika kilikuwa kifo kilichosikitisha sana, kifo ambacho kilihitimisha urithi wa kimizimu katika ukoo.

Sajenti Minja alilia kama mtoto kutokana na yote aliyofanya katika kumlinda Kayoza na uhai wake, lakini ilikuwa kama bure, na mbaya zaidi aliyakumbuka maneno ya Kayoza ya jana yake, ambayo Kayoza alidai anataka sherehe ifanyike leo kwa sababu anataka kufanya jambo la kukumbukwa daima.

"kumbe jambo lenyewe ndio hili, umelifanya mapema sana mjomba, ungesubiri mjomba, kama ungesubiri nina uhakika uhai wako usingetoweka", Sajenti Minja aliongea mbele ya jeneza la Kayoza ambalo liliwekwa mbele ya watu kwa ajili ya kuuaga mwili wa marehemu Kayoza.

Mama Kayoza alianguka na kuzimia mara nne, kitendo ambacho kilisababisha apelekwe hospitali na ikagundulika mshtuko wa moyo.

Mambo ya maziko yalienda kama kawaida na kumalizika salama.

Kwa upande wa Mkuu wa Polisi, mwili wake ulizikwa na manispaa ya mkoa wa Kigoma kutokana na kutopatikana kwa kichwa chake ambacho Sajenti Minja alikificha makusudi ili kupoteza ushahidi na baada ya Siku alienda kukizika.

Uko kwao Shinyanga hawakupata taharifa yoyote, habari zilizotangazwa kwa wafanyakazi wenzake yaani polisi wenzie ni kuwa amepotea na hajulikani halipo.

BAADA YA MIAKA 3

Anaonekana Sajenti Joel Minja akiwa na familia yake, wakiweka shahada la maua katika kaburi la Mama Kayoza ambae alikufa mwaka mmoja uliopita kutokana na ugonjwa wa mshtuko wa moyo alioupata kutokana na mshtuko wa kifo cha mwanaye kipenzi (Kayoza).

Sajenti Minja aliacha kazi kutokana na ulemavu alioupata, sasa hivi ni mjasiliamali ambae ana kampuni yake binafsi ya usafirishaji wa abiria, ambayo inamiliki mabasi, maroli, daladala na taxi. Mabasi yake ni maarufu sana katika mikoa ya Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya na Tanga, Yanaitwa GHOST MEMORY.

Ana mke na watoto wawili, wa kwanza anaitwa Kayoza, na wapili anaitwa Omari, ikiwa kumbukumbu kwa watu wake wa karibu.

******* MWISHO ********

the Legend☆
 
KIJIJINI KWA BIBI--60

SEHEMU YA MWISHO.

....lakini risasi haikutoka, Mkuu wa polisi akajaribu tena, lakini hali ikawa ile ile, bastola ilikua haina risasi, Mkuu wa Polisi akaruka mpaka kwenye kabati, akachukua mfuko wa risasi, Kayoza kuona hivyo, akaikimbilia chupa ya soda aliyokuja nayo, ambayo ilikuwa karibu na mlango, ile kuikota ili amuwai akakuta tayari Mkuu wa Polisi anaikoki bastola, Kayoza akamuwai, akarusha ile chupa ambayo iliupiga mkono wa Mkuu wa Polisi ambao ulikua umeshika ile bastola na kufanya ile bastola iende chini, Kayoza akaruka juu na kumpiga teke Mkuu wa Polisi, Mkuu wa Polisi akadondoka chini, Kayoza akaiokota ile bastola na kumfyatulia Mkuu wa Polisi risasi zisizo na idadi mpaka akafa. Kisha hapo ndipo akakiri kuwa ana kosa sasa la mauaji, kwa maana ameua kwa kukusudia tofauti na anavyoua kipindi mzimu unapompanda.

Kayoza akaenda katika kabati na kuvunja kioo, akachukua kipande cha kioo, kisha akachukua ndoo iliyo mule ndani na kwenda sehemu ulipo mwili wa Mkuu wa Polisi, akaanza kuuchinja huku akikinga damu kwa kutumia ile ndoo, mpaka aliporidhika. Na kumbuka kipindi chote hicho alikuwa na kitambaa puani ambacho alikipulizia pafyumu kwa ajili ya kuzuia harufu ya damu ya aina yoyote ile.

Baada ya kufanya ukatili huo ambayo hakutaka kabisa kuujutia, Kayoza alicheka mwenyewe ndani ya chumba ambacho alifanyia mauaji na kisha Kazi kubwa ambayo ilimkabiri kwa wakati huo ikawa ni kutoka nje, maana watu walishajaa nje.

Akachukua kichwa cha Mkuu wa Polisi akakiweka ndani ya ndoo, kisha akaifunika ndoo, safari ya kwenda nje ikaanza, alipofungua mlango watu wote wakatawanyika, kwa maana waliamini Kayoza sio mtu wa kawaida kabisa, na ili kuwatisha zaidi, Kayoza akapiga risasi hewani, watu wakakaa nae mbali kabisa, nguo zote alizozivaa zilikuwa zimetapakaa damu, ila yeye hakuweza kuisikia harufu ya damu kutokana na kitambaa alichojifunga puani kwa ajili ya kuhofia mzimu kumpanda endapo harufu ya damu itapenya puani mwake.

Akatoka na ndoo yake mpaka kwao, huku akifuatwa na kundi la watu na waandishi wa habari walikuwepo, tena wengi walikuwa na furaha kwa sababu ya kupata habari itakayouza magazeti yao.

Njia nzima alikuwa akitembea huku kundi kubwa sana la watu likimfuata na kila mmoja akisema lake kutokana na ukatili ule waliokuwa wanaushuhudia mubashara, kwa maana vitu kama vile walishazoea kuviona katika filamu za watu wa mashariki mpwa dunia au kukutana navyo katika simulizi za wakina ALEX KILEO.

Alipofika kwao, akatoa onyo kuwa, mtu yeyote asimsogelee, na mtu ataekaidi amri, atampiga risasi. na kweli walimuogopa kwa maana Kayoza wa siku hiyo hakuwa na chembe za ubinadamu kabisa, hata sura yake ilidhihirisha hiyo kwa maana zile damu zilizomtapakaa mwili mzima na macho yake yalivyokuwa mekundu yalionesha hakuna hatari anayoiona mbele yake. Tayari alishaamua kuwa mnyama na aliona hiyo ndiyo bora ya kufanya kwa wakati huo.

Baada ya kufika kwao, Kayoza akaingia katika chumba chake akajifungia mlango kwa ndani, hapo ndipo alipodhamilia kufanya kama Maelezo ya mganga wa mwisho kumtembelea yalivyosema, akakumbuka kuwa mganga alisema kuwa njia ya kuundoa huo mzimu inaweza kugharimu na maisha yake, yaani maisha ya Kayoza, hata Sajenti Minja alipouliza ni njia gani hiyo? Mganga alijibu kuwa itabidi achinjwe kondoo alafu Kayoza awekwe katika kitanzi ili harufu ya damu itakapoingia puani kwa Kayoza ni lazima mzimu umpande, na hapo ndipo ile kamba ya kitanzi ivutwe na imnyonge kayoza, ni lazima kayoza ni lazima afe na mzimu ufe kwa maana mzimu hutegemea pumzi katika kutoka na kuingia katika mwili wa Kayoza.

Baada ya Kayoza kuyakumbuka maneno hayo, alijikuta akitabasamu, tabasamu la umauti lililokuwa linatoka pasipokuwa na furaha ila hasira zilizotokana na kukata tamaa ya kupata suluhisho la matatizo yake.

kisha akachukua kamba akaitundika juu na kuweka kitanzi, kisha akaweka stuli na kupanda juu, alafu akaifunua ile ndoo ambayo aliiwekea damu ya Mkuu wa Polisi, akakitoa kile kichwa na kukitupia chini ya kitanda, kisha akajifungua kile kitambaa puani, harufu ya damu ikampenya sawa sawa katika matundu ya pua yake, alivyoanza kuhisi dalili ya kupandwa na mzimu akaitupa ile ndoo, na kuitegua stuli, mzimu ukawa tayari umeshampanda, na kitanzi kikambana sawa sawa, Kayoza na mzimu wake, akaanza kupiga kelele kwa sauti ya ajabu, hali iliyofanya watu waliokuwa nje ya nyumba watawanyike.

Nje, kwanza ilipiga radi kubwa sana, huku ikifuatiwa na upepo mkali sana, mpaka nyumba zenye udhaifu zilianguka, alafu ikanyesha mvua kubwa sana ikiambatana na jua kali sana.

Kayoza ilimchukua kama dakika thelathini kuangaika juu ya kitanzi, mwishowe alitulia kimya kabisa, na ukawa ndio mwisho wa maisha yake na mzimu wake.

Polisi ndio walikuja kuvunja mlango na kuukuta mwili wa Kayoza unatoa moshi na ulikuwa mweusi sana kuashiria alikuwa anaungua, macho na masikio yalikuwa yametoboka, hakika kilikuwa kifo kilichosikitisha sana, kifo ambacho kilihitimisha urithi wa kimizimu katika ukoo.

Sajenti Minja alilia kama mtoto kutokana na yote aliyofanya katika kumlinda Kayoza na uhai wake, lakini ilikuwa kama bure, na mbaya zaidi aliyakumbuka maneno ya Kayoza ya jana yake, ambayo Kayoza alidai anataka sherehe ifanyike leo kwa sababu anataka kufanya jambo la kukumbukwa daima.

"kumbe jambo lenyewe ndio hili, umelifanya mapema sana mjomba, ungesubiri mjomba, kama ungesubiri nina uhakika uhai wako usingetoweka", Sajenti Minja aliongea mbele ya jeneza la Kayoza ambalo liliwekwa mbele ya watu kwa ajili ya kuuaga mwili wa marehemu Kayoza.

Mama Kayoza alianguka na kuzimia mara nne, kitendo ambacho kilisababisha apelekwe hospitali na ikagundulika mshtuko wa moyo.

Mambo ya maziko yalienda kama kawaida na kumalizika salama.

Kwa upande wa Mkuu wa Polisi, mwili wake ulizikwa na manispaa ya mkoa wa Kigoma kutokana na kutopatikana kwa kichwa chake ambacho Sajenti Minja alikificha makusudi ili kupoteza ushahidi na baada ya Siku alienda kukizika.

Uko kwao Shinyanga hawakupata taharifa yoyote, habari zilizotangazwa kwa wafanyakazi wenzake yaani polisi wenzie ni kuwa amepotea na hajulikani halipo.

BAADA YA MIAKA 3

Anaonekana Sajenti Joel Minja akiwa na familia yake, wakiweka shahada la maua katika kaburi la Mama Kayoza ambae alikufa mwaka mmoja uliopita kutokana na ugonjwa wa mshtuko wa moyo alioupata kutokana na mshtuko wa kifo cha mwanaye kipenzi (Kayoza).

Sajenti Minja aliacha kazi kutokana na ulemavu alioupata, sasa hivi ni mjasiliamali ambae ana kampuni yake binafsi ya usafirishaji wa abiria, ambayo inamiliki mabasi, maroli, daladala na taxi. Mabasi yake ni maarufu sana katika mikoa ya Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya na Tanga, Yanaitwa GHOST MEMORY.

Ana mke na watoto wawili, wa kwanza anaitwa Kayoza, na wapili anaitwa Omari, ikiwa kumbukumbu kwa watu wake wa karibu.

******* MWISHO ********

the Legend☆

Dah!Mungu akujalie sana mwandishi wetu 💪💪🔥🔥
 
Back
Top Bottom