RIWAYA: Mifupa 206

RIWAYA: Mifupa 206

[emoji274][emoji274][emoji274][emoji274][emoji274][emoji274]
 
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Kama vipi mkuu toa namba hii kitu tuinunue kabisa bobu
 
MIALE YA MWANGA WA JUA LA ASUBUHI ulipenya kupitia kioo cha
dirisha la chumbani na kuyapa uhai macho yangu na hapo nikayafumbua
taratibu na kuanza kupepesa huku na kule. Hisia zangu zikanieleza kuwa
nilikuwa kwenye mazingira tofauti kabisa na yale niliyoyazoea. Hapa ni wapi? Wakati
nikiendelea kujiuliza kumbukumbu za matukio yote yaliyotokea siku ya jana ikaanza
kujitengeneza upya kichwani mwangu.
Nikaanza kukumbuka namna nilivyokutana na Pastor Romanus wa kanisa la The
Last Days Ministry na kufanya naye kikao kifupi chenye majadiliano ya kina juu ya yale
yanayoendelea katika ulimwengu huu. Nikaendelea kukumbuka namna nilivyopata
dodoso chache juu ya Gabbi Masebo na msichana aliyefunga naye ndoa ambaye
alisemekana kuwa alikuwa muumini wa kanisa lile. Kufikia hapo nikakumbuka namna
nilivyokuwa nimemuomba Pastor Romanus anitafutie taarifa zote muhimu za Gabbi
Masebo na yule msichana aliyefunga naye ndoa likiwemo jina la msichana huyo na
mahali ndoa yao ilipofungwa. Nikakumbuka namna nilivyomuachia Pastor Romanus
kadi yangu ya mawasiliano ili anifahamishe haraka pale atakapokuwa amepata taarifa
hizo. Baadaye nikakumbuka namna nilivyofanikiwa kuwatoroka wale wanausalama
kule Botanical Garden maeneo ya posta ikiwa ni muda mfupi mara baada ya kutoka
kuonana na Pastor Romanus.
Sasa nilikumbuka vizuri kuwa mara baada ya kufanikiwa kuwatoroka wale watu
kwenye lile eneo la Botanical Garden maeneo ya posta nilikuwa nimekodi teksi
na kuelekea mahali ilipo Hotel Agent 11 kuonana na mwanamama wa kinaijeria
aliyejitambulisha kwangu kwa jina la Iko-Ojo Obaje wakati ule nilipokutana naye
usiku ndani ya Vampire Casino. Ni dhahiri kuwa kitendo cha Iko-Ojo Obaje kunipa
mwongozo wa anwani ya kumpata kupitia ile kadi aliyonipa usiku ule kule Vampire
Casino siyo tu kilikuwa kimefungua milango wazi ya kukuza urafiki wetu lakini vilevile
nilikuwa katika nafasi nzuri kabisa ya kuugusa moyo wake.
Nilipoendelea kukumbuka nini kilichofuata baada ya kupewa mapokezi mazito
na mwanamke yule wa kinaijeria wakati nilipokifikia chumba chake mle hotelini na
kugonga hodi ndiyo nikakumbuka vizuri kuwa pale nilikuwa wapi.
Nilikuwa ndani ya chumba namba 22 cha jengo la ghorofa la Hotel Agent
11 huku mwenyeji wa chumba kile akiwa ndiye yule mama wa kinaijeria Iko-Ojo
Obaje. Nikaendelea kukumbuka namna nilivyozama kwenye mapenzi motomoto
ya mwanamama yule katika kitanda kile muda mfupi baada ya kukaribishwa vizuri
mle ndani ya kile chumba usiku wa jana. Loh! kumbukumbu ile ikanipelekea nianze
kutabasamu taratibu pale kitandani kisha pasipo kugeuka nikaupeleka mkono wangu
kwa kiumbe kile. Mara hii sikufanikiwa na jitihada zangu zikagonga mwamba. Hisia
zangu zikanieleza kuwa nilikuwa nimeachwa peke yangu pale kitandani. Moyo
wangu ukalipuka ghafla,nikatupa shuka pembeni na kuketi pale kitandani. Mara hii
nikagundua kuwa sikuwa na nguo hata moja mwilini kama nilivyozaliwa. Hata hivyo
hali ile haikunishtua sana kama kile kitendo cha kutokumuona mwenyeji wangu akiwa
pale kitandani.
Kwa sekunde kadhaa nikaendelea kuketi pale kitandani huku nikiupisha utulivu
kichwani mwangu. Nilipoyatembeza macho yangu mle ndani nikajiridhisha kuwa
mandhari ya kile chumba yalikuwa hayajabadilika. Upande wangu wa kushoto
kulikuwa na dirisha pana lililofunikwa kwa pazia refu na jepesi. Mbele ya kile kitanda
kulikuwa na runinga kubwa ukutani na pembeni ya runinga ile kulikuwa na kabati
kubwa la nguo. Nilipoyatembeza macho yangu upande wa kulia nikaona makochi
mawili ya sofa yanayotazamana na meza fupi ya mbao ya mti wa mpingo pembeni ya
chungu kikubwa chenye ua la kupandwa la asili. Juu ya meza ile kulikuwa na glasi mbili
na chupa nne tupu za pombe kali tupu kando ya kibakuli kidogo cha majivu ya sigara
chenye vipisi vingi vya sigara vilivyotelekezwa.
Hatua chache kutoka pale yalipokuwa yale makochi na ile meza kulikuwa na
mlango wa kuingilia mle chumbani na nyuma ya mlango ule nikaziona nguo zangu
zikiwa zimening’inizwa katika sehemu maalum. Mlango ule ulikuwa ukitazamana na
mlango mwingine wa kile chumba kwa upande wa pili ambao haraka nilipouchunguza
nikagundua kuwa ulikuwa ni mlango wa kuelekea sehemu ya maliwato ya kile chumba.
Kiyoyozi makini bado kilikuwa kikiendelea kusambaza hewa safi mle ndani.
Haraka nikajisogeza pembeni na kushuka kwenye kile kitanda huku nikivinyoosha
viungo vyangu mwilini kuondoa uchovu kisha nikaelekea kwenye lile kabati la nguo
mle ndani. Nilipolifungua ndani yake nikaziona nguo nyingi za kike zilizotundikwa
kwenye sehemu maalum ya kuning’inizia nguo mle ndani na chini yake kulikuwa na
sanduku dogo la nguo lililokuwa wazi. Ndani ya sanduku lile kulikuwa na nguo nzuri
za kike za bei ya ghari zilizonyooshwa na kupangwa vizuri na sehemu ya juu ya lile
sanduku kulijaa vipodozi vya kila namna.
Nilishawishika kutaka kupekua lile sanduku na kwa kufanya vile nikaviona vibunda
vya noti nyingi vya dola za kimarekani vikiwa vimepangwa kuifunika sehemu yote ya
chini ya lile sanduku chini ya nguo. Ilikuwa fedha nyingi sana kwani pamoja na kuwa
ingelinichukua muda mrefu kukaa chini kwa utulivu na kuhesabu kiasi kile cha fedha
lakini kwa tathmini yangu ya awali ilikuwa ni vigumu kidogo kwa raia wa kawaida wa
kiafrika kumiliki kiasi kikubwa cha fedha za kigeni kama kile. Lakini vilevile lingekuwa
ni jambo la hatari kwa mtu kuweza kutembea na kiasi kingi cha pesa kama kile kwenye
sanduku badala ya kuweka benki ambapo ndiyo sehemu salama zaidi ya kutunzia
fedha
Niliendelea na upekuzi wangu kwenye lile sanduku na hapo nikakutana na kadi
nyingi za ATM za benki tofauti za kimataifa zenye majina tofauti ya kike na ya kiume
na pasi moja ya kimataifa ya kusafiria yenye picha ya yule mwenyeji wangu huku ikiwa
na jina la Chimamanda Okechukwu,mwanamke raia wa Nigeria iliyogongwa mihuri
mingi katika namna ya kunieleza kuwa mmiliki wa pasi ile ya kusafiria alikuwa ni
mtu wa safari nyingi za kimataifa nje ya taifa lake. Niliitazama pasi ile ya kusafiria
kwa makini huku hisia za kudanganywa zikianza kupenya taratibu nafsini mwangu.
Nilianza kuhisi kuwa Iko-Ojo Obaje alikuwa amenidanganya juu ya jina lake kutokana
na ile pasi ya kusafiria yenye jina tofauti na lile alilojitambulisha kwangu huku ikiwa
na picha yake na kwa kweli sikujua kwa nini alikuwa amefanya vile.Nilimaliza upekuzi
wangu pasipo kuchukua kitu chochote kutoka ndani ya lile sanduku ingawa hisia
tofauti juu ya yule mwanamke zilikuwa zimeanza kuniingia moyoni.
Mwanzoni nilidhani kuwa Iko-Ojo Obaje huwenda angekuwa ndani ya kile
chumba cha maliwato akijifanyia usafi na kuoga hata hivyo nilipousogelea ule mlango
na kuufungua sikumuona mtu yeyote mle ndani hali iliyonipelekea niamini kuwa Iko-
Ojo Obaje hakuwepo katika mazingira yam le ndani ya kile chumba. Ameenda wapi
na amewezaje kuondoka mle ndani kimyakimya pasipo mimi kushtuka huku sote
tukiwa tumelala kitanda kimoja?. Kwa nini hakutaka kuniaga?. Niliendelea kujiuliza
bila kupata majibu ingawa kwa namna moja au nyingine niliamini kuwa asingekuwa
mbali na maeneo yale kwa vile vitu vyake vyote bado vilikuwa mle ndani pamoja na
kiasi kile kikubwa cha fedha sandukuni.
Nafsi yangu ikanionya kuwa sikutakiwa kuwa na haraka badala yake nilipaswa
kuvuta subira. Hivyo taratibu nikazitupa hatua zangu hafifu kuelekea nyuma ya ule
mlango wa kile chumba mahali nguo zangu zilipokuwa zimening’inizwa. Nilipofika
nikafanya upekuzi wa haraka wa vifaa vyangu vyote muhimu vya kazi kwenye mifuko
ya nguo zile. Kitendo cha kuikuta bastola yangu ikiwa salama kwenye mfuko wa
lile koti langu la kijasusi na vifaa vyangu vyote vya kazi kikanipa matumaini kuwa
sikupaswa kuwa mashaka sana nafsini mwangu.
Nikiwa bado nimesimama pale nyuma ya mlango nikaendelea kuyatembeza
macho yangu taratibu mle ndani na kwa kufanya vile nikaiona simu ya mezani ikiwa
juu ya stuli ndefu ya mbao iliyokuwa kando ya kitanda cha mle ndani. Wazo jipya
likawa limeumbika kichwani mwangu baada ya kuwaza kuwa ule ungekuwa ndiyo
muda mzuri wa kufanya mawasiliano na Mwasu kule ofisini kwangu ili kumueleza
mambo yote yaliyotokea na kumtoa hofu juu ya kwanini hakuniona ofisini mapema
kama ilivyokuwa kawaida yangu. Hata hivyo ni kama niliyekuwa nikibahatisha tu
kwani sikuwa na hakika ya moja kwa moja kama simu ile ilikuwa na uwezo wa kutoka
nje ya lile jengo la ile Hotel Agent 11.
Hatimaye nilifanikiwa kwani baada ya miito kadhaa simu ya upande wa pili
ikapokelewa na Mwasu hata hivyo kupitia sauti yake nikagundua ni kama mtu
aliyekuwa na wasiwasi juu jambo fulani nisilolifahamu.
“Mwasu ni mimi Chaz Siga” niliwahi kujitambulisha.
“Habari za asubuhi,upo wapi Chaz?. Nilianza kupatwa na mashaka nikidhani
jambo baya limekutokea” Mwasu akaongea kwa shauku akionesha kujali.
“Nzuri tu,ondoa shaka Mwasu mimi bado niko salama ingawa changamoto za
hapa na pale hazikosekani kama unavyojua” niliongea kwa utulivu huku nikitengeneza
sauti ya kirafiki kisha nilipokohoa kidogo kuliweka koo langu sawa Mwasu akawahi
kuniuliza.
“Vipi utakuja ofisini leo?”
“Bado sina hakika,kwani vipi,kuna mtu yeyote anashida na mimi?” nikauliza.
“Wapo ila imenibidi niwatake waniachie namba zao za simu ili utakapofika
niwapigie na kuwafahamisha kuwa umerudi”
“Umefanya vyema sana Mwasu hata hivyo ningependa nikutahadharishe kuwa
kuanzia sasa kuwa makini kwani nimeanza kuhisi hatari kubwa katika kushughulika
na huu upelelezi wa Mifupa 206”
“Una maana gani?” Mwasu akauliza kwa shauku
“Kutoweka kwa Gabbi Masebo siyo tukio jepesi kama nilivyokuwa nimelichukulia
hapo awali. Nimefikia hatua ya kuhisi kuwa kuna jambo la hatari zaidi lililofichika
nyuma ya kutoweka kwake na jambo hilo huwenda lina mtazamo mkubwa wa
kimaslahi kwa serikali au viongozi wachache wa serikalini. Hali inayonipelekea nianze
kuhisi kila hatua ninayoipiga kwenda mbele ndiyo ninavyozidi kukikaribia kifo na siyo
tamati ya haraka ya mkasa huu” niliweka kituo na hapo nikasikia sauti hafifu ya mguno
wa Mwasu kutoka upande wa pili wa ile simu.
“Kama ni hivyo kwanini usiachane nao na kurudisha kiasi cha pesa ulichokichukua
kama malipo ya awali ya kazi yenyewe. Mimi nadhani ungemuita mzee James Risasi na
kumueleza bayana kuwa hutoweza tena kuendelea na kazi yake na kumrudishia pesa
yake” Mwasu akaongea kwa msisitizo.
“Hapana Mwasu siwezi kufanya hivyo”
“Kwa nini usifanye hivyo na kazi yenyewe ni ya hatari namna hiyo?”
“Hii kazi nimeshapiganayo hatua istoshe bado ninauhitaji mkubwa pesa. Nahitaji
kukulipa mshahara lakini vilevile kodi ya pango inatusubiri na matumizi mengine
madogomadogo na nikisema hii kazi imenishinda huu utakuwa ndiyo mwanzo wa
kufukuza wateja”
“Sasa pesa yenyewe itakuwa na faida gani kama utakuwa mfu?” Mwasu akauliza
kwa jazba kwa vile alikuwa akinipenda sana,kuniheshimu na kunijali vinginevyo
angeweza hata kunitukana.
“Bado sijafikia hatua hiyo Mwasu. Hebu ngoja tuone nini kitakachofuata baada
ya hapa” nikaweka kituo kisha nikaanza kumuelezea Mwasu mlolongo wa matukio
yote yaliyotokea mpaka kufikia muda ule. Hata hivyo katika maongezi yangu nilikuwa
makini kutomtaja Iko-Ojo Obaje,mwanamke wa kinaijeria ambaye alikuwa ameniacha
mle chumbani katika mazingira yasiyoelezeka. Nilipomaliza kusimulia nikamsikia
Mwasu akitua chini pumzi nyingi kama mtu aliyeanza kuingiwa na mashaka.
“Ndiyo maana nikakusisitiza kuwa uwe makini sana kuanzia sasa” nikahitimisha.
“Nimekuelewa” hatimaye Mwasu akaongea kwa sauti tulivu.
“Bado nipo mitaani naendelea na kazi hivyo kila nitakapopata muda nitakuwa
nikikufahamisha yanayoendelea. Wewe endelea kutengeneza ripoti nzuri yenye
maelezo yanayojitosheleza kuhusiana na huu mkasa wa Mifupa 206. Nitakapokuja
ofisini nitajazia vipengele vilivyosalia. Kazi njema,” niliwahi kumuaga Mwasu lakini
kabla sijamaliza akanikatisha.
“Chaz…”
“Naam! zungumza Mwasu nakusikia”
“Umepata taarifa juu ya mlipuko wa bomu uliyotokea posta?. Nasikia magaidi
wameingia jijini Dar es Salaam”
“Nani aliyekwambia?” nikamuuliza Mwasu kwa udadisi huku nikitabasamu
“Gazeti moja limeandika hivyo”
“Siyo magaidi Mwasu ni mimi” nikaongea huku nikicheka na kabla Mwasu
hajanitupia swali jingine nikawahi kukata ile simu.
Nilipogeuka nyuma Iko-Ojo Obaje alikuwa nyuma yangu kiasi cha umbali wa
hatua moja huku tabasamu jepesi likiwa limejivinjari usoni mwake. Moyo wangu
ukalipuka na kupiga kite kwa nguvu huku kijasho chepesi kikinitoka maungoni
mwangu. Nikamtazama Iko-Ojo Obaje kwa utulivu huku usoni nikilazimisha
tabasamu ingawaje sikuwa nimeona kitu chochote cha kunifanya nitabasamu mbele
yake. Hata hivyo taratibu nikafanikiwa kuumeza mshtuko ule na kuvaa tabasamu la
asili.
Iko-Ojo Obaje alikuwa amevaa suruali nyepesi nyeusi ya jeans iliyolichora
vyema umbo lake maridhawa lenye uwezo wa kuziteka hisia za mwanaume yeyote.
Miguuni alikuwa amevaa viatu virefu vyekundu vya mikanda. Kichwani nywele zake
za rasta alikuwa amezikusanya na kuzifunga kwa nyuma kama mkia wa farasi na
kumpelekea azidi kupendeza. Machoni alikuwa amevaa miwani myeusi ya jua huku
kingo za mdomo wake zikiwa zimekolea vizuri rangi nzuri nyekundu ya mdomoni.
Shingoni alikuwa amening’iniza mkufu mzuri wa Almasi uliyoizunguka shingo yake
na kupotelea katikati ya matiti yake yaliyotuna vizuri na kuhifadhiwa ndani ya sidiria
yake nyeupe na blauzi ya rangi ya damu ya mzee. Mkononi alikuwa ameshika mfuko
mzuri wa nailoni uliotuna.
“Ulikuwa wapi mpenzi?” nikamuuliza kwa lugha ya kiingereza huku nikiwa na
shauku ya kutaka kufahamu.
“Nilishtuka mapema sana kutoka usingizi nikaona nishuke chini ya hili jengo
nikaogelee kwenye bwawa. Niliporudi na kukuta bado hujaamka sikutaka kukusumbua
nikawa nimepata wazo la kutoka na kwenda kukununulia nguo nyingine za kubadilisha
katika duka moja lililopo katikati ya jiji” Iko-Ojo Obaje akaongea kwa utulivu huku
akiutupa ule mfuko juu ya kile kitanda na kuvua miwani yake kisha taratibu akizitupa
hatua zake na kwenda kuketi kwenye kochi moja la sofa lililokuwa mle ndani. Maelezo
ya Iko-Ojo Obaje yakawa yameniacha njia panda. Kwanza lilikuwa ni jambo gumu
sana nilale na mtu halafu ashtuke kutoka usingizini na kutoka kitandani pasipo
kumsikia lakini vilevile nilikuwa nimeshangazwa sana na kitendo cha Iko-Ojo Obaje
kuweza kufanya mambo yote yale aliyonisimulia pasipo mimi kushtuka usingizini mle
ndani.
“Nashukuru sana” hatimaye nikamwambia huku nikitabasamu kisha nikaitupia
macho saa yangu ya mkononi. Ilikuwa ikielekea kutimia saa nne asubuhi hali
iliyonipelekea nishtuke na kujilaumu kwa kulala muda mrefu kiasi kile.
“Ulikuwa ukiongea na nani kwenye simu?” Iko-Ojo Obaje akaniuliza huku akitoa
sigara kutoka kwenye pakiti mfukoni na kuibana mdomoni kisha kwa msaada wa
kiberiti cha gesi kutoka mfukoni mwake akajiwashia na kuanza kuvuta huku mguu
wake mmoja akiupandisha juu ya mwingine.
“Mfanyakazi mwenzangu kuna mambo machache ya kiofisi tulikuwa tukiwekana
sawa” niliongea kwa utulivu huku nikirudi pale kitandani na kujilaza.
“Huyo mfanyakazi mwenzako anafahamu kuwa wewe upo hapa?” swali la Iko-
Ojo Obaje likanipelekea nigeuke na kumtazama kwa udadisi hata hivyo sikuona
tashwishwi yoyote usoni mwake.
“Hapana” nikamjibu kivivuvivu.
“Huendi kazini leo?”
“Nitaenda hata hivyo nimechelewa sana” niliongea huku nikiamka kivivuvivu pale
kitandani na kuketi tena huku nikimzama Iko-Ojo Obaje na macho yetu yalipokutana
kila mmoja akaangua tabasamu.
“Vipi uchovu?” hatimaye nikamuuliza.
“Umepungua” Iko-Ojo Obaje akaongea huku akiangua kicheko hafifu baada ya
kuitoa sigara yake mdomoni kisha akaendelea
“Wewe ni mwanaume uliyenifanya niukumbuke ujana wangu kwa usiku mmoja
tu” akaongea huku akinikata jicho la mahaba na kutabasamu.
“Unaonekana mwanamke wa miaka thelathini na kitu lakini kitandani hautofautiani
na binti wa sekondari” nilichombeza utani na kupelekea wote tuangue kicheko
mle ndani. Hatimaye nikasimama na kuelekea bafuni kuondoa uchovu. Nilikuwa
nimekumbuka kazi iliyokuwa ikinikabili mbele yangu hivyo sikutaka kuendelea
kupoteza muda zaidi mle ndani. Iko-Ojo Obaje akanisindikiza kwa macho yake
nyuma yangu hadi pale nilipopotelea kwenye kile chumba cha bafu la mle ndani na
kufunga mlango nyuma yangu.
Muda mfupi baadaye nilitoka ndani ya kile chumba cha bafu nikiwa mwepesi
na mbali na uchovu na hapo nikamkuta Iko-Ojo Obaje akiwa tayari amekwisha
agiza kifungua kinywa chenye taftahi za kila aina. Mle ndani pale kitandani nilikuta
Iko-Ojo Obaje akiwa ameshazitoa zile nguo kwenye ule mfuko na kuzitandaza
pale kitandani nami nikajiridhisha kuwa alikuwa amefanya uchaguzi mzuri wenye
kuzingatia vigezo vyangu. Alikuwa ameninunulia suruali nyeusi ya kadeti,boksa ya
rangi ya bluu bahari,bukta safi ya rangi nyeupe,singlet nyeupe,fulana moja ya kijivu
yenye mstari mweusi kifuani na kofia nyeusi ambapo nilipomaliza kuvaa viliubadili
kabisa muonekano wangu na kunifanya nipendeze na hapo nikageuka kumshukuru
Iko-Ojo Obaje ambaye alikuwa akinitazama kwa makini pale kwenye kochi alipoketi.
Nilipomaliza kujiandaa nikasogea kwenye ile meza na kuketi tukipata kifungua kinywa
kile kwa pamoja. Asubuhi hii mbele yangu nilimuona Iko-Ojo Obaje katika uzuri
wa hali ya juu. Macho yake yaliponitazama yakapeleka hisia kali za mapenzi moyoni
mwangu na kunipelekea nijisifu moyoni mwangu kwa kustarehe na mwanamke mzuri
kama yule. Ingawa nilikuwa sijaamua kabisa kuwekeza kwenye masuala ya mahusiano
ya mapenzi lakini sasa mbele ya Iko-Ojo Obaje mpango huo taratibu ulikuwa
umeanza kuumbika kichwani mwangu. Iko-Ojo Obaje alikuwa amefanikiwa kuuteka
moyo wangu,mwanamke mwenye sifa zote za uzuri ambaye ingenichukuwa miaka
mingi sana kusahau aliyonifanyia kwenye kitanda cha mle ndani kwa muda wa usiku
mmoja tu tuliyokuwa pamoja.
Wakati nikiendelea kupata kile kifungua kinywa nikajikuta nikimtazama Iko-Ojo
Obaje kwa udadisi mbele yangu. Kwa namna moja au nyingine sikuwa nimemuelewa
vizuri mwanamke yule kuwa alikuwa ni mtu wa namna gani hasa pale nilipokumbuka
kiasi kingi cha zile pesa za kigeni,dola za kimarekani kilichokuwa chini ya nguo
kwenye lile sanduku mle ndani kabatini pamoja na zile kadi nyingi za ATM za benki
za kimataifa. Kisha nikajikuta nikiikumbuka ile pasi yake ya kusafiria yenye picha yake
na jina la Chimamanda Okechukwu. Ingawa Iko-Ojo Obaje hakuwa ameniambia
kiundani zaidi juu ya masuala yake lakini kwa tafsiri ya haraka nilianza kumfananisha
na mfanyabiashara mkubwa ingawa bado sikuweza kufahamu ni biasha gani ambayo
angekuwa akiifanya. Labda hakutaka kuniweka wazi jina lake kama walivyo wanawake
wengi wa zama hata hivyo nikajikuta nikijiuliza ni kwanini alikuwa na kadi nyingi za
ATM za benki nyingi za kimataifa tena zenye majina tofauti kiasi kile.
Hatimaye nilimaliza kupata kifungua kinywa kile na kumshukuru Iko-Ojo Obaje
kwa ukarimu wake kisha nikasimama na kuelekea dirishani ambapo nilisogeza pazia
pembeni na kutazama mandhari ya chini ya hoteli ile. Nikiwa pale dirishani mawazo
mengi yakawa yakipita kichwani mwangu nikifikiria juu ya kazi iliyokuwa ikinikabili
mbele yangu. Sikufahamu kuwa mara baada ya kutoka pale nilipaswa kuelekea wapi
na kufanya nini hata hivyo niliamini kuwa kuendelea kukaa mle ndani isingekuwa
suluhisho la kupata majibu ya maswali yangu. Nilihitaji kupiga hatua nyingine zaidi
katika harakati zangu.
Wingu zito la mvua lilikuwa limeanza kutanda angani na hivyo kuipelekea miale
ya jua lile la asubuhi kufifia hali iliyonipelekea nilikumbuka lile koti langu nyuma ya
mlango wa kile chumba kuwa lingeweza kunisaidia kufanya mizunguko yangu mitaani
bila kulowana endapo mvua ile ingeanza kunyesha. Hatimaye nikaliacha lile dirisha
na kufunga pazia kisha nikageuka na kumtazama Iko-Ojo Obaje pale kwenye kochi
alipoketi.
“Ni lini umepanga kuondoka hapa Dar es Salaam?” nikamuuliza kwa utulivu huku
nikimtazama kwa sura ya kirafiki.
“Viza yangu inaniruhusu kukaa hapa nchini kwa muda wa mwezi mmoja hata
hivyo kuwenda nikaondoka mapema zaidi kutegemeana na nitakavyoamua” Iko-Ojo
Obaje akanijibu kwa utulivu baada ya kutoa sigara mdomoni na kuupuliza moshi
pembeni huku taratibu akiutikisa mguu wake mmoja kwenye lile kochi.
“Nahitaji kuelekea kazini sasa”nikamwambia Iko-Ojo Obaje huku nikiitazama saa
yangu ya mkononi kisha nikayapeleka tena macho yangu kumtazama.
“Usiku wa leo tutaonana?” Iko-Ojo Obaje akaniuliza huku usoni akiumba
tabasamu hafifu
“Nipo tayari kuja tena kama utanikaribisha” nikaongea huku nikitabasamu.
“Nitapenda kukuona tena kama utapata nafasi” jibu la Iko-Ojo Obaje likanipelekea
niangue kicheko hafifu kwani ni dhahiri kuwa nilikuwa nipo tayari kujifungia mle
chumbani na mrembo yule hadi pale ambapo angenichoka lakini kizingiti kikubwa
sasa kilikuwa ni juu ya majukumu yaliyokuwa mbele yangu.
“Nashukuru sana” hatimaye nikamwambia kisha nikasogea kwenye ule mlango
na kulichukua lile koti langu na kulivaa halafu nikamuaga Iko-Ojo Obaje na kufungua
mlango nikitoka nje.
_____
NILIKUWA SIJAFIKA MBALI BAADA YA KUSHUKA kwenye teksi eneo
la posta nikitoka kule Hotel Agent 11 wakati simu yangu ilipoanza kuita mfukoni.
Haraka nikaingiza mkono mfukoni na kuichukua hata hivyo kabla sijaipokea simu
ile nikageuka haraka na kuyatembeza macho yangu eneo lile kuzikagua sura za watu.
Sikuona sura yoyote ya kuitilia mashaka hivyo haraka nikalitazama jina la mpigaji na
kuiweka simu sikioni kabla ya kubofya kitufe cha kupokelea. Mwasu alikuwa akinipigia
na tukio lile lilikuwa limenipelekea niingiwe na wasiwasi kwani muda mfupi tu uliyopita
nilikuwa nimetoka kuongea naye kwa simu. Sauti ya Mwasu ilikawia kunifikia sikioni
ingawaje nilipotega vizuri sikio langu kusikiliza kwenye ile simu nikagundua kuwa
Mwasu alikuwa akitembea nusu ya kukimbia huku akihema ovyo.
“Mwasu kuna nini?”
“Chaz…”
“Nakusikia Mwasu zungumza kuna nini?” nikauliza kwa mashaka.
“Upo wapi?” Mwasu akauliza huku akihema ovyo na kupitia kitetemeshi cha sauti
yake nikahisi jambo la hatari.
“Niko maeneo ya posta nje ya jengo la Benjamin William Mkapa Tower. Niambie
Mwasu kuna nini?”
“Kuna wanaume watatu wako nyuma yangu wananifuatilia. Chaz tafadhali nahitaji
msaada wako” Mwasu akaongea kwa hofu.
“Wanaume watatu?,wameanza kukufuatilia kutoka wapi na wewe upo wapi sasa
hivi?” nikamuuliza Mwasu kwa udadisi.
“Walikuja ofisini kukuulizia walipoona haupo wakataka kunikamata nikafanikiwa
kuwatoroka hata hivyo wamenishtukia na sasa wapo nyuma yangu wananifuata.
Tafadhali nahitaji msaada wako Chaz hawa watu wanaonekana kuwa si wema”
Mwasu akaendelea kunitahadharisha huku akitembea kwa kasi.
“Niambie tafadhali upo wapi?” nikamuuliza Mwasu kwa papara hata hivyo Mwasu
hakunijibu badala yake nikamsikia akianza kutimua mbio.
“Mwasu niambie tafadhali upo wapi mbona huongei?” nikamuuliza huku
nimeshikwa na taharuki. Nikiwa bado nimeishikilia simu yangu sikioni mara sauti ya
Mwasu ikarudi tena hewani.
“Nahitani msaada wako wa haraka Chaz hawa watu wanakaribia kunifikia na
wameshika bastola mikononi mwao” Mwasu akalalamika kwa hofu.
“Okay!Mwasu niambie mahali ulipo nitafika sasa hivi” nikaongea kwa msisitizo.
“Nipo kwenye barabara ya mtaa wa Jamhuri nakaribia kwenye mashine za ATM
za benki ya NMB eneo la posta” Mwasu akaongea kwa msisitizo huku sauti yake
ikitawaliwa na hofu. Maelezo ya Mwasu yakaipelekea akili yangu kuanza kufanya
kazi haraka. Kutoka pale nilipokuwa nilitambua kuwa sikuwa mbali sana na sehemu
alipokuwa Mwasu hivyo bado nilikuwa kwenye nafasi nzuri ya kuweza kumuokoa
kutoka kwa watu wale hatari. Bila kupoteza muda nikaanza kutimua mbio nikishika
ule uelekeo wa kwenda kukutana na ile barabara ya Jamhuri upande wa kulia.
“Nakuja Mwasu nipo hapa jengo la Benjamin William Mkapa Tower ondoa shaka
nafika hapo sasa hivi” nikamtoa hofu Mwasu na kuanza kutimua mbio
“Fanya haraka Chaz hawa watu ni hatari” Mwasu akasisitiza huku akiendelea
kutimua mbio
“Umebeba kitu chochote?” nikamuuliza
“Nimebeba mkoba wangu na ndani una External hard disc yenye mafaili ya kazi
zote za ofisini” Mwasu akanitanabaisha.
“Hakikisha kwa namna yoyote ile hao watu hawafanikiwi kuupata huo mkoba”
nikamsisitiza Mwasu huku nikitimua mbio kuelekea kule alipokuwa. Baadhi ya
watu waliopishana na mimi wakati nikitimua mbio kuelekea kule alipokuwa Mwasu
waligeuka na kunishangaa hata hivyo sikuwatilia maanani badala yake nikaendelea
kuchanganya miguu nikitimua mbio huku nikitazama huku na kule mbele yangu.
Nilipofika kwenye ile kona ya kuingia barabara ya mtaa wa Jamhuri nikapunguza
mwendo na kusita kidogo baada ya kuona kundi kubwa la watu wakitimua mbio
kutoka kwenye ile barabara. Haraka nikajikuta nikiingiza mkono kwenye koti langu na
kuikamata vyema bastola yangu hata hivyo nikajikuta nikiachana na mpango ule baada
ya kuhisi kuwa sikuwa na ushahidi wa kutosha juu ya nini kilichokuwa kikiendelea
eneo lile. Sikutaka kupoteza muda hivyo bila kusubiri nikaongeza tena mwendo
nikilipangua lile kundi la watu mbele yangu na wakati nikifanya vile nikasikia baadhi
ya watu wakisema kule nyuma kulikuwa na majambazi watatu waliokuwa wakitaka
kuupora mkoba wa dada mmoja wenye pesa.Tathmini yangu ya haraka ikaniambia
kuwa watu hao hawakuwa majambazi ila wangekuwa ndiyo wale watu waliokuwa
wakimfukuza Mwasu.
Mara tu nilipoingia kwenye ila barabara ya mtaa wa Jamhuri nikamuona mwanamke
mmoja aliyevaa blauzi nyeupe na suruali ya bluu ya jeans akitimua mbio usawa wa
zile mashine za ATM za benki ya NMB. Alikuwa ni Mwasu nilipomchunguza vizuri
nikamtambua na mkononi alikuwa amebeba mkoba wake wa ngozi. Mwasu hakuwa
na viatu vyake virefu vya mikanda miguuni kama nilivyozoea kumuona badala
yake alikuwa akitimua mbio pekupeku hali iliyowapelekea watu waliokuwa eneo
lile kumshangaa kwa kitendo kile. Nilipoendelea kuchunguza nyuma yake kiasi cha
umbali usiopungua hatua thelathini nikawaona wanaume watatu waliovaa suti nadhifu
nyeusi na miwani nyeusi machoni mwao wakitimua mbio kumfukuza Mwasu huku
wameshika bastola zao mikononi.
Kwa mwendo ule wa kasi ya wale watu nilifahamu fika kuwa Mwasu asingefika
mbali kabla ya wale watu hawajamfikia na kumkamata ingawa nilikuwa na hakika
kuwa hadi kufikia pale Mwasu alikuwa amejitahidi sana kukimbia katika kuhakikisha
kuwa wale watu hawamkamati. Sikutaka kusubiri hadi nione wale watu ambavyo
wangemfikia Mwasu na kumkamata hivyo haraka nikauingiza mkono wangu kwenye
mfuko wa koti na kuichomoa bastola yangu mafichoni. Muda mfupi uliofuata
nilikuwa nikikatisha kwenye ile barabara ya Jamhuri na kuelekea ule upande wa pili
wa ile barabara kumuokoa Mwasu. Hata hivyo sikufanikiwa kwani magari mengi
yaliyokuwa yakikatisha mbele yangu yakanizuia kama siyo kunichelewesha na wakati
nikisubiri yale magari yapite mbele yangu ili niweze kuvuka na kwenda upande wa pili
wa ile barabara jambo moja la kushangaza likatokea.
Ghafla nikaliona gari moja jeusi aina ya Toyota Noah likichomoza kwa kasi kutokea
barabara ya Morogoro. Haraka nikafahamu ni maana ya tukio lile hivyo nikapiga
kelele kumuita Mwasu upande wa pili wa ile barabara. Mwasu akawahi kunisikia na
kugeuka upande ule kunitazama hata hivyo hakupunguza mwendo kwani wale watu
walikuwa mbioni kumfikia. Nikiwa nimeanza kuhisi nini ambacho kingefuatia baada
ya pale sikutaka kuendelea kusubiri yale magari mbele yangu yamalize kupita ndiyo
nivuke ile barabara. Hivyo nikaongeza kasi na kujitupa kimgongomgongo juu ya
boneti ya Toyota Cresta iliyokuwa ikikatisha mbele yangu. Dereva wa lile gari kuona vile
akawahi kushika breki hata hivyo wakati akisimama mimi tayari nilikuwa nimeshatua
chini upande wa pili wa ile barabara alipokuwa Mwasu na wale watu waliokuwa
wakimkimbiza. Wale watu ni kama walikuwa hawajaniona au huwenda walikuwa
wamenipuuza badala yake waliendelea kutimua mbio na bastola zao mikononi huku
makoti yao ya suti yakipepea kama vishada kumfukuza Mwasu.
Mwasu alikuwa ameniona wakati nilipokuwa kwenye jitihada za kuvuka
ile barabara hivyo nilikuwa na hakika kuwa pia aliamini kuwa wakati ule tayari
ningekuwa nimeshavuka ile barabara na kuingia ule upande aliokuwa yeye na wale
watu wanaomfukuza hivyo akageuka nyuma na kunitazama. Macho yetu yalipokutana
nikaiona hofu iliyotanda usoni mwake hata hivyo Mwasu hakusimama na wakati
akiifikia ile barabara ya Morogoro ile gari Toyota Noah nyeusi nayo tayari ilikuwa usawa
wake nikakazana kutimua mbio nikikata upepo kuwakaribia wale watu kwa nyuma.
Hata hivyo kabla sijawafikia wale watu ghafla nikauona mlango wa ubavuni wa
ile Toyota Noah nyeusi ukifunguliwa kisha wakashuka watu wawili kwa haraka sana na
kumkamata Mwasu wakimbeba mzegamzega na kumtupia ndani ya lile gari. Haraka
nikapaza sauti kumuita Mwasu,Mwasu akageuka kwa taabu kunitazama katika uso wa
kukata tamaa huku amebebwa juu juu hadi alipotupiwa ndani ya lile gari.
Matumaini ya kumuokoa yakiwa yamepungua sikutaka kuendelea kusubiri zaidi
hivyo nikaikamata vyema bastola yangu mkononi. Niliwaona wale watu watatu
waliokuwa wakimfukuza Mwasu wakizidisha mbio kuukaribia mlango wa ile gari
Toyota Noah nyeusi na hapo nikajua kuwa wale watu waliokuwa wakimkimbiza
Mwasu walikuwa shirika moja na watu waliokuwa ndani ya ile gari. Nikiwa naikaribia
ile gari nikawaona wale watu nao wakiingia kwenye ile Toyota Noah nyeusi. Kuona vile
nikautupa mkono wangu wa shabaha na kuvuta kilimi cha bastola. Majibu yalikuwa
ya hakika na yaliyonifurahisha. Risasi zangu mbili nilizozifyatua zikampata vizuri yule
mtu wa nyuma kabisa kati ya wale watu watatu waliokuwa wakimfukuza Mwasu.
Risasi moja ikapenya kwenye mfupa wa paja la mguu wake wa kushoto na nyingine
ikampata begani mwake. Yule mtu akapiga yowe kali la hofu na kupiga mwereka
wa nguvu akianguka chini huku bastola yake ikimponyoka mkononi. Wale wenzake
kuona vile wakasita kidogo lakini kitendo cha kugeuka nyuma na kuniona wakawahi
kujirusha ndani ya ile Toyota Noah nyeusi na hapo ule mlango ukafungwa kwa pupa
huku ile gari ikiondoka kwa kasi eneo lile.
Sikukata tamaa nikampita yule mtu niliyemchapa risasi na kuzidi kutimua
mbio nikilifukuza lile gari kwa nyuma na wakati nikifanya vile nikawa nikiendelea
kumuita Mwasu kama mwehu. Watu waliokuwa wakifuatilia lile tukio wakasimama
na kunishangaa hata hivyo sikuwatilia maanani badala yake nikaendelea kutimua
mbio nikilifukuza lile gari. Lile gari likaendelea na safari kwa mwendo wa kasi na
lilipomaliza kuuvuka ule mzunguko wa barabara wa Askari Monument nikaona kitu
fulani kikirushwa kutoka kwenye dirisha moja la upande wa kushoto wa lile gari
na kuangukia kando ya ile barabara.Mara nikaliona lile gari likipunguza mwendo
lakini ghafla likaongeza kasi tena pale nilipoanza kulinyooshea bastola. Hata hivyo
nikaachana na mpango wa kulifyatulia risasi kwani lile gari tayari lilikuwa limeingia
kwenye eneo la msongamano ingawa dereva wa lile gari alikuwa makini na alipopata
upenyo mdogo akautumia vizuri kuniacha solemba.
Muda mfupi uliofuata nikavuka ile barabara nikienda kuokota kile kitu
kilichotupwa dirishani kutoka katika lile gari nililokuwa nikilifukuza ambalo sasa
lilikuwa limefanikiwa kunitoroka. Nilipofika lile eneo nikauona ule mkoba wa ngozi
wa Mwasu na hapo nikapata matumaini kidogo. Haraka nikauokota ule mkoba na
nilipolitazama lile gari nikaliona kuwa tayari lilikuwa limeshapita eneo la New Afrika
Hotel na lilipofika mbele likaingia upande wa kushoto kuifuata ile barabara ya Kivukoni
na baada ya muda mfupi lile gari likawa limepotea kabisa machoni mwangu. Mwasu
alikuwa ametekwa.
Niliendelea kusimama lile eneo huku mikono yangu nimejishika kiunoni katika
hali ya kukata tamaa na mawazo mengi yakipita kichwani mwangu. Watu wakawa
wakinishanga hata hivyo sikujishughulisha nao. Nilitamani kukodi bodaboda na
kuanza kulifukuza lile gari hata hivyo wazo hilo nikaliweka kando kwani eneo lile
halikuwa na huduma ya usafiri wa bodaboda kutokana na sheria za jiji la Dar es
Salaam kukataza usafiri wa bodaboda maeneo ya mijini katika namna ya kupunguza
msongamano barabarani. Labda usafiri wa teksi ungeweza kunisaidia lakini nilijua
kuwa kwa muda ule tayari nilikuwa nimechelewa kwani kutoka pale nilipokuwa
hadi kwenye eneo la maegesho ya teksi kulikuwa na umbali kiasi kwamba hadi pale
ambapo ningefanikiwa kupata usafiri lile gari lingekuwa tayari limekwisha fika mbali
hivyo nikaachana na mpango ule.
Watu walikuwa wameanza kukusanyika wakinishangaa na kwa kweli sikuipenda
kabisa hali ile hivyo haraka nikairudisha bastola yangu ndani ya koti na kuanza kurudi
haraka kule nilipotoka. Nilimkuta yule mtu niliyempiga risasi akiwa bado amelala pale
chini huku akigugumia kwa maumivu makali ya zile risasi sambamba na damu nyingi
iliyokuwa ikiendelea kutoka kwenye yale majeraha. Hata hivyo wakati huu yule mtu
alikuwa amezungukwa na kundi kubwa la mashuhuda ambao mara tu waliponiona
wakaanza kutawanyika. Sikutaka kupoteza muda eneo lile hivyo nilipomfikia yule
mtu nikaiokota ile bastola yake kisha nikamnyanyua yule mtu na kumtupia begani
kwangu halafu nikielekea kwenye maegesho ya teksi yaliyokuwa jirani na eneo lile.
Muda mfupi uliyofuata mimi na mateka wangu tulikuwa kwenye teksi tukielekea eneo
la Magomeni sehemu kulipokuwa na hospitali moja ya kichochoroni yenye huduma
nzuri ambapo niliamini kuwa yule mateka wangu angepatiwa tiba ya kuaminika kabla
ya mahojiano ya kina kufuatia.
 
CHUMBA KILIKUWA KIKUBWA chenye umbo mraba la kuta safi
zilizonyooka vizuri. Kulikuwa na mlango mmoja tu wa chuma mkubwa na
mweusi uliokuwa kwenye kona moja ya kile chumba upande wa kushoto na
mlango ule ulikuwa umefungwa kikamilifu kwa nje. Ukutani hapakuwa na dirisha
hata moja na hivyo kupelekea giza zito kutanda mle ndani. Sakafu ya chumba kile
ilitengenezwa kwa tarazo nadhifu yenye nakshi nzuri za kila namna. Joto la chumba
lilikuwa kali ingawa hewa ya mle ndani ingeweza kumruhusu binadamu yeyote kuishi.
Katikati ya chumba kulikuwa na meza ya mbao ndefu na pana kiasi yenye umbo
mstatili chini ya balbu ya umeme yenye mwanga mkali iliyokuwa imeshikiliwa na waya
mrefu wa umeme kutoka juu ya dari ya chumba kile. Upande wa pili wa meza ile
kulikuwa na viti vitatu vya ofisini vyenye foronya laini vyeusi. Upande mwingine wa
meza ile kulikuwa na kiti kimoja cha chuma chenye mikanda maalum na nikatika kiti
kile ndipo Mwasu alipokuwa ameketi na zaidi ya pale hapakuwa na mtu mwingine mle
ndani isipokuwa ukimya wa kutisha.
Fahamu zilikuwa zimeanza kumrudia Mwasu taratibu huku kumbukumbu sahihi
zikianza kujitengeneza upya kichwani mwake. Taratibu akayafumbua macho yake kwa
shida kabla ya kuanza kuyatembeza mle ndani. Hata hivyo ubongo wake ukakawia
kumletea tafsiri ya haraka juu ya taswira zilizokuwa zikijengeka machoni mwake na
badala yake akajikuta akipambana na maumivu makali yaliyofufuka upya kutoka
sehemu ya nyuma ya kichwa chake na kusambaa mwili mzima. Kabla ya kuanza
kujiuliza pale ni wapi taratibu akajikuta akianza kukumbuka mambo yaliyomtokea
huko nyuma.
Akiwa bado ameketi kwenye kile kiti Mwasu akajikuta akiwakumbuka wanaume
watatu waliovaa suti nyeusi nadhifu wakati walipofika ofisini kwake na kumuulizia
Chaz Siga huku wakijitia kuwa walikuwa wakihitaji msaada wake wa haraka.
Akaendelea kukumbuka namna alivyowakaribisha vizuri wanaume wale ofisini kabla
ya kuanza kuingiwa na mashaka dhidi yao baada ya kumuona mmoja miongoni mwao
akiwa ameichomeka bastola yake kiunoni kwa hila huku amening’iniza pingu pindi
alipolisogeza koti la suti yake kwa bahati mbaya wakati alipokuwa akijiandaa kuketi
katika viti vya wageni vilivyokuwa mle ndani ofisini.
Mwasu akaendelea kukumbuka namna alivyowahadaa watu wale kuwa ile
haikuwa ofisi ya Chaz Siga ama mtu waliyekuwa wakihitaji kumuona kauli ambayo
wale watu hawakuwa tayari kuiamini hata kidogo kiasi cha kutoa vitambulisho
vyao vinavyowatanabaisha kuwa wao ni wanausalama na kumwonesha huku
wakimtahadharisha kuwa wangemuweka chini ya ulinzi endapo angekataa kuwapa
ushirikiano wa kutosha. Mwasu akaendelea kukumbuka namna alivyojitia kukubaliana
na hoja ya wale watu huku akijidai kuingia kwenye ofisi ya Chaz Siga na kumpigia
simu Chaz Siga ili kumfahamisha kuwa kulikuwa na watu waliokuwa wakimsubiri
pale ofisini. Mwasu akaendelea kukumbuka namna alivyoutumia mlango wa dharura
uliokuwa kwenye ofisi ya Chaz Siga kuwatoroka wale watu huku wakiwa bado
wameketi kwenye viti vya wageni vya ile ofisi wakimsubiri.
Mwasu bado akaendelea kukumbuka namna alivyogeuka nyuma wakati alipokuwa
akitembea kwenye barabara ya tatu kutoka kule ilipokuwa ile ofisi na kushtukia kuwa
wale watu aliowatoroka kule ofisini walikuwa nyuma yake hatua chache karibu
kumfikia hali iliyompelekea aanze kutimua mbio akiwakimbia wale watu kabla ya
kumpigia simu Chaz Siga na kumfahamisha juu ya tukio lile. Kumbukumbu kamili
zikiwa mbioni kujengeka kichwani mwake Mwasu akajikuta akikumbuka namna
alivyoitwa na Chaz Siga katika yale makutano ya barabara ya Jamhuri na barabara ya
Morogoro muda mfupi kabla hajatekwa na wale watu waliokuwa ndani ya gari nyeusi
aina ya Toyota Noah iliyokuja na kusimama ghafla kando yake wakati alipokuwa
akiendelea kutimua mbio kuwakimbia wale watu waliokuwa wakimfukuza nyuma
yake. Kufikia pale akajikuta akikumbuka namna alivyomuona Chaz Siga akitimua
mbio kulifukuza lile gari lililotumika kumteka muda mfupi baada ya milio miwili ya
risasi kusikika nyuma yake kabla ya wale watu wawili miongoni mwa wale watu watatu
waliokuwa wakimfukuza nao kuingia kwenye lile gari na kisha lile gari kuondoka kwa
kasi eneo lile.
Kumbukumbu zile zikapelekea tabasamu jepesi kuanza kuchomoza usoni kwa
Mwasu pale alipokumbuka namna alivyofanikiwa kuurusha mkoba wake wa ngozi
kupitia kwenye dirisha moja la lile gari wakati alipogeuka nyuma na kumuona Chaz
Siga akitimua mbio kulifukuza lile gari nyuma yao. Ni katika ule mkoba wake wa
ngozi ndiyo kulipokuwa na taarifa zote muhimu za ofisini ikiwemo ile External hard
disc yenye mafaili chungu mzima ndani yake likiwemo faili la upelelezi wa mkasa wa
Mifupa 206 ambalo upelelezi wake ulikuwa bado ukiendelea kufanyika pamoja na simu
yake ya mkononi. Hivyo alikuwa na hakika kuwa hadi kufikia wakati ule wale watekaji
walikuwa hawajafanikiwa kupata kitu chochote cha maana kutoka kwake na hivyo
kujikuta akipata faraja.
Mwasu akaendelea kukumbuka namna alivyopigwa na kitu kizito nyuma ya kichwa
chake muda mfupi mara baada ya lile gari jeusi Toyota Noah liliyotumika kumteka
lilipoingia kwenye barabara ya Kivukoni na kuanza kutimua mbio. Kufikia pale
hakufahamu tena kilichoendelea hali iliyompelekea aamini kuwa alikuwa amepoteza
fahamu baada ya shambulio lile la nyuma ya kichwa chake.
Ndani ya chumba kile kikubwa Mwasu akajikuta akiyatembeza macho yake
taratibu mle ndani huku mawazo mengi yakipita kichwani mwake. Sasa hakuwa na
shaka yoyote kuwa watekaji wale ndiyo waliokuwa wamemfikisha kwenye chumba
kile huku akiwa bado amepotewa na fahamu. Alipoanza kujichunguza akagundua
kuwa mikono na miguu yake ilikuwa imefungwa kwa mikanda maalum ya kile kiti cha
chuma alichoketi hata hivyo hali ile haikumshtua kwani alifahamu haraka ni maana
ya tukio lile.
Hivyo akaendelea kuyachunguza mandhari yale huku akili yake ikiendelea
kusumbuka katika kutaka kufahamu pale alikuwa wapi ingawaje hisia zake zilimueleza
kuwa alikuwa kwenye chumba fulani cha siri katika jengo moja la ghorofa lililoko
kando kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Giza lililokuwa mle ndani likampelekea ashindwe
kufahamu muda ule ulikuwa ni saa ngapi na kama mchana au usiku huku akiwaza nini
ambacho kingefuatia baada ya pale.
Kelele za ghafla za kufunguliwa kwa mlango wa kile chumba zikayakatisha mawazo
ya Mwasu na hapo akageuka nyuma na kuutazama ule mlango kama bomu lililokuwa
limebakisha sekunde chache kabla ya kulipuka. Muda mfupi uliofuata ule mlango
ukafunguliwa kisha wakaingia wanaume wanne,watatu miongoni mwao wakiwa ni
wenye umri wa kati ya miaka arobaini na tano hadi hamsini na mbili. Mmoja alikuwa
kijana wa miaka thelathini na kitu huku wote wakiwa wamevaa suti nyeusi nadhifu
zilizowakaa vyema katika miili yao mikubwa na mirefu yenye afya.
Mara tu wale watu walipoingia mle ndani yule kijana akaufunga ule mlango nyuma
yao wakati wale wanaume wengine watatu walipokuwa wakielekea kwenye vile viti
vitatu vilivyokuwa upande wa pili wa ile meza katika nyuso zisizokuwa na chembe
ya mzaha. Walipofika wakavuta vile viti nyuma na kuketi huku yule kijana akienda
na kusimama kwa nyuma. Kitambo kifupi cha ukimya kikafuata mle ndani huku kila
mmoja akionekana kumtegea mwenzake kuongea. Mwasu alipoyatembeza macho
yake kuwatazama wale watu akagundua kuwa wote sura zao zilikuwa ngeni kabisa
machoni mwake isipokuwa yule kijana aliyesimama mwisho wa ile meza ambaye
haraka alimkumbuka kuwa alikuwa miongoni mwa wale watu watatu waliofika kule
ofisini kumuulizia Chaz Siga.
Mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa M.D. Kunzugala sasa alikuwa
ameketi katikati ya kamishina wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini Evans Mchafu
upande wa kulia na mkuu wa intelijensia ya usalama wa taifa Sulle Kiganja upande wa
kushoto. Taarifa za kukamatwa kwa Mwasu kama mmoja wa washukiwa waliokuwa
wakitafutwa kuhusiana na mauaji ya wanausalama wake zilikuwa zimeifikia ofisi yake
mapema sana na hivyo kurejesha tumaini kubwa la kuendelea kutetea wadhifa wake.
Na sasa M.D Kunzugala na wanausalama wake waandamizi walikuwa wameingia
kwenye chumba kile cha siri kufanya mahojiano na Mwasu kufuatia matukio ya mauaji
ya maafisa usalama yaliyokuwa yakiendelea kutokea jijini Dar es Salaam.
Ukimya kidogo ulipokuwa mbioni kutawala mle ndani M.D.Kunzugala akageuka
na kuwatazama wale maafisa usalama wenzake aliyoongozana nao mle ndani kisha
akakohoa kidogo na kuyapeleka macho yake kwa Mwasu kabla ya kuvunja ukimya.
“Binti,tunachohitaji sasa kutoka kwako ni ushirikiano wako mzuri katika maswali
yetu ili kuturahisishia kumpata mhusika wetu tunayemuhitaji na baada ya hapo
tutakuachia huru ukaendelee na shughuli zako. Lakini vilevile kama utakuwa mkaidi
bado tunazo njia nyingi za kukulazimisha kuongea ambazo siyo nzuri kwa afya yako
ingawa hatutakuwa na namna ila kuzitumia pale tutakapohitajika kufanya hivyo”
M.D. Kunzugala akaweka kituo huku akimtazama Mwasu kwa makini kisha akaingiza
mkono katika mfuko wa koti lake la suti na kuchukua redio ndogo ya kijasusi yenye
uwezo wa kurekodi mazungumzo yale ambapo aliiwasha na kisha kuiweka pale juu
mezani. Kitendo ambacho kiliwapelekea na wale maafisa wengine walioketi kando
yake kuchukua vitabu vidogo na kalamu kutoka mifukoni mwao na kuviweka juu
ya ile meza tayari kuandika maelezo yote muhimu ambayo yangefanyika katika
mahojiano yam le ndani.
“Jina lako unaitwa nani?” M.D. Kunzugala akavunja tena ukimya.
“Mwasu”Mwasu akajibu kwa woga huku akitetemeka.
“Jina lako kamili” mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini Evans
Mchafu akadakia na kusisitiza .
“Mwasu Mayanja” Mwasu akaongea huku akiwatazama wale watu kwa mashaka
“Taja umri wako,kabila na dini” Sulle Kiganja akadakia na Mwasu alipomaliza
kutaja mahojiano yale yakaendelea.
“Unaishi wapi hapa Dar es Salaam?” M.D.Kunzugala akauliza.
“Eneo la Fire” Mwasu akaongea kwa utulivu.
“Namba ya nyumba unayoishi?” Evans Mchafu akauliza huku akimtazama
Mwasu kwa makini.
“Nyumba namba 27” Mwasu akafafanua.
“Unamfahamu mtu anayeitwa Chaz Siga?” M.D. Kunzugala akauliza huku
watu wote mle ndani wakimtazama Mwasu kwa uyakinifu. Mwasu akajikuta
akitaka kushawishika kukataa kuwa alikuwa hafahamu chochote kuhusu Chaz Siga
lakini alipokumbuka lile onyo alilopewa awali kabla ya kuanza kwa mahojiano yale
akanyoosha maelezo.
“Namfahamu”
“Yeye ni nani kwako?” Sulle Kiganja akadakia.
“Mwajiri wangu”
“Umeanza kufanya kazi kwake kwa muda gani?” Evans Mchafu akatumbukiza
swali.
“Zaidi ya mwaka mmoja sasa” Mwasu akajibu huku akiyatembeza macho yake
kuwatazama wale watu
“Kabla ya hapo ulikuwa ukifanya kazi wapi?” M.D Kunzugala akauliza huku
wenzake wakiinama na kuandika maelezo yale kwenye vile vitabu vyao katika kila
hatua muhimu iliyokuwa ikifikiwa katika mahojiano yale.
“Sikuwa na kazi” Mwasu akafafanua.
“Kazi gani uliyokuwa ukiifanya katika ofisi ya Chaz Siga?” M.D Kunzugala
akauliza huku akivigongesha vidole vyake juu ya ile meza.
“Katibu muhtasi” Mwasu akajibu kwa utulivu na kupelekea kitambo kifupi cha
ukimya kutokea mle ndani kabla ya Evans Mchafu kuvunja ukimya ule kwa swali.
“Ofisi yenu inashughulika na nini binti?”
“Upelelezi binafsi” jibu la Mwasu likawapelekea wale watu mle ndani wageuke na
kutazamana hata hivyo hakuna aliyemsemesha mwenzake ingawaje kupitia nyuso zao
kulikuwa na kila hakika kuwa hoja fulani zilikuwa zimeibuliwa vichwani mwao.
“Ofisi yenu ina leseni inayowaruhusu kufanya hivyo?” M.D Kunzugala akauliza
“Mimi sifahamu labda mwajiri wangu” Mwasu akajitetea
“Unatambua kuwa sheria za nchi hii zinamkataza mtu yeyote kuunda jeshi,kikundi
cha ulinzi au taasisi yoyote ya usalama inayoshabihiana na kazi zinazofanywa na ofisi
yenu?” Evans Mchafu akatumbukiza hoja.
“Hapana,sifahamu” Mwasu akajibu kwa woga kabla ya M.D Kunzugala kuendelea.
“Una hisia zozote juu ya sababu za kwa nini upo hapa?”
“Hapana” Mwasu akajibu kwa utulivu hata hivyo macho yake yalikataa kudanganya.
“Mwajiri wako Chaz Siga anahusishwa na mauaji ya watu kadhaa wakiwemo
wanausalama yanayoendelea kutokea hapa Dar es Salaam. Unafahamu chochote juu
ya hilo?” Sulle Kiganja akauliza huku akimtazama Mwasu kwa makini.
“Sifahamu” Mwasu akaitikia.
“Unaamini kuwa mwajiri wako Chaz Siga anaweza kuhusika na mauaji haya?”
M.D Kunzugala akauliza kwa utulivu baada ya kuingiza mkono mfukoni na kuchukua
picha tofauti zilizopigwa kwenye matukio ya vifo vya wanausalama wale na kuzisogeza
karibu na Mwasu.
“Siamini”
“Kwa nini huamini?” Evans Mchafu akauliza.
“Kwa kipindi chote nilichofanya kazi na Chaz Siga namtambua kama mtu
mpenda haki utu na wakala mkubwa wa amani hapa nchini kupitia tabia yake. Hivyo
sioni namna inayoweza kuniridhisha nikubaliane na nyinyi kuwa Chaz Siga ni muuaji
na ndiye aliyehusika na unyama huu” Mwasu akafafanua kiasi cha kuwapelekea wale
watu mle ndani watazamane kidogo na kisha kuyapeleka macho yao kwake.
“Ofisi yenu kwa sasa inahusika na upelelezi wa kesi ya namna gani?” Sulle Kiganja
akauliza swali lililompelekea kwa mara ya kwanza Mwasu ajikute akibabaika kabla ya
kudanganya pale alipoanza kuhisi madhara ambayo yangejitokeza baada ya kusema
ukweli.
“Upelelezi wa kesi nyingi ambazo siyo rahisi kuzikumbuka zote kwa pamoja”
Kamishna wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini Evans Mchafu akawa wa kwanza
kugundua kuwa Mwasu alikuwa akidanganya kabla ya wenzake nao kushtukia hata
hivyo hakuna aliyetia neno.
“Taja baadhi ya kesi unazozikumbuka” M.D Kunzugala akatumbukiza hoja huku
akimkata Mwasu jicho la udadisi. Lilikuwa swali la mtego lililompelekea Mwasu aanze
kubabaika tena huku akifikiria namna ya kujieleza.
“Nyingi ni kesi za watu binafsi zinazohusiana na usaliti katika mapenzi” Mwasu
akadanganya.
“Na hizo chache zilizosalia?” Evans Mchafu akauliza huku tabasamu la kinafiki
likichomoza usoni mwake.
“Zinahusu wizi na ubadhirifu wa fedha katika taasisi binafsi” Mwasu akadanganya
hata hivyo ni kama aliyejidanganya mwenyewe kwani uongo wake ulikosa ushawishi
kabisa kwa wale magwiji wa shughuli za kiusalama nchini na kuwafanya waishie
kutabasamu huku wakifahamu fika kuwa Mwasu alikuwa akikwepa kuzungumza
ukweli juu ya jambo fulani.
“Mwajiri wako anaishi wapi?” M.D Kunzugala akauliza.
“Sijawahi kufika nyumbani kwake kama yeye ambavyo hajawahi kufika kwangu”
“Hujawahi kumsikia hata siku moja akizungumzia juu ya mahali anapoishi hapa
jijini Dar es Salaam?” Sulle Kiganja akauliza huku akiacha kuandika na kumtazama
Mwasu.
“Hapana” Mwasu akajibu huku akitikisa kichwa kuonesha kukataa hata hivyo wale
maafisa usalama wakafahamu haraka kuwa Mwasu alikuwa akiwadanganya kwani
ilikuwa ni vigumu sana kwa ofisi ndogo kama ile halafu wafanyakazi wasifahamiane
wanapoishi kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja.
“Kwa nini uliwatoroka watu wangu ofisini kwako wakati walipotaka kuonana na
mwajiri wako?” Sulle Kiganja akauliza.
“Nilihisi kuwa hawakuwa watu wema” Mwasu akajitetea na hapo kitambo kifupi
cha ukimya kikafuatia mle ndani kabla ya M.D Kunzugala kuibua hoja.
“Wakati watu wetu walipokuwa wakikuchukua kistaarabu kwenye gari
inasemekana kuwa uliutupa mkoba wako dirishani. Unaweza kutueleza nini maana
ya kitendo kile?”
“Ni kama nilivyosema kuwa nilihisi wale watu waliokuja ofisini na hatimaye
baadaye kuniteka hawakuwa wema ndiyo kisa nikaamua kuurusha nje mkoba wangu
kwani ndani yake kulikuwa na taarifa muhimu za ofisi na sikujua watu wenu walikuwa
na nia gani na mimi” Mwasu akajitetea.
“Mtu uliyemrushia huo mkoba ni nani?” Evans Mchafu akauliza na kumpelekea
Mwasu ashikwe tena na kigugumizi.
“Tuambie binti usitupotezee muda wetu” M.D Kunzugala akaongea
“Mwajiri wangu” Mwasu akaongea kwa woga
“Chaz Siga?” Sulle Kiganja akauliza kwa shauku
“Ndiyo”
“Alijuaje kama wewe ulikuwa pale?”
“Nilimpigia simu” Mwasu akaongea kwa utulivu na baada kitambo kifupi kingine
cha ukimya huku wale makachero wakitazamana na kunong’onezana jambo mmoja
akavunja ukimya.
“Ofisi yenu ina wafanyakazi wangapi?” M.D Kunzugala akauliza baada ya
kukumbuka kuwa taarifa za kifo cha mmoja wa maafisa wake wa juu wa usalama
aitwaye Mbingu Balimenya kilichotokea kule kwenye korido ya jengo moja la ghorofa
lililoko maeneo posta kilikuwa kimetokana na risasi iliyofyatuliwa na mtu mwingine
na siyo Chaz Siga.
“Tupo wafanyakazi wawili tu,mimi na mwajiri wangu Chaz Siga” Mwasu akajibu
kwa utulivu kitendo kilichompelekea Sulle Kiganja kutumbukiza mkono mfukoni na
kutoa karatasi ndogo yenye namba za gari alizozipata kutoka kwa vijana wake wa
kazi,Fulgency Kassy,Pweza na Kombe. Ilikuwa ni namba ya gari la Momba lililokuwa
likitumika na Koplo Tsega. Sulle Kiganja akaisogeza karatasi ile karibu na Mwasu pale
mezani kabla ya kumuuliza
“Unalifahamu gari lenye namba hizi?” Mwasu akainama na kuzitazama zile namba
za gari kwenye ile karatasi kwa makini kabla ya kutikisa kichwa chake katika namna
ya kukataa.
“Sizifahamu”
“Hujawahi kuliona popote gari lenye namba hizi?” Sulle Kiganja akauliza katika
namna ya kutaka kupata hakika huku akimtazama Mwasu kwa makini.
“Hapana” Mwasu akajibu kwa utulivu na hapo Sulle Kiganja akakichukuwa kile
kikaratasi na kukitia mfukoni huku taratibu akiegemea kiti na kuvigongesha vidole
vyake juu ya ile meza kama mtu afikiriaye jambo fulani kisha kikafuata kitambo kifupi
cha ukimya kabla ya M.D Kunzugala kukohoa kidogo na kuvunja tena ukimya.
“Unadhani ni wapi tunapoweza kumpata mwajiri wako?”
“Sehemu pekee tunayokutana mimi na yeye ni ofisini zaidi ya pale hakuna sehemu
nyingine ninayoifahamu” Mwasu akafafanua kisha kitambo kifupi cha ukimya
kikafuatia tena mle ndani huku wale makachero wakimtazama.
“Sikiliza binti pengine ukawa hufahamu kuwa sisi ni akina nani na uzito wa suala
tunalojitahidi kulitatua ili maafa yasiongezeke. Hakuna namna nyingine itakayokuweka
huru kama hutotupa ushirikiano. Tunaamini kuwa katika mazingira fulani
tusiyoyafahamu unaweza kutusaidia kumkamata mwajiri wako vinginevyo tunaweza
kutumia njia zetu nyingine lakini wewe hutokuwa salama na sidhani kama unapenda
tufike huko” Evans Mchafu akaongea kwa utulivu huku akimtazama Mwasu na
wakati akifanya vile Sulle Kiganja akawa akiandika maelezo fulani kwenye kile kitabu
chake kidogo huku akimtazama Mwasu katika uso ulioanza kupoteza uvumilivu.
“Nitajie namba za simu za mwajiri wako” Sulle Kiganja akauliza kwa makini huku
akimtazama Mwasu usoni. Lilikuwa swali la kushtukiza lililompelekea Mwasu ababaike
na kushindwa kujibu haraka. Ukimya kidogo ukapita huku Mwasu akiyatembeza
macho yake taratibu kuwatazama wale watu mbele yake kama afikiriaye jambo kisha
akaongea kwa utulivu.
“Namba za simu ya mwajiri wangu bado sijazishika kichwani” Sulle Kiganja
kuona vile akashindwa kuvumilia akainuka na kumchapa Mwasu kofi moja la nguvu
usoni kiasi cha kumpelekea Mwasu apige yowe kali la maumivu huku damu nyepesi
ikimtoka mdomoni.
“Chaz Siga mpaka sasa anamshikilia mateka mmoja wa maafisa wangu wa usalama
baada ya jaribio lake la kumuua kushindikana. Kama hutoshirikiana nasi katika
kumnasa mwajiri wako basi huyo mateka anayemshikilia huwenda naye akauwawa
kama ilivyokuwa kwa maafisa usalama wangu wengine na hatuwezi kukubali mtu wetu
apoteze maisha huku wewe ukiendelea kuishi vizuri katika chumba hiki. Nadhani
unafahamu ninachokiongea” M.D Kunzugala akafoka huku akimtazama Mwasu kwa
hasira kisha akasogeza kiti nyuma na kusimama akifuatiwa na wale wenzake kisha
pasipo kuongea neno wakaanza kuondoka mle ndani wakielekea kwenye ule mlango
wa kutokea nje ya kile chumba. Yule kijana akawahi kuwafungulia ule mlango na
walipotoka nje na yeye akafuatia nyuma yao huku ule mlango ukifungwa.
Kitambo kifupi cha ukimya kikafuata huku maswali mengi yakipita kichwani
kwa Mwasu juu ya mahojiano aliyomaliza kufanyiwa na wale watu waliyotoka mle
ndani muda mfupi uliopita. Mawazo yake hatimaye yakahamia kwa Chaz Siga na
kumpelekea kwa mara ya kwanza ajikute akijuta kuwa sehemu ya mkasa huu.
Muda mfupi mara baada ya wale watu kuondoka akiwa katikati ya mawazo mara
Mwasu akajikuta akishikwa na wasiwasi baada ya kuusikia ule mlango wa kile chumba
ukifunguliwa tena na kisha wanaume watatu wengine kuingia mle ndani. Wawili
walikuwa vijana na mmoja mzee wa makamo. Yule mzee alikuwa amevaa mavazi ya
kidaktari,koti jeupe, stetheskopu shingoni na miwani yake mikubwa machoni huku
mkononi akiwa ameshika kisanduku kidogo chenye dhana muhimu za kazi. Wale
vijana wawili mikononi walikuwa wamevaa glovu nyepesi za mpira huku kila mmoja
amebeba kiboksi kidogo. Ingawa sura za watu wale hazikuonesha tashwishi yoyote
lakini Mwasu alipowatazama akajikuta akianza kuwalaani hata kabla hawajamfikia
huku akianza kuijutia nafsi yake.
Mlango wa kile chumba ulipofungwa wale watu wakamsogelea Mwasu pale
kwenye kiti na kumtazama kana kwamba hawakuwahi kumuona kiumbe kama yule
tangu wazaliwe.
“Hujambo binti mzuri?” yule daktari mzee akamsogelea Mwasu akimuuliza kwa
utulivu na kumshika bega huku wale vijana wenye miili mikubwa wakiwa kando yake.
Hata hivyo Mwasu hakusema neno badala yake akabaki akiwatazama tu.
“Hatujawahi kumpokea mgeni wa aina yako humu ndani. Kazi yetu ni
kushughulika na wanaume hasa wale walioshindikana kutupatia taarifa tunazozihitaji.
Wewe umekuwa changamoto mpya kwetu. Hata hivyo hakuna mtu aliyewahi kuingia
humu ndani na kutoka na siri yake moyoni kwani tuna hakika na huduma hii. Kwa
muda wa miaka thelathini na mbili tangu nianze kuifanya hii kazi ni wanaume
wawili tu waliokufa humu ndani na siri zao moyoni na nikikutazama wewe huelekei
kuivunja rekodi hiyo. Msichana mrembo kama wewe ingefaa uwe nyumbani kulea
watoto badala ya kujiingiza kwenye mambo hatari kama haya” yule mzee akaongea
kwa utulivu huku akitia jitihada za kuvaa glovu mikononi mwake baada ya kuacha
kumtazama Mwasu na kufungua kile kisanduku chake chekundu chenye vifaa vingi
visivyoelezeka kikiwemo kibunda cha glovu nyingi za mpira. Yule daktari alipomaliza
akageuka tena na kumtazama Mwasu.
“Hiki ni chumba ambacho hakiruhusu sauti ya namna yoyote kupenya na kutoka
nje hivyo usipoteze muda wako kupiga kelele.
“Mnataka kunifanya nini?” Mwasu akauliza kwa hofu huku akijitahidi kufurukuta
kwenye kile kiti bila mafanikio kwani mwili wake ulikuwa umefungwa kwa mikanda.
“Tunataka utueleze kila kitu unachokifahamu kuhusu huyu mtu anayeitwa Chaz
Siga ambaye wewe umejinadi kuwa ni mwajiri wako” yule daktari akaongea kwa
utulivu huku akikisogeza kiboksi kimoja kati ya vile viboksi viwili walivyokujanavyo
wale vijana.
“Kitu gani?” Mwasu akauliza huku amejawa hofu hata hivyo hakuna aliyemjibu
badala yake kijana mmoja aliyekuwa nyuma yake akasogea na kuichana blauzi yake
kifuani na alipomaliza akafungua na sidiria yake na kuitupa kando kabla ya kuyatazama
matiti ya Mwasu kwa utulivu kama mtafiti. Yule daktari mzee alipofungua kiboksi
kimoja akatumbukiza mkono na kuchukuwa kilichokuwa ndani yake. Alipoutoa
mkono wake ulikuwa umeshika panya buku mkubwa mwenye meno makali
yaliyojitokeza nje huku akiuchezeshachezesha mkia wake kwa usongo na kupiga
kelele kali inayoumiza masikio.
“Mnataka kunifanya nini?” Mwasu akauliza huku akitetemeka kwa hofu.
“Rafiki yetu John hajakula kwa muda wa siku tatu” yule daktari akaongea huku
akimuinua juu yule panya na kumgeuzageuza katika namna ya kumchunguza.
“Naomba mniache nimeshawaambia kila kitu ninachokifahamu?” Mwasu akafoka
hata hivyo hakuna aliyemsemesha badala yake wale watu kwa pamoja wakaangua
kicheko cha dhihaka kisha yule daktari mzee akachukua mfuko mweusi wa kitambaa
kutoka kwa mmoja wa wale vijana na kumtumbukiza yule panya ndani ya ule
mfuko. Kufumba na kufumbua wale vijana wakauchukua ule mfuko na kumvalisha
Mwasu hadi sehemu za matiti yake kifuani. Kilichofuata baada ya pale ni yule panya
buku mwenye njaa kali kuanza kuzitafuna sehemu mbalimbali za mwili wa Mwasu
yakiwemo matiti yake. Kiwiliwili cha Mwasu kikiwa ndani ya ule mfuko mweusi wa
nguo wenye panya Mwasu akaanza kupiga mayowe ya hofu iliyotokana na maumivu
makali ya majeraha ya kutafunwa na yule panya huku akikukurika kwa nguvu zake
zote pale kwenye kiti. Hata hivyo Mwasu hakufanikiwa kujinasua kutoka katika kadhia
ile na hapo zoezi lile likaendelea huku yule panya akiendelea kuzitafuna sehemu za
mwili wake hadi pale yule daktari alipowaambia wale vijana wasitishe na kuuondoa
ule mfuko wenye panya.
Ule mfuko ulipoondolewa Mwasu alikuwa akilia kwa maumivu makali yaliyotokana
na majeraha ya yule panya huku macho yamemtoka na kuwa mekundu kwa hofu
Yule panya alikuwa amemtafuna na kumtia majeraha kila mahali zikiwemo sehemu
za matiti yake na kusababisha damu nyingi kumtoka. Mwasu akaendelea kulia huku
akihema ovyo.
“Tuambie binti,Chaz Siga ni nani na anapeleleza kitu gani?” yule daktari mzee
akaongea kwa utulivu huku akichukua sigara moja kutoka katika pakiti yake mfukoni
alipoiweka mdomoni akajiwashia kwa kiberiti chake cha gesi na kuvuta mapafu
kadhaa kabla ya kuupuliza moshi pembeni.
“Nimekwisha waambia kuwa mimi sifahamu chochote zaidi ya hicho nilichowaeleza
kwenye mahojiano na maafisa wenu” Mwasu akaongea huku akiendelea kulia. Yule
daktari mzee akamtazama kwa utulivu kabla ya kuvunja ukimya.
“Sikiliza binti,katika miaka yote niliyofanya hii kazi na kulipwa mshahara mzuri
wa kumudu kuilea familia yangu vizuri na kusomesha watoto wangu hadi chuo kikuu
nimekuwa nikichukia sana kitendo cha kuiona roho ya binadamu pale inapouacha
mwili. Hata hivyo nimejikuta nikifurahi sana pale ninapokutana na mtu mkaidi kama
wewe”
“Nimekwisha waeleza kuwa sifahamu chochote” Mwasu akasisitiza huku
akiendelea kulia hali iliyompelekea yule daktari mzee afungue tena kiboksi kingine
na kuingiza mkono ndani yake kumchukua panya mwingine mkubwa zaidi ya yule
wa awali mwenye meno makali zaidi na njaa kali. Yule panya akawa akipiga kelele na
kuuchezesha chezesha mkia wake huku na kule huku akijipindapinda katika namna
ya kutafuta nafasi nzuri ya kutaka kutafuna vidole vya yule daktari mzee. Yule daktari
mzee bila kupoteza muda akamtia yule panya kwenye mfuko mwingine mweusi wa
nguo na bila kuchelewa ule mfuko akavalishwa tena Mwasu,mara hii akipiga mayowe
makubwa zaidi ya hofu huku akijitahidi kujinasua kwenye kile kiti bila mafanikio. Hata
hivyo sauti yake haikwenda popote mle ndani badala yake ikamezwa na sauti nzito
ya vicheko vya wale wanaume wakati yule panya alipokuwa akianza kuzishambulia
sehemu mbalimbali za mwili wake.
 
KUITAFUTA BENKI YA ZANZIBAR MARINE jijini Dar es Salaam halikuwa
jambo jepesi hata kidogo kwa kuzingatia kuwa hii ilikuwa ni benki mpya kabisa kuwahi
kufanya shughuli zake jijini Dar es Salaam. Ni katika benki hii ndipo mtu mwenye jina
la Aden Mawala aliposemekana kufanya kazi kama meneja wa benki hiyo. Kupitia
barua yenye ujumbe mfupi ndani ya bahasha ndogo ya kaki ambayo Koplo Tsega
alikuwa ameiichukua kule nyumbani kwa Balimenya usiku ule baada ya kupambana
na wale wanausalama wawili na hatimaye kuwaangamiza. Maelekezo ndani ya barua
ile kutoka kwa mtu mmoja asiyefahamika jina lake yalikuwa yameweka bayana kuwa
meneja wa benki ya Zanzibar Marine tawi la jijini Dar es Salaam ndugu Aden Mawala
alikuwa amepewa maelekezo yote muhimu ya kuhakikisha kuwa kiasi fulani cha fedha
nyingi sana zilizoingizwa kwenye benki yake anazifanyia mgao sahihi kufuatana na
orodha ya majina yote ya watu waliokuwa wameorodheshwa katika barua ile kutokea
tarehe fulani. Maelezo yale yaliendelea kuelekeza kuwa watu hao wangefika kwenye
benki hiyo pamoja na vitambulisho vyao vya kazi huku wakiwa na hundi zao tayari
kulipwa mgao wao katika fedha hizo. Mtoa taarifa kupitia barua ile ambaye hakutaja
jina lake aliendelea kusisitiza kuwa shughuli yote ya mgao wa fedha hizo ilipaswa
kufanywa katika mazingira yenye usiri mkubwa sana ingawa hakueleza kuwa ni lini
mgao huo ulipaswa kufanyika.
Kupitia orodha ya majina ya watu waliokuwa katika barua ile Koplo Tsega alikuwa
ameongeza ziada nyingine katika utafiti wake. Jambo moja muhimu aliloligundua
ni kuwa majina yote yaliyokuwa katika zile hundi alizozikuta kwenye ile bahasha
nyumbani kwa Meja Khalid Makame yalikuwa pia kwenye ile barua aliyoikuta
nyumbani kwa Balimenya isipokuwa majina ya watu wanne tu ambao hakuwafahamu.
Pili, hundi zile alizozipata nyumbani kwa Meja Khalid Makame zilikuwa ni za benki
ya Zanzibar Marine. Hivyo kwa namna moja au nyingine ni kuwa meneja wa benki ya
Zanzibar Marine jijini Dar es Salaam ndugu Aden Mawala alikuwa akifahamu kila kitu
kilichokuwa kikiendelea akiwemo yule mtu aliyetoa maelekezo yale kwenye ile barua.
Zanzibar Marine Bank ilikuwa kando ya barabara kuu ya Bagamoyo upande
wa kulia umbali mfupi baada ya kuyapita makutano ya barabara ya Kawawa na ile
barabara ya Mwai Kibaki eneo la Morocco kando ya jengo refu la ghorofa la Drive
Inn Plaza. Baada ya safari ndefu ya kuzunguka katika vitongoji vingi vya jiji la Dar
es Salaam na ulizauliza ya hapa na pale hatimaye Koplo Tsega akawa ameyafumania
maficho makini ya benki hii change jijini Dar es Salaam.
Mchana huu foleni ya magari katika barabara ya Bagamoyo ilikuwa kubwa na yenye
kukera hivyo Koplo Tsega akaona kuwa lingekuwa ni jambo la usumbufu sana kusubiri
foleni ile hadi ipungue ili apate nafasi nzuri ya kuchepuka upande wa pili wa barabara
ilipokuwa ile benki hivyo badala yake akaingia upande wa kushoto na kuegesha gari
lake kwenye eneo la maegesho ya magari la mgahawa maarufu wa kichina uitwao
Seafoods kisha akafungua mlango na kushuka akiwa katika mwonekano mpya kabisa
wa kofia nyeusi ya Sombrero kichwani, miwani nyeusi ya jua machoni, blauzi nyeusi
ya pullneck aliyoitanguliza ndani ya shati zito la jeans la rangi ya bluu bahari. Chini
alikuwa amevaa suruali nyepesi ya jeans iliyolichora vyema umbo lake maridhawa la
kike na buti ngumu za rangi ya udongo aina ya Travolta. Kwa kukwepa aina yoyote ya
bahati mbaya pale ambapo rabsha zozote zingejitokeza mbele ya safari Koplo Tsega
alikuwa ameamua kushuka na begi lake la mgongoni jeusi, jembamba na refu lenye
zana zote muhimu za kazi ikiwemo Sniper Rifle 338 Lapua Magnum, bunduki maalum
kwa ajili ya kudungulia windo sumbufu la umbali wa masafa marefu.
Kulikuwa na watu wachache waliokuwa wameketi kwenye sehemu ya nje ya
mgahawa ule wakijipatia huduma. Wakati Koplo Tsega alipokuwa akishuka kwenye
gari watu wale waligeuka na kumtazama hata hivyo hakutoa nafasi yoyote ya kugeuka
kuvutia badala yake akafunga mlango haraka na kuvuka barabara akielekea upande wa
pili eneo lilipokuwa lile jengo la benki ya Zanzibar Marine huku akikatisha katikati ya
foleni ndefu ya magari katika barabara ile.
Akiwa na hakika kuwa hakuna mtu yeyote aliyekuwa akimfuatilia nyuma yake mara
tu alipomaliza kuvuka barabara ile Koplo Tsega akatembea kandokando ya barabara
ile akishika uelekeo wa upande wa kulia hadi pale alipokifikia kizuizi cha mbele cha
kuingia kwenye benki ile kando ya kibanda cha mlinzi kilichokuwa na askari polisi
wawili ambapo alipita pembeni ya kizuizi kile katika njia ya wazi ya watembea kwa
miguu iliyopakana na bustani nzuri ya nyasi za kijani kibichi na miti mirefu ya miashoki
iliyopandwa katika mstari mnyoofu wa kupendeza mbele ya jengo lile la benki.
Koplo Tsega akaendelea kutembea kwa utulivu akielekea kwenye ile benki huku
kumbukumbu zake zikimueleza kuwa kabla ya jengo lile kutumika na Zanzibar Marine
Bank hapo awali lilikuwa likitumika kama makao makuu ya shirika fulani la mtandao
wa mawasiliano ya simu. Tangu kutokea mauaji ya Sikawa kwenye kile chumba
namba 18 cha Hotel 92 Dar es Salaam eneo la Ubungo, Koplo Tsega alikuwa ameamua
kuhamishia makazi yake kwenye chumba kimoja alichokuwa akiishi Sikawa kati ya
vyumba vingi vya uani vya wapangaji katika nyumba moja iliyokuwa eneo la Mwenge
mtaa wa Mama Ngoma. Huku akirudi usiku wa manane wakati wapangaji wote
wakiwa usingizini na kuondoka mapema sana alfajiri kabla ya watu wote hawajaamka
katika kile chumba kidogo cha kijana wa mjini chenye kitanda kidogo cha futi tano
kwa sita, kabati dogo la nguo, seti moja ya runinga juu ya meza yenye deki moja ya ya
dvd, spika dhaifu za muziki wa gheto na ndoo nyingi za maji zilizokuwa kwenye kona
mojawapo ya chumba kile. Ili kumuenzi Sikawa, Koplo Tsega alikuwa amejiapiza
kulipa kisasi kwa wote walio husika na kifo chake.
Nje ya jengo lile la benki ya Zanzibar Marine kwenye eneo la maegesho ya magari
kulikuwa na magari machache yaliyokuwa yameegeshwa. Koplo Tsega alipochunguza
akajikuta akifurahi baada ya kugundua kuwa miongoni mwa magari yaliyokuwa katika
maegesho yale lilikuwepo gari moja aina ya Landcruiser jeupe lililokuwa limeegeshwa
katika sehemu maalum ya maegesho yenye utambulisho wa cheo cha meneja wa benki
ile. Uwepo wa lile gari eneo lile ikawa ni ishara tosha kuwa meneja wa benki ile ndugu
Aden Mawala alikuwepo ofisini kwake kama kawaida akiendelea na shughuli zake za
kiofisi kama ilivyo ada. Hata hivyo mandhari ya nje ya ile benki yalitosha kuthibitisha
kuwa benki ile haikuwa na msongamano mkubwa wa wateja kama zilivyokuwa benki
nyingine zenye umri mrefu jijini Dar es Salaam.
Koplo Tsega akaendelea kutembea kwa utulivu akikatisha kuelekea sehemu ya
mbele ya benki ile yenye baraza pana ya sakafu ya marumaru za kuvutia na juu yake
imefunikwa na paa zuri na imara ya zege iliyoezekwa kwa vigae na kushikiliwa na
nguzo mbili upande wa kushoto na kulia. Koplo Tsega alipozifikia ngazi za baraza ile
akazipanda kwa utulivu kisha baada ya safari ya hatua chache mbele yake akausukuma
mlango mkubwa wa kioo na kupotelea mle ndani.
Ndani ya benki ile kulikuwa na watu wachache ambao kwa idadi yao wengi wao
walikuwa ni wazanzibar kama siyo watu wenye asili ya bara la Asia. Mandhari ya benki
ile mle ndani yalikuwa tulivu na ya kisomi. Viyoyozi makini vya mle ndani vilikuwa
vikiendelea kusukuma hewa safi yenye baridi ya wastani. Mara baada ya kuingia mle
ndani upande wa kushoto kulikuwa na ngazi za kuelekea juu ghorofani kwenye ofisi
nyingine za idara tofauti za benki ile kama idara ya mikopo, idara za sera, mipango
na utawala na nyinginezo. Sehemu ya chini katikati ya jengo kulikuwa na nguzo mbili
kubwa za uviringo zilizoishikilia sehemu ya juu ya jengo lile na sakafu ya mle ndani
ilifunikwa kwa zulia zuri la rangi ya kijivu.
Mara baada ya kuingia mle ndani Koplo Tsega akasita kidogo na kusimama
akijitahidi kuyazoea mandhari ya mle ndani kwa kuyatembeza macho yake taratibu.
Upande wa kushoto kulikuwa na meza ya ukutani ambayo ilikuwa ikitumiwa na wateja
wa benki ile kwa ajili ya kuandikia au kujaza taarifa za benki kwenye slips zao. Mara
baada ya kuipita meza ile kulikuwa na viti vingi katika sehemu maalum ambapo wateja
wa benki ile wangeketi na kusubiri wakati shida zao zikishughulikiwa na maafisa wa
benki ile. Baada ya kuipita sehemu ile ya mangojeo mbele kidogo kulikuwa na dawati
kubwa lenye umbo la nusu mkate mbele ya msichana mrembo wa idara ya huduma
kwa wateja aliyevaa Hijabu.
Upande wa kulia mle ndani kulikuwa na vibanda vinne vya tellers wa benki
vilivyotengenezwa kwa mbao nyepesi ya mahogani sehemu za chini na kuta safi za
vioo vyenye matundu mbele yake. Ndani ya vile vibanda kulikuwa na wafanyakazi wa
benki ile waliokuwa wakiendelea kuwahudumia wateja wachache waliokuwa kwenye
foleni fupi kuelekea vibanda vile.
Akiwa ameridhishwa na tathmini ya mandhari yale taratibu Koplo Tsega akapiga
hatua zake kuelekea kwenye lile dawati la huduma kwa wateja ama customer care
alilokuwa ameketi yule dada mlimbwende aliyekuwa eneo lile akimuelekeza mteja
mmoja namna ya kujaza taarifa zake kwenye fomu maalum ya benki iliyokuwa juu
ya lile dawati. Wakati Koplo Tsega akifika sehemu ile yule dada mlimbwende wa
mapokezi alikuwa tayari amekwisha maliza kumuhudumia yule mteja hivyo haraka
akageuka na kumtazama Koplo Tsega katika uso wenye tabasamu la kibiashara.
“Karibu dada”
“Ahsante” Koplo Tsega akaitikia kisha kabla ya kusema neno akageuka kidogo
kuyatembeza macho yake makali yaliyojificha nyuma ya miwani kuchunguza eneo lile
na alipoona kuwa hali ilikuwa shwari akayarudisha tena macho yake kwa yule dada.
“Karibu tafadhali naomba nikusaidie dada yangu” yule mlimbwende akasisitiza
huku akimtazama Koplo Tsega katika uso wenye tabasamu jepesi. Koplo Tsega
akasogea vizuri karibu ya lile dawati na kuongea huku usoni akilazimisha tabasamu.
“Nahitaji kuonana na meneja wa benki”
“Una shida gani dada yangu labda huwenda nikakusaidia” yule dada akaongea
kiungwana
“Nahitaji mishahara yote ya wafanyakazi wa kampuni yetu ipitie kwenye benki
yenu” Koplo Tsega akaamua kudanganya kwa kutengeneza hoja yenye ushawishi
mkubwa ambayo kwa namna moja au nyingine aliamini kuwa ilikuwa nje ya uwezo
wa yule dada wa idara ya huduma kwa wateja.
“Ofisi ya meneja wa benki ipo mwisho wa hili jengo upande wa kushoto ukifika
utaona korido. Fuata korido hiyo ukifika mwisho utauona mlango”
“Ngoja nipige simu ofisini kwake kuuliza kama atakuwa na mgeni yeyote” yule
dada akaongea kwa utulivu na kabla Koplo Tsega hajatia neno kiwambo cha simu
ya mezani iliyokuwa juu ya meza fupi kando yake tayari ilikuwa sikioni. Baada ya
kubonyeza tarakimu kadhaa ile simu ikawa hewani na hapo kukafuatiwa na maongezi
mafupi baina yake na mtu wa upande wa pili wa ile simu kabla ya yule dada kukata
simu na kugeuka akimtazama Koplo Tsega katika uso wenye tabasamu la matumaini.
“Unaweza kwenda yupo ofisini kwake na hana mgeni yeyote”
“Nashukuru” Koplo Tsega akatoa shukrani zake huku tabasamu hafifu la
kutengeza likiumbika usoni mwake
“Karibu tena” yule dada akaitikia huku akijiandaa kumsikiliza mteja mwingine
aliyefika eneo lile. Bila kupoteza muda Koplo Tsega akaanza kuzitupa hatua zake
taratibu akikatisha eneo lile kuelekea mwisho wa lile jengo kama alivyoelekezwa na
wakati alipokuwa akitembea akagundua macho ya wanaume wote waliokuwa kwenye
vile vibanda vya tellers wa ile benki yalikuwa yakimtazama kwa uchu kupitia kuta safi
za vioo zilizowazunguka na hali ile ikampa faraja kidogo huku taratibu akizichezesha
malighafi muhimu za mwili wake.
Mara tu alipofika mwisho wa lile jengo upande wa kushoto akaiona korido fupi
kama alivyoelekezwa hivyo Koplo Tsega akaifuata korido ile. Ilikuwa ni korido fupi
iliyokuwa ikitazamana na milango mitatu. Mlango mmoja upande wa kushoto,mlango
mwingine upande wa kulia na mlango wa mwisho ulikuwa mwisho wa ile korido kwa
mbele. Wakati Koplo Tsega akiendelea kutembea akawa akiyatembeza macho yake
taratibu kuichunguza ile milango na kupitia vibao vidogo vyeusi vyenye maandishi
meupe akagundua kuwa mlango wa kwanza upande wa kushoto ulikuwa ni wa ofisi
ya Line manager wa kitengo cha Import and Export. Mlango uliyofuata upande wa
kulia ulikuwa ni wa ofisi inayoshughulikia miamala yenye kuhusisha kiasi kikubwa cha
fedha ama Bulk transaction na ule mlango uliyokuwa mbele mwisho wa ile korido
ndiyo uliyokuwa wa kuelekea kwenye ofisi ya meneja wa benki ile hali iliyompelekea
Koplo Tsega ajikute akitabasamu peke yake. Mandhari ya eneo lile yalikuwa tulivu
mno hata hivyo hali ile haikumaanisha kuwa ndani vyumba vile hapakuwa na shughuli
za kiofisi zilizokuwa zikiendelea.
Hatimaye Koplo Tsega akawa ameufikia ule umlango wa kuingia kwenye ile ofisi
ya meneja wa ile benki. Alipofika pale mlangoni akasimama kidogo akijipa utulivu na
kujitengeneza vizuri na baada ya kugeuka nyuma na kuhakikisha kuwa hapakuwa na
mtu yeyote mwingine eneo lile akausogelea mlango wa ile ofisi na kushika kitasa chake
huku akikisukuma taratibu. Tofauti na matarajio yake mlango ule mzito ukafunguka
taratibu na hapo Koplo Tsega akaingia mle ndani.
Kama zilivyokuwa ofisi nyingi za kisasa za zama hizi ofisi ile ilikuwa ya kisasa zaidi.
Sakafu yake ilifunikwa kwa zulia maridadi la rangi ya kijivu lenye michoro ya maua
meusi na meupe. Upande wa kushoto kulikuwa na dirisha kubwa lililofunikwa kwa
pazia jepesi. Kando ya dirisha lile kulikuwa na rafu nne kubwa ya chuma zenye droo
nyingi zilizosimama wima kama milima meza. Kabla ya kuzifikia rafu zile kulikuwa na
seti moja ya makochi laini meupe ya sofa yaliyoizunguka meza fupi ya kioo iliyokuwa
na majarida na vipeperushi vinavyohusiana na huduma zinazotolewa na ile benki.
Upande wa kulia wa yale makochi kulikuwa na jokofu kubwa la vinywaji baridi
na kupitia mlango wa kioo wa lile jokofu isingemuwia vigumu mtu yeyote kuona
kilichokuwa mle ndani. Kiyoyozi makini bado kilikuwa kazini kusambaza hewa safi
iliyokinzana na hali ya joto kali ya jiji la Dar es Salaam mle ndani.
Kama zilivyokuwa ofisi nyingi zinazotoa huduma kwa jamii na kuchangia pato la
taifa,katikati ya ofisi ile ukutani kulikuwa na picha mbili za marais zilizotundikwa. Rais
wa serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na rais wa serikali ya mapinduzi ya
Zanzibar.
Koplo Tsega akasumbuka kidogo katika kutaka kufahamu ni wapi alipokuwa
mwenyeji wa ofisi ile mle ndani na hali ile ilitokana na namna ya mpangilio wa ofisi
ile ulivyokuwa. Baada ya kuufunga ule mlango na kusogea upande wa kulia akizipita
rafu nyingine mbili ndefu za chuma zilizopakana na rafu nyingine kubwa zenye
vitabu,mafaili na nyaraka nyingine za ofisi hatimaye Koplo Tsega akamuona meneja
wa benki ile akiwa ameketi kwenye kiti chake cha utukufu nyuma ya meza kubwa
ya ofisi yenye kompyuta kubwa ya mezani,tray ndogo yenye ngazi tano kwa ajili ya
kuwekea nyaraka nyepesi za ofisi,simu ya mezani,mhuri na kidau cha wino pamoja
na mlima wa mafaili mengi mbele yake. Upande wa kushoto eneo lile kulikuwa na
meza nyingine ndogo na fupi ya mbao na juu ya meza ile kulikuwa na mashine tatu za
ofisi printer,scanner na mashine ya kudurufu. Pembeni yake upande wa kulia wa ile
meza ya ofisi kulikuwa na rafu ndogo ya chuma ambayo isingemlazimu meneja yule
wa benki kusimama hadi kuifikia. Mbele ya ile meza kulikuwa na kiti kimoja kikubwa
cha ofisi.
“Karibu binti” mzee mfupi mwenye kipara cha afya njema,mnene mwenye kitambi
cha ukwasi na macho makubwa ya hila yaliyojificha nyuma ya miwani kubwa alikuwa
amesita kuendelea kufanya alichokuwa akikifanya na kisha kuiegemeza mikono yake
mezani kabla ya kumkaribisha Koplo Tsega. Uso wake wa duara na ndevu zilizokatiwa
vizuri kuuzunguka mdomo wake,umri wake usingekuwa zaidi ya miaka hamsini. Uso
wake ulituama kama maji ya mtungini pasina kuonesha tashwishwi yoyote usoni.
Koti lake la suti ya kijivu alikuwa amelitundika nyuma kwenye kiti chake cha ofisi
kinachoweza kuzunguka nyuzi mia tatu sitini na hivyo kuusanifu vizuri mwonekano
wake mpya wa shati jeusi la mikono mirefu bila tai shingoni hali iliyoupelekea mkufu
wake mkubwa wa dhahabu uliotia nanga shingoni mwake kuonekana kwa usahihi
kama mng’aro wa kito cha thamani katikati ya giza.
“Ahsante” Koplo Tsega akaitikia kwa nidhamu kama iwavyo kwa mtu yeyote
mgeni aingiapo katika ofisi nyeti za mijini kisha taratibu akapiga hatua zake za woga
wa kujifanyisha akikaribia kile kiti cha ofisi kilichokuwa kikitazamana na ile meza ya
ofisini ya yule meneja na alipokaribia akasita kidogo.
“Karibu uketi binti” yule mzee akaongea kwa mamlaka huku akimtazama Koplo
Tsega kwa utulivu kabla ya kujiegemeza taratibu kwenye foronya laini ya kiti chake
cha ofisini.
“Nashukuru” Koplo Tsega akaongea kwa utulivu kisha akasogea karibu na kile kiti
kabla ya kukisogeza nyuma na kuketi. Kibao kidogo chenye utambulisho wa jina na
cheo cha mhusika wa ofisi ile kikamtanabaisha Koplo Tsega kuwa yule mtu aliyeketi
mbele yake nyuma ya ile meza ya ofisini ndiye mwenye jina la Aden Mawala,meneja
wa benki ya Zanzibar Marine jijini Dar es Salaam na hapo akajikuta akimeza funda
kubwa la mate kuzimeza hisia zake moyoni. Kitambo kifupi cha ukimya kikafuata mle
ndani huku kila mmoja akiwaza lake kichwani kabla ya yule mzee meneja wa benki
kuegemeza tena mikono yake mezani na kuvunja ukimya.
“Nipo tayari kukusikiliza shida yako binti,nimebanwa na kazi na bahati mbaya
sana leo sina muda wa kutosha”
“Nahitaji kuonana na ndugu Aden Mawala meneja wa benki hii bila shaka ndiyo
wewe” Koplo Tsega akaongea kwa utulivu katika uso wa kazi huku akimtazama yule
mzee kwa makini.
“Hujakosea” yule meneja wa benki akaitikia kwa utulivu na Koplo Tsega alipozidi
kumchunguza moyoni akahitimisha kuwa alikuwa ni mtu mgeni kabisa machoni
mwake. Yule meneja wa benki kuona vile akapeleka mkono na kuvuta mtoto wa
meza kabla ya kutoa kabrasha fulani na kuliweka pale mezani.
“Nimeambiwa kuwa unahitaji mishahara ya wafanyakazi wa kampuni yenu ipitie
kwenye benki yetu. Unatokea kampuni gani hapa Dar es Salaam?” yule meneja wa
benki akauliza huku taratibu akianza kupekua karatasi za lile kabrasha aliloliweka
mezani.
“T.P.D.F” Koplo Tsega akavunja ukimya.
“Ndiyo kampuni gani hiyo mbona sijawahi kuisikia tangu nizaliwe” yule meneja
wa benki akaongea huku akipunguza kasi ya kupekua kurasa za lile kabrasha.
“Tanzania People Defense Force”
“Kampuni ya ulinzi?” yule meneja wa benki akauliza huku akiangua kicheko
hafifu chenye dharau ndani yake.
“Jeshi la wananchi wa Tanzania” Koplo Tsega akafafanua huku akionesha kuanza
kuchoshwa na dharau za kisomi. Maelezo ya Koplo Tsega yakampelekea yule meneja
wa benki asitishe ghafla kile alichokuwa akikifanya na kuyasimamisha macho yake
akimtazama Koplo Tsega kwa mashaka.
“Jeshi la wananchi wa Tanzania siyo kampuni nadhani kuna jambo lingine
lililokuleta humu ndani” yule meneja wa benki akaongea kwa jazba kidogo huku
akiendelea kumtazama Koplo Tsega kwa udadisi. Pasipo kutia neno Koplo Tsega
akaingiza mkono mfukoni kuchukua ile bahasha aliyoipata nyumbani kwa Balimenya.
Kisha akafungua ile bahasha na kutoa ile barua fupi iliyokuwa ndani ya ile bahasha na
kuitupa pale mezani karibu na yule meneja wa benki. Kuona vile yule meneja wa benki
akaichukua ile karatasi na kuanza kusoma maelezo yaliyokuwa ndani yake. Koplo
Tsega akiwa makini kuzitazama nyendo za yule meneja wa benki akashtukia kuwa
kadiri yule meneja wa benki alivyokuwa akizidi kuyapitia maelezo kwenye ile karatasi
ndivyo mikono yake ilivyokuwa ikizidi kutetemeka. Mwishowe yule meneja wa ile
benki akamaliza kuyapitia maelezo kwenye ile karatasi na kuiweka pale juu ya meza
huku uso wake ukiwa umepoteza utulivu kabisa sambamba na vitone vya jasho jepesi
vikichomoza kwenye paji la uso wake.
“Wewe ni nani?” yule meneja wa benki akajikaza na kumuuliza Koplo Tsega kwa
sauti iliyopwaya.
“Tiglis Tsega,Koplo na Komandoo wa daraja la kwanza,askari wa jeshi la wananchi
wa Tanzania” Koplo Tsega akajitambulisha kwa kujigamba huku akimtazama meneja
wa ile benki kwa udadisi.
“Nani aliyekupa hii barua?” yule meneja wa benki akauliza kwa hofu
“Nahitaji ushirikiano wako vinginevyo nisingetumia hila kufika humu ndani”
Koplo Tsega akaongea kwa utulivu huku akimtazama yule meneja wa benki kwa
makini. Kitambo kifupi cha ukimya kikafuata huku yule meneja wa benki akiachama
mdomo wake kwa mshangao wakati mawazo mengi yakipita kichwani mwake. Sasa
mshtuko alioupata meneja yule ulikuwa dhahiri usoni mwake huku akionekana kama
mtu aliyekuwa akifikiria kukurupuka ghafla na kuanza kutimua mbio ingawa mazingira
yakufanya vile hayakuwepo.
“Ushirikiano upi unaouhitaji kutoka kwangu?’’ baada ya kubabaika kidogo yule
meneja wa benki akajikaza na kuongea kwa sauti ya kupwaya.
“Nafahamu kuwa unatumika na watu wenye mamlaka zaidi juu yako na kutokana
na mazingira uliyonayo huwezi kukataa.Hata hivyo hiyo haimaanishi kuwa hufahamu
kinachoendelea na humfahamu kabisa mtu aliyetoa maagizo haya. Niko tayari
kukulinda wewe na maslahi yako kama utakuwa muwazi na kunipa ushirikiano wa
kutosha katika kumfichua mtu au watu waliopo nyuma ya mtandao huu mchafu”
Koplo Tsega akaongea kwa msisitizo huku macho yamemtoka na mishipa ya shingo
imemtuna hata hivyo kicheko cha mahoka kilichofuata kutoka kwa yule meneja wa
benki kikampelekea ashikwe na butwaa huku akimtazama yule meneja wa benki kama
kituko.
“Binti nadhani umechanganyikiwa bila shaka nani aliyekwambia kuwa mimi
nahitaji ulinzi kutoka kwako na huo mtandao mchafu unaozungumzia mbona
sikuelewi?” yule meneja wa benki akaongea kwa dharau huku akiendelea kuangua
kicheko
“Kwa hiyo unataka niamini kuwa hilo jina la kwenye hii barua siyo lako na hii siyo
benki ya Zanzibar Marine?’’Koplo Tsega akauliza kwa jazba huku akimkata jicho la
hasira yule meneja wa benki.
“Mimi sikatai kuwa Aden Mawala ni jina langu na hii ni benki ya Zanzibar Marine
lakini huu siyo ushahidi tosha wa kunifanya nikubaliane na kile unachokiamini binti.
Jiji hili la Dar es Salaam limejaa matapeli wa kila aina. Mimi ni mtu ninayefahamiana
na watu wengi kutokana na kazi yangu hivyo mtu yeyote mwenye hila mbaya anaweza
kulitumia jina langu kujipatia fedha kwa ujanjaujanja” yule meneja wa benki akajitetea.
“Sikiliza mzee usijaribu kuiondoa hoja yangu ya msingi kwenye mstari. Mimi
sijafika hapa kufuata pesa na wala sina haja na pesa zako badala yake ninachohitaji
kufahamu ni kuwa hizi fedha zilizoandikwa kwenye hii barua ambazo hadi wakati huu
naamini kuwa tayari zimeshaingizwa kwenye benki yako zimetoka kwa nani na ninani
aliyekupa maagizo haya”
“Hakuna pesa yoyote ya kiasi hicho iliyoingia kwenye benki yangu na hata kama
pesa hiyo ingekuwa imeingia taratibu za kibenki haziniruhusu kutoa taarifa za akaunti
ya mhusika kwa mtu mwingine isipokuwa kwa idhini ya mhusika tu” yule meneja wa
benki akaweka kituo huku akiunyanyua mkono wake kuitazama saa yake ya mkononi.
Kuona vile Koplo Tsega akaingiza tena mkono wake mfukoni na kuichukua ile
bahasha ya kaki aliyoipata kule nyumbani kwa Meja Khalid Makame ambayo ndani
yake ilikuwa na hundi nyingi zenye majina ya watu tofauti. Alipoitoa ile bahasha
mfukoni Koplo Tsega akaingiza mkono ndani yake na kuzitoa zile hundi kabla ya
kuzitupia pale mezani karibu na yule mzee meneja wa benki.
“Huwenda huo ukawa ni ushahidi tosha kwako kuwa mimi sijachanganyikiwa
kama unavyodhani na badala yake ninahakika na kile ninachokizungumza.
Ukichunguza kwa utulivu utagundua kuwa majina ya watu yaliyopo kwenye hundi
hizo ndiyo yale pia yaliyopo kwenye ile barua niliyokupa awali hivyo sijakosea njia”
Koplo Tsega akaongea kwa utulivu huku akijitahidi kuidhibiti hasira yake kifuani.
Yule meneja wa benki akainama kwa makini na kuanza kuzichunguza zile hundi pale
mezani huku akionekana kuingiwa na mshtuko kadiri alivyokuwa akimalizia kupitia
hundi moja na kuichukua nyingine. Hata hivyo yule meneja wa benki alikuwa mkaidi
kwani alipomaliza kuzipitia zile hundi akazikusanya kwa pamoja na kuzisogeza karibu
na Koplo Tsega pale mezani.
“Hizi ni taarifa nyepesi sana za kufoji binti na huwezi kunifungamanisha nazo
labda kama unashida nyingine za kibenki mbali na hii nitakusaidia ila kama huna hoja
za msingi utakuwa muungwana sana ukisimama na kuondoka uniache niendelee
na kazi zangu” yule meneja wa benki akaongea kwa dharau huku akiunyanyua tena
mkono wake na kuitazama saa yake mkononi. Koplo Tigls Tsega akazichukua zile
hundi na kuzirudishia kwenye ile bahasha kabla ya kuitia ile bahasha mfukoni pasipo
kuonesha tashwishwi yoyote usoni. Hata hivyo Koplo Tsega alikuwa makini kufuatilia
kwa hila nyendo za meneja yule wa benki hivyo wakati akijitia kuzama katika kuiweka
ile bahasha ya hundi mfukoni mwake alikuwa amemuona yule meneja wa benki jinsi
alivyokuwa akiupeleka mkono wake taratibu kuuvuta mtoto mmoja wa ile meza ya
ofisini.
Akiwa ameshaanza kuhisi nini maana ya tukio lile Koplo Tigils Tsega hakutaka
kusubiri hivyo kwa kasi ya ajabu akaisukuma ile meza ya ofisini kwa miguu yake
kumbana yule meneja wa benki kwenye kiti chake ukutani huku mkono wake mmoja
ukiwa tayari umezama mafichoni kuikamata vyema bastola yake. Yule meneja wa
benki alipotaka kufurukuta mahesabu yake yakagonga mwamba kwani mdomo wa
bastola ya Koplo Tsega ulikuwa tayari ukimtazama usoni. Kisha Koplo Tseakajitetea
karibu na yule meneja wa benki na kuupenyeza mkono wake katika ule mtoto wa
meza uliofunguliwa kwa hila na yule meneja wa benki na alipopapasa papasa bastola
aina ya 22 Caliber Revolver ikaenea vyema kwenye kiganja chake tukio lililompelekea
yule meneja wa benki ashikwe na kihoro baada ya kuona hila yake imeshtukiwa na
kugonga mwamba. Koplo Tsega alipoitoa ile bastola akaichomoa magazini yake na
kuitupa kando kabla ya kugeuka na kumtazama kwa utulivu yule meneja wa benki
ambaye wakati huu alikuwa amebanwa kwenye kile kiti na ile meza yake ya ofisini
huku macho yamemtoka kwa hofu.
“Sura yako inaonekana ni mtu msomi,mkarimu,mtulivu na mzalendo lakini
matendo yako ni ya kinyama kama walivyo wanamtandao wenzako wengine. Watu
kama nyinyi hamtakiwi kuundiwa tume ya uchunguzi huku mkiendelea na kazi kama
ilivyozoeleka badala yake mnastahili kifo cha aibu tena ikiwezekana hadharani ili vizazi
vijavyo visijifunze chochote kutoka kwenu’’Koplo Tsega akaongea kwa utulivu huku
akimzunguka yule meneja wa benki pale kwenye kiti.
“Unajidanganya bure binti hata ukiniua mimi huwezi kufika popote” yule meneja
wa benki akaongea kwa msisitizo huku akihisi kuzidiwa ujanja.
“Maelezo yako yanaonesha kuwa mtandao wenu ni mpana sana na una watu
wengi sana kiasi cha kujipa hakika kuwa hata nikikuua sitofika mbali” Koplo Tsega
akaongea kwa utulivu
“Huelewi unachokizungumza’’ yule meneja wa benki akaongea kwa kujiamini
“Niambie hizi fedha zilizoingia kwenye benki yako zimetoka kwa nani na huo
mtandao wenu unaongozwa na nani?’’
“Nimekwisha kwambia kuwa sifahamu chochote kuhusu hizo hundi wala hiyo
barua uliyokuja nayo. Ndiyo kwanza nimeviona kwako na hakuna kiasi cha pesa kama
hicho kilichoingizwa kwenye benki yangu” yule meneja wa benki akafoka kwa jazba.
“Unadhani ninaweza kukuamini kupitia maneno yako?. Huo ni uongo wa
mwisho usiokuwa na ushawishi niliowahi kuusikia kwa binadamu hapa duniani.
Nahitaji kuiona Cash flow ya hii benki inayoonesha miamala ya pesa zilizoingizwa
na kutolewa” Koplo Tsega akaongea kwa utulivu huku akimtazama yule meneja wa
benki kwa makini na alichokiona mbele yake ni mshtuko mkubwa uliojengeka usoni
kwa yule meneja wa benki.
“Nimekwisha kwambia kuwa taratibu zangu za kazi haziniruhusu kutoa taarifa
za namna hiyo kwa mtu asiyehusika” yule meneja wa benki akasisitiza huku akianza
kutokwa na kijasho chepesi usoni.
“Nahitaji kuona Cash flow statement ya hii benki ndugu Aden Mawala,usinipotezee
muda wangu” Koplo Tsega akasisitiza huku taratibu akikata kipande cha waya wa
simu ya pale mezani,yule meneja wa benki akashindwa kuelewa nini maana ya tukio
lile.
“Unataka kunifanya nini?” yule meneja wa benki akauliza kwa hofu baada ya
kumuona Koplo Tsega akimsogelea pale kwenye kiti na kipande cha waya wa ile simu
mkononi
“Cash flow statement…”
“What…?” yule meneja wa benki kabla hajamaliza kuongea kile kipande cha waya
tayari kilikuwa shingoni mwake na hapo Koplo Tsega akaanza kukikaza taratibu kwa
mikono yake. Yule meneja wa benki kuona vile akaanza kufurukuta katika kutaka
kujinasua huku akitupa mikono na miguu yake huku na kule huku mishipa ya kichwa
ikimchomoza na ulimi na macho vikimtoka. Jitihada zake za kujinasua hazikufua
dafu kwani hapakuwa na nafasi ya kuchomeka mikono yake kwenye ule waya
shingoni na kuuzuia usimkabe. Koplo Tsega akaendelea kuukaza ule waya hadi pale
alipomuona yule meneja wa benki akianza kuishiwa nguvu ndiyo akalegeza taratibu
hali iliyompelekea yule meneja wa benki aanze kukohoa ovyo akiurekebisha mfumo
wa upumuaji wake.
“Fungua kompyuta yako nahitaji kuona Cash flow statement ya hii benki” Koplo
Tsega akanong’ona kwa sauti tulivu sikioni mwa yule meneja wa benki.
“Okay…!” yule meneja wa benki akaitikia kwa shida huku hofu imemshika na
muda mfupi uliyofuata akaifungua ile kompyuta yake ya ofisini pale mezani huku
Koplo Tsega akiwa makini nyuma yake. Ile kompyuta ilipofunguka yule meneja wa
benki huku mikono ikimtetemeka akafungua mafaili kadhaa mle ndani ya kompyuta
hadi alipolifikia faili lenye rekodi za miamala ya pesa zilizoingia na kutoka kwenye ile
benki kufikia mwezi ule.
Kitambo kifupi cha ukimya kikapita mle ndani huku Koplo Tsega akijaribu
kuichunguza taarifa ile kwa maikini. Aliporidhikanayo akamwambia yule meneja wa
benki aiprint.Yule meneja wa benki akasita kidogo lakini macho yake yalipokutana
na macho ya Koplo Tsega hofu ikamuingia tena na hapo akalainika na kufanya vile
alivyoagizwa. Haraka akaiamuru ile kompyuta kuprint ile taarifa ya benki kwenye
printer iliyokuwa juu ya meza ndogo kando ya eneo lile.
Mara baada ya yule meneja wa benki kuprint ile taarifa ya benki Koplo Tsega
haraka akaichukua na kuanza kuipitia katika namna ya kuichunguza kama angeweza
kupata taarifa yoyote ya kumsaidia. Kupitia taarifa ile ya benki Koplo Tsega akagundua
kuwa kulikuwa na miamala mingi iliyofanywa kwenye ile benki kwa kipindi cha miezi
kadhaa iliyopita na alipozidi kuchunguza akagundua kuwa miamala mingi ilikuwa
imefanywa na kampuni nyingi zilizokuwa jijini Dar es Salaam ambazo kwa namna
moja au nyingine hazikupaswa kutiliwa mashaka kutokana na aina ya biashara
kampuni zile zilizokuwa zikifanya. Kulikuwa pia na miamala mingine iliyofanywa na
watu binafsi ambayo fedha zao zilikuwa za kawaida kwa vile benki ile ilikuwa imejikita
kwenye biashara ya uuzaji wa bidhaa nje ya nchi na uingizaji wa bidhaa ndani nchi.
Katika kuendelea kuchunguza Koplo Tsega akajikuta akivutiwa na akaunti moja
ambayo ilikuwa imetumika kufanya muamala wa pesa nyingi sana za kigeni kwa mara
moja. Akaunti ile ilikuwa na jina moja la Zanzibar Stone City Bazaar. Koplo Tsega
alipozidi kuchunguza akagundua kuwa kupitia rekodi zilizokuwa kwenye taarifa ile
ya benki akaunti ile ilikuwa ni mpya kabisa kwani hapakuonekana rekodi nyingine
zilizoonesha kuwa akaunti ile ilikuwa ikitumika huko siku za nyuma. Lilikuwa ni
jambo la kustaajabisha lakini vilevile linaloweza kuaminika.
Koplo Tsega alipozidi kuchunguza mashaka juu ya kile alichokuwa akikihisi
yakazidi kuongezeka. Muamala wa fedha nyingi uliofanywa kupitia akaunti ile ulikuwa
umefanyika siku chache baada ya wao kuondolewa kwenye ile tume ya udhibiti na
upambanaji wa biashara ya dawa za kulevya nchini na hatimaye kuingizwa kwenye
vikosi vya kijeshi vya kuimarisha amani ya kudumu-MONUSCO nchini jamhuri ya
kidemokrasia ya nchi ya Kongo. Lakini vile vile jina la akaunti ile lilifanana na jina
la akaunti iliyokuwa kwenye zile hundi alizozipata kule nyumbani kwa Meja Khalidi
Makame. Kwa sekunde kadhaa Koplo Tsega akajikuta ameganda kama nyamafu
huku akiendelea kuikodolea macho taarifa ile ya benki kwenye ile karatasi na mkono
wake mmoja ukiwa umeikamata bastola yake vyema mkononi na kuielekezea kifuani
kwa yule meneja wa benki ambaye mashaka yalionekana dhahiri usoni mwake.
“Nahitaji bank statement ya hii akaunti” Koplo Tsega akasogea karibu na
kumwambia yule meneja wa benki huku akimuelekeza kwa kidole chake kwenye ile
akaunti ya benki ya Zanzibar Stone City Bazaar. Yule meneja wa benki akaikodolea
macho ile akaunti kabla ya kusita huku akigeuka na kumtazama Koplo Tsega kwa
mashaka.
“Print…” Koplo Tsega akaongea kwa utulivu huku akifanya ishara ya kichwa
kumaanisha kile alichokuwa akikisema kisha akaihamisha bastola yake kichwani kwa
yule meneja wa benki. Yule meneja wa benki kuona vile akainama tena kwenye ile
kompyuta yake mezani na kuanza kushughulika nayo na baada ya muda mfupi ile
kompyuta ikaanza kuprint ile Bank statement ya akaunti ya Zanzibar Stone City Bazaar
ikionyesha kiasi cha pesa,mwaka,mwezi,siku,saa na tarehe ambayo muamala ule wa
fedha nyingi kwenye ile akaunti ulikuwa umefanyika.
Jambo moja la kushangaza ni kuwa fedha zilizoingizwa kwenye akaunti ile
zilionekana kuwa zilikuwa zimetokea kwenye benki mama iliyokuwa kisiwani
Zanzibar. Koplo Tsega akaendelea kuikodolea macho akaunti ile huku akishindwa
kuamini kile kilichokuwa kwenye ile karatasi.
“Kiongozi wa mtandao wenu anaitwa nani?’’ Koplo Tsega akavunja ukimya
akimuuliza yule meneja wa benki hata hivyo yule meneja wa benki hakuzungumza
neno badala yake akatikisa kichwa chake kuonesha kuwa alikuwa hafahamu chochote.
“Kukaa kimya haitakusaidia kitu ndugu Aden Mawala kwani ni vizuri ukawa
muwazi na kunieleza ni nani anayehusika na ugawaji wa mamilioni ya fedha nyingi
kiasi hiki huku akisisitiza mambo yenu yafanyike kwa usiri mkubwa’’
“Nimekwisha kukueleza kuwa mimi sifahamu chochote” yule meneja wa benki
akasisitiza hata hivyo kabla hajamaliza risasi moja kutoka kwenye bastola ya Koplo
Tsega yenye kiwambo cha kuzuia sauti ikapenya na kuuvunja mfupa wa paja lake.
Yule meneja wa benki akapiga yowe kali la maumivu huku akigugumia kwa maumivu
makali yaliyoambatana na jeraha linalovuja damu.
“Niambie Aden ni nani anayehusika na fedha hizi?” Koplo Tsega akauliza
“White…’’
“White ndiyo nani?” Koplo Tsega akauliza kwa shauku
“White Sugar…!” yule meneja wa benki akaongea huku akilalama kwa maumivu
makali ya jeraha la risasi pajani mwake.
“Niambie,huyo White Sugar ndiyo nani?’’ Koplo Tsega akauliza kwa utulivu.
“Meneja wa Zanzibar Stone City Bazaar”
“Anaishi wapi?’’
“Sifahamu na wala sijawahi kuonana naye” yule meneja wa benki akajitetea lakini
kitendo cha kumuona Koplo Tsega akiunyoosha mkono na kuelekezea bastola yake
kwenye paja la mguu wake mwingine akaingiwa na hofu.
“Duka lake lipo ndani ya Mlimani City Shopping Mall linatazamana na duka
kubwa la vinyago la African art craft” yule meneja wa benki akafafanua hata hivyo
mduwao mwingine ukamshika wakati alipouona mdomo wa ile bastola ya Koplo
Tsega ukielekezewa kwenye kifua chake.
“Tafadhali usiniue...!”
“Sikuui Aden nakupumzisha tu!’’ kabla yule meneja wa benki hajaongea neno
risasi mbili za bastola ya Koplo Tsega zikapenya kifuani mwake na kutengeneza
matundu makubwa mawili yanayovuja damu kwenye moyo na hapo yule meneja wa
benki akatikisika kidogo kwenye kile kiti chake cha ofisini kabla ya kutulia huku roho
yake ikiwa mbali na mwili.
Koplo Tsega hakutaka kuendelea kupoteza muda hivyo akaingiza mkono
mfukoni na kuchukua pipi ya kijiti na kuimenya kabla ya kuitia mdomoni. Kisha
haraka akachukua kilicho chake mle ndani na kuelekea kwenye mlango wa ile
ofisi. Alipoufungua mlango wa ile ofisi na kutoka nje pale mlangoni akakutana na
mwanaume mmoja aliyekuwa akielekea kwenye ile ofisi ya meneja wa benki.
“Subiri kidogo kuna mtu anazungumza na meneja” Koplo Tsega akamwambia
yule mwanaume wakati akipishananaye kwenye ile korido.
“Sawa!” yule mwanaume akaitikia huku akigeuza na kurudi kule alipotoka. Muda
mfupi uliofuata Koplo Tsega alikuwa akikatisha kando ya lile dawati la idara ya
huduma kwa wateja. Yule dada mlimbwende mfanyakazi wa idara ile alipomuona
Koplo Tsega akatabasamu na kumuuliza
“Vipi amekusikiliza haja yako?”
“Ndiyo nashukuru sana dada kwani amekwisha nielekeza cha kufanya. Nitarudi
tena mapema sana baada ya kukamilisha taratibu zote” Koplo Tsega akajinadi kwa
hila huku akijifanya ni mwenye haraka.
“Karibu tena”
“Ahsante na kazi njema” Koplo Tsega akashukuru na kuaga huku akielekea
kwenye mlango mkubwa wa kioo mbele ya lile jengo la benki ya Zanzibar Marine.
Alipofika akausukuma ule mlango na kutokomea nje huku macho ya yule dada
mlimbwende wa idara ya huduma kwa mteja yakimsindikiza kwa nyuma.
 
SAA TISA ALASIRI KASORO dakika chache Koplo Tsega akaegesha gari
lake kwenye eneo kubwa la wazi la maegesho ya magari la Mlimani City Shopping
Mall. Kabla ya kushuka akayatembeza macho yake taratibu kuyachunguza magari
yaliyokuwa eneo lile kwa utulivu. Mvua ilikuwa imeanza kunyesha hivyo hakumuona
mtu yeyote eneo lile au kama kungekuwa na watu basi huwenda watu hao wangekuwa
wamejifungia ndani ya baadhi ya magari yaliyokuwa yameegeshwa eneo lile.
Tangu alipotoka kwenye ile benki ya Zanzibar Marine akili yake ilikuwa imejikita
katika kumtafakari yule mtu aliyekuwa akifahamika kama White Sugar meneja wa
duka la Zanzibar Stone City Bazaar kama yule meneja wa benki ya Zanzibar Marine
alivyotanabaisha. Kwa namna moja au nyingine Koplo Tsega aliamini kuwa huyo
mtu aliyekuwa akifahamika kwa jina la White Sugar ndiye ambaye angekuwa kiungo
muhiimu sana katika ule mtandao mchafu ulioshiriki kikamilifu katika kusuka
mpango wa kuwaengua yeye na Sajenti Chacha Marwa kutoka katika tume maalum
inayoshughulika na udhibiti na upambanaji wa biashara haramu ya dawa za kulevya
nchini Tanzania.
Hisia za Koplo Tsega zikamtanabaisha kuwa kumpata White Sugar lingekuwa ni
jambo muhimu sana katika kuwafahamu watu wote waliohusika na njama chafu dhidi
yao lakini vilevile kumpata White Sugar kungeweza kutatua maswali mengi yaliyokuwa
yakiisimanga vibaya nafsi yake. Maswali kama mtandao ule mchafu uliotumika
kuwahujumu ulikuwa ukimhusisha nani na nani vilevile ulikuwa ukifadhiliwa na nani.
Meja Khadid Makame,kiongozi wa kijeshi aliyekuwa akiheshimika sana kwa weledi
wake alikuwa na nafasi gani katika mpango ule mchafu na kama alihongwa fedha
basi alihongwa na nani na fedha hizo zilikuwa kiasi gani. Kufikia pale Koplo Tsega
akayahamisha mawazo yake na kuanza kumfikiria yule mwanaume aliyemuokoa
kutoka mikononi mwa wale wanausalama kule kwenye lile jengo refu la ghorofa
lililokuwa katikati ya maeneo ya posta jijini Dar es Salaam. Maswali bado yalikuwa
mengi na majibu yake yalihitaji muda na uchunguzi makini.
Hatimaye Koplo Tsega akafungua mlango na kushuka kwenye gari kisha akaanza
kuzitupa hatua zake kwa haraka akielekea kwenye mlango mkubwa wa kuingilia
kwenye lile duka kubwa la kisasa na la kimataifa-Mlimani city shopping mall. Begi lake
likiwa mgongoni,kofia ya sombrero kichwani na miwani myeusi machoni taratibu
Koplo Tsega akawa akiyatembeza macho yake kwa uficho mkubwa na kuwatazama
watu wote waliokuwa eneo lile. Hakumuona mtu yeyote wa kumtilia mashaka hivyo
akaendelea kuzitupa hatua zake kwa utulivu kuelekea kwenye lile jengo.
Kulikuwa na watu wengi ndani ya maduka yale ya kisasa waliokuwa wamefika
kupata huduma tofauti na baadhi ya watu wale walikuwa wamesimama kwenye korido
za maduka yale wengine wakinunua bidhaa na wengine wamesimama wakisubiri
mvua ile iishe ili waondoke baada ya kumaliza kununua mahitaji yao.
Koplo Tsega alipofika katikati ya korido zile akasimama kwa utulivu akiyachunguza
mazingira yale. Kulikuwa na korido mbili kubwa na pana,moja upande wa mbele na
nyingine upande wa kulia. Korido zile zilikuwa zikitazamana na maduka mbalimbali
 
Back
Top Bottom